Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Huwa natafutaaaaaa cha kujifunza humu kama wengine wanavyodai wana pata lesson kwenye hii story ila waaap!!naambulia patupu kabisaaa..

Naishia kusogeza muda tu na ki enjoy simulizi basi
unafanya mishe gani kiongozi.? mana yamkini umeshafanikiwa ama upo kwenye ajira ambayo inakufanya uwe centred na hiyo ajira.
 
SEASON 02
CHAPTER 40

“TRUE STORY BY INSIDER MAN”

PREVIOUS:
Baada ya kuwasili pale JNIA, tulikaa na kuendelea na mazungumzo. Nilimsihi sana Hilda aisimamie kampuni vizuri hadi nitakaporudi, nikijua kuwa ilikuwa muhimu kwa ajili ya usimamizi mzuri. Baada ya dakika 20, tuliagana kwa kukumbatiana, nami nikacheck-in kwa ajili ya kuanza safari yangu kuelekea South Africa, nilijua ni mwanzo wa safari muhimu na nilikuwa na matumaini makubwa.

CONTINUE:

Nikiwa kwenye harakati za kukamilisha taratibu kabla ya safari, simu ya Mary iliingia, na bila kusita niliipokea. Katika mazungumzo, nilikumbuka kuwa sikuwa nimemjulisha rasmi kwamba naondoka kwenda Afrika Kusini, ingawa tayari nilikuwa nishamgusia kuhusu safari hii. Nilipompa taarifa kamili, Mary hakuweza kuzichukua kwa urahisi. Alionyesha hisia kali na kunilalamikia kwa kuondoka bila kumuaga rasmi, jambo ambalo halikumfurahisha hata kidogo.

Nilimkumbusha kwamba tayari nilishamgusia kuhusu safari hii, lakini bado hakutaka kuelewa. Alisisitiza kuwa nilipaswa kumjulisha mapema zaidi, na sio kusubiri mpaka anipigie simu ndipo nimpe taarifa hizi. Hasira zake ziliongezeka, na hatimaye alikata simu ghafla. Kwa upande wangu, sikuona haja ya kuendelea kumfikiria, kwani niliona anachukulia jambo hili kwa namna ya kitoto. Niliamua kuacha nifikirie mambo muhimu zaidi na kuendelea na safari yangu.

Safari ya kuelekea Afrika Kusini ilianza vizuri, na nilibahatika kupata siti ya upande wa dirishani. Pembeni yangu aliketi binti Mtanzania, aliyenipa tabasamu la salamu tulipokutana macho. Ingawa tulisalimiana kwa heshima, sikuwa na hamu ya kuendelea na mazungumzo. Mawazo yangu yalikuwa mbali sana, nikitafakari kwa kina juu ya hatima ya maisha yangu na mustakabali wangu baada ya safari hii. Nilihisi kama nilikuwa kwenye hatua ya mabadiliko, na kila kitu kingine kilionekana kama kelele zisizo na maana wakati huo.

Nilipokuwa nikitazama anga za mbali kupitia dirisha la ndege, matumaini yangu ya kuwa baba wa watoto wawili yalijaa ndani yangu. Niliamini kwa dhati kuwa Iryn angejifungua salama, na hilo lilinipa faraja. Hata hivyo, mawazo yangu yalivutwa kwa nguvu kuelekea mahusiano yangu na Mary. Maneno ya Jane yalinirudia kichwani, na kadri nilivyoyatafakari, niliona alikuwa sahihi. Ikiwa mahusiano yangu na Mary yangekuja kufahamika kwenye familia yake, ningekabiliwa na shida kubwa. Hili lilikuwa jambo lililonitatiza sana.

Kilichonifanya nisijisikie vizuri zaidi ni kwamba, licha ya kuelewa athari za uhusiano huu, nilikuwa kwenye dilema kali kuhusu hatua sahihi ya kuchukua. Nilijua kwamba kumuacha Mary kungekuwa ngumu, na wakati huo huo, kuendelea naye kulionekana kama kuzidisha tatizo. Mawazo yangu yalikuwa magumu sana, nikikosa maamuzi ya busara kuhusu mustakabali wa uhusiano wetu.

Kadri safari ilivyoendelea, nilijikuta nikitafakari zaidi kuhusu maisha yangu tangu nilipoanza biashara za Uber. Kipindi hicho kilikuwa mwanzo wa mabadiliko makubwa, ambapo nilikutana na watu wengi sana ambao kwa njia moja au nyingine wamekuwa msaada mkubwa katika safari yangu ya kimaisha. Nilipitia mengi mazuri na magumu, na kila tukio lilionekana kuwa na nafasi yake maalum katika hadithi ya maisha yangu. Nilihisi kama maisha yangu yalikuwa kama filamu, yenye mlolongo wa matukio ya kipekee.

Kutokana na hayo, wazo moja lilianza kuota mizizi, kuandika kitabu. Kitabu ambacho kingekuwa ukumbusho wa safari yangu, changamoto nilizokutana nazo, mafanikio niliyoyapata, na watu waliokuja na kuondoka. Hili lilionekana kuwa jambo la maana, sio tu kwa ajili yangu binafsi, bali pia kwa wengine, ili waweze kujifunza kutokana na yale niliyoyapitia kwa muda mfupi sana lakini yenye uzito mkubwa.

Tulipowasili Johannesburg, tulipewa muda wa mapumziko wa takriban saa moja kabla ya kubadilisha ndege ya kuelekea Cape Town. Nikiwa nimechoka kidogo lakini bado nikiwa na ari ya kufika, nilitumia muda huo vizuri kufanya booking ya hoteli. Nilichagua hoteli ileile ambayo mimi na dada yangu tulifikia safari iliyopita, Southern Sun Newlands Hotel.

Baada ya lisaa na dakika kadhaa, tulianza safari yetu ya kwenda Cape Town. Ndege iliondoka Johannesburg saa mbili asubuhi, na tulifika Cape Town majira ya saa tano asubuhi. Nilipomaliza taratibu za uhamiaji na kuchukua mizigo, nilichukua tax moja kwa moja kuelekea kwenye hoteli niliyokuwa nimefanya booking.

Nilipowasili hotelini, jambo la kwanza kabisa nilifanya ni kuoga ili kuondoa uchovu wa safari. Baada ya hapo, niliamua kutoka kwenda kupata chakula kwani nilikuwa na njaa kubwa. Nilipokuwa nikila, nilikuwa pia nawasiliana na sister, ambaye aliniongoza kuhusu hospitali walikokuwa. Aliniambia kuwa nikianza kuondoka niwajulishe ili tuweze kukutana. Mawasiliano hayo yalifanya nianze kujiandaa kisaikolojia kwa hatua zinazofuata.

Nilipokuwa hotelini, mawazo yangu yalirudi nyuma, nikamkumbuka yule dada niliyempa pesa kipindi kile nilipoondoka na dada yangu hapa hotelini. Hali hiyo ilinifanya nianze kuhisi tamaa, hisia zangu zikielekea kwake. Nilikuwa nalikumbuka jina lake vizuri, hivyo nilichukua hatua ya kumuuliza mhudumu mmoja wa hoteli kuhusu yule dada. Alinijibu kwa ufupi kuwa ataingia shift ya jioni.

Sasa, baada ya kupata taarifa hizo, nilihisi msukumo wa kutaka kuomba namba yake ya simu, lakini nikaamua kujizuia. Niliona ni busara zaidi kuwa mpole na kuacha mambo yaende kwa utaratibu wake, kwani nilijua tutaonana hivyo, niliamua kusubiri kwa utulivu.

Kipindi nikiwa hapa na sister, ukweli ni kwamba nilivutiwa sana na yule dada mhudumu, lakini nilijizuia kwa heshima ya sister. Nilijua wakati ule haikuwa sahihi kuchukua hatua yoyote zaidi ya mazungumzo ya kawaida. Lakini moyoni nilihisi kwamba siku moja nitarudi tena Afrika Kusini, na nitaishia kufikia hoteli hii, ambapo nitapata fursa ya kumuona tena. Hata ile hatua ya kumpa pesa haikuwa tu msaada wa kawaida, nilikuwa najenga mazingira mapema kwa ajili ya kupata "mzigo" bila vikwazo hapo mbeleni.

Nilihisi tamaa kubwa ya kupiga game la mwisho kabla ya Iryn kujifungua, kwa sababu ya heshima na umuhimu wa mtoto ambaye alikuwa njiani kuja. Nilijua kuwa pindi Iryn atakapojifungua, singeweza tena kupiga game mpaka nitakaporudi Tanzania, na wakati huo nisingejua nitatumia muda gani huku Afrika Kusini. Hali hii ilifanya hisia zangu kuwa za ndani zaidi, kwani nilijua kuwa na mabadiliko makubwa yanakuja, na ningeweza kupoteza fursa za kufanya mambo niliyoyapenda.

Wakati nikiwa na mawazo yangu, Jimmy alinitafuta kupitia WhatsApp na kunijulisha kwamba yuko njiani anakuja. Nilimjibu kwa kumwambia niliko, pamoja na hoteli niliyofikia. Alifurahishwa na taarifa hiyo na kusema kwamba naye atafikia hoteli hii. Jimmy aliomba niweze kumfanyia booking ya chumba mapema ili asije kukosa nafasi. Niliamua kumsaidia na kuanza kupanga jinsi ya kumtafutia chumba, huku nikijua kuwa uwepo wake jirani ungekuwa muhimu kwangu.

Saa 8 mchana, niliondoka kuelekea hospitali, nikiwa nimetumia usafiri wa Uber. Dereva aliyekuja kunichukua alikuwa ni choko, na njiani alinitafutia mazungumzo mengi ambayo yalinisababisha kuhisi kero. Nilijua niko katika nchi ya watu na sikutaka kuonesha tabia yoyote isiyofaa. Hivyo, nilimjibu maswali yake kwa ustaarabu, lakini moyoni nilikuwa nikiomba tu kufika hospitali mapema. Katika maisha yangu ninaaminu kwamba kukutana na watu hawa kunaweza kuwa kama mikosi kwangu.

Umbali kutoka hotelini hadi Mediclinic hospital ni kama kilomita 15, sawa na kutoka Mwenge hadi Kivukoni, na nilijua Iryn hakuwa akiishi mbali sana na chuo anachosoma wala hoteli niliyofikia. Nilipokaribia hospitali, shauku yangu ilikuwa kubwa sana, nikitamani kwa dhati kumuona Iryn.

Mara baada ya kufika, nilimkuta sister akiwa ananisubiri pamoja na Samantha pale nje. Tulipokutana, tulisalimiana, lakini niliona wazi kwamba sister hakuwa sawa. Hisia zangu zikanifanya nishuku kuwa huenda ilikuwa ni kuhusu lile suala la mama J. Nilihisi kwamba sister bado alikuwa na mawazo mengi kichwani mwake. Sikutaka kumuuliza sana kuhusu hilo, kwani nilikuwa na hamu ya kuzungumza na Samantha, ambaye hatukuweza kukutana kwa muda mrefu. Hivyo, nilijaribu kuelekeza mazungumzo yangu kwake, nikifurahia kuungana tena na shem wangu.

Tulipoingia ndani ya hospitali, tulielekea moja kwa moja hadi wodi aliyokuwa amelazwa Iryn. Nilipofungua mlango na kuingia ndani ya chumba, jambo la kwanza lililoshika macho yangu lilikuwa ni Vivian, aliyekuwa amesimama pembeni akizungumza na daktari, kana kwamba alikuwa akipokea maelekezo muhimu. Lakini hata hivyo, macho yangu yote yalivutwa kwa Iryn.

Alikuwa amelala kitandani, akiwa uchi, na jasho likimtoka kwa wingi, ishara ya uchovu wa mwili uliomlemea. Mwili wake ulionekana dhaifu sana, hali ambayo ilinipatia hisia za huruma kali. Nywele zake ndefu na nzuri zilikuwa zimetifuka, zikionesha uchovu aliokuwa nao. Matiti yake yalionekana kuvimba, na mwili wake wote ulionekana kubadilika kwa kiasi kikubwa.

Iryn alikuwa akihema kwa shida, kila pumzi ikionekana kuwa mzigo kwake. Hali yake ilinishtua, nikitambua kuwa huu ulikuwa wakati mgumu sana kwake. Hisia za huzuni na wasiwasi zilijaa ndani yangu, huku nikijua kwamba nilihitaji kuwa na nguvu kwa ajili yake katika kipindi hiki kigumu.

Wasiwasi wangu ulianza kuongezeka mara moja, nikijiuliza kama hali yake ni mbaya zaidi ya nilivyofikiria. Nilimwona akiugua kimya kimya, na moyo wangu ulianza kushuka, nikihisi uzito wa hali hii. Sikujua nini kingetokea, lakini nilihisi kwamba sasa kila kitu kilikuwa nje ya uwezo wangu, na yote niliyoweza kufanya ni kumwombea awe salama.

Nilisogea karibu na kitanda cha Iryn, nikamshika shavu lake kwa upole, na mara moja nilihisi joto lake lilikuwa limepanda. Japo mwili wake ulikuwa dhaifu, niliweza kugundua alifurahi kuniona, ingawa hakuwa na nguvu za kuonyesha ile furaha waziwazi. Lakini kwa namna fulani, niliweza kuhisi furaha yake ndani ya hali ile ngumu aliyokuwa nayo.

Nikiwa nimemshika mkono, nilijikuta nikilegea kando yake, nikamshika tumbo lake kwa upole na kwa sauti ya faraja nikamwambia, “You will be alright, my love."

Alinitazama kwa macho yenye uchovu lakini yenye matumaini, na kwa upole akatikisa kichwa chake, akionyesha kukubaliana nami. Huo ulikuwa ni wakati wa kimya, lakini pia wa utulivu.

Nilipoanza kuzungumza na kina Sister kuhusu maendeleo ya Iryn, walinifahamisha kuwa njia ya mtoto bado haijafunguka, lakini kuna matumaini ya kujifungua salama kwa njia ya kawaida (Normal Vaginal Delivery). Pia waliongeza kuwa, kama hali hiyo itaendelea na njia ya uzazi itaendelea kusumbua, basi madaktari watalazimika kumfanyia upasuaji (OP) ili kuinusuru afya ya Iryn pamoja na mtoto.

Ingawa taarifa hizo zilikuwa na changamoto, kulikuwa na faraja katika kujua kwamba walikuwa tayari kuchukua hatua sahihi kwa kuhakikisha usalama wa Iryn na mtoto. Hali hii ilinipa matumaini ya kumalizika kwa hali hii kwa usalama.

Madaktari na wauguzi walikuwa wakiingia na kutoka ndani ya chumba, wakionekana kuwa na shughuli nyingi sana, wakihangaika kuhakikisha kila kitu kipo sawa. Hali ile ya harakati na uzito wa mazingira ilinifanya nishindwe kuvumilia kukaa ndani kwa muda mrefu. Nilitambua kuwa ni bora niwapishe waendelee na kazi zao bila usumbufu wowote, hivyo nikaamua kutoka nje ili kupata hewa na kutuliza mawazo yangu, huku nikisubiri kwa matumaini kila kitu kitakwenda sawa.

Pale nje, kwenye benchi, Samantha alikuwa amekaa akisubiri kwa utulivu, maana hakuwa ameruhusiwa kuingia ndani kwa sababu ya hali ya dada yake, Iryn, ambaye alikuwa kwenye mazingira ya faragha. Isingekuwa busara, wala heshima, kwa Samantha kumuona dada yake katika hali ile ya udhaifu.

Nikiwa nimekaa naye, tulianza kuzungumza kwa upole, huku mawazo yangu yakiendelea kuzunguka hali ya Iryn. Katika mazungumzo, nilimwambia Samantha kuwa tungehitaji kwenda shopping ili kununua baadhi ya vitu vya mtoto. Samantha alinijibu kuwa wao tayari walikuwa wamenunua kila kitu kinachohitajika, lakini nikamwambia kwamba safari hiyo ilikuwa muhimu kwa upande wangu, nilihitaji kununua vitu kwa ajili ya mtoto wetu.

Wakati tunaendelea kuzungumza, mama yake mdogo wa Iryn, ambaye ni mke wa baba yake, alifika na kutusalimia kabla ya kuingia ndani. Nilipomwona, nilihisi kama nimemfananisha na mtu niliyewahi kumuona mahali fulani, lakini sikuweza kukumbuka wapi. Samantha aliniambia kuwa huyo ni mama mdogo wa Iryn, na hapo ndipo nikakumbuka kwamba nilimwona kwenye picha kupitia simu ya Iryn.

Baada ya dakika 20, Vivian alitoka ndani, na tulikubaliana kuondoka kuelekea moja ya shopping mall ili kununua vitu vya mtoto. Safari yetu ilianza kwa furaha, na tulitumia takribani masaa mawili kufanya manunuzi ya vitu mbalimbali muhimu, ikiwa ni pamoja na mavazi, toys, na vitu vingine vingi.

Tulikuwa na mazungumzo mazuri huku tukichagua bidhaa, na kila bidhaa tuliyoinunua iliongeza hisia zetu za furaha na matarajio. Baada ya kumaliza manunuzi, tukarudi tena hospitali, tukijua kuwa vitu hivi vitakuwa na umuhimu mkubwa kwa Iryn na mtoto. Moyo wangu ulijaa matumaini na furaha, nikihisi kwamba nilikuwa nikichangia kwa njia fulani katika maisha ya familia yetu mpya.

Baada ya kufika hospitali, bila kutegemea, nilikutana na mama Janeth. Baada ya kusalimiana, aliniambia kwamba alikuwa pale tangu asubuhi, lakini alikuwa ameenda sehemu fulani kwa muda mfupi. Mama Janeth alionekana kufurahia sana kuniona, na alisema alifurahi pia kumuona dada yangu.

Aliniondoa wasiwasi wote kuhusu afya ya Iryn, akisema niondoe hofu, kwani aliamini Iryn atajifungua salama. Maneno yake yalinipa faraja kubwa, na nilihisi kama mzigo mzito ulishuka kutoka kwenye bega langu. Utu wake na uhakikisho wake vilinipa nguvu na matumaini zaidi, nikijua kwamba nilikuwa na watu wa kutegemea katika kipindi hiki kigumu.

Nilipouliza kuhusu dada yangu, mama Janeth alinijulisha kwamba alikuwa ametoka kwa muda mfupi kurudi nyumbani kufuata baadhi ya vitu na kwamba atarudi hivi karibuni. Aliongeza kwamba dada yangu alikuwa amejitolea sana katika suala hili, akifanya kila liwezekanalo kumsaidia Iryn.

Hali hii ilinifanya niwe na matumaini zaidi, nikijua kwamba familia ilikuwa ikifanya kazi pamoja ili kusaidia Iryn katika kipindi hiki muhimu. Utu wa dada yangu na jitihada zake zilinifanya nihisi kuwa siko peke yangu katika changamoto hii, bali kuna watu wengi waliokuwa tayari kumsaidia na kuhakikisha kuwa Iryn anapata kila kitu anachohitaji. Nilihisi faraja kuona kwamba walikuwa wakijali afya ya Iryn kwa namna ya pekee, na nilimuacha mama aendelee na majukumu yake.

Wakati nimetulia kwenye benchi, Jimmy alinitumia ujumbe kunitaarifu kuwa amefika salama na yuko hotelini. Alisema anapumzika kidogo kabla ya kuja hospitali. Nilihisi furaha kubwa kusikia taarifa hizi kutoka kwake, maana sikuwa na mtu mwingine wa kunipa kampani zaidi yake katika kipindi hiki cha wasiwasi.

Kwa mbali, nilimuona mzee Virgil, baba yake Iryn, akitokea na kuja kwenye upande wangu. Sikuwa na mawazo ya kuonana naye wakati huu, na kwa upande wake, hakutegemea kuniona pia. Alikuwa ameambatana na binti yake mwingine, ambaye ni kama mdogo wa Iryn kupitia kwa mke mdogo.

Baada ya kusalimiana, tulianza mazungumzo ambapo mzee Virgil alisema amefurahi kuniona na alinipa hongera kwa kuwa baba. Aliongeza kwamba amefurahi kumfahamu dada yangu, akisema amekuwa mstari wa mbele sana katika kumsaidia Iryn.

Nilijua kwamba maneno yake yalionyesha kuthamini juhudi za dada yangu, na hilo lilinipa faraja kubwa. Mzee Virgil ni mtu poa sana; katika suala la Iryn, hajawahi kuonesha mtazamo tofauti, na anathamini sana mchango wangu kwa Iryn.

Baada ya mazungumzo ya kina kuhusu Iryn, mzee alinitafutia njia nyingine ya kuzungumza, akileta mada ya maisha na changamoto zake. Pia, alinikaribisha nyumbani kwake, akisisitiza umuhimu wa kukutana na familia yake ili tufahamiane vizuri zaidi. Maneno yake yalionyesha wazi kuwa aliona mbali, akaniambia kuwa mimi tayari ni sehemu ya familia hiyo, na hiyo ilinionyesha jinsi alivyothamini uwepo wangu katika maisha yao.

Saa 2 za usiku, Jimmy alifika hospitali akiwa na Amara (mwanamke aliyezaa naye) pamoja na mtoto wao. Tulisalimiana, na mara moja nilianza mazungumzo na Amara, maana mara ya mwisho nilipokutana naye ilikuwa ni Ethiopia. Wakati huu, mtoto wake alikuwa akicheza kwa furaha na babu yake (Baba Iryn), akimuita "Grandpa," huku sauti yake ikijaza chumba kwa furaha.

Mtoto wa Jimmy ni mzuri sana, ni mtoto ambaye ukimuona, moyo wako utajawa na tamaa ya kumiliki. Mama yake Amara pia ni mzuri, uzuri wake ulijitokeza wazi, na hapo ndipo nikajikuta nikijiuliza, inawezekanaje Jimmy asikubali kum-oa dada huyu?

Licha ya tabia za kihuni za Jimmy, upendo wa Amara kwake ni mkubwa sana, ni anampenda sana Jimmy. Hali hii haijabaki kuwa ya siri, kwani familia yao yote inampenda Amara kwa dhati. Hata Iryn, ambaye mara nyingi anashindwa kuelewa kwanini Jimmy anashikilia mbali ndoa, huwa anatamani sana siku moja aone Jimmy akimuoa Amara, niligusia hili (Season 2: Chapter 10).

Saa 4 za usiku, mama Janeth alikuja na kuniita kwa haraka, uso wake ukiwa na wasiwasi. Aliniambia kwamba Iryn anataka kujifungua na anahitaji uwepo wangu wakati huu muhimu. Niliweza kuhisi uzito wa maneno yake, lakini ndani yangu nilihisi hofu kubwa kuhusu kushuhudia mchakato huu wa kipekee. Ingawa singependa kushiriki katika tukio hili, nilijua kuwa Iryn alihitaji faraja yangu katika wakati wa shida. Kwa hivyo, licha ya woga wangu, sikuweza kukataa.

Movie ilianza mle chumbani, ambapo daktari wawili na wauguzi wawili walikuwa wakifanya maandalizi. Kwa upande wetu, tulikuwa mimi, mama Janeth, na mama yake mdogo, jumla tukiwa saba ndani ya chumba hicho. Hata ingawa sitaki kuzungumzia kwa undani, ninatambua jinsi hali ilikuwa ngumu. Iryn alijifungua salama baada ya mchakato mgumu wa kupush. Walimwongezea njia kwa sababu mtoto alikuwa mkubwa, uzito wa 3.95 kg sio mchezo. Nakumbuka jinsi nilivyohisi uzito wa tukio hilo, nadhani mmeelewa ninachomaanisha.

Baada ya kujifungua, sauti ya mtoto ikaanza kusikika kwa kilio chake. Kila mtu alifurahia kwa dhati, lakini kwa upande wa Iryn, niliona alionesha dalili za kuchoka kupita kiasi na kuishiwa nguvu. Uso wake ulionekana dhaifu, na kwa njia fulani, nilihisi hofu kwamba alikuwa katika hali mbaya zaidi.

Hili lilikuwa ni tukio lenye historia kubwa sana katika maisha yangu. Kwa mara ya kwanza, nilipata nafasi ya kushuhudia moja kwa moja mchakato mzima wa Ariana akiletwa duniani. Tukio hili litabaki kwenye kumbukumbu zangu daima, likionyesha jinsi maisha ya binadamu yanavyoanza.

Kutokana na tukio hili, kila mmoja aliyekuwepo hospitalini alionekana na uso wa furaha. Siku hiyo tulikesha tukipiga stori mbalimbali, kwani hatukuwa tena kwenye wasiwasi wa awali. Kuhusu maendeleo ya Iryn, tuliambiwa kwamba itabidi asubiri kidogo kwa ajili ya uangalizi wa afya yake, lakini kulikuwa na matumaini kwamba siku ya Ijumaa angeweza kuruhusiwa. Hali ilionekana kuwa nzuri, na hiyo ilitufanya tuwe na moyo wa furaha na matumaini.

Asubuhi, mama Janeth alitoka akiwa amembeba mtoto, na alinipa mimi kwanza nimshike, kisha wengine walifuata. Nilifurahi sana kumuona binti yangu Aria; alionekana kuwa kibonge sana, na ngozi yake nyeupe kama mzungu iliongeza uzuri wake.

Baada ya kumshika Aria, nilimpa babu yake, ‘Baba Iryn,’ amshike naye. Babu alifurahi sana kumuona mjukuu wake na alisikika akisema, “Thank God, today I have seen my grandchild before I die.” Kila mtu aliyekuwepo pale alipata nafasi ya kumshika Aria, na furaha ilitawala.

Nilichukua ua langu na kuingia ndani ili kuonana na Iryn. Baada ya kuingia, nilimkuta amelala kitandani huku nurse akimhudumia. Bila kusita, nilimkiss shavuni na kumkabidhi zawadi yake ya ua. Nilivuta kiti, nikaketi, na kuanza kuongea naye. Kwanza kabisa, nilianza kumshukuru kwa kunizalia mtoto mzuri kama yeye. Mazungumzo yetu yalikuwa ya kufurahisha, yakijenga uhusiano wetu zaidi na kuleta tabasamu kwenye nyuso zetu.

