Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

SEASON 02
CHAPTER 36

“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”

IN LOVING MEMORY OF MR. PAMA (2022).

PREVIOUS:


Baada ya nusu saa mama Janeth ananipigia simu, kwanza kabisa nilishangaa kuiona simu yake, hivyo nilimuaga mzee naenda washroom mara moja. Nilipokea simu ya mama na habari kubwa alisema tuonane usiku huu kwani kesho ana safari, pia ana maongezi muhimu sana nami.

CONTINUE:

Nilipovuta kumbukumbu, nilikumbuka jinsi alivyonifanyia nyodo siku za nyuma. Je, sasa anataka niende kwa sababu Iryn kaenda? Alikuwa wapi muda wote huu? Nilijaribu kufikiria kwa haraka, lakini nikaona hakuna haja ya kukubaliana. Acha nivimbe, kwanza siwezi kumuacha mzee Juma, hasa wakati bado tuko kwenye maongezi muhimu.

Niliamua kumjibu kwa utulivu na kumwambia kuwa niko mbali sana, na nitarudi usiku wa manane, hivyo tuonane akirudi kutoka safari yake. Baada ya kumalizana na mama, nilirudi kwa mzee Juma kuendelea na mazungumzo yetu, nikiwa na utulivu na mtazamo mpya.

Niliendelea kuzungumza na mzee, na habari kubwa aliyonieleza ni kwamba itabidi tuondoke Ijumaa kwenda Tabora kwa ajili ya ukumbusho wa kifo cha marehemu Pama. Nilijikuta nawaza kwa haraka, nikiweka kila kitu kwenye mizani, na nikaona sina sababu ya kuukataa wito huu. Kwa kweli, marehemu Pama alikuwa ni mzee muhimu sana kwangu, na heshima yangu kwake haiwezi kupuuzwa.

MZEE: “Tutaondoka pamoja na Cami naye lazima aende.”

MIMI: “Sawa mzee haina shida, kesho nitaanza kujiandaa kwaajili ya safari.”

MZEE: “Tutaondoka kwa ndege, hivyo tutawahi kufika, na zoezi lenyewe litafanyika Jumamosi.” Aliongeza mzee Juma, akisisitiza umuhimu wa safari hiyo.

MIMI: “Sawa mzee wangu.”

Tuliendelea na maongezi na mzee hadi saa nne za usiku ndipo tukamaliza na kuondoka. Wakati huo, simu yangu ilikuwa ikiita mara kwa mara, ni Iryn alikuwa akinipigia sana. Pia alikuwa amenitumia ujumbe akiniomba nimnunulie maziwa ya mtindi.

Nilipokuwa kwenye Uber nikirudi, njiani niliamua kumpigia Jane na kumtaarifu kwamba nami nitakwenda Tabora. Jane alifurahi sana kusikia taarifa hizi na akaniambia kwamba yeye ataondoka kesho pamoja na Mary.

Nilibaki nashangaa kwa muda,

MIMI: “Kwani uliongea na Mary kuhusu kwenda Tabora?"

JANE: “Ndiyo, tuliongea kwa simu tangu jana, maana sina kampani."

MIMI: “Sawa, vizuri. Mimi hajanambia kabisa kuhusu hili."

JANE: “Hata mimi nimeshangaa kusikia kwamba unaenda Tabora. Nilijua una ratiba nyingi."

MIMI: “Ni kweli ratiba zangu hazieleweki, lakini sina jinsi, lazima niende."

JANE: “Sawa, sisi mtatukuta Tabora."

Baada ya mazungumzo na Jane kumalizika, nilianza kufikiria namna ya kumweleza mama kijacho wangu, Iryn, kuhusu safari hii. Mawazo yangu yalinipeleka mbali, kwanza kwa hali aliyokuwa nayo, kumuacha peke yake nyumbani ilikuwa hatari. Pili, niliwaza haitakuwa rahisi kukubaliwa kuondoka, hasa kwa kipindi hiki kigumu kwake.

Suala la kwenda Tabora tulikuwa tumezungumza na Jane kipindi tulipoenda na Mary pale kwake. Hata hivyo, kwa upande wangu niliona ni ngumu sana kuamua kwenda kwa sababu ya hali ya Iryn. Niliamua kwamba nitakwenda siku nyingine kwa nafasi yangu, pindi nitakapokuwa na uhuru zaidi.

Baada ya kufika kwenye apartment, nilimkuta Iryn amelala sebuleni, akiwa uchi kama kawaida yake. Nilimsalimia kwa upole, kisha nikapita moja kwa moja hadi chumbani kwenda kuoga. Nilihisi ni bora nifanye hivyo haraka, maana nilikuwa nimekunywa, na sikutaka ajue chochote kuhusu hilo.

Nilioga haraka huku nikijisafisha vizuri, ikiwemo kinywa changu ili kusiwe na dalili zozote za harufu ya pombe. Baada ya kumaliza, nilirudi sebuleni na nikakaa pembeni yake. Macho yake yalikuwa yamenikazia, akinitazama kwa makini, kana kwamba alikuwa akisubiri niseme kitu au kufanya jambo.

IRYN: “Ulikuwa wapi?” Aliuliza.

MIMI: “Mishemishe, halafu kuna jambo nataka nikwambie.”

IRYN: “Jambo gani?”

MIMI: “Ijumaa nitaondoka kwenda Tabora kwa ajili ya ukumbusho wa kifo cha mzee wangu. Kwa hivyo, itabidi uende kwa mama Janeth hadi nitakaporudi. Sawa, mummy?"

IRYN: “Darling, kwa nini? Unajua jinsi gani ninavyokuhitaji kipindi hiki. Kwa nini usiende nikiondoka?"

MIMI: "Baby, yule alikuwa kama mzee kwangu. Jumamosi ndiyo siku ya tukio, na nitaenda pamoja na mzee Juma, ingekuwa ni dhihaka kumkatalia. Pia, ingeonekana kama sina heshima kwa marehemu. Nakuhakikishia nitarudi haraka iwezekanavyo."

IRYN: “Kwanini unanipa taarifa kwa kunishtukiza?”

MIMI: “Sikuwa na mpango wa kwenda huko, lakini sasa sina jinsi, lazima niende. Nitarudi Jumapili mapema sana, mpenzi wangu. Tafadhali, nakuomba uende kwa mama Janeth ili kama kuna jambo lolote, iwe rahisi kusaidiwa."

IRYN: “Mama hajakwambia ana safari?”

MIMI: “Ameniambia, lakini kuna dada wa kazi wawili kwa mama, na bado huwa hapakosi wageni.”

IRYN: “Claire amerudi kutoka safari, nitaongea naye aje tukae pamoja.”

MIMI: “Umekula?”

Alitikisa kichwa kukubali ‘ndio nimekula’ na nilienda chumbani, nikaanza kupitia taarifa za dukani Dodoma na kuwapa maelekezo vijana wangu.

Asubuhi, Mary alinipigia simu na kunitaarifu kwamba ataenda Tabora pamoja na Jane, na atanijulisha atakaporudi. Alisema hatuwezi kuonana weekend kama tulivyokubaliana. Kwa upande wangu, sikutaka kumwambia kuhusu mpango wangu wa kwenda pia, nilitaka kumsurprise kwa hilo.

Niliendelea na usafi pamoja na kumuandalia chakula mama kijacho wangu. Iryn alikuja jikoni na kunijulisha kwamba Claire yuko njiani. Baada ya dakika tano, Claire alifika, na Iryn alitoka kumpokea. Claire alinikuta nimekaa sebuleni wakati waliporejea.

CLAIRE: “Waow! I didn’t think Insider would be here."

MIMI: “Umeanza unafiki, sema kilichokuleta hapa ni nini.?”

IRYN: “Mhh na wewe ushaanza mambo yako.”

CLAIRE: “Nambie shemu wangu za siku? Mara ya mwisho kuonana unamtafuta Iryn.”

MIMI: “Miezi imekata ni muda mrefu, juzi tu hapa niliambiwa uko safari na umerudi lini?”

CLAIRE: “Nimerudi jana, mnaweza kunipa majibu kwanini wote mlikuwa hampatikani kwenye simu?”

MIMI: “Claire achana na hizi story utanipa hasira bure, ukitaka majibu muulize best yako.”

CLAIRE: “Hongera lakini, unaenda kuwa baba.”

MIMI: “Malizia baba wa watoto wawili.”

Na waliishia kucheka na Iryn maana hawakutegemea jibu langu,

“Nikuletee kinywaji gani?”

CLAIRE: “Maji yanatosha shem wangu.”

Nilimletea maji na nikawaacha waendelee na maongezi yao, nikaenda chumbani.

Wakati nikiwa chumbani, nilijipanga kwenda Mikocheni kuonana na Lucy ili tumalize tofauti zetu, kwani alikuwa kachukia sana. Niliona ni busara kumuomba msamaha, kwani nilijua kwamba nilikuwa nimemkosea sana kama mtu wangu wa karibu.

Niliingia bafuni kuoga na baada ya kutoka nilianza kujiandaa kwa haraka sana. Simu ilianza kuita na kucheki alikuwa ni Allen akinipigia na baada ya maongezi, alisema niende ofisini kwake, kwa mazungumzo muhimu ambayo tulihitaji kuyashauriana.

Allen alikuwa ananisaidia kuandaa taarifa za fedha kwa ajili ya kutuma TRA (Financial Statement). Alikuwa na mambo ya kodi aliyotaka tushauriane kabla hajamaliza kazi yake, ili kuhakikisha kwamba kama kuna marekebisho yanayohitajika, yafanyike mapema.

Nilitoka seblen na nikawaaga natoka mara moja na sitachelewa kurudi;

IRYN: “Darling, pitia nyumbani kwa mama uchukue gari, huoni tunavyoteseka?.”

MIMI: “Mama anataarifa?”

IRYN: “Ile gari ni yangu alinipa mwenyewe, na jana alinikumbusha niichukue.”

MIMI: “Sawa nimekuelewa, point yangu ni kwamba, funguo zipo? Maana amesafiri leo asubuhi.”

IRYN: “Funguo za gari huwa zinakaa kwenye droo yake, wewe nenda kachukue. Jessie anajua funguo zinako kaa.”

MIMI: “Sawa mpigie simu.”

IRYN: “Darling, nani ambaye hakujui pale kwa mama?.”

Nilijiona mjinga na nikamuaga kwa kumkiss shavuni. Break ya kwanza ilinipeleka nyumbani kwa mama, ambapo nilipata fursa ya kuzungumza na Jessie kuhusu dhamira yangu. Bila kusita, Jessie alikubali na alileta funguo za gari kwangu.

Jessie ni mfanyakazi wa nyumbani kwa mama na ni mzungu kutoka Ulaya. Ameajiriwa kwa kazi kubwa ya kuwahudumia watoto wake. Huenda ukashangaa kuona wazungu wakifanya kazi za nyumbani, lakini ni kweli na wana elimu ya hali ya juu katika sekta hiyo. Jessie amesomea Housekeeping na analipwa mshahara mkubwa kwa juhudi zake za kipekee katika kuangalia watoto wa mama.

Baada ya kuchukua gari, niliondoka kutoka kwa mama kuelekea kwa Allen. Niliona ni bora kumalizana na Allen kwanza kwa sababu kulikuwa na suala muhimu, na baada ya kumaliza hilo, ndipo ningeweza kuelekea kwa Lucy.

Nilitumia muda mfupi kufika ofisini kwake, ambapo tuliweza kuonana na kujadili suala aliloniitia. Baada ya kufikia makubaliano, tuliendelea na mazungumzo mengine, ambapo Allen alieleza kuwa angependa kumjua Iryn.

Hakuwa na lengo hilo pekee, pia alianza kuzungumzia kuhusu Hilda na mipango yake ya kumtafuta, huku akiniuliza mbinu za kumsaidia, kufanikisha jambo hili.

MIMI: “Kaka unamtaka Hilda kwa lengo la mahusiano au kupita tu.?”

ALLEN: “Niwe namla tu mambo ya mahusiano hapana.”

MIMI: “Hilda huwezi kumpata kihivyo amini kwamba.”

ALLEN: “Chief nampango wa kuweka mzigo, sidhani kama atachomoa hapa.”

MIMI: “Hilda sio b*tch, hana tamaa kabisa, usijaribu kufanya hivyo.”

ALLEN: “Kaka Hilda akiwa kwako hawezi kuonesha rangi zake, kwanza wewe ni bossy wake lazima ajue ku-behave.”

MIMI: “Nimemsoma vizuri sana tangu anavyoajiriwa na kuwa karibu naye. Kama Hilda angekuwa mtu mwenye tamaa, ningemsoma mapema sana. Ananunua vitu vya kuweka nyumbani kwake kwa mshahara wake, mpaka pesa zingine nilikuwa namkopa.”

ALLEN: “Duuh! Kwahiyo unashauri nisiweke mzigo.”

MIMI: “Ungekuwa huna mke ningekuweka pale, ila sitaki lawama pambana mwenyewe hapo. Umedata kwa Hilda tayari, pole sana.”

ALLEN: “Kaka acha tu, nimeoa lakini bado nahangaika.”

Wakati nilipokuwa nikizungumza na Allen, Iryn alinitumia ujumbe akiniambia kuwa ananisubiri nimpeleke Cocobeach. Alisema anahamu sana na mihogo, na pia anajisikia njaa kubwa.

Niliona ni vyema kumuaga Allen kwani hatukuwa na mazungumzo ya muhimu, na nikaona bora nimpeleke mama kijacho akale. Nilirudi haraka, nikawakuta wakiwa sebleni, kisha nikawaambia tuondoke.

Tulienda moja kwa moja hadi Coco Beach kwa jamaa wa sikuzote, na baada ya kutuona alifurahi sana kwani hakutegemea ujio wetu pale. Tuliagiza mihogo na mishikaki, na jamaa aliniomba pembeni ili tuzungumze mara moja, lakini Iryn alimzuia.

IRYN: “Kaka huwezi kuongea hapahapa mpaka pembeni?”

MIMI: “Mhh! Baby, sio kila jambo ni busara kuongea mbele yenu. Unataka kujua ni jambo gani anataka kunambia hata kama haliwahusu?.”

Niliongozana na jamaa huku tukizungumza, na habari kuu ilikuwa kuhusu Sia. Aliniambia kwamba Sia alifika pale mwezi wa nne na alimpa namba yangu ya simu, lakini nikawa sipatikani.

MIMI: “Ni kweli kaka nilikuwa sipatikani, nilikuwa nje ya nchi.”

JAMAA: “Nitakupa namba zake umtafute, subiri nichukue simu nikupe.”

MIMI: “Si unamuona mama kijacho alivyo makini kuangalia huku? Nafikiri anahisi kuna jambo linaendelea. Wewe cha kufanya nitumie namba kwenye simu, mimi nitaiona.”

Nilirudi kuendelea kujumuika nao na Iryn uvumilivu ulimshinda na akaanza maswali;

IRYN: “Darling! Anashida gani?”

MIMI: “Mambo ya wanaume mummy, hakutaka kuongea hapa mbele yenu, haitakuwa busara nikisema.”

Muda huu, Claire alikuwa akitabasamu, na nilihisi kama aliona kwamba Iryn anazingua, kwani alikuwa na maswali mengi kama vile ni polisi.

Nilianza mazungumzo na Claire na nikamuomba anisaidie kumuangalia Iryn kwa kipindi ambacho sitokuwepo. Kwa upande wake, hakuwa na shida na aliahidi kumuangalia kwa jicho la kipekee, ukizingatia kuwa ni rafiki yake wa kitambo.

Tulishinda Coco hadi jioni, kisha tukaondoka kurudi na tukamuacha Claire pale Marina kabla ya kurudi kwenye apartment yetu. Baada ya kurudi, nilifanya mawasiliano na Jane, ambaye alisema wamefika Tabora salama. Niliendelea kumsisitiza asimwambie Mary kuhusu mpango wangu wa kuja kesho.

Baada ya kuongea na Jane, nilimpigia simu Cami ili anipe ratiba ya safari ya kesho. Alisema safari itaanza saa sita mchana, hivyo ni lazima niende kwao mapema sana.
*****

Ilikuwa Ijumaa saa tatu asubuhi nilipoondoka mapema kuelekea Mikocheni kwa mzee Juma kwa ajili ya kuanza safari ya kwenda Tabora. Nilipofika, nilikaribishwa sebleni na Cami, kisha akaaga akienda kujiandaa.

Nilikaa kwa muda mrefu sebuleni nikimsubiri, na baada ya nusu saa, Cami alitoka. Tulianza kuzungumza taratibu, tukijadili mambo mbalimbali. Dakika ishirini zilipita, wazee walitoka, na nilishangazwa kugundua kuwa tutaenda na Mrs. Juma. Nilimsaidia Cami kubeba mabegi na kuyaweka kwenye gari, kisha tukaanza safari ya kuelekea JNIA.

Tulipofika uwanja wa ndege, tulikutana na marafiki zake wengine wawili, hivyo tukawa jumla ya watu sita. Safari yetu ilianza saa 7 mchana kwa kutumia private jet kuelekea Tabora, na tulifika saa 9 kasoro. Tulipowasili Tabora, gari aina ya Noah lilitufikia na kutupokea, tayari kutupeleka kijijini.

Barabara ndefu ya lami ilijaa mandhari ya kijani, miti ya miembe na migomba ikipita haraka pembeni. Kulikuwa na utulivu wa kina, kama kwamba tulikuwa tunaelekea mahali pa heshima kuu na tunapaswa kuwa kimya. Mzee Pama alikuwa mtu wa heshima, na urithi wake ulikuwa na athari kubwa kwa kila mmoja wetu.

Tulipofika kijijini jioni, hali ya hewa ilibadilika ghafla na kuwa baridi kali. Bila kupoteza muda, tulienda moja kwa moja hadi kwenye lodge maarufu kijijini pale. Mzee Juma alitazama mazingira kwa utulivu kisha akasema kwa sauti ya kujiamini, "Tutafikia hapa, kule kwa Pama hapatatosha, watu ni wengi sana na hatuwezi kupata sehemu ya kulala."

Mzee alikuwa amelipia vyumba vitatu, kimoja kwa ajili yao, kimoja kwa Cami, na kimoja kwa ajili yangu. Alituambia tupumzike kwanza, kisha baadaye tutaenda msibani kutazama mazingira.

Saa moja usiku tulifika nyumbani kwa Mzee Pama na tulielekea moja kwa moja ndani, kwaajili ya kuwasalimia ndugu na kuwapa pole. Mrs. Pama alikuwa pale, pamoja na Jane, wote wakiwa na huzuni nyusoni mwao. Kulikuwa na ukimya mzito, lakini tulihisi upendo wa familia iliyoungana kwenye kipindi hiki kigumu. Mary, alishtuka sana kuniona. Macho yake yalionyesha mshangao, hakutarajia kabisa ujio wangu Tabora.

Cami na mama yake walibaki sebuleni, wakijumuika na wengine, huku mimi na Mzee Juma tukatoka nje. Tulijiunga na wazee wenzetu waliokuwa wamekaa kwenye garden, wakiendelea na mazungumzo ya taratibu, yakiwa na mchanganyiko wa huzuni na kumbukumbu za maisha ya Mzee Pama.

Kwa upande mwingine, vinywaji vilikuwa vya kutosha, soda, bia za local na za kisasa, wines na spirit zikiwa zimepangwa kwa ustadi, bila kusahau nyama choma ya ng'ombe na mbuzi. Watu walikuwa wengi, wengi zaidi kuliko nilivyotarajia. Marafiki wa Mzee Pama, wafanyakazi wenzake, na wafanyabiashara waliokuwa wakishirikiana naye walikuwa wamejaa kwenye viunga vya nyumba.

Kila kona ilijaa sauti za mazungumzo ya taratibu, huku wengine wakiwa kwenye makundi wakikumbuka safari ndefu ya maisha ya mzee Pama, aliacha alama nyingi kwa watu waliomzunguka.

Saa 5 za usiku Mary alikuja niliko na alianza kumsalimia mzee Juma na wazee wengine waliokuwa jirani. Macho yangu yalivutwa kwake, nikijiuliza, "Mary amekuja kufanya nini hapa tena?". Alikuja mpaka nilikokaa maana nilikuwa na vijana wenzangu na nikasogea kumpa seat, akakaa.

MARY: “Bae, kwanini hujanambia kama unakuja? Sijapenda.”

MIMI: “Jane anajua, ila nilitaka nikusurprise, usichukie bhana.” Huku nikimtuliza kwa kumchezea paja lake.

MARY: “Honey, nakuonea huruma, umetoka safari na sijui utalala wapi maana vyumba vimejaa.”

MIMI: “Usijali, mzee Juma alitutafutia lodge ya kufikia.”

Huku akitabasamu,

MARY: “Nimefurahi kukuona mpenzi wangu, acha nirudi ndani, kabla ya kuondoka niambie sawa?”. Mary aliambia kwa upole, akinihakikishia kwa macho ya upendo.

MIMI: “Usijali mpenzi wangu.”

Mary aliondoka nami niliendelea kupiga story na masela pale tukicheka na kubadilishana mawazo kama kawaida. Ghafla, jamaa mmoja akauliza, "Vipi huyu ni shemu wetu?"nikamjibu, "Ndiyo, bro." Kisha akaanza kumsifia Mary. "Aisee, huyu dada ni mzuri sana. Niaje sasa, una miliki chombo kikali mno, sio wa kawaida huyu." Jamaa alikuwa ni mtu wa Arusha.

Tulicheka pale kwa furaha, kila mmoja akitoa maoni yake. Jamaa wengine nao walijiunga kwenye mazungumzo, wakimsifia sana Mary. "Aisee, huyo ni pisi kali," wakionekana kuvutiwa na uzuri wa Mary. Maneno yao yalileta ufahari kidogo moyoni mwangu, nikatambua kwa undani zaidi thamani ya Mary.

Ilipofika saa sita kasoro, nilipokea ujumbe kwenye simu kutoka kwa Mary uliosomeka, "Mpenzi wangu, nimekumiss sana, naomba tuonane, tafadhali." Ujumbe wake ulinigusa sana, bila kusita nilimjibu kwa kumuandikia, "Baby, si tulikuwa pamoja hapa muda si mrefu?"

Tukaanza kuchati zaidi, akaniambia, "Naomba tukutane sehemu tulivu, tuzungumze tafadhali."

Nilijiuliza wapi ningeweza kukaa na Mary katika mazingira haya yenye watu kila kona. Nikamuuliza, "Baby, unaona mazingira haya? Unafikiri tutaongelea wapi?"

Jibu lake lilinishangaza sana, hakika sikutegemea kama angenipa wazo zito namna ile. Aliniandikia, "Mpenzi wangu, twende nje ya geti, kuna magari mengi, hatutakosa sehemu tulivu ya kuzungumza."

Nilireply, "Sawa, ngoja nianze kutoka nikague usalama, nitakutumia ujumbe uje."

Nilitoka nje ya uzio kukagua usalama, na kukuta magari mengi sana yakiwa yamepaki pale nje. Nilitafuta sehemu nzuri ya kuweza kusimama kwa usalama, kisha nikamtumia ujumbe aje. Nilimsisitiza sana afiche uso wake hata kwa kutumia ushungi, ili asiwe rahisi kutambulika.

Haikuchukua muda Mary aliwasili eneo la tukio. Aliponiona, alinikumbatia kwa nguvu na kunibusu kwa shauku, akianza kunipa ulimi wake, na tukaanza kubadilishana lita kazaa. Mary alisema tunaondoka wote kwenda kulala, lakini kwa upande wangu niliona ni jambo lisilowezekana.

Baby hili haliwezekani kabisa, na Jane atalala na nani?”

“Nimemuaga nakuja kukesha na wewe, pia nimemuachia simu yangu, lazima tuondoke wote.”


Mary alionekana kuwa na hamu sana ya kuwa nami, na nilihisi hisia zake. Nilijiwazia kwa muda pale, kisha nikaamua, "Wacha tu niondoke naye tukalale pamoja." Kurudi ndani kuaga niliona itakuwa shida, kwanza mzee Juma alikuwa bize sana na marafiki zake, wakiongea na kucheka. Nikaona haina haja ya kuvunja mazungumzo yao, bora niondoke kimyakimya na Mary.

Tulipofika lodge, tukaanza kupiga stori, na gumzo kubwa likawa suala la Mary kunizalia mtoto. Alikuwa na mawazo mengi kuhusu hilo, lakini kwa upande wangu, niliona wazi kwamba Mary alikuwa mwanamke sahihi wa kunizalia mtoto. Pia, mtoto angekuwa sehemu salama, mtu ambaye ningeweza kumtegemea kwa maisha yetu ya baadaye.

Hata hivyo, sikutaka kumlazimisha kabisa. Nilijua kwamba hili lilikuwa suala nyeti, na nilitaka afanye maamuzi kwa hiari yake mwenyewe. Nilimwambia hilo, ili asijisikie shinikizo lolote na afanye maamuzi sahihi.

Lakini mawazo yangu hayakuishia hapo. Nilianza kuwa na wasiwasi kuhusu familia yake. Nikajiuliza, ikijulikana kwao itakuwa vipi? Nini kitakachotokea hasa pindi mdogo wake, Prisca, atakapojua? Je, atalichukuliaje? Lakini mwishowe, niliamua kujituliza. Nikajisemea kimoyomoyo, "Potelea mbali, ni maisha yangu."

Baada ya nusu saa kupita nilisikia mlango ukigongwa, na nilisogea taratibu kwenda kufungua, niliuliza ‘nani?’ Akajibu ‘Cami’ ndo kufungua mlango na kutoka pale koridoni.

Cami alikuwa amevaa sweta la Prova na mkononi alikuwa kashika mfuko, alinikabidhi pale;

CAMI: “Mama alisema nikuletee, nikakukosa. Nakupigia hupokei simu, nikahisi utakuwa umerudi kulala.”

MIMI: “Ahsante sana! Nimechoka nikasema nitoroke nirudi.”

CAMI: “Haya wewe lala tutaonana asubuhi.”

Niliingia chumbani, na Mary hakuwa na nia ya kupoteza muda hata kidogo. Zoezi letu lilianza kwa kasi ya ajabu, kama vile tupo kwenye mbio za ushindani. Kadri dakika zilivyozidi kusonga, mchezo ulionekana kuwa mrefu zaidi, kila sekunde ikihesabika. Ilikuwa mechi ndefu, sauti za mashabiki zilisikika kwa mbali, zikiongezeka na kupungua, kulingana na jinsi ambavyo spidi ya mchezo ilikuwa inabadilika. Baada ya timu zote kufungana bao za kutosha, hatimaye mechi iliisha kwa timu zote kupumzika.

Saa 11 alfajiri, Mary aliondoka kurudi kwa Jane ili kusaidia na majukumu, maana ilikuwa siku maalum ya ukumbusho wa kifo cha Pama. Nami niliingia bafuni haraka kuoga na kujiandaa ili niwahi kufika eneo la tukio kusaidia kazi. Kabla ya kuondoka, nilijaribu kumpigia simu mama kijacho, lakini hakupokea. Niliwaza huenda bado amelala, kwa hiyo nikamwandikia ujumbe mzuri wa kumtakia asubuhi njema.

