Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

SEASON: 02
CHAPTER 12:

“A TRUE STORY BY INSIDER MAN.”

NYUMA:
WIFE: “Naomba tiketi zako za ndege sahivi nizione na hapa ndo tutajua nani msema kweli?”

Damn it, nilikuwa mpole ghafla maana nilikuwa nimekamatika na nilihisi joto kupanda kwa kasi.

ENDELEA:

MIMI: “Ina maana huniamini?”

WIFE: “Sio sikuamini ila nataka kuprove kama kweli ulikuwa Kenya ni mara ngapi umekuwa ukinidanganya?”

MIMI: “Kwanini unapenda kukumbushia mambo ya nyuma ambayo yalishapita?”

WIFE: “Nioneshe hizo tickets baba J mbona unakuwa mzito?”

MIMI: “Nasikitika kuona ninaishi na mwanamke ambaye haniamini.”

WIFE: “Nakuamini tena sana-sana.”

MIMI: “If so! Why do you keep asking for tickets? Seems you don’t trust me. Nitakupa hizo tickets hapa sina nilikatiwa, nitaziomba nitakupa.”

WIFE: “Lini?”

Mimi sikumjibu nilipanda kitandani kulala, nilianza kuchekecha akili nitafanyaje? Niliwaza kama nitasema zimepotea utakuwa msala mkubwa, ni sawa na kumwagia petrol kwenye moto.

Kitandani niliona ni pamoto nikatoka nje ili niweze kuongea na Iryn, lakini baada ya kumpigia simu alinitumia ujumbe kuwa yuko busy na atanirudia ASAP. Niliona Iryn ndo mtu pekee anayeweza kunisaidia hili jambo kwa wakati huu, ukweli Iryn yuko vizuri sana kwenye kufanya maamuzi ya haraka.

Niliendelea kusubiri pale nje kwa dakika 30 nikampigia tena lakini hakupokea simu, hivyo nikaamua kuachana naye, nikarudi ndani kulala.

Asubuhi niliamka mapema sana na ilikuwa ni jumamosi nikajiandaa kwenda ofisini na target zangu nianze na Mikocheni ili nikamiti na Lucy. Muda huu wife alikuwa bado kalala wakati naondoka nilisikia akiongea,

“Baba J kesho ni sikukuu unashindwa hata kutenga muda wa kukaa na mama? Tangu urudi hutulii home. Wewe mwanaume ni too much nimekushindwa hata kutenga muda na familia hauna, na ukirudi badae naomba uje na tickets.”

“Nitawahi kurudi.”

Niliishiwa kufyonzwa na mimi nikaondoka kwenda Mikocheni, na njiani niliona mama J yuko sahihi maana toka nirudi nimekuwa mtu wa kutotulia home.

Kipindi hiki cha sikukuu ofisi zote zilikuwa busy sana hata wafanyakazi walikuwa wanawahi mapema kutokana na kuwa na kazi nyingi. Baada ya kuwasili pale Mikocheni nilionana na Lucy na tulianza kuongea habari za Ethiopia, pia nilimuuliza maendeleo yake cha chuo akanambia anapambana ila shule ni ngumu.

Kwa upande wa Mikocheni sinaga shida na Lucy maana yuko vizuri kwakweli ndomana huwa sipendelei kwenda sana sababu yuko vizuri kwenye usimamizi.

Lucy alikwenda kuendelea na majukumu yake na mimi nilitoa simu ili nifanye mawasiliano na Iryn. Nilimpigia simu bila mafanikio maana alikuwa hapokei na nikamtumia ujumbe anitafute kuna jambo muhimu nataka kuzungumza naye.

Niliagana na Lucy lakini mpango wangu wa kwenda Masaki ulikwama nikaamua kurudi home nikakae na familia yangu. Wakati narudi home nilikuwa nawaza namna ya kudeal na mama J, kuhusu hizo tickets na nilikuwa nafikiria namna nzuri ya kuongea naye bila kuleta shida.

Njiani nilipigiwa simu na mtendaji wa kule kijijini Mondo ambako Iryn alitoa msaada na akanambia yule mzee tuliyemsadia ametoa mbuzi kwaajili ya sikukuu na leo ataituma ije Dar. Nilimshukuru sana na kwa upande wake alitaka kujua ni lini tutarudi kule tena? Niliishia kumwambia soon tutakwenda tena kuwasalimia.

Baada ya kuwasili home nilianza kucheza na Junior pale nje na mama alikuja tukaanza kuongea,

MAMA: “Mwanangu upo busy sana, unapataga muda wa kukaa na familia?”

MIMI: “Muda napata mama ni kwa vile kipindi hiki cha sikukuu nimekuwa busy, hata wewe si uliona ofisi nayofanyia kazi?”

MAMA: “Ni kweli bhasi jitahidi hata weekend uwe unatenga muda wa kukaa na familia. Muda wote uko busy, hapana mwanangu haipendezi naomba hili ulitizame.”

MIMI: “Mama kuhusu hili najitahidi sana kuna kipindi nilikuwa nakwenda na Junior kazini wakati dada hayupo.”

MAMA: “Kwa kipindi nilichokaa hapa nimeona upo busy sana. Naomba badae wote twende kanisani kwaajili ya mkesha, mama Junior nimeongea naye tayari.”

MIMI: “Sawa mama haina shida mimi leo nipo nyumbani tutakwenda.”

Mama aliondoka na mimi nilikumbuka badae nina miadi na Ghati, je nimzingue tena kwa mara ya pili?. Hii siku pia nilikuwa nina miadi na Allen maana tulikubalina mshindi wa Worldcup atajaziwa wese full tank na mimi nilikuwa nasubiri call ya Allen, kutimiza makubaliano.

Nilikumbuka kumpigia simu Iryn kwani alikuwa bado hajanirudia na hii ilifanya nipatwe na hasira maana niliona analeta dharau. Nilimpigia simu hakupokea na alitumia ujumbe kuwa yuko busy atanirudia badae, nikamtext back palepale,

Nimekutumia ujumbe nahitaji kuongea na wewe na ni muhimu lakini unaleta dharau inamaana huoni ujumbe wangu?”

“Sitaki kuongea na wewe na sitaki usumbufu ndomana.”

“Hio text umemaanisha ije kwangu au umekosea?”

“Ni yako baba mtoto.”


Niliamua kuachana nae maana alizidi kunipa hasira na wakati nafikiria nini cha kufanya kwa upande mwingine Muajemi alipiga simu kwa whatsapp na nikapokea kwa haraka sana,

MIMI: “Brother, how are you? It’s been a while. You didn’t even answer my calls or text me back.”

MUAJEMI: “I’m sorry, brother. I was very busy. How are you and your family?”

MIMI: ”Thank God we're good. How about you?.”

MUAJEMI: “We’re good too. I got your message bro! What is the important information you wanted to share from Iryn?"

MIMI: “Iryn called me and told me that you are bothering her. She says she doesn't want any disturbances from you because she has decided to focus on her life. Brother, why don't you let her go on with her life?.”

MUAJEMI: “This woman has captured my mind. I am still fighting, hoping that maybe one day she will love me. She is pretty and fine, perfectly designed. I hope she can read my mind."

Nilicheka sana maana niliona Muajemi anazingua kwakweli maana ni kama anaota,

MIMI: “Do you remember when I told you she’s pregnant?. Brother, use this energy to focus on other ladies.”

MUAJEMI: “I don’t know why I can’t let her go.”

MIMI: “The bad news is that you want to use the money and materials to get her, here is where you are wrong. The truth is, she's not pleased with these gestures, which is why she conveyed to me her desire for no further disturbances from you."

MUAJEMI: “I made horrible mistakes.”

MIMI: “She gave me your things, the gifts you bought for her that day, and asked me to return them to you.”

MUAJEMI: “No! No! It can't be like that. This is ridiculous. Tell me, bro! What should I do next?"

MIMI: “Bro, just tell me how you plan to retrieve your belongings."

MUAJEMI: “Keep it. I will see you in January, God willing."

Baada ya kumalizana na Muajemi nilimpigia simu mama wa2, nikampa taarifa nimerudi Tanzania na akanambia kesho atakuja home na binti zake kula sikukuu.

Saa 2 usiku tulitoka familia nzima kwenda kanisani kwenye ibada ya mkesha wa Christmas pale KKKT Mbezi Beach. Kwa upande mwingine kuhusu Ghati nilimpanga tutaonana next time na Allen nilimwambia pesa yangu ya mafuta aendelee kunitunzia mpaka tutakavyo meet.

Kwa upande wa Ghati mzuka wa kumtokea ulinikata baada ya kugundua ana mtoto na niliwaza ni bora nikatoka na Prisca au Asmah sababu hawa wanawake tayari nina historia nao kuliko kukutana na wanawake wapya.

Kanisani ibada ilikuwa nzuri sana hii siku na ilikwenda mpaka saa 6 za usiku ndo kurudi home. Baada ya kurudi Asmah alikuwa kaniwish Mary Christmas na nilimpa mwaliko wa kuja kula sikukuu home na yeye kwa upande wake alifurahi sana akasema atakuja.

******
Asubuhi mapema niliondoka kwenda Mbezi-kimara kuchukua mbuzi, nilikuwa nimefanya mawasiliano na jamaa tukabidhiane pale ndo rahisi kwangu, wao walikuwa wanakwenda Pugu.

Baada ya kurudi home nilisaidiana na jirani yangu kumchinja Mbuzi pamoja na kumuandaa kabisa. Tulianza kumuandaa kwaajili ya kuchomwa, kuchanganga viungo nknk, kwenye hii sekta niko vizuri sana.

Mida ya saa 4 asubuhi mama Janeth alinipigia simu kuniwish Mary Christmas pamoja na kunipa mwaliko maana alipenda sana tukajumuike pamoja pale kwake. Suala la kwenda kwake lilikuwa gumu na niliishia kumwambia siku ya mwakampya tuwe pamoja na aliishia kuunga mkono wazo langu.

Jane naye hakuwa mbali kuniwish Mary Christmas na alinipa mwaliko niende kwake pamoja na familia yangu, lakini nilimdanganya nakwenda ukweni na nitakwenda kwake kesho.

Mida ya saa 7 mchana Asmah aliwasili pale home na nilimkaribisha ndani nikamtambulisha kwa mama na wife. Nilimtambulisha kuwa yeye ndo HR wa kampuni na ndo msaidizi wangu pale ambapo nakuwa sipo, yeye ndo anakaimu. Muda ambao nafanya utambulisho wife alikuwa akiniangalia sana dizaini kama hakupendezwa na ugeni wa Asmah pale home.

Nilimkaribisha Asmah nje ili tuendelee kupiga story huku tunachoma nyama pamoja, muda huu wife alitoka nje na Asmah alikuwa makini sana kumtizama,

ASMAH: “Insider unajua kuchagua mke yuko vizuri sana.”

MIMI: “Laiti angelijua wewe ni mchepuko wangu angekutia risasi ya kichwa.”

ASMAH: “Hivi kwanini huridhiki ukatulia na mwanamke mmoja? Una…”

Na mimi nilimkatisha maaongezi yake,

MIMI: “Asmah mwanaume rijali mwanamke mmoja hatoshi, mama watoto wangu ni kipengele akiamsha mashetani yake nyumba utaona chungu. Tuachane na haya naomba kujua mustakabali wa lile jambo letu kama kujifikiria muda umekuwa nao wa kutosha.”

ASMAH: “Insider kwa hili hapana rafiki yangu, nitakuwa ni mwanamke wa ajabu sana kukubali wakati naona una familia na still bado unatoka na bossy wangu. Impossible!”

MIMI: “Mimi nataka uwe mchepuko wangu wa siri na nimekuchagua wewe sababu tuna historia tayari. “

ASMAH: “Insider namuheshimu sana Iryn sababu kanisaidia vitu vingi sana mpaka sasa, kutembea na wewe sio heshima. Nafanya hivi kwa faida yako na pia kuepusha matatizo yatakayokuja kutokea badae, tuendelee kuwa marafiki tu.”

MIMI: “Kusema kuendelea kuwa marafiki ni uongo labda unambie friend with benefits hapo sawa nitakuelewa. Najua unanipenda sana ila unataka kufanya mambo yawe magumu na kupoteza muda.”

Kwa upande mwingine alionekana Junior akija usawa wetu na alikuwa akiniita na Asmah ndo aliyembeba na mada ikabadilika,

ASMAH: “Umefanana sana na mwanao hata mama yako mmefanana sana, nimefurahi sana kuiona familia yako leo.”

MIMI: “Ahsante bila shaka umefurahi kumuona mama mkwe wako wa siri.”

Asmah aliishia kucheka tu pale na mimi nilitoa simu mfukoni nikapiga picha zile nyama nazochoma then nikasend kwenda kwa Iryn na nikam-wish “Mary Christmas”. Licha ya kuendelea kunifanyia drama zake mimi sikutaka kuonesha nina kinyongo naye maana nilijua ni mimba inayo mchanganya wala si kingine.

Kwa upande mwingine ndugu yangu Dullah aliwasili pale home kwaajili ya kula sikukuu pamoja, nilikuwa nimempa mwaliko mapema sana aje home siku ya Christmas tusherehekee.

Mida ya saa 8 mchana mama wawili aliwasili home na nilistaajabu kumuona akidrive harrier new model mpya “Macho ya panzi” maana alinipiga surprise sana. Nilimkaribisha ndani na nilifanya utambulisho kwa mama yangu mzazi ila kwa upande wa wife haikuwa shida anamjua.

Mama wa2 alikuwa kaongozana na binti zake wawili na mimi nilifurahi sana kumuona pili maana alionekana kuzidi kukua kwa kasi.
Nilitoka nje na Pili tukiendelea kuongea kuhusu maendeleo yake ya shule na alinambia january wanafungua shule, pia anatarajia kumaliza form 6 mwezi may.

Saa 9 za mchana tulipata chakula cha pamoja, kwa upande mwingine mama wa2 alikuwa busy sana akiongea na mama yangu. Mama wa2 alikuwa anamwambia mama kuwa amebariwa kupata kijana mchapakazi na mtu wa watu, kwa upande wa mama yeye aliishia kufurahi tu pale.