Nilimpa maneno matamu sana kiasi kwamba alikuwa akitabasamu tu. Nilimwambia kuwa katika zawadi zote alizowahi kunipa, hii ya mtoto ndiyo zawadi yenye thamani zaidi kwangu. Nilimwambia aniambie anataka nifanye nini kama shukrani yangu kwake, naye alijibu kwamba anataka kuwajua bibi na babu yake Aria. Alionyesha hamu ya kukutana nao, kwani ilikuwa ni fursa nzuri kwake kujenga uhusiano na familia yangu.

Nilimwambia asiwe na shaka juu ya hili na aniachie suala hilo, kwani kila kitu kitakuwa sawa na atafurahi. Wakati tunaongea, baba yake aliingia ndani, na niliona ni vizuri niwapishe waongee, maana mzee alikuwa hajapata nafasi ya kuzungumza na binti yake tangu nilipofika.

Nilikuwa nimechoka sana, hivyo tulishauriana na Jimmy tuondoke hotelini kupumzika, na baadaye turudi tena. Kabla ya kuondoka, nilimuaga dada yangu na kufanya utambulisho ili dada na Jimmy wafahamiane. Jimmy alifurahi sana kumfahamu dada yangu, na dada yangu naye alifurahi kufahamiana na Jimmy.

Baada ya hapo, tuliondoka kwa Uber kuelekea hotelini, na tukiwa njiani, tulikuwa tukizungumza mambo mengi hadi tulipofika. Mazungumzo yetu yalikuwa ya kufurahisha, yakijenga uhusiano wetu na kuongeza furaha ya safari yetu.

Baada ya kufika hotelini, tulikubaliana tuoge kwanza kisha tuonane kwa ajili ya kupata kifungua kinywa. Ndani ya dakika 20, tulionana tena na kukaa kwenye restaurant, tukipata kifungua kinywa huku mazungumzo yetu yakiendelea.

Nilikuwa na hamu ya kujua kwa nini mama yake hajaja kwenye jambo hili muhimu la binti yake, lakini Jimmy alijibu kwamba mama yake alipata dharura ya kikazi na atakuja wiki hii kabla haijaisha.

Kwa upande wangu, nilimuuliza kuhusu mahusiano yake na Amara, na nikamshauri kwa dhati afanye kumwoa yule mwanamke. Nilimwona Amara kuwa ni mtu mzuri na mwenye mvuto wa kipekee. Ingawa, licha ya yote, amemzalia mtoto mzuri, na anaonekana kujielewa sana katika maisha yao. Hata hivyo, maneno haya hayakuwa rahisi kwake kuyakubali, Jimmy alionekana kutopenda kabisa kuyasikia wala kuyazungumzia. Kila nilipomzungumzia suala la ndoa, lilikuwa kama mtihani mzito kwake, lililojaa hofu na wasiwasi.

Baada ya kupata kifungua kinywa, tulikubaliana kupumzika kidogo ili jioni turudi tena hospitalini. Nikiwa chumbani, nilitumia muda huo kuwasiliana na kina Hilda ili kuwataarifu kwamba Iryn kajifungua salama. Pia, nilimcheki Allen na Dullah, nikawapa taarifa hiyo ili wawe na habari sahihi kuhusu hali ya Iryn. Kwa upande wao walifurahi sana kuzisikia taarifa hizi, kwani habari hii iliwafariji na kuwapa matumaini.

Saa 10 jioni, tuliondoka kurudi hospitalini, na kila hatua ya safari ilikuwa inanipeleka kwenye mawazo ya kumuona mwanangu, Aria. Upendo nilionao kwa Aria na mama yake ulikuwa ni wa kipekee, na kwa muda huu, haukuweza kuelezeka kwa maneno. Moyo wangu ulijawa na furaha na matarajio, nikiwa na shauku kubwa ya kuwaona na kuwa nao karibu.

Baada ya kufika hospitalini, nilikutana na Madam Merlinda, ‘academic supervisor wa Iryn’, aliyekuwa amekaa akiongea na Mama Janeth kwenye benchi pale nje. Tulisalimiana, kwa furaha, huku anipongeza kwa kuwa baba. Mama Janeth, wakati wote, alikuwa akishangaa kuona mazungumzo yangu na Madam, kama vile alikuwa akijiuliza ni lini tulikuwa tumefahamiana.

Baadaye, Madam alimweleza jinsi tulivyokutana, na Mama Janeth alibaki akishangaa tu. Madam Merlinda pia aliongeza kuwa alifurahia sana kumuona dada yangu, kwani ndiye alikuwa wa kwanza kukutana naye pindi alivyofika hospitalini.

Niliingia ndani kumuangalia Iryn, na nilimkuta akizungumza na Jimmy. Alionekana kuwa na afya nzuri zaidi, na hali yake ilikuwa inaendelea kuimarika. Aliponiona, uso wake uliangaza kwa tabasamu zuri, tabasamu ambalo lilinihakikishia kuwa alikuwa anapona vizuri. Ile furaha ya kumuona katika hali hiyo ilinigusa sana, na nilihisi amani moyoni, nikijua kuwa mambo yalikuwa yanaenda vizuri kwa mke wangu.

Kaka yake Jimmy alianza kumpa jokes na Iryn alikuwa akitabasamu tu;

JIMMY: “Hatimaye umekuwa mama, ulikuwa unanionea sana wivu mimi kuwa baba watoto."

Iryn alibaki kimya, akimwangalia kaka yake kwa tabasamu la upole, huku Jimmy akiendelea kuzungumza kwa utani.

“Dada yangu, una nguvu sana. Umeweza ku-push kilo 4? Bado siamini! Inaonekana shemeji yangu, Insider, alifanya kazi yake vizuri sana."

Iryn alianza kucheka kwa kugugumia, akiwa na maumivu madogo ya baada ya kujifungua. Hapo ndipo nilipoamua kumzingua Jimmy kwa utani wangu, nikijaribu kupunguza mzaha wake kabla mambo hayajaenda mbali zaidi.

Jimmy, acha tu hiyo, kazi yote ya kilo 4 ilikuwa kwenye team effort,” nilimwambia kwa kicheko, tukizidi kuleta hali ya furaha ndani ya chumba.

Tuliendelea kuzungumza na nesi aliyekuwa akimhudumia Iryn, tukitaka kujua kuhusu muda ambao angeweza kuondoka hospitalini. Nesi alitueleza kwamba maendeleo ya Iryn yalikuwa mazuri na ya kuridhisha, na akatuhakikishia kuwa kesho angeweza kuruhusiwa kwenda nyumbani. Habari hizo zilileta faraja kubwa, tukijua kwamba muda wa kurejea nyumbani na kuanza safari ya maisha mapya na mtoto wetu ulikuwa umekaribia.

Nilikaa muda mrefu pale hospitalini, na kwa mara ya kwanza, niliweza kuzungumza na mama yake mdogo Iryn, kwani mara nyingi tulikuwa tukipishana. Mama yake mdogo ni mwanamke mwenye haiba ya kipekee, mzaliwa wa Afrika Kusini kule kule, na alikuwa na utulivu wa hali ya juu. Katika mazungumzo yetu, hakutoa ishara zozote za hisia za wazi, alikuwa mtulivu na wa kutafakari. Mazungumzo yetu yalikuwa ya kawaida, lakini nilihisi kama alikuwa akinisoma kwa makini, bila kuonesha mengi. Ilikuwa ni mazungumzo yenye hisia za kufahamiana na kuelewana kwa undani zaidi.

Saa 7 za usiku, niliamua kuondoka na Jimmy kurudi hotelini. Bahati nzuri, baada ya kufika, nilikutana na "Nala," yule dada niliyekuwa namtafuta. Lakini cha kushangaza, sikuwa na hisia zozote za kuvutiwa naye kama ilivyokuwa awali. Tangu Iryn ajifungue, nilihisi mabadiliko makubwa ndani yangu. Hisia zangu zilikuwa zimebadilika kabisa, na upendo wangu kwa Iryn na mtoto wetu ulizidi kuwa na nguvu zaidi. Mambo ambayo yalikuwa yananivutia zamani yalionekana kupoteza maana mbele ya furaha mpya ya familia yangu.

Tulisalimiana pale, na alinikumbuka mara moja, aliniambia alikuwa amepata taarifa kuwa nilikuwa namtafuta. Nilimuomba namba yake ya simu, lakini akasema kuwa mazingira ya kazi hayamruhusu kutoa namba yake ya simu. Alieleza kwamba ni kinyume cha utaratibu kutoa mawasiliano binafsi akiwa kazini. Hata hivyo, aliahidi kunitumia namba hiyo kwa njia nyingine, akisema ataiandika kwenye karatasi na kutafuta namna ya kunipatia baadaye. Baada ya mazungumzo hayo, nilimuaga na nikaenda kulala. Uchovu ulikuwa umechukua nafasi, na nilihitaji kupumzika baada ya siku ndefu.
*****

Kesho yake asubuhi, tulipokea taarifa njema kwamba Iryn alikuwa ameruhusiwa kutoka hospitalini. Kwa haraka, tulijiandaa mapema ili tuwahi kufika hospitali kumchukua. Hata hivyo, kichwani mwangu nilikuwa pia na wazo lingine. Nilitamani sana kuonana na dada yangu na kuzungumza naye kwa undani zaidi, kwani hatukuwa kwenye maelewano mazuri kwa muda. Nilihisi umuhimu wa kuweka sawa mambo baina yetu, kurejesha amani na uhusiano wetu wa kifamilia. Ilikuwa ni siku muhimu sana, si tu kwa ajili ya Iryn na mtoto wetu, bali pia kwa kuweka sawa tofauti zangu na dada yangu.

Saa nne asubuhi, tulifika hospitalini na tukakutana na mzee Virgil, ambaye alitusaidia kumchukua binti yake, Iryn, na kumpeleka nyumbani kwake, wengine tulitumia usafiri wa Uber kufika huko. Baada ya kufika kwenye apartment yake, ambayo ilikuwa na vyumba vitatu, ilibainika kuwa nafasi ilikuwa haitoshi kutokana na idadi ya wageni waliokuwepo pale. Kwa hiyo, mimi na Jimmy tulikubaliana kuendelea kulala hotelini ili kutoa nafasi zaidi kwa wengine. Japokuwa tulitamani kukaa karibu na familia, uamuzi huo ulikuwa wa busara ili kuhakikisha kila mtu anapata nafasi ya kupumzika vizuri.

Mara tu baada ya kurudi nyumbani, marafiki zake wa chuo walifika kumtembelea. Walikuwa wakiingia na kutoka mfululizo, wakionesha upendo na shauku ya kumuona Iryn pamoja na kumpongeza kwa kujifungua salama. Kila mmoja alikuwa amekuja na zawadi, na hakika walimletea vitu vingi sana. Ile hali ya furaha ilitanda nyumbani, na zawadi nyingi walizomletea zilijaza kila kona ya apartment, zikionesha jinsi walivyothamini sana uhusiano wao na Iryn.

Kutokana na idadi kubwa ya watu waliokuwa wakiingia na kutoka kumtembelea Iryn, mimi niliamua kutoka nje na kukaa kibarazani ili kupata utulivu. Nikiwa pale, nilikuwa na Samantha, tukipiga story za hapa na pale. Mazungumzo yetu yalikuwa ya kawaida, lakini kwa upande wake, Samantha alionekana kuwa na jambo muhimu la kuniambia. Aliniambia kwa dhati kwamba dada yake, Iryn, ananipenda sana, hivyo nisije kumuumiza dada yake. Maneno hayo yalikuwa na uzito, na kwa muda ule, nilihisi hali ya utulivu na kuthamini zaidi kile kilichopo kati yangu na Iryn.

Jioni, Jimmy alinipatia wazo la kuondoka kwenye maeneo haya na kutafuta sehemu nyingine ambapo tunaweza kupoteza muda. Alisema kwamba nyumbani kumekuwa na wageni wengi, na kwa sisi wanaume, ilikuwa ni kuchoreshana tu bila maana. Niliona kuwa wazo lake lilikuwa zuri, hivyo tukakubaliana kutafuta sehemu tulivu ambapo tungeweza kuzungumza na kufurahia muda wetu bila bughudha.

Kabla ya kuondoka, nilipata wazo kwamba ningekuwa na busara kuonana na dada yangu ili tuzungumze, lakini alionekana kuwa busy sana, hivyo sikupata nafasi. Saa moja usiku, tuliondoka kimyakimya bila kuaga, tukielekea hotelini ili kubadilika kabla ya kutoka.

Nilikuwa sijui tunakoelekea, hivyo ilinibidi kumuliza Jimmy tutaenda wapi. Aliniambia kwamba tungeenda “Soho nightclub.” Jambo hilo lilinivutia, kwani nilijua ilikuwa ni sehemu maarufu ya burudani, kwani nilikuwaga naisikia tu.

Baada ya kujiandaa, tulikutana kwenye restaurant kwa ajili ya kupata dinner kabla ya kuondoka. Muda wote, tulikuwa kimya, hadi Jimmy aliposikika akilalamika kwa mbali, na ndipo tulipoanza mazungumzo.

MIMI: “Bro, what’s wrong?"

JIMMY: “My texts go green."

MIMI: “What do you mean?"

JIMMY: “I was texting my girlfriend, but she is no longer online."

Nilishangazwa kuona Jimmy akihangaika kuwatafuta wanawake wengine, hasa akiwa na Amara.

MIMI: “Bro, how about Amara?”

JIMMY: “Today she will sleep at my sister's house."

Sikutaka kuendeleza mazungumzo haya, kwani nilihisi ilikuwa si sahihi kuzungumzia mambo hayo. Hivyo, nikaamua kumwambia tuondoke, maana tulikuwa tumemaliza kula. Nilijua ni bora tushughulike na mambo mengine ya burudani zaidi usiku huu.

Tuliondoka na Uber kuelekea Soho, na nilipowasili na kushuka, nilianza kushangaa mazingira ya eneo hili pamoja na warembo walikuwa wakiingia, ilikuwa ni balaa. Baada ya kuingia ndani, nilijikuta nikipagawa kabisa, kulikuwa na warembo wa kila rangi na mtindo. Nilijisemea kuwa duniani kuna warembo wakali sana, na nikaona kuwa Dar es Salaam bado kuna safari ndefu kufikia level kama hizi.

JIMMY: “Bro, umepagawa?” Jimmy aliniuliza.

Nilikuwa nikiwa mbali sana kimawazo, kwani kulikuwa na mrembo mmoja aliyevuta kabisa umakini wangu. Nilikuwa nampigia hesabu kichwani, nikijaribu kufikiria jinsi ningekuwa na nafasi ya kuzungumza naye. Jimmy aliona wazi kuwa nilikuwa nimesahaulika, na alijaribu kunikumbusha kuwa nipo kwenye tukio la furaha.

MIMI: “Bro, this place is insane! another reason why men cheat.”

Jimmy alicheka sana kusikia kauli yangu.

JIMMY: “Naona umevutiwa na warembo wa hapa.”

MIMI: “Ni warembo wakali, lakini bado sijaona wa kumzidi Iryn.”

Jimmy alinyamaza kimya, maana hakutegemea kama ningetoa jibu kama hili na aliniangalia kisha akatabasamu.

JIMMY: “Umevutiwa na yule mrembo?”

MIMI: “Yeah! Yuko vizuri sana.”

JIMMY: “Unataka tumuite hapa?”

MIMI: “Kama kaja na mtu wake si tutaanzisha ugomvi hapa?.”

JIMMY: “Mwanamke yoyote utakayemkuta club ni mali yako. Hata siku moja usije kuogopa, mfate akukatalie mwenyewe. Mwanamke anayejitambua hawezi kuingia club kama hizi, kuna maeneo mengi sana ya kwenda.”

Nilinyamaza kwa sekunde, nikitafakari maneno ya Jimmy. Kwa kweli, alikuwa na pointi nzuri, lakini nilifikiria haraka haraka. Kwa nini Jimmy ananiunga mkono kuhusiana na wanawake wengine wakati nimemzalisha dada yake? Iliniuma kuona kwamba hakuwa na huruma yoyote kwake. Nilijua kuwa mahusiano yanaweza kuwa na changamoto, lakini kwa upande wangu, nilihisi kuwa heshima kwa Iryn ilipaswa kuwa ya kwanza.

MIMI: “Bro, I got your sister pregnant, but you're still supporting me in flirting with other women?"

Bro nimemzalisha dada yako, lakini bado unanisapoti nitongoze wanawake wengine?

JIMMY: “Brother, we are men, and the truth is I can't tell you what to do, even if you're in a relationship with my sister. When you're with Iryn, I'll respect you as my brother-in-law, but when you're with me here, I'll treat you as my friend. That's why, back then, when Iryn told me she loves you and that you're a married man, I didn't want to say anything. I just told her that the most important thing is for her to be happy.”

Kaka, sisi ni wanaume, na ukweli ni kwamba siwezi kukwambia nini cha kufanya hata kama uko kwenye mahusiano na dada yangu. Ukiwa na Iryn, nitakuheshimu kama shemeji yangu, lakini ukiwa na mimi hapa hivi, nitakuchukulia kama rafiki yangu. Ndomana, kipindi kile Iryn aliponiambia anakupenda na kwamba wewe ni mume wa mtu, sikutaka kusema lolote. Nilimwambia tu cha muhimu ni awe na furaha."

MIMI: “Bro, really?”

JIMMY: “Just be free when you’re with me, and don’t pretend you’re not a cheater. The most important thing is to make sure you’re very careful, don’t let them know that you cheat on them. Remember, you now have two women, and both of them love you.”

Tulinyamaza kwa dakika kadhaa wakati dada akitufungulia vinywaji vyetu, na baada ya kumaliza kazi yake tulianza kunywa, tukaendelea na maongezi yetu.

MIMI: “I still can’t believe whether Iryn really loves me.”

Jimmy aliniangalia, kisha akaipeleka glass yake ya kinywaji na akaanza kufunguka pale;

Ndugu yangu, naona kuwa hujikubali, lakini nisikilize kwa makini. Wewe ni mmoja wa watu muhimu sana katika maisha ya Iryn, na nakushukuru sana kwa yote uliyofanya kwa dada yangu. Kuna siri nyingi ambazo huenda Iryn bado hajakuambia, lakini leo, nitazungumzia hapa.

Tangu mamdogo afariki (mama Iryn), maisha ya Iryn yalibadilika sana, ni kama alichanganyikiwa na hakuwa katika maelewano mazuri na baba yake. Ukweli ni kwamba, hata familia yetu kwa ujumla haikuwa na maelewano na mzee Virgil kutokana na siri kubwa aliyokuwa ameificha kwa muda mrefu.

Iryn alianza kukutana na Isabella, na hii ilipelekea kutengeneza urafiki wa karibu sana. Unaweza kujiuliza, Isabella ni nani? Ni jirani yetu kule Ethiopia-Bahir, na ni mrembo maarufu sana nchini Ethiopia, pia ni International bi***ch. Huyu ndiye aliyemuingiza Iryn kwenye biashara za massage na kuanza kumpa connection za wateja.

Nilijua Iryn alijiingiza kwenye biashara hizi kupitia Isabella, maana mwenyewe ndiye aliyeniambia, kwani ni Ex wangu. Kwa sababu namjua vizuri Isabella ni nani, nilihofia kwamba dada yangu anaweza kuendeleza tabia kama za Isabella. Hivyo, ilibidi nimpigie simu Iryn na kumuomba tuonane, maana kipindi hicho alikuwa ameenda Ufaransa.

Baada ya kuonana na Iryn, nilimshauri sana aache hizi biashara na aje tusaidiane kuisimamia organization. Hata hivyo, alinikatalia na kuniambia hataki kazi zitakazompa stress, kwani biashara ya massage inamuingizia pesa nyingi sana.

Ingawa yeye alichukulia biashara ya massage kama kazi nyingine, kwa upande wangu, nilichukulia tofauti, niliona ni kazi ya kujiuza tu. Kutokana na suala hili, mimi na Iryn tuligombana sana siku hiyo, na nilimuacha aendelee na maisha yake.

Mwishoni mwa Februari 2021, nilikutana na Iryn nchini Ufaransa, na alikuwa na bwana wake (Griezmann), ambaye alinimtambulisha kwangu. Habari kubwa aliyonambia ilikuwa kuhusu mpango wake wa kurudi Tanzania, kutuliza akili na kufuatilia mafao aliyoacha mama yake.

Nilimshauri afanye hivyo maana ni jambo zuri, ukizingatia kwamba mama yake alifanya yote haya kwa ajili yake. Kabla ya kuondoka kwenda Tanzania, alikuja Bahir na kukaa kwa wiki moja, kisha akaondoka kuelekea Tanzania na alifikia kwa mama Janeth. Licha ya kuja Tanzania, bado aliendelea na biashara zake za massage kwa siri. Sikutaka kumpangia chakufanya kwenye maisha yake, hivyo nilimuacha aamue mwenyewe kuhusu maisha yake.

Mara ya kwanza tulipokutana Dar es Salaam, nilihisi Iryn anakupenda, ingawa alinikatalia kabisa nilipomuuliza. Baada ya miezi miwili, alinipa taarifa kuwa mpo katika mahusiano na ameamua kuacha biashara yake, yote kwa sababu yako. Alisema anakupenda sana na kwamba wewe ni mwanaume wa tofauti sana, hivyo anawaza kukupa zawadi ya mtoto. Kwa upande wangu, nilimwambia afanye maamuzi ambayo anaona ni sahihi kwake, lakini sikujua kama hakukushirikisha kuhusu hili. Hata hivyo, nilikuwa najua mipango yake.

Brother, wewe umechangia sana katika kubadilika kwa Iryn na kumuweka sawa kama zamani. Hata suala la mimba, niliwaambia nyumbani kwamba wewe ndiyo sababu Iryn kuwa na furaha, hivyo tumuache afanye anachoona kwake ni sawa.

Nimekwambia haya yote ili ujue kwamba unathamani kubwa sana kwa Iryn. Upendo na uaminifu wako kwake vimefanya akupende sana na kukuamini. Mimi kama kaka yake, nakushukuru sana na ninakupa heshima yangu. Hata kama utakuja kuachana na dada yangu, bado tutaendelea kuwa pamoja.


Tuliongea mambo mengi sana na Jimmy kuhusu Iryn. Kwa upande wake, alinifungukia vitu vingi, hadi kuhusu lifestyle yake, hivyo nilifahamu mambo mengi kupitia kwake. Alisema ameamua kuniambia haya yote kwa sababu ananiamini sana.

Baadaye, Jimmy alitoka na akarudi na mwanamke mzuri, ambaye alinitambulisha kama girlfriend yake. Tulikaa hadi saa 7 za usiku, na tukashauriana na Jimmy tuondoke maana muda ulikuwa umeenda sana. Tuliondoka kurudi hotelini ambapo Jimmy alikuwa na pisi yake.

Saa tano asubuhi, Jimmy alikuja kunigongea mlango na kunitaarifu kwamba Iryn amepiga simu nyingi na ameanza kumpa lawama kwamba ananifundisha tabia mbaya. Jimmy alisema nijiandae haraka ili tuende kwa Iryn maana anatuhitaji. Nilikuwa nina uchovu sana, hivyo niliingia bafuni kuoga haraka na kujiandaa. Nilipowasha data, nikakuta missed calls nyingi kutoka kwa Iryn na dada yangu, nilihisi huko kuna kitu, nitajua nikifika.

Tuliondoka kwenda nyumbani kwa mama mtoto, na ndani ya muda mfupi tulifika. Baada ya kuingia ndani, nakutana uso kwa uso na mama yake mkubwa, akiwa amemshika mtoto, na tukaanza kuangaliana pale.
 
SEASON 02
CHAPTER 41

“BY INSIDER MAN”

CONTINUE:

Kwa upande wangu, sikutarajia hata kidogo kukutana na mama mkubwa. Niliposogea, nilimsalimia kwa heshima. Alinijibu kwa upole, kisha akaniangalia kwa makini, macho yake yakitua pia kwa Aria aliyekuwa kamshika. Sekunde chache zilivyopita, alinitazama tena na kusema kwa sauti tulivu, “Umefanana sana na mtoto.” Kabla sijapata nafasi ya kujibu, Mama Janeth naye alidakia, akinitazama kwa tabasamu na kusema, “Ni kweli kabisa, mnafanana sana wewe na Aria.”

Niliishia kutabasamu baada ya kusikia maneno yale kutoka kwa mama mkubwa, kisha nikatafuta sehemu ya kuketi. Sebleni palikuwa na wageni wengi sana, hali iliyonifanya nijisikie kutokuwa na utulivu, lakini sikuwa na namna. Nilibaki pale, nikijaribu kuzoea hali ile, huku nikionesha utulivu ambao sikuwa nao ndani yangu.

Baada ya dakika nyingi kupita, niliamua kwenda chumbani kwa Iryn ili kumsalimia na kumjulia hali. Nilipofika, niligundua hakuwa peke yake, alikuwa na wageni wawili. Niliwasalimia wote kwa heshima, na bila kusita, Iryn alinitambulisha kwa marafiki zake akisema, “Hawa ni marafiki zangu, tumesoma nao chuo Ufaransa.”

Nilimuuliza Iryn kuhusu maendeleo ya kidonda chake, na aliniambia kuwa anaendelea vizuri kabisa. Tulipokuwa tunaendelea kuzungumza, ghafla Jimmy aliingia chumbani. Mara tu Iryn alipomuona, uso wake ulibadilika kabisa.

JIMMY: “Hata ukininunia, freshy tu."

IRYN: “Jimmy, nakuchukia sana!"

JIMMY: “Hujaanza leo, na sishangai kabisa.”

IRYN: “Jana ulimpeleka wapi Insider?”

Jimmy alinitazama kwa wasiwasi, akihisi labda nimemueleza Iryn kuhusu tulikokuwa usiku huo. Nilimpa ishara kuwa sina ufahamu wowote juu ya jambo hilo.

JIMMY: “Sawa, tulienda Soho kuburudika, na tulirudi salama."

Iryn, akiwa amekasirika, alitazama pembeni na kuona bakuli karibu yake. Alilichukua kisha akamrushia Jimmy kwa hasira, huku akimfyonza kwa dhihaka.

