Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Boss wangu alikuwa anachukua 30
 
Mkuu wanawake wenye Pesa wanapenda vitu vidogo vidogo sana, kama Iryn alikua na pesa. Huwezi kumshawishi kwa pesa kabisa, Iryn nilikuaga namfanyia vituko sana na alikua anafurahi sana.
Kaka insider inamaana kwa sasa hauna mawasiliano au ukaribu tena Ireen maana unatumia sana nyakati zilipotipa kwenye uandishi kama vile kwa sasa hampo pamoja tena, yaani kila mtu ana hamsini zake kwa sasa
 

Kuna machalii walikuja toka England baba yao anamiliki migodi walimfanya Fred vunja bei akimbie kulipa bills mzee wale jamaa wana-spend ni [emoji91][emoji91] afu hata hawawazi yan
 
Chai chai.

Madereva wa uber wenyewe wanashangaa haya maisha anayoishi mwenzao.
Kama chai ndg kinachokuganya uwe hapa kumfuatilia ni nini hasa embu wakati mwingine tupunguze chuki na wivu wa kijinga kwa watu tusio wafahamu!
Fanya na wewe kutunga hadithi yako uilete hapa pia, tuone vile utapata wasomaji acheni wivu na chuki za kijinga walimwengu
 
Mimi naona kila kinachosimuliwa ni kweli hata kama kuna vinogesho kidogo wala sio shida zangu.

Kuhusu pesa nyie mnadhani hela zote zilizowahi kutengenezwa na BOT hapa nchini zipo wapi?
Hela zipo humuhumu nchini watu wanazo[emoji28][emoji28]!!....

Ni bahati tu ya pesa ukiwa nayo unateleza tu, halafu sio kila mtu lazima ateseke ili kupata pesa,wengine wana nyota ya pesa,zinawafata zenyewe.
 
Haya mambo mtu kama hayupo kwenye system ya ulaji hawezi yajua

Mimi kuna mshikaji nilifanya nae kazi mwaka 2012 tulikuwa same level economic hata mshahara

Baadae mshahara wake ukaanza kupanda na vyeo na akapata connection kuhama ofice nyingine...na hiyo ofice ina malupu lupu kibao...

Alinipiga gap la hatari...now yupo vizuri saana kiuchuni...ana gari 3 zenye thamna ya 240milion, ana ghorofa ya kuishi...ashajenga apartment yenye ghorofa Goba Goba...kwenye list ya magari imo Range

Hii inamanisha kuna mtu mambo yake yakiwa sawa au akifunguliwa na Mungu...kuhonga milioni moja /3 kwake sio issue

Na maisha yanatofautiana

Mfano mwingine

Hivi mnajua mtu anaueishi apartment zile za upanga za akina Fida Hissein analipa kodi 2,500$ Usd...kwa madafu ni kama 5.8 kwa mwezi....je mtu huyu kwa mwaka anaingiza sh ngapi?? kama kodi ya mwezi tu analipia milion 6

Kuna watu wanamaisha basi tu
 
Kulipwa 45million kwa mwezi si sawa na dola elfu 20, wako wanaolipwa zaidi ya hizo, tatizo umaskini wetu tunachukulia vitu vingi haviwezdkanj, wakati ni kawaida kwa wenzetu, nchi hii hii IST wanalipa ada kwa mwa 65million wakati UDSM milioni 2 hutaki kutoa. Tunatofautiana.
 
Kitu kingine Mungu hana upendeleo,hata kama kuna maisha unaishi unahisi huwezi kufika kiwango fulani mwambie Mungu.

Muombe Mungu bila kuchoka huku ukijishughulisha kwa shughuli hata kama unaona kabisa hutoboi.

Mungu akiamua kukupa wala hakuandikii barua, unaona tu kila unalogusa linaenda tu bila kutumia nguvu. Na ndio kama ndugu yetu insider yanayomtokea.

Sasa wenye imani haba hudhani stori chai au kama haiwezekani.

Kuna watu wana nyumba mpaka 70! Kuna jamaa ana bajaji 123 kazitawanya mikoa mbali mbali zinapiga kazi.
 
NAONA MMEAMUA KUMTETEA BWANA WENU.

Tajiri niliobahatika kukutana nao ni wagumu Sana kwenye malipo.

Swali langu nauliza Hata kama story ni ya ukweli.

Ila kwa mtu mwenye jicho la tatu lazima ujue msimuliaji kaamua kuongeza sukari kunogesha genge.

City vingi anavyooongea havina.uhalisia na haviendani na maisha ya sasa.

Kama iryn aliweza Kubagain nae malipo mwanzoni kabisa mpaka ikawa laki 3 sidhani sass ataweza kuwa mrahisi kutoa hela ovyoovyo kwa kiasi hicho.

From no where muajemi anakupa million 3.

From no where prisca tena mwanafunzi wa chuo anakupa laki 3.

Ofa unapata wewe tu.

Hadi umemsahau mke wako.

Mzee hizi kamba zako tumegundua usitupange Sana punguza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…