Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

EPISODE 13

TUNAENDELEA………….

Jumapili niliamka mapema sana nikaenda Sokoni nikanunua Jogoo mkubwa wa kienyeji aliyenona vizuri, nikanunua stake ya nyama 2kg, nikanunua maini 2kg, nikanunua matunda, nikanunua mayai ya kienyeji tray 1, nikanunua na mchele safi ule OG wa kyela 5kg, nikaelekea kwa Iryn.

Nilifika pale saa 2 asubuhi na Iryn alikua kaamka anafanya usafi wa ndani. Nikatoa vitu kwenye gari nikaingiza jikoni, alifurahi sana hii siku kama nilimsaprize na alinishukuru sana pale.

Baada ya kupata chai ile asubuhi tukaondoka kwenda kufanya shopping ya vitu. Tulikwenda moja kwa moja Mlimani city na tukaenda Shoppers.

Tulifanya shopping na hii siku alinunua vitu vingi sana vya jikoni, alinunua vyombo, na mazaga mengine mengi. Tulitoka hapo tukaingia duka la michezo akanunua vifaa vya michezo kama track, kamba za kuruka na vitu vingine vingi.

Baada ya kumaliza shopping tukaanza kurudi home. Tulirudi home na muda huo tukaingia jikoni. Nilimsaidia kumkata kata kata yule kuku vipande, na yeye alikua akiandaa vitu vingine.

Mimi kuhusu mambo ya jikoni niko vizuri sana, sasa nilikua namsaidia kazi nyingi sana mle jikoni huku tunapiga story.

IRYN: “Insider haya mambo umeyajulia wapi wewe?”

MIMI : “Mama yangu alikua ananifundisha toka nikiwa mdogo na pia nilikua najifunza mwenyewe ukubwani.”

IRYN : “Upo vizuri natamani nipate mwanaume kama wewe, mke wako atakuja kupata raha sana.”

MIMI : “Hata wewe pia naona uko vizuri sana, nilikua nakuchukulia poa ila umekamilika kuanzia uzuri, pesa, mpaka jikoni.”

IRYN : “Nataka leo nikupikie Pilau ambalo hujawai kula.”

MIMI: “Heshima yangu kwako leo imefika Nyota 5.”

IRYN: “Insider mimi sio kama wale mnaowaita slay queens tuheshimiane”

Muda huu nilikua nakataka vitunguu, nyanya, karoti na hoho, Iryn alikua ananiangalia sana huku anatabasamu. Ni kama alikua haamini macho yake mwanaume anayefanya yale mautundu ndo mimi Insider. The way tulivyokua kule jikoni akija mtu angesema sisi ni wapenzi hata Mama J angeona asinge weza nisamehe.

Muda ule tulisikia mtu akigonga mlango, Iryn alikwenda na baada ya dakika 3 alikua karudi na cake. Ni jiran ambaye alikua amezileta na zilikua tamu sana zile cake.

MIMI : “So Iryn hapa toka uhamie una muda gani?”

IRYN: “Hapa nimeamia mwaka jana mwezi june”

MIMI: “Na ulikuja lini Tanzania?”

IRYN: “Toka utokee msiba wa mama sikuwai kupanga kurudi Tanzania tena, kwa sasa ningekua zangu Ufaransa. Nimerudi Dar es salaam April mwaka jana.”

MIMI : “Chanzo cha kurudi?”

IRYN : “Insider Mama kabla ya kifo chake alinisisitiza sana nizisimamie biashara zake. Pia alinipa Diary ambayo inasiri nyingi sana, pia niligundua mama alikua ana nyumba 2 hapa Dsm alizoziacha. Pia nafatilia mafao ya mama aliyoacha kule kazini kwake, maana mama aliniandika mimi kama mrithi wake so ni pesa nyingi sana Insider. Sitaki kumuudhi mama yangu huko aliko nataka nivienzi na kuviendeleza alivyoviacha.”

Hapo ndo nikajua kumbe Iryn mama yake alimwachia urithi binti yake, pia baada ya kifo chake Iryn aliingiziwa kama 150million za rambirambi na michango kutoka kwa wafanyakazi wa Mama yake, vikundi mbalimbali na Organization. Pia mazishi ya mama yake yaligharamiwa na Organization.

MIMI : “So umeweza kuzijua mali zote alizoacha mama?”

IRYN : “Yeah pia Mama alikua na kampuni ya usafi ambayo anashirikiana na rafiki yake (Mama Janeth). Hii natakiwa kuchange Director name niweke Jina langu lakini nitaacha Mama Janeth aendelee kuisimamia mimi nitakua nakwenda kwenye vikao muhimu. Pia kule Masaki kuna Saloon nyingine ambayo nayo wanashirikina na Mama Janeth sijataka kuziingilia kabisa, as long as I get my profits no problem naona Mama Janeth aendelee kuzisimamia. Mama Janeth, pia ndo kama Mama mlezi wangu kwa sasa.”

MIMI: “Kama Mama Janeth unaona ataweza zisimamia acha aendelee wewe simamia hizi ambazo mama alikua anatumia kampuni yake binafsi.”

IRYN : “Insider hata hivyo mama alikua ananipenda sana, nilikuja kujua alikua anaweka akiba ya 30% kila mwezi kwa ajili yangu. Mama kama aliona future yake.”

MIMI : “Mama kweli alikupenda, alikutengenezea njia. You have to make her proud Iryn”

IRYN : “I promise”

MIMI: “But nina ushauri, ulisema Baba anakutafuta muongee kwanini usimpe nafasi Baba yako?. Msikilize ujue anataka kukuambia nini, pia kumbuka Baba ndo only hope you have now. Naamini Baba yako anakupenda sana, na kitendo cha kutowasiliana naye atakua anajiskia vibaya sana.”

Muda huo mimi nikamsogelea yeye alikua amekaa kwenye kiti nikazunguka nyuma yake nika mshika mabega yake kama vile nayasugua.

“Iryn mtafute Baba msikilize anataka kusema nini, najua alimkosea sana mama yako mpaka kumsababishia kifo, lakini naamini alimwomba msamaha mama yako. Sisi binadamu hakuna aliyemkamilifu mbele za Mungu sote ni wakoseaji, naamini huko Mama yako aliko atakua anatamani muyamalize na Baba yako. Huu ndo ushauri wangu kwako Iryn.”

Nilivyoona amekaa kwenye kiti haongei kitu nikawaza nitakua nimemkwaza, maana Iryn mkiongelea story za mama yake alikua anabadilika sana.

“Huu ulikua ni ushauri wangu kwako kama nimekukwaza naomba nisamehe Iryn”

Muda huo nilikua nimemwacha nimeanza kwenda seblen

“Insider………”

Bhasi Iryn akasimama akaja spidi akani-hug akawa analia. Ofcoz na mimi upande wangu nilianza kujiskia vibaya sana.

“Insider nashukuru sana kwayote unajua toka nimekutana na wewe naona lifestyle ya maisha yangu inabadilika tararibu. Wewe ndo mtu pekee ambaye tunakaa tunaongea masuala ya maisha na mambo mengine mengi. Wewe ndo mtu pekee ambaye tunakua wote kwa muda mwingi, wewe ni moja ya rafiki zangu muhimu sana. Nimetokea kukuamini sana kwa muda mfupi sikutegemea kuna siku ningekua na mtu wa karibu hapa Dsm kama wewe.”

Bhasi nikamwangalia nikamfuta machozi na vidole vyangu nikaenda seblen.

Ile nimefika sebleni kucheki simu nakuta missed calls (3) za Prisca alikua pia kanitumia na message juu. Ikabidi nisome ile message na ilikua inasema:

“Insider mbona hupokei simu zangu? Toka jana tumeachana hata kunijulia hali hakuna. Unajua mimi naumwa, nataka unipeleke hospital.”

Nilikua pale kwenye coach nikajisemea kwa hii spidi ya Prisca nikimfanya mchepuko wangu atanisumbua akili sana na atakuja kuniletea matatizo kwa Mama J. Palepale nikamwandikia:

“Am sorry. Jana wakati tumeachana nilikwenda kwa mamdogo nikarudi night sana, nimemka sio muda mrefu sana na niko huku Bunju bado. Sitoweza kukupeleka Hospital kama nitawai kurudi nitakuja kukuona.”

Ofcourse ile show nilompelekea tena ya kibabe na hasira, nilijua kwa mtoto laini kama yule ambaye hajaizoea mikiki lazima angepata homa tu.

Muda ule niko seblen, Iryn alikua ameshaanza kuandaa chakula mezani na mimi nikatoka kwenda kumsaidia kukata matunda.

Hii ndo siku ya kwanza naonja mapishi ya Iryn kiukweli lile pilau lilikua ni tamu sana, pilau lilikua na mixer ya maini afu kuku walikua wa kuroast. Kile chakula kilikua kitamu sana, kweli nikaamini Iryn hata kwenye mapishi yuko vizuri sana. Na muda huo nakula alikua ananiangalia kama mtu ambaye akisubiri nitoe neno.

MIMI: “Mama upo vizuri sana nilikuachukulia poa ila nimekunyooshea mikono.”

IRYN : “Si ulikua unanidharau?, mimi sijaamua tu kuingia jikoni.”

MIMI: “Ulijifunzia wapi haya mapishi maana hili pilaua ni tamu sana.”

IRYN: “Nimejifunzia chuo mapishi mengi sana hasa ya Ufaransa kama hili pilau nimelipika kifaransa. Wakati niko chuo nilijiunga na CLUB za Catering, Dancing na Gardening. Na nilipata Certificates kwenye CLUB zote pale chuoni.

MIMI : “So hizo CLUBS ni kama short course au?”

IRYN : “No tuseme ni kama Extracurricular activities. Pale chuoni kulikua na CLUBS nyingi sana wewe unaamua ujiunge na zipi na ilikua hutakiwi kujiunga zaidi ya 5. Na zote mnaingia darasani mnafundishwa na mnafanya practical, mfano kama mapishi najua kupika mapishi mengi sana na yote nilifaulu. Najua kupika mapishi mengi ya Europe, pia upande wa Gardening tumefundishwa jinsi ya kuandaa garden, kupamba maua na kumbi za sherehe. Hapa Tanzania sijaona garden ilopambwa vizuri labda kwa Masaki na Oysterbay kidogo atlist. Kuna mbinu za kutengeneza Garden Insider, na plan mbeleni huko kuanzisha kampuni yangu ya upambaji na utengenezaji wa Garden naamini nitapata sana hela.”

Muda huo akawa ananionesha picha za Garden walizokuwa wanatengeneza chuo na zile za Mapishi.

MIMI: “Vipi kuhusu Dancing”

IRYN : “Dancing tumejifunza dancing nyingi sana especially za Europe mfano minuet, Tarantella, Ballet, waltz dance nknk “. Na hizi Dance zinatumika sehemu tofauti kulingana na mazingira. Na ninajua dance zaidi ya 20.”