Na wakati huu, Amara aliingia chumbani na kuanza kuuliza, “Shida ni nini?" Jimmy, kwa haraka, alimnyanyua juu juu na kutoka naye hadi sebleni. Lilikuwa tukio la ghafla na la kufurahisha, kiasi kwamba kila mtu aliishia kucheka, hata wageni.

Niliamua kuondoka chumbani ili kumpa Iryn nafasi na wageni wake. Hata hivyo, wakati nilipokuwa natoka, ghafla nilisikia akiniita kwa sauti ya upole, “Subiri kidogo...”

IRYN: “Darling, where are you going?”

MIMI: “Nipo mke wangu, huna haja ya kuwa na wasiwasi.”

IRYN: “Usije ukanitoroka kama jana ulivyofanya.”

MIMI: “ Leo nipo na wewe baby.”

Baada ya kurudi sebleni, nilitambua kuwa watu watatu hawakuwepo, nao ni dada yangu, Vivian, na Samantha. Nilipouliza, niliambiwa kuwa walitoka kwenda supermarket kununua vitu kwa ajili ya mama mtoto.

Baada ya takriban saa moja, mzee Virgil aliwasili na familia yake yote. Ilikuwa siku ya kipekee kwani niliweza kuwafahamu wadogo zake wote kupitia mama mdogo, kasoro kaka yake ambaye mzee alimzaa na mwanamke mwingine.

Mchana tulikula chakula cha pamoja, ambacho kiliagizwa kutoka kwa wapishi wa nje. Baada ya lunch, mama Janeth alitusalimu na kutuaga, akituambia kwamba anaondoka kwa safari ya kwenda Tanzania, kisha ataendelea na safari yake kwenda Marekani (USA).

Kabla ya mama Janeth kuondoka, tulipata nafasi ya kuzungumza. Nilimshukuru sana kwa kujitoa kwake na kuhakikisha Iryn anajifungua salama. Mama Janeth alinituliza, akisema kwa upole, “Iryn ni binti yangu, huna haja ya kunishukuru kwa hili.”Maneno yake yalikuwa ya faraja, yakiniondolea wasiwasi.

Jioni nilikutana na dada yangu, na tukatafuta sehemu tulivu kwa ajili ya mazungumzo yetu. Mara tu baada ya kuketi, dada alianza kuzungumza kwa hisia, akilalamika kuhusu tabia zangu mpya ambazo nimeanza kuonesha waziwazi mbele ya mama J. Aliuliza kwa upole lakini kwa msisitizo, “Kipindi kile ulipolala nje, ulikuwa wapi?” Akiongeza kwa tahadhari, alisema, “Na kama utathubutu kunidanganya, itakuwa ndio mwisho wa maongezi yetu.” Maneno yake yalikuwa na uzito, yakinifanya nifikirie kwa makini kuhusu majibu yangu.

Niliwaza pale na kuamua ni bora niwe mkweli ili tuweze kumaliza mambo haya.

MIMI: “Nilikuwa na mwanamke mwingine.”

SISTER: “Una matatizo gani? Tuliongea vizuri kabisa kuhusu haya, lakini bado unaendelea kuyafanya. Je, unanidharau mimi dada yako? Nilitegemea utaanza kufocus na watoto wako, lakini unazidi kuhangaika na wanawake wengine?”

MIMI: “Dada yangu, najua nimezingua. Mwanamke huyu alinifata Dodoma mwenyewe, na kipindi kile nilikuwa nimegombana na mama J, na Iryn alikuwa hana dalili za kurudi.”

Majibu yangu yalimfanya dada yangu aonekane mwenye wasiwasi zaidi, lakini pia nilijua ni muhimu kuwa mkweli ili kuweza kuendelea mbele.

SISTER: “Nisikilize kwa makini, bro. Usinione kama mjinga kukusaidia na kesi zako za kila siku ambazo unafanya kwa makusudi. Leo nakupa onyo la mwisho, kama una wanawake nje na hawa mama watoto wako, nikaja kupata kesi, utakuwa umefunga kufuli la mimi kukusaidia.”

MIMI: “Dada yangu, usifike huko, nimekuelewa na sitokuangusha.”

SISTER: “Na kilichofanya uondoke bila kumuaga mama J ni nini? Unaonesha dharau kama hizi kwa mke wako.”

MIMI: “Mimi naondoka tumegombana kwa sababu alimpigia mama yangu simu na kumwambia nililala nje. Niliona ananichonganisha na mama yetu, kwa kitu ambacho hana ushahidi nacho.”

SISTER: “Unataka kuachana na mama J, kisa Iryn?. Ukitaka mambo yako yaanze kuharibika tena, bhasi jichanganye ufanye huo ujinga unaotaka kuufanya, utayakumbuka maneno yangu.”

MIMI: “Siwezi kumuacha mama J, hili nakuapia dada yangu.”

Baada ya kumaliza tofauti zetu, dada aliniahidi kunisaidia kuliweka sawa suala la Iryn. Alinishauri nisubiri mtoto afike miezi sita ndipo nianze hatua za kuwaambia wazazi. Alisema ni bora nianze kumshirikisha mzee, na kisha yeye ndiye atakayemwambia mama. Maneno yake yaliniweka katika hali ya matumaini, kwani nilijua kwamba kwa msaada wake, naweza kupata njia sahihi ya kukabiliana na hali hii.

Dada alinionyesha mbinu ya kuanza kumuandaa kisaikolojia mama J, akisema kwamba nianze kufanya hivi taratibu ili aanze kuhisi mapema kuwa nina mtoto nje. Hata hivyo, nilishindwa kumuelewa alimaanisha nini, hivyo ilibidi nimuulize.

MIMI: “Mbinu gani natakiwa kuanza kuitumia?”

SISTER: “Katika maongezi yenu, unaweza kumuuliza, 'Hivi, ukija kufahamu kuwa nina mtoto nje, utafanyaje?' Inatakiwa uwe unamuuliza mara kwa mara hadi pale atakapozoea na kuona ni jambo la kawaida.”

MIMI: “Dada yangu, sio kwa mama J, hachelewi kulianzisha.”

SISTER: “Hawezi kufanya chochote kwa sababu atakuwa hana ushahidi. Kwa mara ya kwanza atapata shida kadri anavyozidi kusikia kutoka kwako, lakini atazoea na kuona ni jambo la kawaida. Wewe cha kuzingatia ni kuwa unachukua note ya majibu anayotoa, na utakuwa unanitumia.”

Maneno yake yalikuwa na maana, lakini nilihisi bado kuna changamoto kubwa katika kutekeleza mbinu hiyo. Lakini dada alizidi kukazia kwamba mbinu hii itaanza kumuandaa kisaikolojia, na baada ya muda atazoea hali hiyo. Alisisitiza kwamba hata nitakapokuja kumpa taarifa rasmi, haitaleta shida sana na atakuwa na uwezo wa kuelewa vizuri. Maneno yake yalinipa matumaini, kwani niliweza kuona uwezekano wa kumfikia mama J kwa njia ambayo ingekuwa rahisi na ya busara.

Kuhusu suala la kumpa taarifa rasmi, dada alishauri ni bora nisubiri hadi nitakapomalizana na wazee na kila kitu kipo sawa. Alisema kwamba ni hapo ndipo nianze hatua za kumwambia mama J. Dada alinihakikishia kwamba atanisaidia kadri anavyoweza kwa kutumia uwezo wake wote hadi mambo yawe sawa. Maneno yake yalijenga imani ndani yangu, na nilihisi kuwa na msaada wa dada yangu kutanisaidia kukabiliana na changamoto hii.

Baada ya kumaliza maongezi yetu muhimu, dada aliniaga na kuniambia kwamba kesho, Jumapili, ataondoka kurudi Tanzania. Alisisitiza kwamba pindi nitakaporudi Dar es Salaam, nimtaarifu ili aje tuyaweke sawa na mama J.

Nilimuuliza dada kama amelipia tiketi ya ndege, naye akasema kwamba wifi yake, Iryn, alikuwa amelipia tayari na amemwingizia pesa nyingi kwenye akaunti yake, ingawa hakutaka pesa hizo. Dada alifungua app ya benki na kunionesha kiasi ambacho aliingiziwa, na nilibaki nikishangaa.

Mwishoni, dada alinipongeza kwa kuwa baba, akisema kuwa Aria ni damu yetu halali. Maneno yake yalinipa furaha kubwa na kunitia moyo zaidi. Tuliagana kwa kukumbatiana, kisha tukarudi ndani kuendelea na mambo mengine, kwani tulikuwa tumetumia muda mwingi sana kwenye maongezi yetu.

Kibarazani, akina Jimmy walikuwa wanacheza last card, na mimi nilijiunga nao, tukawa jumla wanne: Mimi, Jimmy, Vivian, na Samantha. Mchezo ulikuwa mzuri sana, maana tulianza hadi kuweka hela kwa mshindi, na hali hiyo ilifanya ushindani uwe mkali. Baadaye, dada alikuja na tukawa jumla watano, na mchezo ukawa na ladha mpya, huku kila mmoja akijaribu kushinda kwa njia yake. Kicheko na furaha vilijaza hewa, na ilikuwa ni fursa nzuri ya kuondoa mawazo na kufurahia muda pamoja.

Ninataka niwaambie kuhusu undugu wa Jimmy, Iryn, Vivian, na Samantha. Ninarudisha hadi chapter 9, siku ambayo nilifika Ethiopia kwa mara ya kwanza. Katika siku hiyo, dada watatu walikuja kumpokea Iryn, ambapo alinitambulisha. Yule dada mkubwa ndiye alikuwa Vivian, mtoto wa Pili wa mama mkubwa, huku Jimmy akiwa mtoto wa kwanza akifuatiwa na mdogo wake katika wale wawili waliokuwa wamekuja kumpokea Iryn.

Hawa watatu wa kwanza, Vivian, Jimmy, na mdogo wao, wanatoka kwenye tumbo moja, wakiwa na mama na baba mmoja, ingawa baba yao alishatangulia mbele za haki. Mama mkubwa alizaa watoto wengine wawili na mume mwingine, Samantha na mdogo wake wa mwisho. Huyu mdogo wa mwisho ndiye mmoja kati ya wale dada wawili wadogo ambao Iryn alinifahamisha kama wadogo zake.

Mama mkubwa ana jumla ya watoto watano. Watatu wa kwanza wanashiriki baba mmoja, wakati hawa wawili wa mwisho wanashiriki baba mwingine. Kati ya watoto hao watano, Jimmy pekee ndiye mtoto wa kiume. Kwa Iryn, watoto hawa ni kama binamu zake (cousins), ingawa yeye hupenda kuwaita dada na kaka.


Nilikaa sana pale nyumbani, na hatimaye mimi na Jimmy tuliondoka saa 6 usiku kurudi hotelini. Nilipitia mapokezi kuchukua kadi yangu, na dada wa mapokezi akaniambia kuwa kuna ujumbe wangu. Alinipa kadi na kikaratasi kidogo. Nilielewa kinachoendelea mara moja, na Jimmy aliona yote hayo, akabaki kutabasamu.

Baada ya kuingia chumbani, nilifungua kile kinote na kugundua kuwa ilikuwa ni namba ya simu ya Nala. Niliweka pembeni na kuelekea bafuni kuoga. Baada ya kumaliza kuoga, nilijilaza kitandani, nikiwa nimechoka lakini mawazo yakiwa hayajakaa sawa. Nilianza kuyapitia kwa kina yale mazungumzo yangu na sister, nikitafakari maana yake na mwelekeo wa mambo.

Ukweli ni kwamba, Sister alizungumza mambo mengi sana, lakini kubwa kuliko yote, aliniapia kwamba nikifanya makosa tena, basi atajiondoa kabisa kwenye huu msala, na niachwe nipambane peke yangu. Sister ndiye kiungo muhimu katika kufanikisha hili jambo, hivyo niliona ni busara kutulia na kuwekeza nguvu zangu kwa umakini kwenye familia zangu.

Niliwaza sana kuhusu wazo la kumuacha Mary, lakini kila nilipofikiria, nilijikuta nikipoteza nguvu kwa sababu bado nampenda. Hata hivyo, kutokana na ushauri wa Sister, niliona sina budi kufanya hivyo. Ni bora nimuache mapema kuliko kusubiri na kuleta matatizo makubwa zaidi huko mbeleni.

Niliwaza sana na hatimaye nikaamua kwamba nitakaporudi Dar es Salaam, nitamtafuta Mary ili tuzungumze wazi kuhusu hili suala. Kilichonipa faraja kidogo ni kwamba Mary tayari alikuwa anafahamu kinachoendelea kuhusu mahusiano yangu na Iryn, hivyo nilihisi mazungumzo yetu yangeweza kuwa ya uwazi zaidi.

Jambo lingine lililoanza kunisumbua kichwani ni jinsi wazazi wangu watakavyopokea taarifa za mimi kuzaa na Iryn. Swali kubwa lililozunguka mawazoni mwangu lilikuwa, je, watalichukuliaje suala hili? Nilijua kuwa na mtihani mgumu mbele yangu, lakini kwa sababu Sister aliahidi kunisaidia, nilijisemea kwamba kila kitu kitakuwa sawa. Hata hivyo, sikupuuza uzito wa hali hiyo.

Kwa upande wangu, nilitamani sana kuona Junior na Aria wakifahamiana tangu utotoni ili waweze kujenga uhusiano wa karibu na bond nzuri. Kuhusu hili suala, nilihisi mzee ndiye anayeweza kunipa ushauri mzuri zaidi. Hivyo, nilianza kupata hamasa ya kumtafuta mapema ili tuweze kuzungumza na kupanga namna bora ya kufanikisha hili.
*****

Asubuhi, baada ya kuamka, nilimpigia simu mama J ili kumsalimia, lakini hakupokea, hivyo nilihisi labda alikuwa ameenda kanisani. Niliingia bafuni haraka kuoga na kujiandaa ili tuweze kwenda kwa mama mtoto. Ilikuwa saa mbili asubuhi, na nilihisi muda ulikuwa unayoyoma. Nilimpigia simu Jimmy kumjulisha kuwa tuanze safari, lakini naye hakuwa akipokea. Hatimaye, nikaamua kwenda kumgongea chumbani kwake.

Baada ya kufika kwenye chumba chake, maana yeye alikuwa floor ya juu, niligonga mlango na alitoka kufungua. Alikuwa haja jiandaa, hivyo nilipompa taarifa ya kuondoka, aliniambia nimsubiri ajiandae haraka. Nikamwambia atanikuta kwenye restaurant nikimsubiri.

Nilielekea kwenye restaurant kupata kifungua kinywa, na wakati huo nilikuwa nawasiliana na Iryn, ambaye alikuwa akinisisitizia nianze safari mapema ili niweze kucheza na mtoto. Baada ya nusu saa, nilimuona Jimmy akiwa ameongozana na mwanamke mwenye asili ya kizungu, na nikahisi huenda alikuwa amelala naye. Hali hii iliniacha na maswali mengi kichwani mwangu.

Walipofika, waliketi pamoja nami, na Jimmy alifanya utambulisho wa kawaida, na mimi pia nilimsalimia yule dada. Waliagiza kifungua kinywa, na baada ya kumaliza, tuliondoka kwenye eneo hilo, tukimwacha dada akisubiri usafiri wa kumpeleka kwake.

Wakati tuko kwenye Uber, nilianza kumuuliza Jimmy maswali kuhusu yule mwanamke. Nilikuwa na hamu ya kujua zaidi kuhusu mahusiano yao, na jinsi alivyomjua.

MIMI: “Bro, yule ni nani tena?”

JIMMY: “Tulikutana juzi Soho club, tukabadilishana namba, jana baada ya kuchat naye, nilimpanga aje hotelini akakubali.”

MIMI: “She’s a hoe?”

JIMMY: “I don’t think so, anafanyia kazi kwenye moja ya ubalozi hapa South Africa.”

Nilibaki kimya, nikitafakari kwa undani. Jimmy alikuwa amenishinda kabisa kwa tabia zake. Nilijiuliza mara ngapi ameweza kukutana na wanawake kama yule, na ni wangapi mpaka sasa? Spidi yake ilikuwa ya kutisha, na ilinifanya nishindwe kuelewa vizuri mwelekeo wake. Nilijikuta nawaza kama angeweza kudhibiti hali hii, au kama ilikuwa sehemu ya maisha yake ya kila siku.

Baada ya kuwasili, mazingira yalionekana kuwa kimya na tulivu sana. Tulipofika kibarazani, mtoto wa Jimmy alionekana akicheza peke yake. Jimmy alimnyanyua kwa furaha, kisha tukaingia ndani kuzungumza na mama mtoto ili tupate kujua ratiba ya siku ile.

Pale sebuleni, dada yangu alikuwa amemshika mtoto, na tukaingia kwenye mazungumzo kuhusu safari yake. Alisema anatarajia kuanza safari saa 11 jioni. Wakati huo, Iryn alitoka sebuleni na kuja kukaa pembeni yangu. Alionekana kuzidi kuimarika kadri siku zilivyokuwa zinaenda, jambo lililonipa faraja. Mazungumzo yetu yaliendelea kwa utulivu, na hali ilikuwa ya amani.

Baada ya kula chakula cha mchana, mimi, dada yangu, na mama mkubwa tuliamua kuwa na kikao chetu binafsi. Tulitafuta utulivu nje kwenye bustani, mbali na kelele na muingiliano wa watu wengine. Hapa tuliweza kuzungumza kwa uwazi na utulivu, tukijadili mambo muhimu bila usumbufu wowote. Mazingira yalikuwa tulivu, na kikao kilikuwa na uzito wa kipekee.

Mama alianza kwa kumshukuru sana sister kwa kujitolea kwake kwa kipindi chote hadi Iryn alipojifungua. Sister alisaidia sana, hasa kwenye mazoezi na mbinu mbalimbali za kuhakikisha Iryn anajifungua salama. Kwa kuwa sister yangu tayari alikuwa na watoto wawili, alikuwa na uzoefu mwingi ambao ulimsaidia kumwelekeza Iryn vyema wakati wa ujauzito na hadi wakati wa kujifungua. Mama alionyesha shukrani za dhati kwa mchango wake mkubwa.

Ukiachana na yote, Sister aliweza pia kutengeneza mahusiano mazuri sana na wifi zake, kama Vivian na Samantha. Wote walionekana kumpenda sana dada yangu kwa jinsi alivyojitoa na kujali. Uhusiano wao ulijengeka kwa upendo na uelewa, na hilo lilifanya familia kuwa karibu zaidi.

Kuhusu suala la mimi kumpa mimba binti yake, mama alisema hawezi kusema lolote kwa sababu Iryn mwenyewe alifanya maamuzi yake, na ni mtu mzima ambaye anaelewa vyema anachokifanya. Alionyesha kutambua kwamba Iryn alikuwa na uwezo wa kuchukua maamuzi yake binafsi, na hakutaka kuingilia zaidi. Hii ilileta hali ya unafuu kidogo, ingawa suala hilo bado lilikuwa na uzito wake.

Mama aliniuliza swali ambalo lilikuwa zito kulijibu:

“Una mpango na malengo gani juu ya Iryn?"

Nilihisi uzito wa swali hilo, lakini nilijua dhumuni la mama kuuliza ni nini. Nikajua kwamba ni muhimu kufikiri kwa umakini na kuepuka kutoa ahadi ambazo huenda nisitekeleze. Kwa kutumia busara na tahadhari, nilimjibu hivi:

MIMI: “Asante mama kwa kuniuliza swali hili muhimu. Ninamuheshimu sana Iryn na ninatambua nafasi yake katika maisha yangu. Nimeliona hili suala kwa uzito wake, na ninataka kuhakikisha kwamba mimi na Iryn tunajenga msingi mzuri wa ushirikiano, hasa kwa ajili ya ustawi wa mtoto wetu. Nataka tuchukue mambo hatua kwa hatua, huku tukijadiliana na kupanga vizuri mustakabali wa familia yetu. Ninaendelea kutafakari juu ya mpango mzuri na utakaokuwa bora kwa wote, na nataka kuhakikisha kwamba kila kitu kinawekwa wazi na kwa manufaa ya pande zote mbili.”

Mama na Sister waliniangalia kimya kwa muda, wakitafakari majibu yangu. Mama, hasa, alionekana kutotarajia jibu langu. Niliona machoni mwake kwamba alitarajia kitu tofauti, labda ahadi thabiti au mpango ulio wazi zaidi kuhusu mustakabali wangu na Iryn.

MAMA: “Naona umejibu kwa hekima, lakini bado sijapata uhakika. Wewe na Iryn, mna mpango wa kuwa pamoja au hili ni suala tu la mtoto?”

MIMI: “Naelewa unavyohisi mama, na ni swali lenye uzito. Kwa sasa, mimi na Iryn tunaendelea kuzungumza juu ya mstakabali wetu. Kipaumbele chetu kikubwa ni kuhakikisha mtoto anakua katika mazingira bora, lakini bado tupo kwenye hatua ya kufikiria kwa kina jinsi ya kutatua hali yetu ya kibinafsi. Siwezi kusema kwa hakika wakati huu, ila nataka iwe wazi kwamba sitamtelekeza Iryn wala mtoto wetu.”

MAMA: “Hilo ni jambo jema kusikia, lakini ningependa kuona mnapanga mustakabali wenye utulivu zaidi, hasa kwa ajili ya binti yangu. Matarajio yangu ni kwamba, kama kuna upendo na nia njema, basi mtachukua hatua ya kusonga mbele pamoja.”

MIMI: “Ninakubaliana na wewe kabisa mama, Iryn ni mtu muhimu kwangu na sina mpango wa kufanya maamuzi ya haraka bila kufikiria kila mtu aliyehusika. Ni muhimu kwangu kwamba wote tunakuwa na maelewano mazuri kwa ajili ya mtoto na hatimae, kwa Iryn pia.”

MAMA: “Nashukuru kwa uwazi wako, ningependa tu kuona unachukua hatua thabiti, maana Iryn anastahili uhakika. Si kwamba nakuwekea shinikizo, lakini ningependa kuona binti yangu akiwa kwenye mikono salama.”

MIMI: “Naelewa mama, na ninakuhakikishia kwamba natilia maanani kila kitu unachosema. Nitafanya kila niwezalo kuhakikisha mambo yanaenda vizuri kwa Iryn na mtoto wetu.”

Mama aliniangalia kwa makini, na nilihisi alikua akiwaza, labda akijiuliza, “Huyu jamaa ana akili sana.” Nilijua kuwa niliyajibu maswali yake yote kwa umakini na hekima. Hata dada yangu alionesha tabasamu, akionyesha kushangazwa na jinsi nilivyoweza kujibu maswali ya mama kwa njia ambayo haikuniingiza kwenye mtego.

Mama aliendelea na mazungumzo, akasema angependa kuwajua wazazi wetu, akisisitiza kuwa ni muhimu kwa mustakabali wa mtoto. Aliongeza kwamba sasa sisi tumeshakuwa muunganiko wa familia, na ni muhimu kuimarisha uhusiano huu kwa kuhakikisha kila mmoja anajua historia na asili ya mwingine. Mama alionyesha kuwa na hamu ya kujenga mshikamano ndani ya familia yetu, ili mtoto apate msingi mzuri wa malezi na urithi wa kihisia.

Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, Sister alijiandaa kwa ajili ya safari yake ya kurudi Tanzania. Hali ilikuwa ya huzuni kidogo, lakini pia ya furaha kwa sababu tulikuwa tumepata muda mzuri wa kuzungumza na kujenga uhusiano wetu zaidi.

Saa 9 mchana, Sister alitoka na begi lake na kutuaga pale sebuleni. Tulitoka nje na kupiga picha za pamoja kama kumbukumbu ya wakati wetu mzuri pamoja. Baada ya hapo, mimi na Vivian tulimpa kampani hadi uwanja wa ndege. Safari hiyo ilikuwa ya furaha, ingawa tulihisi huzuni kidogo kwa sababu ya kuachana. Tulizungumza mengi katika gari, tukijadili mipango ya baadaye na sister kuahidi kukutana tena na kina Vivian hivi karibuni.

Tukiwa airport, tulizungumza mambo mengi sana, na Sister aliendelea kunisitiza kwamba nitakaporudi Dar es Salaam, nimpe taarifa ili aje nyumbani kuweka sawa masuala yangu na mama J. Kabla ya kucheck in, aligana na Vivian kwa kukumbatiana kwa upendo, na niliona jinsi walivyokuwa na uhusiano mzuri. Baada ya hapo, tuliondoka maeneo hayo, tukielekea nyumbani, tukiwa njiani story na Vivian ziliendelea na niseme hawa mashem zangu wananikubali na tunapatana sana.

Usiku, niliwasiliana na mama J pamoja na mwanangu Junior. Nilimdanganya kwamba nipo China nikifuatilia mzigo, na baada ya hapo nitatoka kwenda South Africa kumuona Iryn, ambaye amejifungua mtoto. Mama J hakutoa maoni mengi kuhusu hilo, zaidi alisema atawasiliana na Iryn kumpa hongera. Ingawa alionekana kutokuwa sawa na hali hiyo, nilijua ujumbe wangu ulikuwa umemfikia.
*****

Wiki inayofuata, ambayo ilikuwa ni wiki ya kwanza ya mwezi wa 7, idadi ya wageni iliongezeka sana pale kwa Iryn. Ndugu zake kutoka Ethiopia walifika, na pia marafiki zake wa chuo waliosoma pamoja Ufaransa walikuwa wakija na kuondoka. Sebuleni, kila kona ilikuwa imejaa zawadi za mtoto, na hapo ndipo nilipogundua kwa kweli kwamba Iryn alikuwa na mtandao mpana wa watu. Hali hiyo ilionyesha jinsi alivyokuwa akipendwa na kuungwa mkono na watu wengi, na ilifanya moyo wangu ujaze faraja na kujivunia kuwa sehemu ya maisha yake.