Nilipofika eneo la tukio, nilikutana na vijana wenzangu ambao tulikuwa tumekaa pamoja usiku uliopita. Kazi kubwa iliyokuwa ikiendelea ilikuwa ni kuandaa mahema, kupanga viti vya wageni, na baadhi ya wengine walikuwa wameenda makaburini kufanya usafi. Kila mtu alikuwa na majukumu yake, na hali ya maandalizi ilikuwa imechukua kasi.

Kwa upande mwingine, nilipowaona binti watatu wa Pama wakiwa wamesimama kwa mbali, nilisogea taratibu na kwenda kuwasalimia. Walionekana wenye furaha kuniona, na tulibadilishana salamu kwa heshima. Nilipata pia nafasi ya kuonana na Jane, na tukafanya mazungumzo ya kina, kwani nilikuwa na hamu ya kujua jinsi ndugu wa Pama wanavyomchukulia na kumtendea pale nyumbani.

Siku hii ilikuwa na ugeni mkubwa sana wa watu, na idadi yao ilizidi matarajio. Hata baadhi ya viongozi wakubwa walifika eneo la tukio. Kila mmoja kwa nafasi yake alienda kutembelea kaburi la mzee Pama, akitoa maneno ya faraja na mawazo ya dhati kutoka moyoni, kwa heshima ya kumbukumbu yake. Mazingira yalikuwa ya utulivu na ya heshima kubwa kwa marehemu.

Saa 11 jioni nilipanga niondoke nikapumzike lodge na kichwani nilikuwa na mipango ya kesho kuanza safari ya kurudi Dar es Salaam. Hata hivyo, sikuwa bado nimempa taarifa Mzee Juma, kwani alikuwa na shughuli nyingi mchana kutwa. Niliwaza kumtafuta baadaye ili kumfahamisha kuhusu mpango wangu wa kuondoka kesho.

Wakati natoka nakutana na Cami getini akiwa na binti mkubwa wa mzee Pama, na alinivuta pembeni ili tuzungumze;

CAMI: “Insider unaenda wapi?”

MIMI: “Unataka twende wote.?”

CAMI: “Kama sio mbali naweza kukupa kampani.”

MIMI: “Mimi naenda kulala ili badae niwe na nguvu ya kukesha.”

CAMI: “Halafu wewe mwanaume, kwahiyo umeamua kuhonga sweta nililokuletea jana.”

Nilicheka pale;

MIMI: “Mary aliomba, nisingeweza kumkatalia ukizingatia ni mtoto wa kike.”

CAMI: “Haya, kapumzike hata mimi nitakuja sio muda mrefu.”

Nilipanda bodaboda na kuelekea lodge, lakini nilipofika, nilikuta dada wa mapokezi hayupo, na nilikuwa tumeacha funguo kwake. Nilimuulizia lakini hakupatikana, na baada ya kupewa namba zake, nilijaribu kumpigia lakini hakupokea. Nikiwa sina njia nyingine, nikaamua kukaa kwenye sofa kupumzika kidogo nikisubiri.

Baada ya kama dakika 15, dada wa mapokezi alirudi. Alivyoniona, aliomba radhi kwa kuniweka nikisubiri, akisema alikuwa ameenda kutafuta chakula. Mimi sikuwa na la kusema, hivyo nilichukua funguo kimya kimya na kuelekea chumbani. Nilikuwa nimechoka sana, hivyo mara tu nilipofika, nikalala.

Saa 2 usiku, baada ya kuamka, nilikuta ujumbe kutoka kwa Cami ukisomeka, "Hey Insider, unavyoenda msibani nijulishe." Wakati huohuo, mama kijacho pia alikuwa amenitafuta, hivyo nilimpigia simu haraka. Iryn alitaka kujua lini narudi Dar es Salaam, kwani nilikuwa nimeahidi kurudi kesho Jumapili. Nikamwambia nitaweka mambo sawa na kuhakikisha narudi kama nilivyoahidi.

Baada ya hapo, nilimpigia simu Cami na kumtaarifu ajiandae kwa ajili ya kuondoka. Baada ya dakika 10, alinigongea ili tuondoke na tukiwa njiani, nilimwambia kwamba kesho nitaondoka kurudi Dar es Salaam. Hata hivyo, Cami alinijulisha kwamba haitowezekana kwa sababu mzee alikuwa amekata tiketi za kurudi, hivyo, tutaondoka wote jumatatu.

Baada ya kufika, niliona mazingira yalikuwa yamebadilika sana, kwani kulikuwa na projector kubwa ikionesha highlights za fainali ya ‘UEFA Champions League’. Hapo ndipo nilikumbuka kwamba leo ni fainali kati ya Manchester City na Inter Milan.

Nafasi za kukaa zilikuwa zimejaa sana, hasa kwa upande wa mbele ambapo kila meza ilikuwa na watu wanne. Nilijitahidi kutafuta sehemu nzuri mwishoni, nikaamua kukaa hapo kusubiri mechi. Haikuchukua muda, Mary alifika na tukakaa pamoja. Aliniuliza kuhusu mechi inayoendelea, nikamweleza kuhusu fainali ya ‘UEFA Champions League’. Baada ya dakika 20, Cami alifika akiwa na binti wa pili wa mzee Pama ambaye anasoma Australia, na hivyo tulikuwa jumla wanne.

Tuliletewa wine mbili, lakini binti wa Pama alisema yeye hatumii kilevi, hivyo alikunywa maji. Nilipata nafasi ya kuongea naye kwa mara nyingine na kwa undani zaidi, aliniambia kuwa alikuwa na taarifa zangu, lakini hakuwa ananijua kwa sura.

Mary alisema baada ya mechi, tutaenda wote kulala lodge, na kwa kuwa sikuwa na nguvu ya kumkatalia kutokana na mazingira, niliamua kukubaliana na mpango huo. Cami naye alisema tutaondoka wote kurudi lodge. Hii ilifanya niwe na wasiwasi, kwani nikisema tuondoke wote, atajua kinachoendelea kati yangu na Mary. Nilihitaji kufikiria jinsi ya kuondoka na hawa wanawake, bila Cami kujua kinachoendelea.

Mnakumbuka kwamba nilishawahi kuwambia kuhusu Cami na Mary kwamba wanasoma chuo kimoja, ingawa wanachukua faculty tofauti?. Tangu kipindi kile walipokutana hospitalini na kutambuana, Cami alikuwa na hisia kwamba mimi na Mary tuna uhusiano wa kimapenzi toka muda mrefu. Kwa kwenda nao wote lodge, Cami angeweza kujihakikishia kuwa hisia zake ni za kweli.

Nilimwambia Mary atangulie lodge, na mimi nitarudi ndani ya muda mfupi. Mary alipofika, alinitumia ujumbe kunijulisha kuwa amefika salama. Hapo ndipo mimi niliondoka na Cami kuelekea lodge.

Jumapili asubuhi nilionana na mzee Juma, ambaye alinipa taarifa kwamba tutaondoka kesho asubuhi kurudi Dar es Salaam na aliniaga anaenda kuendelea na kikao chake. Nilirudi chumbani kuendelea na mambo yangu, nikifanya kupitia mipango yangu na ku-update baadhi ya taarifa za biashara yangu na kampuni kwa ujumla.

Simu yangu ilianza kuita, na nilipoangalia, niliona kuwa ni mama kijacho akipiga video call. Kwa hiyo, niliamua kutoka kwenda kupokea simu mbali, kwani Mary alikuwa bado amelala kitandani. Nilienda hadi mapokezi, nikakaa na kupokea simu yake ambayo imeita kwa muda mrefu. Tulianza maongezi, ambapo alitaka kujua kama kweli narudi leo. Nikiwa na hisia mchanganyiko, nilijikuta nikimdanganya kuwa ndiyo, ingawa itakuwa usiku.

Wakati nilikuwa naongea na Iryn, simu ya Jane ilikuwa inaingia. Baada ya kumaliza maongezi yangu na Iryn, nilimpigia Jane. Aliniuliza kama niko na Mary, kwani tangu aamke hajamuona na simu yake aliiacha kwake. Nilimjibu na kumwambia kuwa Mary yupo pamoja nami na atarudi hivi karibuni.

Mary alikuwa bado amelala, hivyo nilimuamsha ili kumpa taarifa kuhusu Jane aliyekuwa akimtafuta, na alisema atarudi mchana. Nilimwambia ajiandae ili tukatafute kitu chochote cha kula, na alikubaliana kwani pia alisema anasikia njaa. Vita ya usiku ilikuwa ngumu sana.

Tulienda katika mgahawa mmoja wa karibu na lodge, tukapata supu. Katika muda huu, nilitumia nafasi kumuuliza Mary atarudi lini Dar, lakini alijibu kuwa bado hajapata taarifa kutoka kwa Jane. Baada ya hapo, tulirudi lodge na kwa bahati mbaya tukakutana uso kwa uso na Cami pale mapokezi.

Cami alionyesha kushangazwa kumuona Mary maeneo haya, na nilihisi kama alihisi kuwa kuna something fishy kinaendelea kati yetu. Tulisalimiana, na mimi nikaondoka kuelekea chumbani nikiwaacha wakiendelea kuongea.

Mchana tulienda nyumbani kwa Pama ambapo watu walizidi kuja kutembelea kaburi lake na kuondoka. Pia, nilimuaga Jane pamoja na ndugu wengine wa Pama, akiwemo mama yake mzazi. Nilifanikiwa kuonana na Mrs. Pama, nikamsalimia na kumpa pole kwa mara nyingine tena. Mrs. Pama alifurahi sana kuniona na alinishukuru kwa ujio wangu.

Niliendelea kushinda eneo la tukio hadi jioni, na baada ya kuona kwamba hakuna jambo muhimu lililobaki, niliondoka kurudi lodge ili nijiandae kwa safari. Mama J alinipigia simu na kuuliza nitarudi lini nyumbani, kwani muda umeenda na bado sijarudi, hivyo alikuwa na wasiwasi mkubwa kuhusu hali yangu.

Baada ya lisaa kupita, Mary alikuja lodge akiwa na karata, na tukaanza kucheza mchezo wa 'last card'. Tulikubaliana masharti, mimi nilikuwa naweka pesa kwa kila mzunguko, ambapo kama Mary atashinda, angechukua 10,000. Kwa upande wake, tuliweka sharti kwamba ikiwa ningeweza kumshinda, angevua nguo moja kwa kila mara ningeweza kumshinda. Na kama ningemvua nguo zote, ningeonekana mshindi, na mchezo wa kwichikwichi ungeanza. Ilikuwa ni game ndefu sana ambayo mshindi kupatikana ilikuwa ni ngumu, lakini baadae uvumilivu ulitushinda tukaanza kupeana kwichikwichi.

Jumatatu asubuhi na mapema tulianza safari ya kurudi Dar es Salam na tuliwasili JNIA saa sita mchana. Kwa upande mwingine mama kijacho wangu alikuwa amenuna sana, maana nilimdanganya nimepitia Dodoma mara moja kuweka mambo sawa.

Gari lilifika kutuchukua pale JNIA, na safari yetu kuelekea Mikocheni ikaanza kwa kutumia barabara ya Posta ili kuepuka foleni. Nilipendekeza wanishushe 'Dar Free Market' ili iwe rahisi kwangu kufika Masaki. Mzee Juma aliniambia kuwa baada ya kumaliza mipango yetu, tuwasiliane kwa ajili ya kupanga tukutane tena.

Nilichukua bodaboda ya kunipeleka na ndani ya muda mfupi niliwasili, na kwa bahati mbaya Iryn hakuwepo. Nilimpigia simu akanambia yuko kwa Claire na atarudi sio muda mrefu, hivyo niliingia bafuni kuoga.

Baada ya hapo nilimkumbuka Sia na nilitamani sana kuongea naye maana ni muda mrefu sana ulikuwa umeshapita. Nilimpigia simu na iliita kwa muda mrefu na akapokea;

MIMI: “Hello Sia, ni mimi Insider.”

SIA: “Insider au Khalid?”

Nikakumbuka kuwa nilimdanganya jina langu siku tuliyokutana Coco beach;

MIMI: “Nimekumiss sana mrembo.”

SIA: “Namba yako ilikuwa haipatikani mpaka nikahisi labda kaka alikosea kuniandikia, hata baada ya kurudi tena alinambia ipo sawa nayeye alisema hupatikani pia.”

MIMI: “Ni kweli nilikuwa nje ya mji, lakini nimerudi. Nambie lini tuoanane maana nina maongezi muhimu sana na wewe.”

SIA: “Kesho kutwa nina safari ya kwenda nje, kesho nitakuwa busy sana, naomba tuonane nikirudi kama inawezekana.”

MIMI: “Alright, unatarajia kurudi lini?”

SIA: “After one week, nitakuwa nimerudi.”

MIMI: “Alright, no problem.”

Baada ya kuagana na Sia, nilipanda kitandani kisha nikalala, ajabu sikuwa na usingizi kabisa, nilijikuta naanza kuingia kwenye mawazo tofauti kuhusu maisha yangu yote kwa ujumla.

Baada ya masaa 2 kupita, Iryn alirudi na habari kubwa aliyonipa ni kwamba anajisikia dalili za kujifungua, hivyo ijumaa ataondoka kwenda South Africa. Nilitamani kujua huko South Africa atajifungulia wapi? Na alisema atajifungulia kwake.

Kujifungulia kwake niliona ni wazo baya, kwani alihitaji kuwa na mtu mwenye uzoefu na haya mambo;

MIMI: “Baby kwanini usiende kwa mzee uwe karibu na mama mdogo?”

IRYN: “Kwa mama mdogo? You can’t be serious. Mara 100 nikaenda Ethiopia kwa mama mkubwa nitakuwa salama.”

MIMI: “Unamaanisha mama mdogo atakufanyia kitu kibaya? Sindo wewe ulisema mpo cool?”

IRYN: “Anaweza kupretend, lakini hawezi kuwa na upendo wa kweli.”

MIMI: “Sasa utakuwa na nani huko South, ushaanza kunipa wasiwasi mapema hivi.”

IRYN: “Dada yangu ‘Vivian’ wa Ethiopia atakuja Dar siku ya alhamis na tutaondoka wote kwenda South Africa.”

Niliwaza pale nikaona kuna haja ya kuwasiliana na dada yangu na kumpanga kuhusu hili suala ili kama itawezekana, bhasi awahi kwenda South Africa na wifi yake.

Nilimpigia simu Sister na kuzungumza naye kuhusu suala la Iryn. Alisema kwamba lilikuwa kwenye mipango yake, lakini alikuwa anasahau kuniuliza tarehe sahihi ambayo Iryn anaweza jifungua. Sister aliongeza kuwa atakuja Dar siku ya Ijumaa, na siku ya Jumamosi wataondoka pamoja na Iryn kuelekea South.

Nilimpa Iryn taarifa kuhusu safari yake ya kuelekea South pamoja na dada yangu. Alifurahi sana kusikia habari hizi na alinishukuru kwa kumjali. Aliomba nijiandae ili tuende Karambezi kwa ajili ya chakula cha mchana.

Tukiwa Karambezi, tulipanga mipango mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuitisha kikao cha dharura kitakachohusisha viongozi pekee. Pia, tulijadiliana kuhusu sakata la ofisi ya Mikocheni, kwani muda tuliopatiwa ulikuwa umekwisha na tulitakiwa kuondoka kutoka ofisini.

MIMI: “Baby, hivi kwanini ulishindwa kupanunua pale na uwezo unao.”

IRYN: “Nilikuwa tayari kupanunua, tatizo bei ni kubwa sana mpaka nikakata tamaa.”

MIMI: “Alitaka kiasi gani?”

IRYN: “Alikuwa anaanza na billion 1, mwisho kabisa alisema million 900. Unaona hio bei ni sawa na thamani ya kiwanja? Ndomana niliamua kuacha tu.”

MIMI: “Duuh! Mzee wa watu anazingua, au sababu ni Mikocheni?”

IRYN: “Hata kama ni Mikocheni kuna maeneo ukiambiwa hiyo amount unatoa maana unaweza kufanya investment yoyote na pesa yako ikarudi, pale labda ujenge apartments napo pesa yako kurudi itachukua muda mrefu sana.”

MIMI: “Wewe ulikuwa tayari kulipia kiasi gani?”

IRYN: “Kwa 500M ningelipia maana ni fair price. Lakini bado alinikatalia akasema ninamtukana.”

MIMI: “Bhasi, tutatafuta plan B.”

IRYN: “Nakuachia hii kazi, ijumaa tunapokutana uwe na majibu juu ya hili.”

Tulitumia masaa mawili pale Karambezi, kisha tukaondoka kurudi kwenye apartment yetu. Baada ya kufika, nilianza kumtengeneza nywele zake na kuzipaka mafuta, kwani alisema hana mpango wa kwenda salon au kusuka. Wakati huo, simu yangu ilikuwa ikilia, na aliichukua kwa haraka sana, alisema, “Hivi huyu Asmah anataka nini kwako? Nafikiri hanijui vizuri.”

TO BE CONTINUED.
Iendelee
 
Hivi wewe huogopi unavozurura kukutana letsay na shemeji wako au mkeo au mkwe yani whoever wakat unadai upo Dom unazurura Dar au ni vile huo mji mkubwa mana ingekua hapa Ilembula ungeshakamatwa ndani ya dk 14 za mwanzo
Pale ilembula ukitoka tuu stend unaenda igula lazima ukutane nae pale kona kwa zakaria
 
SEASON 02
CHAPTER 37

BY INSIDERMAN”

PART A

Siku ile nilipokutana na Asmah, nilimwambia kwamba afocus zaidi kwenye maisha yake. Nia yangu haikuwa kumuumiza au kumvunja moyo, bali nilihisi ni muhimu kukaa naye mbali kwa muda ili nirekebishe mambo kati yangu na Iryn. Pia, nilitamani Asmah apate nafasi ya kutafuta mtu ambaye atakuwa sahihi kwake, kwa maisha yake ya mbele.

Tangu siku ile tulipoonana, Asmah amekuwa akinipigia simu mara kwa mara na kuomba tukutane. Hata hivyo, mara zote nimekuwa nikimkatalia kwa visingizio vya kuwa na shughuli nyingi, nikimwambia nitamtafuta baadaye, lakini ukweli ni kwamba sijawahi kufanya hivyo.

Wakati nikiwa Tabora, tuliwasiliana na nikampa ahadi kwamba tutakutana Jumatatu mara tu nitakaporudi Dar ili tuzungumze na tuliweke sawa hili jambo. Niliporudi nyumbani, Asmah alinipigia simu mara nyingi, lakini sikujua kwa wakati huo kuwa alinitafuta sana. Kumbe, mama kijacho alikuwa anaziona simu na ujumbe wake kabla mimi sijapata nafasi ya kuona.

Katika kipindi hiki ambacho Iryn ni mjamzito, nilijitahidi kuepuka ugomvi wowote naye. Simu yangu kubwa mara nyingi nilikuwa namuachia kwa sababu sikuwa na chats zozote zenye utata. Mary, kwa upande mwingine, alikuwa anajua kinachoendelea, na tulikuwa tunawasiliana kwa kutumia namba mpya niliyokuwa natumia nikiwa Dodoma. Pia, Mary alishauri tuendelee kutumia namba hiyo mpya ili Prisca asigundue chochote kinachoendelea kati yetu.

Wakati nikiwa na Iryn pale sebuleni, simu ya Asmah ilipoita tena, Iryn alichoka na hali hiyo na akaamua kuipokea mwenyewe. Alionekana kushindwa kuvumilia zaidi, huku wivu ukiwa unamsumbua.


CONTINUE:

Mimi muda huu sikuwa na uwezo wowote wa kumzuia, hivyo niliamuacha aongee naye na aliweka loud speaker.

IRYN: “Asmah, habari yako.”

Asmah hakutegemea kwamba Iryn angekuwa ndiye anayepokea simu, na ghafla akawa mpole.

ASMAH: “Ooh! Bossy, habari yako.”

IRYN: “I'm good. What's your problem? You have been calling Insider nonstop."

ASMAH: “Alinambia yuko Tabora msibani, nilitaka kujua kama karudi.”

IRYN: “What is really going on between you and Insider? Please tell me the truth."

ASMAH: “Nothing is going on between us. He is one of my closest friends, and I really appreciate that."

IRYN: “Asmah, why are you doing this? I know you’re lying to me. Why are you disrespecting me like that? Fu**cking with my Man, and you know I’m pregnant with his child.”

ASMAH: "I didn't mean what I said."

IRYN: “You know I gave you all my respect, but you still sneak around and sleep with my Man. Usione nimenyamaza kimya, najua kila mchezo mnaocheza. Nilitegemea ungekuwa na heshima zaidi kwangu hasa baada ya mimi kuwa mjamzito, lakini hujali hata kidogo."

ASMAH: “What are you talking about.?”

IRYN: “Are you just pretending not to know what I’m talking about? You’re such a bad bitch, mpuuzi kabisa…..”

Nilipoona Iryn ameanza kupandisha hasira, ilibidi nimtulize na kumnyang’anya simu kwa sababu alikuwa amevuka mipaka. Alisimama kwa hasira, akaibamiza simu yangu kwa nguvu kwenye sakafu, na kisha akaelekea chumbani.

Nilishindwa kuelewa kwa nini Iryn alikuwa na hasira kubwa kiasi hiki, wakati Asmah hakuwa amesema chochote kibaya. Nilipoinama na kujaribu kuokota simu yangu, niligundua kwamba skrini ilikuwa imevunjika, betri ilikuwa imevimba, na sehemu nyingine zilikuwa zimeharibika. Nilimfata chumbani, lakini mlango ulikuwa umefungwa. Nilisikia sauti ya kilio kutoka ndani, na ilikuwa ni kilio cha maumivu makali.

Baby, please fungua mlango.”

Nilianza kugonga mlango pale, lakini hakuonesha dalili za kufungua

Baby, naomba tuongee. Tafadhali fungua mlango, mpenzi wangu."

Bado alibaki kimya na hakuzungumza chochote, aliendelea kulia kwa sauti kubwa. Hali hii ilinisababisha nijisikie vibaya sana, na niliona kama nimemkosea sana.

Niliamua kurudi seating room na kukaa kwenye sofa huku nikitafakari namna ya kutatua hali hii. Niliwaza kwa haraka nikaona ni busara niwe mpole na kumuomba msamaha ili kuepusha matatizo, ukizingatia hali aliyonayo kwasasa hatakiwa kuwa katika hali hii.

Ilipita nusu saa, lakini bado hakuonyesha dalili za kufungua mlango, na hapa nikaingiwa na wasiwasi kwa kuwa nilihisi anaweza kufanya jambo lolote baya. Nilimgongea tena, lakini hakutaka kufungua mlango. Hali hii iliponitatiza zaidi, nikaona ni bora nimtafute Claire kwa msaada, kwani sikuwa na jinsi nyingine ya kumsaidia Iryn.

Kumpata Claire ikawa ni shida maana simu yangu imezingua, nikaanza kuchanganyikiwa maana kuondoka na kumuacha peke yake mle chumbani ni jambo lisingewezekana kwanza ni hatari.

Baada ya kufikiri sana nikakumbuka home ninasimu nyingine ambayo inanamba ya Claire, hivyo nilimpigia simu mama J. Baada ya kumpigia alisema yuko chuo, hivyo ikabidi nimpigie Elena dada wa nyumbani na kumuelekeza.

Ndani ya dakika 5, Elena alinitumia namba ya Claire na bila kuchelewa nikampigia simu;.

MIMI: “Mambo, it’s me Insider.”

CLAIRE: “Hey! Insider mambo.”

MIMI: “Mambo mabaya shem wangu, naomba uje home haraka, please.”

CLAIRE: “Kuna nini? Iryn anataka kujifungua?”

MIMI: “Just come, please.”

CLAIRE: “I will be there soon”

Ndani ya dakika 15 Claire alifika na alikuwa akihema sana kama mtu ambaye alikuwa anakimbizwa, na alianza kuniuliza ni nini kinaendelea?

MIMI: “Claire, Iryn kajifungia ndani chumbani ni lisaa limepita, hataki kufungua mlango.”

CLAIRE: “Na hii simu vipi mbona imepasuka, mlikuwa mnagombana?”

MIMI: “Hapana, ni hasira zake ndo kaibamiza simu chini.”

CLAIRE: “Shem niambie ni nini kinaendelea ili nijue namna ya kuongea na Iryn, usinidanganye.”

MIMI: “Sikia Claire, huu sio muda wa kuanza kuulizana kinachoendelea, Iryn amejifungia na lisaa limepita, anaweza fanya jambo baya. Please, naomba unisaidie kuongea naye, ili afungue mlango, mengine tutaongea.”

CLAIRE: “Iryn, alikuwa analalamika sana, amekumiss, sasa umerudi mmegombana, mapenzi yenu siyawezi asee.”

Tuliongozana hadi mlango wa chumbani, na CLAIRE alianza kumuita Iryn kwa sauti ya upole. Baada ya kusikia sauti ya Cami, Iryn alijibu kwa hasira kwamba hataki kabisa kuniona mimi, na alitaka niondoke maeneo hayo.

CLAIRE: “Shem wewe ondoka, acha mimi niongee naye, akikaa sawa nitakupigia simu uje.”

Sikutaka kuwa mbishi juu ya hili, hivyo nilichukua funguo ya gari na kuondoka maeneo haya na akili yangu iliniambia nenda kwa Asmah. Saa yangu ilikuwa inasoma ni saa 10 jioni, nilihisi lazima Asmah atakuwa ofisini muda huu, nikaelekea moja kwa moja mpaka ofisini kwake.

Baada ya kufika nilipark gari parking ya nje kabisa na nikaingia ndani, nilikuwa niko spidi sana hata mapokezi sikusalimia. Nilimkuta Asmah yuko ofisini na moja ya mfanyakazi mwenzie na baada ya kuniona alisimama na kuja usawa wangu.

“Insider are you okay?.”

Sikutaka hata kuongea naye, nilimshika mkono na kuanza kuondoka naye pale ofisini, hata jamaa aliyekuwa naye alibaki akishangaa, kilikuwa ni kitendo cha haraka sana. ‘In a blink of an eye’.

Asmah alianza kulalamika pale,

“Wait, where are you taking me?”

Sikuwa hata nikimsikiliza muda huu, tulipofika nje ya geti nikampa ishara aingie ndani ya gari na akafanya hivyo, hata yeye alikuwa mpole na alianza kuogopa. Mlinzi alishuhudia lile tukio, lakini hakutaka kuingilia maana ananijua vizuri sana, hivyo alikuwa mpole.

Baada ya kuingia ndani ya gari tulianza kuangaliana na Asmah alionekana kuwa na wasiwasi sana;

MIMI: “Unajua kosa lako ni nini?”

ASMAH: “Insider, sikujua kama Iryn atapokea.”

Na nilimkatisha maongezi yake;

MIMI: “Umeniletea matatizo kwa mama kijacho wangu, unapiga simu wakati unajua fika naishi naye kwasasa na nilikupa taarifa mapema kuwa nitakucheki.”

ASMAH: “Insider, I’m really sorry, lakini haya yote wewe ndo sababu kaa ukijua hilo.”

MIMI: “Unamaanisha nini?”