Baada ya kupata chakula mimi na Dullah tulitoka nje kwenye nyama choma na tulianza kukimbizia bia taratibu. Baadae Asmah na Jirani walikuja tukawa tuko wa 4 pale, zilikuwa ni bia na nyama choma ilikuwa ni hatari sana. Kwa upande mwingine Dullah alinambia anatarajia kufunga ndoa na Latifah mwakani mwezi february na habari kubwa alisema anataka kuacha biashara ya Uber, kwani ana mpango wa kufungua biashara ya chakula soon.

Kipindi tunafanya maongezi, Iryn alinipigia simu na nilisogea pembeni ili tuongee vizuri,

IRYN: “Darling, Marry Christmas too.”

MIMI: “Leo mashetani yako ndo yanajisikia kuongea na mimi?”

IRYN: “I don’t think so, how is your day going?.”

MIMI: “Kama hivi tunachoma mbuzi na alitumwa kwaajili yako na yule mzee wa kule kijijini Dodoma.”

IRYN: “Waow! Mwambie ahsante sana, naona unamchoma unanitamanisha, nakumbuka kipindi kile tuko na Grizz nyama zilikuwa tamu sana.”

Baada ya maongezi mafupi, ilinilazimu nimwambie kinachoendelea kuhusu ishu ya wife kuomba ticket za ndege maana nilijua yeye atakuwa msaada kwa hili lakini cha ajabu Iryn alianza kunicheka,

MIMI: “Sasa tunafanyaje? I believe wewe unaweza kuwa msaada kwangu, lakini unaanza kucheka.”

IRYN: “Nilijua lazima mama J atafute kila namna ya kuprove hili na niseme you dead.”

MIMI: “What do you mean? Kwamba huna option ya kunisaidia hili?”

IRYN: “What should I do? Hizo ticket mimi nazipata wapi? Ni mtihani unanipa ambao nita score 0.”

MIMI: “Sasa tunafanyaje? Uko tayari kuona nina achana na mama J? Ukizingatia nilikuwa Ethiopia na wewe?”

IRYN: “Hata sijui nakusaidiaje kwa hili baby, wewe ulishakosea toka mapema, kabla ya kufanya maamuzi uwe unafikiria na mbele itakuwaje. Ilikuwaje ukamwambia unakwenda Kenya? Hukufikiri mama J atakuomba ticket? Ndomana nakwambia you dead.”

Na Iryn aliendelea kucheka na hapa ndo alianza kunipa hasira,

MIMI: “Unacheka kuonesha mazuri sindio? Sawa nashukuru.” Nikakata simu.

Nilijifikiria pale nikaona kweli nilizingua Iryn yuko sawa, kabla ya kufanya maamuzi nilitakiwa kufikiria na mbele itakuwaje?. Simu yangu ilianza kuita na alikuwa ni mzee Juma akipiga na bila kujifikiria nilipokea simu yake tukaanza maongezi.

Mzee Juma alikuwa ananisalimia na aliuliza niliko kwani nimekuwa mtu adimu sana kipindi hiki hata kwenye 40 ya mtoto sikuwepo. Niliomba radhi na nikwambia ni masuala ya kikazi ndo yalipelekea hivyo na akanambia yeye hana maongezi mengi ila tuoanane jumanne ya wiki ijayo.

Nilirudi kwa washikaji kuendelea kupiga vyombo na baada ya dakika 20 Asmah aliniaga anaondoka kwenda home sababu dada yake anakuja kumtembelea. Tuliagana pale na nilimsindikiza nje ya geti na kabla ya kupanda Uber tulikumbatiana na nika mkiss shavuni. Ukweli moyo wangu ulikuwa umeshamchagua Asmah tayari na nilijisemea lazima nimpate kwa njia yoyote ile na awe kwenye himaya yangu.

Baada ya kuachana na Asmah nilirudi ndani na Dullah alianza kunipeleleza kama natoka na Asmah maana alihisi something fishy kinaendelea kati yetu. Nilimgomea na yeye alisema bhasi ninamla maana tunaonesha tuko kwa mahusiano, kwa upande wake aliishia kumsifia Asmah ni mzuri.

Kwa upande mwingine kule ndani akina wife walikubaliana tutoke out familia yangu pamoja na ya mama 2 na mimi ilibidi nijiandae ili tutoke out kama walivyopanga. Kwa upande wangu sikukubaliana nao lakini sikuwa na jinsi, na point yangu kubwa kwa siku za sikukuu kuna kuwa na watu wengi sana, hata usalama unakuwa ni mdogo.

Baada ya kujiandaa na kurudi seblen walisema wazo langu ni zuri, bhasi twende sehemu ambayo haitakuwa na mwingiliano mkubwa wa watu na wakashauri twende “The whitesand hotel.”

Dullah aliniaga anaondoka maana asingeweza kuongazana na sisi, hivyo akaondoka kuendelea na ratiba zake na sisi tukaondoka kwenda Whitesand.

Wakati tuko pale hotelini nilikuwa napiga story na mama wa2 kuhusu gari yake mpya maana ilikuwa chombo kwelikweli. Yeye alinambia kwenye ile gari katoa pesa ndogo sana ila kiasi kikubwa kimetolewa na baba watoto zake, niliishia kumpongeza kwa maendeleo ya kununua gari.

*****
Boxing day tulikwenda ukweni kusalimia, pia mama alitaka kuwaaga wakwe maana isingekuwa busara kuja Dar na akaondoka bila kwenda kuwasalimia. Baada ya kuwasili ukweni tulipokelewa vizuri sana, na kwa upande wetu sisi tulikuwa tumekwenda familia nzima.

Mazungumzo yalianza na mengi yalibase upande wetu sisi, na kubwa walitupongeza kwa kukaa muda mrefu bila kugombana na walisisitiza sana suala la ndoa kwani muda unakwenda na hatuoneshi mpango wowote wa ndoa.

Mama yangu mzazi naye alikuwa upande wa wakwe naye alisema nitoe ahadi ni lini tunafunga ndoa sababu mimi ndo kila kitu kwenye maamuzi. Nilikuwa kwenye wakati mgumu sana, ukizingatia makubaliano yetu na wife tufunge ndoa pindi atakapomaliza chuo.

“Wazazi wangu hili jambo hata sisi tunatamani liwe hata leo, lakini bado tunaweka mambo sawa ya kiuchumi. Tulikubalina pindi mama J atakapomaliza chuo ndio tufunge ndoa, ila kwa sasa bado hatujajipanga na tunaomba mtuvumilie kidogo.”

Ni kauli ambazo hazikuwafurahisha kabisa na muda huu ilibidi mama amuulize mama J kama anakubalina na haya maneno yangu, na yeye alisema anaweza kufunga ndoa hata kama bado anasoma ila ugumu unatoka kwangu.

Wife alinigeuka hivyo ilibidi nihitimishe kwa kuwaambia kufikia january nitakuwa na tarehe pamoja na mwezi wa harusi yetu, maana niliona kunakoelekea nitajiwekea kitanzi shingoni. Side zote zilikuwa against na mimi, hivyo ilibidi nitumie mbinu ya kujihami mapema.

Baadae nilipata muda wa kuongea na mama mkwe na kubwa ilikuwa kuhusu jambo la Jane na baada ya kuzungumza naye aliniambia hakuna shida, siku yoyote niende naye ili ampe mchanganuo wa kuanza biashara ya mini-supermarket.

Mida ya mchana tulirudi home, sasa kipindi niko chumbani na wife nilianza kumzingua kwanini amekwenda kinyume na makubaliano yetu na mimi naonekana kuwa ndo shida?. Kwa upande wake alitaka nimuoneshe ticket za ndege maana siku zimepita, afu dizaini kama najisahulisha. Na hapa ndo alinikera yaani namuuliza vitu vingine na yeye analeta story zingine, nikamtia kibao na ugomvi ndo kuanza.

Zilikuwa ni kurupushani mle ndani na alikuwa analia na kwa mbali nilisikia mama akiniita,

“Insider…. Insider….mnashida gani huko ndani?”

Wife alitoka na mama alianza kumuuliza shida ni nini? Na mimi nilitoka muda huu nikaamua kuondoka nikamwambia mama tutaongea vizuri badae.

Mawazo yangu yalinituma niende Mikocheni nikaonane na Lucy. Kwa upande wangu nilijua ule tayari ni msala na mama atajua kinachoendelea, ni bora nionane na Lucy huenda akanipa mawazo what to do.

Baada ya kuwasili pale ofisini nilimkuta yuko ofisini na alikuwa anachezea laptop yake na nilimsalimia kisha nikajiangusha kwenye sofa kama mtu ambaye amechoka sana,

LUCY: “Bossy uko sawa kweli?.”

MIMI: “Actually I’m not, nina stress tu hapa hata sijui nitachomokaje kwenye huu msala, wanasema za mwizi ni arobaini, naona kwangu zimeshatimia.”

LUCY: “Kuna nini mshikaji wangu? Mbona sikuelewi ni nini kinaendelea?”

Na Lucy alitoka akaja kukaa pembeni yangu,

MIMI: “Acha tu, ile safari yangu ya Ethiopia nilimdanganya wife nakwenda Kenya, sasa anataka kuziona ticket na ugomvi umetokea home sio muda. Naona mambo yashaharibika tayari mshikaji wangu na mama atajua kila kitu maana wife haelewi.”

LUCY: “Duuh! Huu msala ni wa moto sana, sasa hapa unafanyaje?.”

MIMI: “Yaani! Hata sijui na nikishindwa kuprove hili nafikiri tutaanza migogoro mle ndani na yule mwanamke ni kisirani sana, hata sijui nafanyaje.”

LUCY: “Wifi yangu umeongea naye kuhusu hili? Iryn atakusaidia ongea naye hili jambo mapema akusaidie.”

MIMI: “Nimeongea naye lakini anasema liko chini ya uwezo wake, jinsi ya kupata hizo ticket ndo kipengele anazipataje?”

LUCY: “Mhh! Ni kweli hapo ni kipengele ila bado anaweza kufanya jambo. Iryn ana watu hilo jambo kwake ni dogo sana, wewe mkamie mwambie ukiona nimeachana na mama J na uwezo wa kunisaidia unao, sitakusamehe kwa hili.”

MIMI: “Lucy huoni kama najiwekea kamba shingoni mwenyewe? Hili jambo kweli ni gumu hata mimi naforce tu bhasi ila sio rahisi. Kama nitamwambia hivyo kwa level aliyofikia sidhani kama itasaidia, ile mimba kwasasa inamchanganya sana, nikimwambia haya maneno utafikiri itakuaje?”

LUCY: “Ngoja nikwambia kitu Insider, the moment ambayo unaonesha mapenzi kwa wife wako unafanya Iryn akupende zaidi. Usijaribu hata siku moja ukaachana na mama J, utaona jinsi upepo utakavyo change, wewe mkamie naamini atafanya jambo ukizingatia ulikuwa nae huko Ethiopia.”

Lucy aliongea maneno fulani hivi ambayo yaligusa hisia zangu na niliamua kuondoka nirudi home na sikutaka kupoteza muda pale. Wakati niko njiani nikirudi simu yangu ilianza kuita na alikuwa ni Asmah akipiga na nilipokea kumsikiliza,

ASMAH: “Hey dear, umemwambia Iryn mimi nilikuwa kwako jana?”

MIMI: “Hapana sijaongea na Iryn chochote kuhusu wewe, ilikuwaje mpaka akakuuliza hivyo?”

ASMAH: “Hata mimi nimeshangaa sababu aliniuliza kama mtu ambaye anajua kila kitu na akaongelea masuala ya kuchoma nyama.”

MIMI: “Mhh! this is ridiculous, how did she know?”

ASMAH: “I don’t know kwakweli mawazo yangu yote ni wewe ulimwambia.”

MIMI: “Hapana dear sijafanya hivyo, ila jana muda ule nimetoka pale nilikuwa naongea naye, lakini hatukuongea chochote kuhusu wewe.”

ASMAH: “Mhh sawa! Ila hajaonesha kumind.”

Baada ya kuachana na Asmah niliwaza huenda wife alichat na Iryn akamwambia, lakini niliona bado ni ngumu sana.

Niliwasili home ilikuwa jioni na baada ya kuingia ndani nilimkuta mama yuko seblen na nilishangaa sana kuona akiangalia marudio ya worldcup. Mama baada ya kuniona aliniomba nikae chini ili tuzungumze jambo liliotokea masaa machache nyuma. Mama aliniambia wife kamwambia kila kitu na alinitaka nioneshe hizo ticket ili kuepusha ugomvi usio kuwa na maana. Kwa upande wangu nilimwambia mama kuwa ticket zipo kwa bossy na amesema atanitumia muda wowote, na pindi atakapozituma nita muonesha wife.

Mama alinisihi niende ndani nikayamalize na wife na mimi nilifanya hivyo kama alivyonielekeza na nilimkuta yuko chumbani anaongea na simu alikuwa kaweka loud speaker. Baada ya kutulia ndo kujua anaongea na Iryn na alikuwa anamfundisha,

“Yes dear, Nyati Company should appoint independent non-executive directors to the audit committee, and the CEO and CFO should not be members of this committee to ensure the objectivity of financial oversight.”

Na mimi niliamua kupanda kitandani nikalala nikamuacha apewe shule na mke mdogo, na walikuwa wakicheka sana pale. Kwa upande wangu nilikuwa naona ufahari sana kuona wake zangu wakipendana namna hii. Iryn ni mkubwa kwa mama J na wamepisha mwaka mmoja tu ni vile masuala ya mimba yalisababisha wife asimamishe masomo.

*******
Jumanne nilikuwa nina appointment ya kuonana na mzee Juma ambaye alisema tuonane mchana. Ile asubuhi baada ya kupata breakfast nilipata wazo la kwenda Masaki kule shuleni nikaonane na dada, niliwaza huenda akawa na mawasiliano na Kizoka.