Siku ya Jumatano, mama mkubwa aliondoka kurudi Ethiopia ili kuendelea na majukumu yake. Pia, dada wa kazi kutoka Ethiopia alifika nyumbani kusaidia katika kazi mbalimbali. Iryn alieleza kuwa hakutaka dada wa kazi mwenyeji kwa sababu ya tabia zao, hivyo alihitaji mtu ambaye wangeweza kuendana kiutamaduni. Hali hiyo ilionyesha umuhimu wa mazingira yanayofanana na utamaduni wao, na niliona ni busara kwa Iryn kuchagua mtu ambaye angeweza kuleta utulivu na uelewano katika familia.

Siku ya Jumapili, Jimmy pamoja na familia yake waliondoka kurudi Ethiopia, hivyo aliyebaki ni dada Vivian. Baada ya kuondoka kwa Jimmy, nilienda kukaa na Iryn, maana idadi ya watu ilikuwa imepungua, na mle ndani tulikuwa jumla watano. Hali hiyo ilituletea fursa nzuri ya kuzungumza kwa undani zaidi na kujenga uhusiano wetu.

Wiki ya pili ya mwezi wa 7, Jumatatu, bibi yao ‘Momo’ alifika South Africa kumuona kitukuu chake. Aliwasili jioni, na mimi na Samantha tulikwenda kumpokea pale airport. Momo, ambaye sasa ana umri wa miaka 70, ni bibi mwenye uzoefu wa maisha, lakini bado ana nguvu za kujiendesha. Momo ana tabia ya kutabasamu na kuwa na nishati, na nilijua kwamba uwepo wake ungeongeza furaha na umoja katika familia yetu.

Tangu tupo kwenye gari hadi tulipofika nyumbani, Bibi alikuwa na furaha sana na alionyesha hamu kubwa ya kumuona kitukuu wake. Alikuwa akizungumza kwa lugha yao ya nyumbani, lakini Samantha alikuwa ananiambia kila kilichokuwa kinaendelea, akitafsiri maneno ya bibi kwa urahisi. Ilikuwa ni furaha kubwa kusikia shauku ya bibi, na niliweza kuhisi upendo wake wa dhati kwa familia.

Baada ya kufika nyumbani, Iryn hakuwa mbali kumpokea bibi yake, na walikumbatiana kwa furaha na kumkaribisha ndani. Kitu cha kwanza bibi alichomba ni kumuona kitukuu wake, na alifurahi sana baada ya kumuona. Uso wake ulijawa na tabasamu la furaha, na Iryn alionekana pia akifurahia moment hiyo. Nilijua kuwa bibi alikuwa na matumaini makubwa kwa ajili ya kitukuu chake, na nilihisi furaha kuona jinsi familia ilivyokuwa ikijenga uhusiano mzuri katika kizazi tofauti.

Baada ya bibi kurudi nyumbani, mazingira yalichangamka sana, kwani bibi ni mwongeaji sana, na wajukuu zake wanampenda sana. Bibi alisema ataendelea kukaa na Iryn na hafikirii kurudi Ethiopia mapema, jambo lililomfanya Iryn ajisikie vizuri. Iryn ni mjukuu ambaye bibi yake anampenda sana, na hii ni kwa sababu Iryn humjali sana bibi yake, akimpa huduma na kumuhudumia kwa upendo.

Kwa upande wangu, tangu nilipofika South Africa, tayari wiki mbili zilikuwa zimepita, na nilipanga kuondoka Jumapili ya weekend. Niliangalia hali yangu na kugundua kwamba kuendelea kukaa huku kungeweza kuathiri mambo yangu mengi, kuanzia kampuni hadi biashara zangu. Nilijua ni muhimu kurejea nyumbani ili kusimamia masuala yangu na kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa. Ingawa nilifurahia wakati niliokuwa pamoja na Iryn na familia, nilihisi ni lazima nitafute njia ya kuleta uwiano kati ya majukumu yangu ya kifamilia na biashara zangu.

Kesho yake asubuhi, nilimfata Iryn chumbani ili niweze kuzungumza naye kuhusu suala langu la kuondoka. Pembeni yake kulikuwa na diary, hivyo niliichukua na kuanza kuisoma. Niliona alikuwa akiandika mipango yake, na nilicheka baada ya kuona ameandika mpango wa kuanza gym.

Of course, alikuwa ameanza kunenepa sana kutokana na kuwa mama na vyakula anavyokula, lakini bado haikufanya apoteze uzuri na shape yake. Kinyume chake, niliona kuwa mabadiliko hayo yaliongeza mvuto wake, na alikuwa akionekana kuwa na uzuri wa kipekee ambao unakuja na umama.

MAMA ARIA: “Darling, unacheka nini?”

MIMI: “Nimefurahi kuona una mpango wa kuanza Gym, lakini bado mapema sana.”

MAMA ARIA: “I know, baada ya miezi 3 nitaanza mazoezi ya kupunguza huu mwili.”

Nami, nikasogea kukaa pembeni yake;

MIMI: “Nimekumiss baby mama.”

Iryn alianza kuangalia usawa wa bunduki yangu na akanishika kidevu changu na tukaanza kuangaliana pale;

MAMA ARIA: “Are you horny?”

MIMI: “Ofcourse yes.”

MAMA ARIA: “Pole! nadhani unakumbuka siwezi kusex kwasasa hadi nipone vizuri, doctor alishauri baada ya miezi 3, ila mwezi ujao nitaenda kuangalia maendeleo.”

MIMI: “Naelewa usijali, mimi nitavumilia kwa hili.”

Usawa wa matiti yake ulionekana kulowa maziwa, kwani chuchu zake zilikuwa bado zimesimama. Baada ya kumuona vile, ilibidi nimwambie kwamba analowa, akicheka kidogo kwa aibu. Alijua kwamba hali hiyo ni ya kawaida kwa mama anapokuwa katika kipindi hiki, lakini nilijua kwamba ilikuwa ni muhimu kwake kujisikia vizuri kuhusu mwili wake.

MAMA ARIA: “Mwanao hataki kunyonya, halafu mama yake nina maziwa mengi sana. Uwe unamsaidia mwanao kunyonya, kwani naishia kuyakamua na kuyamwaga. Nikupe unyonye? Yatakusaidia kiafya.”

Nilihisi aibu baada ya kusikia haya maneno kutoka kwa Iryn. Aliponigeukia na kunipa ishara ya kunyonya, sikuona sababu ya kukataa, kwani alikuwa anayamwaga. Nilijisemea, si afadhali nikanywa mimi kuliko yamwagwe. Nilianza kuyanyonya taratibu hadi aliposema basi, ndio kuacha na yalikuwa ni matamu sana.

MAMA ARIA: “Vipi matamu?”

MIMI: “Yeah! Aria anafaidi sana.”

MAMA ARIA: “Mwanao mpole kama wewe, naona huyu atarithi tabia zako.”

MIMI: “Bado mtoto, akikua ndio tutajua tabia zake, hata Junior alikuwa mpole kama Aria, ila sasahivi ni balaa.”

Tulipoanza mazungumzo yetu, alizungumzia suala lake la kurudi shule na akaniambia kuwa analiwazia kwa umakini. Nami nikamshirikisha mpango wangu wa kurudi shule mwezi wa kumi, ambapo alinisisitiza kwa upendo kuwa ni vema nisomee masomo yangu ya masters nchini Afrika Kusini ili tuwe karibu na mtoto wetu.

Ingawa wazo hilo lilikuwa zuri, nilijua kuwa kulikuwa na changamoto nyingi zinazoweza kufanya isiwezekane. Hivyo, nilimpatia jibu lililofikiriwa vizuri, ambalo alielewa kwa upole na busara.

Nilimwambia kwa upole,

Baby mama, nikisomea huku, kumbuka kuwa mambo mengi yanaweza kuyumba, kuanzia kampuni yako hadi miradi yangu. Ufuatiliaji wa karibu ni muhimu sana. Acha mimi nisomee Dar ili niwe karibu na biashara zetu. Kuhusu Aria, nitakuwa nakuja mara kwa mara kuwasalimu, siwezi kukaa muda mrefu bila kumuona binti yangu. Kama vile wakati wa ujauzito wako ulivyokuwa ukija Dar es Salaam mara kwa mara, sasa ni zamu yangu kuja Cape Town. Tutaendelea kuwa karibu, hata kama nitakuwa huku.”

Mama Aria alifurahi sana kusikia maneno yangu, na hakuwa na la kusema zaidi. Baadaye, nilimueleza kuhusu mpango wangu wa kuondoka Jumapili. Hata hivyo, kwenye suala la kuondoka, alionekana kulipokea tofauti na aliniomba niondoke mwisho wa mwezi. Nilijaribu kumsihi kwa upole, na kumuomba aniruhusu niondoke wiki ijayo, huku nikiahidi kuwa nitarudi mapema kwa ajili ya sherehe ya "Simchat Bat" ya mtoto wetu.

Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, aliamua kwenda kuoga. Wakati huo, Aria alikuwa ameamka, hivyo nilimbeba na kutoka naye sebleni ili tupate muda wa kukaa pamoja. Sikuwa na shughuli nyingi za kufanya kipindi hicho nikiwa Afrika Kusini, zaidi ya kutumia muda wangu mwingi kucheza na Aria. Sikutoka kwenda sehemu yoyote mara kwa mara, isipokuwa tu kwenda supermarket pale panapohitajika.

Haikupita muda mrefu kabla mama Aria hajarudi kwenye seating room, na kunijulisha kuhusu ujio wa mgeni. Aliniambia kuwa anayekuja ni kaka yake, ambaye ni wa kwanza kwa upande wa mama mwingine. Nilikuwa nimeshaongelea kidogo kuhusu huyu kaka yake, katika Season 1: EP10.

Mchana ule, kaka yake alifika nyumbani kumsalimia Iryn pamoja na mtoto, akiwa ameongozana na mpenzi wake. Hii ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona kaka yake kwa upande wa baba. Ni kijana mwenye haiba fulani ya "manton," kwa mbali anataka kuendana na rappa AKA.

Tulisalimiana pale, kisha tukaingia kwenye mazungumzo ambapo alinikaribisha sana Afrika Kusini kwa ukarimu. Iryn akaanza kumuuliza kaka yake kuhusu maisha na kazi kwa ujumla. Ingawa kaka yake Iryn yuko vizuri kiuchumi, tatizo lake kubwa ni matumizi ya madawa, jambo ambalo limemuharibu sana. Niliwahi kugusia kuhusu hili hapo awali.

Baada ya kupata chakula cha mchana kwa pamoja, kaka yake na mpenzi wake waliondoka. Mama Aria kisha alinipa taarifa nyingine kwamba siku ya Jumamosi tungeenda nyumbani kwa baba yake. Aliongeza kuwa kuna mambo kadhaa watakayokwenda kuyapanga na mzee wake, na akaniambia atanishirikisha katika hayo mazungumzo siku hiyo.

*****

Hatimaye, siku ya Jumamosi ilifika, siku ambayo ilikuwa ni ya kwenda kwa mzee Virgil, baba mkwe wangu. Mzee Virgil alikuwa akija mara kwa mara nyumbani kumuona mjukuu wake, na kitendo cha Iryn kujifungua kilimfurahisha sana. Hakuwa na maswali mengi kuhusu malengo yangu kwa binti yake, wala hakujishughulisha na hilo. Kile kilichomgusa zaidi kilikuwa ni upendo mkubwa aliokuwa nao kwa mjukuu wake. Ilionekana kana kwamba alikuwa akitamani kwa muda mrefu sana kupata mjukuu, na sasa alikuwa akifurahia kila muda aliokuwa naye.

Saa nne asubuhi, gari lilikuja kutuchukua kwa ajili ya safari ya kwenda nyumbani kwa mzee Virgil. Tuliondoka watatu tu, mimi, Iryn, na Samantha. Safari yetu ilikuwa na umbali wa takriban kilomita 45 hadi kufika nyumbani kwa mzee, Somerset West, ambayo iko pembezoni mwa Cape Town. Huu ni sawa na umbali wa kutoka Mwenge hadi Bagamoyo. Njia ilikuwa nzuri, na tulikuwa na mazungumzo mazuri kwenye gari, tukiwa na hamu ya kufika na kumtembelea mzee.

Mzee aliamua kujenga na kuishi nje kidogo ya mji wa Cape Town, na tulivyoanza kuingia katika maeneo haya, nilikuwa nikiona majumba ya kifahari ambayo yalivutia sana macho yangu. Mazingira ya hapa ni kama Ulaya, ni masafi, na kote ni lami, hakuna vumbi. Nyumba zimepangiliwa kwa ustadi wa hali ya juu, mandhari yake ikiwa ya kijani kibichi. Wakati tunaingia Somerset, tulikuwa tukipishana na magari ya kifahari, hali iliyoongeza uzuri wa eneo hili.

Gari lilipaki nje ya geti kubwa, na haikuchukua muda mrefu likafunguliwa, ingawa pale getini hakuonekana mtu yeyote aliyefungua. Tulipofika ndani, gari lilitembea kwa mwendo wa takriban mita 100, na njiani tulipishana na bustani nzuri ya kuvutia.

Baada ya kufika usawa wa nyumba, tulishuka na mbele yangu nikaona bonge la mjengo wa kifahari, aina ya villa. Ilikuwa nyumba kubwa ya kisasa ya ghorofa moja, na kila kipengele chake kilionekana kuwa kimepangwa kwa umaridadi. Ujenzi wa nyumba hiyo ulikuwa wa kisasa na wa kuvutia, ukionyesha ushawishi wa hali ya juu wa usanifu. Ilionekana kama ni mahali pazuri pa kuishi, ambapo mandhari ya karibu iliongeza uzuri na raha ya mazingira.

Wakati huu, mama yake mdogo alitoka kutupokea akiwa na wanae, na haikuchukua muda mzee Virgil akatoka kumkaribisha binti yake. Alikuwa na furaha kubwa sana kutuona na aliomba kumbeba Aria, Mzee Virgil alionyesha upendo mkubwa kwa mjukuu wake.

Nilisikia sauti ya upole kutoka kwa Iryn ikinikaribisha kwa furaha:

“Baba Aria, hapa ndiyo nyumbani, karibu sana.”

Tulipokuwa tunaingia ndani, nilikutana na bonge la msebule uliojaa mapambo ya thamani kubwa kama crystals na marbles. Nimeingia katika nyumba nyingi za kifahari, lakini sebule ya kwa Mzee Virgil ilikuwa ya kipekee kabisa. Ukarabati wa ndani ulikuwa wa kiwango cha juu, na kila kipande cha samani na mapambo kilionyesha umaridadi na mtindo wa kipekee, ikifanya iwe mahali pa kuvutia.

Iryn alianza kunitambulisha kwa wadogo zake wa pale nyumbani kwa upande wa mama mdogo. Mama mdogo ana watoto watatu tu; mtoto wa kwanza ni wa kike, ambaye nilimfahamu nikiwa hospitalini, alikuwa akitarajia kuanza chuo mwaka huo na wawili ni wa kiume, wenye umri wa miaka 13 na 8. Walionekana kufurahia kuniona na walikuwa na shauku ya kujua kuhusu mimi, hali ambayo ilileta maongezi yawe mengi zaidi.

Baada ya lisaa, wageni watano walifika, na kati yao, mmoja tu alikuwa na asili ya Afrika; wengine wote walikuwa wazungu. Kati ya wageni hao, mmoja alikuwa ni babu, na aliomba amshike Aria. Mzee Virgil alifanya utambulisho pale, akimwambia Iryn kwamba wale ni ndugu zake. Iryn alifurahi sana kusikia hivyo, kwani kwa upande wake alikuwa kwenye mission ya kuwasogeza karibu ndugu wote wa upande wa baba yake. Hali hiyo ilileta hisia za umoja na furaha, na ilikuwa ni fursa nzuri kwa familia kukutana na kuimarisha uhusiano wao.

Tulipata chakula cha mchana pamoja, na baada ya wageni kuondoka, Iryn alitoka nje na mzee wake kufanya mazungumzo. Walionekana kuwa na mazungumzo ya karibu na ya kina, hii ilikuwa ni nafasi nzuri kwao kujadili mambo ya familia na kujenga msingi mzuri wa ushirikiano.

Wakati huu, nilikuwa na mama mdogo tukifanya mazungumzo, ambapo aliendelea kunikaribisha kwa ukarimu. Alizungumza kwa upole, akielezea furaha yake kuwa na familia pamoja na jinsi alivyovutiwa na ujio wangu.

Baada ya lisaa, Iryn aliniita nitoke nje ili tuweze kuzungumza na mzee wake. Alimweleza baba yake jinsi ambavyo nimekuwa msaada mkubwa sana katika biashara zake. Mzee wake alishukuru kwa dhati na kusema niendelee kuwa na moyo huo huo. Alionyesha furaha kubwa kwa mimi kuwa sehemu ya familia yake.

Kuhusu suala la kumzalisha binti yake, mzee hakuwa na neno lolote la kukatisha tamaa. Badala yake, alitutakia mafanikio mema na kusema angetamani kuona tukifika mbali zaidi katika maisha yetu.

Mzee aliondoka pamoja na mjukuu wake, na kutuacha mimi na Iryn tukiendelea na mazungumzo yetu. Iryn alianza kunishirikisha kuhusu kazi kubwa aliyonayo katika kuzisimamia kampuni za baba yake. Aliniambia kuhusu mali mbalimbali anazomiliki baba yake hapa Afrika Kusini, ikiwa ni pamoja na apartments, mashamba ya zabibu, na kampuni ambayo ni miongoni mwa waexporter wakubwa wa wines.

Alielezea jinsi alivyohusika katika kusimamia shughuli hizi na jinsi anavyopanga mipango ya kuziendeleza zaidi. Hali hiyo ilionyesha kiwango cha juu cha kujitolea kwake na uelewa wa biashara, na ilinipa mtazamo mzuri kuhusu familia yao na malengo yao ya kifamilia.

Tangu siku ile tulipokutana na Iryn na kuanza mahusiano yetu, hakujawahi kuwa na wakati ambapo alitaja utajiri wa baba yake. Badala yake, alijikita zaidi katika kunieleza kuhusu majukumu aliyokabidhiwa ya kuwa msimamizi wa kampuni za baba yake. (SEASON 1: EP40)

Hii ndiyo siku nilipogundua kwamba mzee Virgil si mtu wa kawaida, kwani ana utajiri wa kutisha. Lakini ukimwona, unaweza kumchukulia kuwa mtu wa kawaida sana. Kama mnavyojua, wazungu hawana tabia ya kujionesha kama wana fedha, tofauti na sisi Waafrika, ambao mara nyingi tunapenda maonyesho ya kifahari.

Iryn aliendelea kunieleza jinsi mzee wake alivyotokea kunikubali sana. Aliniambia kwamba amemshauri atulie nami, kwani kwa sasa wanaume wengi hawaaminiki. Maneno hayo yalikuwa ya faraja kutoka kwa Iryn, yakiwa na uzito wa maana. Nilimuhakikishia kuwa nitajitahidi kumsaidia kadri ya uwezo wangu, kwa sababu uaminifu ni msingi wa mahusiano yetu.

Nilimuuliza Iryn kuhusu mgawanyo wa mali za mzee na jinsi anavyowaangalia watoto wengine, wakiwemo Smith na kaka yake mkubwa, ambapo jumla yao ni watoto sita wa mzee Virgil. Iryn alijibu kwamba hadi sasa, watoto wanne tu wanatambulika rasmi, ambao ni yeye pamoja na wadogo zake watatu kwa upande wa mamdogo. Aliongeza kuwa kuhusu kaka yake na Smith, bado hawajazungumza na mzee wao kuhusu suala hilo, lakini wanatarajia kuangalia namna nyingine ya kufanikisha mambo yao.

MIMI: “Na vipi kuhusu mama mdogo?”

IRYN: “Mama mdogo si mmoja wa mrithi wa hizi mali. Alifunga ndoa ya mkataba na mzee, na moja ya makubaliano ni kwamba hatahusika kwenye urithi wa mali zaidi ya watoto tu.”

MIMI: “Baba yako ni genius sana.”

IRYN: “Mali nyingi sana mzee kazipata akiwa na mama yangu. Ndiyo maana unaona mimi nikiwa kipaumbele cha kwanza, hata wakati ambapo hatuko kwenye maelewano na mzee. Kwa upande wake, alikuwa anapata tabu sana kuhusu hili.”

Iryn alikuwa huru kunifungukia mambo mengi sana. Alisema kwamba hata kitendo cha kuzaa na mimi si kwamba alikurupuka tu kufanya maamuzi hayo, bali alifikiria kuhusu mustakabali wake na mali za baba yake. Alieleza kwamba kipindi kile baada ya kurudi kutoka South Africa kumwona mzee wake, aliona kuna umuhimu wa kuwa na watoto ambao wataweza kurithi mali hizo, kwani hata yeye atakufa.

Iryn alifikiria kwa kina na kugundua kwamba hakuna mtu anayemuamini zaidi yangu kwa sasa. Alijisemea atafanya kila mbinu ili anizalie mtoto, lakini lengo lake kubwa ni kuhakikisha urithi wa mali za baba yake unakuwa salama. Aliendelea kueleza kwamba, mama mkubwa wake na ndugu zake wanamuona kama mjinga sana, lakini hawajui mipango yake ya siri. Hakuwa na nia ya kuona mali ambazo mama yake alizichuma na baba yake zikipotea kwa watoto wengine. Kwa hiyo, alichukua maamuzi haya magumu, lakini yaliyojikita katika manufaa ya kizazi chake.

Nilishusha pumzi ndefu sana, nikijisemea kwamba kumbe Iryn yuko very calculated na alikuwa na mipango mikubwa ambayo sikuwa na habari nayo. Nilikuwa bado siamini kwamba Iryn anaweza kubeba mimba kwa sababu ya kijinga kama aliyokuwa akinambia, lakini leo ndiyo nimeelewa kuwa alikuwa anawaza extra miles. Iryn alikuwa na malengo ya dhati, na sasa nilianza kuelewa uzito wa maamuzi yake.

IRYN: “Baba Aria, naomba nisamehe sana kwa kutokushirikisha hili mapema, nilijua ipo siku ungekuja kujua ukweli. Nilikuwa nauwezo wa kuzaa na mwanaume yoyote yule ninayemtaka hata kwa kumlipa na nikapata mtoto, lakini niliona wewe ndio unafaa.”

MIMI: “Naomba tuachane na haya, Aria ni mtoto wetu tuangalie namna gani ya kumlea na kumtunza ili tuje tujisifu kuwa naye.”

IRYN: “Babu yake kafurahi sana kumuona, ndio mjukuu wake wa kwanza. Pia unakumbuka nilikwambia kuhusu afya ya mzee wangu? Hana maisha marefu sana hapa duniani ni pesa tu zinafanya anaendelea kuishi.”

MIMI: “Nakumbuka baby, naamini ataishi muda mrefu zaidi hapa duniani, tusichoke kumuombea.”

IRYN: “Natamani kupata mtoto mwingine, hata nikiwa natembea barabarani, kushoto nina Aria na kulia nina mdogo wake nakuwa na bodyguards wangu.”

MIMI: “Naona unanipa greenlight ya kukupa mimba ya pili.”

IRYN: “Yes! Why not, unafikiri atakuwa nani zaidi yako?”

MIMI: “Sawa baby subiri kwanza Aria akue mengine tutapanga.”

Baada ya mazungumzo marefu, tulianza kutembea na kutalii mazingira ya nyumba yao. Aisee, nyumba yao imezungukwa na bustani nzuri, huku ukubwa wa kiwanja ukiwa kama ekari tano. Tuliposhuka chini, tulikuta mizabibu mingi imepandwa, kuzunguka upande wa nyuma nakutana na swimming pool mbili, moja ya wakubwa na nyingine kwa ajili ya watoto. Nyumba hiyo ilikuwa na mvuto wa kipekee, na mbele zaidi kulikuwa na nyumba ndogo ya wafanyakazi ambao kazi yao ni kutengeneza zile bustani na kumwagilia mimea.

Nilishindwa kuelewa kwanini Iryn ameshindwa kukaa na baba yake na ameamua kupanga aishi peke yake. Sikutaka kumuuliza kuhusu hili, kwani nilijua Iryn ana akili sana na huwa hafanyi jambo lolote bila sababu. Nilihisi kuwa kuna mambo mengi nyuma ya uamuzi wake, lakini kwa heshima yake, niliona bora nisubiri hadi atakapojisikia kuzungumzia.

Saa mbili usiku, tulipata dinner ya pamoja, na baada ya hapo tuliagana kuwa tunaondoka. Walitusindikiza hadi nje, ambapo dereva alikuwa amekuja kutufuata tayari. Tukiwa pale nje, mzee aliendelea kuongea na binti yake, na nilipata fursa ya kubaini upendo mkubwa sana alionao kwa Iryn. Mazungumzo yao yalionyesha uhusiano wa karibu na wa kipekee kati yao, na ilikuwa wazi kwamba Iryn alikuwa na nafasi maalum katika moyo wa baba yake.

Dereva aliyekuwa amekuja kutufuata ni ameajiriwa na mzee na kazi yake ni kwaajili ya kuwapeleka watoto shule na kuwarudisha, au kuwapeleka matembezini.

*****

Wiki ya tatu, nilipanga kuondoka Cape Town siku ya Ijumaa, nikijitayarisha kurudi Dar es Salaam na kuendelea na ratiba zangu za kila siku. Hata hivyo, nikiwa South sikuwa na kazi yoyote ya kufanya zaidi, nilijikuta nikicheza sana na Aria, kwani hiyo ndiyo ilikuwa shughuli pekee iliyonipa furaha na kunifanya nijisikie hai.

Kwa upande wa Mary, mawasiliano yetu yalikuwa yanaendelea vizuri, na yeye kwa upande wake alionyesha wazi hamu ya kuniona na alitaka anione mapema iwezekanavyo. Alikuwa akiendelea kuniambia kwa kusisitiza ni kwa sababu ya kutamani kuungana tena na mimi, na alilalamika kidogo kuhusu kuchelewa kwangu kurudi.