ASMAH: “Umenichunia sana hadi najisikia vibaya, pale napokukumbuka.”

MIMI: “Mimi sijakuchunia kama unavyosema, ila nilikwambia kwasasa niache nifocus na maisha yangu. Kila siku nagombana na Iryn, juu yako, kwasasa sitaki haya yatokee ndomana nikakwambia vile. Pia, tambua natamani sana upate mwanaume atakayekupenda na kukuoa.”

ASMAH: “Stage niliyofikia, kukaa mbali na wewe ni ngumu. Insider nimekuzoea sana ujue, nawezaje kukaa mbali na wewe kwa yote uliyonifanyia?. Umejitoa sana kwangu, kipindi kile nimepata ajali, bado umenisaidia mambo mengi sana, najiona nina deni kwako.”

MIMI: “Huna haja ya kuwa na deni, sababu nilifanya toka moyoni na sihitaji unilipe. Asmah naomba utambue kwamba nakupenda sana, asingekuwa Iryn, huenda tungekuwa wapenzi na asingekuwa mama J, ningekuweka ndani kabisa.”

ASMAH: “Unataka kusema nini?.”

MIMI: “Upendo niliokuwa nao kwako, kwasasa umehamia kwa Iryn. Na sitaki kumpoteza kisa wewe, naomba uheshimu hili, yule ni mke wangu tayari na nitarajia kupata mtoto soon.”

ASMAH: “Hongera sana kwa kutarajia kupata mtoto soon.”

MIMI: “Please, move on kwa usalama wangu na wa kwako pia, tutaendelea kushirikiana kwenye mambo mengine, lakini tuwe na mipaka. Kwa mara ya kwanza leo Iryn, amepaniki live na ametoa maneno makali juu yako.”

ASMAH: “Hata mimi nimeogopa sana, kwa mara ya kwanza nazifeel hasira zake, na sikutoa neno lolote baya.”

MIMI: “Wasiwasi wake, mimi na wewe tuko kwenye mahusiano ya siri, kipindi hiki cha ujauzito amekuwa na wivu sana.”

ASMAH: “Sasa nafanyaje?

MIMI: “Mpigie simu, omba kuonana naye ili muongee juu ya hili, naamini atakubali muonane.”

ASMAH: “Insider mimi naogopa ujue.”

MIMI: “Mpigie simu sahivi, mwambie unataka kukutana naye, ukionana naye atatulia.”

Asmah alitoa simu yake mfukoni na akampigia Iryn, simu iliita bila kupokelewa, akapiga kwa mara ya pili, ndiyo kupokelewa na akamwambia dhumuni lake ni kuonana ili waongee na Iryn alimkubalia, akasema anamtumia location.

ASMAH: “Mimi naogopa siwezi kwenda.”

MIMI: “Sasa unaogopa nini?, nenda kajisafishe na unisafishe na mimi. Usikubali kitu chochote kile atakachokuuliza, wewe ni mtu mzima utajua utaongea nini.”

ASMAH: “What if kama anaushahidi kwamba we had sex.?”

MIMI: “I don’t think so, nafikiri kuna mtu kamjaza haya maneno, Iryn hana ushahidi juu ya hili.”

ASMAH: “Unajuaje kama hana evidence? Na ameongea vile mbele yangu.”

MIMI: “I know her, ingekuwa kweli anazo mimi ningejua tu, Asmah niamini mimi. You have to clean up the mess for me.”

ASMAH: “Sawa acha niende, kama kuna lolote nitakupigia simu.”

MIMI: “Nipigie kwa namba hii kama utapata shida, nitakuwa around.”

Baada ya kuachana na Asmah nilienda Cocobeach- Wavuvi kempu kutulia. Niliagiza heineken zangu mbili huku namsubiri Asmah. Muda huu nilitumia kuchat na Claire, nilimuuliza kuhusu maendeleo ya Iryn ana akasema yuko sawa, japo alilia sana. Nilimuuliza Iryn anafanya nini kwasasa, akasema amekaa kwa balconi na yuko na mgeni, nikajua ni Asmah wala si mwingine.

Kwa upande mwingine, Claire aliendelea kuniuliza shida ni nini, kwani hata Iryn hakuwa amemwambia sababu halisi ya ugomvi wetu. Nilimwambia aendelee kuwa mpole, na kwamba Iryn mwenyewe atamwambia tu chanzo cha ugomvi wetu.

Iryn ni mmoja wa wanawake ambao hawapendi kuweka maisha yao public, ni mtu ambaye anajali sana faragha ya mambo yetu ya ndani na hataki kuyaeleza kwa watu wengine. Hata kitendo kile cha kumpiga kule hotelin kilibaki kuwa siri yake pekee, hakuna mtu yeyote aliyemwambia kuhusu hilo.

Baada ya masaa mawili kupita na hakuna dalili za Asmah kunicheki, nilianza kuingiwa na wasiwasi. Nilijiuliza kwa nini anachelewa kutoka na nini kinaendelea?. Nilijaribu kufikiria kuhusu kumtumia ujumbe, lakini nikaona kwamba ilikuwa ni wazo baya.

Baada ya nusu saa, Asmah alipiga simu na kuniuliza nilipo. Nikamwambia aje Cocobeach tukutane. Ndani ya muda mfupi alifika Cocobeach na alisema yuko karibu na chupa ya Cocacola akinisubiri.

Nilitoka pale Wavuvi, nikamchukua Asmah, na nikaendesha gari kwa kasi hadi karibu na mitaa ya restaurant ya ‘Amigos’. Huko ndipo nilipokipaki gari na kuanza mazungumzo.

MIMI: “Nipe mrejesho wa mlichozungumza na mama kijacho.”

ASMAH: “Kila kitu kipo sawa kwasasa, nimeongea naye muda mrefu sana na amenielewa. Nimesema ukweli kwamba mimi na wewe tulikuwa kwenye mahusiano zamani wakati tumefahamiana, lakini tuliachana na kwasasa sisi ni marafiki.”

MIMI: “Una uhakika amekuelewa?”

ASMAH: “Trust me japo nimebanwa sana, juu yako. Alisema yeye yuko tayari kutuacha tuendelee na mahusiano, huenda yeye ndiye amedandia treni la watu. Nimemwambia Insider anakupenda sana na hayuko tayari kukupoteza na kila siku anajidai utamzalia mtoto wa kike.”

MIMI: “Umefanya jambo la muhimu sana, ahsante.”

ASMAH: “Nimekubali matokeo, japo nilikupenda sana naomba uendelee na Iryn, kwa heshima na wadhifa wake.

MIMI: “Leo ndo unakiri kuwa unanipenda sana?.”

ASMAH: “Ni kweli, kipindi umeanza mahusiano na Iryn nilikuwa naumia sana hujui tu.”

Simu yangu ilianza kuita na kuangalia ni Iryn alikuwa anapiga simu, nilimuonesha Asmah kuwa Iryn anapiga, naye akasema nipokee haraka. Baada ya kupokea aliniuliza niliko, nikamwambia niko Cocobeach, akasema nirudi home mapema.

Ilikuwa ni saa mbili usiku tayari, hivyo sikutaka kupoteza muda na nilimuaga Asmah kwa kumpa ahadi ya kuonana naye hivi karibuni na nikaondoka kurudi home.

Nilitumia muda mfupi sana kufika, kuingia ndani nawaona wamekaa sebleni, nami nikaketi pembeni ya mama kijacho. Wakati huu
Claire alikuwa akitabamu, kana kwamba kuna kitu anataka kuongea. Haikuchukua muda na aliaga anaondoka kurudi kwake, maana alikuwa na majukumu mengine ya kufanya.

Nilimpa kampani mpaka kwake na tukiwa njiani tulikuwa tunaongea na kubwa alisema, Iryn hajasema chanzo cha ugomvi wetu. Pia, aliendelea kusisitiza kwamba Iryn ananipenda sana. Baada ya kufika kwake, nilimshukuru sana kwa msaada wake na tukaagana pale, nami nikageuza kurudi home.

Baada ya kufika, Iryn alikuwa amekaa kwa balconi, hivyo nilienda na nikakaa pembeni yake. Palikuwa na hewa safi na upepo wa bahari ukipiga eneo hili kwa utulivu sana. Tulianza kuangaliana pale, nami niliamua kuvunja ukimya;

MIMI: “Nambie mke wangu, upo tayari tuongee?”

IRYN: “I’m listening.”

MIMI: “Mummy, mimi na Asmah hatuko kwenye mahusiano naku-apia kwa hili. Usipende kusikiliza maneno ya wabongo, hakuna anayependa kuona mimi niko na mwanamke mrembo kama wewe.”

IRYN: “Lazima niwe na maswali, kwanini Asmah tu, akupigie simu nonstop?. Mchana kabla ya kwenda lunch, alipiga simu mara 3 na bado akatuma message akilalamika sana kuwa unamtenga. Kwa haya yaliyotokea, na ninajua fika wewe na Asmah mlikuwa na historia unafikiri nitawaza nini?.”

MIMI: “Nakwambia ukweli, lastweek niliongea na Asmah akae mbali na mimi, na haya yote ni kwasababu yako, sikutaka uendelee kuwa na wasiwasi juu ya ukaribu wetu.

Ilibidi nimueleze ukweli kuhusu mipango yangu juu ya Asmah, ili aweze kuelewa na sikuona haja kumficha juu ya hili.

IRYN: “Unajielezea sana, nimekuelewa tuachane na haya.”

MIMI: “Baby, I don’t want another woman, and I”ll never disrepect you or my daughter like that.”

IRYN: “Unakumbuka tulikubaliana kwamba mtoto akiwa wa kike jina utampa wewe?”

MIMI: “Yes! Darling, unataka nikutajie jina kabisa?”

IRYN: “Don’t tell me hujaandaa jina bado.”

MIMI: “Niliandaa mummy, from today nitakuita ‘mama Ariana’, do you like the baby’s name?”

IRYN: “Yeah, it’s a beautiful name, and I like it. Thank you baba Aria.”

Furaha yetu ilirudi kama zamani na nilimwambia tuende chumbani tukalale maana muda ulikuwa umeyoyoma tayari.

Saa nne asubuhi nilitoka kwenda Mikocheni kuonana na Lucy, pia nilitamani sana tumalize tofauti zetu. Nilipofika pale ofisini niliweza kuonana na Lucy, bila kupoteza muda nilianza kumuomba radhi kwa kumkosea.

Lucy kwa upande wake alisema, aliumia sana kwa kitendo cha mimi kwenda Dodoma bila kumuaga wala kumtafuta, halafu nikawa nawasialiana na Hilda kwa siri, hiki ndo kilimuuma sana. Lucy, aliendelea kusema kwamba hakutegemea mimi ningemfanyia vile, ukizingatia sisi ni washikaji wa muda mrefu sana.

Ukweli nilikuwa nimemkosea sana, hivyo niliendelea kumuomba radhi na baada ya kumuelekeza sana dhumuni la mimi kufanya vile, hapa ndiyo aliweza kunielewa na kunisamehe.

Tulianza kuongea masuala mengine kwa ujumla na kubwa lilikuwa sakata la Asmah. Alinisisitiza sana kama nina mahusiano ya siri na Asmah, bhasi niache mara moja, kwani Iryn alimpigia simu na kulalamika kwamba anahisi kuna jambo linaendelea kati yangu na Asmah.

Baadae tulianza kuongea masuala ya ofisi maana landlord alikuwa ameanza kusumbua tuondoke, kwani alitoa taarifa mapema.

MIMI: “Iryn kaniachia hili suala nifanye maamuzi, wewe ndo manager wa hapa, unashaurije.?”

LUCY: “Hii location ilikuwa nzuri sana na imekaa kimkakati, tunapata wapi tena eneo zuri kama hili?”

MIMI: “Wateja wako wanaokuja hapa ni loyal customers?.”

LUCY: “Ndiyo na wageni wanakuja wengi sana.”

MIMI: “Nimewaza sana asubuhi nikaona ni bora ofisi ihamie Masaki. Tutaepusha cost nyingi sana, pia Masaki hatulipi pango bado pana nafasi kubwa ya kutosha.”

LUCY: “Kumbuka Mikocheni, tulitarget na wale wa kipato cha kati, tukihamia Masaki si tutawakosa hawa customers.?”

MIMI: “Bei zitabaki kuwa zilezile, na sikuzote mteja anafuata huduma bora, ukiwaambia tumehamia Masaki watakuja tu. Halafu, ijumaa tutakuwa na kikao asubuhi, fikiria hili vizuri na kesho unipe majibu ili tufanye maamuzi mapema.”

LUCY: “Sawa bossy, nipe muda nijifikirie juu ya hili.”

Baada ya maongezi marefu na Lucy, nilimuacha aendelee na majukumu yake huku mimi nikiendelea kukagua ofisi kwa ujumla.

Nilipigiwa simu na mama wawili, na wakati nilipoipokea, sauti ya Pili ilisikika. Alinisalimia na kusema kwamba nimewatenga sana, tofauti na zamani. Maneno haya yaliniuma sana, hivyo nikamuuliza yuko wapi. Alisema yupo ofisini kwa mama yake, na nikamwambia nitakuwa hapo baada ya lisaa.

Baada ya kumaliza ukaguzi, nilimuaga Lucy kisha nikaondoka kwenda ofisini kwa mama wawili. Nilipowapa taarifa kwamba nimefika, walikuja haraka, na Pili alinikumbatia mara tu alipoona.

Tulianza mazungumzo na mama wawili, ambapo habari kuu ilikuwa kuhusu mpango wa binti yake kusoma nje. Nilimuuliza Pili kama anaridhia kusoma nje, na alithibitisha. Baada ya hapo, nilimuomba Pili atupishe ili niweze kuzungumza na mama yake kwa faragha.

Mama wawili alifurahi sana kuniona na aliniuliza kuhusu agenda yangu Dodoma. Nikamwambia project nayoifanya kule na alinipongeza kwa hatua hii, kisha tukandelea na mazungumzo mengine kwa muda mrefu. Baada ya mazungumzo, niliomba niondoke na Pili na kumrudisha baadaye. Mama wawili hakuwa na tatizo na ombi hilo na aliniruhusu.

Niliondoka na Pili kwenda Mlimani na lengo langu lilikuwa kutimiza ahadi ya kumpa zawadi ya simu niliyomuahidi baada ya kumaliza shule. Pale Mlimani, nilionana na jamaa yangu, nikamwambia anipe bei ya iPhone 12, kisha nikampa nafasi Pili achague rangi ya simu anayoipenda. Ilikuwa ni surprise ambayo Pili hakutegemea, na alifurahi sana. Baada ya hapo, tukaenda kula pizza pamoja.

Jioni, nilimrudisha Pili kwa mama yake ofisini, ambapo mama wawili alifurahi sana na kunishukuru kwa zawadi niliyompa Pili. Baada ya hapo, nikaondoka kuelekea Masaki kuonana na Hilda ili nimpe taarifa kuhusu kikao kilichopangwa ijumaa.

Nilimshirikisha Hilda kuhusu mpango wa kufunga branch ya Mikocheni na kuwaleta Masaki, na yeye alikubaliana na wazo hili na kusema ni zuri. Nilimpa taarifa za kikao kilichopangwa na nikamwambia aandae ripoti zake vizuri ili aweze kujibu maswali pindi atakapoulizwa.

Muda ulikuwa umeenda, hivyo nikarudi nyumbani ili niwahi kumpikia mama kijacho. Mara tu baada ya kufika, aliniambia ana hamu ya kula chips na yai. Hapo hapo nikatoa simu na kumpigia Sele ili aandae sahani mbili na firigisi. Nikamuaga naenda kuzifuata, lakini akasema tuende wote, kwani amechoka kukaa ndani peke yake, hivyo tukaondoka kwenda kwa Sele.

Sele alishangaa sana kumuona Iryn akiwa mjamzito tena mimba kubwa, na alisema tuingie ndani tukae tusubiri kwani chips ziko jikoni. Iryn kwa upande wake, alisema anakulia palepale na aliagiza atengenezewe zingine za kuondoka nazo.

Baada ya Iryn kuingia ndani, nilibaki nikipiga story na sele;

SELE: “We mhuni unabalaa hujataka kuchelewesha, umemjaza upepo mrembo.”

MIMI: “Hata ile siku nakuuliza mahindi, yeye ndo alihitaji.”

SELE: “Bossy umetisha sana, unakojolea pazuri sana. Mwanamke kama huyu unapataje nguvu ya kuchepuka?.”

Tuliishia kucheka nami, nikaingia ndani kwa mama kijacho wangu ili tule.

Baada ya kumaliza kula, nilimlipa Sele pesa yake na alikata sahani mbili tu, moja alitoa offa kwa mama kijacho wangu, Iryn alifurahi na tukaondoka maeneo haya.

Baada ya kurudi nyumbani, Iryn alikwenda kulala, nami nilitumia nafasi hiyo kuwasiliana na Mary. Nilitamani kujua mpango wake wa kurudi Dar, na alisema kwamba anarudi kesho, Jumatano, pamoja na Jane. Alitamani sana tungeonana, lakini nilimkatalia na kumwambia avumilie hadi Jumamosi, kwani Iryn ataondoka hiyo siku.

PART B

Siku ya Alhamisi ile asubuhi, Iryn alinipa taarifa kuhusu ujio wa dada yake kutoka Ethiopia na alisema ataingia usiku sana. Nilimuuliza atafikia wapi? Akasema anafanya mpango ili afikie Sea cliff hotel.

Saa tano asubuhi, aliniaga kuwa anakwenda kwa mama Janeth kuonana na Jessie, hivyo nilimpa kampani ya ride hadi kwa mama, kisha nikaondoka kuelekea ofisini.

Nilikuwa nakazi ya kukagua hesabu za mauzo vizuri, kwani ni muda mrefu ulikuwa umepita pasipo kufanya ukaguzi. Niliweza kubaini matatizo madogo ambayo ambayo Hilda aliweza kuyajibia, hivyo nikaendelea kupitia ripoti na kuzicompile.

Saa 10 jioni, nilipigiwa simu na Iryn, kisha akaomba niende Mikocheni na alimpa simu jamaa ili anielekeze. Jamaa kunielekeza yalikuwa ni maeneo ya karibu na Shopperz, hivyo bila kupoteza muda niliondoka kuelekea huko.

Ndani ya muda mfupi nilikuwa nimewasili na jamaa alinielekeza hadi napark gari kwenye moja ya showroom ya magari. Sasa, baada ya kushuka ndiyo namuona Iryn na Jessie wamekaa na nikatembea mpaka usawa wao nikawasalimia.

Muda huu Jessie alikuwa ananiangalia tu, namimi nilikuwa namzingua pale;

IRYN: “Darling, follow me.”

Nilimfuata kwa nyuma, hadi ilikokuwa imepark Marcedes Benz.

IRYN: “Darling, hii gari ni nzuri? Unaionaje?”

MIMI: “Ni nzuri sana, halafu hii colour naona unique kwa benz.”

IRYN: “Mimi na Jessie wote tumeipenda.”

Alimuita jamaa ambaye ana asili ya uarabu na akamwambia aiotoe nje ili tuondoke nayo, na palepale aliomba account namba ili afanye malipo. Mimi nilikuwa sijui kinachoendelea kwakweli, nilihisi moja kwa moja gari ni ya Jessie.

Benz ilitolewa showroom mpaka nje kwaajili ya kuondoka, gari ilikuwa ni nzuri ikivutia sana. Aliniita akasema niache taarifa zangu kwaajili ya usajili, hapa sasa ndo nikahisi gari itakuwa yangu.

Sikutaka kubisha na nikafanya kama alivyosema. Jamaa aliahidi kwamba kesho kufikia saa 4 asubuhi kila kitu kitakuwa sawa, hivyo tukachukue plate namba. Baada ya malipo kufanyika, tuliondoka na Jessie akaondoka na ile Audi, wakati sisi tukaondoka na ile Benz. Uvumilivu ulinishinda na nikaanza kuuliza maswali;

MIMI: “Baby, bado sijui kinachoendelea kuhusu hii gari.”

IRYN: “Mimi kama MD, ofisi imekununulia gari ili iwe inakusaidia kwenye majukumu yako pamoja na ya ofisi.”

Niliishiwa hata niseme nini maana sikutarajia kuona Iryn akinifanyia surprise kama hii. Nilikuwa bado siamini kama kweli hii benz nayoendesha kweli ni yangu.

MIMI: “Baby nashukuru sana, hata sijui niseme nini kwahaya yote unayonifanyia. May God bless you.”

IRYN: “Kampuni ina imani kubwa sana na wewe, na hii ni moja ya shukrani yangu. Mimi bado sijakupa zawadi, ila nitaanza kwanza na nyumba mengine yatafuata.”

Tulienda mpaka kwenye apartment yetu, tukapark ile gari, kisha tukaondoka tena na Jessie kumrudisha kwa mama. Baada ya kurudi nilianza kuiangalia ile Benz kwa mara nyingine tena, jinsi ilivyo nzuri na kuvutia, na niliishia kutabasamu.

Kesho yake, ijumaa tulikutana kwaajili ya kikao kifupi ambacho kilihusisha viongozi tu, na tulifanyia pale Giraffe hotel, Mbezi Beach. Kikao kilianza saa 4 kamili asubuhi na kilihusisha watu sita tu, pamoja na Iryn.

Iryn alishukuru sana uongozi wa kampuni kwa kujitoa katika kipindi kigumu, hasa wakati ambapo hatukuwa na mawasiliano. Kama MD, aliahidi kuongeza mshahara kwa 30% kwa viongozi kutokana na kazi nzuri waliyofanya. Hakuishia hapo, aliongeza kuwa baada ya kikao, atatoa zawadi kwa wote.

Baada ya bossy kuongea, nilisimama kutoa taarifa ya mwenendo wa kampuni pamoja na kuifunga branch ya Mikocheni. Lucy na Hilda, walikuwa wanajua kinachoendelea kasoro wengine walikuwa hawajui, hivyo walibaki wakishangaa baada ya kuzisikia taarifa hizi;

IRYN: “Why? I didn’t expect you would come up with this bad idea.”

Nilianza kuwaeleza sababu ya kufanya maamuzi haya;

MIMI: “Tumejadili suala hili kwa undani pamoja na Hilda na Lucy. Tumeona kuwa gharama tunazolipa kwa pango ni kubwa sana, na kuongezeka kwa gharama za umeme, maji, vibali vya leseni na mamlaka nyingine ni mzigo mkubwa. Badala ya kutafuta ofisi mpya, ni bora wateja wetu wa Mikocheni waje Masaki. Hii itatusaidia kupunguza gharama nyingi na kuongeza faida kubwa. Kwa hivyo, tunataka ufahamu kuwa maamuzi haya tumeyachunguza kwa makini na hatuja kurupuka."

Baada ya kuwapa sababu ya kuifunga ofisi ya Mikocheni, kila mtu alinyamaza kimya akifikiria maana ni sababu ambayo ilimake sense vichwani mwao na baada ya dakika kupita, Iryn alianza kuongea.

IRYN: “Mnashaurije juu ya hili, lengo tupate maamuzi sahihi, kila mtu ajaribu ku-assess risks kabla ya kukubali haya maamuzi.”

Baada ya majadiliano ya dakika 20, kila mtu aliunga mkono wazo langu la kuhamishia branch Masaki. Bossy akatoa maelekezo tuanze taratibu mapema ili tusigombane na mwenye nyumba.

Ni kikao kilicho chukua masaa 2 na baada ya kumaliza, tulipata lunch ya pamoja bila kusahu kupiga picha za ukumbusho, nami nilitumia nafasi hii kupiga picha na mama kijacho wangu, kama ukumbusho wa ujauzito wake.

Baada ya kumaliza kila kitu, tuliwaaga na kuelekea Sea cliff hotel kuonana na dada yake ambaye aliingia Dar usiku sana, akitokea Ethiopia.

Tulipofika hotelini, tulimsubiri pale reception na haikuchukua muda alitoka na wakaishia kukumbatiana na Iryn. Dada yake yuko vizuri pia, sio wa kitoto ni mzuri kwelikweli, ila bado hafiki kwa Iryn.

IRYN: “This is Insider, my boyfriend. Do you recognise him?”

VIVIAN: “Of course I do. How are you, brother-in-law?”

MIMI: “I’m fine and happy to see you again."

Mkononi, Viviani alikuwa ameshika kimfuko kidogo na alimpa Iryn, naye akanikabidhi mimi na alinikonyeza, ile kuangalia ndani kuna nini, naona si simu, nikavunga.

Baada ya maongezi mafupi, tuliongozana mpaka parking ili tuondoke, njiani macho yote yalikuwa kwetu. Kwanza niliona ufahari sana kuongozana na wanawake warembo duniani, ni wanaume wachache sana wenye bahati kama hii.

Kwa upande mwingine Sister yangu alinipa taarifa kwamba yuko Airport na anatarajia kuingia Dar, jioni. Nilimpa taarifa Iryn na alisema tufanye booking ya room palepale Sea cliff hotel mapema.

Saa 10 jioni, tuliondoka kwenda JNIA kumpokea dada yangu. Iryn aligoma kabisa kubaki nyumbani na Vivian, alisema haitakuwa vizuri ikiwa nitakwenda peke yangu kumpokea dada yangu wakati yeye yupo

Baada ya kufika JNIA, tulikaa sehemu ya kusubiri abiria. Kama ilivyo kawaida, kila mtu aligeuka kumtizama Iryn kutokana na uzuri wake wa kipekee. Alikuwa kivutio maalum pale, akiwa na mimba yake.

Ndani ya nusu saa, sister aliwasili na waliishia kukumbatiana na wifi yake kisha tukapotea eneo hili. Tulianza kwanza kupitia Sea cliff hotel, ambapo tuliacha mabag yake, kisha tukaelekea home.

Apartment ilikuwa imechangamka sana maana walikuwa wanawake watatu wakipiga story, huku wakicheka. Mimi niliamua kuwapa space na nilienda kutulia chumbani nikipanga mambo yangu.

Nilitoa ile simu kwenye mfuko na ilikuwa ni Iphone 14 kama ileile aliyoivunja hadi rangi na niliweka laini yangu. Nilimpigia simu mama J kumpa taarifa kwamba kesho nitarudi, lakini ni kama aliipokea hii taarifa kwa kutojali.

Wakati huu, nilipata ujumbe kutoka kwa Asmah ambao ulisomeka anataka kuacha kazi, ilikuwa ni taarifa mbaya kwangu, hivyo nikampandia hewani. Nilimuuliza kwanini anataka kuacha kazi, akasema yeye ameamua hivyo kwani anataka kurudi shule kusoma. Nilifunga mazungumzo kwa kumpa ahadi ya kuonana kesho ili tuzungumze vizuri kuhusu suala hili, kwani ilikuwa ni ghafla sana.

Saa 2 usiku, tulitoka kwenda kupata dinner ya pamoja pale Karambezi Café. Wao waliendelea kuzungumza, na story zao nyingi zilikuwa zinahusu leba, wakati mimi nilikuwa nasikiliza kwa sikio la kuiba huku nikijifanya nipo bize na simu

Wakati naongea na dada yangu, nilimshukuru sana kwa kujitoa kwake na kukubali kwenda South Africa. Baada ya masaa mawili kupita, tuliagana ili wajiandae mapema kwa ajili ya safari ya kesho. Walielekea hotelini na sisi tukaelekea kwenye apartment yetu.