MIMI: “Mwalimu naye anakua anajua kucheza kabisa?”

IRYN : “Ndio mwalimu lazima ajue kucheza na pia kuna clip videos ambazo tunakua tunaangalia class. Yaani kama kukata mauno unafundishwa stage kwa stage, tofauti ya mauno ya Africa na Europe ni kwamba wadada wa Europe mauno yao ni ya mapozi yale ya taratibu ila Waafrica anazungusha kama pia. Wazungu wanasema ni uchafu na fujo, kiuno kinatakiwa kuzungushwa taratibu huku unashuka chini kwa mapozi huku umelegeza macho.”

MIMI : “Aah aisee ni noma, wazungu wameendelea sana haya mambo Bongo vyuoni hakuna kabisa.”

IRYN : “Wenzetu vyuo vyao vinakufundisha na ujasiriamali kama hapo ukimaliza chuo unaweza kwenda kuajiriwa hata na Restaurant au Garden yoyote ile na ukapata hela. Tanzania hawatoi elimu za ujasiriamali kwa vitendo.”

MIMI: “Tanzania bado tunasafari ndefu sana.”

IRYN : “Mimi nimesoma International Business Administration lakini tumefundishwa jinsi ya kubehave as Managing Director, tunafundishwa jinsi ya kudress, jinsi ya kuongea na customers au wafanyakazi na viongozi wa nchi nknk. Na tulikua tunafanya practical, ukizingua course una carry. Unafundishwa pia jinsi ya kuwa confident unavyokuwa kwenye vikao, vyombo vya habari na jinsi ya kutuma mails na kuongea kwenye simu. Insider kama unataka mtoto wako apate elimu bora mpeleke akasome nje.

Tuliongea mambo mengi na hapo nikajua kumbe Iryn ana Bachelor ya International Business Administration, zaidi ya hapo pia ana ujuzi mbalimbali.

Baada ya kumaliza kula nilimshukuru kwa chakula na mimi nikatoa vyombo mezani na kupeleka jikonii na palepale nikaanza kuviosha.

Iryn aliniaga anakwenda kulala na mimi muda huo nikasema nimpigie simu mama J. Nilipiga simu lakini hakupokea, nikasema acha nimwache mwanamke ukimlazimisha atakusumbua acha atanitafuta mwenyewe.

Mzee pia alinipigia simu kupitia “Whatsapp call” na tuliongea sana, moja ya maongezi yaliyonifurahisha ni pamoja na Mzee kunambia ameshachora ramani ya nyumba. Baada ya mazungumzo haikuchukua sekunde akanitumia ile ramani. Niliipenda ile ramani sababu mzee alikua ameidizaini vizuri sana, licha ya kujenga hizo nyumba 2 za vyumba viwili bado kuna eneo kwa juu ningeweza kujenga chumba na sebule hapo baadae. Pia kulikua na sehem ya kujenga tank la maji na parking ilikua kubwa.

Nililala pale kwenye coach, Iryn ndo aliyekuja niamsha na muda huo ilikua tayari saa 1 kasoro usiku. Hii siku Iryn alipanga nimpeleke Kidimbwi akasafishe macho na alitamani sana kufika eneo hili.

IRYN : “Insider amka kajiandae bhasi”

MIMI : “Wewe uko tayari?”

IRYN : “Bado kuvaa tu.”

Kama mnavyojua wanaume hatunaga mambo mengi, nilikwenda kwenye gari nikatoa kibag changu, nikatoa pamba zangu. Ndani ya muda mfupi nilikua niko tayari nikimsubiri yeye.

Haikuchukua muda na yeye akawa ametoka tukaondoka kuelekea Kidimbwi. Tulifika pale kwenye saa2 na tulipark gari sio mbali sana na geti la kuingilia ndani. Palepale Masai sijui alitokea wapi akaja kugonga upande wangu.

MASAI: “Bossy usipark gari hapa, kuna mtu anakuja kupark”

Iryn akadakia maongezi yetu…

IRYN: “Masai huyo mtu yukowapi? Mbona simwoni”

MASAI : “Amenipigia simu anakuja nimwekee parking.”

IRYN : “Bhasi utamtafutia eneo lingine sisi tunapark hapa. Na anakulipa sh. ngapi?”

MASAI : “Ananilipaga 3,000”

IRYN : “Ok mimi nitakupa 10,000, pia naomba uilinde hii gari, sawa?”

Muda huu tulikua tumeshashuka sasa mimi nina lock mlango wa gari.

MASAI : “Sawa haina shida Bossy”

Masai akanambia bro una demu mzuri sana wewe ni noma, dizaini kama Iryn alisikia yale maneno ya Masai, japo masai alikua akiongea kwa sauti ya chini. Nlimpiga jicho Iryn aliishia kutabasam na kutingisha kichwa cha kusikitika.


Tulivyoingia ndani ya eneo la tukio walionekana watu wakiwa wamekaa kaunta, wengine kwenye viukuta, wengine wakitoka na kuingia, kwa mbele kaunta zilionekana screen watu wakiangali mpira, mambo ya EPL.

Wakati tunasogea kuna dada akawa ameshakuja kutuwahi

“Karibuni guys mmependeza sana”

IRYN : “Thank you. Nataka tukae sehem ambayo imetulia lakini ina vibe”

“Sehemu nyingi zimechukuliwa na zingine ziko reserved.”

MIMI : “Dada najua huwez kosa sehemu ya kutuweka, wewe fanya mambo tutakufurahisha sana.”

“Sawa nisubirini hapa nikawaandalie sehem nakuja kuwachukua”

Muda huo Iryn macho yote yalikua yakiitizama hili eneo kwa umakini sana. Kwa upande mwingine tulikua tukipigwa sana macho na watu mbalimbali. Na sisi tulikua tumekaa kwenye kiukuta pembeni ya kaunta.

IRYN : “I love this place, watu kuwa wengi hivi kutanifanya nisiipende.”

MIMI: “Wewe ni certified ANTISOCIAL siwezi kukushangaa”

Akanipiga na kibao cha pajani

Na muda huo dada alikua kafika kutuchukua na kutupeleka kwenye meza yetu. Ilikua ni meza ya duara iliyounganishwa na mlingoti na viti virefu vya kukaa, na pale kulikua na viti vinne vya mzunguko.

“Mtakaa hapa kuna wengine watakuja watakaa na nyinyi kwa upande huu”

IRYN: “Hapa nimepapenda pia pako karibu na DJ nitavibe. Insider ulishawai kutumia Moet?”

MIMI : “Hapana but naskia ni sweet”

Muda huu dada waiter alikua akitabasamu sana..

IRYN : “Ni kama champagne ila ni nzuri sana. Dada naomba tuletee ile Moet Imperial Rose.”

MIMI : “Usisahau maji ya kunywa chupa kubwa na pia usilete Moet na yale mataa yenu, hatuko kuuza sura hapa.”

“Sawa haina shida msijali”

Hivi viwanja vikubwa ukinunua vinywaji vya gharama huwa vinaletwa na watu special wameshika mataa yao, sikuhizi wanaandika na jina la mnunuaji.

Baada ya muda mfupi dada alikua kaleta vinywaji na tukaanza kupeleka taratibu maana ilikua mapema sana na eneo halikua na watu kihivyoo. Muda ule tuliendelea na story taratibu

IRYN : “Insider Kuna jambo inatakiwa ulifahamu”

MIMI : “Jambo gani hilo?”

IRYN: “Ipo hivi kuna jambo sikukwambia Insider nataka leo nikuweke wazi. Grizz mwakajana December alinipa pesa ndefu tu ninue gari, sasa mimi sikutaka kuikataa pesa yake. Mimi kama unavyoniona sina mpango wa kununua gari kwa sasa naona itaniletea shida tu, hata ningenunua ningeishia kuipark sina mpango na gari kwa sasa. Nilivyoona gari yako nzuri na inavutia ndo nikapata wazo niwe nakutumia kama my driver. Grizz anajua hilo gari ni yangu na anajua wewe ni dereva wangu nimekuajiri.”

MIMI: “Mimi sina shida kabisa Bossy wangu.”

IRYN : “Ile siku ambayo hatukwenda wote, Grizz aliniuliza nakulipaje mshahara nikamwambia kama tulivyokubaliana kwa mwezi 1,200,000/= (Tulikubaliana na Iryn kwa weekend ni 300,000). Na yeye aliuniuliza nimeshakulipa kiasi gani, nikawambia nimeshakulipa miez 2 tayari ambayo ni 2.4 million. Grizz akasema suala la mshahara wako litakua chini yake na akasema atanirudishia pesa niliyokuwa nimekulipa na atatoa pesa ya mwezi huu. Alivyonipa ile bahasha kuhesabu zile pesa zilikua ni Euro 1,500 lakini mimi sikutaka kutoa kiasi chochote pale niliamua kukupa.

MIMI : “Thank you lakini ulikua ushanilipa kwanini usingetoa? Ungeacha hata ya mwezi huu, mimi nilijua ni zawadi kutoka kwa Grizz.”

IRYN : “Insider natambua wewe pia unamajukumu sana japo bado hujaniweka wazi kuhusu maisha yako, lakini mimi nikikutizama naelewa. Hiyo pesa kwangu sio ya kuni fanya nikakosa ubinadamu. Kwa muda ambao tumefanya kazi na wewe nimeingiza pesa nyingi sana, na pia huwa najiskia vibaya unavyonisubiri usiku hata kama ni kazi yako lakini umejitoa kwangu.

MIMI: “Niseme tu Ahsante sana kwa yote, niseme ukweli toka nikutane na wewe umekua ukinijali sana. Unanifanya niendelee kuvimba hapa mjini, naomba usinilipe mpaka thamani ya hii pesa itakapotimia.”

IRYN : “Insider sisi tushakua familia tayari, ni muda muafaka wa kuniweka wazi kuhusu maisha yako. Sijui historia yako, najua unaishi Mbezi lakini sikujui kwako, wewe unakuja kwangu mimi kwako sikujui what Kind of friendship do we have?”

Palepale nikawaza sijui nimwambie ukweli kama nina mke na mtoto. Nikaona kama mapema sana, lakini nikapata wazo siku nitamsaprizi nitamleta kwangu.

Na muda huo dada alikua amekuja kutuuliza kama tunahitaji chochote, bhasi tukaagiza portion 2 za mbuzi choma.

MIMI: “So Grizz alishaondoka?”

IRYN: “Alishaondoka,unajua Grizz anakukubali sana Insider.”

MIMI : “Kwanini unasema hivo?”

IRYN: “Ile siku ambayo tulikwenda kule Oysterbay na ukaanza kuchoma nyama na kujichanganya nao, bhasi Grizz anasema ni Waafrica wachache ambao wanajiamini kama wewe.”