Siku ya Jumatano, nilitoka na Iryn kwenda kukagua biashara yake ya saloon, ambayo ni kubwa sana na ina wafanyakazi wengi. Iryn alionekana kuguswa sana na hali ya wafanyakazi, akilalamika kuhusu jinsi watoto wa South walivyo wavivu katika kazi zao. Alisema anafikiria kuandaa mpango wa kuajiri watu kutoka nchi za jirani ili kuongeza ufanisi na kuleta mabadiliko chanya katika biashara yake.

Ijumaa usiku, kabla ya safari yangu, nilikuwa na mazungumzo ya mwisho na baby mama yangu. Katika mazungumzo yetu, habari kubwa aliyonipa ilikuwa kuhusu kufuatilia kampuni ya mzee wake, ambayo alidhulumiwa na wabongo. Alionyesha wasiwasi kuhusu jinsi anavyoweza kusaidia katika kurejesha haki na kuleta uwazi katika mambo haya.

Nakumbuka niliwagusia kidogo kuhusu kampuni za ujenzi na umeme ambazo baba yake alikuwa anazimiliki hapa Dar es Salaam, mwanzoni mwa Season 1: EP 10. Baada ya Rais JPM kuingia madarakani mambo yalibadilika kwa kiasi kikubwa, hasa katika masuala ya tenda na kuamua kufunga kampuni na kurejea South ili kuendeleza kampuni zake zingine, huku akikabiliana na changamoto nyingi kutokana na mabadiliko hayo.

Kuna kampuni moja ya masuala ya electronics ambayo baba yake aliiacha, lakini wabongo wazee wa fursa walicheza na umiliki wake. Ingawa mzee wake alionekana kupotezea suala hilo, Iryn alisisitiza kwamba hali hii haiwezekani na alitaka kuchukua hatua dhidi ya watu waliofanya uhuni huo. Alijua kuwa alikuwa na hati zote zinazohitajika, na hivyo alikusudia kudeal na wahusika ili kurejesha haki na kumaliza tatizo hilo.

Iryn alinikabidhi hati zote na kuniagiza nianze kufuatilia suala hili pamoja na mwanasheria. Alinisihi sana kuhakikisha tunafanikiwa katika juhudi hizi. Aliongeza kuwa atarudi Tanzania mwezi Desemba kuangalia maendeleo ya kesi hiyo, na pia tutajadili kuhusu mradi wa kufanya Dodoma. Alionekana kuwa na matumaini kwamba kwa pamoja tunaweza kupata suluhisho na kuendeleza mipango yetu ya baadaye.

Niliingia chumbani kujiandaa, na Iryn alinifuatia kwa nyuma, akinikumbatia huku akizungusha mikono yake mbele yangu. Tulianza kukumbatiana kwa mahaba mazito, na hisia zangu zilianza kuwa na nguvu sana, kwani ilikuwa muda mrefu sijaonja ile furaha. Hali yangu ilizidi kuwa mbaya, nikijua jinsi nilivyokuwa na tamaa ya kuwa karibu naye. Tulianza kupigana makisi ya mwisho mwisho lakini sikuwa na uwezo wa kufanya chochote, sababu ya afya yake. Alichokifanya mama mtoto, alikoki RPG kwa mkono wake laini, hadi pale ambapo risasi za moto zilipotoka kwa kasi.

Nilihisi mabadiliko katika mwili wangu, na nikapata wepesi wa haraka. Tulikwenda kuoga pamoja, na nilijiandaa kwa haraka ili niweze kuongea kidogo na Momo na kumuaga kabisa. Nilitaka kuhakikisha kuwa kila kitu kiko sawa kabla ya kuondoka.

Nilimshukuru Momo kwa uwepo wake nyumbani, kwani alikuwa anatusaidia sana kucheza na mtoto. Nilimuaga kwa kumkiss shavuni, na kisha tukaanza safari yetu kwenda airport. Niliongozana na Iryn pamoja na Samantha, ambao walinipa kampani na njiani tulikuwa tunapiga story za mwisho.

Baada ya kufika uwanja wa ndege, niliagana na mama Aria, kwani sikutaka aanze kunisubiri hadi nimalize mchakato wa kucheck-in. Sikuona haja ya wao kufanya hivyo. Nilianza kwa kumkumbatia Samantha, na nikamalizia kwa kumkumbatia mama mtoto. Cha ajabu, alinionyesha upendo kwa kunipa na ulimi, na hiyo ilileta hisia mpya za mshangao na furaha.

Saa 7 usiku, safari yangu ya kurudi Dar es Salaam ilianza, na njiani kote nilikuwa na furaha sana. Nikiwa kwenye ndege, mawazo yangu yalizunguka kuhusiana na watoto wangu, Junior na Aria. Nilitamani sana kuona wanangu wakianza kujuana mapema na kutembeleana, kwani ni damu zangu. Nikaona kuna umuhimu wa kumtafuta mzee wangu na kumshirikisha kuhusu jambo hili mapema ili kila kitu kiwe wazi. Nilijisemea, "I'm running out of time; let me do this." Hali hiyo ilinipa msukumo wa kutenda haraka ili kuhakikisha familia yangu inakuwa na muungano mzuri.

THE END OF SEASON 2

Thank you for your time!
 
SEASON 02
CHAPTER 40

“TRUE STORY BY INSIDER MAN”

PREVIOUS:
Baada ya kuwasili pale JNIA, tulikaa na kuendelea na mazungumzo. Nilimsihi sana Hilda aisimamie kampuni vizuri hadi nitakaporudi, nikijua kuwa ilikuwa muhimu kwa ajili ya usimamizi mzuri. Baada ya dakika 20, tuliagana kwa kukumbatiana, nami nikacheck-in kwa ajili ya kuanza safari yangu kuelekea South Africa, nilijua ni mwanzo wa safari muhimu na nilikuwa na matumaini makubwa.

CONTINUE:

Nikiwa kwenye harakati za kukamilisha taratibu kabla ya safari, simu ya Mary iliingia, na bila kusita niliipokea. Katika mazungumzo, nilikumbuka kuwa sikuwa nimemjulisha rasmi kwamba naondoka kwenda Afrika Kusini, ingawa tayari nilikuwa nishamgusia kuhusu safari hii. Nilipompa taarifa kamili, Mary hakuweza kuzichukua kwa urahisi. Alionyesha hisia kali na kunilalamikia kwa kuondoka bila kumuaga rasmi, jambo ambalo halikumfurahisha hata kidogo.

Nilimkumbusha kwamba tayari nilishamgusia kuhusu safari hii, lakini bado hakutaka kuelewa. Alisisitiza kuwa nilipaswa kumjulisha mapema zaidi, na sio kusubiri mpaka anipigie simu ndipo nimpe taarifa hizi. Hasira zake ziliongezeka, na hatimaye alikata simu ghafla. Kwa upande wangu, sikuona haja ya kuendelea kumfikiria, kwani niliona anachukulia jambo hili kwa namna ya kitoto. Niliamua kuacha nifikirie mambo muhimu zaidi na kuendelea na safari yangu.

Safari ya kuelekea Afrika Kusini ilianza vizuri, na nilibahatika kupata siti ya upande wa dirishani. Pembeni yangu aliketi binti Mtanzania, aliyenipa tabasamu la salamu tulipokutana macho. Ingawa tulisalimiana kwa heshima, sikuwa na hamu ya kuendelea na mazungumzo. Mawazo yangu yalikuwa mbali sana, nikitafakari kwa kina juu ya hatima ya maisha yangu na mustakabali wangu baada ya safari hii. Nilihisi kama nilikuwa kwenye hatua ya mabadiliko, na kila kitu kingine kilionekana kama kelele zisizo na maana wakati huo.

Nilipokuwa nikitazama anga za mbali kupitia dirisha la ndege, matumaini yangu ya kuwa baba wa watoto wawili yalijaa ndani yangu. Niliamini kwa dhati kuwa Iryn angejifungua salama, na hilo lilinipa faraja. Hata hivyo, mawazo yangu yalivutwa kwa nguvu kuelekea mahusiano yangu na Mary. Maneno ya Jane yalinirudia kichwani, na kadri nilivyoyatafakari, niliona alikuwa sahihi. Ikiwa mahusiano yangu na Mary yangekuja kufahamika kwenye familia yake, ningekabiliwa na shida kubwa. Hili lilikuwa jambo lililonitatiza sana.

Kilichonifanya nisijisikie vizuri zaidi ni kwamba, licha ya kuelewa athari za uhusiano huu, nilikuwa kwenye dilema kali kuhusu hatua sahihi ya kuchukua. Nilijua kwamba kumuacha Mary kungekuwa ngumu, na wakati huo huo, kuendelea naye kulionekana kama kuzidisha tatizo. Mawazo yangu yalikuwa magumu sana, nikikosa maamuzi ya busara kuhusu mustakabali wa uhusiano wetu.

Kadri safari ilivyoendelea, nilijikuta nikitafakari zaidi kuhusu maisha yangu tangu nilipoanza biashara za Uber. Kipindi hicho kilikuwa mwanzo wa mabadiliko makubwa, ambapo nilikutana na watu wengi sana ambao kwa njia moja au nyingine wamekuwa msaada mkubwa katika safari yangu ya kimaisha. Nilipitia mengi mazuri na magumu, na kila tukio lilionekana kuwa na nafasi yake maalum katika hadithi ya maisha yangu. Nilihisi kama maisha yangu yalikuwa kama filamu, yenye mlolongo wa matukio ya kipekee.

Kutokana na hayo, wazo moja lilianza kuota mizizi, kuandika kitabu. Kitabu ambacho kingekuwa ukumbusho wa safari yangu, changamoto nilizokutana nazo, mafanikio niliyoyapata, na watu waliokuja na kuondoka. Hili lilionekana kuwa jambo la maana, sio tu kwa ajili yangu binafsi, bali pia kwa wengine, ili waweze kujifunza kutokana na yale niliyoyapitia kwa muda mfupi sana lakini yenye uzito mkubwa.

Tulipowasili Johannesburg, tulipewa muda wa mapumziko wa takriban saa moja kabla ya kubadilisha ndege ya kuelekea Cape Town. Nikiwa nimechoka kidogo lakini bado nikiwa na ari ya kufika, nilitumia muda huo vizuri kufanya booking ya hoteli. Nilichagua hoteli ileile ambayo mimi na dada yangu tulifikia safari iliyopita, Southern Sun Newlands Hotel.

Baada ya lisaa na dakika kadhaa, tulianza safari yetu ya kwenda Cape Town. Ndege iliondoka Johannesburg saa mbili asubuhi, na tulifika Cape Town majira ya saa tano asubuhi. Nilipomaliza taratibu za uhamiaji na kuchukua mizigo, nilichukua tax moja kwa moja kuelekea kwenye hoteli niliyokuwa nimefanya booking.

Nilipowasili hotelini, jambo la kwanza kabisa nilifanya ni kuoga ili kuondoa uchovu wa safari. Baada ya hapo, niliamua kutoka kwenda kupata chakula kwani nilikuwa na njaa kubwa. Nilipokuwa nikila, nilikuwa pia nawasiliana na sister, ambaye aliniongoza kuhusu hospitali walikokuwa. Aliniambia kuwa nikianza kuondoka niwajulishe ili tuweze kukutana. Mawasiliano hayo yalifanya nianze kujiandaa kisaikolojia kwa hatua zinazofuata.

Nilipokuwa hotelini, mawazo yangu yalirudi nyuma, nikamkumbuka yule dada niliyempa pesa kipindi kile nilipoondoka na dada yangu hapa hotelini. Hali hiyo ilinifanya nianze kuhisi tamaa, hisia zangu zikielekea kwake. Nilikuwa nalikumbuka jina lake vizuri, hivyo nilichukua hatua ya kumuuliza mhudumu mmoja wa hoteli kuhusu yule dada. Alinijibu kwa ufupi kuwa ataingia shift ya jioni.

Sasa, baada ya kupata taarifa hizo, nilihisi msukumo wa kutaka kuomba namba yake ya simu, lakini nikaamua kujizuia. Niliona ni busara zaidi kuwa mpole na kuacha mambo yaende kwa utaratibu wake, kwani nilijua tutaonana hivyo, niliamua kusubiri kwa utulivu.

Kipindi nikiwa hapa na sister, ukweli ni kwamba nilivutiwa sana na yule dada mhudumu, lakini nilijizuia kwa heshima ya sister. Nilijua wakati ule haikuwa sahihi kuchukua hatua yoyote zaidi ya mazungumzo ya kawaida. Lakini moyoni nilihisi kwamba siku moja nitarudi tena Afrika Kusini, na nitaishia kufikia hoteli hii, ambapo nitapata fursa ya kumuona tena. Hata ile hatua ya kumpa pesa haikuwa tu msaada wa kawaida, nilikuwa najenga mazingira mapema kwa ajili ya kupata "mzigo" bila vikwazo hapo mbeleni.

Nilihisi tamaa kubwa ya kupiga game la mwisho kabla ya Iryn kujifungua, kwa sababu ya heshima na umuhimu wa mtoto ambaye alikuwa njiani kuja. Nilijua kuwa pindi Iryn atakapojifungua, singeweza tena kupiga game mpaka nitakaporudi Tanzania, na wakati huo nisingejua nitatumia muda gani huku Afrika Kusini. Hali hii ilifanya hisia zangu kuwa za ndani zaidi, kwani nilijua kuwa na mabadiliko makubwa yanakuja, na ningeweza kupoteza fursa za kufanya mambo niliyoyapenda.

Wakati nikiwa na mawazo yangu, Jimmy alinitafuta kupitia WhatsApp na kunijulisha kwamba yuko njiani anakuja. Nilimjibu kwa kumwambia niliko, pamoja na hoteli niliyofikia. Alifurahishwa na taarifa hiyo na kusema kwamba naye atafikia hoteli hii. Jimmy aliomba niweze kumfanyia booking ya chumba mapema ili asije kukosa nafasi. Niliamua kumsaidia na kuanza kupanga jinsi ya kumtafutia chumba, huku nikijua kuwa uwepo wake jirani ungekuwa muhimu kwangu.

Saa 8 mchana, niliondoka kuelekea hospitali, nikiwa nimetumia usafiri wa Uber. Dereva aliyekuja kunichukua alikuwa ni choko, na njiani alinitafutia mazungumzo mengi ambayo yalinisababisha kuhisi kero. Nilijua niko katika nchi ya watu na sikutaka kuonesha tabia yoyote isiyofaa. Hivyo, nilimjibu maswali yake kwa ustaarabu, lakini moyoni nilikuwa nikiomba tu kufika hospitali mapema. Katika maisha yangu ninaaminu kwamba kukutana na watu hawa kunaweza kuwa kama mikosi kwangu.

Umbali kutoka hotelini hadi Mediclinic hospital ni kama kilomita 15, sawa na kutoka Mwenge hadi Kivukoni, na nilijua Iryn hakuwa akiishi mbali sana na chuo anachosoma wala hoteli niliyofikia. Nilipokaribia hospitali, shauku yangu ilikuwa kubwa sana, nikitamani kwa dhati kumuona Iryn.

Mara baada ya kufika, nilimkuta sister akiwa ananisubiri pamoja na Samantha pale nje. Tulipokutana, tulisalimiana, lakini niliona wazi kwamba sister hakuwa sawa. Hisia zangu zikanifanya nishuku kuwa huenda ilikuwa ni kuhusu lile suala la mama J. Nilihisi kwamba sister bado alikuwa na mawazo mengi kichwani mwake. Sikutaka kumuuliza sana kuhusu hilo, kwani nilikuwa na hamu ya kuzungumza na Samantha, ambaye hatukuweza kukutana kwa muda mrefu. Hivyo, nilijaribu kuelekeza mazungumzo yangu kwake, nikifurahia kuungana tena na shem wangu.

Tulipoingia ndani ya hospitali, tulielekea moja kwa moja hadi wodi aliyokuwa amelazwa Iryn. Nilipofungua mlango na kuingia ndani ya chumba, jambo la kwanza lililoshika macho yangu lilikuwa ni Vivian, aliyekuwa amesimama pembeni akizungumza na daktari, kana kwamba alikuwa akipokea maelekezo muhimu. Lakini hata hivyo, macho yangu yote yalivutwa kwa Iryn.

Alikuwa amelala kitandani, akiwa uchi, na jasho likimtoka kwa wingi, ishara ya uchovu wa mwili uliomlemea. Mwili wake ulionekana dhaifu sana, hali ambayo ilinipatia hisia za huruma kali. Nywele zake ndefu na nzuri zilikuwa zimetifuka, zikionesha uchovu aliokuwa nao. Matiti yake yalionekana kuvimba, na mwili wake wote ulionekana kubadilika kwa kiasi kikubwa.

Iryn alikuwa akihema kwa shida, kila pumzi ikionekana kuwa mzigo kwake. Hali yake ilinishtua, nikitambua kuwa huu ulikuwa wakati mgumu sana kwake. Hisia za huzuni na wasiwasi zilijaa ndani yangu, huku nikijua kwamba nilihitaji kuwa na nguvu kwa ajili yake katika kipindi hiki kigumu.

Wasiwasi wangu ulianza kuongezeka mara moja, nikijiuliza kama hali yake ni mbaya zaidi ya nilivyofikiria. Nilimwona akiugua kimya kimya, na moyo wangu ulianza kushuka, nikihisi uzito wa hali hii. Sikujua nini kingetokea, lakini nilihisi kwamba sasa kila kitu kilikuwa nje ya uwezo wangu, na yote niliyoweza kufanya ni kumwombea awe salama.

Nilisogea karibu na kitanda cha Iryn, nikamshika shavu lake kwa upole, na mara moja nilihisi joto lake lilikuwa limepanda. Japo mwili wake ulikuwa dhaifu, niliweza kugundua alifurahi kuniona, ingawa hakuwa na nguvu za kuonyesha ile furaha waziwazi. Lakini kwa namna fulani, niliweza kuhisi furaha yake ndani ya hali ile ngumu aliyokuwa nayo.

Nikiwa nimemshika mkono, nilijikuta nikilegea kando yake, nikamshika tumbo lake kwa upole na kwa sauti ya faraja nikamwambia, “You will be alright, my love."

Alinitazama kwa macho yenye uchovu lakini yenye matumaini, na kwa upole akatikisa kichwa chake, akionyesha kukubaliana nami. Huo ulikuwa ni wakati wa kimya, lakini pia wa utulivu.

Nilipoanza kuzungumza na kina Sister kuhusu maendeleo ya Iryn, walinifahamisha kuwa njia ya mtoto bado haijafunguka, lakini kuna matumaini ya kujifungua salama kwa njia ya kawaida (Normal Vaginal Delivery). Pia waliongeza kuwa, kama hali hiyo itaendelea na njia ya uzazi itaendelea kusumbua, basi madaktari watalazimika kumfanyia upasuaji (OP) ili kuinusuru afya ya Iryn pamoja na mtoto.

Ingawa taarifa hizo zilikuwa na changamoto, kulikuwa na faraja katika kujua kwamba walikuwa tayari kuchukua hatua sahihi kwa kuhakikisha usalama wa Iryn na mtoto. Hali hii ilinipa matumaini ya kumalizika kwa hali hii kwa usalama.

Madaktari na wauguzi walikuwa wakiingia na kutoka ndani ya chumba, wakionekana kuwa na shughuli nyingi sana, wakihangaika kuhakikisha kila kitu kipo sawa. Hali ile ya harakati na uzito wa mazingira ilinifanya nishindwe kuvumilia kukaa ndani kwa muda mrefu. Nilitambua kuwa ni bora niwapishe waendelee na kazi zao bila usumbufu wowote, hivyo nikaamua kutoka nje ili kupata hewa na kutuliza mawazo yangu, huku nikisubiri kwa matumaini kila kitu kitakwenda sawa.

Pale nje, kwenye benchi, Samantha alikuwa amekaa akisubiri kwa utulivu, maana hakuwa ameruhusiwa kuingia ndani kwa sababu ya hali ya dada yake, Iryn, ambaye alikuwa kwenye mazingira ya faragha. Isingekuwa busara, wala heshima, kwa Samantha kumuona dada yake katika hali ile ya udhaifu.

Nikiwa nimekaa naye, tulianza kuzungumza kwa upole, huku mawazo yangu yakiendelea kuzunguka hali ya Iryn. Katika mazungumzo, nilimwambia Samantha kuwa tungehitaji kwenda shopping ili kununua baadhi ya vitu vya mtoto. Samantha alinijibu kuwa wao tayari walikuwa wamenunua kila kitu kinachohitajika, lakini nikamwambia kwamba safari hiyo ilikuwa muhimu kwa upande wangu, nilihitaji kununua vitu kwa ajili ya mtoto wetu.

Wakati tunaendelea kuzungumza, mama yake mdogo wa Iryn, ambaye ni mke wa baba yake, alifika na kutusalimia kabla ya kuingia ndani. Nilipomwona, nilihisi kama nimemfananisha na mtu niliyewahi kumuona mahali fulani, lakini sikuweza kukumbuka wapi. Samantha aliniambia kuwa huyo ni mama mdogo wa Iryn, na hapo ndipo nikakumbuka kwamba nilimwona kwenye picha kupitia simu ya Iryn.

Baada ya dakika 20, Vivian alitoka ndani, na tulikubaliana kuondoka kuelekea moja ya shopping mall ili kununua vitu vya mtoto. Safari yetu ilianza kwa furaha, na tulitumia takribani masaa mawili kufanya manunuzi ya vitu mbalimbali muhimu, ikiwa ni pamoja na mavazi, toys, na vitu vingine vingi.

Tulikuwa na mazungumzo mazuri huku tukichagua bidhaa, na kila bidhaa tuliyoinunua iliongeza hisia zetu za furaha na matarajio. Baada ya kumaliza manunuzi, tukarudi tena hospitali, tukijua kuwa vitu hivi vitakuwa na umuhimu mkubwa kwa Iryn na mtoto. Moyo wangu ulijaa matumaini na furaha, nikihisi kwamba nilikuwa nikichangia kwa njia fulani katika maisha ya familia yetu mpya.

Baada ya kufika hospitali, bila kutegemea, nilikutana na mama Janeth. Baada ya kusalimiana, aliniambia kwamba alikuwa pale tangu asubuhi, lakini alikuwa ameenda sehemu fulani kwa muda mfupi. Mama Janeth alionekana kufurahia sana kuniona, na alisema alifurahi pia kumuona dada yangu.

Aliniondoa wasiwasi wote kuhusu afya ya Iryn, akisema niondoe hofu, kwani aliamini Iryn atajifungua salama. Maneno yake yalinipa faraja kubwa, na nilihisi kama mzigo mzito ulishuka kutoka kwenye bega langu. Utu wake na uhakikisho wake vilinipa nguvu na matumaini zaidi, nikijua kwamba nilikuwa na watu wa kutegemea katika kipindi hiki kigumu.

Nilipouliza kuhusu dada yangu, mama Janeth alinijulisha kwamba alikuwa ametoka kwa muda mfupi kurudi nyumbani kufuata baadhi ya vitu na kwamba atarudi hivi karibuni. Aliongeza kwamba dada yangu alikuwa amejitolea sana katika suala hili, akifanya kila liwezekanalo kumsaidia Iryn.

Hali hii ilinifanya niwe na matumaini zaidi, nikijua kwamba familia ilikuwa ikifanya kazi pamoja ili kusaidia Iryn katika kipindi hiki muhimu. Utu wa dada yangu na jitihada zake zilinifanya nihisi kuwa siko peke yangu katika changamoto hii, bali kuna watu wengi waliokuwa tayari kumsaidia na kuhakikisha kuwa Iryn anapata kila kitu anachohitaji. Nilihisi faraja kuona kwamba walikuwa wakijali afya ya Iryn kwa namna ya pekee, na nilimuacha mama aendelee na majukumu yake.

Wakati nimetulia kwenye benchi, Jimmy alinitumia ujumbe kunitaarifu kuwa amefika salama na yuko hotelini. Alisema anapumzika kidogo kabla ya kuja hospitali. Nilihisi furaha kubwa kusikia taarifa hizi kutoka kwake, maana sikuwa na mtu mwingine wa kunipa kampani zaidi yake katika kipindi hiki cha wasiwasi.

Kwa mbali, nilimuona mzee Virgil, baba yake Iryn, akitokea na kuja kwenye upande wangu. Sikuwa na mawazo ya kuonana naye wakati huu, na kwa upande wake, hakutegemea kuniona pia. Alikuwa ameambatana na binti yake mwingine, ambaye ni kama mdogo wa Iryn kupitia kwa mke mdogo.

Baada ya kusalimiana, tulianza mazungumzo ambapo mzee Virgil alisema amefurahi kuniona na alinipa hongera kwa kuwa baba. Aliongeza kwamba amefurahi kumfahamu dada yangu, akisema amekuwa mstari wa mbele sana katika kumsaidia Iryn.

Nilijua kwamba maneno yake yalionyesha kuthamini juhudi za dada yangu, na hilo lilinipa faraja kubwa. Mzee Virgil ni mtu poa sana; katika suala la Iryn, hajawahi kuonesha mtazamo tofauti, na anathamini sana mchango wangu kwa Iryn.

Baada ya mazungumzo ya kina kuhusu Iryn, mzee alinitafutia njia nyingine ya kuzungumza, akileta mada ya maisha na changamoto zake. Pia, alinikaribisha nyumbani kwake, akisisitiza umuhimu wa kukutana na familia yake ili tufahamiane vizuri zaidi. Maneno yake yalionyesha wazi kuwa aliona mbali, akaniambia kuwa mimi tayari ni sehemu ya familia hiyo, na hiyo ilinionyesha jinsi alivyothamini uwepo wangu katika maisha yao.

Saa 2 za usiku, Jimmy alifika hospitali akiwa na Amara (mwanamke aliyezaa naye) pamoja na mtoto wao. Tulisalimiana, na mara moja nilianza mazungumzo na Amara, maana mara ya mwisho nilipokutana naye ilikuwa ni Ethiopia. Wakati huu, mtoto wake alikuwa akicheza kwa furaha na babu yake (Baba Iryn), akimuita "Grandpa," huku sauti yake ikijaza chumba kwa furaha.