Usiku ulikuwa mrefu sana kwani nilikuwa nakazi ya mwisho kuhakikisha barabara inakuwa safi kwaajili ya mtoto kupita. Baada ya kazi ya muda mrefu, japo niliichafua sana, lakini mama kijacho aliridhika na kazi yangu na tukalala.

Asubuhi na mapema nilimuamsha ili tujiandae kwaajili ya safari. Baada ya hapo tuliondoka kuelekea Sea cliff hotel, ambapo tuliwachukua akina sister na tukaelekea Airport. Baada ya kuwasili pale JNIA tulipiga tena picha za mwisho kama ukumbusho, kisha tukachoma ndani.

Nilianza maongezi deep na Iryn na kubwa nilimtakia kila la kheri katika kuanza safari yake mpya ya kuwa mama na nilimpa ahadi ya kwenda South Africa kujumuika naye.

IRYN: “Baba Aria, nakupenda sana na naomba uheshimu hili. Kama nilivyokuahidi before, sitoweza kuwa na mwanaume mwingine zaidi yako, napenda sana nikuzalie mtoto mwingine baada ya huyu.”

Nilipenda sana kusikia akiniita Baba Aria na nilimshika mkono wake nikauweka pajani;

MIMI: “Wewe ni mke wangu tayari, nitaangalia namna ya kuwaoa wote, kuhusu watoto hata ukitaka dozen kwangu ni kazi ndogo.”

IRYN: “Promise me unakuja lini South?”

MIMI: “Mama Aria, ninaomba kwanza nikae na familia yangu, nime-mmiss sana mwanao Junior na mama J. Nitakuja before hujajifungua natamani niwe na wewe leba hadi unajifungua.”

Iryn alifurahi sana kusikia maneno matamu kutoka kwangu na tuliagana kwa kukumbatiana maana muda wa kucheck-in ulikuwa umewadia. Niliwaaga akina sister pamoja na Viviani na niliwaambia nitawaona soon, na kabla ya kuondoka Iryn alinikumbatia kwa mara nyingine tena.

Niliondoka pale JNIA nikiwa na furaha sana, na niliwasha gari kuondoka kurudi Masaki.

Baada ya kufika kwa apartment nilipark vizuri gari, Audi maana nilikuwa naiacha pale, kisha niliingia ndani kuchukua bag, pamoja na funguo za benz yangu, nikaanza safari ya kwenda home, Mbezi Beach.

Katika maisha yangu, hakuna siku niliwaza kama nitakuja kumiliki benz, lakini ndoto yangu ilitimia kwa kuendesha benzi kali. Barabarani nilikuwa mdogo mdogo sana, kama vile namuendesha bibi harusi. Baada ya kufika home, nilimpigia simu Elena akatoka kunifungulia gate.

Junior alikuwa amesimama kibarazani akishangaa gari, kwani anapenda sana magari na baada ya kuniona baba yake, alikuja spidi nikamnyanyua juu. Na alianza kulilia aingie ndani ya gari, bhasi nilimfungulia mlango akaanza kunyonga steering.

Kwa upande mwingine, nilishtuka kuona gari yangu nyingine siioni na baada ya kuuliza, Elena alisema mama J kaondoka nayo. Niliuliza kwani anajua kuendesha? Akanijibu ndio ni mwezi sasa anaiendesha, nilibaki nikishangaa.

Nilifurahi kusikia wife amejua kuendesha gari, kwani ilikuwa ni hatua nzuri kwa upande wetu. Nilikuwa nimechoka sana pamoja na usingizi, hivyo nilienda chumbani kulala. Kwa bahati mbaya sikuweza kulala mapema sababu Junior alikuwa akinisumbua sana.

Jioni, baada ya kuamka niligundua kwamba mama J karudi na nilienda seblen kukaa, lakini nilimsikia akiongea na simu huku akicheka kwa mbali. Nilitulia pale seblen nikishangaa TV na zilipita dakika tano, bado mama J anaongea na simu. Nilihisi haya si maongezi ya kawaida na nilisogea mpaka dirishani kusikiliza, maana alikuwa kasimama pale kibarazani.

Na aliendelea kuongea, tena kwa sauti ya chini, haya ni baadhi ya maneno aliyokuwa anajibu;

Ndiyo, najua… ah, nimekumisi sana

Wewe pia unajua jinsi unavyonifanya nijisikie… usijali, nitakutafuta muda"

Tutaonana tena, usijali.


Baada ya kuona amemaliza kuongea na simu, nilirudi chumbani kwa spidi ya kunyata ili asinishtukie. Baada ya dakika 5 alirudi chumbani na nilijifanya nimelala, aliweka simu chaji akaondoka. Niliamka kwa lengo la kuikagua simu yake, kwa bahati mbaya alikuwa kabadilisha passcode, hivyo nikawa sina option nyingine.

Nilipata wazo nikague mkoba wake, na nikaona kuna risiti za Samakisamaki, Elements, KFC na nyinginezo. Nilianza kukagua za KFC zilionesha tarehe ya leo, za Elements zilionesha ni weekend iliyopita, lakini kilicho nishangaza zilionesha zimeprintiwa saa 4 usiku.

Nilibaki najiuliza mama J sio mtu wa marafiki wala kutoka out, huku Samakisamaki, Elements alikuwa na nani?. Huyu mtu waliokuwa wanaongea wote kwenye simu ni nani? Hapa sasa nikahisi kuna SOMETHING FISHY kinaendelea.

CHAPTER 38
 
SEASON 02
CHAPTER 37

BY INSIDERMAN”

PART A

Siku ile nilipokutana na Asmah, nilimwambia kwamba afocus zaidi kwenye maisha yake. Nia yangu haikuwa kumuumiza au kumvunja moyo, bali nilihisi ni muhimu kukaa naye mbali kwa muda ili nirekebishe mambo kati yangu na Iryn. Pia, nilitamani Asmah apate nafasi ya kutafuta mtu ambaye atakuwa sahihi kwake, kwa maisha yake ya mbele.

Tangu siku ile tulipoonana, Asmah amekuwa akinipigia simu mara kwa mara na kuomba tukutane. Hata hivyo, mara zote nimekuwa nikimkatalia kwa visingizio vya kuwa na shughuli nyingi, nikimwambia nitamtafuta baadaye, lakini ukweli ni kwamba sijawahi kufanya hivyo.

Wakati nikiwa Tabora, tuliwasiliana na nikampa ahadi kwamba tutakutana Jumatatu mara tu nitakaporudi Dar ili tuzungumze na tuliweke sawa hili jambo. Niliporudi nyumbani, Asmah alinipigia simu mara nyingi, lakini sikujua kwa wakati huo kuwa alinitafuta sana. Kumbe, mama kijacho alikuwa anaziona simu na ujumbe wake kabla mimi sijapata nafasi ya kuona.

Katika kipindi hiki ambacho Iryn ni mjamzito, nilijitahidi kuepuka ugomvi wowote naye. Simu yangu kubwa mara nyingi nilikuwa namuachia kwa sababu sikuwa na chats zozote zenye utata. Mary, kwa upande mwingine, alikuwa anajua kinachoendelea, na tulikuwa tunawasiliana kwa kutumia namba mpya niliyokuwa natumia nikiwa Dodoma. Pia, Mary alishauri tuendelee kutumia namba hiyo mpya ili Prisca asigundue chochote kinachoendelea kati yetu.

Wakati nikiwa na Iryn pale sebuleni, simu ya Asmah ilipoita tena, Iryn alichoka na hali hiyo na akaamua kuipokea mwenyewe. Alionekana kushindwa kuvumilia zaidi, huku wivu ukiwa unamsumbua.


CONTINUE:

Mimi muda huu sikuwa na uwezo wowote wa kumzuia, hivyo niliamuacha aongee naye na aliweka loud speaker.

IRYN: “Asmah, habari yako.”

Asmah hakutegemea kwamba Iryn angekuwa ndiye anayepokea simu, na ghafla akawa mpole.

ASMAH: “Ooh! Bossy, habari yako.”

IRYN: “I'm good. What's your problem? You have been calling Insider nonstop."

ASMAH: “Alinambia yuko Tabora msibani, nilitaka kujua kama karudi.”

IRYN: “What is really going on between you and Insider? Please tell me the truth."

ASMAH: “Nothing is going on between us. He is one of my closest friends, and I really appreciate that."

IRYN: “Asmah, why are you doing this? I know you’re lying to me. Why are you disrespecting me like that? Fu**cking with my Man, and you know I’m pregnant with his child.”

ASMAH: "I didn't mean what I said."

IRYN: “You know I gave you all my respect, but you still sneak around and sleep with my Man. Usione nimenyamaza kimya, najua kila mchezo mnaocheza. Nilitegemea ungekuwa na heshima zaidi kwangu hasa baada ya mimi kuwa mjamzito, lakini hujali hata kidogo."

ASMAH: “What are you talking about.?”

IRYN: “Are you just pretending not to know what I’m talking about? You’re such a bad bitch, mpuuzi kabisa…..”

Nilipoona Iryn ameanza kupandisha hasira, ilibidi nimtulize na kumnyang’anya simu kwa sababu alikuwa amevuka mipaka. Alisimama kwa hasira, akaibamiza simu yangu kwa nguvu kwenye sakafu, na kisha akaelekea chumbani.

Nilishindwa kuelewa kwa nini Iryn alikuwa na hasira kubwa kiasi hiki, wakati Asmah hakuwa amesema chochote kibaya. Nilipoinama na kujaribu kuokota simu yangu, niligundua kwamba skrini ilikuwa imevunjika, betri ilikuwa imevimba, na sehemu nyingine zilikuwa zimeharibika. Nilimfata chumbani, lakini mlango ulikuwa umefungwa. Nilisikia sauti ya kilio kutoka ndani, na ilikuwa ni kilio cha maumivu makali.

Baby, please fungua mlango.”

Nilianza kugonga mlango pale, lakini hakuonesha dalili za kufungua

Baby, naomba tuongee. Tafadhali fungua mlango, mpenzi wangu."

Bado alibaki kimya na hakuzungumza chochote, aliendelea kulia kwa sauti kubwa. Hali hii ilinisababisha nijisikie vibaya sana, na niliona kama nimemkosea sana.

Niliamua kurudi seating room na kukaa kwenye sofa huku nikitafakari namna ya kutatua hali hii. Niliwaza kwa haraka nikaona ni busara niwe mpole na kumuomba msamaha ili kuepusha matatizo, ukizingatia hali aliyonayo kwasasa hatakiwa kuwa katika hali hii.

Ilipita nusu saa, lakini bado hakuonyesha dalili za kufungua mlango, na hapa nikaingiwa na wasiwasi kwa kuwa nilihisi anaweza kufanya jambo lolote baya. Nilimgongea tena, lakini hakutaka kufungua mlango. Hali hii iliponitatiza zaidi, nikaona ni bora nimtafute Cami kwa msaada, kwani sikuwa na jinsi nyingine ya kumsaidia Iryn.

Kumpata Cami ikawa ni shida maana simu yangu imezingua, nikaanza kuchanganyikiwa maana kuondoka na kumuacha peke yake mle chumbani ni jambo lisingewezekana kwanza ni hatari.

Baada ya kufikiri sana nikakumbuka home ninasimu nyingine ambayo inanamba ya Cami, hivyo nilimpigia simu mama J. Baada ya kumpigia alisema yuko chuo, hivyo ikabidi nimpigie Elena dada wa nyumbani na kumuelekeza.

Ndani ya dakika 5, Elena alinitumia namba ya Cami na bila kuchelewa nikampigia simu;.

MIMI: “Mambo, it’s me Insider.”

CAMI: “Hey! Insider mambo.”

MIMI: “Mambo mabaya shem wangu, naomba uje home haraka, please.”

CAMI: “Kuna nini? Iryn anataka kujifungua?”

MIMI: “Just come, please.”

CAMI: “I will be there soon”

Ndani ya dakika 15 Cami alifika na alikuwa akihema sana kama mtu ambaye alikuwa anakimbizwa, na alianza kuniuliza ni nini kinaendelea?

MIMI: “Claire, Iryn kajifungia ndani chumbani ni lisaa limepita, hataki kufungua mlango.”

CAMI: “Na hii simu vipi mbona imepasuka, mlikuwa mnagombana?”

MIMI: “Hapana, ni hasira zake ndo kaibamiza simu chini.”

CAMI: “Shem niambie ni nini kinaendelea ili nijue namna ya kuongea na Iryn, usinidanganye.”

MIMI: “Sikia Claire, huu sio muda wa kuanza kuulizana kinachoendelea, Iryn amejifungia na lisaa limepita, anaweza fanya jambo baya. Please, naomba unisaidie kuongea naye, ili afungue mlango, mengine tutaongea.”

CAMI: “Iryn, alikuwa analalamika sana, amekumiss, sasa umerudi mmegombana, mapenzi yenu siyawezi asee.”

Tuliongozana hadi mlango wa chumbani, na Cami alianza kumuita Iryn kwa sauti ya upole. Baada ya kusikia sauti ya Cami, Iryn alijibu kwa hasira kwamba hataki kabisa kuniona mimi, na alitaka niondoke maeneo hayo.

CAMI: “Shem wewe ondoka, acha mimi niongee naye, akikaa sawa nitakupigia simu uje.”

Sikutaka kuwa mbishi juu ya hili, hivyo nilichukua funguo ya gari na kuondoka maeneo haya na akili yangu iliniambia nenda kwa Asmah. Saa yangu ilikuwa inasoma ni saa 10 jioni, nilihisi lazima Asmah atakuwa ofisini muda huu, nikaelekea moja kwa moja mpaka ofisini kwake.

Baada ya kufika nilipark gari parking ya nje kabisa na nikaingia ndani, nilikuwa niko spidi sana hata mapokezi sikusalimia. Nilimkuta Asmah yuko ofisini na moja ya mfanyakazi mwenzie na baada ya kuniona alisimama na kuja usawa wangu.

“Insider are you okay?.”

Sikutaka hata kuongea naye, nilimshika mkono na kuanza kuondoka naye pale ofisini, hata jamaa aliyekuwa naye alibaki akishangaa, kilikuwa ni kitendo cha haraka sana. ‘In a blink of an eye’.

Asmah alianza kulalamika pale,

“Wait, where are you taking me?”

Sikuwa hata nikimsikiliza muda huu, tulipofika nje ya geti nikampa ishara aingie ndani ya gari na akafanya hivyo, hata yeye alikuwa mpole na alianza kuogopa. Mlinzi alishuhudia lile tukio, lakini hakutaka kuingilia maana ananijua vizuri sana, hivyo alikuwa mpole.

Baada ya kuingia ndani ya gari tulianza kuangaliana na Asmah alionekana kuwa na wasiwasi sana;

MIMI: “Unajua kosa lako ni nini?”

ASMAH: “Insider, sikujua kama Iryn atapokea.”

Na nilimkatisha maongezi yake;

MIMI: “Umeniletea matatizo kwa mama kijacho wangu, unapiga simu wakati unajua fika naishi naye kwasasa na nilikupa taarifa mapema kuwa nitakucheki.”

ASMAH: “Insider, I’m really sorry, lakini haya yote wewe ndo sababu kaa ukijua hilo.”

MIMI: “Unamaanisha nini?”

ASMAH: “Umenichunia sana hadi najisikia vibaya, pale napokukumbuka.”

MIMI: “Mimi sijakuchunia kama unavyosema, ila nilikwambia kwasasa niache nifocus na maisha yangu. Kila siku nagombana na Iryn, juu yako, kwasasa sitaki haya yatokee ndomana nikakwambia vile. Pia, tambua natamani sana upate mwanaume atakayekupenda na kukuoa.”

ASMAH: “Stage niliyofikia, kukaa mbali na wewe ni ngumu. Insider nimekuzoea sana ujue, nawezaje kukaa mbali na wewe kwa yote uliyonifanyia?. Umejitoa sana kwangu, kipindi kile nimepata ajali, bado umenisaidia mambo mengi sana, najiona nina deni kwako.”

MIMI: “Huna haja ya kuwa na deni, sababu nilifanya toka moyoni na sihitaji unilipe. Asmah naomba utambue kwamba nakupenda sana, asingekuwa Iryn, huenda tungekuwa wapenzi na asingekuwa mama J, ningekuweka ndani kabisa.”

ASMAH: “Unataka kusema nini?.”

MIMI: “Upendo niliokuwa nao kwako, kwasasa umehamia kwa Iryn. Na sitaki kumpoteza kisa wewe, naomba uheshimu hili, yule ni mke wangu tayari na nitarajia kupata mtoto soon.”

ASMAH: “Hongera sana kwa kutarajia kupata mtoto soon.”

MIMI: “Please, move on kwa usalama wangu na wa kwako pia, tutaendelea kushirikiana kwenye mambo mengine, lakini tuwe na mipaka. Kwa mara ya kwanza leo Iryn, amepaniki live na ametoa maneno makali juu yako.”

ASMAH: “Hata mimi nimeogopa sana, kwa mara ya kwanza nazifeel hasira zake, na sikutoa neno lolote baya.”

MIMI: “Wasiwasi wake, mimi na wewe tuko kwenye mahusiano ya siri, kipindi hiki cha ujauzito amekuwa na wivu sana.”

ASMAH: “Sasa nafanyaje?

MIMI: “Mpigie simu, omba kuonana naye ili muongee juu ya hili, naamini atakubali muonane.”

ASMAH: “Insider mimi naogopa ujue.”

MIMI: “Mpigie simu sahivi, mwambie unataka kukutana naye, ukionana naye atatulia.”

Asmah alitoa simu yake mfukoni na akampigia Iryn, simu iliita bila kupokelewa, akapiga kwa mara ya pili, ndiyo kupokelewa na akamwambia dhumuni lake ni kuonana ili waongee na Iryn alimkubalia, akasema anamtumia location.

ASMAH: “Mimi naogopa siwezi kwenda.”

MIMI: “Sasa unaogopa nini?, nenda kajisafishe na unisafishe na mimi. Usikubali kitu chochote kile atakachokuuliza, wewe ni mtu mzima utajua utaongea nini.”

ASMAH: “What if kama anaushahidi kwamba we had sex.?”

MIMI: “I don’t think so, nafikiri kuna mtu kamjaza haya maneno, Iryn hana ushahidi juu ya hili.”

ASMAH: “Unajuaje kama hana evidence? Na ameongea vile mbele yangu.”

MIMI: “I know her, ingekuwa kweli anazo mimi ningejua tu, Asmah niamini mimi. You have to clean up the mess for me.”

ASMAH: “Sawa acha niende, kama kuna lolote nitakupigia simu.”

MIMI: “Nipigie kwa namba hii kama utapata shida, nitakuwa around.”

Baada ya kuachana na Asmah nilienda Cocobeach- Wavuvi kempu kutulia. Niliagiza heineken zangu mbili huku namsubiri Asmah. Muda huu nilitumia kuchat na Cami, nilimuuliza kuhusu maendeleo ya Iryn ana akasema yuko sawa, japo alilia sana. Nilimuuliza Iryn anafanya nini kwasasa, akasema amekaa kwa balconi na yuko na mgeni, nikajua ni Asmah wala si mwingine.

Kwa upande mwingine, Cami aliendelea kuniuliza shida ni nini, kwani hata Iryn hakuwa amemwambia sababu halisi ya ugomvi wetu. Nilimwambia aendelee kuwa mpole, na kwamba Iryn mwenyewe atamwambia tu chanzo cha ugomvi wetu.

Iryn ni mmoja wa wanawake ambao hawapendi kuweka maisha yao public, ni mtu ambaye anajali sana faragha ya mambo yetu ya ndani na hataki kuyaeleza kwa watu wengine. Hata kitendo kile cha kumpiga kule hotelin kilibaki kuwa siri yake pekee, hakuna mtu yeyote aliyemwambia kuhusu hilo.

Baada ya masaa mawili kupita na hakuna dalili za Asmah kunicheki, nilianza kuingiwa na wasiwasi. Nilijiuliza kwa nini anachelewa kutoka na nini kinaendelea?. Nilijaribu kufikiria kuhusu kumtumia ujumbe, lakini nikaona kwamba ilikuwa ni wazo baya.

Baada ya nusu saa, Asmah alipiga simu na kuniuliza nilipo. Nikamwambia aje Cocobeach tukutane. Ndani ya muda mfupi alifika Cocobeach na alisema yuko karibu na chupa ya Cocacola akinisubiri.

Nilitoka pale Wavuvi, nikamchukua Asmah, na nikaendesha gari kwa kasi hadi karibu na mitaa ya restaurant ya ‘Amigos’. Huko ndipo nilipokipaki gari na kuanza mazungumzo.

MIMI: “Nipe mrejesho wa mlichozungumza na mama kijacho.”

ASMAH: “Kila kitu kipo sawa kwasasa, nimeongea naye muda mrefu sana na amenielewa. Nimesema ukweli kwamba mimi na wewe tulikuwa kwenye mahusiano zamani wakati tumefahamiana, lakini tuliachana na kwasasa sisi ni marafiki.”

MIMI: “Una uhakika amekuelewa?”

ASMAH: “Trust me japo nimebanwa sana, juu yako. Alisema yeye yuko tayari kutuacha tuendelee na mahusiano, huenda yeye ndiye amedandia treni la watu. Nimemwambia Insider anakupenda sana na hayuko tayari kukupoteza na kila siku anajidai utamzalia mtoto wa kike.”

MIMI: “Umefanya jambo la muhimu sana, ahsante.”

ASMAH: “Nimekubali matokeo, japo nilikupenda sana naomba uendelee na Iryn, kwa heshima na wadhifa wake.

MIMI: “Leo ndo unakiri kuwa unanipenda sana?.”

ASMAH: “Ni kweli, kipindi umeanza mahusiano na Iryn nilikuwa naumia sana hujui tu.”

Simu yangu ilianza kuita na kuangalia ni Iryn alikuwa anapiga simu, nilimuonesha Asmah kuwa Iryn anapiga, naye akasema nipokee haraka. Baada ya kupokea aliniuliza niliko, nikamwambia niko Cocobeach, akasema nirudi home mapema.

Ilikuwa ni saa mbili usiku tayari, hivyo sikutaka kupoteza muda na nilimuaga Asmah kwa kumpa ahadi ya kuonana naye hivi karibuni na nikaondoka kurudi home.

Nilitumia muda mfupi sana kufika, kuingia ndani nawaona wamekaa sebleni, nami nikaketi pembeni ya mama kijacho. Wakati huu
Claire alikuwa akitabamu, kana kwamba kuna kitu anataka kuongea. Haikuchukua muda na aliaga anaondoka kurudi kwake, maana alikuwa na majukumu mengine ya kufanya.

Nilimpa kampani mpaka kwake na tukiwa njiani tulikuwa tunaongea na kubwa alisema, Iryn hajasema chanzo cha ugomvi wetu. Pia, aliendelea kusisitiza kwamba Iryn ananipenda sana. Baada ya kufika kwake, nilimshukuru sana kwa msaada wake na tukaagana pale, nami nikageuza kurudi home.

Baada ya kufika, Iryn alikuwa amekaa kwa balconi, hivyo nilienda na nikakaa pembeni yake. Palikuwa na hewa safi na upepo wa bahari ukipiga eneo hili kwa utulivu sana. Tulianza kuangaliana pale, nami niliamua kuvunja ukimya;

MIMI: “Nambie mke wangu, upo tayari tuongee?”

IRYN: “I’m listening.”

MIMI: “Mummy, mimi na Asmah hatuko kwenye mahusiano naku-apia kwa hili. Usipende kusikiliza maneno ya wabongo, hakuna anayependa kuona mimi niko na mwanamke mrembo kama wewe.”

IRYN: “Lazima niwe na maswali, kwanini Asmah tu, akupigie simu nonstop?. Mchana kabla ya kwenda lunch, alipiga simu mara 3 na bado akatuma message akilalamika sana kuwa unamtenga. Kwa haya yaliyotokea, na ninajua fika wewe na Asmah mlikuwa na historia unafikiri nitawaza nini?.”

MIMI: “Nakwambia ukweli, lastweek niliongea na Asmah akae mbali na mimi, na haya yote ni kwasababu yako, sikutaka uendelee kuwa na wasiwasi juu ya ukaribu wetu.

Ilibidi nimueleze ukweli kuhusu mipango yangu juu ya Asmah, ili aweze kuelewa na sikuona haja kumficha juu ya hili.

IRYN: “Unajielezea sana, nimekuelewa tuachane na haya.”

MIMI: “Baby, I don’t want another woman, and I”ll never disrepect you or my daughter like that.”

IRYN: “Unakumbuka tulikubaliana kwamba mtoto akiwa wa kike jina utampa wewe?”

MIMI: “Yes! Darling, unataka nikutajie jina kabisa?”

IRYN: “Don’t tell me hujaandaa jina bado.”

MIMI: “Niliandaa mummy, from today nitakuita ‘mama Ariana’, do you like the baby’s name?”

IRYN: “Yeah, it’s a beautiful name, and I like it. Thank you baba Aria.”

Furaha yetu ilirudi kama zamani na nilimwambia tuende chumbani tukalale maana muda ulikuwa umeyoyoma tayari.

Saa nne asubuhi nilitoka kwenda Mikocheni kuonana na Lucy, pia nilitamani sana tumalize tofauti zetu. Nilipofika pale ofisini niliweza kuonana na Lucy, bila kupoteza muda nilianza kumuomba radhi kwa kumkosea.

Lucy kwa upande wake alisema, aliumia sana kwa kitendo cha mimi kwenda Dodoma bila kumuaga wala kumtafuta, halafu nikawa nawasialiana na Hilda kwa siri, hiki ndo kilimuuma sana. Lucy, aliendelea kusema kwamba hakutegemea mimi ningemfanyia vile, ukizingatia sisi ni washikaji wa muda mrefu sana.

Ukweli nilikuwa nimemkosea sana, hivyo niliendelea kumuomba radhi na baada ya kumuelekeza sana dhumuni la mimi kufanya vile, hapa ndiyo aliweza kunielewa na kunisamehe.

Tulianza kuongea masuala mengine kwa ujumla na kubwa lilikuwa sakata la Asmah. Alinisisitiza sana kama nina mahusiano ya siri na Asmah, bhasi niache mara moja, kwani Iryn alimpigia simu na kulalamika kwamba anahisi kuna jambo linaendelea kati yangu na Asmah.

Baadae tulianza kuongea masuala ya ofisi maana landlord alikuwa ameanza kusumbua tuondoke, kwani alitoa taarifa mapema.

MIMI: “Iryn kaniachia hili suala nifanye maamuzi, wewe ndo manager wa hapa, unashaurije.?”

LUCY: “Hii location ilikuwa nzuri sana na imekaa kimkakati, tunapata wapi tena eneo zuri kama hili?”

MIMI: “Wateja wako wanaokuja hapa ni loyal customers?.”

LUCY: “Ndiyo na wageni wanakuja wengi sana.”

MIMI: “Nimewaza sana asubuhi nikaona ni bora ofisi ihamie Masaki. Tutaepusha cost nyingi sana, pia Masaki hatulipi pango bado pana nafasi kubwa ya kutosha.”