Kizoka ndo alichukua tenda zote za kuwachukua watoto pale shule baada ya mimi kuachana na kazi ya Uber. Kwa upande mwingine nilikuwa nina wasiwasi wa kumpata yule dada, kwani shule zilikuwa zimefungwa. Nilijisemea kama na huu mpango utakwama bhasi nitatafuta Plan B ya kutafuta mtu mwingine wa kuingia naye mkataba.

Kabla ya kwenda ofisini nilipitia pale shuleni na bahati nzuri niliweza kukutana na mlinzi akanipa namba za yule dada secretary. Palepale nilimpigia simu na uzuri alikuwa na namba yangu hivyo sikupata shida kujitambulisha na nilimwambia shida yangu ni kupata namba ya jamaa. Baada ya maongezi alinambia ananitumia sio muda mrefu na tukaagana.

Ilipita dakika 5 akanitumia namba zote za jamaa na mimi nilifanya kumpigia simu ndugu yangu, lakini nayo ikawa haipatikaniki. Baada ya kufika ofisini nilianza kuhakiki mauzo pamoja na EFD na baada ya kujiridhisha niliondoka kwenda kuonana na Mzee Juma.

Ndani ya muda mfupi niliwasili home na baada ya kukaribishwa ndani pale seblen alikuwepo mzee Juma pamoja na Mrs, bila kumsahau Camila na kulikuwa na watu wawili ambao ni ndugu zao.

Niliwasalimia wote na haikuchukua muda dada alikuja na juice kwenye glass,

MZEE: “Insider akija hapa huwa mnamletea juice zenu amewaambia anazipenda?. Tuletee wine na glass tuendelee kunywa hapa, juice ni za wagonjwa.”

CAMI: “Hata wine wanakunywa wagonjwa mzee.”

MZEE: “Afadhali hii kuliko juice. Insider karibu kijana wangu umekuwa adimu sana na kubwa kutokukuona kwenye lile tukio muhimu bila taarifa yoyote hapa ndo ilinipa maswali sana.”

MIMI: “Hapana mzee nilitamani sana niwepo ile siku, sema mambo yakaingiliana. Jane nilimpa taarifa kuwa ninaweza kurudi ontime na nikahudhuria tukio.”

MZEE: “Za huko Kenya? na ulikuwa na jambo gani huko.”

Muda huu Cami alikuwa makini sana kusikiliza maongezi yetu na mzee,

MIMI: “Kuna kampuni napiga nayo kazi, nilikwenda kuangalia masuala ya mizigo ndo hilo tu.”

MZEE: “Kama maswala ya kazi ni sawa huna haja ya kuwa na wasiwasi, kampuni ina deal na nini na iko wapi?”

MIMI: “Kampuni ina deal na masuala ya beauty na iko Masaki, pia tunabranch hapo Mikocheni.”

MZEE: “Vizuri, last time tuliongea kuhusu masuala ya project na nilikwambia nitaanza January. Sasa nakuomba utafanya kama tulivyoongea na utasaidiana na Cami, ninaimani na nyinyi.”

MIMI: “Sawa mzee haina shida, ondoa na wasiwasi kabisa.”

MZEE: “Tutaonana mara ya mwisho kuweka mambo sawa kuhusu hili, pia nilitaka nijue na afya yako kwa ujumla pamoja na maendeleo ya familia yako. Jambo lingine sisi kama rafiki za Pama kupitia umoja wetu tuliandaa zawadi ya kukupa kwakuwa nasi kupindi chote. Tunathamini kwa kujitoa kwako tangu kipindi cha msiba mpaka Jane anajifungua, na tuliona ni busara tukafanya jambo kwaajili yako.”

Mzee Juma alimuagiza binti yake Cami ndani akachukue bag lake na baada ya Cami kurudi na kumkabidhi bag, Mzee alitoa bahasha imetuna na akanikabidhi.

Nilishukuru sana pale maana sikutegemea kama nitapata hii zawadi ilikuwa ni surprise na tuliendelea kuongea masuala mengine ya maisha na baadae nikawaaga nikaondoka maeneo yale.

Baada ya kurudi home ule usiku migogoro na wife iliendelea na wimbo ni uleule alikuwa anataka tickets za safari ya Kenya na alikuwa haelewi kabisa,

WIFE: “Hivi inawezekanaje unapanda ndege bila kuwa na ticket?”

MIMI: “Ticket nilikatiwa na mama, airport nilitaja jina nikaonesha ID nikaruhusiwa. Kama huniamini muulize Iryn atakwambia kama mimi nasema ukweli au nadanganya.”

WIFE: “Si ndo wewe ulinambia masuala ya kazi na binafsi Iryn asihusishwe?. Kinacholeta ugumu kwenye ticket ni nini? Ndomana nakuwa na wasiwasi juu yako kwanini hili jambo liwe gumu hivi?”

Ukweli nilikuwa sijui nafanyaje kuhusu hili jambo na niliwaza asubuhi niongee na Iryn, ili anishauri nitumie mbinu gani kumaliza hili jambo. Licha ya yote bado niliamini Iryn anaweza kunisaidia nikasovu, na kama itashindikana bhasi liwalo na liwe.

Asubuhi nilifanya mawasiliano na Iryn kumuomba aangalie means yoyote ya kunisaidia, na yeye aliendelea kusimamia kwa hili suala hata yeye hajui anafanyaje sababu ni gumu kwake.

IRYN: “Baby I wish nikusaidie lakini nakosa mbinu ya kukusaidia, ulishakosea toka mapema.”

MIMI: “Remember nilijitoa kuja Ethiopia kwaajili yako, nilimuacha mama yangu mzazi home kwaajili yako. Ukiona nimeachana na wife na wewe una uwezo wa kunisaidia sitakusamehe kwa hili na nime maanisha.”

IRYN: “What the f*ck are you talking about? Kwamba mimi kwako sio kitu? Sihitaji mapenzi kutoka kwako?. Anyway hayo yote ulifanya kwaajili ya mwanao na sio mimi na kama ukiona hata mwanao hastahili kufanyiwa hayo acha. Thank you.”

MIMI: “Baby sijamaa……”. Alikata simu.

Nilishusha pumzi ndefu sana nikajisemea hapa kweli nimezingua na sijui itakuwaje. Niliwasha gari nikaondoka kwenda Mikocheni kuendelea na majukumu yangu.

Mchana mama alinipigia simu akanambia nijitahidi sana leo navyorudi niwe na hizo tickets maana tabia nazozionesha mbele yake sio nzuri. Mama alisisitiza sana nifanye hivo ili kurudisha amani ndani ya nyumba na pia anakikao na sisi, itakuwa ngumu kukaa kama hakuna amani.

Niliona wananichanganya tu na ile jioni niliondoka na Lucy kwenda Mlimani city kupoteza muda na tulikaa Samakisamaki. Tuliagiza vinywaji na tuliendelea na story pale na nilimpa mrejesho wa mazungumzo yangu na Iryn na jinsi tulivyotofautiana, akanishauri nitulize akili nitafute Plan B.

Mida ya saa 2 tuliagana nikarudi home na wakati niko njiani nilikuwa nawaza namna ya kuongea ili nieleweke kwa mama na wife.

Sawa nitawaambia mama kasafiri na amesema ticket ziko kwenye laptop yake ambayo iko Dar na akirudi atanipa ili niweke kwenye matumizi ya kampuni.”

Kwa upande mwingine nilijikuta najuta kwa kutofikiria mapema na nilijisemea kweli “njia ya muongo ni fupi.

Baada ya kuwasili home sikutaka kuingia ndani na nilipark gari pembeni ya fense nikaendele kutafakari. Nilichukua simu yangu, nikawasha data na palepale iliingia whatsap notification ya text kutoka kwa Iryn. Baada ya kufungua sikuamini nachokiona mbele yangu nilijikuta najawa na furaha sana muda huu, alikuwa kanitumia ticket 2 za Kenya Airways. Ticket zote zilikuwa zinasoma jina langu na ticket ya kwanza ilikuwa na tarehe ya kuondoka na ticket nyingine ilikuwa na tarehe ya kurudi.

Alituma zile tickets bila kuandika chochote na mimi nilijikuta nafurahi tu muda huu maana alikuwa kacheza kama Pele. Nilimpigia simu ili kumshukuru kwa alichofanya maana ningekuwa ni mpumbavu kutomshukuru kwa hili jambo alilokuwa kalifanya,

MIMI: “Baby thank you, you really surprised me.”

IRYN: “Don’t be, sikupenda kauli ulizoongea asubuhi nilijua ni hasira tu.”

MIMI: “I’m really sorry, nili-panick mummy ndomana ikawa hivyo.”

IRYN: “Darling wewe ni mzembe sana, ile siku niliyokuomba simu yako tukiwa airport nilifuta picha zote ulizokuwa umepiga pamoja na ile video uliyonichukua na Jimmy tukicheza. Nilijua mama J lazima atakuchunguza, jenga tabia ya kubadili mara kwa mara passcode za simu, unajiachia mno baby.”

MIMI: “Mimi nilikuwa sina hata habari kama umefuta picha, you're so ingenious. Leo umenifurahisha sana baby nambie nikupe zawadi gani, chochote unachotaka nitafanya.”

IRYN: “Nipeleke kwenu nikaijue familia yako, sihitaji kingine zaidi ya hili.”

TUTAENDELEA
Unazidi kujikaanga siku hadi siku🤣😀
 
Mkubwa INSIDER MAN mbona nilikuwa mule mule na sijapata zawad?
Screenshot_2024-08-01-05-11-29-407_com.android.chrome.jpg
 
SEASON 02
EPISODE 21:

“BY INSIDER MAN”

ILIKOISHIA:
Kwa lile tukio hata Hilda alibaki anashangaa maana hakutegemea kuona mama akinifanyia vile, ukizingatia mimi ni mtu ambaye ananikubali na kuniamini, ukweli nilijisikia vibaya sana baada ya hili tukio…..

ENDELEA:

Hilda uvumilivu ulimshida na alianza kuniuliza pale shida ni nini? Mbona kama mama anaonekana hayuko sawa toka anione na walikuwa wakiongea vizuri tu?

HILDA: “Insider what’s is really going on? Mbona mama kabadilika ghafla?”

MIMI: “Hata sijui labda kuna kitu nitakuwa nimezingua, acha niende ndani nikaongee nae.”

HILDA: “No usiende hayuko sawa, wewe mtafute private muongee hapa ni ofisini inaweza leta matatizo, cha kukushauri wewe ondoka.”

Niliwaza kwa sekunde kadhaa nikaona Hilda yuko sawa, cha kufanya nimtafute mama private ili tuongee. Ofcourse nilikuwa nishajua tatizo ni nini na hapa nikaanza kumblame Iryn maana tangu muda mrefu nilikuwa namsisitiza aongee na mama kabla mambo hayajaharibika.

Niliondoka kurudi tena kwa Allen na muda wote ambao niko njiani nilikuwa nawaza kuhusu mama Janeth maana alionekana kunichukia sana. Sasa, kumpigia simu Iryn sikuwa na nguvu sababu alikuwa kaniblock, palepale nilipata wazo niende kwa Sumaiya nikaongee nae maana yeye na mama ndo zinaiva sana.

Nilipiga U-turn nikaanza safari ya kwenda kwa Sumaiya afu hata sikumpigia simu na baada ya kuwasili ofisini kwake nilitulia parking, nilimpigia simu akanambia nimsubiria soon atakuwa kafika. Baada ya dakika 10 Sumaiya alikuja na alikaa siti ya mbele, kama kawaida yake alianza kunifanyia vituko vyake, lakini mimi mawazo yangu yalikuwa mbali sana, hata yeye alihisi something wrong;

SUMAIYA: “Insider upo sawa? Sijakuzoea hivi.”

MIMI: “Sumaiya nimeharibu tayari sijui hata mama atanielewaje kwahili.”

SUMAIYA: “Mama Janeth huyuhuyu?”

MIMI: “Ndio mshikaji wangu yaani daah!”

SUMAIYA: “Kwani amejua unatoka kimahusiano na binti yake? ila hata kama akijua shida ni nini? Au anataka umkaze na yeye?”

MIMI: “Hivi kuna jambo lolote Iryn kakwambia kuhusu yeye?.”

SUMAIYA: “Hapana ni muda hatujawa intouched, embu niambie ni nini kinaendelea kati yako na mama?”

Nilijifikiria pale nikaona acha nimwambie kinachoendelea hakuna haja ya kumficha,

MIMI: “Sikia, Iryn ni mjamzito ana mimba yangu ina miezi 4 sasa…”

Alinikatisha maongezi yangu,

SUMAIYA: “Wewee usinambie! Hapa sasa nakupa nyota zote umecheza kama Messi, yaani usingempa mimba ningekulaumu sana.”

MIMI: “Sijamaliza kuongea, hapa unavyoniona nina mke na mtoto, sikuwahi kukwambia hii kitu.”

SUMAIYA: “Wee Insider una mke toka lini?.”

MIMI: “Kitambo sana na mtoto anafukuzia miaka 2.”

SUMAIYA: “Duuh! Unasiri sana Insider kumbe ulikuwa unanichora tu, kwanini hukunambia?.”

MIMI: “Hata ningekwambia ingekusaidia nini?.”

SUMAIYA: “So, Iryn anafahamu kuwa una mke?”

MIMI: “Anafahamu na alibeba mimba kwa ridhaa yake.”

SUMAIYA: “Aisee upo vizuri, nyota yako ni international.”

MIMI: “Mama anajua kinachoendelea ndomana amenichukia ghafla, na kibaya zaidi anajua mimi nina mke na mtoto, hili pia limechangia mama kunichukia, ukizingatia alishawahi kuniuliza kuhusu mahusiano yangu na Iryn.”

SUMAIYA: “Hapo kweli pagumu na mama anavyompenda Iryn lazima akuchukie kwa hili, Kuna jambo pia nafikiri hulifahamu hata Iryn pia halijui ila mimi najua.”

MIMI: “Ni jambo gani hilo tena?”