Mtoto wa Jimmy ni mzuri sana, ni mtoto ambaye ukimuona, moyo wako utajawa na tamaa ya kumiliki. Mama yake Amara pia ni mzuri, uzuri wake ulijitokeza wazi, na hapo ndipo nikajikuta nikijiuliza, inawezekanaje Jimmy asikubali kum-oa dada huyu?

Licha ya tabia za kihuni za Jimmy, upendo wa Amara kwake ni mkubwa sana, ni anampenda sana Jimmy. Hali hii haijabaki kuwa ya siri, kwani familia yao yote inampenda Amara kwa dhati. Hata Iryn, ambaye mara nyingi anashindwa kuelewa kwanini Jimmy anashikilia mbali ndoa, huwa anatamani sana siku moja aone Jimmy akimuoa Amara, niligusia hili (Season 2: Chapter 10).

Saa 4 za usiku, mama Janeth alikuja na kuniita kwa haraka, uso wake ukiwa na wasiwasi. Aliniambia kwamba Iryn anataka kujifungua na anahitaji uwepo wangu wakati huu muhimu. Niliweza kuhisi uzito wa maneno yake, lakini ndani yangu nilihisi hofu kubwa kuhusu kushuhudia mchakato huu wa kipekee. Ingawa singependa kushiriki katika tukio hili, nilijua kuwa Iryn alihitaji faraja yangu katika wakati wa shida. Kwa hivyo, licha ya woga wangu, sikuweza kukataa.

Movie ilianza mle chumbani, ambapo daktari wawili na wauguzi wawili walikuwa wakifanya maandalizi. Kwa upande wetu, tulikuwa mimi, mama Janeth, na mama yake mdogo, jumla tukiwa saba ndani ya chumba hicho. Hata ingawa sitaki kuzungumzia kwa undani, ninatambua jinsi hali ilikuwa ngumu. Iryn alijifungua salama baada ya mchakato mgumu wa kupush. Walimwongezea njia kwa sababu mtoto alikuwa mkubwa, uzito wa 3.95 kg sio mchezo. Nakumbuka jinsi nilivyohisi uzito wa tukio hilo, nadhani mmeelewa ninachomaanisha.

Baada ya kujifungua, sauti ya mtoto ikaanza kusikika kwa kilio chake. Kila mtu alifurahia kwa dhati, lakini kwa upande wa Iryn, niliona alionesha dalili za kuchoka kupita kiasi na kuishiwa nguvu. Uso wake ulionekana dhaifu, na kwa njia fulani, nilihisi hofu kwamba alikuwa katika hali mbaya zaidi.

Hili lilikuwa ni tukio lenye historia kubwa sana katika maisha yangu. Kwa mara ya kwanza, nilipata nafasi ya kushuhudia moja kwa moja mchakato mzima wa Ariana akiletwa duniani. Tukio hili litabaki kwenye kumbukumbu zangu daima, likionyesha jinsi maisha ya binadamu yanavyoanza.

Kutokana na tukio hili, kila mmoja aliyekuwepo hospitalini alionekana na uso wa furaha. Siku hiyo tulikesha tukipiga stori mbalimbali, kwani hatukuwa tena kwenye wasiwasi wa awali. Kuhusu maendeleo ya Iryn, tuliambiwa kwamba itabidi asubiri kidogo kwa ajili ya uangalizi wa afya yake, lakini kulikuwa na matumaini kwamba siku ya Ijumaa angeweza kuruhusiwa. Hali ilionekana kuwa nzuri, na hiyo ilitufanya tuwe na moyo wa furaha na matumaini.

Asubuhi, mama Janeth alitoka akiwa amembeba mtoto, na alinipa mimi kwanza nimshike, kisha wengine walifuata. Nilifurahi sana kumuona binti yangu Aria; alionekana kuwa kibonge sana, na ngozi yake nyeupe kama mzungu iliongeza uzuri wake.

Baada ya kumshika Aria, nilimpa babu yake, ‘Baba Iryn,’ amshike naye. Babu alifurahi sana kumuona mjukuu wake na alisikika akisema, “Thank God, today I have seen my grandchild before I die.” Kila mtu aliyekuwepo pale alipata nafasi ya kumshika Aria, na furaha ilitawala.

Nilichukua ua langu na kuingia ndani ili kuonana na Iryn. Baada ya kuingia, nilimkuta amelala kitandani huku nurse akimhudumia. Bila kusita, nilimkiss shavuni na kumkabidhi zawadi yake ya ua. Nilivuta kiti, nikaketi, na kuanza kuongea naye. Kwanza kabisa, nilianza kumshukuru kwa kunizalia mtoto mzuri kama yeye. Mazungumzo yetu yalikuwa ya kufurahisha, yakijenga uhusiano wetu zaidi na kuleta tabasamu kwenye nyuso zetu.

Nilimpa maneno matamu sana kiasi kwamba alikuwa akitabasamu tu. Nilimwambia kuwa katika zawadi zote alizowahi kunipa, hii ya mtoto ndiyo zawadi yenye thamani zaidi kwangu. Nilimwambia aniambie anataka nifanye nini kama shukrani yangu kwake, naye alijibu kwamba anataka kuwajua bibi na babu yake Aria. Alionyesha hamu ya kukutana nao, kwani ilikuwa ni fursa nzuri kwake kujenga uhusiano na familia yangu.

Nilimwambia asiwe na shaka juu ya hili na aniachie suala hilo, kwani kila kitu kitakuwa sawa na atafurahi. Wakati tunaongea, baba yake aliingia ndani, na niliona ni vizuri niwapishe waongee, maana mzee alikuwa hajapata nafasi ya kuzungumza na binti yake tangu nilipofika.

Nilikuwa nimechoka sana, hivyo tulishauriana na Jimmy tuondoke hotelini kupumzika, na baadaye turudi tena. Kabla ya kuondoka, nilimuaga dada yangu na kufanya utambulisho ili dada na Jimmy wafahamiane. Jimmy alifurahi sana kumfahamu dada yangu, na dada yangu naye alifurahi kufahamiana na Jimmy.

Baada ya hapo, tuliondoka kwa Uber kuelekea hotelini, na tukiwa njiani, tulikuwa tukizungumza mambo mengi hadi tulipofika. Mazungumzo yetu yalikuwa ya kufurahisha, yakijenga uhusiano wetu na kuongeza furaha ya safari yetu.

Baada ya kufika hotelini, tulikubaliana tuoge kwanza kisha tuonane kwa ajili ya kupata kifungua kinywa. Ndani ya dakika 20, tulionana tena na kukaa kwenye restaurant, tukipata kifungua kinywa huku mazungumzo yetu yakiendelea.

Nilikuwa na hamu ya kujua kwa nini mama yake hajaja kwenye jambo hili muhimu la binti yake, lakini Jimmy alijibu kwamba mama yake alipata dharura ya kikazi na atakuja wiki hii kabla haijaisha.

Kwa upande wangu, nilimuuliza kuhusu mahusiano yake na Amara, na nikamshauri kwa dhati afanye kumwoa yule mwanamke. Nilimwona Amara kuwa ni mtu mzuri na mwenye mvuto wa kipekee. Ingawa, licha ya yote, amemzalia mtoto mzuri, na anaonekana kujielewa sana katika maisha yao. Hata hivyo, maneno haya hayakuwa rahisi kwake kuyakubali, Jimmy alionekana kutopenda kabisa kuyasikia wala kuyazungumzia. Kila nilipomzungumzia suala la ndoa, lilikuwa kama mtihani mzito kwake, lililojaa hofu na wasiwasi.

Baada ya kupata kifungua kinywa, tulikubaliana kupumzika kidogo ili jioni turudi tena hospitalini. Nikiwa chumbani, nilitumia muda huo kuwasiliana na kina Hilda ili kuwataarifu kwamba Iryn kajifungua salama. Pia, nilimcheki Allen na Dullah, nikawapa taarifa hiyo ili wawe na habari sahihi kuhusu hali ya Iryn. Kwa upande wao walifurahi sana kuzisikia taarifa hizi, kwani habari hii iliwafariji na kuwapa matumaini.

Saa 10 jioni, tuliondoka kurudi hospitalini, na kila hatua ya safari ilikuwa inanipeleka kwenye mawazo ya kumuona mwanangu, Aria. Upendo nilionao kwa Aria na mama yake ulikuwa ni wa kipekee, na kwa muda huu, haukuweza kuelezeka kwa maneno. Moyo wangu ulijawa na furaha na matarajio, nikiwa na shauku kubwa ya kuwaona na kuwa nao karibu.

Baada ya kufika hospitalini, nilikutana na Madam Merlinda, ‘academic supervisor wa Iryn’, aliyekuwa amekaa akiongea na Mama Janeth kwenye benchi pale nje. Tulisalimiana, kwa furaha, huku anipongeza kwa kuwa baba. Mama Janeth, wakati wote, alikuwa akishangaa kuona mazungumzo yangu na Madam, kama vile alikuwa akijiuliza ni lini tulikuwa tumefahamiana.

Baadaye, Madam alimweleza jinsi tulivyokutana, na Mama Janeth alibaki akishangaa tu. Madam Merlinda pia aliongeza kuwa alifurahia sana kumuona dada yangu, kwani ndiye alikuwa wa kwanza kukutana naye pindi alivyofika hospitalini.

Niliingia ndani kumuangalia Iryn, na nilimkuta akizungumza na Jimmy. Alionekana kuwa na afya nzuri zaidi, na hali yake ilikuwa inaendelea kuimarika. Aliponiona, uso wake uliangaza kwa tabasamu zuri, tabasamu ambalo lilinihakikishia kuwa alikuwa anapona vizuri. Ile furaha ya kumuona katika hali hiyo ilinigusa sana, na nilihisi amani moyoni, nikijua kuwa mambo yalikuwa yanaenda vizuri kwa mke wangu.

Kaka yake Jimmy alianza kumpa jokes na Iryn alikuwa akitabasamu tu;

JIMMY: “Hatimaye umekuwa mama, ulikuwa unanionea sana wivu mimi kuwa baba watoto."

Iryn alibaki kimya, akimwangalia kaka yake kwa tabasamu la upole, huku Jimmy akiendelea kuzungumza kwa utani.

“Dada yangu, una nguvu sana. Umeweza ku-push kilo 4? Bado siamini! Inaonekana shemeji yangu, Insider, alifanya kazi yake vizuri sana."

Iryn alianza kucheka kwa kugugumia, akiwa na maumivu madogo ya baada ya kujifungua. Hapo ndipo nilipoamua kumzingua Jimmy kwa utani wangu, nikijaribu kupunguza mzaha wake kabla mambo hayajaenda mbali zaidi.

Jimmy, acha tu hiyo, kazi yote ya kilo 4 ilikuwa kwenye team effort,” nilimwambia kwa kicheko, tukizidi kuleta hali ya furaha ndani ya chumba.

Tuliendelea kuzungumza na nesi aliyekuwa akimhudumia Iryn, tukitaka kujua kuhusu muda ambao angeweza kuondoka hospitalini. Nesi alitueleza kwamba maendeleo ya Iryn yalikuwa mazuri na ya kuridhisha, na akatuhakikishia kuwa kesho angeweza kuruhusiwa kwenda nyumbani. Habari hizo zilileta faraja kubwa, tukijua kwamba muda wa kurejea nyumbani na kuanza safari ya maisha mapya na mtoto wetu ulikuwa umekaribia.

Nilikaa muda mrefu pale hospitalini, na kwa mara ya kwanza, niliweza kuzungumza na mama yake mdogo Iryn, kwani mara nyingi tulikuwa tukipishana. Mama yake mdogo ni mwanamke mwenye haiba ya kipekee, mzaliwa wa Afrika Kusini kule kule, na alikuwa na utulivu wa hali ya juu. Katika mazungumzo yetu, hakutoa ishara zozote za hisia za wazi, alikuwa mtulivu na wa kutafakari. Mazungumzo yetu yalikuwa ya kawaida, lakini nilihisi kama alikuwa akinisoma kwa makini, bila kuonesha mengi. Ilikuwa ni mazungumzo yenye hisia za kufahamiana na kuelewana kwa undani zaidi.

Saa 7 za usiku, niliamua kuondoka na Jimmy kurudi hotelini. Bahati nzuri, baada ya kufika, nilikutana na "Nala," yule dada niliyekuwa namtafuta. Lakini cha kushangaza, sikuwa na hisia zozote za kuvutiwa naye kama ilivyokuwa awali. Tangu Iryn ajifungue, nilihisi mabadiliko makubwa ndani yangu. Hisia zangu zilikuwa zimebadilika kabisa, na upendo wangu kwa Iryn na mtoto wetu ulizidi kuwa na nguvu zaidi. Mambo ambayo yalikuwa yananivutia zamani yalionekana kupoteza maana mbele ya furaha mpya ya familia yangu.

Tulisalimiana pale, na alinikumbuka mara moja, aliniambia alikuwa amepata taarifa kuwa nilikuwa namtafuta. Nilimuomba namba yake ya simu, lakini akasema kuwa mazingira ya kazi hayamruhusu kutoa namba yake ya simu. Alieleza kwamba ni kinyume cha utaratibu kutoa mawasiliano binafsi akiwa kazini. Hata hivyo, aliahidi kunitumia namba hiyo kwa njia nyingine, akisema ataiandika kwenye karatasi na kutafuta namna ya kunipatia baadaye. Baada ya mazungumzo hayo, nilimuaga na nikaenda kulala. Uchovu ulikuwa umechukua nafasi, na nilihitaji kupumzika baada ya siku ndefu.
*****

Kesho yake asubuhi, tulipokea taarifa njema kwamba Iryn alikuwa ameruhusiwa kutoka hospitalini. Kwa haraka, tulijiandaa mapema ili tuwahi kufika hospitali kumchukua. Hata hivyo, kichwani mwangu nilikuwa pia na wazo lingine. Nilitamani sana kuonana na dada yangu na kuzungumza naye kwa undani zaidi, kwani hatukuwa kwenye maelewano mazuri kwa muda. Nilihisi umuhimu wa kuweka sawa mambo baina yetu, kurejesha amani na uhusiano wetu wa kifamilia. Ilikuwa ni siku muhimu sana, si tu kwa ajili ya Iryn na mtoto wetu, bali pia kwa kuweka sawa tofauti zangu na dada yangu.

Saa nne asubuhi, tulifika hospitalini na tukakutana na mzee Virgil, ambaye alitusaidia kumchukua binti yake, Iryn, na kumpeleka nyumbani kwake, wengine tulitumia usafiri wa Uber kufika huko. Baada ya kufika kwenye apartment yake, ambayo ilikuwa na vyumba vitatu, ilibainika kuwa nafasi ilikuwa haitoshi kutokana na idadi ya wageni waliokuwepo pale. Kwa hiyo, mimi na Jimmy tulikubaliana kuendelea kulala hotelini ili kutoa nafasi zaidi kwa wengine. Japokuwa tulitamani kukaa karibu na familia, uamuzi huo ulikuwa wa busara ili kuhakikisha kila mtu anapata nafasi ya kupumzika vizuri.

Mara tu baada ya kurudi nyumbani, marafiki zake wa chuo walifika kumtembelea. Walikuwa wakiingia na kutoka mfululizo, wakionesha upendo na shauku ya kumuona Iryn pamoja na kumpongeza kwa kujifungua salama. Kila mmoja alikuwa amekuja na zawadi, na hakika walimletea vitu vingi sana. Ile hali ya furaha ilitanda nyumbani, na zawadi nyingi walizomletea zilijaza kila kona ya apartment, zikionesha jinsi walivyothamini sana uhusiano wao na Iryn.

Kutokana na idadi kubwa ya watu waliokuwa wakiingia na kutoka kumtembelea Iryn, mimi niliamua kutoka nje na kukaa kibarazani ili kupata utulivu. Nikiwa pale, nilikuwa na Samantha, tukipiga story za hapa na pale. Mazungumzo yetu yalikuwa ya kawaida, lakini kwa upande wake, Samantha alionekana kuwa na jambo muhimu la kuniambia. Aliniambia kwa dhati kwamba dada yake, Iryn, ananipenda sana, hivyo nisije kumuumiza dada yake. Maneno hayo yalikuwa na uzito, na kwa muda ule, nilihisi hali ya utulivu na kuthamini zaidi kile kilichopo kati yangu na Iryn.

Jioni, Jimmy alinipatia wazo la kuondoka kwenye maeneo haya na kutafuta sehemu nyingine ambapo tunaweza kupoteza muda. Alisema kwamba nyumbani kumekuwa na wageni wengi, na kwa sisi wanaume, ilikuwa ni kuchoreshana tu bila maana. Niliona kuwa wazo lake lilikuwa zuri, hivyo tukakubaliana kutafuta sehemu tulivu ambapo tungeweza kuzungumza na kufurahia muda wetu bila bughudha.

Kabla ya kuondoka, nilipata wazo kwamba ningekuwa na busara kuonana na dada yangu ili tuzungumze, lakini alionekana kuwa busy sana, hivyo sikupata nafasi. Saa moja usiku, tuliondoka kimyakimya bila kuaga, tukielekea hotelini ili kubadilika kabla ya kutoka.

Nilikuwa sijui tunakoelekea, hivyo ilinibidi kumuliza Jimmy tutaenda wapi. Aliniambia kwamba tungeenda “Soho nightclub.” Jambo hilo lilinivutia, kwani nilijua ilikuwa ni sehemu maarufu ya burudani, kwani nilikuwaga naisikia tu.

Baada ya kujiandaa, tulikutana kwenye restaurant kwa ajili ya kupata dinner kabla ya kuondoka. Muda wote, tulikuwa kimya, hadi Jimmy aliposikika akilalamika kwa mbali, na ndipo tulipoanza mazungumzo.

MIMI: “Bro, what’s wrong?"

JIMMY: “My texts go green."

MIMI: “What do you mean?"

JIMMY: “I was texting my girlfriend, but she is no longer online."

Nilishangazwa kuona Jimmy akihangaika kuwatafuta wanawake wengine, hasa akiwa na Amara.

MIMI: “Bro, how about Amara?”

JIMMY: “Today she will sleep at my sister's house."

Sikutaka kuendeleza mazungumzo haya, kwani nilihisi ilikuwa si sahihi kuzungumzia mambo hayo. Hivyo, nikaamua kumwambia tuondoke, maana tulikuwa tumemaliza kula. Nilijua ni bora tushughulike na mambo mengine ya burudani zaidi usiku huu.

Tuliondoka na Uber kuelekea Soho, na nilipowasili na kushuka, nilianza kushangaa mazingira ya eneo hili pamoja na warembo walikuwa wakiingia, ilikuwa ni balaa. Baada ya kuingia ndani, nilijikuta nikipagawa kabisa, kulikuwa na warembo wa kila rangi na mtindo. Nilijisemea kuwa duniani kuna warembo wakali sana, na nikaona kuwa Dar es Salaam bado kuna safari ndefu kufikia level kama hizi.

JIMMY: “Bro, umepagawa?” Jimmy aliniuliza.

Nilikuwa nikiwa mbali sana kimawazo, kwani kulikuwa na mrembo mmoja aliyevuta kabisa umakini wangu. Nilikuwa nampigia hesabu kichwani, nikijaribu kufikiria jinsi ningekuwa na nafasi ya kuzungumza naye. Jimmy aliona wazi kuwa nilikuwa nimesahaulika, na alijaribu kunikumbusha kuwa nipo kwenye tukio la furaha.

MIMI: “Bro, this place is insane! another reason why men cheat.”

Jimmy alicheka sana kusikia kauli yangu.

JIMMY: “Naona umevutiwa na warembo wa hapa.”

MIMI: “Ni warembo wakali, lakini bado sijaona wa kumzidi Iryn.”

Jimmy alinyamaza kimya, maana hakutegemea kama ningetoa jibu kama hili na aliniangalia kisha akatabasamu.

JIMMY: “Umevutiwa na yule mrembo?”

MIMI: “Yeah! Yuko vizuri sana.”

JIMMY: “Unataka tumuite hapa?”

MIMI: “Kama kaja na mtu wake si tutaanzisha ugomvi hapa?.”

JIMMY: “Mwanamke yoyote utakayemkuta club ni mali yako. Hata siku moja usije kuogopa, mfate akukatalie mwenyewe. Mwanamke anayejitambua hawezi kuingia club kama hizi, kuna maeneo mengi sana ya kwenda.”

Nilinyamaza kwa sekunde, nikitafakari maneno ya Jimmy. Kwa kweli, alikuwa na pointi nzuri, lakini nilifikiria haraka haraka. Kwa nini Jimmy ananiunga mkono kuhusiana na wanawake wengine wakati nimemzalisha dada yake? Iliniuma kuona kwamba hakuwa na huruma yoyote kwake. Nilijua kuwa mahusiano yanaweza kuwa na changamoto, lakini kwa upande wangu, nilihisi kuwa heshima kwa Iryn ilipaswa kuwa ya kwanza.

MIMI: “Bro, I got your sister pregnant, but you're still supporting me in flirting with other women?"

Bro nimemzalisha dada yako, lakini bado unanisapoti nitongoze wanawake wengine?

JIMMY: “Brother, we are men, and the truth is I can't tell you what to do, even if you're in a relationship with my sister. When you're with Iryn, I'll respect you as my brother-in-law, but when you're with me here, I'll treat you as my friend. That's why, back then, when Iryn told me she loves you and that you're a married man, I didn't want to say anything. I just told her that the most important thing is for her to be happy.”

Kaka, sisi ni wanaume, na ukweli ni kwamba siwezi kukwambia nini cha kufanya hata kama uko kwenye mahusiano na dada yangu. Ukiwa na Iryn, nitakuheshimu kama shemeji yangu, lakini ukiwa na mimi hapa hivi, nitakuchukulia kama rafiki yangu. Ndomana, kipindi kile Iryn aliponiambia anakupenda na kwamba wewe ni mume wa mtu, sikutaka kusema lolote. Nilimwambia tu cha muhimu ni awe na furaha."

MIMI: “Bro, really?”

JIMMY: “Just be free when you’re with me, and don’t pretend you’re not a cheater. The most important thing is to make sure you’re very careful, don’t let them know that you cheat on them. Remember, you now have two women, and both of them love you.”

Tulinyamaza kwa dakika kadhaa wakati dada akitufungulia vinywaji vyetu, na baada ya kumaliza kazi yake tulianza kunywa, tukaendelea na maongezi yetu.

MIMI: “I still can’t believe whether Iryn really loves me.”

Jimmy aliniangalia, kisha akaipeleka glass yake ya kinywaji na akaanza kufunguka pale;

Ndugu yangu, naona kuwa hujikubali, lakini nisikilize kwa makini. Wewe ni mmoja wa watu muhimu sana katika maisha ya Iryn, na nakushukuru sana kwa yote uliyofanya kwa dada yangu. Kuna siri nyingi ambazo huenda Iryn bado hajakuambia, lakini leo, nitazungumzia hapa.

Tangu mamdogo afariki (mama Iryn), maisha ya Iryn yalibadilika sana, ni kama alichanganyikiwa na hakuwa katika maelewano mazuri na baba yake. Ukweli ni kwamba, hata familia yetu kwa ujumla haikuwa na maelewano na mzee Virgil kutokana na siri kubwa aliyokuwa ameificha kwa muda mrefu.

Iryn alianza kukutana na Isabella, na hii ilipelekea kutengeneza urafiki wa karibu sana. Unaweza kujiuliza, Isabella ni nani? Ni jirani yetu kule Ethiopia-Bahir, na ni mrembo maarufu sana nchini Ethiopia, pia ni International bi***ch. Huyu ndiye aliyemuingiza Iryn kwenye biashara za massage na kuanza kumpa connection za wateja.

Nilijua Iryn alijiingiza kwenye biashara hizi kupitia Isabella, maana mwenyewe ndiye aliyeniambia, kwani ni Ex wangu. Kwa sababu namjua vizuri Isabella ni nani, nilihofia kwamba dada yangu anaweza kuendeleza tabia kama za Isabella. Hivyo, ilibidi nimpigie simu Iryn na kumuomba tuonane, maana kipindi hicho alikuwa ameenda Ufaransa.

Baada ya kuonana na Iryn, nilimshauri sana aache hizi biashara na aje tusaidiane kuisimamia organization. Hata hivyo, alinikatalia na kuniambia hataki kazi zitakazompa stress, kwani biashara ya massage inamuingizia pesa nyingi sana.

Ingawa yeye alichukulia biashara ya massage kama kazi nyingine, kwa upande wangu, nilichukulia tofauti, niliona ni kazi ya kujiuza tu. Kutokana na suala hili, mimi na Iryn tuligombana sana siku hiyo, na nilimuacha aendelee na maisha yake.

Mwishoni mwa Februari 2021, nilikutana na Iryn nchini Ufaransa, na alikuwa na bwana wake (Griezmann), ambaye alinimtambulisha kwangu. Habari kubwa aliyonambia ilikuwa kuhusu mpango wake wa kurudi Tanzania, kutuliza akili na kufuatilia mafao aliyoacha mama yake.

Nilimshauri afanye hivyo maana ni jambo zuri, ukizingatia kwamba mama yake alifanya yote haya kwa ajili yake. Kabla ya kuondoka kwenda Tanzania, alikuja Bahir na kukaa kwa wiki moja, kisha akaondoka kuelekea Tanzania na alifikia kwa mama Janeth. Licha ya kuja Tanzania, bado aliendelea na biashara zake za massage kwa siri. Sikutaka kumpangia chakufanya kwenye maisha yake, hivyo nilimuacha aamue mwenyewe kuhusu maisha yake.

Mara ya kwanza tulipokutana Dar es Salaam, nilihisi Iryn anakupenda, ingawa alinikatalia kabisa nilipomuuliza. Baada ya miezi miwili, alinipa taarifa kuwa mpo katika mahusiano na ameamua kuacha biashara yake, yote kwa sababu yako. Alisema anakupenda sana na kwamba wewe ni mwanaume wa tofauti sana, hivyo anawaza kukupa zawadi ya mtoto. Kwa upande wangu, nilimwambia afanye maamuzi ambayo anaona ni sahihi kwake, lakini sikujua kama hakukushirikisha kuhusu hili. Hata hivyo, nilikuwa najua mipango yake.