LUCY: “Kumbuka Mikocheni, tulitarget na wale wa kipato cha kati, tukihamia Masaki si tutawakosa hawa customers.?”

MIMI: “Bei zitabaki kuwa zilezile, na sikuzote mteja anafuata huduma bora, ukiwaambia tumehamia Masaki watakuja tu. Halafu, ijumaa tutakuwa na kikao asubuhi, fikiria hili vizuri na kesho unipe majibu ili tufanye maamuzi mapema.”

LUCY: “Sawa bossy, nipe muda nijifikirie juu ya hili.”

Baada ya maongezi marefu na Lucy, nilimuacha aendelee na majukumu yake huku mimi nikiendelea kukagua ofisi kwa ujumla.

Nilipigiwa simu na mama wawili, na wakati nilipoipokea, sauti ya Pili ilisikika. Alinisalimia na kusema kwamba nimewatenga sana, tofauti na zamani. Maneno haya yaliniuma sana, hivyo nikamuuliza yuko wapi. Alisema yupo ofisini kwa mama yake, na nikamwambia nitakuwa hapo baada ya lisaa.

Baada ya kumaliza ukaguzi, nilimuaga Lucy kisha nikaondoka kwenda ofisini kwa mama wawili. Nilipowapa taarifa kwamba nimefika, walikuja haraka, na Pili alinikumbatia mara tu alipoona.

Tulianza mazungumzo na mama wawili, ambapo habari kuu ilikuwa kuhusu mpango wa binti yake kusoma nje. Nilimuuliza Pili kama anaridhia kusoma nje, na alithibitisha. Baada ya hapo, nilimuomba Pili atupishe ili niweze kuzungumza na mama yake kwa faragha.

Mama wawili alifurahi sana kuniona na aliniuliza kuhusu agenda yangu Dodoma. Nikamwambia project nayoifanya kule na alinipongeza kwa hatua hii, kisha tukandelea na mazungumzo mengine kwa muda mrefu. Baada ya mazungumzo, niliomba niondoke na Pili na kumrudisha baadaye. Mama wawili hakuwa na tatizo na ombi hilo na aliniruhusu.

Niliondoka na Pili kwenda Mlimani na lengo langu lilikuwa kutimiza ahadi ya kumpa zawadi ya simu niliyomuahidi baada ya kumaliza shule. Pale Mlimani, nilionana na jamaa yangu, nikamwambia anipe bei ya iPhone 12, kisha nikampa nafasi Pili achague rangi ya simu anayoipenda. Ilikuwa ni surprise ambayo Pili hakutegemea, na alifurahi sana. Baada ya hapo, tukaenda kula pizza pamoja.

Jioni, nilimrudisha Pili kwa mama yake ofisini, ambapo mama wawili alifurahi sana na kunishukuru kwa zawadi niliyompa Pili. Baada ya hapo, nikaondoka kuelekea Masaki kuonana na Hilda ili nimpe taarifa kuhusu kikao kilichopangwa ijumaa.

Nilimshirikisha Hilda kuhusu mpango wa kufunga branch ya Mikocheni na kuwaleta Masaki, na yeye alikubaliana na wazo hili na kusema ni zuri. Nilimpa taarifa za kikao kilichopangwa na nikamwambia aandae ripoti zake vizuri ili aweze kujibu maswali pindi atakapoulizwa.

Muda ulikuwa umeenda, hivyo nikarudi nyumbani ili niwahi kumpikia mama kijacho. Mara tu baada ya kufika, aliniambia ana hamu ya kula chips na yai. Hapo hapo nikatoa simu na kumpigia Sele ili aandae sahani mbili na firigisi. Nikamuaga naenda kuzifuata, lakini akasema tuende wote, kwani amechoka kukaa ndani peke yake, hivyo tukaondoka kwenda kwa Sele.

Sele alishangaa sana kumuona Iryn akiwa mjamzito tena mimba kubwa, na alisema tuingie ndani tukae tusubiri kwani chips ziko jikoni. Iryn kwa upande wake, alisema anakulia palepale na aliagiza atengenezewe zingine za kuondoka nazo.

Baada ya Iryn kuingia ndani, nilibaki nikipiga story na sele;

SELE: “We mhuni unabalaa hujataka kuchelewesha, umemjaza upepo mrembo.”

MIMI: “Hata ile siku nakuuliza mahindi, yeye ndo alihitaji.”

SELE: “Bossy umetisha sana, unakojolea pazuri sana. Mwanamke kama huyu unapataje nguvu ya kuchepuka?.”

Tuliishia kucheka nami, nikaingia ndani kwa mama kijacho wangu ili tule.

Baada ya kumaliza kula, nilimlipa Sele pesa yake na alikata sahani mbili tu, moja alitoa offa kwa mama kijacho wangu, Iryn alifurahi na tukaondoka maeneo haya.

Baada ya kurudi nyumbani, Iryn alikwenda kulala, nami nilitumia nafasi hiyo kuwasiliana na Mary. Nilitamani kujua mpango wake wa kurudi Dar, na alisema kwamba anarudi kesho, Jumatano, pamoja na Jane. Alitamani sana tungeonana, lakini nilimkatalia na kumwambia avumilie hadi Jumamosi, kwani Iryn ataondoka hiyo siku.

PART B

Siku ya Alhamisi ile asubuhi, Iryn alinipa taarifa kuhusu ujio wa dada yake kutoka Ethiopia na alisema ataingia usiku sana. Nilimuuliza atafikia wapi? Akasema anafanya mpango ili afikie Sea cliff hotel.

Saa tano asubuhi, aliniaga kuwa anakwenda kwa mama Janeth kuonana na Jessie, hivyo nilimpa kampani ya ride hadi kwa mama, kisha nikaondoka kuelekea ofisini.

Nilikuwa nakazi ya kukagua hesabu za mauzo vizuri, kwani ni muda mrefu ulikuwa umepita pasipo kufanya ukaguzi. Niliweza kubaini matatizo madogo ambayo ambayo Hilda aliweza kuyajibia, hivyo nikaendelea kupitia ripoti na kuzicompile.

Saa 10 jioni, nilipigiwa simu na Iryn, kisha akaomba niende Mikocheni na alimpa simu jamaa ili anielekeze. Jamaa kunielekeza yalikuwa ni maeneo ya karibu na Shopperz, hivyo bila kupoteza muda niliondoka kuelekea huko.

Ndani ya muda mfupi nilikuwa nimewasili na jamaa alinielekeza hadi napark gari kwenye moja ya showroom ya magari. Sasa, baada ya kushuka ndiyo namuona Iryn na Jessie wamekaa na nikatembea mpaka usawa wao nikawasalimia.

Muda huu Jessie alikuwa ananiangalia tu, namimi nilikuwa namzingua pale;

IRYN: “Darling, follow me.”

Nilimfuata kwa nyuma, hadi ilikokuwa imepark Marcedes Benz.

IRYN: “Darling, hii gari ni nzuri? Unaionaje?”

MIMI: “Ni nzuri sana, halafu hii colour naona unique kwa benz.”

IRYN: “Mimi na Jessie wote tumeipenda.”

Alimuita jamaa ambaye ana asili ya uarabu na akamwambia aiotoe nje ili tuondoke nayo, na palepale aliomba account namba ili afanye malipo. Mimi nilikuwa sijui kinachoendelea kwakweli, nilihisi moja kwa moja gari ni ya Jessie.

Benz ilitolewa showroom mpaka nje kwaajili ya kuondoka, gari ilikuwa ni nzuri ikivutia sana. Aliniita akasema niache taarifa zangu kwaajili ya usajili, hapa sasa ndo nikahisi gari itakuwa yangu.

Sikutaka kubisha na nikafanya kama alivyosema. Jamaa aliahidi kwamba kesho kufikia saa 4 asubuhi kila kitu kitakuwa sawa, hivyo tukachukue plate namba. Baada ya malipo kufanyika, tuliondoka na Jessie akaondoka na ile Audi, wakati sisi tukaondoka na ile Benz. Uvumilivu ulinishinda na nikaanza kuuliza maswali;

MIMI: “Baby, bado sijui kinachoendelea kuhusu hii gari.”

IRYN: “Mimi kama MD, ofisi imekununulia gari ili iwe inakusaidia kwenye majukumu yako pamoja na ya ofisi.”

Niliishiwa hata niseme nini maana sikutarajia kuona Iryn akinifanyia surprise kama hii. Nilikuwa bado siamini kama kweli hii benz nayoendesha kweli ni yangu.

MIMI: “Baby nashukuru sana, hata sijui niseme nini kwahaya yote unayonifanyia. May God bless you.”

IRYN: “Kampuni ina imani kubwa sana na wewe, na hii ni moja ya shukrani yangu. Mimi bado sijakupa zawadi, ila nitaanza kwanza na nyumba mengine yatafuata.”

Tulienda mpaka kwenye apartment yetu, tukapark ile gari, kisha tukaondoka tena na Jessie kumrudisha kwa mama. Baada ya kurudi nilianza kuiangalia ile Benz kwa mara nyingine tena, jinsi ilivyo nzuri na kuvutia, na niliishia kutabasamu.

Kesho yake, ijumaa tulikutana kwaajili ya kikao kifupi ambacho kilihusisha viongozi tu, na tulifanyia pale Giraffe hotel, Mbezi Beach. Kikao kilianza saa 4 kamili asubuhi na kilihusisha watu sita tu, pamoja na Iryn.

Iryn alishukuru sana uongozi wa kampuni kwa kujitoa katika kipindi kigumu, hasa wakati ambapo hatukuwa na mawasiliano. Kama MD, aliahidi kuongeza mshahara kwa 30% kwa viongozi kutokana na kazi nzuri waliyofanya. Hakuishia hapo, aliongeza kuwa baada ya kikao, atatoa zawadi kwa wote.

Baada ya bossy kuongea, nilisimama kutoa taarifa ya mwenendo wa kampuni pamoja na kuifunga branch ya Mikocheni. Lucy na Hilda, walikuwa wanajua kinachoendelea kasoro wengine walikuwa hawajui, hivyo walibaki wakishangaa baada ya kuzisikia taarifa hizi;

IRYN: “Why? I didn’t expect you would come up with this bad idea.”

Nilianza kuwaeleza sababu ya kufanya maamuzi haya;

MIMI: “Tumejadili suala hili kwa undani pamoja na Hilda na Lucy. Tumeona kuwa gharama tunazolipa kwa pango ni kubwa sana, na kuongezeka kwa gharama za umeme, maji, vibali vya leseni na mamlaka nyingine ni mzigo mkubwa. Badala ya kutafuta ofisi mpya, ni bora wateja wetu wa Mikocheni waje Masaki. Hii itatusaidia kupunguza gharama nyingi na kuongeza faida kubwa. Kwa hivyo, tunataka ufahamu kuwa maamuzi haya tumeyachunguza kwa makini na hatuja kurupuka."

Baada ya kuwapa sababu ya kuifunga ofisi ya Mikocheni, kila mtu alinyamaza kimya akifikiria maana ni sababu ambayo ilimake sense vichwani mwao na baada ya dakika kupita, Iryn alianza kuongea.

IRYN: “Mnashaurije juu ya hili, lengo tupate maamuzi sahihi, kila mtu ajaribu ku-assess risks kabla ya kukubali haya maamuzi.”

Baada ya majadiliano ya dakika 20, kila mtu aliunga mkono wazo langu la kuhamishia branch Masaki. Bossy akatoa maelekezo tuanze taratibu mapema ili tusigombane na mwenye nyumba.

Ni kikao kilicho chukua masaa 2 na baada ya kumaliza, tulipata lunch ya pamoja bila kusahu kupiga picha za ukumbusho, nami nilitumia nafasi hii kupiga picha na mama kijacho wangu, kama ukumbusho wa ujauzito wake.

Baada ya kumaliza kila kitu, tuliwaaga na kuelekea Sea cliff hotel kuonana na dada yake ambaye aliingia Dar usiku sana, akitokea Ethiopia.

Tulipofika hotelini, tulimsubiri pale reception na haikuchukua muda alitoka na wakaishia kukumbatiana na Iryn. Dada yake yuko vizuri pia, sio wa kitoto ni mzuri kwelikweli, ila bado hafiki kwa Iryn.

IRYN: “This is Insider, my boyfriend. Do you recognise him?”

VIVIAN: “Of course I do. How are you, brother-in-law?”

MIMI: “I’m fine and happy to see you again."

Mkononi, Viviani alikuwa ameshika kimfuko kidogo na alimpa Iryn, naye akanikabidhi mimi na alinikonyeza, ile kuangalia ndani kuna nini, naona si simu, nikavunga.

Baada ya maongezi mafupi, tuliongozana mpaka parking ili tuondoke, njiani macho yote yalikuwa kwetu. Kwanza niliona ufahari sana kuongozana na wanawake warembo duniani, ni wanaume wachache sana wenye bahati kama hii.

Kwa upande mwingine Sister yangu alinipa taarifa kwamba yuko Airport na anatarajia kuingia Dar, jioni. Nilimpa taarifa Iryn na alisema tufanye booking ya room palepale Sea cliff hotel mapema.

Saa 10 jioni, tuliondoka kwenda JNIA kumpokea dada yangu. Iryn aligoma kabisa kubaki nyumbani na Vivian, alisema haitakuwa vizuri ikiwa nitakwenda peke yangu kumpokea dada yangu wakati yeye yupo

Baada ya kufika JNIA, tulikaa sehemu ya kusubiri abiria. Kama ilivyo kawaida, kila mtu aligeuka kumtizama Iryn kutokana na uzuri wake wa kipekee. Alikuwa kivutio maalum pale, akiwa na mimba yake.

Ndani ya nusu saa, sister aliwasili na waliishia kukumbatiana na wifi yake kisha tukapotea eneo hili. Tulianza kwanza kupitia Sea cliff hotel, ambapo tuliacha mabag yake, kisha tukaelekea home.

Apartment ilikuwa imechangamka sana maana walikuwa wanawake watatu wakipiga story, huku wakicheka. Mimi niliamua kuwapa space na nilienda kutulia chumbani nikipanga mambo yangu.

Nilitoa ile simu kwenye mfuko na ilikuwa ni Iphone 14 kama ileile aliyoivunja hadi rangi na niliweka laini yangu. Nilimpigia simu mama J kumpa taarifa kwamba kesho nitarudi, lakini ni kama aliipokea hii taarifa kwa kutojali.

Wakati huu, nilipata ujumbe kutoka kwa Asmah ambao ulisomeka anataka kuacha kazi, ilikuwa ni taarifa mbaya kwangu, hivyo nikampandia hewani. Nilimuuliza kwanini anataka kuacha kazi, akasema yeye ameamua hivyo kwani anataka kurudi shule kusoma. Nilifunga mazungumzo kwa kumpa ahadi ya kuonana kesho ili tuzungumze vizuri kuhusu suala hili, kwani ilikuwa ni ghafla sana.

Saa 2 usiku, tulitoka kwenda kupata dinner ya pamoja pale Karambezi Café. Wao waliendelea kuzungumza, na story zao nyingi zilikuwa zinahusu leba, wakati mimi nilikuwa nasikiliza kwa sikio la kuiba huku nikijifanya nipo bize na simu

Wakati naongea na dada yangu, nilimshukuru sana kwa kujitoa kwake na kukubali kwenda South Africa. Baada ya masaa mawili kupita, tuliagana ili wajiandae mapema kwa ajili ya safari ya kesho. Walielekea hotelini na sisi tukaelekea kwenye apartment yetu.

Usiku ulikuwa mrefu sana kwani nilikuwa nakazi ya mwisho kuhakikisha barabara inakuwa safi kwaajili ya mtoto kupita. Baada ya kazi ya muda mrefu, japo niliichafua sana, lakini mama kijacho aliridhika na kazi yangu na tukalala.

Asubuhi na mapema nilimuamsha ili tujiandae kwaajili ya safari. Baada ya hapo tuliondoka kuelekea Sea cliff hotel, ambapo tuliwachukua akina sister na tukaelekea Airport. Baada ya kuwasili pale JNIA tulipiga tena picha za mwisho kama ukumbusho, kisha tukachoma ndani.

Nilianza maongezi deep na Iryn na kubwa nilimtakia kila la kheri katika kuanza safari yake mpya ya kuwa mama na nilimpa ahadi ya kwenda South Africa kujumuika naye.

IRYN: “Baba Aria, nakupenda sana na naomba uheshimu hili. Kama nilivyokuahidi before, sitoweza kuwa na mwanaume mwingine zaidi yako, napenda sana nikuzalie mtoto mwingine baada ya huyu.”

Nilipenda sana kusikia akiniita Baba Aria na nilimshika mkono wake nikauweka pajani;

MIMI: “Wewe ni mke wangu tayari, nitaangalia namna ya kuwaoa wote, kuhusu watoto hata ukitaka dozen kwangu ni kazi ndogo.”

IRYN: “Promise me unakuja lini South?”

MIMI: “Mama Aria, ninaomba kwanza nikae na familia yangu, nime-mmiss sana mwanao Junior na mama J. Nitakuja before hujajifungua natamani niwe na wewe leba hadi unajifungua.”

Iryn alifurahi sana kusikia maneno matamu kutoka kwangu na tuliagana kwa kukumbatiana maana muda wa kucheck-in ulikuwa umewadia. Niliwaaga akina sister pamoja na Viviani na niliwaambia nitawaona soon, na kabla ya kuondoka Iryn alinikumbatia kwa mara nyingine tena.

Niliondoka pale JNIA nikiwa na furaha sana, na niliwasha gari kuondoka kurudi Masaki.

Baada ya kufika kwa apartment nilipark vizuri gari, Audi maana nilikuwa naiacha pale, kisha niliingia ndani kuchukua bag, pamoja na funguo za benz yangu, nikaanza safari ya kwenda home, Mbezi Beach.

Katika maisha yangu, hakuna siku niliwaza kama nitakuja kumiliki benz, lakini ndoto yangu ilitimia kwa kuendesha benzi kali. Barabarani nilikuwa mdogo mdogo sana, kama vile namuendesha bibi harusi. Baada ya kufika home, nilimpigia simu Elena akatoka kunifungulia gate.

Junior alikuwa amesimama kibarazani akishangaa gari, kwani anapenda sana magari na baada ya kuniona baba yake, alikuja spidi nikamnyanyua juu. Na alianza kulilia aingie ndani ya gari, bhasi nilimfungulia mlango akaanza kunyonga steering.

Kwa upande mwingine, nilishtuka kuona gari yangu nyingine siioni na baada ya kuuliza, Elena alisema mama J kaondoka nayo. Niliuliza kwani anajua kuendesha? Akanijibu ndio ni mwezi sasa anaiendesha, nilibaki nikishangaa.

Nilifurahi kusikia wife amejua kuendesha gari, kwani ilikuwa ni hatua nzuri kwa upande wetu. Nilikuwa nimechoka sana pamoja na usingizi, hivyo nilienda chumbani kulala. Kwa bahati mbaya sikuweza kulala mapema sababu Junior alikuwa akinisumbua sana.

Jioni, baada ya kuamka niligundua kwamba mama J karudi na nilienda seblen kukaa, lakini nilimsikia akiongea na simu huku akicheka kwa mbali. Nilitulia pale seblen nikishangaa TV na zilipita dakika tano, bado mama J anaongea na simu. Nilihisi haya si maongezi ya kawaida na nilisogea mpaka dirishani kusikiliza, maana alikuwa kasimama pale kibarazani.

Na aliendelea kuongea, tena kwa sauti ya chini, haya ni baadhi ya maneno aliyokuwa anajibu;

Ndiyo, najua… ah, nimekumisi sana

Wewe pia unajua jinsi unavyonifanya nijisikie… usijali, nitakutafuta muda"

Tutaonana tena, usijali.


Baada ya kuona amemaliza kuongea na simu, nilirudi chumbani kwa spidi ya kunyata ili asinishtukie. Baada ya dakika 5 alirudi chumbani na nilijifanya nimelala, aliweka simu chaji akaondoka. Niliamka kwa lengo la kuikagua simu yake, kwa bahati mbaya alikuwa kabadilisha passcode, hivyo nikawa sina option nyingine.

Nilipata wazo nikague mkoba wake, na nikaona kuna risiti za Samakisamaki, Elements, KFC na nyinginezo. Nilianza kukagua za KFC zilionesha tarehe ya leo, za Elements zilionesha ni weekend iliyopita, lakini kilicho nishangaza zilionesha zimeprintiwa saa 4 usiku.

Nilibaki najiuliza mama J sio mtu wa marafiki wala kutoka out, huku Samakisamaki, Elements alikuwa na nani?. Huyu mtu waliokuwa wanaongea wote kwenye simu ni nani? Hapa sasa nikahisi kuna SOMETHING FISHY kinaendelea.

ITAENDELEA
Mama J dakika za jioooooooni anapiga come back
 
SEASON 02
CHAPTER 37

BY INSIDERMAN”

PART A

Siku ile nilipokutana na Asmah, nilimwambia kwamba afocus zaidi kwenye maisha yake. Nia yangu haikuwa kumuumiza au kumvunja moyo, bali nilihisi ni muhimu kukaa naye mbali kwa muda ili nirekebishe mambo kati yangu na Iryn. Pia, nilitamani Asmah apate nafasi ya kutafuta mtu ambaye atakuwa sahihi kwake, kwa maisha yake ya mbele.

Tangu siku ile tulipoonana, Asmah amekuwa akinipigia simu mara kwa mara na kuomba tukutane. Hata hivyo, mara zote nimekuwa nikimkatalia kwa visingizio vya kuwa na shughuli nyingi, nikimwambia nitamtafuta baadaye, lakini ukweli ni kwamba sijawahi kufanya hivyo.

Wakati nikiwa Tabora, tuliwasiliana na nikampa ahadi kwamba tutakutana Jumatatu mara tu nitakaporudi Dar ili tuzungumze na tuliweke sawa hili jambo. Niliporudi nyumbani, Asmah alinipigia simu mara nyingi, lakini sikujua kwa wakati huo kuwa alinitafuta sana. Kumbe, mama kijacho alikuwa anaziona simu na ujumbe wake kabla mimi sijapata nafasi ya kuona.

Katika kipindi hiki ambacho Iryn ni mjamzito, nilijitahidi kuepuka ugomvi wowote naye. Simu yangu kubwa mara nyingi nilikuwa namuachia kwa sababu sikuwa na chats zozote zenye utata. Mary, kwa upande mwingine, alikuwa anajua kinachoendelea, na tulikuwa tunawasiliana kwa kutumia namba mpya niliyokuwa natumia nikiwa Dodoma. Pia, Mary alishauri tuendelee kutumia namba hiyo mpya ili Prisca asigundue chochote kinachoendelea kati yetu.

Wakati nikiwa na Iryn pale sebuleni, simu ya Asmah ilipoita tena, Iryn alichoka na hali hiyo na akaamua kuipokea mwenyewe. Alionekana kushindwa kuvumilia zaidi, huku wivu ukiwa unamsumbua.


CONTINUE:

Mimi muda huu sikuwa na uwezo wowote wa kumzuia, hivyo niliamuacha aongee naye na aliweka loud speaker.

IRYN: “Asmah, habari yako.”

Asmah hakutegemea kwamba Iryn angekuwa ndiye anayepokea simu, na ghafla akawa mpole.

ASMAH: “Ooh! Bossy, habari yako.”

IRYN: “I'm good. What's your problem? You have been calling Insider nonstop."

ASMAH: “Alinambia yuko Tabora msibani, nilitaka kujua kama karudi.”

IRYN: “What is really going on between you and Insider? Please tell me the truth."

ASMAH: “Nothing is going on between us. He is one of my closest friends, and I really appreciate that."

IRYN: “Asmah, why are you doing this? I know you’re lying to me. Why are you disrespecting me like that? Fu**cking with my Man, and you know I’m pregnant with his child.”

ASMAH: "I didn't mean what I said."

IRYN: “You know I gave you all my respect, but you still sneak around and sleep with my Man. Usione nimenyamaza kimya, najua kila mchezo mnaocheza. Nilitegemea ungekuwa na heshima zaidi kwangu hasa baada ya mimi kuwa mjamzito, lakini hujali hata kidogo."

ASMAH: “What are you talking about.?”

IRYN: “Are you just pretending not to know what I’m talking about? You’re such a bad bitch, mpuuzi kabisa…..”

Nilipoona Iryn ameanza kupandisha hasira, ilibidi nimtulize na kumnyang’anya simu kwa sababu alikuwa amevuka mipaka. Alisimama kwa hasira, akaibamiza simu yangu kwa nguvu kwenye sakafu, na kisha akaelekea chumbani.

Nilishindwa kuelewa kwa nini Iryn alikuwa na hasira kubwa kiasi hiki, wakati Asmah hakuwa amesema chochote kibaya. Nilipoinama na kujaribu kuokota simu yangu, niligundua kwamba skrini ilikuwa imevunjika, betri ilikuwa imevimba, na sehemu nyingine zilikuwa zimeharibika. Nilimfata chumbani, lakini mlango ulikuwa umefungwa. Nilisikia sauti ya kilio kutoka ndani, na ilikuwa ni kilio cha maumivu makali.

Baby, please fungua mlango.”

Nilianza kugonga mlango pale, lakini hakuonesha dalili za kufungua

Baby, naomba tuongee. Tafadhali fungua mlango, mpenzi wangu."

Bado alibaki kimya na hakuzungumza chochote, aliendelea kulia kwa sauti kubwa. Hali hii ilinisababisha nijisikie vibaya sana, na niliona kama nimemkosea sana.

Niliamua kurudi seating room na kukaa kwenye sofa huku nikitafakari namna ya kutatua hali hii. Niliwaza kwa haraka nikaona ni busara niwe mpole na kumuomba msamaha ili kuepusha matatizo, ukizingatia hali aliyonayo kwasasa hatakiwa kuwa katika hali hii.

Ilipita nusu saa, lakini bado hakuonyesha dalili za kufungua mlango, na hapa nikaingiwa na wasiwasi kwa kuwa nilihisi anaweza kufanya jambo lolote baya. Nilimgongea tena, lakini hakutaka kufungua mlango. Hali hii iliponitatiza zaidi, nikaona ni bora nimtafute Cami kwa msaada, kwani sikuwa na jinsi nyingine ya kumsaidia Iryn.

Kumpata Cami ikawa ni shida maana simu yangu imezingua, nikaanza kuchanganyikiwa maana kuondoka na kumuacha peke yake mle chumbani ni jambo lisingewezekana kwanza ni hatari.

Baada ya kufikiri sana nikakumbuka home ninasimu nyingine ambayo inanamba ya Cami, hivyo nilimpigia simu mama J. Baada ya kumpigia alisema yuko chuo, hivyo ikabidi nimpigie Elena dada wa nyumbani na kumuelekeza.

Ndani ya dakika 5, Elena alinitumia namba ya Cami na bila kuchelewa nikampigia simu;.

MIMI: “Mambo, it’s me Insider.”

CAMI: “Hey! Insider mambo.”

MIMI: “Mambo mabaya shem wangu, naomba uje home haraka, please.”

CAMI: “Kuna nini? Iryn anataka kujifungua?”

MIMI: “Just come, please.”