MIMI: “Hahaaha unajua Iryn haya maisha sometimes ni kujitoa ufahamu tu, siku ile niliona hawajui kuchoma nyama ikabidi niwasaidie.”

IRYN : “Sasa Grizz hapo ndo alipokukubali na alisema next time akija tutafanya party ya kuchoma nyama tu.”

MIMI : “Mimi sina shida tena hio siku nitawaonesha mautundu yangu yote”

IRYN : “Unajua ile siku uliyolala home wakati tumetoka Samaki samaki tulikua tumelewa. Mimi hata sikuwa nimelewa I was just pretending. Hata tulivyofika home ukanipandisha kitandani nilikua na akili zangu zote, ukanivua koti nilikua nakuangalia tu. Baada ya kutoka pale ulirudi seblen baada ya dk15 mimi nilitoka kukuangalia nikaona umelala na mimi nikarudi kulala. Nilikufanyia makusudi ili nijue wewe ni Mwanaume wa aina gani na toka siku ile unaona ukaribu wangu kwako umeongezeka.

MIMI: “Aisee yaani kumbe yale yote nililokuwa nafanya ulikua unaoana.”

IRYN: “Yes, nilitaka kujua wewe ni Mwanaume wa aina gani ila nikajua wewe ni More than Gentleman. Insider Kitendo cha kunywa pombe na kutokunifanya chochote nili realize wewe sio mtu mwenye tamaa na ni wanaume wachache sana wenye tabia kama yako.

MIMI : “Hata ile siku ungenitaka kimapenzi nisingekukubalia kabisa”. (Nilimjibu hivo kuonesha uzuri alionao hauni babaishi)

IRYN : “I’m proud of you. Jumanne tutakwenda kwa Mama Janeth Masaki kuna mambo natakiwa kuongea naye.”

MIMI : “Sawa haina shida utanambia tu muda wa kwenda.”

Hapa ndo nikajua kumbe nilikua nimewekewa mtego kama ningekua natabia za kifisi kama wale wazee wa kula Kimasihara bhasi kibarua kingeota nyasi.

IRYN : “Insider I need your company nataka kwenda washroom, huko njian nitasumbuliwa sana.”

Na mimi hata sikutaka kumgomea na pale kwenye table alikuwepo jamaa na dem wake tukaomba watuangalizie. Na muda huo watu walikua wengi sana ilikua saa4 tayari na watu walizidi kumiminika pale.

Nilimpeleka Iryn mpaka washroom na mimi nikazama upande wa “Gents” kupunguza mafuta. Nilitoka nikawa namsubiri kwa pale nje, na baada ya dakika kadhaa akawa ametoka. Sasa ile tunarudi macho ya mafisi yalikua yakimwangalia sana Iryn na macho ya madem yalikua kwangu.

Tulirudi kwenye meza yetu kuendelea na vinywaji na muda huo dada alikua ameshaleta zile portion za mbuzi. Iryn akaagiza Moet nyingine kama ileile kwa dada. Moet ina kilevi cha 13% ndomana mademu wanazipenda sana afu pia ni sweet.

Muda ule nilikua nawaza jinsi ya kumuingia Iryn kuhusu suala la Muajemi, lakini nikasema acha kwanza moet imkolee. Na muda huu DJ alikua kashaanza kuchanganya mangoma, dizaini kama vibe lilianza kupanda.

DJ aliipiga ngoma ya “Ruger-bounce” na palepale Iryn alitoka kwenye kiti akaanza kukatika taratibu, yaani ni alikua anakata kiuno kwa mapozi, taratibu alikua anashuka chini kwa beat na kupanda. Nilipigwa na butwaa maana nilikuaga namchukulia simple sana, hata jamaa na dem wake ilibidi wawe wanamwangalia.

Majirani wa karibu walianza kuyaelekeza macho kwake jinsi alivyokua akikata kiuno kwa mpangilio. Nafikiri walishangaa sana kuona mrembo mzuri kama yule anajua kukata mauno, na muda huo dada alikua ameleta moet tayari.

Kilikua ni kitendo cha dakika lakini was amazing, kiliweza kuteka attention ya watu pale. Nikamwambia naona umeamua kuniprove wrong, sina cha kusema tena. Niseme tu nakuongezea nyota zingine 5 ziwe 10.

Hii siku Iryn alikua na furaha sana maana vibe alilokua nalo ni hatari. Aliendelea kucheza na mimi nilikua nikimsapoti kwa kumshika kiuno na kumbambia.

IRYN: “Insider unajua ni muda sana sijatoka out kama hivi, last time kuenjoy hivi ilikua ni Ufaransa.”

MIMI : “Mara moja moja inatakiwa uwe unatoka unafurahia maisha. Unajua kukata mauno asee sikupatii picha kwa bed.”

IRYN : “Pombe zimeanza kukuingia eeh.”

MIMI : “Unakumbuka hata kule Coral unikazia namba ya yule mzungu ulisema nimelewa.”

IRYN : “Kumbe husahau tu..”

MIMI: “Kuna jambo nataka nikwambie kuhusu yule Mwarabu wa siku ile unamkumbuka?”

IRYN: “Yeah. Kwani mnawasiliana naye?”

MIMI : “Exactly, alichukua my number that day. Hata hivyo sio Mwarabu ni Muajemi.”

IRYN : “Nakusikiliza , Go on”

MIMI : “Alinipigia simu akaomba tuonane, nikamwelezea Iryn mkanda mzima wa siku ile. Muajemi ana connection nyingi sana anaweza kukusaidia hasa kwa dubai anaonekana sio mtu wa kawaida. Yeye alikua anaomba muonane tu, sijui anataka muongee nini.

IRYN : “Do you trust him?”

MIMI : “Ofcourse, he can be strusted”

IRYN : “Ok will discuss about this”

Muda huu aliomba nimpe tena company anakwenda toilet, nikampeleka nikamsubiri tukarudi mezani. Ofcourse kwa yale mazingira angekua anakwenda peke yake angesumbuliwa sana na wahuni. Na Iryn ni kinda ya mwanamke ambaye hapendi sana kusumbuliwa au kusimamishwa anaonaga kama ni dharau.

Tulikaa pale mpaka saa8 tukaamua tuondoke, alikuja dada na bill, nakumbuka bill ilikua 573,000/= Iryn alilipa na akampa dada 50,000 ya huduma yake. Dada alishukuru sana ni kama hakuamini na akaomba next time tuwe tunamtafuta yeye alitutajia jina. (Huyu dada ni rafiki yangu mpaka sasa navyoandika hapa, nikienda pale Kidimbwi huwa ananipa huduma yeye).

Tulivyofika pale getini Maasai baada ya kutuona akaja chap, sababu niliskia muda ule Iryn anasema atampa elfu 10, bhasi nikatoa nikampa. Masai alifurahi sana na Iryn akamwambia next time nikija ole wako ulete uswahili.

Nikamshukuru Iryn kwa out then nikawasha gari tuondoke tukalale, wakati tumevuka geti la Kidimbwi kuna gari ilikuja kwa spidi sana na ikatugonga “BOOM”. Ilisikika sauti ya Iryn “Mamaaaa…….”.

TO BE CONTINUED……….

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
Hii story inafanya niitamani kazi ya uber... Ila akili ikirudi kwenye uhalisia napotezea
 
SEASON : 02
CHAPTER 8
“A TRUE STORY BY INSIDERMAN”

PREVIOUS
Baada ya game kuisha hatukukaa sana tukaondoka kurudi home na wife ndo alikuwa wakwanza kushuka kwa gari. Muda huu niliikumbuka ile voice ambayo nilikuwa nimerecord kule hotelini, hivyo niliona ndo muda sahihi wa kuisikiliza.

CONTINUE

Niliangalia tena kama kuna usalama na nili-lock gari nikaanza kuisikiliza ile voice na ukweli nilikuwa nahamu sana ya kujua mazungumzo yao. Nilifanikiwa kuiplay na haya ndo yalikuwa maongezi yao na zaidi ya 90% yalikuwa kwa kiingereza,

CLAIRE: “Baby vipi kuhusu mimba yako, so unakwenda kuwa mama? You said you don’t trust him.”

IRYN: “Huyu mtoto nimempa zawadi Insider, kama atafanya ujinga ni juu yake.”

CLAIRE: “Ulikuwa unalalamika Insider ana mahusiano ya siri na moja ya wafanyakazi wako, mimi naona Insider atakusumbua tu best yangu. Hio mimba bado ni changa sana you can abort before it’s too late, Insider loves you because you are a rich and nothing more, listen to me."

IRYN: “No Claire Insider hana habari na Pesa zangu hakuna hata siku alishaomba pesa kutoka kwangu na juzi tu hapa amenambia hataki tumlipe mshahara maana ni dharau kwake. Kuhusu kunipenda hili naweza ku-agree Kuwa Insider huenda hana mapenzi kwangu lakini ana mapenzi kwa huyu mtoto tumboni.”

CLAIRE: “Mwanaume kama hana mapenzi kwa mama how come awe na mapenzi kwa mtoto? Acha kujidanganya, haimake sense kabisa na ukizingatia Insider ni mme wa mtu tayari, fanya maamuzi magumu kabla ya mambo kuharibika. Usipokuwa makini utaweza poteza familia yako pamoja na ndugu zote na bado Insider akakupiga na kitu kizito, ukajikuta unarudi ulikotoka na majuto juu.”

IRYN: “Remember, Insider is the only one who cared about me during that bad time, and now you're talking shit about him?"

CLAIRE: “I know you love him lakini kubali kupokea ushauri na kumbuka sisi ni marafiki tangu utotoni, sitapenda kuona best yangu unapata shida hapo baadae. Una miezi 9 ya kulea tumboni bado una miaka 3 ya kulea mtoto afu aje akufanyie ujinga unafikiri mimi nitajiskiaje?”

Iryn alinyamaza kimya kwa sekunde kadhaa na aliendelea kuongea,

IRYN: “Claire kama Insider atabadilika huyu mtoto atabaki kuwa furaha kwangu na siwezi ku abort kwahili sikuungi mkono dear. Pia nikwambie kama kuna lolote litatokea lawama zije kwangu maana mimi ndo niliyeamua kubeba hii mimba bila kumshirikisha.”

CLAIRE: “Anyway, umejipangaje huko Ethiopia? Nakumbuka uliniambia ndo jambo linalokupa stress kwasasa na hatukamaliza maongezi yetu.”

IRYN: “I don’t know maana nitakapotoa taarifa watataka kumjua Insider then lazima waseme suala la ndoa na hapa ndo utata utakuja maana Insider ana mke tayari.”

CLAIRE: “You told me bado hajafunga ndoa, hapo inaweza kuwa 50-50 anything can happen. Mimi cha kukushauri get him to marry you first.”

IRYN: “I don’t think it will work, he’s always smart and he knows what he is doing."