SUMAIYA: “Insider hii ishu nakwambia ila naomba ufunge mdomo wako usije kujaribu kuropoka kwa Iryn, nakwambia iwe siri yako na nina kuamini.”

MIMI: “Usiwe na wasiwasi you have my word.”

SUMAIYA: “Yule Smith mtoto wa mwisho wa mama ni mdogo wake Iryn, mama kazaa na baba yake.”

Mimi nilikuwa najua kuhusu hii ishu kupitia Iryn mwenyewe, lakini bado alisema anaendelea na uchuguzi, sasa kusikia Sumaiya naye anajua kila kitu, bhasi nilijisemea Sumaiya atakuwa anajua siri nyingi sana, mimi nilijifanya sijui kinachoendelea;

MIMI: “Umejuaje hili? Mbona kama siamini amini.”

SUMAIYA: “Ndo uniamini sasa, mama na baba Iryn wanamahusiano ya siri sana na mama anakwenda sana South Africa, hata juzi kati kabla ya kurudi alikuwa huko kupewa dudu.”

MIMI: “Wewe ulijuaje Smith ni mdogo wa Iryn?”

SUMAIYA: “Mama mwenyewe aliniambia, ndomana unaona anampenda sana Iryn sababu ya hii.”

MIMI: “So mama Janeth alikuwa anamzunguka mama yake Iryn kwa kutembea na mume wake sindio?”

SUMAIYA: “Insider haya mambo mengine sisi hayatuhusu, tujadili jambo lako uliloweka mezani.”

MIMI: “Embu nipe mawazo nini nifanye? Kidogo wewe una mazoea na mama unajua namna ya kumuingia na kutoka, nisaidie kwa hili, lengo langu tuongee tuliweke sawa hili.”

SUMAIYA: “Insider huna haja ya kuhangaika kwa hili, Master ni Iryn ndo anatakiwa aliweke sawa hili, wewe hata usihangaike, mama atakaa sawa tu hata usijipe stress, wewe fanya yako hata usiwaze kuhusu yeye.”

MIMI: “Sometimes ni bora ukajifanya mjinga ili mambo yaende, mimi lengo langu niliweke sawa hili jambo, kwahiyo unanishaurije?”

SUMAIYA: “Wewe tulia hayo ni mambo ya familia waachie wao, the truth is, she can’t hate you forever, wewe ni mkwe tayari atake asitake, mama nae uchi wa Iryn afu yeye anaumia.”

Akaanza kucheka pale,

MIMI: “Nawaza mpaka kuacha kazi ujue, sitoweza kufanya kazi kwa mazingira kama haya.”

SUMAIYA: “Acha ufala wewe, upo kwaajili ya mama au Iryn? Yaani uache kumsaidia mke wako kisa mama? Acha ujinga Insider, Iryn anakutegemea usifanye maamuzi ya kijinga, kwanza mama ataona umemwogopa, wewe fanya yako.”

MIMI: “Sawa bhana kumbe unaweza kumshauri mtu, ukiwa serious unakuwa na akili nzuri.”

SUMAIYA: “Leo unanipa gari yangu, najiona niko vizuri kuingia road.”

MIMI: “Nilitaka nikuwekee android TV ni vile nimekuwa na mambo mengi, kama unaharaka nayo ichukue.”

SUMAIYA: “Kwahiyo unataka kunipa lini?”

MIMI: “Ijumaa na leseni yako itakuwa tayari ili nikupe vyote kwa pamoja.”

SUMAIYA: “Sawa, ila unanipeleka home.”

MIMI: “Sawa haina shida, ila ndani sitaingia naishia nje tu”

SUMAIYA: “Haya baba twende.

Nilimpeleka Sumaiya kwake na muda ambao ninarudi home nilikuwa nawaza kuhusu mama Janeth pamoja na maneno aliyokuwa anaongea Sumaiya, niliwaza huenda anajua siri nyingi sana, hivyo itabidi nianze kumchimba taratibu.

Kwenye hili suala lawama zangu zote zilikuwa kwa Iryn maana alipaswa kumwambia mama hili jambo mapema sana, lakini alikuwa anasuasua mpaka mama amefahamu. Jambo lingine lililokuwa linaniumiza kichwa ni vile Iryn kuninunia afu nashindwa kuwasiliana nae ili tuyaweke mambo sawa.

Kwa upande mwingine allen alinitafuta kuniuliza kama narudi tena tuendelee na topic yetu maana nilikuwa nimemuaga kwa kumpa ahadi ya kurudi tena, nilimwomba kumtafuta kesho ili tumalize maongezi yetu.

Baada ya kurudi home nilikwenda chumbani kuoga na nilimkuta Junior akichezea simu ya mama yake, nikapata wazo la kuipekua simu yake, kimbembe Junior alikuwa hataki kunipa simu, kila nikitaka kuchukua alikuwa analia. Palepale nikapata wazo nimuwekee cartoon kwenye PC ili atoe simu, na nilifanya hivo plan yangu ikawa imetiki.

Nilianza kuipekua simu upande wa whatsapp na nilianza direct kutafuta chats zake na Iryn, lakini hakukuwa na chats zozote walizochat hivi karibuni, na niliendelea kuangalia chats zingine na nilibaini kuna Mafisi wanamtongoza sana, nikapotezea. Niliona chats za dada yake na nilifungua ili nisome chats zao, baada ya kufungua niliweza kugundua kwamba dada yake ndo anayemkomalia wife kuhusu mimi na Iryn kuwa na mahusiano, na mbaya zaidi alikuwa anamwambia afanye investigation ya ukaribu wetu.

Wife kwa upande wake alikuwa amemwambia dada yake kuhusu ujio wa Iryn pale home ile usiku na kuhusu mapenzi yake kwa Junior, dada yake alikuwa anakamia sana mimi na Iryn tuko kwa mahusiano. Alikuwa anamwambia mdogo wake aendelee kuwa karibu na Iryn maana yeye ndo rahisi kumchunguza na kujua ukweli, mbaya zaidi alimwambia itabidi waonane kwa maongezi zaidi.

Baada ya kusoma hizi chats zao hapa sasa nikajua tatizo sio mama J bali ni dada yake ambaye anasmell something fishy kati yangu na Iryn. Nilijisemea nitakuwa makini sana kuanzia kwenye simu yangu hasa kwenye chats zangu na Iryn, niliona niko vitani hivyo natakiwa kuwa makini sana kwa kipindi hiki.

Baada ya dakika 15 nilimsikia wife akija chumbani na alikuwa akimuita Junior;

“Junior nipe simu yangu nimpigie bibi.”

Na ile kuingia chumbani anatuona tuko busy na cartoon, akachukua simu yake akaondoka.

Muda huu nilipata wazo la kumcheki Iryn ili tuongee lakini alikuwa bado kaniwekea tofali. Niliwaza pale labda nimcheki kwa namba nyingine ili tuongee huenda ikasaidia, lakini niliona nitakuwa kama najimbeleza kwake, cha msingi nipotezee, kwa upande mwingine yale maneno ya kaka Allen yalikuwa yananipa jeuri na kiburi.

Kesho yake niliwahi sana kwenda Masaki na kipindi niko ofisini nilibaini Iryn bado hajaingiza mishahara kwa wafanyakazi maana yeye ndo huwa anahusika, sasa tumeanza mwezi mpya february afu hajafanya chochote niliona anazingua.

Nilimtumia mail kumkumbusha hili suala maana ni muhimu na mimi niliendelea kuandaa ripoti zingine, niliendelea kuwaza namna ugumu wa kazi unavyokuwa hasa ukichanganya mapenzi na kazi. Suluhisho na kuepusha matatizo kama haya niliona ni bora nika quit sababu vitu binafsi vina impact mpaka utendaji wa kampuni.

Baada ya nusu saa Hilda aliwasili ofisini huku kavaa skirt fupi sana kiasi kwamba ilikuwa ikimchora barabara. Mimi baada ya kumuona vile nilijifanya niko busy na kazi zangu na sikutaka kuongea chochote, ila yeye ndo alinza kunisalimia na akakaa kwenye sofa;

HILDA: “Insider tangu jana nafikiria kuhusu mama mkwe wako.”

Niliona Hilda ameanza kuvuka mipaka, niliona ameanza kufuatilia mambo yasiyo mhusu,

MIMI: “Ulikuwa unafikiria nini?”

HILDA: “Au hajapenda kumuona Iryn vile, afu na wewe ndo mhusika?”

MIMI: “I don’t know, ikifika muda kila kitu kitakuwa wazi.”

HILDA: “Jana nimekutumia ripoti ya mwezi, stock imeisha sidhani kama itaweza kusurvive muda mrefu.”

MIMI: “Stock haina shida kuna mzigo soon utakuwa bandarini, mimi natoka mara moja soon narudi.”

HILDA: “Sawa uwahi kurudi ili twende lunch.”

MIMI: “Leo nipo na wewe mpaka jioni sema ulivyovaa hivo utanifanya niingie matatizoni.”

Hilda aliishia kutabasam na niliondoka kwenda kuonana na Allen ofisini kwake ili tumalizie maongezi yetu.

Nilitumia muda mfupi sana kuwasili pale kwenye kampuni yao na nilikwenda moja kwa moja ofisini kwake nikaambiwa yuko kwenye kikao. Nilimtumia ujumbe kumpa taarifa na akanambia tuoanane mchana muda wa lunch kuanzia saa 7 mchan ili tuongee vizuri, na mimi kuondoka kurudi ofisini.

Kabla ya kurudi ofisini nilipitia shoppers kununua mazaga ya kupeleka ofisini kwaajili ya sisi na wateja kama maji ya kunywa, juice, soda na bites. Kipindi nanunua vitu simu yangu ilianza kuita na alikuwa ni Mary akinipigia na nilipokea kwa haraka sana;

MIMI: “Hi Mary.”

MARY: “Hi Insider za wewe?”

MIMI: “Salama mummy, nimefurahi kusikia sauti yako hata sikutegemea.”

MARY: “Ahsante sana dear, nilikuwa nakusalimia tu.”

MIMI: “Thank you, unasomeka pande zipi?”

MARY: “Niko Posta ofisini kwa mama but I won’t be here for too long.”

MIMI: “Karibu Masaki upajue ofisini kwangu.”

MARY: “Thank you leo nitakuja, navyotoka huku nitakujulisha.”

MIMI: “Karibu sana Mary.”

Saa sita na nusu Allen alinipigia simu ili tuoane kwaajili ya mazungumzo na tulikubaliana tukutane pale Salt restaurant. Sikutaka kupoteza muda na niliondoka kwenda eneo la tukio na yeye alikuwa ameshafika tayari na tulisalimiana tukaanza story;

ALLEN: “Bro sorry sana nilikuwa nina kikao afu sikutegemea kama ungekuja asubuhi.”

MIMI: “Usijali mimi ndo nilizingua nilipaswa kukupa taarifa mapema.”

ALLEN: “Mama kijacho anaendeleaje?”

MIMI: “Hakuna lolote kutoka kwake anajiandaa na mitihani kwasasa. Tuendelee na topic yetu ya jana maana tulizungumza vingi lakini hatukamaliza.”

ALLEN: “Ni sawa kabisa ila leo tutakuwa na solution ya hili jambo, usiwe na wasiwasi.”

MIMI: “Toka jana tuongee kidogo naona mabadiliko, ila kaka kuna jambo inatakiwa ujue, hata kama tukisubiri Iryn ajifungue ndo twende, bado mimi siwezi kumuoa unafikiri wazazi watakubali?”

ALLEN: “Una uhakika hutakuja kumuoa Iryn?”

MIMI: “Ndio siwezi kumuoa, yeye ni kama mchepuko kwangu na anajua hili.”

ALLEN: “Our future is an uncertainty, you never know, kinachomtofautisha Iryn na mama J ni kutambulika kwa wazazi na vile umemlipia mahali, lakini vingine vyote wako sawa na huyu soon atakuwa na mtoto wako.”

MIMI: “Upo sahihi lakini sasa…”

Alinikatisha maongezi yangu,

ALLEN: “Bado sijamaliza ipo hivi, mimi naona ni busara Iryn akaongea ukweli huko kwao kuhusu wewe kuwa una mke na mtoto, na ameridhia kuwa mke mdogo kwa hiyari yake.”

MIMI: “Kaka huoni kama nitaweza kukosa mtoto kizembe wakijua ukweli?”

ALLEN: “Toka jana nakwambia kuhusu hili, mwenye maamuzi na hii mimba ni dada mwenyewe na sio wazazi au sisi, yeye akisema ninazaa na kweli atazaa huna haja ya kuwa na wasiwasi.”

MIMI: “Sidhani kama atakuwa tayari kuwaambia wazazi hivyo, hawezi kubali anaweza kutengwa na ukoo.”

ALLEN: “Sasa ni bora kuwa wakweli kuhusu hili au tudanganye? Na kama tukiwaambia tutamuoa kumbuka tutakuwa tumeshaingia kwenye makubaliaono ya wazazi na tusipofanya hivyo tutakuwa matatizoni, kama unaona ni sawa kuwadanganya niko tayari kukupa kampani mpaka Ethiopia.”

MIMI: “Hapana naona option ya pili imekaa kimkakati sana ila kuna possibility ya kumkosa mtoto au hata akizaliwa akapewa ukoo wa kwao.”

ALLEN: “Haiwezekani huyo mtoto ni wako na sifikirii kama mama yake atakuwa tayari kukuweka mbali na mwanao, never. Hili suala wa kulimaliza ni Iryn mwenyewe wala sio sisi ni mwenyewe akae na familia yake awaambie ukweli kuhusu wewe na maridhio yake.”

MIMI: “Kaka usije ukanijaza kichwa afu mambo yakaenda viceversa maana sitaki kumpoteza huyu mtoto.”

ALLEN: “Na ukionesha weakness ya uhitaji sana wa mtoto ndo utampoteza sasa, just kuwa normal usioneshe wenge lolote.”

MIMI: “Duuh sawa bro nashukuru kwa mawazo yako.”