CAMI: “I will be there soon”

Ndani ya dakika 15 Cami alifika na alikuwa akihema sana kama mtu ambaye alikuwa anakimbizwa, na alianza kuniuliza ni nini kinaendelea?

MIMI: “Claire, Iryn kajifungia ndani chumbani ni lisaa limepita, hataki kufungua mlango.”

CAMI: “Na hii simu vipi mbona imepasuka, mlikuwa mnagombana?”

MIMI: “Hapana, ni hasira zake ndo kaibamiza simu chini.”

CAMI: “Shem niambie ni nini kinaendelea ili nijue namna ya kuongea na Iryn, usinidanganye.”

MIMI: “Sikia Claire, huu sio muda wa kuanza kuulizana kinachoendelea, Iryn amejifungia na lisaa limepita, anaweza fanya jambo baya. Please, naomba unisaidie kuongea naye, ili afungue mlango, mengine tutaongea.”

CAMI: “Iryn, alikuwa analalamika sana, amekumiss, sasa umerudi mmegombana, mapenzi yenu siyawezi asee.”

Tuliongozana hadi mlango wa chumbani, na Cami alianza kumuita Iryn kwa sauti ya upole. Baada ya kusikia sauti ya Cami, Iryn alijibu kwa hasira kwamba hataki kabisa kuniona mimi, na alitaka niondoke maeneo hayo.

CAMI: “Shem wewe ondoka, acha mimi niongee naye, akikaa sawa nitakupigia simu uje.”

Sikutaka kuwa mbishi juu ya hili, hivyo nilichukua funguo ya gari na kuondoka maeneo haya na akili yangu iliniambia nenda kwa Asmah. Saa yangu ilikuwa inasoma ni saa 10 jioni, nilihisi lazima Asmah atakuwa ofisini muda huu, nikaelekea moja kwa moja mpaka ofisini kwake.

Baada ya kufika nilipark gari parking ya nje kabisa na nikaingia ndani, nilikuwa niko spidi sana hata mapokezi sikusalimia. Nilimkuta Asmah yuko ofisini na moja ya mfanyakazi mwenzie na baada ya kuniona alisimama na kuja usawa wangu.

“Insider are you okay?.”

Sikutaka hata kuongea naye, nilimshika mkono na kuanza kuondoka naye pale ofisini, hata jamaa aliyekuwa naye alibaki akishangaa, kilikuwa ni kitendo cha haraka sana. ‘In a blink of an eye’.

Asmah alianza kulalamika pale,

“Wait, where are you taking me?”

Sikuwa hata nikimsikiliza muda huu, tulipofika nje ya geti nikampa ishara aingie ndani ya gari na akafanya hivyo, hata yeye alikuwa mpole na alianza kuogopa. Mlinzi alishuhudia lile tukio, lakini hakutaka kuingilia maana ananijua vizuri sana, hivyo alikuwa mpole.

Baada ya kuingia ndani ya gari tulianza kuangaliana na Asmah alionekana kuwa na wasiwasi sana;

MIMI: “Unajua kosa lako ni nini?”

ASMAH: “Insider, sikujua kama Iryn atapokea.”

Na nilimkatisha maongezi yake;

MIMI: “Umeniletea matatizo kwa mama kijacho wangu, unapiga simu wakati unajua fika naishi naye kwasasa na nilikupa taarifa mapema kuwa nitakucheki.”

ASMAH: “Insider, I’m really sorry, lakini haya yote wewe ndo sababu kaa ukijua hilo.”

MIMI: “Unamaanisha nini?”

ASMAH: “Umenichunia sana hadi najisikia vibaya, pale napokukumbuka.”

MIMI: “Mimi sijakuchunia kama unavyosema, ila nilikwambia kwasasa niache nifocus na maisha yangu. Kila siku nagombana na Iryn, juu yako, kwasasa sitaki haya yatokee ndomana nikakwambia vile. Pia, tambua natamani sana upate mwanaume atakayekupenda na kukuoa.”

ASMAH: “Stage niliyofikia, kukaa mbali na wewe ni ngumu. Insider nimekuzoea sana ujue, nawezaje kukaa mbali na wewe kwa yote uliyonifanyia?. Umejitoa sana kwangu, kipindi kile nimepata ajali, bado umenisaidia mambo mengi sana, najiona nina deni kwako.”

MIMI: “Huna haja ya kuwa na deni, sababu nilifanya toka moyoni na sihitaji unilipe. Asmah naomba utambue kwamba nakupenda sana, asingekuwa Iryn, huenda tungekuwa wapenzi na asingekuwa mama J, ningekuweka ndani kabisa.”

ASMAH: “Unataka kusema nini?.”

MIMI: “Upendo niliokuwa nao kwako, kwasasa umehamia kwa Iryn. Na sitaki kumpoteza kisa wewe, naomba uheshimu hili, yule ni mke wangu tayari na nitarajia kupata mtoto soon.”

ASMAH: “Hongera sana kwa kutarajia kupata mtoto soon.”

MIMI: “Please, move on kwa usalama wangu na wa kwako pia, tutaendelea kushirikiana kwenye mambo mengine, lakini tuwe na mipaka. Kwa mara ya kwanza leo Iryn, amepaniki live na ametoa maneno makali juu yako.”

ASMAH: “Hata mimi nimeogopa sana, kwa mara ya kwanza nazifeel hasira zake, na sikutoa neno lolote baya.”

MIMI: “Wasiwasi wake, mimi na wewe tuko kwenye mahusiano ya siri, kipindi hiki cha ujauzito amekuwa na wivu sana.”

ASMAH: “Sasa nafanyaje?

MIMI: “Mpigie simu, omba kuonana naye ili muongee juu ya hili, naamini atakubali muonane.”

ASMAH: “Insider mimi naogopa ujue.”

MIMI: “Mpigie simu sahivi, mwambie unataka kukutana naye, ukionana naye atatulia.”

Asmah alitoa simu yake mfukoni na akampigia Iryn, simu iliita bila kupokelewa, akapiga kwa mara ya pili, ndiyo kupokelewa na akamwambia dhumuni lake ni kuonana ili waongee na Iryn alimkubalia, akasema anamtumia location.

ASMAH: “Mimi naogopa siwezi kwenda.”

MIMI: “Sasa unaogopa nini?, nenda kajisafishe na unisafishe na mimi. Usikubali kitu chochote kile atakachokuuliza, wewe ni mtu mzima utajua utaongea nini.”

ASMAH: “What if kama anaushahidi kwamba we had sex.?”

MIMI: “I don’t think so, nafikiri kuna mtu kamjaza haya maneno, Iryn hana ushahidi juu ya hili.”

ASMAH: “Unajuaje kama hana evidence? Na ameongea vile mbele yangu.”

MIMI: “I know her, ingekuwa kweli anazo mimi ningejua tu, Asmah niamini mimi. You have to clean up the mess for me.”

ASMAH: “Sawa acha niende, kama kuna lolote nitakupigia simu.”

MIMI: “Nipigie kwa namba hii kama utapata shida, nitakuwa around.”

Baada ya kuachana na Asmah nilienda Cocobeach- Wavuvi kempu kutulia. Niliagiza heineken zangu mbili huku namsubiri Asmah. Muda huu nilitumia kuchat na Cami, nilimuuliza kuhusu maendeleo ya Iryn ana akasema yuko sawa, japo alilia sana. Nilimuuliza Iryn anafanya nini kwasasa, akasema amekaa kwa balconi na yuko na mgeni, nikajua ni Asmah wala si mwingine.

Kwa upande mwingine, Cami aliendelea kuniuliza shida ni nini, kwani hata Iryn hakuwa amemwambia sababu halisi ya ugomvi wetu. Nilimwambia aendelee kuwa mpole, na kwamba Iryn mwenyewe atamwambia tu chanzo cha ugomvi wetu.

Iryn ni mmoja wa wanawake ambao hawapendi kuweka maisha yao public, ni mtu ambaye anajali sana faragha ya mambo yetu ya ndani na hataki kuyaeleza kwa watu wengine. Hata kitendo kile cha kumpiga kule hotelin kilibaki kuwa siri yake pekee, hakuna mtu yeyote aliyemwambia kuhusu hilo.

Baada ya masaa mawili kupita na hakuna dalili za Asmah kunicheki, nilianza kuingiwa na wasiwasi. Nilijiuliza kwa nini anachelewa kutoka na nini kinaendelea?. Nilijaribu kufikiria kuhusu kumtumia ujumbe, lakini nikaona kwamba ilikuwa ni wazo baya.

Baada ya nusu saa, Asmah alipiga simu na kuniuliza nilipo. Nikamwambia aje Cocobeach tukutane. Ndani ya muda mfupi alifika Cocobeach na alisema yuko karibu na chupa ya Cocacola akinisubiri.

Nilitoka pale Wavuvi, nikamchukua Asmah, na nikaendesha gari kwa kasi hadi karibu na mitaa ya restaurant ya ‘Amigos’. Huko ndipo nilipokipaki gari na kuanza mazungumzo.

MIMI: “Nipe mrejesho wa mlichozungumza na mama kijacho.”

ASMAH: “Kila kitu kipo sawa kwasasa, nimeongea naye muda mrefu sana na amenielewa. Nimesema ukweli kwamba mimi na wewe tulikuwa kwenye mahusiano zamani wakati tumefahamiana, lakini tuliachana na kwasasa sisi ni marafiki.”

MIMI: “Una uhakika amekuelewa?”

ASMAH: “Trust me japo nimebanwa sana, juu yako. Alisema yeye yuko tayari kutuacha tuendelee na mahusiano, huenda yeye ndiye amedandia treni la watu. Nimemwambia Insider anakupenda sana na hayuko tayari kukupoteza na kila siku anajidai utamzalia mtoto wa kike.”

MIMI: “Umefanya jambo la muhimu sana, ahsante.”

ASMAH: “Nimekubali matokeo, japo nilikupenda sana naomba uendelee na Iryn, kwa heshima na wadhifa wake.

MIMI: “Leo ndo unakiri kuwa unanipenda sana?.”

ASMAH: “Ni kweli, kipindi umeanza mahusiano na Iryn nilikuwa naumia sana hujui tu.”

Simu yangu ilianza kuita na kuangalia ni Iryn alikuwa anapiga simu, nilimuonesha Asmah kuwa Iryn anapiga, naye akasema nipokee haraka. Baada ya kupokea aliniuliza niliko, nikamwambia niko Cocobeach, akasema nirudi home mapema.

Ilikuwa ni saa mbili usiku tayari, hivyo sikutaka kupoteza muda na nilimuaga Asmah kwa kumpa ahadi ya kuonana naye hivi karibuni na nikaondoka kurudi home.

Nilitumia muda mfupi sana kufika, kuingia ndani nawaona wamekaa sebleni, nami nikaketi pembeni ya mama kijacho. Wakati huu
Claire alikuwa akitabamu, kana kwamba kuna kitu anataka kuongea. Haikuchukua muda na aliaga anaondoka kurudi kwake, maana alikuwa na majukumu mengine ya kufanya.

Nilimpa kampani mpaka kwake na tukiwa njiani tulikuwa tunaongea na kubwa alisema, Iryn hajasema chanzo cha ugomvi wetu. Pia, aliendelea kusisitiza kwamba Iryn ananipenda sana. Baada ya kufika kwake, nilimshukuru sana kwa msaada wake na tukaagana pale, nami nikageuza kurudi home.

Baada ya kufika, Iryn alikuwa amekaa kwa balconi, hivyo nilienda na nikakaa pembeni yake. Palikuwa na hewa safi na upepo wa bahari ukipiga eneo hili kwa utulivu sana. Tulianza kuangaliana pale, nami niliamua kuvunja ukimya;

MIMI: “Nambie mke wangu, upo tayari tuongee?”

IRYN: “I’m listening.”

MIMI: “Mummy, mimi na Asmah hatuko kwenye mahusiano naku-apia kwa hili. Usipende kusikiliza maneno ya wabongo, hakuna anayependa kuona mimi niko na mwanamke mrembo kama wewe.”

IRYN: “Lazima niwe na maswali, kwanini Asmah tu, akupigie simu nonstop?. Mchana kabla ya kwenda lunch, alipiga simu mara 3 na bado akatuma message akilalamika sana kuwa unamtenga. Kwa haya yaliyotokea, na ninajua fika wewe na Asmah mlikuwa na historia unafikiri nitawaza nini?.”

MIMI: “Nakwambia ukweli, lastweek niliongea na Asmah akae mbali na mimi, na haya yote ni kwasababu yako, sikutaka uendelee kuwa na wasiwasi juu ya ukaribu wetu.

Ilibidi nimueleze ukweli kuhusu mipango yangu juu ya Asmah, ili aweze kuelewa na sikuona haja kumficha juu ya hili.

IRYN: “Unajielezea sana, nimekuelewa tuachane na haya.”

MIMI: “Baby, I don’t want another woman, and I”ll never disrepect you or my daughter like that.”

IRYN: “Unakumbuka tulikubaliana kwamba mtoto akiwa wa kike jina utampa wewe?”

MIMI: “Yes! Darling, unataka nikutajie jina kabisa?”

IRYN: “Don’t tell me hujaandaa jina bado.”

MIMI: “Niliandaa mummy, from today nitakuita ‘mama Ariana’, do you like the baby’s name?”

IRYN: “Yeah, it’s a beautiful name, and I like it. Thank you baba Aria.”

Furaha yetu ilirudi kama zamani na nilimwambia tuende chumbani tukalale maana muda ulikuwa umeyoyoma tayari.

Saa nne asubuhi nilitoka kwenda Mikocheni kuonana na Lucy, pia nilitamani sana tumalize tofauti zetu. Nilipofika pale ofisini niliweza kuonana na Lucy, bila kupoteza muda nilianza kumuomba radhi kwa kumkosea.

Lucy kwa upande wake alisema, aliumia sana kwa kitendo cha mimi kwenda Dodoma bila kumuaga wala kumtafuta, halafu nikawa nawasialiana na Hilda kwa siri, hiki ndo kilimuuma sana. Lucy, aliendelea kusema kwamba hakutegemea mimi ningemfanyia vile, ukizingatia sisi ni washikaji wa muda mrefu sana.

Ukweli nilikuwa nimemkosea sana, hivyo niliendelea kumuomba radhi na baada ya kumuelekeza sana dhumuni la mimi kufanya vile, hapa ndiyo aliweza kunielewa na kunisamehe.

Tulianza kuongea masuala mengine kwa ujumla na kubwa lilikuwa sakata la Asmah. Alinisisitiza sana kama nina mahusiano ya siri na Asmah, bhasi niache mara moja, kwani Iryn alimpigia simu na kulalamika kwamba anahisi kuna jambo linaendelea kati yangu na Asmah.

Baadae tulianza kuongea masuala ya ofisi maana landlord alikuwa ameanza kusumbua tuondoke, kwani alitoa taarifa mapema.

MIMI: “Iryn kaniachia hili suala nifanye maamuzi, wewe ndo manager wa hapa, unashaurije.?”

LUCY: “Hii location ilikuwa nzuri sana na imekaa kimkakati, tunapata wapi tena eneo zuri kama hili?”

MIMI: “Wateja wako wanaokuja hapa ni loyal customers?.”

LUCY: “Ndiyo na wageni wanakuja wengi sana.”

MIMI: “Nimewaza sana asubuhi nikaona ni bora ofisi ihamie Masaki. Tutaepusha cost nyingi sana, pia Masaki hatulipi pango bado pana nafasi kubwa ya kutosha.”

LUCY: “Kumbuka Mikocheni, tulitarget na wale wa kipato cha kati, tukihamia Masaki si tutawakosa hawa customers.?”

MIMI: “Bei zitabaki kuwa zilezile, na sikuzote mteja anafuata huduma bora, ukiwaambia tumehamia Masaki watakuja tu. Halafu, ijumaa tutakuwa na kikao asubuhi, fikiria hili vizuri na kesho unipe majibu ili tufanye maamuzi mapema.”

LUCY: “Sawa bossy, nipe muda nijifikirie juu ya hili.”

Baada ya maongezi marefu na Lucy, nilimuacha aendelee na majukumu yake huku mimi nikiendelea kukagua ofisi kwa ujumla.

Nilipigiwa simu na mama wawili, na wakati nilipoipokea, sauti ya Pili ilisikika. Alinisalimia na kusema kwamba nimewatenga sana, tofauti na zamani. Maneno haya yaliniuma sana, hivyo nikamuuliza yuko wapi. Alisema yupo ofisini kwa mama yake, na nikamwambia nitakuwa hapo baada ya lisaa.

Baada ya kumaliza ukaguzi, nilimuaga Lucy kisha nikaondoka kwenda ofisini kwa mama wawili. Nilipowapa taarifa kwamba nimefika, walikuja haraka, na Pili alinikumbatia mara tu alipoona.

Tulianza mazungumzo na mama wawili, ambapo habari kuu ilikuwa kuhusu mpango wa binti yake kusoma nje. Nilimuuliza Pili kama anaridhia kusoma nje, na alithibitisha. Baada ya hapo, nilimuomba Pili atupishe ili niweze kuzungumza na mama yake kwa faragha.

Mama wawili alifurahi sana kuniona na aliniuliza kuhusu agenda yangu Dodoma. Nikamwambia project nayoifanya kule na alinipongeza kwa hatua hii, kisha tukandelea na mazungumzo mengine kwa muda mrefu. Baada ya mazungumzo, niliomba niondoke na Pili na kumrudisha baadaye. Mama wawili hakuwa na tatizo na ombi hilo na aliniruhusu.

Niliondoka na Pili kwenda Mlimani na lengo langu lilikuwa kutimiza ahadi ya kumpa zawadi ya simu niliyomuahidi baada ya kumaliza shule. Pale Mlimani, nilionana na jamaa yangu, nikamwambia anipe bei ya iPhone 12, kisha nikampa nafasi Pili achague rangi ya simu anayoipenda. Ilikuwa ni surprise ambayo Pili hakutegemea, na alifurahi sana. Baada ya hapo, tukaenda kula pizza pamoja.

Jioni, nilimrudisha Pili kwa mama yake ofisini, ambapo mama wawili alifurahi sana na kunishukuru kwa zawadi niliyompa Pili. Baada ya hapo, nikaondoka kuelekea Masaki kuonana na Hilda ili nimpe taarifa kuhusu kikao kilichopangwa ijumaa.

Nilimshirikisha Hilda kuhusu mpango wa kufunga branch ya Mikocheni na kuwaleta Masaki, na yeye alikubaliana na wazo hili na kusema ni zuri. Nilimpa taarifa za kikao kilichopangwa na nikamwambia aandae ripoti zake vizuri ili aweze kujibu maswali pindi atakapoulizwa.

Muda ulikuwa umeenda, hivyo nikarudi nyumbani ili niwahi kumpikia mama kijacho. Mara tu baada ya kufika, aliniambia ana hamu ya kula chips na yai. Hapo hapo nikatoa simu na kumpigia Sele ili aandae sahani mbili na firigisi. Nikamuaga naenda kuzifuata, lakini akasema tuende wote, kwani amechoka kukaa ndani peke yake, hivyo tukaondoka kwenda kwa Sele.

Sele alishangaa sana kumuona Iryn akiwa mjamzito tena mimba kubwa, na alisema tuingie ndani tukae tusubiri kwani chips ziko jikoni. Iryn kwa upande wake, alisema anakulia palepale na aliagiza atengenezewe zingine za kuondoka nazo.

Baada ya Iryn kuingia ndani, nilibaki nikipiga story na sele;

SELE: “We mhuni unabalaa hujataka kuchelewesha, umemjaza upepo mrembo.”

MIMI: “Hata ile siku nakuuliza mahindi, yeye ndo alihitaji.”

SELE: “Bossy umetisha sana, unakojolea pazuri sana. Mwanamke kama huyu unapataje nguvu ya kuchepuka?.”

Tuliishia kucheka nami, nikaingia ndani kwa mama kijacho wangu ili tule.

Baada ya kumaliza kula, nilimlipa Sele pesa yake na alikata sahani mbili tu, moja alitoa offa kwa mama kijacho wangu, Iryn alifurahi na tukaondoka maeneo haya.

Baada ya kurudi nyumbani, Iryn alikwenda kulala, nami nilitumia nafasi hiyo kuwasiliana na Mary. Nilitamani kujua mpango wake wa kurudi Dar, na alisema kwamba anarudi kesho, Jumatano, pamoja na Jane. Alitamani sana tungeonana, lakini nilimkatalia na kumwambia avumilie hadi Jumamosi, kwani Iryn ataondoka hiyo siku.

PART B

Siku ya Alhamisi ile asubuhi, Iryn alinipa taarifa kuhusu ujio wa dada yake kutoka Ethiopia na alisema ataingia usiku sana. Nilimuuliza atafikia wapi? Akasema anafanya mpango ili afikie Sea cliff hotel.

Saa tano asubuhi, aliniaga kuwa anakwenda kwa mama Janeth kuonana na Jessie, hivyo nilimpa kampani ya ride hadi kwa mama, kisha nikaondoka kuelekea ofisini.

Nilikuwa nakazi ya kukagua hesabu za mauzo vizuri, kwani ni muda mrefu ulikuwa umepita pasipo kufanya ukaguzi. Niliweza kubaini matatizo madogo ambayo ambayo Hilda aliweza kuyajibia, hivyo nikaendelea kupitia ripoti na kuzicompile.

Saa 10 jioni, nilipigiwa simu na Iryn, kisha akaomba niende Mikocheni na alimpa simu jamaa ili anielekeze. Jamaa kunielekeza yalikuwa ni maeneo ya karibu na Shopperz, hivyo bila kupoteza muda niliondoka kuelekea huko.

Ndani ya muda mfupi nilikuwa nimewasili na jamaa alinielekeza hadi napark gari kwenye moja ya showroom ya magari. Sasa, baada ya kushuka ndiyo namuona Iryn na Jessie wamekaa na nikatembea mpaka usawa wao nikawasalimia.

Muda huu Jessie alikuwa ananiangalia tu, namimi nilikuwa namzingua pale;

IRYN: “Darling, follow me.”

Nilimfuata kwa nyuma, hadi ilikokuwa imepark Marcedes Benz.

IRYN: “Darling, hii gari ni nzuri? Unaionaje?”

MIMI: “Ni nzuri sana, halafu hii colour naona unique kwa benz.”

IRYN: “Mimi na Jessie wote tumeipenda.”

Alimuita jamaa ambaye ana asili ya uarabu na akamwambia aiotoe nje ili tuondoke nayo, na palepale aliomba account namba ili afanye malipo. Mimi nilikuwa sijui kinachoendelea kwakweli, nilihisi moja kwa moja gari ni ya Jessie.

Benz ilitolewa showroom mpaka nje kwaajili ya kuondoka, gari ilikuwa ni nzuri ikivutia sana. Aliniita akasema niache taarifa zangu kwaajili ya usajili, hapa sasa ndo nikahisi gari itakuwa yangu.

Sikutaka kubisha na nikafanya kama alivyosema. Jamaa aliahidi kwamba kesho kufikia saa 4 asubuhi kila kitu kitakuwa sawa, hivyo tukachukue plate namba. Baada ya malipo kufanyika, tuliondoka na Jessie akaondoka na ile Audi, wakati sisi tukaondoka na ile Benz. Uvumilivu ulinishinda na nikaanza kuuliza maswali;

MIMI: “Baby, bado sijui kinachoendelea kuhusu hii gari.”

IRYN: “Mimi kama MD, ofisi imekununulia gari ili iwe inakusaidia kwenye majukumu yako pamoja na ya ofisi.”

Niliishiwa hata niseme nini maana sikutarajia kuona Iryn akinifanyia surprise kama hii. Nilikuwa bado siamini kama kweli hii benz nayoendesha kweli ni yangu.

MIMI: “Baby nashukuru sana, hata sijui niseme nini kwahaya yote unayonifanyia. May God bless you.”

IRYN: “Kampuni ina imani kubwa sana na wewe, na hii ni moja ya shukrani yangu. Mimi bado sijakupa zawadi, ila nitaanza kwanza na nyumba mengine yatafuata.”

Tulienda mpaka kwenye apartment yetu, tukapark ile gari, kisha tukaondoka tena na Jessie kumrudisha kwa mama. Baada ya kurudi nilianza kuiangalia ile Benz kwa mara nyingine tena, jinsi ilivyo nzuri na kuvutia, na niliishia kutabasamu.

Kesho yake, ijumaa tulikutana kwaajili ya kikao kifupi ambacho kilihusisha viongozi tu, na tulifanyia pale Giraffe hotel, Mbezi Beach. Kikao kilianza saa 4 kamili asubuhi na kilihusisha watu sita tu, pamoja na Iryn.

Iryn alishukuru sana uongozi wa kampuni kwa kujitoa katika kipindi kigumu, hasa wakati ambapo hatukuwa na mawasiliano. Kama MD, aliahidi kuongeza mshahara kwa 30% kwa viongozi kutokana na kazi nzuri waliyofanya. Hakuishia hapo, aliongeza kuwa baada ya kikao, atatoa zawadi kwa wote.

Baada ya bossy kuongea, nilisimama kutoa taarifa ya mwenendo wa kampuni pamoja na kuifunga branch ya Mikocheni. Lucy na Hilda, walikuwa wanajua kinachoendelea kasoro wengine walikuwa hawajui, hivyo walibaki wakishangaa baada ya kuzisikia taarifa hizi;

IRYN: “Why? I didn’t expect you would come up with this bad idea.”

Nilianza kuwaeleza sababu ya kufanya maamuzi haya;

MIMI: “Tumejadili suala hili kwa undani pamoja na Hilda na Lucy. Tumeona kuwa gharama tunazolipa kwa pango ni kubwa sana, na kuongezeka kwa gharama za umeme, maji, vibali vya leseni na mamlaka nyingine ni mzigo mkubwa. Badala ya kutafuta ofisi mpya, ni bora wateja wetu wa Mikocheni waje Masaki. Hii itatusaidia kupunguza gharama nyingi na kuongeza faida kubwa. Kwa hivyo, tunataka ufahamu kuwa maamuzi haya tumeyachunguza kwa makini na hatuja kurupuka."

Baada ya kuwapa sababu ya kuifunga ofisi ya Mikocheni, kila mtu alinyamaza kimya akifikiria maana ni sababu ambayo ilimake sense vichwani mwao na baada ya dakika kupita, Iryn alianza kuongea.

IRYN: “Mnashaurije juu ya hili, lengo tupate maamuzi sahihi, kila mtu ajaribu ku-assess risks kabla ya kukubali haya maamuzi.”

Baada ya majadiliano ya dakika 20, kila mtu aliunga mkono wazo langu la kuhamishia branch Masaki. Bossy akatoa maelekezo tuanze taratibu mapema ili tusigombane na mwenye nyumba.

Ni kikao kilicho chukua masaa 2 na baada ya kumaliza, tulipata lunch ya pamoja bila kusahu kupiga picha za ukumbusho, nami nilitumia nafasi hii kupiga picha na mama kijacho wangu, kama ukumbusho wa ujauzito wake.

Baada ya kumaliza kila kitu, tuliwaaga na kuelekea Sea cliff hotel kuonana na dada yake ambaye aliingia Dar usiku sana, akitokea Ethiopia.