CLAIRE: “Nafikiri bado hujaamua na umekubali kuwa mchepuko, lakini kama utakubali ushauri wangu hakuna kisichowezekana.”

IRYN: “Claire we can stop here, he’s coming tutaongea haya.”

Baada ya kuisikiliza voice hapa ndo nilikuwa na uhakika wa 100% kuwa Claire ni snitch kwangu na niliona kama ana wivu wala sio kingine. Kwa upande mwingine nilijilaumu sana kuwahi kurudi maana maongezi yao yaliishia pazuri sana na Claire alikuwa ametema sumu kali sana.

Niliwaza kuhusu suala la kwenda Ethiopia na niliona kama nilifanya maamuzi ya haraka sana kumkubalia Iryn. Kwenda Ethiopia ni kama kutembea na kitanzi shingoni, niliwaza na kuona sina sababu ya kwenda huko.

“Nimeshampa ahadi ya kwenda huko tena kukaa week nzima, daah huu ni msala. Week ni kubwa sana kukaa kule lolote linaweza tokea, ikitokea Iryn akanitambulisha kwa familia yake kuwa mimi ndo mpenzi wake? Na wakija kujua mimi na mke tayari itakuaje?.”

Niliona naumiza kichwa kwa matatizo yaliyosababishwa na Iryn mwenyewe, tatizo langu mimi lilikuwa kwenye mtoto tu maana niliona lolote linaweza tokea, ukizingatia ile mimba bado ni ndogo. Niliona Claire bado ananguvu sana ya ushawishi kwa Iryn na lolote linaweza kutokea.

Niliona kuna umuhimu wa kutafuta wazee wa busara wa kunipa ushauri juu ya hili suala na kuna mzee wangu wangu tulikuwa tunapatana sana kipindi niko taasisi X, hivyo niliona kuna haja ya kwenda kuongea naye kuhusu hii ishu.

Suala la kuwaambia wazazi na ndugu zangu wa karibu niliona bado ni mapema sana na sitakiwi kuwa na haraka sana atleast mimba ifike miezi 6 kidogo naweza kuwa na ujasiri wa kumwambia hata dada yangu. Mimba ya mama J nilikaa miezi 6 ndo nilitoa taarifa kwa dada then nikampa taarifa mama, sikuona umuhimu wa kushirikisha familia yangu kwasasa.

Niliwaza mama anakuja jumamosi na atakaa na sisi mwezi mzima hapohapo nina safari ya kwenda Ethiopia na Iryn. Niliwaza hili jambo mbona linakuwa gumu sana? Na roho yangu kwenda Ethiopia ilikuwa inasitasita kwakweli. Kwa mbali nilimuona mama J katoka nje na amesimama kibarazani na akiangalia usawa wangu ni kama alikuwa anajiuliza mbona huyu mwanaume hatoki shida ni nini?.

Baada ya kuingia ndani nilikaa seblen nikicheza na Junior maana tulikuwa wawili tu pale sebleni na muda huu nilichukua simu yangu kuangalia kama Iryn amefika au laah. Hakukuwa na text yoyote kutoka kwake na mimi nilimtumia ujumbe kumuuliza kama amefika salama.

Nilianza kuview status za whatsapp maana na niliview status za Prisca nikaona kam-wish mama yake happy birthday. Nilireply kwa ujumbe uliosomeka “Happy birthday to our beautiful mama” na haikuchua muda Prisca alireply na tukaanza kuchati pale. Tuliendelea kuchat pale na kubwa alitaka nimpe majibu ya ile text yake ya mwisho kunitumia ya kuwa friends with benefits na mimi nilimwambia hilo halina shida kama karidhia.

Nilifikiri nikaona kuna haja ya kuendelea kuwa na Prsica kama mchepuko wangu ukizingatia tuna historia tayari. Niliona kama kaanza kujielewa hivi, hivyo hatonisumbua kama zamani na itakuwa rahisi sana kumcontroll.
******
Siku ya jumamosi mama yangu mzazi alikuja Dar es Salaam na alisema ataendelea kukaa na sisi mpaka Christmass ndio ataondoka kurudi mkoani. Asubuhi tulikuwa na usafi wa jumla pale home, kwa upande mwingine kila jumamosi ya mwisho wa mwezi huwa tunafanya usafi wa pamoja kwa wapangaji wote. Hii ni ratiba iliyowekwa na sisi tuliukuta huu utaratibu baada ya kuhamia.

Saa 10 jioni niliondoka na wife kwenda Magufuli bus terminal kwaajili ya kumpokea mama na aliwasili mida ya saa 11 jioni. Baada ya mama kuwasili tulikumbatiana na alimgeukia wife wakakumbatiana pia, ndo kuondoka kurudi home. Barabarani zilikuwa ni story za huko nyumbani na wife ndo alikuwa busy na mama mkwe wake, huku mimi nikiwa busy na usukani.

Baada ya kurudi home mama ombi lake la kwanza lilikuwa ni kumuona mjukuu wake na bahati nzuri Junior alikuwa pale seblen na furaha ya mama ilitimia baada ya kumuona. Mara ya mwisho mama kuja Dar ilikuwa ni baada ya wife kujifungua na kipindi hicho Junior alikuwa na miezi 2 tu. Kwa upande mwingine mama alifurahi sana kumuona dada bado tuko naye ukizingatia tumeishi naye toka Junior ni mdogo na kipindi kile mama anakuja Elena alikuwepo.

Baada ya kupata chakula cha usiku tulifanya ibada ya pamoja pale seblen na baada ya hapo mimi niliaga nakwenda kulala na niliwaacha wakiongea.

Jumapili asubuhi niliamka mapema kwenda kazini maana nilikuwa nina kazi ya kuanza kuandaa bonus za mwaka kwaajili ya wafanyakazi. Ni utaratibu wa kampuni kwa kila mwisho wa mwaka kutoa bonus na mshahara double, hivyo nilitaka nikamilishe hesabu mapema ili mishahara iwahi kutoka kwaajili ya sikukuu za Chtristmas na mwaka mpya.

Asubuhi wakati naondoka mama alikuwa bado kalala hivyo nilimuaga wife na kuondoka kwenda Masaki. Ilikuwa ni mida ya saa 2 asubuhi wakati nawasili pale ofisini kwa upande mwingine nilikuta wafanyakazi wako busy sana. Kwa siku za weekend kunakuwa na wateja wengi sana, hasa kuanzia ile asubuhi mpaka usiku.

Mimi niliendelea na majukumu yangu na baada ya nusu saa Hilda alikuwa kawasili na alikuja ofisini kunisalimia, tukapiga story mbili tatu akaondoka kwenda kuendelea na majukumu yake. Kwa upande mwingine stock ilikuwa umekata na tulikuwa na odda nyingi sana, hivyo niliona niwasiliane na Iryn maana toka tuongee kabla hajaondoka hakunipa ripoti.

Iryn yeye ndo huwa anaagiza mzigo pamoja na kulipia baada ya hapo ndo ananiachia mimi kwenye masuala ya kodi na clearing. Baada ya kumpigia simu alipokea na tukaanza mazungumzo na habari mbaya alisema anaumwa,

MIMI: “Mummy unasumbuliwa na nini?”

IRYN: “Nahisi mabadiliko ya mimba natapika sana.”

MIMI: “Pole mke wangu, nilitaka kukuliza kuhusu mzigo umefikia wapi? Tuna odda nyingi na stock hakuna kitu, mzigo wa mwisho uliagiza mdogo.”

IRYN: “Kuna mzigo uko njiani unakuja ni week tayari nilikuwa busy na wewe sikufuatilia mails, soon nakutumia details. Kuna mwingine nimefanya payment tayari lakini shida ni Meli niliyopata gharama za usafirishaji ziko juu sana kwa contena, supplier anaendelea kucheki meli nyingine.”

MIMI: “Ok sawa haina shida baby, mimi naomba nikuache maana nina kazi kibao hapa.”

IRYN: “Wait, ushaanza kufuatilia Passport?.”

Ukweli sikuwa nimenza process zozote na sikutaka kumdanganya hivyo nilimwambia ukweli,

MIMI: “Bado baby but kesho jumatatu nitaanza usiwe na wasiwasi.”

IRYN: “Why you’re not serious?. Tarehe 16 tutaondoka kwenda Ethiopia.”

MIMI: “Baby muda bado upo mwingi sana hili lisikupe mawazo.”

Baada ya kuachana na Iryn pale niliona tayari nishajiingiza kwenye kitanzi maana waswahili wanasema ahadi ni deni. Niliwaza hivi kama nitaghairi hii safari Iryn atachukua hatua gani? yani nilikuwa sina imani kabisa ya kwenda huko Ethiopia.

Muda huu Asmah aliingia ofisini amependeza sana na alikuwa ndo anafika na mimi kama kawaida yangi nilimpa sifa pale na nilimzingua kwanini kachelewa?”

MIMI: “HR unaingia saa 4 asubuhi serious?”

ASMAH: “Jana nimechelewa kulala na ulivyonambia utakuja ofisini mapema bhasi nikawa na amani. Insider stock haina kitu zimebaki wigi chache sana kwaajili ya wateja na unajua december hii customer ni wengi.”

MIMI: “Ni kweli, hizo pisi msitoe nje zibaki kwaajili ya sisi lakini kuna mzigo unakuja na soon utakuwa umewasili tayari.”

ASMAH: “Umeongea na Iryn mwenyewe?”

MIMI: “Yeah ameconfirm na mwingine bado anahangaika na meli analalamika gharama zimekuwa kubwa za usafirishaji.”

Baada ya mazungumza na Asmah, alitoka kwenda kuweka utaratibu na mimi muda huu nilianza kuyambuka yale mazungumzo ya Iryn na Claire na nilijisemea I have to do something.

Saa 9 za mchana niliondoka ofisini na lengo kubwa niende Mbweni kumsalimia Jane maana ilikuwa ni wiki imeisha bila kukanyaga pale kwake. Kipindi niko njiani nilimkumbuka yule dada ambaye tulibadilishana namba pale car wash lakini alikuwa hajanicheki, niliona dada ana dharau sana.

Baada ya kuwasili kwa Jane nilimkuta mama Pama pale seblen akiwa na wageni, nilimsalimia tukaendelea na maongezi na baadae Jane alitoka na alifurahi sana kuniona.

Pale kwa Jane ukweli ni wananiheshimu sana tena sana ilifika stage mpaka baadhi ya marafiki zake Jane walidhani mimi ni ndugu damu wa Pama. Jane alinipa ishara na mimi nilijua tu anataka tutoke nje tuongee na mimi ndo nilikuwa wa kwanza kutoka na yeye alifuata.

Tulikaa garden tukizungumza na kubwa ilikuwa ni suala la Mary maana Jane alitaka tuyamalize haya mambo haraka sana. Jane alionekana kuwa serious sana kwenye maongezi yake,

“Shem unajua wewe na Mary ndo watu wangu muhimu sana na nina waheshimu, sipendi jinsi mnavyoishi kwasasa kwanini msikae chini mkamaliza tofauti zenu?”