Wakati tunaendelea na mazungumzo Mary alipiga simu kunipa taarifa anatoka Posta hivyo nimuelekeze ofisi ilipo ili aje na mimi nilimwambia aje Salt atanikuta hapa, alisema haijui ilipo nimtumie location, nikamwambia akifika Cocobeach anipigie nimuelekeze.

Ndani ya dakika 30 alinipigia kunipa taarifa anakaribia na nikamueleekeza mpaka anafika na kwa mbali nilimuona akishuka kwa Vanguard, alikuwa amependeza sana na alizidi kuonekana ni mrembo sana.

Aliingia ndani akaja usawa wetu na tulianza kusalimiana pale na nilimtambulisha kwa Allen na story zingine zikaendelea;

MIMI: “Nambie mummy, mama mkwe hajambo?”

MARY: “Afu anakuulizia sana na mbaya zaidi Prisca anakosaga majibu ya kutoa.”

MIMI: “Hahahaa, msalimie sana, kumbe unajua kudrive ndinga nilikuwa sijui.”

MARY: “Yeah kimtindo kama hivi.”

MIMI: “Agiza food ule ili tuondoke najua hujala.”

Allen aliniaga anawahi ofisini na niliendelea kubaki pale na Mary nikimsubiri amalize kula, na baada ya kumaliza tuliondoka kwenda ofisini.

Baada ya kufika ofisini nilimpeleka moja kwa moja mpaka show room ili aangalie mawigi, kwa upande wake alionekana kuyapenda na alikuwa akishangaa bei zake,

MARY: “Insider wigs ni nzuri ila kwa hizi bei hapana mimi siwezi.”

MIMI: “Wig la gharama kuvaa ni bei gani?”

MARY: “Nakumbuka laki 5 na mama ndo alinunuliaga, hii Lace nimeipenda kwakweli niambie sifa zake.”

MIMI: “Huku sasa mimi ndo sijui ngoja nikuitie mtaalamu wa hizi kitu akuelekeze.”

Nilimuita Winny ili amuelekeze Mary kwa sifa za wigi ambazo atahitaji maelekezo;

WINNY: “Mrembo hio ni frontal lace natural hair black kutoka France, hio ni mkataba utavaa mpaka uichoke, haipukutishi na ni laini kama unavyoiona. Ukinunua hio wigi utapewa wig cap, brush, shampoo, sprays, gels na wig stand, bado una offa ya kuja hapa kusetiwa free mara 3.”

MARY: “Wow amazing, Insider hii wigi nimeipenda kwakweli ila sasa milion 2 ninatolea wapi?”

MIMI: “Kama umeipenda, nakupa offa ichukue kama zawadi yangu kwako, umenifanyia mambo mengi sana hio ni shukrani yangu.”

MARY: “Thank you Insider.”

Winny alishangaa sana kuona nampa Mary ofa ya wigi na nilimwambia yeye ndo atakaye mhudumia Mary. Mary alisema atakuja jumamosi kwaajili ya kuweka wigi na tuliondoka tukaenda ofisini kuendelea na mazungumzo.

MARY: “Insider Salon yenu ni international sijaona Salon hapa Dar ya kushindana na nyie.”

MIMI: “Ofcourse hata wateja wetu alimia 95 ni foreigners, naona unazidi kuwa mrembo nipe siri ya mafanikio.”

MARY: “Nakula vizuri, nalala kwa wakati, sina stress kwanini nisiwe mzuri?”

MIMI: “Hahahaaa hata mimi naona sio kwa kung’aa huko mpaka unafanya mapigo ya moyo wangu yaongezeke spidi.”

MARY: “Mhhh! Prisca mnawasiliana?”

MIMI: “Yeah tuko intouched ila sio sana, nafurahi kuona amemove on.”

MARY: “How did you know?”

MIMI: “I know na ni jambo zuri, tuachane na haya yalishapita, vipi kuhusu wewe usinambie bado upo single sitokuelewa.”

MARY: “Bado niko sokoni, soko gumu sana huku nje..”

Tulianza kucheka wote pale na aliendelea kuongea;

“Insider kuna kitu nataka kushare na wewe, nimepata kazi Posta, kuna kampuni nitakuwa nafanya nayo kazi but nataka nitafute apartment karibu.”

MIMI: “Unataka kuondoka home? Kwamba utashindwa kuamka mapema uwahi kazini?.”

MARY: “Si unajua nasoma pia, bado research na muda mwingi nitakuwa nashinda library, pia nimekuwa mtu mzima nahitaji kukua.”

MIMI: “Mimi sikushauri uhame home, unataka majukumu ya nini mapema hivi? Hizo pesa za kodi si bora uziweke zije zikusaidie hapo baadae?”

MARY: “Bhana, wewe na mama lenu moja naye hataki kabisa kusikia hizi habari, but weekend nakuwa narudi home.”

MIMI: “Mmh, wewe fanya kutokana na moyo wako unavyotaka na angalia mipango yako, ukiona kuna haja ya kupanga ni sawa.”

Hilda aliingia ofisini alikuwa lunch na baada ya kumuona Mary walisalimiana, kisha akaanza kunilamikia nimemdanganya kuhusu kwenda kula lunch na mimi nikajitetea nilikuwa na mgeni ndomana nikashindwa.

Mary aliniaga anaondoka kwa ahadi ya kurudi jumamosi kwaajili ya kuweka wigi, na mimi sikuchukua muda nikamuaga Hilda naondoka kwenda Mikocheni kuonana na Lucy. Lengo la kwenda kuonana na Lucy ni sakata la Landlord na niliona ni busara tukaonana face to face kuliko kuongea kwa simu.

Baada ya kuwasili Mikocheni ofisini nilionana na Lucy tukaanza mazungumzo na kubwa alisema ameongea na Iryn ila yuko kwenye maandalizi ya mitihani hivyo mpaka weekend ndo watapanga vizuri.

MIMI: “Unajua Iryn kaniblock.”

LUCY: “Uliniambia, si hutaki nikumbelezee unaleta ubeberu shauri zako.”

MIMI: “Shida ukiongea nae atajua mimi nimekwambia kinachoendelea afu yeye mpaka sasa hajakwambia, atleast akufungukie hapo kidogo itakuwa na nguvu.”

LUCY: “Sema mke wako kabadilika sahivi, sijui ndo mimba inamchanganya yaani simuelewi kabisa.”

MIMI: “Afadhali hata wewe umeliona hili maana unaonaga mimi ndo mwenye shida.”

Baada ya maongezi ya muda mfupi nilimuaga Lucy nikaondoka kurudi home mapema kabisa.

Kipindi niko home nilikuwa nikitafakari ushauri wa Allen na niliona yuko sahihi ni bora Iryn akasema ukweli huko kwao kuhusu mimi before it’s too late au wazazi wakajua kupitia mama Janeth.

Usiku Jane alinipigia simu kunipa taarifa kuwa ameanza biashara na nilimuahidi kwenda dukani siku ya kesho na nitashinda siku nzima. Jane alionesha kuwa na furaha sana baada ya kuanza biashara hata mimi kwa upande wangu nilijisikia vizuri sana kuona Jane akiwa na furaha ukizingatia marehemu Pama alinipa task ya kuhakikisha Jane anakuwa salama na mtoto.

Kesho yake nilikwenda dukani kwa Jane kama nilivyokuwa nimemuahidi ili kuona maendeleo kwa ujumla, duka lilikuwa limejaa sana na lilionekana kupendeza sana, wateja nao hawakuwa mbali walikuwa wanakuja kwa wingi.

Nilishinda siku 2 mfululizo dukani na nilikuwa nikisaidiana kazi na dada ambaye alimtoa home na kumleta dukani sababu alikuwa anamuamini, Jane alikuwa anakuja pale shop na kuondoka maana asingeweza kumwacha mtoto home.
******

Jumamosi nikiwa ofisini nilipata wazo nimpigie simu mama niombe kuonana nae ili tuzungumze, nilipiga simu mara 2 bila majibu na niliamua kumtumia ujumbe ambao niliandika kuomba kuonana nae kwaajili ya mazungumzo, lakini sikujibiwa ni kama vile hakuiona message yangu.

Nilikumbuka maneno ya Sumaiya nikaona alikuwa sahihi kusema haya mambo ni ya familia, hivyo niwaachie wao wenyewe wayamalize na nikiendelea kujibembeleza nitapoteza thamani yangu. Kwa upande mwingine kuendelea kufanya kazi kwenye mazingira haya niliona nitazidi kuwa kwenye wakati mgumu, ukizingatia sipo kwenye maelewano mazuri na hawa wahusika wakuu, Iryn na mama yake.

Muda huu Mary alinipigia simu kunipa taarifa kuwa yuko njiani anakuja kuweka wigi lake na kufikia saa 7 mchana atakuwa around. Nilimpanga Winny mapema kuhusu ujio wa Mary, nilitaka yeye ndo amuhudumie na sio mtu mwingine.

Saa 7 mchana Mary aliingia na Vanguard pale ofisini na mimi nilitoka kumpokea na tuliishia kukumbatiana, sasa Mary alikuwa katembea na mdogo wake Ivy, ilikuwa ni surprise kwakweli na sikutegemea kabisa.

MIMI: “Karibu sana naona leo umeamua kunisirprise, Ivy hujambo?”

MARY: “Ahsante, ameforce tuje wote ndomana na sijamwambia nakuja kwako.”

IVY: “Sijambo shem tumekumiss, why can't you come home?”

MIMI: “I will come Ivy, today I am happy to see you again."

IVY: “Me too.”

MARY: “Insider utanisaidia kumpeleka Ivy lunch hajala mchana.”

IVY: “I’m not hungry.”

MIMI: “Ivy tutakwenda wote kula sawa?. Mary wewe kaendelee huko ndani dada anakusubiri zoezi lianze.”

Mary alikwenda ndani, tulikaa nje kibarazani tukipiga story na Ivy maana ni muongeaji, huwezi jutia kuwa naye karibu;

MIMI: “Nani alikwambia mimi ni shem kwako?”

IVY: “Dada Prisca told me.”

MIMI: “Niite Uncle Insider sawa eeh?”

IVY: “Sawa uncle.”

MIMI: “Let’s go tukale lunch, unataka kula nini?”

IVY: “Pizza”

Tuliondoka kwenda kula Pizza, muda ambao tuko njiani mama alinipigia simu, habari kubwa alisema anaona kuna jambo linanisumbua akili lakini siko tayari kushare na mtu, aliendelea kunisisitiza kama nipo tayari bhasi nimwambie ili aangalie namna ya kunisaidia hata kimawazo au ushauri.

Kwa upande wangu sikuwa tayari kumwambia mama kuhusu hili jambo na niliendelea kumkatalia kuwa sio kweli na mimi niko sawa, licha ya kutokubaliana na mawazo yangu

Hili jambo siwezi kushare na wazazi kwa kipindi hiki mpaka pale mambo yatakapokuwa sawa ndo nitashare ila kwasasa mtu wa kushare nae ni sister tu.”

Baada ya kuwasili Pizzahut niliagiza pizza medium na nilikwenda kula pizza kwaajili ya kumpa kampani Ivy, haya madude mimi huwa siyapendelei kabisa. Nilipiga slice 2 nikamuachia Ivy aendelee kula, nikatoa simu kumpigia sister ili nimpe taarifa za kwenda Arusha anipe na ratiba zake mapema kabla ya kwenda.

Tulipiga story nyingi sana na sister na tulikubaliana niende Arusha mwezi wa pili mwishoni maana atakuwa likizo, hivyo atakuwa na muda mzuri wa kukaa na mimi mdogo wake.

Kwa upande mwingine Ivy alikuwa amemaliza kula na alimwambia dada afunge slice 2 zilizobaki na alisema kwaajili ya dada yake Mary na tukaondoka kurudi ofisini.

Kufikia saa 10 jioni Mary alikuwa tayari kamaliza kutengenezwa na alipendeza sana mpaka nikajikuta naanza kupagawa, alikuwa kawaka sana kwa jinsi alivyo mzuri by nature na wigi alilokuwa kawekewa plus madikodiko mengine alikuwa bonge la pisi hata yeye aliishia kufurahi tu.

MIMI: ”Umependeza sana yaani umebadilika umekuwa pisi ya kimataifa.”

MARY: “Thank you Insider, ukweli hata mimi najishangaa sipati picha huko home leo na shoga zangu wakiona lazima waulize nilikokwenda.”

MIMI: ”Wewe wakaribishe sana waje hapa.”

MARY: “Insider naenda home kumpeleka Ivy but naomba badae tutoke kama unanafasi please.”

Nilijifikiria kwa sekunde kadhaa nikaona sina ratiba yoyote, acha nikubali ili niendelee kumfurahisha Mary;

MIMI: ”Sawa haina shida, mimi nitabaki nikikusubiri hapa ofisini so utanambia ukiwa tayari.”

MARY: “See you soon, Ivy twende, mwambie Ahsante shem Insider.”

IVY: ”No, he wants me to call him Uncle Insider.”

Mary aliniangalia afu akatabasamu kwa kutingisha kichwa na nilimsindikiza mpaka parking na kabla ya kuingia kwa gari alikuja akanikumbatia na wakaondoka, kugeuka nyuma namuona Winny yuko kibarazani anatabasamu, nilisogea mpaka usawa wake tukaanza story;

MIMI: “Leo umetisha sana itabidi nikupe zawadi.”

WINNY: “Namuona kafurahi mwenyewe hata haamini kama ni yeye, ni nani uyo?”

MIMI: “Huyo alikuwa shem wangu, nilitokaga na mdogo wake but tuna mawasiliano mazuri.”

WINNY: “Insider unapendwa sana na watu, just imagine umeachana na mdogo wake lakini bado mnacheka vizuri, ni wanaume wachache wenye bahati kama yako.”

MIMI: “Winny umeanza kunichokoza.”

Na nilianza kuslap makalio yake akakimbia ndani na mimi nikaenda ofisini na niliamua kumpa Hilda utawala akapumzike na nilimwambia aniachie ofisi na yeye aliishia kufurahi akaondoka.