Brother, wewe umechangia sana katika kubadilika kwa Iryn na kumuweka sawa kama zamani. Hata suala la mimba, niliwaambia nyumbani kwamba wewe ndiyo sababu Iryn kuwa na furaha, hivyo tumuache afanye anachoona kwake ni sawa.

Nimekwambia haya yote ili ujue kwamba unathamani kubwa sana kwa Iryn. Upendo na uaminifu wako kwake vimefanya akupende sana na kukuamini. Mimi kama kaka yake, nakushukuru sana na ninakupa heshima yangu. Hata kama utakuja kuachana na dada yangu, bado tutaendelea kuwa pamoja.


Tuliongea mambo mengi sana na Jimmy kuhusu Iryn. Kwa upande wake, alinifungukia vitu vingi, hadi kuhusu lifestyle yake, hivyo nilifahamu mambo mengi kupitia kwake. Alisema ameamua kuniambia haya yote kwa sababu ananiamini sana.

Baadaye, Jimmy alitoka na akarudi na mwanamke mzuri, ambaye alinitambulisha kama girlfriend yake. Tulikaa hadi saa 7 za usiku, na tukashauriana na Jimmy tuondoke maana muda ulikuwa umeenda sana. Tuliondoka kurudi hotelini ambapo Jimmy alikuwa na pisi yake.

Saa tano asubuhi, Jimmy alikuja kunigongea mlango na kunitaarifu kwamba Iryn amepiga simu nyingi na ameanza kumpa lawama kwamba ananifundisha tabia mbaya. Jimmy alisema nijiandae haraka ili tuende kwa Iryn maana anatuhitaji. Nilikuwa nina uchovu sana, hivyo niliingia bafuni kuoga haraka na kujiandaa. Nilipowasha data, nikakuta missed calls nyingi kutoka kwa Iryn na dada yangu, nilihisi huko kuna kitu, nitajua nikifika.

Tuliondoka kwenda nyumbani kwa mama mtoto, na ndani ya muda mfupi tulifika. Baada ya kuingia ndani, nakutana uso kwa uso na mama yake mkubwa, akiwa amemshika mtoto, na tukaanza kuangaliana pale.
👍
 
SEASON 02
CHAPTER 40

“TRUE STORY BY INSIDER MAN”

PREVIOUS:
Baada ya kuwasili pale JNIA, tulikaa na kuendelea na mazungumzo. Nilimsihi sana Hilda aisimamie kampuni vizuri hadi nitakaporudi, nikijua kuwa ilikuwa muhimu kwa ajili ya usimamizi mzuri. Baada ya dakika 20, tuliagana kwa kukumbatiana, nami nikacheck-in kwa ajili ya kuanza safari yangu kuelekea South Africa, nilijua ni mwanzo wa safari muhimu na nilikuwa na matumaini makubwa.

CONTINUE:

Nikiwa kwenye harakati za kukamilisha taratibu kabla ya safari, simu ya Mary iliingia, na bila kusita niliipokea. Katika mazungumzo, nilikumbuka kuwa sikuwa nimemjulisha rasmi kwamba naondoka kwenda Afrika Kusini, ingawa tayari nilikuwa nishamgusia kuhusu safari hii. Nilipompa taarifa kamili, Mary hakuweza kuzichukua kwa urahisi. Alionyesha hisia kali na kunilalamikia kwa kuondoka bila kumuaga rasmi, jambo ambalo halikumfurahisha hata kidogo.

Nilimkumbusha kwamba tayari nilishamgusia kuhusu safari hii, lakini bado hakutaka kuelewa. Alisisitiza kuwa nilipaswa kumjulisha mapema zaidi, na sio kusubiri mpaka anipigie simu ndipo nimpe taarifa hizi. Hasira zake ziliongezeka, na hatimaye alikata simu ghafla. Kwa upande wangu, sikuona haja ya kuendelea kumfikiria, kwani niliona anachukulia jambo hili kwa namna ya kitoto. Niliamua kuacha nifikirie mambo muhimu zaidi na kuendelea na safari yangu.

Safari ya kuelekea Afrika Kusini ilianza vizuri, na nilibahatika kupata siti ya upande wa dirishani. Pembeni yangu aliketi binti Mtanzania, aliyenipa tabasamu la salamu tulipokutana macho. Ingawa tulisalimiana kwa heshima, sikuwa na hamu ya kuendelea na mazungumzo. Mawazo yangu yalikuwa mbali sana, nikitafakari kwa kina juu ya hatima ya maisha yangu na mustakabali wangu baada ya safari hii. Nilihisi kama nilikuwa kwenye hatua ya mabadiliko, na kila kitu kingine kilionekana kama kelele zisizo na maana wakati huo.

Nilipokuwa nikitazama anga za mbali kupitia dirisha la ndege, matumaini yangu ya kuwa baba wa watoto wawili yalijaa ndani yangu. Niliamini kwa dhati kuwa Iryn angejifungua salama, na hilo lilinipa faraja. Hata hivyo, mawazo yangu yalivutwa kwa nguvu kuelekea mahusiano yangu na Mary. Maneno ya Jane yalinirudia kichwani, na kadri nilivyoyatafakari, niliona alikuwa sahihi. Ikiwa mahusiano yangu na Mary yangekuja kufahamika kwenye familia yake, ningekabiliwa na shida kubwa. Hili lilikuwa jambo lililonitatiza sana.

Kilichonifanya nisijisikie vizuri zaidi ni kwamba, licha ya kuelewa athari za uhusiano huu, nilikuwa kwenye dilema kali kuhusu hatua sahihi ya kuchukua. Nilijua kwamba kumuacha Mary kungekuwa ngumu, na wakati huo huo, kuendelea naye kulionekana kama kuzidisha tatizo. Mawazo yangu yalikuwa magumu sana, nikikosa maamuzi ya busara kuhusu mustakabali wa uhusiano wetu.

Kadri safari ilivyoendelea, nilijikuta nikitafakari zaidi kuhusu maisha yangu tangu nilipoanza biashara za Uber. Kipindi hicho kilikuwa mwanzo wa mabadiliko makubwa, ambapo nilikutana na watu wengi sana ambao kwa njia moja au nyingine wamekuwa msaada mkubwa katika safari yangu ya kimaisha. Nilipitia mengi mazuri na magumu, na kila tukio lilionekana kuwa na nafasi yake maalum katika hadithi ya maisha yangu. Nilihisi kama maisha yangu yalikuwa kama filamu, yenye mlolongo wa matukio ya kipekee.

Kutokana na hayo, wazo moja lilianza kuota mizizi, kuandika kitabu. Kitabu ambacho kingekuwa ukumbusho wa safari yangu, changamoto nilizokutana nazo, mafanikio niliyoyapata, na watu waliokuja na kuondoka. Hili lilionekana kuwa jambo la maana, sio tu kwa ajili yangu binafsi, bali pia kwa wengine, ili waweze kujifunza kutokana na yale niliyoyapitia kwa muda mfupi sana lakini yenye uzito mkubwa.

Tulipowasili Johannesburg, tulipewa muda wa mapumziko wa takriban saa moja kabla ya kubadilisha ndege ya kuelekea Cape Town. Nikiwa nimechoka kidogo lakini bado nikiwa na ari ya kufika, nilitumia muda huo vizuri kufanya booking ya hoteli. Nilichagua hoteli ileile ambayo mimi na dada yangu tulifikia safari iliyopita, Southern Sun Newlands Hotel.

Baada ya lisaa na dakika kadhaa, tulianza safari yetu ya kwenda Cape Town. Ndege iliondoka Johannesburg saa mbili asubuhi, na tulifika Cape Town majira ya saa tano asubuhi. Nilipomaliza taratibu za uhamiaji na kuchukua mizigo, nilichukua tax moja kwa moja kuelekea kwenye hoteli niliyokuwa nimefanya booking.

Nilipowasili hotelini, jambo la kwanza kabisa nilifanya ni kuoga ili kuondoa uchovu wa safari. Baada ya hapo, niliamua kutoka kwenda kupata chakula kwani nilikuwa na njaa kubwa. Nilipokuwa nikila, nilikuwa pia nawasiliana na sister, ambaye aliniongoza kuhusu hospitali walikokuwa. Aliniambia kuwa nikianza kuondoka niwajulishe ili tuweze kukutana. Mawasiliano hayo yalifanya nianze kujiandaa kisaikolojia kwa hatua zinazofuata.

Nilipokuwa hotelini, mawazo yangu yalirudi nyuma, nikamkumbuka yule dada niliyempa pesa kipindi kile nilipoondoka na dada yangu hapa hotelini. Hali hiyo ilinifanya nianze kuhisi tamaa, hisia zangu zikielekea kwake. Nilikuwa nalikumbuka jina lake vizuri, hivyo nilichukua hatua ya kumuuliza mhudumu mmoja wa hoteli kuhusu yule dada. Alinijibu kwa ufupi kuwa ataingia shift ya jioni.

Sasa, baada ya kupata taarifa hizo, nilihisi msukumo wa kutaka kuomba namba yake ya simu, lakini nikaamua kujizuia. Niliona ni busara zaidi kuwa mpole na kuacha mambo yaende kwa utaratibu wake, kwani nilijua tutaonana hivyo, niliamua kusubiri kwa utulivu.

Kipindi nikiwa hapa na sister, ukweli ni kwamba nilivutiwa sana na yule dada mhudumu, lakini nilijizuia kwa heshima ya sister. Nilijua wakati ule haikuwa sahihi kuchukua hatua yoyote zaidi ya mazungumzo ya kawaida. Lakini moyoni nilihisi kwamba siku moja nitarudi tena Afrika Kusini, na nitaishia kufikia hoteli hii, ambapo nitapata fursa ya kumuona tena. Hata ile hatua ya kumpa pesa haikuwa tu msaada wa kawaida, nilikuwa najenga mazingira mapema kwa ajili ya kupata "mzigo" bila vikwazo hapo mbeleni.

Nilihisi tamaa kubwa ya kupiga game la mwisho kabla ya Iryn kujifungua, kwa sababu ya heshima na umuhimu wa mtoto ambaye alikuwa njiani kuja. Nilijua kuwa pindi Iryn atakapojifungua, singeweza tena kupiga game mpaka nitakaporudi Tanzania, na wakati huo nisingejua nitatumia muda gani huku Afrika Kusini. Hali hii ilifanya hisia zangu kuwa za ndani zaidi, kwani nilijua kuwa na mabadiliko makubwa yanakuja, na ningeweza kupoteza fursa za kufanya mambo niliyoyapenda.

Wakati nikiwa na mawazo yangu, Jimmy alinitafuta kupitia WhatsApp na kunijulisha kwamba yuko njiani anakuja. Nilimjibu kwa kumwambia niliko, pamoja na hoteli niliyofikia. Alifurahishwa na taarifa hiyo na kusema kwamba naye atafikia hoteli hii. Jimmy aliomba niweze kumfanyia booking ya chumba mapema ili asije kukosa nafasi. Niliamua kumsaidia na kuanza kupanga jinsi ya kumtafutia chumba, huku nikijua kuwa uwepo wake jirani ungekuwa muhimu kwangu.

Saa 8 mchana, niliondoka kuelekea hospitali, nikiwa nimetumia usafiri wa Uber. Dereva aliyekuja kunichukua alikuwa ni choko, na njiani alinitafutia mazungumzo mengi ambayo yalinisababisha kuhisi kero. Nilijua niko katika nchi ya watu na sikutaka kuonesha tabia yoyote isiyofaa. Hivyo, nilimjibu maswali yake kwa ustaarabu, lakini moyoni nilikuwa nikiomba tu kufika hospitali mapema. Katika maisha yangu ninaaminu kwamba kukutana na watu hawa kunaweza kuwa kama mikosi kwangu.

Umbali kutoka hotelini hadi Mediclinic hospital ni kama kilomita 15, sawa na kutoka Mwenge hadi Kivukoni, na nilijua Iryn hakuwa akiishi mbali sana na chuo anachosoma wala hoteli niliyofikia. Nilipokaribia hospitali, shauku yangu ilikuwa kubwa sana, nikitamani kwa dhati kumuona Iryn.

Mara baada ya kufika, nilimkuta sister akiwa ananisubiri pamoja na Samantha pale nje. Tulipokutana, tulisalimiana, lakini niliona wazi kwamba sister hakuwa sawa. Hisia zangu zikanifanya nishuku kuwa huenda ilikuwa ni kuhusu lile suala la mama J. Nilihisi kwamba sister bado alikuwa na mawazo mengi kichwani mwake. Sikutaka kumuuliza sana kuhusu hilo, kwani nilikuwa na hamu ya kuzungumza na Samantha, ambaye hatukuweza kukutana kwa muda mrefu. Hivyo, nilijaribu kuelekeza mazungumzo yangu kwake, nikifurahia kuungana tena na shem wangu.

Tulipoingia ndani ya hospitali, tulielekea moja kwa moja hadi wodi aliyokuwa amelazwa Iryn. Nilipofungua mlango na kuingia ndani ya chumba, jambo la kwanza lililoshika macho yangu lilikuwa ni Vivian, aliyekuwa amesimama pembeni akizungumza na daktari, kana kwamba alikuwa akipokea maelekezo muhimu. Lakini hata hivyo, macho yangu yote yalivutwa kwa Iryn.

Alikuwa amelala kitandani, akiwa uchi, na jasho likimtoka kwa wingi, ishara ya uchovu wa mwili uliomlemea. Mwili wake ulionekana dhaifu sana, hali ambayo ilinipatia hisia za huruma kali. Nywele zake ndefu na nzuri zilikuwa zimetifuka, zikionesha uchovu aliokuwa nao. Matiti yake yalionekana kuvimba, na mwili wake wote ulionekana kubadilika kwa kiasi kikubwa.

Iryn alikuwa akihema kwa shida, kila pumzi ikionekana kuwa mzigo kwake. Hali yake ilinishtua, nikitambua kuwa huu ulikuwa wakati mgumu sana kwake. Hisia za huzuni na wasiwasi zilijaa ndani yangu, huku nikijua kwamba nilihitaji kuwa na nguvu kwa ajili yake katika kipindi hiki kigumu.

Wasiwasi wangu ulianza kuongezeka mara moja, nikijiuliza kama hali yake ni mbaya zaidi ya nilivyofikiria. Nilimwona akiugua kimya kimya, na moyo wangu ulianza kushuka, nikihisi uzito wa hali hii. Sikujua nini kingetokea, lakini nilihisi kwamba sasa kila kitu kilikuwa nje ya uwezo wangu, na yote niliyoweza kufanya ni kumwombea awe salama.

Nilisogea karibu na kitanda cha Iryn, nikamshika shavu lake kwa upole, na mara moja nilihisi joto lake lilikuwa limepanda. Japo mwili wake ulikuwa dhaifu, niliweza kugundua alifurahi kuniona, ingawa hakuwa na nguvu za kuonyesha ile furaha waziwazi. Lakini kwa namna fulani, niliweza kuhisi furaha yake ndani ya hali ile ngumu aliyokuwa nayo.

Nikiwa nimemshika mkono, nilijikuta nikilegea kando yake, nikamshika tumbo lake kwa upole na kwa sauti ya faraja nikamwambia, “You will be alright, my love."

Alinitazama kwa macho yenye uchovu lakini yenye matumaini, na kwa upole akatikisa kichwa chake, akionyesha kukubaliana nami. Huo ulikuwa ni wakati wa kimya, lakini pia wa utulivu.

Nilipoanza kuzungumza na kina Sister kuhusu maendeleo ya Iryn, walinifahamisha kuwa njia ya mtoto bado haijafunguka, lakini kuna matumaini ya kujifungua salama kwa njia ya kawaida (Normal Vaginal Delivery). Pia waliongeza kuwa, kama hali hiyo itaendelea na njia ya uzazi itaendelea kusumbua, basi madaktari watalazimika kumfanyia upasuaji (OP) ili kuinusuru afya ya Iryn pamoja na mtoto.

Ingawa taarifa hizo zilikuwa na changamoto, kulikuwa na faraja katika kujua kwamba walikuwa tayari kuchukua hatua sahihi kwa kuhakikisha usalama wa Iryn na mtoto. Hali hii ilinipa matumaini ya kumalizika kwa hali hii kwa usalama.

Madaktari na wauguzi walikuwa wakiingia na kutoka ndani ya chumba, wakionekana kuwa na shughuli nyingi sana, wakihangaika kuhakikisha kila kitu kipo sawa. Hali ile ya harakati na uzito wa mazingira ilinifanya nishindwe kuvumilia kukaa ndani kwa muda mrefu. Nilitambua kuwa ni bora niwapishe waendelee na kazi zao bila usumbufu wowote, hivyo nikaamua kutoka nje ili kupata hewa na kutuliza mawazo yangu, huku nikisubiri kwa matumaini kila kitu kitakwenda sawa.

Pale nje, kwenye benchi, Samantha alikuwa amekaa akisubiri kwa utulivu, maana hakuwa ameruhusiwa kuingia ndani kwa sababu ya hali ya dada yake, Iryn, ambaye alikuwa kwenye mazingira ya faragha. Isingekuwa busara, wala heshima, kwa Samantha kumuona dada yake katika hali ile ya udhaifu.

Nikiwa nimekaa naye, tulianza kuzungumza kwa upole, huku mawazo yangu yakiendelea kuzunguka hali ya Iryn. Katika mazungumzo, nilimwambia Samantha kuwa tungehitaji kwenda shopping ili kununua baadhi ya vitu vya mtoto. Samantha alinijibu kuwa wao tayari walikuwa wamenunua kila kitu kinachohitajika, lakini nikamwambia kwamba safari hiyo ilikuwa muhimu kwa upande wangu, nilihitaji kununua vitu kwa ajili ya mtoto wetu.

Wakati tunaendelea kuzungumza, mama yake mdogo wa Iryn, ambaye ni mke wa baba yake, alifika na kutusalimia kabla ya kuingia ndani. Nilipomwona, nilihisi kama nimemfananisha na mtu niliyewahi kumuona mahali fulani, lakini sikuweza kukumbuka wapi. Samantha aliniambia kuwa huyo ni mama mdogo wa Iryn, na hapo ndipo nikakumbuka kwamba nilimwona kwenye picha kupitia simu ya Iryn.

Baada ya dakika 20, Vivian alitoka ndani, na tulikubaliana kuondoka kuelekea moja ya shopping mall ili kununua vitu vya mtoto. Safari yetu ilianza kwa furaha, na tulitumia takribani masaa mawili kufanya manunuzi ya vitu mbalimbali muhimu, ikiwa ni pamoja na mavazi, toys, na vitu vingine vingi.

Tulikuwa na mazungumzo mazuri huku tukichagua bidhaa, na kila bidhaa tuliyoinunua iliongeza hisia zetu za furaha na matarajio. Baada ya kumaliza manunuzi, tukarudi tena hospitali, tukijua kuwa vitu hivi vitakuwa na umuhimu mkubwa kwa Iryn na mtoto. Moyo wangu ulijaa matumaini na furaha, nikihisi kwamba nilikuwa nikichangia kwa njia fulani katika maisha ya familia yetu mpya.

Baada ya kufika hospitali, bila kutegemea, nilikutana na mama Janeth. Baada ya kusalimiana, aliniambia kwamba alikuwa pale tangu asubuhi, lakini alikuwa ameenda sehemu fulani kwa muda mfupi. Mama Janeth alionekana kufurahia sana kuniona, na alisema alifurahi pia kumuona dada yangu.

Aliniondoa wasiwasi wote kuhusu afya ya Iryn, akisema niondoe hofu, kwani aliamini Iryn atajifungua salama. Maneno yake yalinipa faraja kubwa, na nilihisi kama mzigo mzito ulishuka kutoka kwenye bega langu. Utu wake na uhakikisho wake vilinipa nguvu na matumaini zaidi, nikijua kwamba nilikuwa na watu wa kutegemea katika kipindi hiki kigumu.

Nilipouliza kuhusu dada yangu, mama Janeth alinijulisha kwamba alikuwa ametoka kwa muda mfupi kurudi nyumbani kufuata baadhi ya vitu na kwamba atarudi hivi karibuni. Aliongeza kwamba dada yangu alikuwa amejitolea sana katika suala hili, akifanya kila liwezekanalo kumsaidia Iryn.

Hali hii ilinifanya niwe na matumaini zaidi, nikijua kwamba familia ilikuwa ikifanya kazi pamoja ili kusaidia Iryn katika kipindi hiki muhimu. Utu wa dada yangu na jitihada zake zilinifanya nihisi kuwa siko peke yangu katika changamoto hii, bali kuna watu wengi waliokuwa tayari kumsaidia na kuhakikisha kuwa Iryn anapata kila kitu anachohitaji. Nilihisi faraja kuona kwamba walikuwa wakijali afya ya Iryn kwa namna ya pekee, na nilimuacha mama aendelee na majukumu yake.

Wakati nimetulia kwenye benchi, Jimmy alinitumia ujumbe kunitaarifu kuwa amefika salama na yuko hotelini. Alisema anapumzika kidogo kabla ya kuja hospitali. Nilihisi furaha kubwa kusikia taarifa hizi kutoka kwake, maana sikuwa na mtu mwingine wa kunipa kampani zaidi yake katika kipindi hiki cha wasiwasi.

Kwa mbali, nilimuona mzee Virgil, baba yake Iryn, akitokea na kuja kwenye upande wangu. Sikuwa na mawazo ya kuonana naye wakati huu, na kwa upande wake, hakutegemea kuniona pia. Alikuwa ameambatana na binti yake mwingine, ambaye ni kama mdogo wa Iryn kupitia kwa mke mdogo.

Baada ya kusalimiana, tulianza mazungumzo ambapo mzee Virgil alisema amefurahi kuniona na alinipa hongera kwa kuwa baba. Aliongeza kwamba amefurahi kumfahamu dada yangu, akisema amekuwa mstari wa mbele sana katika kumsaidia Iryn.

Nilijua kwamba maneno yake yalionyesha kuthamini juhudi za dada yangu, na hilo lilinipa faraja kubwa. Mzee Virgil ni mtu poa sana; katika suala la Iryn, hajawahi kuonesha mtazamo tofauti, na anathamini sana mchango wangu kwa Iryn.

Baada ya mazungumzo ya kina kuhusu Iryn, mzee alinitafutia njia nyingine ya kuzungumza, akileta mada ya maisha na changamoto zake. Pia, alinikaribisha nyumbani kwake, akisisitiza umuhimu wa kukutana na familia yake ili tufahamiane vizuri zaidi. Maneno yake yalionyesha wazi kuwa aliona mbali, akaniambia kuwa mimi tayari ni sehemu ya familia hiyo, na hiyo ilinionyesha jinsi alivyothamini uwepo wangu katika maisha yao.

Saa 2 za usiku, Jimmy alifika hospitali akiwa na Amara (mwanamke aliyezaa naye) pamoja na mtoto wao. Tulisalimiana, na mara moja nilianza mazungumzo na Amara, maana mara ya mwisho nilipokutana naye ilikuwa ni Ethiopia. Wakati huu, mtoto wake alikuwa akicheza kwa furaha na babu yake (Baba Iryn), akimuita "Grandpa," huku sauti yake ikijaza chumba kwa furaha.

Mtoto wa Jimmy ni mzuri sana, ni mtoto ambaye ukimuona, moyo wako utajawa na tamaa ya kumiliki. Mama yake Amara pia ni mzuri, uzuri wake ulijitokeza wazi, na hapo ndipo nikajikuta nikijiuliza, inawezekanaje Jimmy asikubali kum-oa dada huyu?

Licha ya tabia za kihuni za Jimmy, upendo wa Amara kwake ni mkubwa sana, ni anampenda sana Jimmy. Hali hii haijabaki kuwa ya siri, kwani familia yao yote inampenda Amara kwa dhati. Hata Iryn, ambaye mara nyingi anashindwa kuelewa kwanini Jimmy anashikilia mbali ndoa, huwa anatamani sana siku moja aone Jimmy akimuoa Amara, niligusia hili (Season 2: Chapter 10).

Saa 4 za usiku, mama Janeth alikuja na kuniita kwa haraka, uso wake ukiwa na wasiwasi. Aliniambia kwamba Iryn anataka kujifungua na anahitaji uwepo wangu wakati huu muhimu. Niliweza kuhisi uzito wa maneno yake, lakini ndani yangu nilihisi hofu kubwa kuhusu kushuhudia mchakato huu wa kipekee. Ingawa singependa kushiriki katika tukio hili, nilijua kuwa Iryn alihitaji faraja yangu katika wakati wa shida. Kwa hivyo, licha ya woga wangu, sikuweza kukataa.

Movie ilianza mle chumbani, ambapo daktari wawili na wauguzi wawili walikuwa wakifanya maandalizi. Kwa upande wetu, tulikuwa mimi, mama Janeth, na mama yake mdogo, jumla tukiwa saba ndani ya chumba hicho. Hata ingawa sitaki kuzungumzia kwa undani, ninatambua jinsi hali ilikuwa ngumu. Iryn alijifungua salama baada ya mchakato mgumu wa kupush. Walimwongezea njia kwa sababu mtoto alikuwa mkubwa, uzito wa 3.95 kg sio mchezo. Nakumbuka jinsi nilivyohisi uzito wa tukio hilo, nadhani mmeelewa ninachomaanisha.

Baada ya kujifungua, sauti ya mtoto ikaanza kusikika kwa kilio chake. Kila mtu alifurahia kwa dhati, lakini kwa upande wa Iryn, niliona alionesha dalili za kuchoka kupita kiasi na kuishiwa nguvu. Uso wake ulionekana dhaifu, na kwa njia fulani, nilihisi hofu kwamba alikuwa katika hali mbaya zaidi.

Hili lilikuwa ni tukio lenye historia kubwa sana katika maisha yangu. Kwa mara ya kwanza, nilipata nafasi ya kushuhudia moja kwa moja mchakato mzima wa Ariana akiletwa duniani. Tukio hili litabaki kwenye kumbukumbu zangu daima, likionyesha jinsi maisha ya binadamu yanavyoanza.