“Shem unajua fika Mary anahisia za kimapenzi kwangu na zile ni hasira ila atakaa sawa tu trust me. Mary namuheshimu sana ndomana sijataka kufanya ujinga wowote kwake maana najua italeta shida huko mbeleni, ni vizuri anichukie lakini kwa faida ya maisha yake kwasasa hawezi kuelewa.”

“I really appreciate naomba nikuulize jambo lakini kuwa honesty na mimi, yule dada (Iryn) ni nani kwako?.”

Niliona Jane anauliza maswali sensitive sana na niliona hata nikimwambia ukweli hakuna faida atakayopata, zaidi mahusiano yangu na Iryn yabaki kuwa ni siri,

“Shem yule ni bossy wangu kama nilivyokutambulisha na nina muheshimu sana, hatuna mahusiano zaidi ya hapa.”

“Sawa Insider mpaka nimekuuliza ujue ile siku kwenye lile sakata la Mary pale seblen niliona mabadiliko yake, na nikahisi mpo kwenye mahusiano”.

“Hiyo sio sababu lile suala alilofanya Mary ni la kitoto na alinikera sana, naamini Mary ndo anakupa hizi taarifa za uongo.”

“Insider naomba mkae na Mary myamalize na umwambie ukweli, sidhani Mary anakuchukia kwa hili kuna vitu unamfanyia ndomana.”

“Sawa shem haina shida nitakaa nae chini usiwe na wasiwasi.”

“Tuachane na haya ila Insider unabalaa sana shem wangu, yule dada alimtetemesha sana Mary afu she is very confident.”

Tulianza kucheka pale na Jane maana hata yeye alimkubali Iryn kuwa ni mrembo makini na kamkubali. Pia, Jane alinipa taarifa kuhusu 40 ya mtoto na alisema baada ya hapo ndo nitamkabidhi rasmi gari yake. Kwa upande mwingine alinipa taarifa ya kupewa zawadi ya gari kutoka kwa Umoja wa kikundi cha Pama na alisema hajui ni gari gani na itakuwa surprise siku hiyo ya 40 ya mtoto.

Saa 12 za jioni niliondoka kurudi nyumbani maana wife alikuwa kashaanza kupiga simu nonstop. Baada ya kuwasili home nilimkuta mama yuko seblen anacheza na mjukuu wake na tulisamiana pale nikakaaa kwenye coach.
Baadae tuliamua kutoka nje kukaa kibarazani kuendelea na maongezi maana niliona mama anakosa uhuru wa kuongea pale seblen,

MAMA: “Mpaka jumapili unakwenda kazini mwanangu?”

MIMI: “Hapana ila mara chache kama kuna jambo huwa nakwenda si unajua mimi ndo kila kitu?”

MAMA: “Bossy wako anaonekana ni mkarimu sana ile siku alinambia mama natamani sana nikujue siku maana Insider ni mchapakazi mzuri.”

MIMI: “Amesafiri mara moja kama atarudi bado upo atakuja kukusalimia na atafurahi sana kukufahamu.”

MAMA: “Yule binti mimba iliyoharibika anaendeleaje?

Nikajisemea mama kaanza kufukua makaburi kumbe hajasahau tu,

MIMI: “Yuko salama mama ila hatuna mawasiliano kwasasa niliamua kukaa naye mbali yale makosa yasijirudie tena.”

MAMA: “Vizuri lakini Roho inanambia bado anakupenda, naomba kuwa makini sana kwa hili mwanangu.”

Ilibidi nibadili mada niliona mama anakoenda siko kabisa,

MIMI: “Nambie harusi ni ya nani kwanza? Maana hatukuongea hili kabisa.”

MAMA: “Ni binti wa mama TUSI , si unamkumbuka yule bint yake wa kwanza?.”

MIMI: “Simkumbuki kabisa, bhasi tutakwenda wote na vipi kuhusu michango?

MAMA: “Tutakwenda na mama J, muwe mnahudhuria harusi za wenzenu ili mpate hamasa ya kuoana mapema. Na suala la harusi yenu mmefikia wapi? Haya ni maamuzi na mipango yenu, lakini siku zinakwenda.”

MIMI: “Harusi tutafunga mama ngoja amalize chuo kwanza nabado najipanga kiuchumi.”

MAMA: “Mwanangu unataka mjipangaje? Unajua kadri mnavyochelewa ndo mnampa nafasi shetani?”

MIMI: “Ndomana mama yangu upo najua unatuombea ili shetani asilete majanga.”

MAMA: “Biblia inasema mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. Mimi nawaombea sana sana, lakini mnatakiwa na nyinyi mkumbuke kujiombea sawa mwanangu?”

Mama akishaanza masuala ya vifungu vya bible huwa nakuwa mpole sana, na muda huu wife alitoka na juice akatupa pamoja na mama. Tulikuwa na maongezi mengi sana na mama lakini cha ajabu lile jambo ambalo alisema kama ameoneshwa namficha hakuliongelea kabisa na mimi wasiwasi wangu ndo ulikuwa pale.

Mama aliniaga anakwenda kumsaidia wife kupika na mimi nilibaki pale kibarazani nikiwaza mambo mbalimbali ambayo yakinichanganya akili, likiwepo suala la Iryn la kwenda huko Ethiopia.

Jumatatu nilikuwa nina ratiba mbili muhimu ya kwanza ni kwenda kuonana na mzee wangu pale taasisi “X” na ratiba ya pili ni kwenda Uhamiaji kufuatilia suala la Passport.

Saa 3 za asubuhi nilikuwa nimewasili taasisi “X”, lakini nilikuta kuna mabadiliko makubwa sana pale, kwani asilimia kubwa ya watu nao fahamiana nao walikuwa hawapo, wamehamishwa. Kwa upande mwingine baadhi walikuwepo tunaofahamiana lakini sura nyingi zilikuwa ngeni. Idara niliyokuwa nafanyia kazi kulikuwa na watu wapya lakini ni watu wawili tu walikuwa wamebakishwa ambao ni kaka na dada yangu, ambao walipelekwa department zingine.

Baada ya kuelekezwa idara walizohamishiwa nilikwenda kwanza kuonana na dada yangu na tulipiga sana story na alinipa taarifa kuwa mzee wangu alikutana na panga kapelekwa mkoani, hivyo sikuwa na jinsi maana plan yangu ikawa imefeli. Namba yake nilikuwa nayo lakini kwa masuala kama haya niliona halina nguvu kuongea kwa simu na niliwaza nitafute plan B maana plan A ishafeli.

Baada ya kuachana na sister nilikwenda onana na brother angu na tulipiga story kadhaa kisha nikaenda msalimia manager wa ile taasisi. Manager baada ya kuniona alifurahi sana na tuliishia kupiga story nyingi sana za maisha maana toka tuachane hatuwahi onana wala hatukuwa na mawasiliano, licha ya kufanya kazi zake nyingi sana.

Habari kubwa manager alisema walikuwa na kikao na majina yetu yalipendekezwa kwaajili ya kupewa ajira maana tuna experience na tulichapa sana kazi kipindi kile. Manager alisisitiza sana hili suala kuwa ni serious na soon tutaanza pigiwa simu kwaajili ya kupewa mikataba. Mimi niliishia kumuitikia lakini nilijisemea hata kama nikweli siwezi kuikubali hio offer ya serikali ya kunilipa mshahara wa 1.5M, afu niache kazi yenye maslahi kwangu ambayo nalipwa mara 3 zaidi.

Kumkosa mzee wangu pale ofisini nilinyong’onyea sana na ukweli sikuwa na option kabisa na mzee aliyekuwa amebakia ni mmoja tu ambaye alinisaidia wakati natoa mahali ya mama J. Niliona kumshirikisha hili jambo italeta matatizo na nilijisemea sitakiwi kutumia nguvu sana kwenye hili suala, mambo yatakaa sawa tu.

Niliondoka kuelekea Kurasini pale Uhamiaji kwaajili ya kufuatilia Passport na nilikuwa tayari nimefanya mawasiliano na jamaa yangu ambaye anafanyia kazi pale na tulisoma Advance pamoja. Baada ya kuwasili pale tulionana na tuliongea kuhusu hili suala na alinihakikishia itatoka haraka nisiwe na wasiwasi kwa hili.

Niliondoka kuelekea Mikocheni na lengo langu nikaonane na Lucy maana toka Iryn aondoke hatukonana na niliwaza huenda ana jambo lolote la kunambia. Mchana nilikuwa nimewasili pale ofisini na nilimkuta anajisomea, baada ya kuniona alinambia anataka kwenda kula lunch, ikabidi na mimi niliunge.

Muda ambao tulikuwa tunapata lunch Lucy alinambia Iryn kamfungukia kuwa anamimba yangu na ananipenda sana. Lucy aliendelea kunisisitiza kwamba kwasasa nisimpe stress zisizo na msingi wala kumkera na nifocus na maendeleo ya kampuni. Kwa upande mwingine tuliendelea na mipango ya kiofisi na kubwa nilimwambia anisaidie kuandaa performance report ya kila mfanyakazi wa pale Mikocheni kwa mwaka mzima ili niweze kuandaa bonus zao zitoke mapema na mishahara.

Baada ya maongezi ya kiofisi tulianza maongezi mengine na nilishangaa kuona Lucy akiniulizia taarifa za Bob na mimi nikawaza huenda Bob kashamtongoza tayari. Japo Lucy hakutaka kuongea lolote nilihisi kuna kitu hakipo sawa na nilijisemea nitamcheki Bob anipe mkanda mzima wa kinachoendelea.

Saa 11 jioni niliamua kurudi home mapema maana niliona kurudi late na mama yupo pale home haiwezi leta picha nzuri ukizingatia mama anaonekana kuwa na maongezi mengi sana na mimi.

Baada ya kurudi home nilimkuta mama yuko nje na Junior akimwendesha kwa gari yake na nilimsalimia na tukaendelea na mazungumzo. Mama alishangaa sana kuona nina gari tatu pale home na mimi nilimwambia yakwangu ni moja tu ambayo ni ile Ist mpya na zingine sio zangu.

Tulianza kupanga mipango ya harusi na alisema harusi itafanyika Tabata na siku ya ijumaa itabidi twende Kariakoo kwaajili ya kununua zawadi za harusi. Mama alisema kama kikundi chao huko mkoani wamechanga kwaajili ya sherehe na yeye ndo mhasibu wa kikundi chao. Kwa upande wangu nilimwambia nitamfanyia shopping na nitampeleka saloon akang’arishwe na aliishia kufurahi.