Nilikaa ofisini mpaka saa 2 za usiku ndo Mary kunipigia simu kunipa taarifa anatoka home anakuja Masaki, nilikuwa nishasahau kama nina miadi ya kukutana na Mary.

Baada ya lisaa aliwasili na tulikutana ofisini nje ya geti alikuwa na Uber, nilimpick tukakubaliana twende Wavuvi Kempu. Baada ya kuwasili eneo la tukio na kushuka hapa sasa ndo namuona Mary vizuri, aisee alikuwa kapendeza sana maana alivaa skin jeans ya light blue ambayo imemkaa vizuri na kiuno kilichoreka na juu alikuwa kavaa top nyeusi iliyoishia chini ya kitovu na glass nyeusi.

Mary kabarikiwa shepu nzuri sana, sasa jinsi alivyokuwa kawaka niliishia kumsifia pale na nilimshika mkono tukazama ndani, tukatafuta sehemu nzuri tukakaa na mhudumu alikuwa tayari kafika kutusikiliza, tukaagiza Hennesy na mixers.

Ndani ya muda mfupi dada alikuwa katuletea kinywaji tukaanza kunywa huku tunapiga story, ofcourse tulikuwa tumemisiana sana maana ni kitambo tulikuwa hatujakaa pamoja.

Story zetu kubwa zilibase kwenye mahusiano na maisha kwa ujumla, Mary kwa upande wake alitaka kujua kama bado nina pasha kiporo na mdogo wake, nilimkatalia katakata.

Tulikuwa deep sana kimaongezi na kadri muda unavyozidi kwenda na pombe kukolea tulianza kuoneshana hisia za kimapenzi waziwazi, kuna muda tulikuwa tunacheza pamoja na kukumbatiana.

Mida ya saa 6 usiku wife alinipigia simu, baada ya kuona ni wife niliwaza haraka nikaona wacha nikapokee simu yake kwenye gari, nisipo-pokea italeta shida, nilimuaga Mary nakwenda washroom lengo nikaongee na wife.

Simu ilikuwa imekata tayari na aliendelea kupiga kwa mara ya pili na baada ya kuingia kwa gari nikapokea na tukaanza mazungumzo;

“Nambie mke wangu hujalala tu?”

“Napataje usingizi na wewe mpaka sasa hujarudi, umepitia wapi?”

Nilipiga hesabu za haraka nikaona acha niwe mkweli,

“Mke wangu siko sawa kabisa nimeona nipitie kunywa ili nikae sawa.”

“Hivi unaakili wewe? Sasa pombe ndo zinakuweka sawa?”

“Nikirudi home makelele si bora ninywe tu.”

“Baba J umekaa chini na mimi kunambia matatizo yako? Nini maana ya kuishi pamoja kama hunambii shida zako? Sijapenda naomba urudi home mapema tuongee, kama huwezi nambie ulipo nikufuate.”

“Haina haja mimi niko sawa na nitarudi home, usiwe na wasiwasi.”

“Haya, sisi tunalala byee, Takecare.”

Baada ya kurudi ndani Mary alianza kulalamika nimemuacha alone, ilibidi nimbembeleze ili atulie na nilimwambia ukweli kwamba nilikuwa naongea na wife.

Mary alikuwa close sana na mimi ‘zero distance’ na tuliendelea kucheza pamoja huku nazungusha mikono kwenye makario yake na yeye alizungusha mikono kwenye kiuno changu. Network yangu ilikuwa ishahama muda mrefu sana na yeye alikuwa kalainika sana, tulikuwa kwenye huba zito sana kiasi kwamba tulianza kupeana makiss bila aibu, licha ya nyomi ya watu iliyokuwepo maeneo haya.

Nilicheki muda simu yangu ilikuwa inaonesha ni saa 7 usiku na madakika, nikamwambia Mary tuondoke akasema sawa. Ile kufika kwenye gari tulianza kuexchange saliva tena kwa fujo kwelikweli na sikuchukua muda nikapandisha mkono kwenye vifuu vyake. Hapa sasa alianza kutoa kelele za nguvu na ile kushusha mkono kwenye bustani yake ilikuwa tapatapa yaani imemwagiliwa vya kutosha na muda huu alikuwa hoi akinitizama tu kwa macho ya kurembua.

Nilimwacha afu nikaanza kujifikiria niondoke naye au nirudi home? Maana kufikia stage hii Mary asingeweza kuwa na jeuri ya kunikazia, kuondoka nae ilikuwa ni lazima 100%.

Wakati naendelea kutafakari, alianza kuongea pale,

“Insider where are you taking me?”

“I don’t know.”


EPISODE 22
COMING SOON:
Imepita hiyo...!
 
Ndugu zangu naongeza 50k nyingine.

1. Kizoka nitampa gari Episode ya ngapi? (25k)

2. Nitakwenda Zanzibar kufuatilia mzigo uliotumwa na Iryn. Nitaongozana na nani? (25k).

Kazi kwenu, niko honestly kwa atakae patia atapata cash yake.

NB: Wa kwanza kupatia ndo atakuwa mshindi.
Epsod ijayo kizoka anakula kitu
 
SEASON 02
EPISODE 21:

“BY INSIDER MAN”

ILIKOISHIA:
Kwa lile tukio hata Hilda alibaki anashangaa maana hakutegemea kuona mama akinifanyia vile, ukizingatia mimi ni mtu ambaye ananikubali na kuniamini, ukweli nilijisikia vibaya sana baada ya hili tukio…..

ENDELEA:

Hilda uvumilivu ulimshida na alianza kuniuliza pale shida ni nini? Mbona kama mama anaonekana hayuko sawa toka anione na walikuwa wakiongea vizuri tu?

HILDA: “Insider what’s is really going on? Mbona mama kabadilika ghafla?”

MIMI: “Hata sijui labda kuna kitu nitakuwa nimezingua, acha niende ndani nikaongee nae.”

HILDA: “No usiende hayuko sawa, wewe mtafute private muongee hapa ni ofisini inaweza leta matatizo, cha kukushauri wewe ondoka.”

Niliwaza kwa sekunde kadhaa nikaona Hilda yuko sawa, cha kufanya nimtafute mama private ili tuongee. Ofcourse nilikuwa nishajua tatizo ni nini na hapa nikaanza kumblame Iryn maana tangu muda mrefu nilikuwa namsisitiza aongee na mama kabla mambo hayajaharibika.

Niliondoka kurudi tena kwa Allen na muda wote ambao niko njiani nilikuwa nawaza kuhusu mama Janeth maana alionekana kunichukia sana. Sasa, kumpigia simu Iryn sikuwa na nguvu sababu alikuwa kaniblock, palepale nilipata wazo niende kwa Sumaiya nikaongee nae maana yeye na mama ndo zinaiva sana.

Nilipiga U-turn nikaanza safari ya kwenda kwa Sumaiya afu hata sikumpigia simu na baada ya kuwasili ofisini kwake nilitulia parking, nilimpigia simu akanambia nimsubiria soon atakuwa kafika. Baada ya dakika 10 Sumaiya alikuja na alikaa siti ya mbele, kama kawaida yake alianza kunifanyia vituko vyake, lakini mimi mawazo yangu yalikuwa mbali sana, hata yeye alihisi something wrong;

SUMAIYA: “Insider upo sawa? Sijakuzoea hivi.”

MIMI: “Sumaiya nimeharibu tayari sijui hata mama atanielewaje kwahili.”

SUMAIYA: “Mama Janeth huyuhuyu?”

MIMI: “Ndio mshikaji wangu yaani daah!”

SUMAIYA: “Kwani amejua unatoka kimahusiano na binti yake? ila hata kama akijua shida ni nini? Au anataka umkaze na yeye?”

MIMI: “Hivi kuna jambo lolote Iryn kakwambia kuhusu yeye?.”

SUMAIYA: “Hapana ni muda hatujawa intouched, embu niambie ni nini kinaendelea kati yako na mama?”

Nilijifikiria pale nikaona acha nimwambie kinachoendelea hakuna haja ya kumficha,

MIMI: “Sikia, Iryn ni mjamzito ana mimba yangu ina miezi 4 sasa…”

Alinikatisha maongezi yangu,

SUMAIYA: “Wewee usinambie! Hapa sasa nakupa nyota zote umecheza kama Messi, yaani usingempa mimba ningekulaumu sana.”

MIMI: “Sijamaliza kuongea, hapa unavyoniona nina mke na mtoto, sikuwahi kukwambia hii kitu.”

SUMAIYA: “Wee Insider una mke toka lini?.”

MIMI: “Kitambo sana na mtoto anafukuzia miaka 2.”

SUMAIYA: “Duuh! Unasiri sana Insider kumbe ulikuwa unanichora tu, kwanini hukunambia?.”

MIMI: “Hata ningekwambia ingekusaidia nini?.”

SUMAIYA: “So, Iryn anafahamu kuwa una mke?”

MIMI: “Anafahamu na alibeba mimba kwa ridhaa yake.”

SUMAIYA: “Aisee upo vizuri, nyota yako ni international.”

MIMI: “Mama anajua kinachoendelea ndomana amenichukia ghafla, na kibaya zaidi anajua mimi nina mke na mtoto, hili pia limechangia mama kunichukia, ukizingatia alishawahi kuniuliza kuhusu mahusiano yangu na Iryn.”

SUMAIYA: “Hapo kweli pagumu na mama anavyompenda Iryn lazima akuchukie kwa hili, Kuna jambo pia nafikiri hulifahamu hata Iryn pia halijui ila mimi najua.”

MIMI: “Ni jambo gani hilo tena?”

SUMAIYA: “Insider hii ishu nakwambia ila naomba ufunge mdomo wako usije kujaribu kuropoka kwa Iryn, nakwambia iwe siri yako na nina kuamini.”

MIMI: “Usiwe na wasiwasi you have my word.”

SUMAIYA: “Yule Smith mtoto wa mwisho wa mama ni mdogo wake Iryn, mama kazaa na baba yake.”

Mimi nilikuwa najua kuhusu hii ishu kupitia Iryn mwenyewe, lakini bado alisema anaendelea na uchuguzi, sasa kusikia Sumaiya naye anajua kila kitu, bhasi nilijisemea Sumaiya atakuwa anajua siri nyingi sana, mimi nilijifanya sijui kinachoendelea;

MIMI: “Umejuaje hili? Mbona kama siamini amini.”

SUMAIYA: “Ndo uniamini sasa, mama na baba Iryn wanamahusiano ya siri sana na mama anakwenda sana South Africa, hata juzi kati kabla ya kurudi alikuwa huko kupewa dudu.”

MIMI: “Wewe ulijuaje Smith ni mdogo wa Iryn?”

SUMAIYA: “Mama mwenyewe aliniambia, ndomana unaona anampenda sana Iryn sababu ya hii.”

MIMI: “So mama Janeth alikuwa anamzunguka mama yake Iryn kwa kutembea na mume wake sindio?”

SUMAIYA: “Insider haya mambo mengine sisi hayatuhusu, tujadili jambo lako uliloweka mezani.”

MIMI: “Embu nipe mawazo nini nifanye? Kidogo wewe una mazoea na mama unajua namna ya kumuingia na kutoka, nisaidie kwa hili, lengo langu tuongee tuliweke sawa hili.”

SUMAIYA: “Insider huna haja ya kuhangaika kwa hili, Master ni Iryn ndo anatakiwa aliweke sawa hili, wewe hata usihangaike, mama atakaa sawa tu hata usijipe stress, wewe fanya yako hata usiwaze kuhusu yeye.”

MIMI: “Sometimes ni bora ukajifanya mjinga ili mambo yaende, mimi lengo langu niliweke sawa hili jambo, kwahiyo unanishaurije?”

SUMAIYA: “Wewe tulia hayo ni mambo ya familia waachie wao, the truth is, she can’t hate you forever, wewe ni mkwe tayari atake asitake, mama nae uchi wa Iryn afu yeye anaumia.”

Akaanza kucheka pale,

MIMI: “Nawaza mpaka kuacha kazi ujue, sitoweza kufanya kazi kwa mazingira kama haya.”

SUMAIYA: “Acha ufala wewe, upo kwaajili ya mama au Iryn? Yaani uache kumsaidia mke wako kisa mama? Acha ujinga Insider, Iryn anakutegemea usifanye maamuzi ya kijinga, kwanza mama ataona umemwogopa, wewe fanya yako.”

MIMI: “Sawa bhana kumbe unaweza kumshauri mtu, ukiwa serious unakuwa na akili nzuri.”

SUMAIYA: “Leo unanipa gari yangu, najiona niko vizuri kuingia road.”

MIMI: “Nilitaka nikuwekee android TV ni vile nimekuwa na mambo mengi, kama unaharaka nayo ichukue.”

SUMAIYA: “Kwahiyo unataka kunipa lini?”

MIMI: “Ijumaa na leseni yako itakuwa tayari ili nikupe vyote kwa pamoja.”

SUMAIYA: “Sawa, ila unanipeleka home.”

MIMI: “Sawa haina shida, ila ndani sitaingia naishia nje tu”

SUMAIYA: “Haya baba twende.

Nilimpeleka Sumaiya kwake na muda ambao ninarudi home nilikuwa nawaza kuhusu mama Janeth pamoja na maneno aliyokuwa anaongea Sumaiya, niliwaza huenda anajua siri nyingi sana, hivyo itabidi nianze kumchimba taratibu.

Kwenye hili suala lawama zangu zote zilikuwa kwa Iryn maana alipaswa kumwambia mama hili jambo mapema sana, lakini alikuwa anasuasua mpaka mama amefahamu. Jambo lingine lililokuwa linaniumiza kichwa ni vile Iryn kuninunia afu nashindwa kuwasiliana nae ili tuyaweke mambo sawa.

Kwa upande mwingine allen alinitafuta kuniuliza kama narudi tena tuendelee na topic yetu maana nilikuwa nimemuaga kwa kumpa ahadi ya kurudi tena, nilimwomba kumtafuta kesho ili tumalize maongezi yetu.