Kutokana na tukio hili, kila mmoja aliyekuwepo hospitalini alionekana na uso wa furaha. Siku hiyo tulikesha tukipiga stori mbalimbali, kwani hatukuwa tena kwenye wasiwasi wa awali. Kuhusu maendeleo ya Iryn, tuliambiwa kwamba itabidi asubiri kidogo kwa ajili ya uangalizi wa afya yake, lakini kulikuwa na matumaini kwamba siku ya Ijumaa angeweza kuruhusiwa. Hali ilionekana kuwa nzuri, na hiyo ilitufanya tuwe na moyo wa furaha na matumaini.

Asubuhi, mama Janeth alitoka akiwa amembeba mtoto, na alinipa mimi kwanza nimshike, kisha wengine walifuata. Nilifurahi sana kumuona binti yangu Aria; alionekana kuwa kibonge sana, na ngozi yake nyeupe kama mzungu iliongeza uzuri wake.

Baada ya kumshika Aria, nilimpa babu yake, ‘Baba Iryn,’ amshike naye. Babu alifurahi sana kumuona mjukuu wake na alisikika akisema, “Thank God, today I have seen my grandchild before I die.” Kila mtu aliyekuwepo pale alipata nafasi ya kumshika Aria, na furaha ilitawala.

Nilichukua ua langu na kuingia ndani ili kuonana na Iryn. Baada ya kuingia, nilimkuta amelala kitandani huku nurse akimhudumia. Bila kusita, nilimkiss shavuni na kumkabidhi zawadi yake ya ua. Nilivuta kiti, nikaketi, na kuanza kuongea naye. Kwanza kabisa, nilianza kumshukuru kwa kunizalia mtoto mzuri kama yeye. Mazungumzo yetu yalikuwa ya kufurahisha, yakijenga uhusiano wetu zaidi na kuleta tabasamu kwenye nyuso zetu.

Nilimpa maneno matamu sana kiasi kwamba alikuwa akitabasamu tu. Nilimwambia kuwa katika zawadi zote alizowahi kunipa, hii ya mtoto ndiyo zawadi yenye thamani zaidi kwangu. Nilimwambia aniambie anataka nifanye nini kama shukrani yangu kwake, naye alijibu kwamba anataka kuwajua bibi na babu yake Aria. Alionyesha hamu ya kukutana nao, kwani ilikuwa ni fursa nzuri kwake kujenga uhusiano na familia yangu.

Nilimwambia asiwe na shaka juu ya hili na aniachie suala hilo, kwani kila kitu kitakuwa sawa na atafurahi. Wakati tunaongea, baba yake aliingia ndani, na niliona ni vizuri niwapishe waongee, maana mzee alikuwa hajapata nafasi ya kuzungumza na binti yake tangu nilipofika.

Nilikuwa nimechoka sana, hivyo tulishauriana na Jimmy tuondoke hotelini kupumzika, na baadaye turudi tena. Kabla ya kuondoka, nilimuaga dada yangu na kufanya utambulisho ili dada na Jimmy wafahamiane. Jimmy alifurahi sana kumfahamu dada yangu, na dada yangu naye alifurahi kufahamiana na Jimmy.

Baada ya hapo, tuliondoka kwa Uber kuelekea hotelini, na tukiwa njiani, tulikuwa tukizungumza mambo mengi hadi tulipofika. Mazungumzo yetu yalikuwa ya kufurahisha, yakijenga uhusiano wetu na kuongeza furaha ya safari yetu.

Baada ya kufika hotelini, tulikubaliana tuoge kwanza kisha tuonane kwa ajili ya kupata kifungua kinywa. Ndani ya dakika 20, tulionana tena na kukaa kwenye restaurant, tukipata kifungua kinywa huku mazungumzo yetu yakiendelea.

Nilikuwa na hamu ya kujua kwa nini mama yake hajaja kwenye jambo hili muhimu la binti yake, lakini Jimmy alijibu kwamba mama yake alipata dharura ya kikazi na atakuja wiki hii kabla haijaisha.

Kwa upande wangu, nilimuuliza kuhusu mahusiano yake na Amara, na nikamshauri kwa dhati afanye kumwoa yule mwanamke. Nilimwona Amara kuwa ni mtu mzuri na mwenye mvuto wa kipekee. Ingawa, licha ya yote, amemzalia mtoto mzuri, na anaonekana kujielewa sana katika maisha yao. Hata hivyo, maneno haya hayakuwa rahisi kwake kuyakubali, Jimmy alionekana kutopenda kabisa kuyasikia wala kuyazungumzia. Kila nilipomzungumzia suala la ndoa, lilikuwa kama mtihani mzito kwake, lililojaa hofu na wasiwasi.

Baada ya kupata kifungua kinywa, tulikubaliana kupumzika kidogo ili jioni turudi tena hospitalini. Nikiwa chumbani, nilitumia muda huo kuwasiliana na kina Hilda ili kuwataarifu kwamba Iryn kajifungua salama. Pia, nilimcheki Allen na Dullah, nikawapa taarifa hiyo ili wawe na habari sahihi kuhusu hali ya Iryn. Kwa upande wao walifurahi sana kuzisikia taarifa hizi, kwani habari hii iliwafariji na kuwapa matumaini.

Saa 10 jioni, tuliondoka kurudi hospitalini, na kila hatua ya safari ilikuwa inanipeleka kwenye mawazo ya kumuona mwanangu, Aria. Upendo nilionao kwa Aria na mama yake ulikuwa ni wa kipekee, na kwa muda huu, haukuweza kuelezeka kwa maneno. Moyo wangu ulijawa na furaha na matarajio, nikiwa na shauku kubwa ya kuwaona na kuwa nao karibu.

Baada ya kufika hospitalini, nilikutana na Madam Merlinda, ‘academic supervisor wa Iryn’, aliyekuwa amekaa akiongea na Mama Janeth kwenye benchi pale nje. Tulisalimiana, kwa furaha, huku anipongeza kwa kuwa baba. Mama Janeth, wakati wote, alikuwa akishangaa kuona mazungumzo yangu na Madam, kama vile alikuwa akijiuliza ni lini tulikuwa tumefahamiana.

Baadaye, Madam alimweleza jinsi tulivyokutana, na Mama Janeth alibaki akishangaa tu. Madam Merlinda pia aliongeza kuwa alifurahia sana kumuona dada yangu, kwani ndiye alikuwa wa kwanza kukutana naye pindi alivyofika hospitalini.

Niliingia ndani kumuangalia Iryn, na nilimkuta akizungumza na Jimmy. Alionekana kuwa na afya nzuri zaidi, na hali yake ilikuwa inaendelea kuimarika. Aliponiona, uso wake uliangaza kwa tabasamu zuri, tabasamu ambalo lilinihakikishia kuwa alikuwa anapona vizuri. Ile furaha ya kumuona katika hali hiyo ilinigusa sana, na nilihisi amani moyoni, nikijua kuwa mambo yalikuwa yanaenda vizuri kwa mke wangu.

Kaka yake Jimmy alianza kumpa jokes na Iryn alikuwa akitabasamu tu;

JIMMY: “Hatimaye umekuwa mama, ulikuwa unanionea sana wivu mimi kuwa baba watoto."

Iryn alibaki kimya, akimwangalia kaka yake kwa tabasamu la upole, huku Jimmy akiendelea kuzungumza kwa utani.

“Dada yangu, una nguvu sana. Umeweza ku-push kilo 4? Bado siamini! Inaonekana shemeji yangu, Insider, alifanya kazi yake vizuri sana."

Iryn alianza kucheka kwa kugugumia, akiwa na maumivu madogo ya baada ya kujifungua. Hapo ndipo nilipoamua kumzingua Jimmy kwa utani wangu, nikijaribu kupunguza mzaha wake kabla mambo hayajaenda mbali zaidi.

Jimmy, acha tu hiyo, kazi yote ya kilo 4 ilikuwa kwenye team effort,” nilimwambia kwa kicheko, tukizidi kuleta hali ya furaha ndani ya chumba.

Tuliendelea kuzungumza na nesi aliyekuwa akimhudumia Iryn, tukitaka kujua kuhusu muda ambao angeweza kuondoka hospitalini. Nesi alitueleza kwamba maendeleo ya Iryn yalikuwa mazuri na ya kuridhisha, na akatuhakikishia kuwa kesho angeweza kuruhusiwa kwenda nyumbani. Habari hizo zilileta faraja kubwa, tukijua kwamba muda wa kurejea nyumbani na kuanza safari ya maisha mapya na mtoto wetu ulikuwa umekaribia.

Nilikaa muda mrefu pale hospitalini, na kwa mara ya kwanza, niliweza kuzungumza na mama yake mdogo Iryn, kwani mara nyingi tulikuwa tukipishana. Mama yake mdogo ni mwanamke mwenye haiba ya kipekee, mzaliwa wa Afrika Kusini kule kule, na alikuwa na utulivu wa hali ya juu. Katika mazungumzo yetu, hakutoa ishara zozote za hisia za wazi, alikuwa mtulivu na wa kutafakari. Mazungumzo yetu yalikuwa ya kawaida, lakini nilihisi kama alikuwa akinisoma kwa makini, bila kuonesha mengi. Ilikuwa ni mazungumzo yenye hisia za kufahamiana na kuelewana kwa undani zaidi.

Saa 7 za usiku, niliamua kuondoka na Jimmy kurudi hotelini. Bahati nzuri, baada ya kufika, nilikutana na "Nala," yule dada niliyekuwa namtafuta. Lakini cha kushangaza, sikuwa na hisia zozote za kuvutiwa naye kama ilivyokuwa awali. Tangu Iryn ajifungue, nilihisi mabadiliko makubwa ndani yangu. Hisia zangu zilikuwa zimebadilika kabisa, na upendo wangu kwa Iryn na mtoto wetu ulizidi kuwa na nguvu zaidi. Mambo ambayo yalikuwa yananivutia zamani yalionekana kupoteza maana mbele ya furaha mpya ya familia yangu.

Tulisalimiana pale, na alinikumbuka mara moja, aliniambia alikuwa amepata taarifa kuwa nilikuwa namtafuta. Nilimuomba namba yake ya simu, lakini akasema kuwa mazingira ya kazi hayamruhusu kutoa namba yake ya simu. Alieleza kwamba ni kinyume cha utaratibu kutoa mawasiliano binafsi akiwa kazini. Hata hivyo, aliahidi kunitumia namba hiyo kwa njia nyingine, akisema ataiandika kwenye karatasi na kutafuta namna ya kunipatia baadaye. Baada ya mazungumzo hayo, nilimuaga na nikaenda kulala. Uchovu ulikuwa umechukua nafasi, na nilihitaji kupumzika baada ya siku ndefu.
*****

Kesho yake asubuhi, tulipokea taarifa njema kwamba Iryn alikuwa ameruhusiwa kutoka hospitalini. Kwa haraka, tulijiandaa mapema ili tuwahi kufika hospitali kumchukua. Hata hivyo, kichwani mwangu nilikuwa pia na wazo lingine. Nilitamani sana kuonana na dada yangu na kuzungumza naye kwa undani zaidi, kwani hatukuwa kwenye maelewano mazuri kwa muda. Nilihisi umuhimu wa kuweka sawa mambo baina yetu, kurejesha amani na uhusiano wetu wa kifamilia. Ilikuwa ni siku muhimu sana, si tu kwa ajili ya Iryn na mtoto wetu, bali pia kwa kuweka sawa tofauti zangu na dada yangu.

Saa nne asubuhi, tulifika hospitalini na tukakutana na mzee Virgil, ambaye alitusaidia kumchukua binti yake, Iryn, na kumpeleka nyumbani kwake, wengine tulitumia usafiri wa Uber kufika huko. Baada ya kufika kwenye apartment yake, ambayo ilikuwa na vyumba vitatu, ilibainika kuwa nafasi ilikuwa haitoshi kutokana na idadi ya wageni waliokuwepo pale. Kwa hiyo, mimi na Jimmy tulikubaliana kuendelea kulala hotelini ili kutoa nafasi zaidi kwa wengine. Japokuwa tulitamani kukaa karibu na familia, uamuzi huo ulikuwa wa busara ili kuhakikisha kila mtu anapata nafasi ya kupumzika vizuri.

Mara tu baada ya kurudi nyumbani, marafiki zake wa chuo walifika kumtembelea. Walikuwa wakiingia na kutoka mfululizo, wakionesha upendo na shauku ya kumuona Iryn pamoja na kumpongeza kwa kujifungua salama. Kila mmoja alikuwa amekuja na zawadi, na hakika walimletea vitu vingi sana. Ile hali ya furaha ilitanda nyumbani, na zawadi nyingi walizomletea zilijaza kila kona ya apartment, zikionesha jinsi walivyothamini sana uhusiano wao na Iryn.

Kutokana na idadi kubwa ya watu waliokuwa wakiingia na kutoka kumtembelea Iryn, mimi niliamua kutoka nje na kukaa kibarazani ili kupata utulivu. Nikiwa pale, nilikuwa na Samantha, tukipiga story za hapa na pale. Mazungumzo yetu yalikuwa ya kawaida, lakini kwa upande wake, Samantha alionekana kuwa na jambo muhimu la kuniambia. Aliniambia kwa dhati kwamba dada yake, Iryn, ananipenda sana, hivyo nisije kumuumiza dada yake. Maneno hayo yalikuwa na uzito, na kwa muda ule, nilihisi hali ya utulivu na kuthamini zaidi kile kilichopo kati yangu na Iryn.

Jioni, Jimmy alinipatia wazo la kuondoka kwenye maeneo haya na kutafuta sehemu nyingine ambapo tunaweza kupoteza muda. Alisema kwamba nyumbani kumekuwa na wageni wengi, na kwa sisi wanaume, ilikuwa ni kuchoreshana tu bila maana. Niliona kuwa wazo lake lilikuwa zuri, hivyo tukakubaliana kutafuta sehemu tulivu ambapo tungeweza kuzungumza na kufurahia muda wetu bila bughudha.

Kabla ya kuondoka, nilipata wazo kwamba ningekuwa na busara kuonana na dada yangu ili tuzungumze, lakini alionekana kuwa busy sana, hivyo sikupata nafasi. Saa moja usiku, tuliondoka kimyakimya bila kuaga, tukielekea hotelini ili kubadilika kabla ya kutoka.

Nilikuwa sijui tunakoelekea, hivyo ilinibidi kumuliza Jimmy tutaenda wapi. Aliniambia kwamba tungeenda “Soho nightclub.” Jambo hilo lilinivutia, kwani nilijua ilikuwa ni sehemu maarufu ya burudani, kwani nilikuwaga naisikia tu.

Baada ya kujiandaa, tulikutana kwenye restaurant kwa ajili ya kupata dinner kabla ya kuondoka. Muda wote, tulikuwa kimya, hadi Jimmy aliposikika akilalamika kwa mbali, na ndipo tulipoanza mazungumzo.

MIMI: “Bro, what’s wrong?"

JIMMY: “My texts go green."

MIMI: “What do you mean?"

JIMMY: “I was texting my girlfriend, but she is no longer online."

Nilishangazwa kuona Jimmy akihangaika kuwatafuta wanawake wengine, hasa akiwa na Amara.

MIMI: “Bro, how about Amara?”

JIMMY: “Today she will sleep at my sister's house."

Sikutaka kuendeleza mazungumzo haya, kwani nilihisi ilikuwa si sahihi kuzungumzia mambo hayo. Hivyo, nikaamua kumwambia tuondoke, maana tulikuwa tumemaliza kula. Nilijua ni bora tushughulike na mambo mengine ya burudani zaidi usiku huu.

Tuliondoka na Uber kuelekea Soho, na nilipowasili na kushuka, nilianza kushangaa mazingira ya eneo hili pamoja na warembo walikuwa wakiingia, ilikuwa ni balaa. Baada ya kuingia ndani, nilijikuta nikipagawa kabisa, kulikuwa na warembo wa kila rangi na mtindo. Nilijisemea kuwa duniani kuna warembo wakali sana, na nikaona kuwa Dar es Salaam bado kuna safari ndefu kufikia level kama hizi.

JIMMY: “Bro, umepagawa?” Jimmy aliniuliza.

Nilikuwa nikiwa mbali sana kimawazo, kwani kulikuwa na mrembo mmoja aliyevuta kabisa umakini wangu. Nilikuwa nampigia hesabu kichwani, nikijaribu kufikiria jinsi ningekuwa na nafasi ya kuzungumza naye. Jimmy aliona wazi kuwa nilikuwa nimesahaulika, na alijaribu kunikumbusha kuwa nipo kwenye tukio la furaha.

MIMI: “Bro, this place is insane! another reason why men cheat.”

Jimmy alicheka sana kusikia kauli yangu.

JIMMY: “Naona umevutiwa na warembo wa hapa.”

MIMI: “Ni warembo wakali, lakini bado sijaona wa kumzidi Iryn.”

Jimmy alinyamaza kimya, maana hakutegemea kama ningetoa jibu kama hili na aliniangalia kisha akatabasamu.

JIMMY: “Umevutiwa na yule mrembo?”

MIMI: “Yeah! Yuko vizuri sana.”

JIMMY: “Unataka tumuite hapa?”

MIMI: “Kama kaja na mtu wake si tutaanzisha ugomvi hapa?.”

JIMMY: “Mwanamke yoyote utakayemkuta club ni mali yako. Hata siku moja usije kuogopa, mfate akukatalie mwenyewe. Mwanamke anayejitambua hawezi kuingia club kama hizi, kuna maeneo mengi sana ya kwenda.”

Nilinyamaza kwa sekunde, nikitafakari maneno ya Jimmy. Kwa kweli, alikuwa na pointi nzuri, lakini nilifikiria haraka haraka. Kwa nini Jimmy ananiunga mkono kuhusiana na wanawake wengine wakati nimemzalisha dada yake? Iliniuma kuona kwamba hakuwa na huruma yoyote kwake. Nilijua kuwa mahusiano yanaweza kuwa na changamoto, lakini kwa upande wangu, nilihisi kuwa heshima kwa Iryn ilipaswa kuwa ya kwanza.

MIMI: “Bro, I got your sister pregnant, but you're still supporting me in flirting with other women?"

Bro nimemzalisha dada yako, lakini bado unanisapoti nitongoze wanawake wengine?

JIMMY: “Brother, we are men, and the truth is I can't tell you what to do, even if you're in a relationship with my sister. When you're with Iryn, I'll respect you as my brother-in-law, but when you're with me here, I'll treat you as my friend. That's why, back then, when Iryn told me she loves you and that you're a married man, I didn't want to say anything. I just told her that the most important thing is for her to be happy.”

Kaka, sisi ni wanaume, na ukweli ni kwamba siwezi kukwambia nini cha kufanya hata kama uko kwenye mahusiano na dada yangu. Ukiwa na Iryn, nitakuheshimu kama shemeji yangu, lakini ukiwa na mimi hapa hivi, nitakuchukulia kama rafiki yangu. Ndomana, kipindi kile Iryn aliponiambia anakupenda na kwamba wewe ni mume wa mtu, sikutaka kusema lolote. Nilimwambia tu cha muhimu ni awe na furaha."

MIMI: “Bro, really?”

JIMMY: “Just be free when you’re with me, and don’t pretend you’re not a cheater. The most important thing is to make sure you’re very careful, don’t let them know that you cheat on them. Remember, you now have two women, and both of them love you.”

Tulinyamaza kwa dakika kadhaa wakati dada akitufungulia vinywaji vyetu, na baada ya kumaliza kazi yake tulianza kunywa, tukaendelea na maongezi yetu.

MIMI: “I still can’t believe whether Iryn really loves me.”

Jimmy aliniangalia, kisha akaipeleka glass yake ya kinywaji na akaanza kufunguka pale;

Ndugu yangu, naona kuwa hujikubali, lakini nisikilize kwa makini. Wewe ni mmoja wa watu muhimu sana katika maisha ya Iryn, na nakushukuru sana kwa yote uliyofanya kwa dada yangu. Kuna siri nyingi ambazo huenda Iryn bado hajakuambia, lakini leo, nitazungumzia hapa.

Tangu mamdogo afariki (mama Iryn), maisha ya Iryn yalibadilika sana, ni kama alichanganyikiwa na hakuwa katika maelewano mazuri na baba yake. Ukweli ni kwamba, hata familia yetu kwa ujumla haikuwa na maelewano na mzee Virgil kutokana na siri kubwa aliyokuwa ameificha kwa muda mrefu.

Iryn alianza kukutana na Isabella, na hii ilipelekea kutengeneza urafiki wa karibu sana. Unaweza kujiuliza, Isabella ni nani? Ni jirani yetu kule Ethiopia-Bahir, na ni mrembo maarufu sana nchini Ethiopia, pia ni International bi***ch. Huyu ndiye aliyemuingiza Iryn kwenye biashara za massage na kuanza kumpa connection za wateja.

Nilijua Iryn alijiingiza kwenye biashara hizi kupitia Isabella, maana mwenyewe ndiye aliyeniambia, kwani ni Ex wangu. Kwa sababu namjua vizuri Isabella ni nani, nilihofia kwamba dada yangu anaweza kuendeleza tabia kama za Isabella. Hivyo, ilibidi nimpigie simu Iryn na kumuomba tuonane, maana kipindi hicho alikuwa ameenda Ufaransa.

Baada ya kuonana na Iryn, nilimshauri sana aache hizi biashara na aje tusaidiane kuisimamia organization. Hata hivyo, alinikatalia na kuniambia hataki kazi zitakazompa stress, kwani biashara ya massage inamuingizia pesa nyingi sana.

Ingawa yeye alichukulia biashara ya massage kama kazi nyingine, kwa upande wangu, nilichukulia tofauti, niliona ni kazi ya kujiuza tu. Kutokana na suala hili, mimi na Iryn tuligombana sana siku hiyo, na nilimuacha aendelee na maisha yake.

Mwishoni mwa Februari 2021, nilikutana na Iryn nchini Ufaransa, na alikuwa na bwana wake (Griezmann), ambaye alinimtambulisha kwangu. Habari kubwa aliyonambia ilikuwa kuhusu mpango wake wa kurudi Tanzania, kutuliza akili na kufuatilia mafao aliyoacha mama yake.

Nilimshauri afanye hivyo maana ni jambo zuri, ukizingatia kwamba mama yake alifanya yote haya kwa ajili yake. Kabla ya kuondoka kwenda Tanzania, alikuja Bahir na kukaa kwa wiki moja, kisha akaondoka kuelekea Tanzania na alifikia kwa mama Janeth. Licha ya kuja Tanzania, bado aliendelea na biashara zake za massage kwa siri. Sikutaka kumpangia chakufanya kwenye maisha yake, hivyo nilimuacha aamue mwenyewe kuhusu maisha yake.

Mara ya kwanza tulipokutana Dar es Salaam, nilihisi Iryn anakupenda, ingawa alinikatalia kabisa nilipomuuliza. Baada ya miezi miwili, alinipa taarifa kuwa mpo katika mahusiano na ameamua kuacha biashara yake, yote kwa sababu yako. Alisema anakupenda sana na kwamba wewe ni mwanaume wa tofauti sana, hivyo anawaza kukupa zawadi ya mtoto. Kwa upande wangu, nilimwambia afanye maamuzi ambayo anaona ni sahihi kwake, lakini sikujua kama hakukushirikisha kuhusu hili. Hata hivyo, nilikuwa najua mipango yake.

Brother, wewe umechangia sana katika kubadilika kwa Iryn na kumuweka sawa kama zamani. Hata suala la mimba, niliwaambia nyumbani kwamba wewe ndiyo sababu Iryn kuwa na furaha, hivyo tumuache afanye anachoona kwake ni sawa.

Nimekwambia haya yote ili ujue kwamba unathamani kubwa sana kwa Iryn. Upendo na uaminifu wako kwake vimefanya akupende sana na kukuamini. Mimi kama kaka yake, nakushukuru sana na ninakupa heshima yangu. Hata kama utakuja kuachana na dada yangu, bado tutaendelea kuwa pamoja.


Tuliongea mambo mengi sana na Jimmy kuhusu Iryn. Kwa upande wake, alinifungukia vitu vingi, hadi kuhusu lifestyle yake, hivyo nilifahamu mambo mengi kupitia kwake. Alisema ameamua kuniambia haya yote kwa sababu ananiamini sana.

Baadaye, Jimmy alitoka na akarudi na mwanamke mzuri, ambaye alinitambulisha kama girlfriend yake. Tulikaa hadi saa 7 za usiku, na tukashauriana na Jimmy tuondoke maana muda ulikuwa umeenda sana. Tuliondoka kurudi hotelini ambapo Jimmy alikuwa na pisi yake.

Saa tano asubuhi, Jimmy alikuja kunigongea mlango na kunitaarifu kwamba Iryn amepiga simu nyingi na ameanza kumpa lawama kwamba ananifundisha tabia mbaya. Jimmy alisema nijiandae haraka ili tuende kwa Iryn maana anatuhitaji. Nilikuwa nina uchovu sana, hivyo niliingia bafuni kuoga haraka na kujiandaa. Nilipowasha data, nikakuta missed calls nyingi kutoka kwa Iryn na dada yangu, nilihisi huko kuna kitu, nitajua nikifika.

Tuliondoka kwenda nyumbani kwa mama mtoto, na ndani ya muda mfupi tulifika. Baada ya kuingia ndani, nakutana uso kwa uso na mama yake mkubwa, akiwa amemshika mtoto, na tukaanza kuangaliana pale.
Imeishia patamu
 
Umeonae, nimependa unavyoweza kusema ukweli. Wengi humu hawawezi kusema/kutambua huo ukweli, wanabakia tu kuomba omba.

Insider atajidai ooh nna kazi zingine, kwanza hamnilipi, anasahau hatukumwita wala kumtumia barua ya maombi.. we are all here for fun.

Naturally tu mtu smart anatakiwa aseme tu, jamn nimebanwa itakuwa mpaka siku flan, au aweke tu ratiba inayoeleweka.

Huyu bwana mdogo ana nyodo za mwali
Jitulize wewe Mwanaume mzima kujiliza kwenye thread za watu, unataka uombwe radhi wewe kama nani?? unamlipa?? unajua raiba zake?? punguza genye kaa kwa kutulia
 
Back
Top Bottom