Tulipofika hotelini, tulimsubiri pale reception na haikuchukua muda alitoka na wakaishia kukumbatiana na Iryn. Dada yake yuko vizuri pia, sio wa kitoto ni mzuri kwelikweli, ila bado hafiki kwa Iryn.

IRYN: “This is Insider, my boyfriend. Do you recognise him?”

VIVIAN: “Of course I do. How are you, brother-in-law?”

MIMI: “I’m fine and happy to see you again."

Mkononi, Viviani alikuwa ameshika kimfuko kidogo na alimpa Iryn, naye akanikabidhi mimi na alinikonyeza, ile kuangalia ndani kuna nini, naona si simu, nikavunga.

Baada ya maongezi mafupi, tuliongozana mpaka parking ili tuondoke, njiani macho yote yalikuwa kwetu. Kwanza niliona ufahari sana kuongozana na wanawake warembo duniani, ni wanaume wachache sana wenye bahati kama hii.

Kwa upande mwingine Sister yangu alinipa taarifa kwamba yuko Airport na anatarajia kuingia Dar, jioni. Nilimpa taarifa Iryn na alisema tufanye booking ya room palepale Sea cliff hotel mapema.

Saa 10 jioni, tuliondoka kwenda JNIA kumpokea dada yangu. Iryn aligoma kabisa kubaki nyumbani na Vivian, alisema haitakuwa vizuri ikiwa nitakwenda peke yangu kumpokea dada yangu wakati yeye yupo

Baada ya kufika JNIA, tulikaa sehemu ya kusubiri abiria. Kama ilivyo kawaida, kila mtu aligeuka kumtizama Iryn kutokana na uzuri wake wa kipekee. Alikuwa kivutio maalum pale, akiwa na mimba yake.

Ndani ya nusu saa, sister aliwasili na waliishia kukumbatiana na wifi yake kisha tukapotea eneo hili. Tulianza kwanza kupitia Sea cliff hotel, ambapo tuliacha mabag yake, kisha tukaelekea home.

Apartment ilikuwa imechangamka sana maana walikuwa wanawake watatu wakipiga story, huku wakicheka. Mimi niliamua kuwapa space na nilienda kutulia chumbani nikipanga mambo yangu.

Nilitoa ile simu kwenye mfuko na ilikuwa ni Iphone 14 kama ileile aliyoivunja hadi rangi na niliweka laini yangu. Nilimpigia simu mama J kumpa taarifa kwamba kesho nitarudi, lakini ni kama aliipokea hii taarifa kwa kutojali.

Wakati huu, nilipata ujumbe kutoka kwa Asmah ambao ulisomeka anataka kuacha kazi, ilikuwa ni taarifa mbaya kwangu, hivyo nikampandia hewani. Nilimuuliza kwanini anataka kuacha kazi, akasema yeye ameamua hivyo kwani anataka kurudi shule kusoma. Nilifunga mazungumzo kwa kumpa ahadi ya kuonana kesho ili tuzungumze vizuri kuhusu suala hili, kwani ilikuwa ni ghafla sana.

Saa 2 usiku, tulitoka kwenda kupata dinner ya pamoja pale Karambezi Café. Wao waliendelea kuzungumza, na story zao nyingi zilikuwa zinahusu leba, wakati mimi nilikuwa nasikiliza kwa sikio la kuiba huku nikijifanya nipo bize na simu

Wakati naongea na dada yangu, nilimshukuru sana kwa kujitoa kwake na kukubali kwenda South Africa. Baada ya masaa mawili kupita, tuliagana ili wajiandae mapema kwa ajili ya safari ya kesho. Walielekea hotelini na sisi tukaelekea kwenye apartment yetu.

Usiku ulikuwa mrefu sana kwani nilikuwa nakazi ya mwisho kuhakikisha barabara inakuwa safi kwaajili ya mtoto kupita. Baada ya kazi ya muda mrefu, japo niliichafua sana, lakini mama kijacho aliridhika na kazi yangu na tukalala.

Asubuhi na mapema nilimuamsha ili tujiandae kwaajili ya safari. Baada ya hapo tuliondoka kuelekea Sea cliff hotel, ambapo tuliwachukua akina sister na tukaelekea Airport. Baada ya kuwasili pale JNIA tulipiga tena picha za mwisho kama ukumbusho, kisha tukachoma ndani.

Nilianza maongezi deep na Iryn na kubwa nilimtakia kila la kheri katika kuanza safari yake mpya ya kuwa mama na nilimpa ahadi ya kwenda South Africa kujumuika naye.

IRYN: “Baba Aria, nakupenda sana na naomba uheshimu hili. Kama nilivyokuahidi before, sitoweza kuwa na mwanaume mwingine zaidi yako, napenda sana nikuzalie mtoto mwingine baada ya huyu.”

Nilipenda sana kusikia akiniita Baba Aria na nilimshika mkono wake nikauweka pajani;

MIMI: “Wewe ni mke wangu tayari, nitaangalia namna ya kuwaoa wote, kuhusu watoto hata ukitaka dozen kwangu ni kazi ndogo.”

IRYN: “Promise me unakuja lini South?”

MIMI: “Mama Aria, ninaomba kwanza nikae na familia yangu, nime-mmiss sana mwanao Junior na mama J. Nitakuja before hujajifungua natamani niwe na wewe leba hadi unajifungua.”

Iryn alifurahi sana kusikia maneno matamu kutoka kwangu na tuliagana kwa kukumbatiana maana muda wa kucheck-in ulikuwa umewadia. Niliwaaga akina sister pamoja na Viviani na niliwaambia nitawaona soon, na kabla ya kuondoka Iryn alinikumbatia kwa mara nyingine tena.

Niliondoka pale JNIA nikiwa na furaha sana, na niliwasha gari kuondoka kurudi Masaki.

Baada ya kufika kwa apartment nilipark vizuri gari, Audi maana nilikuwa naiacha pale, kisha niliingia ndani kuchukua bag, pamoja na funguo za benz yangu, nikaanza safari ya kwenda home, Mbezi Beach.

Katika maisha yangu, hakuna siku niliwaza kama nitakuja kumiliki benz, lakini ndoto yangu ilitimia kwa kuendesha benzi kali. Barabarani nilikuwa mdogo mdogo sana, kama vile namuendesha bibi harusi. Baada ya kufika home, nilimpigia simu Elena akatoka kunifungulia gate.

Junior alikuwa amesimama kibarazani akishangaa gari, kwani anapenda sana magari na baada ya kuniona baba yake, alikuja spidi nikamnyanyua juu. Na alianza kulilia aingie ndani ya gari, bhasi nilimfungulia mlango akaanza kunyonga steering.

Kwa upande mwingine, nilishtuka kuona gari yangu nyingine siioni na baada ya kuuliza, Elena alisema mama J kaondoka nayo. Niliuliza kwani anajua kuendesha? Akanijibu ndio ni mwezi sasa anaiendesha, nilibaki nikishangaa.

Nilifurahi kusikia wife amejua kuendesha gari, kwani ilikuwa ni hatua nzuri kwa upande wetu. Nilikuwa nimechoka sana pamoja na usingizi, hivyo nilienda chumbani kulala. Kwa bahati mbaya sikuweza kulala mapema sababu Junior alikuwa akinisumbua sana.

Jioni, baada ya kuamka niligundua kwamba mama J karudi na nilienda seblen kukaa, lakini nilimsikia akiongea na simu huku akicheka kwa mbali. Nilitulia pale seblen nikishangaa TV na zilipita dakika tano, bado mama J anaongea na simu. Nilihisi haya si maongezi ya kawaida na nilisogea mpaka dirishani kusikiliza, maana alikuwa kasimama pale kibarazani.

Na aliendelea kuongea, tena kwa sauti ya chini, haya ni baadhi ya maneno aliyokuwa anajibu;

Ndiyo, najua… ah, nimekumisi sana

Wewe pia unajua jinsi unavyonifanya nijisikie… usijali, nitakutafuta muda"

Tutaonana tena, usijali.


Baada ya kuona amemaliza kuongea na simu, nilirudi chumbani kwa spidi ya kunyata ili asinishtukie. Baada ya dakika 5 alirudi chumbani na nilijifanya nimelala, aliweka simu chaji akaondoka. Niliamka kwa lengo la kuikagua simu yake, kwa bahati mbaya alikuwa kabadilisha passcode, hivyo nikawa sina option nyingine.

Nilipata wazo nikague mkoba wake, na nikaona kuna risiti za Samakisamaki, Elements, KFC na nyinginezo. Nilianza kukagua za KFC zilionesha tarehe ya leo, za Elements zilionesha ni weekend iliyopita, lakini kilicho nishangaza zilionesha zimeprintiwa saa 4 usiku.

Nilibaki najiuliza mama J sio mtu wa marafiki wala kutoka out, huku Samakisamaki, Elements alikuwa na nani?. Huyu mtu waliokuwa wanaongea wote kwenye simu ni nani? Hapa sasa nikahisi kuna SOMETHING FISHY kinaendelea.

ITAENDELEA
kaka wewe ni messi mtupu , hii stori imebadilisha maisha yangu Big Up Sana INSIDER MAN
 
Pia, Mary alishauri tuendelee kutumia namba hiyo mpya ili Prisca asigundue chochote kinachoendelea kati yetu.
Huyu kichefuchefu 🤮🤮🤮🤮
tuliwasiliana na nikampa ahadi kwamba tutakutana Jumatatu mara tu nitakaporudi Dar
Kosa kubwa unapenda kutoa ahadi hewa, acha kupromise kwa kutaka siku. Zinaumiza sana isipotokea wanawake ASILIMIA KUBWA na uwapunguzia mapenzi
ASMAH: "I didn't mean what I said."
Hajui kudanganya.. Though alijitahidi na eti wa zamani... Kosa zaidi.. Iryn sio mjinga Meneja
Nilishindwa kuelewa kwa nini Iryn alikuwa na hasira kubwa kiasi hiki, wakati Asmah hakuwa amesema chochote kibaya.
Hii kitu mwanamke alijua na kiuhakika deep ndaniiiii haisameheki kabisa, jua ipo imewekwa sehemu. Siku moja hatageuka so ujijue milele
Hali hii ilinisababisha nijisikie vibaya sana, na niliona kama nimemkosea sana.
Hongera tatizo haujakoma..
CAMI: “Na hii simu vipi mbona imepasuka, mlikuwa mnagombana?”

MIMI: “Hapana, ni hasira zake ndo kaibamiza simu chini.”
😂😂😂 Ukaona aibu kumbe unajua kubaunsi kei mbalimbali ila muogaaaaa
Sikutaka hata kuongea naye, nilimshika mkono na kuanza kuondoka naye pale ofisini,
Jambo baya, bahati Iryn hakuweza wa 👂👁️ ila laweza semwa kistory na yoyote.. Ulitakiwe uwe smata kwenye hili
Asmah naomba utambue kwamba nakupenda sana, asingekuwa Iryn, huenda tungekuwa wapenzi na asingekuwa mama J, ningekuweka ndani kabisa.
Wewe ni duh 🤣🤣🤣 maneno ya Sukari 😂😂😂
Hata kitendo kile cha kumpiga kule hotelin kilibaki kuwa siri yake pekee, hakuna mtu yeyote aliyemwambia kuhusu hilo.
Mmmmh
Hapa umesahau!!!

Nilijaribu kufikiria kuhusu kumtumia ujumbe, lakini nikaona kwamba ilikuwa ni wazo baya.
Kumbe unajua kuweweseka 🤣🤣🤣🤣 hapo unakumbuka kukosa life anayokupatia.. Utafikiri unajiheshimu 😅😅😅
nilimuaga Asmah kwa kumpa ahadi ya kuonana naye hivi karibuni na nikaondoka kurudi home.
Haukomi na wewe ikija kei upo baba huruma sana.. Muhunwi
IRYN: “Unajielezea sana, nimekuelewa tuachane na haya.”
Sentensi hii ni muongo wewe.. Sema ndio hivyo Meneja una faida kubwa kwake. Ataendelea kujua juu ya Asmah. Wajanja wa chini hatusemi tunafanya nini kuyajua hata iwejeeeee..
IRYN: “Unajielezea sana, nimekuelewa tuachane na haya.”

MIMI: “Baby, I don’t want another woman, and I”ll never disrepect you or my daughter like that.”
Uongo
Baada ya kurudi nyumbani, Iryn alikwenda kulala, nami nilitumia nafasi hiyo kuwasiliana na Mary.
Muhunwi muhunwi tu damuni, ya A ingekushtua.
MIMI: “Wewe ni mke wangu tayari, nitaangalia namna ya kuwaoa wote, kuhusu watoto hata ukitaka dozen kwangu ni kazi ndogo.”
Oyooooo hii lazima 🤑🤑🤑 na Uzuri wake, ila haumpendi kutoka dipu moyoni.
nime-mmiss sana mwanao Junior na mama J.
Na Mary, Asmah na wengine haujawataja.
nilirudi chumbani kwa spidi ya kunyata ili asinishtukie.
Hii 😂😂😂😂😂😂🤣🤣🤣🤣🥳🥳🥳🥳🥳🥳 Nimecheka sanaaaaa..
Uka nini? 😅😅😅😅 Si una wengine? Why haukupotezea. 🤣🤣🤣🤣🤣💃🏽💃🏽💃🏽💃🏽Ila ingekuwa labda amemumisi mchepuko hata wa kampani tu bila kwichi ningefurahia sana yaani business partner.

Iryn yupo smati sanaaa kupita unafikiri. Noti hili. Kuna mengi amepima akaamua maisha yaendelee.. Ila kuwa makini.. Na tulia.

Twasubiri ndoa zako tukupe Hongera.. Meneja. Mary Tamara, wivu.. atakuwa Prisca cha mtoto siku moja utatambua.
 
SEASON 02
CHAPTER 37

BY INSIDERMAN”

PART A

Siku ile nilipokutana na Asmah, nilimwambia kwamba afocus zaidi kwenye maisha yake. Nia yangu haikuwa kumuumiza au kumvunja moyo, bali nilihisi ni muhimu kukaa naye mbali kwa muda ili nirekebishe mambo kati yangu na Iryn. Pia, nilitamani Asmah apate nafasi ya kutafuta mtu ambaye atakuwa sahihi kwake, kwa maisha yake ya mbele.

Tangu siku ile tulipoonana, Asmah amekuwa akinipigia simu mara kwa mara na kuomba tukutane. Hata hivyo, mara zote nimekuwa nikimkatalia kwa visingizio vya kuwa na shughuli nyingi, nikimwambia nitamtafuta baadaye, lakini ukweli ni kwamba sijawahi kufanya hivyo.

Wakati nikiwa Tabora, tuliwasiliana na nikampa ahadi kwamba tutakutana Jumatatu mara tu nitakaporudi Dar ili tuzungumze na tuliweke sawa hili jambo. Niliporudi nyumbani, Asmah alinipigia simu mara nyingi, lakini sikujua kwa wakati huo kuwa alinitafuta sana. Kumbe, mama kijacho alikuwa anaziona simu na ujumbe wake kabla mimi sijapata nafasi ya kuona.

Katika kipindi hiki ambacho Iryn ni mjamzito, nilijitahidi kuepuka ugomvi wowote naye. Simu yangu kubwa mara nyingi nilikuwa namuachia kwa sababu sikuwa na chats zozote zenye utata. Mary, kwa upande mwingine, alikuwa anajua kinachoendelea, na tulikuwa tunawasiliana kwa kutumia namba mpya niliyokuwa natumia nikiwa Dodoma. Pia, Mary alishauri tuendelee kutumia namba hiyo mpya ili Prisca asigundue chochote kinachoendelea kati yetu.

Wakati nikiwa na Iryn pale sebuleni, simu ya Asmah ilipoita tena, Iryn alichoka na hali hiyo na akaamua kuipokea mwenyewe. Alionekana kushindwa kuvumilia zaidi, huku wivu ukiwa unamsumbua.


CONTINUE:

Mimi muda huu sikuwa na uwezo wowote wa kumzuia, hivyo niliamuacha aongee naye na aliweka loud speaker.

IRYN: “Asmah, habari yako.”

Asmah hakutegemea kwamba Iryn angekuwa ndiye anayepokea simu, na ghafla akawa mpole.

ASMAH: “Ooh! Bossy, habari yako.”

IRYN: “I'm good. What's your problem? You have been calling Insider nonstop."

ASMAH: “Alinambia yuko Tabora msibani, nilitaka kujua kama karudi.”

IRYN: “What is really going on between you and Insider? Please tell me the truth."

ASMAH: “Nothing is going on between us. He is one of my closest friends, and I really appreciate that."

IRYN: “Asmah, why are you doing this? I know you’re lying to me. Why are you disrespecting me like that? Fu**cking with my Man, and you know I’m pregnant with his child.”

ASMAH: "I didn't mean what I said."

IRYN: “You know I gave you all my respect, but you still sneak around and sleep with my Man. Usione nimenyamaza kimya, najua kila mchezo mnaocheza. Nilitegemea ungekuwa na heshima zaidi kwangu hasa baada ya mimi kuwa mjamzito, lakini hujali hata kidogo."

ASMAH: “What are you talking about.?”

IRYN: “Are you just pretending not to know what I’m talking about? You’re such a bad bitch, mpuuzi kabisa…..”

Nilipoona Iryn ameanza kupandisha hasira, ilibidi nimtulize na kumnyang’anya simu kwa sababu alikuwa amevuka mipaka. Alisimama kwa hasira, akaibamiza simu yangu kwa nguvu kwenye sakafu, na kisha akaelekea chumbani.

Nilishindwa kuelewa kwa nini Iryn alikuwa na hasira kubwa kiasi hiki, wakati Asmah hakuwa amesema chochote kibaya. Nilipoinama na kujaribu kuokota simu yangu, niligundua kwamba skrini ilikuwa imevunjika, betri ilikuwa imevimba, na sehemu nyingine zilikuwa zimeharibika. Nilimfata chumbani, lakini mlango ulikuwa umefungwa. Nilisikia sauti ya kilio kutoka ndani, na ilikuwa ni kilio cha maumivu makali.

Baby, please fungua mlango.”

Nilianza kugonga mlango pale, lakini hakuonesha dalili za kufungua

Baby, naomba tuongee. Tafadhali fungua mlango, mpenzi wangu."

Bado alibaki kimya na hakuzungumza chochote, aliendelea kulia kwa sauti kubwa. Hali hii ilinisababisha nijisikie vibaya sana, na niliona kama nimemkosea sana.

Niliamua kurudi seating room na kukaa kwenye sofa huku nikitafakari namna ya kutatua hali hii. Niliwaza kwa haraka nikaona ni busara niwe mpole na kumuomba msamaha ili kuepusha matatizo, ukizingatia hali aliyonayo kwasasa hatakiwa kuwa katika hali hii.

Ilipita nusu saa, lakini bado hakuonyesha dalili za kufungua mlango, na hapa nikaingiwa na wasiwasi kwa kuwa nilihisi anaweza kufanya jambo lolote baya. Nilimgongea tena, lakini hakutaka kufungua mlango. Hali hii iliponitatiza zaidi, nikaona ni bora nimtafute Cami kwa msaada, kwani sikuwa na jinsi nyingine ya kumsaidia Iryn.

Kumpata Cami ikawa ni shida maana simu yangu imezingua, nikaanza kuchanganyikiwa maana kuondoka na kumuacha peke yake mle chumbani ni jambo lisingewezekana kwanza ni hatari.

Baada ya kufikiri sana nikakumbuka home ninasimu nyingine ambayo inanamba ya Cami, hivyo nilimpigia simu mama J. Baada ya kumpigia alisema yuko chuo, hivyo ikabidi nimpigie Elena dada wa nyumbani na kumuelekeza.

Ndani ya dakika 5, Elena alinitumia namba ya Cami na bila kuchelewa nikampigia simu;.

MIMI: “Mambo, it’s me Insider.”

CAMI: “Hey! Insider mambo.”

MIMI: “Mambo mabaya shem wangu, naomba uje home haraka, please.”

CAMI: “Kuna nini? Iryn anataka kujifungua?”

MIMI: “Just come, please.”

CAMI: “I will be there soon”

Ndani ya dakika 15 Cami alifika na alikuwa akihema sana kama mtu ambaye alikuwa anakimbizwa, na alianza kuniuliza ni nini kinaendelea?

MIMI: “Claire, Iryn kajifungia ndani chumbani ni lisaa limepita, hataki kufungua mlango.”

CAMI: “Na hii simu vipi mbona imepasuka, mlikuwa mnagombana?”

MIMI: “Hapana, ni hasira zake ndo kaibamiza simu chini.”

CAMI: “Shem niambie ni nini kinaendelea ili nijue namna ya kuongea na Iryn, usinidanganye.”

MIMI: “Sikia Claire, huu sio muda wa kuanza kuulizana kinachoendelea, Iryn amejifungia na lisaa limepita, anaweza fanya jambo baya. Please, naomba unisaidie kuongea naye, ili afungue mlango, mengine tutaongea.”

CAMI: “Iryn, alikuwa analalamika sana, amekumiss, sasa umerudi mmegombana, mapenzi yenu siyawezi asee.”

Tuliongozana hadi mlango wa chumbani, na Cami alianza kumuita Iryn kwa sauti ya upole. Baada ya kusikia sauti ya Cami, Iryn alijibu kwa hasira kwamba hataki kabisa kuniona mimi, na alitaka niondoke maeneo hayo.

CAMI: “Shem wewe ondoka, acha mimi niongee naye, akikaa sawa nitakupigia simu uje.”

Sikutaka kuwa mbishi juu ya hili, hivyo nilichukua funguo ya gari na kuondoka maeneo haya na akili yangu iliniambia nenda kwa Asmah. Saa yangu ilikuwa inasoma ni saa 10 jioni, nilihisi lazima Asmah atakuwa ofisini muda huu, nikaelekea moja kwa moja mpaka ofisini kwake.

Baada ya kufika nilipark gari parking ya nje kabisa na nikaingia ndani, nilikuwa niko spidi sana hata mapokezi sikusalimia. Nilimkuta Asmah yuko ofisini na moja ya mfanyakazi mwenzie na baada ya kuniona alisimama na kuja usawa wangu.

“Insider are you okay?.”

Sikutaka hata kuongea naye, nilimshika mkono na kuanza kuondoka naye pale ofisini, hata jamaa aliyekuwa naye alibaki akishangaa, kilikuwa ni kitendo cha haraka sana. ‘In a blink of an eye’.

Asmah alianza kulalamika pale,

“Wait, where are you taking me?”

Sikuwa hata nikimsikiliza muda huu, tulipofika nje ya geti nikampa ishara aingie ndani ya gari na akafanya hivyo, hata yeye alikuwa mpole na alianza kuogopa. Mlinzi alishuhudia lile tukio, lakini hakutaka kuingilia maana ananijua vizuri sana, hivyo alikuwa mpole.

Baada ya kuingia ndani ya gari tulianza kuangaliana na Asmah alionekana kuwa na wasiwasi sana;

MIMI: “Unajua kosa lako ni nini?”

ASMAH: “Insider, sikujua kama Iryn atapokea.”

Na nilimkatisha maongezi yake;

MIMI: “Umeniletea matatizo kwa mama kijacho wangu, unapiga simu wakati unajua fika naishi naye kwasasa na nilikupa taarifa mapema kuwa nitakucheki.”

ASMAH: “Insider, I’m really sorry, lakini haya yote wewe ndo sababu kaa ukijua hilo.”

MIMI: “Unamaanisha nini?”

ASMAH: “Umenichunia sana hadi najisikia vibaya, pale napokukumbuka.”

MIMI: “Mimi sijakuchunia kama unavyosema, ila nilikwambia kwasasa niache nifocus na maisha yangu. Kila siku nagombana na Iryn, juu yako, kwasasa sitaki haya yatokee ndomana nikakwambia vile. Pia, tambua natamani sana upate mwanaume atakayekupenda na kukuoa.”

ASMAH: “Stage niliyofikia, kukaa mbali na wewe ni ngumu. Insider nimekuzoea sana ujue, nawezaje kukaa mbali na wewe kwa yote uliyonifanyia?. Umejitoa sana kwangu, kipindi kile nimepata ajali, bado umenisaidia mambo mengi sana, najiona nina deni kwako.”

MIMI: “Huna haja ya kuwa na deni, sababu nilifanya toka moyoni na sihitaji unilipe. Asmah naomba utambue kwamba nakupenda sana, asingekuwa Iryn, huenda tungekuwa wapenzi na asingekuwa mama J, ningekuweka ndani kabisa.”

ASMAH: “Unataka kusema nini?.”

MIMI: “Upendo niliokuwa nao kwako, kwasasa umehamia kwa Iryn. Na sitaki kumpoteza kisa wewe, naomba uheshimu hili, yule ni mke wangu tayari na nitarajia kupata mtoto soon.”

ASMAH: “Hongera sana kwa kutarajia kupata mtoto soon.”

MIMI: “Please, move on kwa usalama wangu na wa kwako pia, tutaendelea kushirikiana kwenye mambo mengine, lakini tuwe na mipaka. Kwa mara ya kwanza leo Iryn, amepaniki live na ametoa maneno makali juu yako.”

ASMAH: “Hata mimi nimeogopa sana, kwa mara ya kwanza nazifeel hasira zake, na sikutoa neno lolote baya.”

MIMI: “Wasiwasi wake, mimi na wewe tuko kwenye mahusiano ya siri, kipindi hiki cha ujauzito amekuwa na wivu sana.”

ASMAH: “Sasa nafanyaje?

MIMI: “Mpigie simu, omba kuonana naye ili muongee juu ya hili, naamini atakubali muonane.”

ASMAH: “Insider mimi naogopa ujue.”

MIMI: “Mpigie simu sahivi, mwambie unataka kukutana naye, ukionana naye atatulia.”

Asmah alitoa simu yake mfukoni na akampigia Iryn, simu iliita bila kupokelewa, akapiga kwa mara ya pili, ndiyo kupokelewa na akamwambia dhumuni lake ni kuonana ili waongee na Iryn alimkubalia, akasema anamtumia location.

ASMAH: “Mimi naogopa siwezi kwenda.”

MIMI: “Sasa unaogopa nini?, nenda kajisafishe na unisafishe na mimi. Usikubali kitu chochote kile atakachokuuliza, wewe ni mtu mzima utajua utaongea nini.”

ASMAH: “What if kama anaushahidi kwamba we had sex.?”

MIMI: “I don’t think so, nafikiri kuna mtu kamjaza haya maneno, Iryn hana ushahidi juu ya hili.”

ASMAH: “Unajuaje kama hana evidence? Na ameongea vile mbele yangu.”

MIMI: “I know her, ingekuwa kweli anazo mimi ningejua tu, Asmah niamini mimi. You have to clean up the mess for me.”

ASMAH: “Sawa acha niende, kama kuna lolote nitakupigia simu.”

MIMI: “Nipigie kwa namba hii kama utapata shida, nitakuwa around.”

Baada ya kuachana na Asmah nilienda Cocobeach- Wavuvi kempu kutulia. Niliagiza heineken zangu mbili huku namsubiri Asmah. Muda huu nilitumia kuchat na Cami, nilimuuliza kuhusu maendeleo ya Iryn ana akasema yuko sawa, japo alilia sana. Nilimuuliza Iryn anafanya nini kwasasa, akasema amekaa kwa balconi na yuko na mgeni, nikajua ni Asmah wala si mwingine.