Baada ya kurudi home nilikwenda chumbani kuoga na nilimkuta Junior akichezea simu ya mama yake, nikapata wazo la kuipekua simu yake, kimbembe Junior alikuwa hataki kunipa simu, kila nikitaka kuchukua alikuwa analia. Palepale nikapata wazo nimuwekee cartoon kwenye PC ili atoe simu, na nilifanya hivo plan yangu ikawa imetiki.

Nilianza kuipekua simu upande wa whatsapp na nilianza direct kutafuta chats zake na Iryn, lakini hakukuwa na chats zozote walizochat hivi karibuni, na niliendelea kuangalia chats zingine na nilibaini kuna Mafisi wanamtongoza sana, nikapotezea. Niliona chats za dada yake na nilifungua ili nisome chats zao, baada ya kufungua niliweza kugundua kwamba dada yake ndo anayemkomalia wife kuhusu mimi na Iryn kuwa na mahusiano, na mbaya zaidi alikuwa anamwambia afanye investigation ya ukaribu wetu.

Wife kwa upande wake alikuwa amemwambia dada yake kuhusu ujio wa Iryn pale home ile usiku na kuhusu mapenzi yake kwa Junior, dada yake alikuwa anakamia sana mimi na Iryn tuko kwa mahusiano. Alikuwa anamwambia mdogo wake aendelee kuwa karibu na Iryn maana yeye ndo rahisi kumchunguza na kujua ukweli, mbaya zaidi alimwambia itabidi waonane kwa maongezi zaidi.

Baada ya kusoma hizi chats zao hapa sasa nikajua tatizo sio mama J bali ni dada yake ambaye anasmell something fishy kati yangu na Iryn. Nilijisemea nitakuwa makini sana kuanzia kwenye simu yangu hasa kwenye chats zangu na Iryn, niliona niko vitani hivyo natakiwa kuwa makini sana kwa kipindi hiki.

Baada ya dakika 15 nilimsikia wife akija chumbani na alikuwa akimuita Junior;

“Junior nipe simu yangu nimpigie bibi.”

Na ile kuingia chumbani anatuona tuko busy na cartoon, akachukua simu yake akaondoka.

Muda huu nilipata wazo la kumcheki Iryn ili tuongee lakini alikuwa bado kaniwekea tofali. Niliwaza pale labda nimcheki kwa namba nyingine ili tuongee huenda ikasaidia, lakini niliona nitakuwa kama najimbeleza kwake, cha msingi nipotezee, kwa upande mwingine yale maneno ya kaka Allen yalikuwa yananipa jeuri na kiburi.

Kesho yake niliwahi sana kwenda Masaki na kipindi niko ofisini nilibaini Iryn bado hajaingiza mishahara kwa wafanyakazi maana yeye ndo huwa anahusika, sasa tumeanza mwezi mpya february afu hajafanya chochote niliona anazingua.

Nilimtumia mail kumkumbusha hili suala maana ni muhimu na mimi niliendelea kuandaa ripoti zingine, niliendelea kuwaza namna ugumu wa kazi unavyokuwa hasa ukichanganya mapenzi na kazi. Suluhisho na kuepusha matatizo kama haya niliona ni bora nika quit sababu vitu binafsi vina impact mpaka utendaji wa kampuni.

Baada ya nusu saa Hilda aliwasili ofisini huku kavaa skirt fupi sana kiasi kwamba ilikuwa ikimchora barabara. Mimi baada ya kumuona vile nilijifanya niko busy na kazi zangu na sikutaka kuongea chochote, ila yeye ndo alinza kunisalimia na akakaa kwenye sofa;

HILDA: “Insider tangu jana nafikiria kuhusu mama mkwe wako.”

Niliona Hilda ameanza kuvuka mipaka, niliona ameanza kufuatilia mambo yasiyo mhusu,

MIMI: “Ulikuwa unafikiria nini?”

HILDA: “Au hajapenda kumuona Iryn vile, afu na wewe ndo mhusika?”

MIMI: “I don’t know, ikifika muda kila kitu kitakuwa wazi.”

HILDA: “Jana nimekutumia ripoti ya mwezi, stock imeisha sidhani kama itaweza kusurvive muda mrefu.”

MIMI: “Stock haina shida kuna mzigo soon utakuwa bandarini, mimi natoka mara moja soon narudi.”

HILDA: “Sawa uwahi kurudi ili twende lunch.”

MIMI: “Leo nipo na wewe mpaka jioni sema ulivyovaa hivo utanifanya niingie matatizoni.”

Hilda aliishia kutabasam na niliondoka kwenda kuonana na Allen ofisini kwake ili tumalizie maongezi yetu.

Nilitumia muda mfupi sana kuwasili pale kwenye kampuni yao na nilikwenda moja kwa moja ofisini kwake nikaambiwa yuko kwenye kikao. Nilimtumia ujumbe kumpa taarifa na akanambia tuoanane mchana muda wa lunch kuanzia saa 7 mchan ili tuongee vizuri, na mimi kuondoka kurudi ofisini.

Kabla ya kurudi ofisini nilipitia shoppers kununua mazaga ya kupeleka ofisini kwaajili ya sisi na wateja kama maji ya kunywa, juice, soda na bites. Kipindi nanunua vitu simu yangu ilianza kuita na alikuwa ni Mary akinipigia na nilipokea kwa haraka sana;

MIMI: “Hi Mary.”

MARY: “Hi Insider za wewe?”

MIMI: “Salama mummy, nimefurahi kusikia sauti yako hata sikutegemea.”

MARY: “Ahsante sana dear, nilikuwa nakusalimia tu.”

MIMI: “Thank you, unasomeka pande zipi?”

MARY: “Niko Posta ofisini kwa mama but I won’t be here for too long.”

MIMI: “Karibu Masaki upajue ofisini kwangu.”

MARY: “Thank you leo nitakuja, navyotoka huku nitakujulisha.”

MIMI: “Karibu sana Mary.”

Saa sita na nusu Allen alinipigia simu ili tuoane kwaajili ya mazungumzo na tulikubaliana tukutane pale Salt restaurant. Sikutaka kupoteza muda na niliondoka kwenda eneo la tukio na yeye alikuwa ameshafika tayari na tulisalimiana tukaanza story;

ALLEN: “Bro sorry sana nilikuwa nina kikao afu sikutegemea kama ungekuja asubuhi.”

MIMI: “Usijali mimi ndo nilizingua nilipaswa kukupa taarifa mapema.”

ALLEN: “Mama kijacho anaendeleaje?”

MIMI: “Hakuna lolote kutoka kwake anajiandaa na mitihani kwasasa. Tuendelee na topic yetu ya jana maana tulizungumza vingi lakini hatukamaliza.”

ALLEN: “Ni sawa kabisa ila leo tutakuwa na solution ya hili jambo, usiwe na wasiwasi.”

MIMI: “Toka jana tuongee kidogo naona mabadiliko, ila kaka kuna jambo inatakiwa ujue, hata kama tukisubiri Iryn ajifungue ndo twende, bado mimi siwezi kumuoa unafikiri wazazi watakubali?”

ALLEN: “Una uhakika hutakuja kumuoa Iryn?”

MIMI: “Ndio siwezi kumuoa, yeye ni kama mchepuko kwangu na anajua hili.”

ALLEN: “Our future is an uncertainty, you never know, kinachomtofautisha Iryn na mama J ni kutambulika kwa wazazi na vile umemlipia mahali, lakini vingine vyote wako sawa na huyu soon atakuwa na mtoto wako.”

MIMI: “Upo sahihi lakini sasa…”

Alinikatisha maongezi yangu,

ALLEN: “Bado sijamaliza ipo hivi, mimi naona ni busara Iryn akaongea ukweli huko kwao kuhusu wewe kuwa una mke na mtoto, na ameridhia kuwa mke mdogo kwa hiyari yake.”

MIMI: “Kaka huoni kama nitaweza kukosa mtoto kizembe wakijua ukweli?”

ALLEN: “Toka jana nakwambia kuhusu hili, mwenye maamuzi na hii mimba ni dada mwenyewe na sio wazazi au sisi, yeye akisema ninazaa na kweli atazaa huna haja ya kuwa na wasiwasi.”

MIMI: “Sidhani kama atakuwa tayari kuwaambia wazazi hivyo, hawezi kubali anaweza kutengwa na ukoo.”

ALLEN: “Sasa ni bora kuwa wakweli kuhusu hili au tudanganye? Na kama tukiwaambia tutamuoa kumbuka tutakuwa tumeshaingia kwenye makubaliaono ya wazazi na tusipofanya hivyo tutakuwa matatizoni, kama unaona ni sawa kuwadanganya niko tayari kukupa kampani mpaka Ethiopia.”

MIMI: “Hapana naona option ya pili imekaa kimkakati sana ila kuna possibility ya kumkosa mtoto au hata akizaliwa akapewa ukoo wa kwao.”

ALLEN: “Haiwezekani huyo mtoto ni wako na sifikirii kama mama yake atakuwa tayari kukuweka mbali na mwanao, never. Hili suala wa kulimaliza ni Iryn mwenyewe wala sio sisi ni mwenyewe akae na familia yake awaambie ukweli kuhusu wewe na maridhio yake.”

MIMI: “Kaka usije ukanijaza kichwa afu mambo yakaenda viceversa maana sitaki kumpoteza huyu mtoto.”

ALLEN: “Na ukionesha weakness ya uhitaji sana wa mtoto ndo utampoteza sasa, just kuwa normal usioneshe wenge lolote.”

MIMI: “Duuh sawa bro nashukuru kwa mawazo yako.”

Wakati tunaendelea na mazungumzo Mary alipiga simu kunipa taarifa anatoka Posta hivyo nimuelekeze ofisi ilipo ili aje na mimi nilimwambia aje Salt atanikuta hapa, alisema haijui ilipo nimtumie location, nikamwambia akifika Cocobeach anipigie nimuelekeze.

Ndani ya dakika 30 alinipigia kunipa taarifa anakaribia na nikamueleekeza mpaka anafika na kwa mbali nilimuona akishuka kwa Vanguard, alikuwa amependeza sana na alizidi kuonekana ni mrembo sana.

Aliingia ndani akaja usawa wetu na tulianza kusalimiana pale na nilimtambulisha kwa Allen na story zingine zikaendelea;

MIMI: “Nambie mummy, mama mkwe hajambo?”

MARY: “Afu anakuulizia sana na mbaya zaidi Prisca anakosaga majibu ya kutoa.”

MIMI: “Hahahaa, msalimie sana, kumbe unajua kudrive ndinga nilikuwa sijui.”

MARY: “Yeah kimtindo kama hivi.”

MIMI: “Agiza food ule ili tuondoke najua hujala.”

Allen aliniaga anawahi ofisini na niliendelea kubaki pale na Mary nikimsubiri amalize kula, na baada ya kumaliza tuliondoka kwenda ofisini.

Baada ya kufika ofisini nilimpeleka moja kwa moja mpaka show room ili aangalie mawigi, kwa upande wake alionekana kuyapenda na alikuwa akishangaa bei zake,

MARY: “Insider wigs ni nzuri ila kwa hizi bei hapana mimi siwezi.”

MIMI: “Wig la gharama kuvaa ni bei gani?”

MARY: “Nakumbuka laki 5 na mama ndo alinunuliaga, hii Lace nimeipenda kwakweli niambie sifa zake.”

MIMI: “Huku sasa mimi ndo sijui ngoja nikuitie mtaalamu wa hizi kitu akuelekeze.”

Nilimuita Winny ili amuelekeze Mary kwa sifa za wigi ambazo atahitaji maelekezo;

WINNY: “Mrembo hio ni frontal lace natural hair black kutoka France, hio ni mkataba utavaa mpaka uichoke, haipukutishi na ni laini kama unavyoiona. Ukinunua hio wigi utapewa wig cap, brush, shampoo, sprays, gels na wig stand, bado una offa ya kuja hapa kusetiwa free mara 3.”

MARY: “Wow amazing, Insider hii wigi nimeipenda kwakweli ila sasa milion 2 ninatolea wapi?”

MIMI: “Kama umeipenda, nakupa offa ichukue kama zawadi yangu kwako, umenifanyia mambo mengi sana hio ni shukrani yangu.”

MARY: “Thank you Insider.”

Winny alishangaa sana kuona nampa Mary ofa ya wigi na nilimwambia yeye ndo atakaye mhudumia Mary. Mary alisema atakuja jumamosi kwaajili ya kuweka wigi na tuliondoka tukaenda ofisini kuendelea na mazungumzo.

MARY: “Insider Salon yenu ni international sijaona Salon hapa Dar ya kushindana na nyie.”

MIMI: “Ofcourse hata wateja wetu alimia 95 ni foreigners, naona unazidi kuwa mrembo nipe siri ya mafanikio.”

MARY: “Nakula vizuri, nalala kwa wakati, sina stress kwanini nisiwe mzuri?”

MIMI: “Hahahaaa hata mimi naona sio kwa kung’aa huko mpaka unafanya mapigo ya moyo wangu yaongezeke spidi.”

MARY: “Mhhh! Prisca mnawasiliana?”

MIMI: “Yeah tuko intouched ila sio sana, nafurahi kuona amemove on.”

MARY: “How did you know?”

MIMI: “I know na ni jambo zuri, tuachane na haya yalishapita, vipi kuhusu wewe usinambie bado upo single sitokuelewa.”

MARY: “Bado niko sokoni, soko gumu sana huku nje..”

Tulianza kucheka wote pale na aliendelea kuongea;

“Insider kuna kitu nataka kushare na wewe, nimepata kazi Posta, kuna kampuni nitakuwa nafanya nayo kazi but nataka nitafute apartment karibu.”

MIMI: “Unataka kuondoka home? Kwamba utashindwa kuamka mapema uwahi kazini?.”

MARY: “Si unajua nasoma pia, bado research na muda mwingi nitakuwa nashinda library, pia nimekuwa mtu mzima nahitaji kukua.”

MIMI: “Mimi sikushauri uhame home, unataka majukumu ya nini mapema hivi? Hizo pesa za kodi si bora uziweke zije zikusaidie hapo baadae?”