Kwa upande mwingine mama alinisisitiza sana nitulie na kama nina wanawake wa nje bhasi niachane nao kwani Mungu amenipa mke bora na nimuheshimu sana mama J. Si unajua tena mambo ya wazazi, mama alinipa sana lectures na alikuwa hakosei sehemu za kupiga point.

Wakati nikiendelea kuongea na mama, Iryn alianza kupiga simu na mimi sikutaka kupokea simu zake muda huu maana nilikuwa na mazungumzo na mama. Baada ya kuona akiendelea kupiga simu kwa fujo nilimuaga mama mara moja nakwenda ndani kuoga then narudi.

Baada ya kupokea simu yake kama kawaida alianza kulalamika kwanini sipokei simu zake na ilibidi nimdanganye kuwa nilikuwa nadrive na simu ilikuwa silent. Sikutaka kumwambia Iryn kuwa mama yuko home maana nilijua angenisumbua sana kutaka kuongea naye na ingeleta tatizo.

Mimi na Iryn huwa tunakuwa na maongezi marefu sana, unakuta tunaweza ongea hata lisaa na bado hakuna dalili za kumaliza maongezi. Kwa upande mwingine aliuliza kuhusu progress za ufuatiliaji wa Passport na nilimwambia tayari nimeanza mchakato na soon nitakuwa nayo. Tangu Iryn arudi Dar na kuondoka niliona wivu kwangu umeongezeka sana na alikuwa akipiga sana simu mpaka kero na hapo anataka tuwe tunaongea tu ndo furaha yake.

*****
Ijumaa tulikwenda Kariakoo kununua hizo zawadi kwaajili ya harusi na tulianza kwanza kufanya shopping maduka ya Sinza, then tukamalizia Kariakoo. Zawadi ambazo mama alikuwa anataka kununua ni pamoja na fridge, Jiko na mazaga mengine. Kwa Kariakoo nina wadau wengi sana pale, hivyo haikuwa shida kwangu na tulipata fridge nzuri na bei kitonga.

Baada ya kumaliza shopping ilibidi twende Tabata kuzipeleka zawadi ili ziwe karibu na eneo la tukio. Break yetu ilikuwa Kinyerezi kwa mama TUSI na alikuwa kafikia kwa binti yake ambaye anaolewa na nilimsalimia pale na alifanya kunitambulisha binti yake maana tulikuwa hatujuani.

Jumamosi asubuhi mama alinipa ratiba kwamba tunatakiwa kuwahi kwenda ukumbini hivyo itabidi wawahi kwenda saloon ili kufikia saa 12 jioni tuwe amefika eneo la tukio. Saa 9 mchana wife na mama waliondoka kwenda Mikocheni na nilikuwa nishampanga tayari Lucy kuwa mama yangu anakuja hivyo asizingue.

Saa 12 jioni niliwapitia pale ofisini na nilikuta wamependeza sana kwakweli yaani ungemuona mama J wangu ungedata. Kwa upande mwingine Lucy aliniita pembeni na alianza umbeya wake na kubwa alifurahi sana kumuona mama yangu na aliishia kunimwagia sifa kuwa tumefanana sana.

Saa 1 usiku na madakika tulikuwa tumewasili Baracuda Highland hall na niliweza kuonana na mama zangu wa mkoani. Niliwasilimia pale na wao walifurahi sana kuniona na kama kawaida ya wamama waliishia kunichamba kwanini nakaa na mtoto wa watu bila kufunga ndoa?. Niliishia kujitetea pale na niliwapa ahadi kuwa soon na mimi nafunga ndoa, waliishia kumfurahia mama J na tukazama ndani eneo la tukio.

Tulikaa upande wa ndugu za Bibi-harusi na Kwenye meza yetu tulikuwa 10, mama alikuwa amekaa kati yangu na wife na muda huu tulikuwa tunapiga story wote watatu. Mama aliendelea kusisitiza tufunge ndoa mapema kwani muda unakwenda na sio lazima tufunge ndoa ya gharama, lawama zote zilikuwa zinakuja kwangu. Wakati story zimenoga kwa upande mwingine Iryn alianza kupiga simu na mimi nilikuwa nazimute maana sikuona sababu ya kuongea naye muda huu, na alipiga mara tatu.

Harusi ilikuwa nzuri sana kwakweli mpaka nikapata ka wivu na mimi nifunge harusi na mama J, lakini nikikumbuka suala la Iryn nikawa nakosa nguvu. Harusi iliisha saa 6 za usiku na tuliendelea kumsubiri mama maana alikuwa ana kikao na wamama wenzake na walitumia kama lisaa ndo tukarudi home kulala.

Jumapili nilichelewa sana kuamka na nilikutana na missed call nyingi tu, missed call 2 ilikuwa ni namba mpya, lakini nilipotezea na nilikwenda seblen kuangalia kama mama kaamka salama. Nilimkuta mama akicheza na mjukuu wake na nikamwambia jioni tutatoka wote kwenda kutembea na kupata dinna.

Nilitoka nje ili niweze kuongea na Iryn maana alikuwa kapiga sana simu pamoja na texts juu, nilimpigia simu na haikuchukua muda akapokea ila alionekana kuchukia sana,

IRYN: “Baby kwanini hupokei simu zangu toka jana?”

MIMI: “Sorry, sikuwa sehem nzuri ndomana.”

IRYN: “Unamaanisha nini kusema hukuwa sehemu nzuri? Na kwanini hujanambia kama mama amekuja Dar?”

Nikajisemea Lucy kashampa taarifa Iryn na nilisahau kumwambia asiseme hivyo sikuona sababu ya kum-mind Lucy,

MIMI: “Ningekwambia mummy kaja juzi na masuala ya harusi ndo yamemleta na ndo nilikuwa naye jana huko kwenye harusi.”

IRYN: “Sijapenda Kutonipa taarifa, four days remain before our trip to Ethiopia na nitakuja Dar ili tuondoke wote. Naomba nikija nimuone mama by any means, this is not for me, it's for your child."

MIMI: “Sawa no problem I’ll do my best”

Sikutaka kumkatalia maana ningeanzisha matatizo mengine hivyo nilikubali lakini nikijua hili jambo haliwezi tokea kwasasa. Muda wa kwenda Ethiopia ulikuwa unakuja kwa spidi sana na niliwaza pale nitatumia gia gani ya kuondokea pale home kwenda huko?. Niliwaza nimuache mama yangu mzazi home then niende na Iryn? Niliona kama haiwezekani.

Wakati nikiendelea kuwaza simu ya Prisca iliingia na baada ya kufanya nae maongezi alinipa taarifa kuwa kwasasa yuko Changanyikeni hivyo niwe nakwenda kumsalimia. Baada ya kuongea na Prisca nilifanya kumpigia simu dogo ripota wangu na nikamwambia aache kumfuatilia Prisca, amuache na maisha yake. Kwa upande wake dogo alishangaa sana na aliuliza kwanini nimeamua hivyo? Nilimwambia kwasasa hatuko kwa mahusiano, hivyo sioni sababu ya kumfuatilia .

Jioni tuliondoka familia nzima kwenda Karambezi cafe kwaajili ya kupata dinna ya pamoja na lengo langu kubwa mama afurahie kuja Dar. Baada ya kuwasili pale tuliagiza chakula lakini kwa mama ilikuwa shida kidogo kwani zile menu zilikuwa zinamshinda na nilifanya kumchagulia chips na beef.

Tuliendelea kupiga story pale na mama alionekana kulipenda sana eneo hili na muda huu simu yangu ilianza kuita na ilikuwa ni namba ambayo ilinitafuta asubuhi. Nilitoka na nikaenda kupokea simu,

ANONYMOUS: “Hello Insider za kwako?”

MIMI: “Salama habari yako pia.”
Wakati nataka kuuliza who’s this kwa haraka alijitambulisha,

ANONYMOUS: “Unaongea na Ghati tulikutana Carwash Mbweni.”

Hapa ndo kumkumbuka yule dada na ile siku tunakutana hakunambia jina lake,

MIMI: “Now nimekufaham mrembo, niliwaza umeamua kunipotezea maana kimya sana mpaka nimesahau.”

ANONYMOUS: “Sorry, nilipata emergence ya haraka, so nilikuwa bush kuna mradi nilienda simamia. Nimerudi sio muda na kitu cha kwanza nimeenda kwenye gari kutafuta business card yako ndo nimekupigia.”

MIMI: “Ooh thank you na pole na safari.”

ANONYMOUS: “Asante, upo pande zipi?”

MIMI: “Seems unataka tuonane.”

ANONYMOUS: “Yeah If possible maana niko tu, na sina pakwenda.”

MIMI: “Kwa leo ratiba ipo taiti mummy nitakucheki next week.”

ANONYMOUS: “No problem basi ngoja mimi nilale byee.”

Baada ya kuachana na dada nilisave namba yake na nikarudi mezani kujumuika na kina mama. Nakumbuka tulikaa pale mpaka saa 4 za usiku ndo kurudi home kulala na hii siku mama alisema atakuwa na kikao na sisi, kwani ana mazungumzo muhimu sana ya kuzungumza nasi.

*****
Tulikuwa tumeanza wiki mpya na zilikuwa zimebaki siku 3 tu za kwenda Ethiopia na ile asubuhi nilikwenda Kurasini kuchukua Passport yangu ilikuwa tayari imetoka. Baada ya kutoka pale Kurasini nilikwenda moja kwa moja mpaka Masaki lakini wakati niko njiani niliwaza nitafute sehemu nitulie kwanza.

Niliamua kwenda Cocobeach kutulia kwanza na kulifikiria hili jambo kwa makini sana before sijafanya mistake yoyote. Pale Coco nilitumia muda mwingi sana kulifiri hili suala na majibu niliyowaza nisiende huko Ethiopia na nilianza kuwaza nitatoa sababu gani?.

“Ok! Iryn anajua mama yuko Dar naweza mwambia tutakuwa na kikao cha familia ambacho ni muhimu niwepo, hivyo sitoweza kwenda Ethiopia. Sasa, Insider kama Iryn umempa ahadi ya kwenda ina maana hukujua mama anakuja? Kumbuka ana mimba yako tayari, kumpeleka Ethiopia kuna shida gani?”

Ni Roho mbili ambazo zilikuwa zinashindana ndani yangu, lakini hii ya kutokwenda ilikuwa na nguvu na nikajisemea potelea mbali kama atanichukia kwa hili, i’ts okay bado nitabaki kuwa baba mtoto ila kwenda huko sitathubutu Roho yangu imekataa.

Nilikuwa kwenye wakati mgumu sana na nikaona kuna haja ya kwenda home kuongea na mama kuhusu hili suala la mimba ya Iryn. Niliona kwa stage niliyofikia ni ngumu sana kuwa na maamuzi sahihi, hivyo nahitaji msaada hata kwa mama yangu mzazi before mambo hayajaharibika.