MARY: “Bhana, wewe na mama lenu moja naye hataki kabisa kusikia hizi habari, but weekend nakuwa narudi home.”

MIMI: “Mmh, wewe fanya kutokana na moyo wako unavyotaka na angalia mipango yako, ukiona kuna haja ya kupanga ni sawa.”

Hilda aliingia ofisini alikuwa lunch na baada ya kumuona Mary walisalimiana, kisha akaanza kunilamikia nimemdanganya kuhusu kwenda kula lunch na mimi nikajitetea nilikuwa na mgeni ndomana nikashindwa.

Mary aliniaga anaondoka kwa ahadi ya kurudi jumamosi kwaajili ya kuweka wigi, na mimi sikuchukua muda nikamuaga Hilda naondoka kwenda Mikocheni kuonana na Lucy. Lengo la kwenda kuonana na Lucy ni sakata la Landlord na niliona ni busara tukaonana face to face kuliko kuongea kwa simu.

Baada ya kuwasili Mikocheni ofisini nilionana na Lucy tukaanza mazungumzo na kubwa alisema ameongea na Iryn ila yuko kwenye maandalizi ya mitihani hivyo mpaka weekend ndo watapanga vizuri.

MIMI: “Unajua Iryn kaniblock.”

LUCY: “Uliniambia, si hutaki nikumbelezee unaleta ubeberu shauri zako.”

MIMI: “Shida ukiongea nae atajua mimi nimekwambia kinachoendelea afu yeye mpaka sasa hajakwambia, atleast akufungukie hapo kidogo itakuwa na nguvu.”

LUCY: “Sema mke wako kabadilika sahivi, sijui ndo mimba inamchanganya yaani simuelewi kabisa.”

MIMI: “Afadhali hata wewe umeliona hili maana unaonaga mimi ndo mwenye shida.”

Baada ya maongezi ya muda mfupi nilimuaga Lucy nikaondoka kurudi home mapema kabisa.

Kipindi niko home nilikuwa nikitafakari ushauri wa Allen na niliona yuko sahihi ni bora Iryn akasema ukweli huko kwao kuhusu mimi before it’s too late au wazazi wakajua kupitia mama Janeth.

Usiku Jane alinipigia simu kunipa taarifa kuwa ameanza biashara na nilimuahidi kwenda dukani siku ya kesho na nitashinda siku nzima. Jane alionesha kuwa na furaha sana baada ya kuanza biashara hata mimi kwa upande wangu nilijisikia vizuri sana kuona Jane akiwa na furaha ukizingatia marehemu Pama alinipa task ya kuhakikisha Jane anakuwa salama na mtoto.

Kesho yake nilikwenda dukani kwa Jane kama nilivyokuwa nimemuahidi ili kuona maendeleo kwa ujumla, duka lilikuwa limejaa sana na lilionekana kupendeza sana, wateja nao hawakuwa mbali walikuwa wanakuja kwa wingi.

Nilishinda siku 2 mfululizo dukani na nilikuwa nikisaidiana kazi na dada ambaye alimtoa home na kumleta dukani sababu alikuwa anamuamini, Jane alikuwa anakuja pale shop na kuondoka maana asingeweza kumwacha mtoto home.
******

Jumamosi nikiwa ofisini nilipata wazo nimpigie simu mama niombe kuonana nae ili tuzungumze, nilipiga simu mara 2 bila majibu na niliamua kumtumia ujumbe ambao niliandika kuomba kuonana nae kwaajili ya mazungumzo, lakini sikujibiwa ni kama vile hakuiona message yangu.

Nilikumbuka maneno ya Sumaiya nikaona alikuwa sahihi kusema haya mambo ni ya familia, hivyo niwaachie wao wenyewe wayamalize na nikiendelea kujibembeleza nitapoteza thamani yangu. Kwa upande mwingine kuendelea kufanya kazi kwenye mazingira haya niliona nitazidi kuwa kwenye wakati mgumu, ukizingatia sipo kwenye maelewano mazuri na hawa wahusika wakuu, Iryn na mama yake.

Muda huu Mary alinipigia simu kunipa taarifa kuwa yuko njiani anakuja kuweka wigi lake na kufikia saa 7 mchana atakuwa around. Nilimpanga Winny mapema kuhusu ujio wa Mary, nilitaka yeye ndo amuhudumie na sio mtu mwingine.

Saa 7 mchana Mary aliingia na Vanguard pale ofisini na mimi nilitoka kumpokea na tuliishia kukumbatiana, sasa Mary alikuwa katembea na mdogo wake Ivy, ilikuwa ni surprise kwakweli na sikutegemea kabisa.

MIMI: “Karibu sana naona leo umeamua kunisirprise, Ivy hujambo?”

MARY: “Ahsante, ameforce tuje wote ndomana na sijamwambia nakuja kwako.”

IVY: “Sijambo shem tumekumiss, why can't you come home?”

MIMI: “I will come Ivy, today I am happy to see you again."

IVY: “Me too.”

MARY: “Insider utanisaidia kumpeleka Ivy lunch hajala mchana.”

IVY: “I’m not hungry.”

MIMI: “Ivy tutakwenda wote kula sawa?. Mary wewe kaendelee huko ndani dada anakusubiri zoezi lianze.”

Mary alikwenda ndani, tulikaa nje kibarazani tukipiga story na Ivy maana ni muongeaji, huwezi jutia kuwa naye karibu;

MIMI: “Nani alikwambia mimi ni shem kwako?”

IVY: “Dada Prisca told me.”

MIMI: “Niite Uncle Insider sawa eeh?”

IVY: “Sawa uncle.”

MIMI: “Let’s go tukale lunch, unataka kula nini?”

IVY: “Pizza”

Tuliondoka kwenda kula Pizza, muda ambao tuko njiani mama alinipigia simu, habari kubwa alisema anaona kuna jambo linanisumbua akili lakini siko tayari kushare na mtu, aliendelea kunisisitiza kama nipo tayari bhasi nimwambie ili aangalie namna ya kunisaidia hata kimawazo au ushauri.

Kwa upande wangu sikuwa tayari kumwambia mama kuhusu hili jambo na niliendelea kumkatalia kuwa sio kweli na mimi niko sawa, licha ya kutokubaliana na mawazo yangu

Hili jambo siwezi kushare na wazazi kwa kipindi hiki mpaka pale mambo yatakapokuwa sawa ndo nitashare ila kwasasa mtu wa kushare nae ni sister tu.”

Baada ya kuwasili Pizzahut niliagiza pizza medium na nilikwenda kula pizza kwaajili ya kumpa kampani Ivy, haya madude mimi huwa siyapendelei kabisa. Nilipiga slice 2 nikamuachia Ivy aendelee kula, nikatoa simu kumpigia sister ili nimpe taarifa za kwenda Arusha anipe na ratiba zake mapema kabla ya kwenda.

Tulipiga story nyingi sana na sister na tulikubaliana niende Arusha mwezi wa pili mwishoni maana atakuwa likizo, hivyo atakuwa na muda mzuri wa kukaa na mimi mdogo wake.

Kwa upande mwingine Ivy alikuwa amemaliza kula na alimwambia dada afunge slice 2 zilizobaki na alisema kwaajili ya dada yake Mary na tukaondoka kurudi ofisini.

Kufikia saa 10 jioni Mary alikuwa tayari kamaliza kutengenezwa na alipendeza sana mpaka nikajikuta naanza kupagawa, alikuwa kawaka sana kwa jinsi alivyo mzuri by nature na wigi alilokuwa kawekewa plus madikodiko mengine alikuwa bonge la pisi hata yeye aliishia kufurahi tu.

MIMI: ”Umependeza sana yaani umebadilika umekuwa pisi ya kimataifa.”

MARY: “Thank you Insider, ukweli hata mimi najishangaa sipati picha huko home leo na shoga zangu wakiona lazima waulize nilikokwenda.”

MIMI: ”Wewe wakaribishe sana waje hapa.”

MARY: “Insider naenda home kumpeleka Ivy but naomba badae tutoke kama unanafasi please.”

Nilijifikiria kwa sekunde kadhaa nikaona sina ratiba yoyote, acha nikubali ili niendelee kumfurahisha Mary;

MIMI: ”Sawa haina shida, mimi nitabaki nikikusubiri hapa ofisini so utanambia ukiwa tayari.”

MARY: “See you soon, Ivy twende, mwambie Ahsante shem Insider.”

IVY: ”No, he wants me to call him Uncle Insider.”

Mary aliniangalia afu akatabasamu kwa kutingisha kichwa na nilimsindikiza mpaka parking na kabla ya kuingia kwa gari alikuja akanikumbatia na wakaondoka, kugeuka nyuma namuona Winny yuko kibarazani anatabasamu, nilisogea mpaka usawa wake tukaanza story;

MIMI: “Leo umetisha sana itabidi nikupe zawadi.”

WINNY: “Namuona kafurahi mwenyewe hata haamini kama ni yeye, ni nani uyo?”

MIMI: “Huyo alikuwa shem wangu, nilitokaga na mdogo wake but tuna mawasiliano mazuri.”

WINNY: “Insider unapendwa sana na watu, just imagine umeachana na mdogo wake lakini bado mnacheka vizuri, ni wanaume wachache wenye bahati kama yako.”

MIMI: “Winny umeanza kunichokoza.”

Na nilianza kuslap makalio yake akakimbia ndani na mimi nikaenda ofisini na niliamua kumpa Hilda utawala akapumzike na nilimwambia aniachie ofisi na yeye aliishia kufurahi akaondoka.

Nilikaa ofisini mpaka saa 2 za usiku ndo Mary kunipigia simu kunipa taarifa anatoka home anakuja Masaki, nilikuwa nishasahau kama nina miadi ya kukutana na Mary.

Baada ya lisaa aliwasili na tulikutana ofisini nje ya geti alikuwa na Uber, nilimpick tukakubaliana twende Wavuvi Kempu. Baada ya kuwasili eneo la tukio na kushuka hapa sasa ndo namuona Mary vizuri, aisee alikuwa kapendeza sana maana alivaa skin jeans ya light blue ambayo imemkaa vizuri na kiuno kilichoreka na juu alikuwa kavaa top nyeusi iliyoishia chini ya kitovu na glass nyeusi.

Mary kabarikiwa shepu nzuri sana, sasa jinsi alivyokuwa kawaka niliishia kumsifia pale na nilimshika mkono tukazama ndani, tukatafuta sehemu nzuri tukakaa na mhudumu alikuwa tayari kafika kutusikiliza, tukaagiza Hennesy na mixers.

Ndani ya muda mfupi dada alikuwa katuletea kinywaji tukaanza kunywa huku tunapiga story, ofcourse tulikuwa tumemisiana sana maana ni kitambo tulikuwa hatujakaa pamoja.

Story zetu kubwa zilibase kwenye mahusiano na maisha kwa ujumla, Mary kwa upande wake alitaka kujua kama bado nina pasha kiporo na mdogo wake, nilimkatalia katakata.

Tulikuwa deep sana kimaongezi na kadri muda unavyozidi kwenda na pombe kukolea tulianza kuoneshana hisia za kimapenzi waziwazi, kuna muda tulikuwa tunacheza pamoja na kukumbatiana.

Mida ya saa 6 usiku wife alinipigia simu, baada ya kuona ni wife niliwaza haraka nikaona wacha nikapokee simu yake kwenye gari, nisipo-pokea italeta shida, nilimuaga Mary nakwenda washroom lengo nikaongee na wife.

Simu ilikuwa imekata tayari na aliendelea kupiga kwa mara ya pili na baada ya kuingia kwa gari nikapokea na tukaanza mazungumzo;

“Nambie mke wangu hujalala tu?”

“Napataje usingizi na wewe mpaka sasa hujarudi, umepitia wapi?”

Nilipiga hesabu za haraka nikaona acha niwe mkweli,

“Mke wangu siko sawa kabisa nimeona nipitie kunywa ili nikae sawa.”

“Hivi unaakili wewe? Sasa pombe ndo zinakuweka sawa?”

“Nikirudi home makelele si bora ninywe tu.”

“Baba J umekaa chini na mimi kunambia matatizo yako? Nini maana ya kuishi pamoja kama hunambii shida zako? Sijapenda naomba urudi home mapema tuongee, kama huwezi nambie ulipo nikufuate.”

“Haina haja mimi niko sawa na nitarudi home, usiwe na wasiwasi.”

“Haya, sisi tunalala byee, Takecare.”

Baada ya kurudi ndani Mary alianza kulalamika nimemuacha alone, ilibidi nimbembeleze ili atulie na nilimwambia ukweli kwamba nilikuwa naongea na wife.

Mary alikuwa close sana na mimi ‘zero distance’ na tuliendelea kucheza pamoja huku nazungusha mikono kwenye makario yake na yeye alizungusha mikono kwenye kiuno changu. Network yangu ilikuwa ishahama muda mrefu sana na yeye alikuwa kalainika sana, tulikuwa kwenye huba zito sana kiasi kwamba tulianza kupeana makiss bila aibu, licha ya nyomi ya watu iliyokuwepo maeneo haya.

Nilicheki muda simu yangu ilikuwa inaonesha ni saa 7 usiku na madakika, nikamwambia Mary tuondoke akasema sawa. Ile kufika kwenye gari tulianza kuexchange saliva tena kwa fujo kwelikweli na sikuchukua muda nikapandisha mkono kwenye vifuu vyake. Hapa sasa alianza kutoa kelele za nguvu na ile kushusha mkono kwenye bustani yake ilikuwa tapatapa yaani imemwagiliwa vya kutosha na muda huu alikuwa hoi akinitizama tu kwa macho ya kurembua.

Nilimwacha afu nikaanza kujifikiria niondoke naye au nirudi home? Maana kufikia stage hii Mary asingeweza kuwa na jeuri ya kunikazia, kuondoka nae ilikuwa ni lazima 100%.

Wakati naendelea kutafakari, alianza kuongea pale,

“Insider where are you taking me?”

“I don’t know.”


EPISODE 22
COMING SOON:
😀 😀 😀 😀 tapa tapa
 
Back
Top Bottom