Niliona sometimes kama mwanaume inatakiwa kuwa na maamuzi magumu, nibora mama ajue mapema kinachoendelea before it’s too late na maamuzi yafanyike mapema. Kwa upande mwingine simu yangu ilianza kuita na kucheki ni Iryn alikuwa anapiga na nikajisemea leo namchana ukweli siendi Ethiopia.

TO BE CONTINUED





Insider unatembelea audi Q7 nyeupe namba za usajil T…………EAX
prove me wrong
 
😂😂😂
Kwan ww huna Yule ex ambaye ni addictive?
Nina ex mmoja ile tunadate mara ya kwanza aliwah niambia siku tumeachana ndo mazima siwezagi kurudiana na mtu nkishaachana nae ... ila hadi sasa tusharudiana mara 5 na tushaachana 😂
 
H
Nina ex mmoja ile tunadate mara ya kwanza aliwah niambia siku tumeachana ndo mazima siwezagi kurudiana na mtu nkishaachana nae ... ila hadi sasa tusharudiana mara 5 na tushaachana 😂
Huyo hamtakaa muachane milele. Popote utakapomuona mtaenda chemba tu.
😂😂😂 ex wangu ninapokuwepo na yeye awepo lazima hali ya hewa ichafuke ndo mioyo itulie.
But Sisi tunafikiria kuoana ili Mambo yasiwe mengi
 
H

Huyo hamtakaa muachane milele. Popote utakapomuona mtaenda chemba tu.
😂😂😂 ex wangu ninapokuwepo na yeye awepo lazima hali ya hewa ichafuke ndo mioyo itulie.
But Sisi tunafikiria kuoana ili Mambo yasiwe mengi

Huu mjadala wenu umenikumbusha ex wangu mmoja, tuliachana na hatukuonana kama miezi 5, paaap tulikuja kukutana kkoo hakuna aliyeweza kuvunga kumchangamkia mwenzake, hapo hapo tukaanza kusaidia shopping .... kuna mda tupo duka moja nikajikuta "daah naona tunapoteza tu muda bora tungeenda zetu kupeana mambo" alinipiga jicho tukaendelea na shopping..

Tulivomaliza muda wa kuagana, ananiuliza kile kitu ulichosema mda ulitaka tukafanyie wapi, haooooooo lodge moja kwa moja
 
Huu mjadala wenu umenikumbusha ex wangu mmoja, tuliachana na hatukuonana kama miezi 5, paaap tulikuja kukutana kkoo hakuna aliyeweza kuvunga kumchangamkia mwenzake, hapo hapo tukaanza kusaidia shopping .... kuna mda tupo duka moja nikajikuta "daah naona tunapoteza tu muda bora tungeenda zetu kupeana mambo" alinipiga jicho tukaendelea na shopping..

Tulivomaliza muda wa kuagana, ananiuliza kile kitu ulichosema mda ulitaka tukafanyie wapi, haooooooo lodge moja kwa moja
😂😂😂😂😇😇 kile kitu 🤣🤣
Hapo mwisho kabisa ndo hatma ya ex asiyeachika kirahisi.
My ex my temptation.
Dee wherever u are I already miss u😍
I envy your msukuma....
 
tat

zo n msmuliaj stor isngepoa tatzo huyo jamaaa yan mpak ajskie kutuma so imepelekea stor kupoa koz hamu ya kupata kitu inaishia pnd kitu knapochelewa kupatkana so stor bado kupoa sema msmuliaj.kapelekea kukosekana radha iliotegemewa ktk vchwa vya weng
HAYO N MAWAZO YANG SIO LAZMA KUYAPOKEA WALA KUYAJIBU
Story ilashaisha mkuu hapa anachofanya ni muendelezo baada ya maombi wadau kuipenda story wakataka kujua nini kiliendelea baada ya kumla Iryn na kumpa mimba na mengine mengi. Hivyo kuwa mpole
 
Story ilashaisha mkuu hapa anachofanya ni muendelezo baada ya maombi wadau kuipenda story wakataka kujua nini kiliendelea baada ya kumla Iryn na kumpa mimba na mengine mengi. Hivyo kuwa mpole
we una uhakika gan kama iliisha
anyway skujua kumbe iliisha na hamsem
 
😂😂😂😂😇😇 kile kitu 🤣🤣
Hapo mwisho kabisa ndo hatma ya ex asiyeachika kirahisi.
My ex my temptation.
Dee wherever u are I already miss u😍
I envy your msukuma....
Ex ni hatari sana 🤣🤣
 
Haya sasa, wapembuzi na wadurusu maamuzi na mahusiano ya watu uwanja ni wenu kwa muda.
 
Kuanzia next week tutaanza kwenda mchakachaka. Ndo kwanza mambo bado huko mbele ndo balaa, tuombe uzima tu.
tuwekee hata kwa wiki mara tatu jamani maana kila siku lazima nichungulie kama umeweka mpya aisee hii arosto hatarii
 
Ndugu zangu wana Jf habari zenu.

Unajua kwenye haya maisha tunapitia mengi sana hasa katika utafutaji kwa upande wa Wanaume. Tunakutana na mambo mengi sana ya aibu, kukatishwa tamaa, kuachwa na tuwapendao na mauzauza mengi sana.

Nakumbuka mzee mmoja alinambia mapambano ya kupata maisha mazuri sio rahisi inatakiwa ujasiri, kujitoa na kuwa na maamuzi magumu sana. Kila aliyefanikiwa ana siri nyingi ambazo sio rahisi kushare na mtu mwingine, sometimes tunakutana humu jf, tuna marafiki zetu wote hapa duniani tuna matatizo lakini matatizo yetu yametofautiana.

Mimi INSIDER nimepitia mambo mengi sana kiasi kwamba nilikata tamaa ya maisha unaweza ukasoma huu uzi wangu “Sitaomba kazi acha niwe jeuri tu”

Sitaomba kazi tena, wacha niwe jeuri tu!!

https://www.jamiiforums.com/index.php?threads/Sitaomba-kazi-tena%2C-wacha-niwe-jeuri-tu%21%21.1619876/ , na story yangu itaanzia hapa, ilikuaje mpaka nikaingia kwenye biashara ya uber??.

Hii ni story ya kweli na siyo ya kutunga, lengo langu nataka ndugu zangu mpate ujumbe kuhusu haya maisha. Kiufupi usikubali kukata tamaa hata kidogo, no matter what you fall, keep fighting, God has plans for all of us.

Kwa wale ndugu zangu wa Uber/Bolt ambao mnataka kuingia kwenye hii biashara utaweza kupata mwanga mzuri kuhusu hii biashara maana nina experience ya kutosha. Tusichoshane acha nianze kumwaga asalii……..,,

Wakati naandika ule uzi wa “ Sitaomba kazi tena wacha niwe jeuri” , nilikua nimerudi mkoani kwa wazazi kuwasalimia. Ofcourse maisha ya mkoani na niko home sikua na wasiwasi kabisa wazungu wanasema “HOME SWEET HOME””.

Chuo mimi nimemaliza moja ya chuo kikubwa hapa Dsm, baada ya kumaliza chuo sikutaka kurudi home kabisa maana niliwaza hata nikienda home kule nitafanya nini? Nikakae na mama tu? Niwe nakula na kulala? nikakukumbuka ule msemo unaosema mtoto kwa mama hakui bali analemaa akili.

Niliamua kwenda kwa Uncle wangu kukaa huku nikiendelea kutafuta kazi hapa mjini, alikua anaishi Mikocheni. Kipindi cha weekend nilikua natoka chuo nakwenda Mikocheni nashinda kule kwa Uncle then jumatatu narudi chuo, pale palikua kama home tu.

Nikaanza kusambaza CV kwenye mataasisi, makampuni, NGO’s kwenye mabank na sehem nyingi tu hapa Dsm lakini patupu sikufanikiwa kupata sehemu hata ya kujitolea.

Kuna siku nilikuwa nimekaa na Uncle tunaongea akaniuliza umemaliza chuo sasa una mpango gani?. Nikamwambia abc zote kwamba nimepeleka maombi yangu sehemu mbalimbali nasubiri majibu kama nitafanikiwa ama laah. Akanambia kuanzia jumatatu tutaanza kwenda wote kazini, lakini utaweza mikiki ya Kariakoo?, nikamwambia ni bora nishinde huko kuliko kubaki hapa home, I hate that.

Kweli jumatatu ikafika tukaenda huko kwa Wachina, ile siku sikutaka kuuliza ni kazi gani lakini nilikua najua Uncle anafanya kazi kiwanda cha mabag. Tulivyofika pale kiwandani Uncle akanitambulisha kwa Mchina.

UNCLE: “Hey Mr ping this is my Uncle, My sister’s son. Call him INSIDER.”

MCHINA: “Ooh you look alike I thought is your son, akacheka. huyu mchina alikua hajui kiswahili hata ngeli alikua anaibia kwa mbali. Mchina akanambia hey “Rafiki” karibu.”

MIMI: “Thank you.”

Uncle akaniita niingie store akanambia kazi yangu itakua ni kusupply mabag kule Kariakoo, kwenye hii kampuni yeye alikua ni Sales and Operation manager na kampuni ilikua inatengeneza journey bags na backpack bags na pilot bags.

Canter ilikua imefika pale tayari kwa upakizi, so tukaanza kupakia mabag mle kwa gari na kuyapanga kuyapeleka Kariakoo kwa wateja. “Ipo hivi pale kiwandani sio kwamba ndo wanaanza kutengeneza hapana wanafanya assembling tu, material zote zinatoka China, pale ni kuassemble na kuyapeleka sokoni”.

Ile siku nilipiga sana kazi nakumbuka tulipiga trip 2 ila kila tripu ilikua na bag 200, sio poa kupakua bag pale Kariakoo ni mtihani yaani foleni za watu zilikua zinakera sana. Uncle akawa ananilipa cash kwa siku 10,000/=, wakati naanza alikua ananinulia chakula ila baadae akaanza kunikataa so nikawa najilipia, kuhusu kwenda kazini tulikuwa tunaondoka wote kwa gari asubuhi.

Nikaimasta kazi kwa muda mfupi sana ikafika stage akawa ananiacha niende peke yangu na dereva mitaa ya Kariakoo na wateja nikawa nimewajua tayari haikuwa ngumu kwangu. Uncle akanambia upo vizuri ikafika stage hata madeni nikawa nakwenda kukusanya then napeleka bank, yaani unakuta nimekusanya madeni mpaka 80million, hiki ndo kipindi nilikua nashika pesa nyingi sana.

Nilikua nimejenga urafiki na baadhi ya wafanyakazi wa pale kiwandani, siku katika kupiga story jamaa akanambia naona sikuhizi umepanda cheo unapeleka mabag mwenyewe Kariakoo. Nikamwambia nimemasta kimtindo akanambia safi inabidi mzee wako majukumu yapungue maana umri unakwenda huko Kariakoo atuachie vijana. Jamaa akaniuliza posho si unapewa ukienda kupeleka mzigo?? nikamwambia sio haba kuliko kukaa bure, akauliza kwani unalipwa kiasi gani? nikamjibu 10,000. Jamaa akasema Uncle wako anakupiga atlist angekupa hata 50,000/= nikamwuuliza kwanini?, jamaa akanambia posho ya kwenda kupeleka mabag kwa siku ni 100,000/=

Jamaa akasema mzee wako anakuonea sio haki ile kazi ni risk, “hii kazi kama jamaa anavyosema kweli ni risk sababu unaweza kuibiwa kweupe, Kariakoo si mnaijua? “Kuna siku tulikua tunapakua mabag nilikua na moja ya wafanyakzi wa pale sasa jamaa alichanganya mafile akampa bag muhuni mwingine. Ilibidi akatwe kwenye mshahara, ni hivi tukikaribia Kariakoo tunawapanga wateja mapema. Kama mnavyojua maduka ya kariakoo yako barabarani plus yale mafoleni ni kichefuchef so huwa tunapakua mabag mlemle kwenye foleni. Mhusika anakuja na vijana wake wabebaji, inatakiwa uwakariri vzr maana ukizingua tu unaweza mpa mzigo mtu mwingine.”

Jamaa baada ya kufunguka hayo pia akanambia mzee wako kila bag anapata commision kwa bag la set 3 analipwa 1,000 na set 2 analipwa 700 (Zile bag za safari, set 3 ndani zinakuwa mbili yaani ukifungua zipu za bag kubwa ndani kuna kuwa na bag 2. Na hizi set 2 ukifungua zip ndani kunakuwa na bag 1), nikawaza hata lunch najilipia, uncle anaplay fouls sio haki.

Nikakumbuka matukio mengi tu mfano sometimes nikipeleka mzigo before sijaondoka atanambia ukifika Kariakoo piga simu kwamba TRA wamekukamata risiti sio sahihi, then utasema wanataka million 2, so mchina alikua anatuma hela. Nilikua nafanya hayo yote afu atanipa 50,000 tu au asinipe kabisa, nikikusanya madeni kama na million 30 atanambia ingiza kwa account ya kampuni maybe million 27 then million 3 nampelekea, zile ndo zilikua commission zake. Uncle wangu alikua anapiga sana hela shida alikua na madem wengi sana.

Kufupisha hii story, Mchina akaanza kunikubali sababu nilikua nampa ushauri baadhi ya mambo, akawa close sana mimi. Hiki kitendo Uncle hakupenda aliona kama nataka kumpokonya ugali wake, nikaona anaanza kunikataa mara anipe kazi ya kwenda kuangalia madogo shuleni, sababu zikawa nyingi mara biashara imekua ngumu sijui mambo yakikaa sawa ataniita. Kama msomi nikajua hapa sina changu, maana jamaa kule kazini alikua ananipa mkanda mzima kinachoendelea. Ukweli hii kazi ilikua inanisaidia sikosi hata pesa za vocha na matumizi yangu binafsi.

Nikaanza kukaa home na Aunt yangu, yeye alikua ni mama wa home tu. Hakuna kitu kigumu kama kuishi na ndugu inahitaji moyo na uvumilivu sana. Aunt yangu ni mvivu sana hata kwenye masuala ya mausafi hayuko active, nafikir ni moja ya sababu Uncle akawa na michepuko mingi. Ubaya sasa Uncle alikua anamsikiliza sana Aunt kwa lolote alilokua anasema yaani ni shida. Sasa hapa home tulikua tunabaki mimi na Aunt, madogo 2 wako boarding mmoja wa kike ndo alikua mdogo ansoma anatoka asbh anarudi jioni.

Nikaanza kuwa house boy wa mle ndani naamka Asubuhi sa12 nimpikie mtoto chai, baada ya hapo nitafanya usafi na kuosha vyombo, mchana nitapika chakula, jioni ninakazi ya kupikia mbwa chakula na kumwagilia miti na maua. Hizo kazi zote nilikua nafanya mwenyewe kila siku na nilikua nafanya kwa moyo wote.

Unaweza kushangaa mwanaume nawezaje kufanya hizo kazi lakini nilifunzwa nikiwa mdogo na mama yangu mzazi pamoja na dada yangu. Ikafika stage akaanza kunipa kufua nguo za Uncle na mdogo wangu ambaye ni mtoto wa mwisho (ambaye huwa naamka asubuhi kumpikia chai), nikaona haya mazoea yamezidi sasa.

Kuna siku nilikua natoka pale home Asubuhi kwenda mjini kwaajili ya interview na kusaka fursa, wahenga wanasema fursa haikufuati nyumbani unatakiwa ukaitafute. Sasa nikiondoka pale asubuhi mara nyingi anakua amelala na uncle wangu huwa anatoka sa11 au 12. Sometimes kuepusha makazi kama hayo nilikua nakwenda mjini au kwa washikaji kupoteza muda tu.

Aunt wangu akawa anampa taarifa Uncle kwamba huwa naondoka bila kuaga afu narudi usiku. Kuna siku Uncle alinikaripia sana nikamwambia Uncle navyotoka huwa anakua kalala kumwamsha sio busara, napia nikitoka sio naenda kuzurura nakwenda kutafuta kazi. Uncle akasema kama umekua mkubwa humu ndani nenda kapange ili uwe huru. Kama mwanaume niakanza kufikiri namna ya kutoka pale ikiwezekana nikapange nianze maisha yangu ya kujitegemea.

Nikapata wazo tangu nimalize chuo sijawai kwenda home mkoa kusalimia acha niende home nikasalimie wazazi wanipe na baraka. Kuna siku Aunt alinitia hasira sana, ilikua usiku inakwenda saa 2 nikatoka kwenda dukani kununua vocha niliacha simu chumbani. Kumbe wakati nimetoka Uncle alirudi akaniulizia hakunikuta ikabidi apige simu ikawa haipokelewi. Wakati nimerudi nikaona gari ipo uwanjani nikajua mzee karudi naingia ndani namkuta seblen kavimba hatari. Nikamsalimia Uncle shikamoo pole na kazi hakujibu, akaniuliza ulikuwa wapi usiku huu? Maana simu hupokei, kabla sijajibu Aunt akaropoka “huyu alikua kwa kidem chake kule bondeni taarifa zake zote ninazo kazi umalaya tu”.

Nikaona hizi dharau sasa nakua kama mtoto nikamwambia Aunt mimi tayari ni mtu mzima hupaswi kunipangia mambo ya kufanya, mimi kama kijana pia nahitaji kuwa na mpenzi na haki yangu naomba uwe na mipaka, nikaenda zangu chumbani. Aunt akasema kama umekua mkubwa si uende ukapange ili uwe huru??, nikajua hapa nishachokwa sipaswi kuendelea kung’ang’ania, akufukuzaye hakwambii toka.

Huyu mwanamke ambaye Aunt alikua anasema kidem changu ndo mama junior wangu mpaka sasa. Ni mke wangu japo sijafunga ndoa ila taratibu zote nimekamilisha kama kulipa mahari, bado ndoa ya kanisani tu. Niseme tumetoka mbali sana from Nothing to something, ni mwanamke anayenipenda sana na kunijari anasifa zote za kuitwa mke. Namshukuru Mungu kwa kuniletea huyu mwanamke kwenye maisha ni moja ya mtu ambaye ameplay part kubwa kwenye mafanikio niliyonayo. Tumebarikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume ana miaka 2 sasa tumwite Junior.

Nilikua kwenye dimbwi kubwa la mawazo sana. Wakati niko room nikawaza jumamosi acha niondoke niende home mkoa kusalimia na pia niongee na wazazi juu ya mustakabali wa future yangu. Kesho yake nikamwaga mama Junior alishtuka sana mbona ghafla? something wrong? nikamwambia NO! nataka nikawasalimie wazazi lakini nitarudi ASAP.

Mama Junior akaomba tusex maana ilikua ni miez 5 toka tuanze mahusiano hatujawai kukutana. Na ile jioni nikaona acha niwaage na hawa akina Uncle wanaweza kufikiri vibaya, nikategea Uncle amekaa seblen nikamsalimia, then nikamwambia Uncle Jumamosi mimi nitakwenda home kusalimia then nitarudi. Uncle akashtuka mbona haraka hivyo kulikoni? nikamwambia ni muda sijakwenda huko ni vizuri kwenda kuwajulia hali wazazi. Uncle akanambia bhasi kesho uende hata Kariakoo ununue vitenge vya mama, nikamwambia kesho ambayo ni “ijumaa” nitakwenda chuo kufuatilia cheti changu hivyo sitoweza kwenda Kariakoo. “Kumbe nilikua na timetable na mama Junior”, uncle akatoa hela akanipa kuhesabu ilikua 100,000 cash.

Jumamosi kweli nikaondoka kwenda home jioni nikiwa na bashasha nikafika mkoa nikashangaa jinsi mji ulivyojengeka maana ni miaka 3 ilipita bila kukanyaga. Nikachukua bajaji mpaka home kushuka mama akaja akanikumbatia….

MAMA: “waaoohh mwanangu nilikumisi sana jamani, naona umepungua sana shida nini?”

MIMI: “Mama maisha haya na stress za ajira nitanenepaje?”

MAMA: “umerudi sasa ule kwa bidii, maziwa, mayai yapo yakutosha akatabasamu, twende ndani. “Maana wakati tunaongea haya tulikua nje getini”.

Kiukweli nilivyofika home nilifarijika sana moyo wangu ulijawa na furaha sana. Bhasi ile jioni tukala dinna as family, wakati tunakula mama akaongea huyu mdogo wako anasoma science lakini hesabu hawezi zero kabisa, itabidi uangalie namna ya kumsaidia. Nikamwambia mama haina shida kesho nitakaa naye chini tuongee vizuri. Baada ya dinna nikakaa na wazee tukaongea sana kuhusu maisha, wakanitia moyo sana, tukafanya maombi tukaenda kulala.

Kipindi naandika ule uzi “Sitaomba kazi acha niwe jeuri tu” nilikua nimeridhika na maisha tayar sina stress niko home. Ilikua ni kucheza PlayStations na masela wa huku home full raha niko home kwa mama stress za maisha natolea wapi!?. Naamka asubuhi chai ya maziwa, mayai 2 ya kuchemsha ya chienyeji, mkate umejaa blue band. Kama unawazazi jitahidi uwapende wazazi wako wakiwa hai, wazazi wanatuombea sana kwakweli na hakuna anayependa kuona mtoto akiteseka.

Itoshe kusema baada ya kurudi home milango ikafunguka sikukaa muda nikapata kazi.

ENDELEA… [emoji116]

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu
Mkuu hongera kwa utunzi mahiri. Nimependa jinsi unavyoweza kuunganisha matukio k2a mtiririko.
 
Back
Top Bottom