Kwa upande mwingine, Cami aliendelea kuniuliza shida ni nini, kwani hata Iryn hakuwa amemwambia sababu halisi ya ugomvi wetu. Nilimwambia aendelee kuwa mpole, na kwamba Iryn mwenyewe atamwambia tu chanzo cha ugomvi wetu.

Iryn ni mmoja wa wanawake ambao hawapendi kuweka maisha yao public, ni mtu ambaye anajali sana faragha ya mambo yetu ya ndani na hataki kuyaeleza kwa watu wengine. Hata kitendo kile cha kumpiga kule hotelin kilibaki kuwa siri yake pekee, hakuna mtu yeyote aliyemwambia kuhusu hilo.

Baada ya masaa mawili kupita na hakuna dalili za Asmah kunicheki, nilianza kuingiwa na wasiwasi. Nilijiuliza kwa nini anachelewa kutoka na nini kinaendelea?. Nilijaribu kufikiria kuhusu kumtumia ujumbe, lakini nikaona kwamba ilikuwa ni wazo baya.

Baada ya nusu saa, Asmah alipiga simu na kuniuliza nilipo. Nikamwambia aje Cocobeach tukutane. Ndani ya muda mfupi alifika Cocobeach na alisema yuko karibu na chupa ya Cocacola akinisubiri.

Nilitoka pale Wavuvi, nikamchukua Asmah, na nikaendesha gari kwa kasi hadi karibu na mitaa ya restaurant ya ‘Amigos’. Huko ndipo nilipokipaki gari na kuanza mazungumzo.

MIMI: “Nipe mrejesho wa mlichozungumza na mama kijacho.”

ASMAH: “Kila kitu kipo sawa kwasasa, nimeongea naye muda mrefu sana na amenielewa. Nimesema ukweli kwamba mimi na wewe tulikuwa kwenye mahusiano zamani wakati tumefahamiana, lakini tuliachana na kwasasa sisi ni marafiki.”

MIMI: “Una uhakika amekuelewa?”

ASMAH: “Trust me japo nimebanwa sana, juu yako. Alisema yeye yuko tayari kutuacha tuendelee na mahusiano, huenda yeye ndiye amedandia treni la watu. Nimemwambia Insider anakupenda sana na hayuko tayari kukupoteza na kila siku anajidai utamzalia mtoto wa kike.”

MIMI: “Umefanya jambo la muhimu sana, ahsante.”

ASMAH: “Nimekubali matokeo, japo nilikupenda sana naomba uendelee na Iryn, kwa heshima na wadhifa wake.

MIMI: “Leo ndo unakiri kuwa unanipenda sana?.”

ASMAH: “Ni kweli, kipindi umeanza mahusiano na Iryn nilikuwa naumia sana hujui tu.”

Simu yangu ilianza kuita na kuangalia ni Iryn alikuwa anapiga simu, nilimuonesha Asmah kuwa Iryn anapiga, naye akasema nipokee haraka. Baada ya kupokea aliniuliza niliko, nikamwambia niko Cocobeach, akasema nirudi home mapema.

Ilikuwa ni saa mbili usiku tayari, hivyo sikutaka kupoteza muda na nilimuaga Asmah kwa kumpa ahadi ya kuonana naye hivi karibuni na nikaondoka kurudi home.

Nilitumia muda mfupi sana kufika, kuingia ndani nawaona wamekaa sebleni, nami nikaketi pembeni ya mama kijacho. Wakati huu
Claire alikuwa akitabamu, kana kwamba kuna kitu anataka kuongea. Haikuchukua muda na aliaga anaondoka kurudi kwake, maana alikuwa na majukumu mengine ya kufanya.

Nilimpa kampani mpaka kwake na tukiwa njiani tulikuwa tunaongea na kubwa alisema, Iryn hajasema chanzo cha ugomvi wetu. Pia, aliendelea kusisitiza kwamba Iryn ananipenda sana. Baada ya kufika kwake, nilimshukuru sana kwa msaada wake na tukaagana pale, nami nikageuza kurudi home.

Baada ya kufika, Iryn alikuwa amekaa kwa balconi, hivyo nilienda na nikakaa pembeni yake. Palikuwa na hewa safi na upepo wa bahari ukipiga eneo hili kwa utulivu sana. Tulianza kuangaliana pale, nami niliamua kuvunja ukimya;

MIMI: “Nambie mke wangu, upo tayari tuongee?”

IRYN: “I’m listening.”

MIMI: “Mummy, mimi na Asmah hatuko kwenye mahusiano naku-apia kwa hili. Usipende kusikiliza maneno ya wabongo, hakuna anayependa kuona mimi niko na mwanamke mrembo kama wewe.”

IRYN: “Lazima niwe na maswali, kwanini Asmah tu, akupigie simu nonstop?. Mchana kabla ya kwenda lunch, alipiga simu mara 3 na bado akatuma message akilalamika sana kuwa unamtenga. Kwa haya yaliyotokea, na ninajua fika wewe na Asmah mlikuwa na historia unafikiri nitawaza nini?.”

MIMI: “Nakwambia ukweli, lastweek niliongea na Asmah akae mbali na mimi, na haya yote ni kwasababu yako, sikutaka uendelee kuwa na wasiwasi juu ya ukaribu wetu.

Ilibidi nimueleze ukweli kuhusu mipango yangu juu ya Asmah, ili aweze kuelewa na sikuona haja kumficha juu ya hili.

IRYN: “Unajielezea sana, nimekuelewa tuachane na haya.”

MIMI: “Baby, I don’t want another woman, and I”ll never disrepect you or my daughter like that.”

IRYN: “Unakumbuka tulikubaliana kwamba mtoto akiwa wa kike jina utampa wewe?”

MIMI: “Yes! Darling, unataka nikutajie jina kabisa?”

IRYN: “Don’t tell me hujaandaa jina bado.”

MIMI: “Niliandaa mummy, from today nitakuita ‘mama Ariana’, do you like the baby’s name?”

IRYN: “Yeah, it’s a beautiful name, and I like it. Thank you baba Aria.”

Furaha yetu ilirudi kama zamani na nilimwambia tuende chumbani tukalale maana muda ulikuwa umeyoyoma tayari.

Saa nne asubuhi nilitoka kwenda Mikocheni kuonana na Lucy, pia nilitamani sana tumalize tofauti zetu. Nilipofika pale ofisini niliweza kuonana na Lucy, bila kupoteza muda nilianza kumuomba radhi kwa kumkosea.

Lucy kwa upande wake alisema, aliumia sana kwa kitendo cha mimi kwenda Dodoma bila kumuaga wala kumtafuta, halafu nikawa nawasialiana na Hilda kwa siri, hiki ndo kilimuuma sana. Lucy, aliendelea kusema kwamba hakutegemea mimi ningemfanyia vile, ukizingatia sisi ni washikaji wa muda mrefu sana.

Ukweli nilikuwa nimemkosea sana, hivyo niliendelea kumuomba radhi na baada ya kumuelekeza sana dhumuni la mimi kufanya vile, hapa ndiyo aliweza kunielewa na kunisamehe.

Tulianza kuongea masuala mengine kwa ujumla na kubwa lilikuwa sakata la Asmah. Alinisisitiza sana kama nina mahusiano ya siri na Asmah, bhasi niache mara moja, kwani Iryn alimpigia simu na kulalamika kwamba anahisi kuna jambo linaendelea kati yangu na Asmah.

Baadae tulianza kuongea masuala ya ofisi maana landlord alikuwa ameanza kusumbua tuondoke, kwani alitoa taarifa mapema.

MIMI: “Iryn kaniachia hili suala nifanye maamuzi, wewe ndo manager wa hapa, unashaurije.?”

LUCY: “Hii location ilikuwa nzuri sana na imekaa kimkakati, tunapata wapi tena eneo zuri kama hili?”

MIMI: “Wateja wako wanaokuja hapa ni loyal customers?.”

LUCY: “Ndiyo na wageni wanakuja wengi sana.”

MIMI: “Nimewaza sana asubuhi nikaona ni bora ofisi ihamie Masaki. Tutaepusha cost nyingi sana, pia Masaki hatulipi pango bado pana nafasi kubwa ya kutosha.”

LUCY: “Kumbuka Mikocheni, tulitarget na wale wa kipato cha kati, tukihamia Masaki si tutawakosa hawa customers.?”

MIMI: “Bei zitabaki kuwa zilezile, na sikuzote mteja anafuata huduma bora, ukiwaambia tumehamia Masaki watakuja tu. Halafu, ijumaa tutakuwa na kikao asubuhi, fikiria hili vizuri na kesho unipe majibu ili tufanye maamuzi mapema.”

LUCY: “Sawa bossy, nipe muda nijifikirie juu ya hili.”

Baada ya maongezi marefu na Lucy, nilimuacha aendelee na majukumu yake huku mimi nikiendelea kukagua ofisi kwa ujumla.

Nilipigiwa simu na mama wawili, na wakati nilipoipokea, sauti ya Pili ilisikika. Alinisalimia na kusema kwamba nimewatenga sana, tofauti na zamani. Maneno haya yaliniuma sana, hivyo nikamuuliza yuko wapi. Alisema yupo ofisini kwa mama yake, na nikamwambia nitakuwa hapo baada ya lisaa.

Baada ya kumaliza ukaguzi, nilimuaga Lucy kisha nikaondoka kwenda ofisini kwa mama wawili. Nilipowapa taarifa kwamba nimefika, walikuja haraka, na Pili alinikumbatia mara tu alipoona.

Tulianza mazungumzo na mama wawili, ambapo habari kuu ilikuwa kuhusu mpango wa binti yake kusoma nje. Nilimuuliza Pili kama anaridhia kusoma nje, na alithibitisha. Baada ya hapo, nilimuomba Pili atupishe ili niweze kuzungumza na mama yake kwa faragha.

Mama wawili alifurahi sana kuniona na aliniuliza kuhusu agenda yangu Dodoma. Nikamwambia project nayoifanya kule na alinipongeza kwa hatua hii, kisha tukandelea na mazungumzo mengine kwa muda mrefu. Baada ya mazungumzo, niliomba niondoke na Pili na kumrudisha baadaye. Mama wawili hakuwa na tatizo na ombi hilo na aliniruhusu.

Niliondoka na Pili kwenda Mlimani na lengo langu lilikuwa kutimiza ahadi ya kumpa zawadi ya simu niliyomuahidi baada ya kumaliza shule. Pale Mlimani, nilionana na jamaa yangu, nikamwambia anipe bei ya iPhone 12, kisha nikampa nafasi Pili achague rangi ya simu anayoipenda. Ilikuwa ni surprise ambayo Pili hakutegemea, na alifurahi sana. Baada ya hapo, tukaenda kula pizza pamoja.

Jioni, nilimrudisha Pili kwa mama yake ofisini, ambapo mama wawili alifurahi sana na kunishukuru kwa zawadi niliyompa Pili. Baada ya hapo, nikaondoka kuelekea Masaki kuonana na Hilda ili nimpe taarifa kuhusu kikao kilichopangwa ijumaa.

Nilimshirikisha Hilda kuhusu mpango wa kufunga branch ya Mikocheni na kuwaleta Masaki, na yeye alikubaliana na wazo hili na kusema ni zuri. Nilimpa taarifa za kikao kilichopangwa na nikamwambia aandae ripoti zake vizuri ili aweze kujibu maswali pindi atakapoulizwa.

Muda ulikuwa umeenda, hivyo nikarudi nyumbani ili niwahi kumpikia mama kijacho. Mara tu baada ya kufika, aliniambia ana hamu ya kula chips na yai. Hapo hapo nikatoa simu na kumpigia Sele ili aandae sahani mbili na firigisi. Nikamuaga naenda kuzifuata, lakini akasema tuende wote, kwani amechoka kukaa ndani peke yake, hivyo tukaondoka kwenda kwa Sele.

Sele alishangaa sana kumuona Iryn akiwa mjamzito tena mimba kubwa, na alisema tuingie ndani tukae tusubiri kwani chips ziko jikoni. Iryn kwa upande wake, alisema anakulia palepale na aliagiza atengenezewe zingine za kuondoka nazo.

Baada ya Iryn kuingia ndani, nilibaki nikipiga story na sele;

SELE: “We mhuni unabalaa hujataka kuchelewesha, umemjaza upepo mrembo.”

MIMI: “Hata ile siku nakuuliza mahindi, yeye ndo alihitaji.”

SELE: “Bossy umetisha sana, unakojolea pazuri sana. Mwanamke kama huyu unapataje nguvu ya kuchepuka?.”

Tuliishia kucheka nami, nikaingia ndani kwa mama kijacho wangu ili tule.

Baada ya kumaliza kula, nilimlipa Sele pesa yake na alikata sahani mbili tu, moja alitoa offa kwa mama kijacho wangu, Iryn alifurahi na tukaondoka maeneo haya.

Baada ya kurudi nyumbani, Iryn alikwenda kulala, nami nilitumia nafasi hiyo kuwasiliana na Mary. Nilitamani kujua mpango wake wa kurudi Dar, na alisema kwamba anarudi kesho, Jumatano, pamoja na Jane. Alitamani sana tungeonana, lakini nilimkatalia na kumwambia avumilie hadi Jumamosi, kwani Iryn ataondoka hiyo siku.

PART B

Siku ya Alhamisi ile asubuhi, Iryn alinipa taarifa kuhusu ujio wa dada yake kutoka Ethiopia na alisema ataingia usiku sana. Nilimuuliza atafikia wapi? Akasema anafanya mpango ili afikie Sea cliff hotel.

Saa tano asubuhi, aliniaga kuwa anakwenda kwa mama Janeth kuonana na Jessie, hivyo nilimpa kampani ya ride hadi kwa mama, kisha nikaondoka kuelekea ofisini.

Nilikuwa nakazi ya kukagua hesabu za mauzo vizuri, kwani ni muda mrefu ulikuwa umepita pasipo kufanya ukaguzi. Niliweza kubaini matatizo madogo ambayo ambayo Hilda aliweza kuyajibia, hivyo nikaendelea kupitia ripoti na kuzicompile.

Saa 10 jioni, nilipigiwa simu na Iryn, kisha akaomba niende Mikocheni na alimpa simu jamaa ili anielekeze. Jamaa kunielekeza yalikuwa ni maeneo ya karibu na Shopperz, hivyo bila kupoteza muda niliondoka kuelekea huko.

Ndani ya muda mfupi nilikuwa nimewasili na jamaa alinielekeza hadi napark gari kwenye moja ya showroom ya magari. Sasa, baada ya kushuka ndiyo namuona Iryn na Jessie wamekaa na nikatembea mpaka usawa wao nikawasalimia.

Muda huu Jessie alikuwa ananiangalia tu, namimi nilikuwa namzingua pale;

IRYN: “Darling, follow me.”

Nilimfuata kwa nyuma, hadi ilikokuwa imepark Marcedes Benz.

IRYN: “Darling, hii gari ni nzuri? Unaionaje?”

MIMI: “Ni nzuri sana, halafu hii colour naona unique kwa benz.”

IRYN: “Mimi na Jessie wote tumeipenda.”

Alimuita jamaa ambaye ana asili ya uarabu na akamwambia aiotoe nje ili tuondoke nayo, na palepale aliomba account namba ili afanye malipo. Mimi nilikuwa sijui kinachoendelea kwakweli, nilihisi moja kwa moja gari ni ya Jessie.

Benz ilitolewa showroom mpaka nje kwaajili ya kuondoka, gari ilikuwa ni nzuri ikivutia sana. Aliniita akasema niache taarifa zangu kwaajili ya usajili, hapa sasa ndo nikahisi gari itakuwa yangu.

Sikutaka kubisha na nikafanya kama alivyosema. Jamaa aliahidi kwamba kesho kufikia saa 4 asubuhi kila kitu kitakuwa sawa, hivyo tukachukue plate namba. Baada ya malipo kufanyika, tuliondoka na Jessie akaondoka na ile Audi, wakati sisi tukaondoka na ile Benz. Uvumilivu ulinishinda na nikaanza kuuliza maswali;

MIMI: “Baby, bado sijui kinachoendelea kuhusu hii gari.”

IRYN: “Mimi kama MD, ofisi imekununulia gari ili iwe inakusaidia kwenye majukumu yako pamoja na ya ofisi.”

Niliishiwa hata niseme nini maana sikutarajia kuona Iryn akinifanyia surprise kama hii. Nilikuwa bado siamini kama kweli hii benz nayoendesha kweli ni yangu.

MIMI: “Baby nashukuru sana, hata sijui niseme nini kwahaya yote unayonifanyia. May God bless you.”

IRYN: “Kampuni ina imani kubwa sana na wewe, na hii ni moja ya shukrani yangu. Mimi bado sijakupa zawadi, ila nitaanza kwanza na nyumba mengine yatafuata.”

Tulienda mpaka kwenye apartment yetu, tukapark ile gari, kisha tukaondoka tena na Jessie kumrudisha kwa mama. Baada ya kurudi nilianza kuiangalia ile Benz kwa mara nyingine tena, jinsi ilivyo nzuri na kuvutia, na niliishia kutabasamu.

Kesho yake, ijumaa tulikutana kwaajili ya kikao kifupi ambacho kilihusisha viongozi tu, na tulifanyia pale Giraffe hotel, Mbezi Beach. Kikao kilianza saa 4 kamili asubuhi na kilihusisha watu sita tu, pamoja na Iryn.

Iryn alishukuru sana uongozi wa kampuni kwa kujitoa katika kipindi kigumu, hasa wakati ambapo hatukuwa na mawasiliano. Kama MD, aliahidi kuongeza mshahara kwa 30% kwa viongozi kutokana na kazi nzuri waliyofanya. Hakuishia hapo, aliongeza kuwa baada ya kikao, atatoa zawadi kwa wote.

Baada ya bossy kuongea, nilisimama kutoa taarifa ya mwenendo wa kampuni pamoja na kuifunga branch ya Mikocheni. Lucy na Hilda, walikuwa wanajua kinachoendelea kasoro wengine walikuwa hawajui, hivyo walibaki wakishangaa baada ya kuzisikia taarifa hizi;

IRYN: “Why? I didn’t expect you would come up with this bad idea.”

Nilianza kuwaeleza sababu ya kufanya maamuzi haya;

MIMI: “Tumejadili suala hili kwa undani pamoja na Hilda na Lucy. Tumeona kuwa gharama tunazolipa kwa pango ni kubwa sana, na kuongezeka kwa gharama za umeme, maji, vibali vya leseni na mamlaka nyingine ni mzigo mkubwa. Badala ya kutafuta ofisi mpya, ni bora wateja wetu wa Mikocheni waje Masaki. Hii itatusaidia kupunguza gharama nyingi na kuongeza faida kubwa. Kwa hivyo, tunataka ufahamu kuwa maamuzi haya tumeyachunguza kwa makini na hatuja kurupuka."

Baada ya kuwapa sababu ya kuifunga ofisi ya Mikocheni, kila mtu alinyamaza kimya akifikiria maana ni sababu ambayo ilimake sense vichwani mwao na baada ya dakika kupita, Iryn alianza kuongea.

IRYN: “Mnashaurije juu ya hili, lengo tupate maamuzi sahihi, kila mtu ajaribu ku-assess risks kabla ya kukubali haya maamuzi.”

Baada ya majadiliano ya dakika 20, kila mtu aliunga mkono wazo langu la kuhamishia branch Masaki. Bossy akatoa maelekezo tuanze taratibu mapema ili tusigombane na mwenye nyumba.

Ni kikao kilicho chukua masaa 2 na baada ya kumaliza, tulipata lunch ya pamoja bila kusahu kupiga picha za ukumbusho, nami nilitumia nafasi hii kupiga picha na mama kijacho wangu, kama ukumbusho wa ujauzito wake.

Baada ya kumaliza kila kitu, tuliwaaga na kuelekea Sea cliff hotel kuonana na dada yake ambaye aliingia Dar usiku sana, akitokea Ethiopia.

Tulipofika hotelini, tulimsubiri pale reception na haikuchukua muda alitoka na wakaishia kukumbatiana na Iryn. Dada yake yuko vizuri pia, sio wa kitoto ni mzuri kwelikweli, ila bado hafiki kwa Iryn.

IRYN: “This is Insider, my boyfriend. Do you recognise him?”

VIVIAN: “Of course I do. How are you, brother-in-law?”

MIMI: “I’m fine and happy to see you again."

Mkononi, Viviani alikuwa ameshika kimfuko kidogo na alimpa Iryn, naye akanikabidhi mimi na alinikonyeza, ile kuangalia ndani kuna nini, naona si simu, nikavunga.

Baada ya maongezi mafupi, tuliongozana mpaka parking ili tuondoke, njiani macho yote yalikuwa kwetu. Kwanza niliona ufahari sana kuongozana na wanawake warembo duniani, ni wanaume wachache sana wenye bahati kama hii.

Kwa upande mwingine Sister yangu alinipa taarifa kwamba yuko Airport na anatarajia kuingia Dar, jioni. Nilimpa taarifa Iryn na alisema tufanye booking ya room palepale Sea cliff hotel mapema.

Saa 10 jioni, tuliondoka kwenda JNIA kumpokea dada yangu. Iryn aligoma kabisa kubaki nyumbani na Vivian, alisema haitakuwa vizuri ikiwa nitakwenda peke yangu kumpokea dada yangu wakati yeye yupo

Baada ya kufika JNIA, tulikaa sehemu ya kusubiri abiria. Kama ilivyo kawaida, kila mtu aligeuka kumtizama Iryn kutokana na uzuri wake wa kipekee. Alikuwa kivutio maalum pale, akiwa na mimba yake.

Ndani ya nusu saa, sister aliwasili na waliishia kukumbatiana na wifi yake kisha tukapotea eneo hili. Tulianza kwanza kupitia Sea cliff hotel, ambapo tuliacha mabag yake, kisha tukaelekea home.

Apartment ilikuwa imechangamka sana maana walikuwa wanawake watatu wakipiga story, huku wakicheka. Mimi niliamua kuwapa space na nilienda kutulia chumbani nikipanga mambo yangu.

Nilitoa ile simu kwenye mfuko na ilikuwa ni Iphone 14 kama ileile aliyoivunja hadi rangi na niliweka laini yangu. Nilimpigia simu mama J kumpa taarifa kwamba kesho nitarudi, lakini ni kama aliipokea hii taarifa kwa kutojali.

Wakati huu, nilipata ujumbe kutoka kwa Asmah ambao ulisomeka anataka kuacha kazi, ilikuwa ni taarifa mbaya kwangu, hivyo nikampandia hewani. Nilimuuliza kwanini anataka kuacha kazi, akasema yeye ameamua hivyo kwani anataka kurudi shule kusoma. Nilifunga mazungumzo kwa kumpa ahadi ya kuonana kesho ili tuzungumze vizuri kuhusu suala hili, kwani ilikuwa ni ghafla sana.

Saa 2 usiku, tulitoka kwenda kupata dinner ya pamoja pale Karambezi Café. Wao waliendelea kuzungumza, na story zao nyingi zilikuwa zinahusu leba, wakati mimi nilikuwa nasikiliza kwa sikio la kuiba huku nikijifanya nipo bize na simu

Wakati naongea na dada yangu, nilimshukuru sana kwa kujitoa kwake na kukubali kwenda South Africa. Baada ya masaa mawili kupita, tuliagana ili wajiandae mapema kwa ajili ya safari ya kesho. Walielekea hotelini na sisi tukaelekea kwenye apartment yetu.

Usiku ulikuwa mrefu sana kwani nilikuwa nakazi ya mwisho kuhakikisha barabara inakuwa safi kwaajili ya mtoto kupita. Baada ya kazi ya muda mrefu, japo niliichafua sana, lakini mama kijacho aliridhika na kazi yangu na tukalala.

Asubuhi na mapema nilimuamsha ili tujiandae kwaajili ya safari. Baada ya hapo tuliondoka kuelekea Sea cliff hotel, ambapo tuliwachukua akina sister na tukaelekea Airport. Baada ya kuwasili pale JNIA tulipiga tena picha za mwisho kama ukumbusho, kisha tukachoma ndani.

Nilianza maongezi deep na Iryn na kubwa nilimtakia kila la kheri katika kuanza safari yake mpya ya kuwa mama na nilimpa ahadi ya kwenda South Africa kujumuika naye.

IRYN: “Baba Aria, nakupenda sana na naomba uheshimu hili. Kama nilivyokuahidi before, sitoweza kuwa na mwanaume mwingine zaidi yako, napenda sana nikuzalie mtoto mwingine baada ya huyu.”

Nilipenda sana kusikia akiniita Baba Aria na nilimshika mkono wake nikauweka pajani;

MIMI: “Wewe ni mke wangu tayari, nitaangalia namna ya kuwaoa wote, kuhusu watoto hata ukitaka dozen kwangu ni kazi ndogo.”

IRYN: “Promise me unakuja lini South?”

MIMI: “Mama Aria, ninaomba kwanza nikae na familia yangu, nime-mmiss sana mwanao Junior na mama J. Nitakuja before hujajifungua natamani niwe na wewe leba hadi unajifungua.”

Iryn alifurahi sana kusikia maneno matamu kutoka kwangu na tuliagana kwa kukumbatiana maana muda wa kucheck-in ulikuwa umewadia. Niliwaaga akina sister pamoja na Viviani na niliwaambia nitawaona soon, na kabla ya kuondoka Iryn alinikumbatia kwa mara nyingine tena.

Niliondoka pale JNIA nikiwa na furaha sana, na niliwasha gari kuondoka kurudi Masaki.

Baada ya kufika kwa apartment nilipark vizuri gari, Audi maana nilikuwa naiacha pale, kisha niliingia ndani kuchukua bag, pamoja na funguo za benz yangu, nikaanza safari ya kwenda home, Mbezi Beach.

Katika maisha yangu, hakuna siku niliwaza kama nitakuja kumiliki benz, lakini ndoto yangu ilitimia kwa kuendesha benzi kali. Barabarani nilikuwa mdogo mdogo sana, kama vile namuendesha bibi harusi. Baada ya kufika home, nilimpigia simu Elena akatoka kunifungulia gate.

Junior alikuwa amesimama kibarazani akishangaa gari, kwani anapenda sana magari na baada ya kuniona baba yake, alikuja spidi nikamnyanyua juu. Na alianza kulilia aingie ndani ya gari, bhasi nilimfungulia mlango akaanza kunyonga steering.

Kwa upande mwingine, nilishtuka kuona gari yangu nyingine siioni na baada ya kuuliza, Elena alisema mama J kaondoka nayo. Niliuliza kwani anajua kuendesha? Akanijibu ndio ni mwezi sasa anaiendesha, nilibaki nikishangaa.

Nilifurahi kusikia wife amejua kuendesha gari, kwani ilikuwa ni hatua nzuri kwa upande wetu. Nilikuwa nimechoka sana pamoja na usingizi, hivyo nilienda chumbani kulala. Kwa bahati mbaya sikuweza kulala mapema sababu Junior alikuwa akinisumbua sana.

Jioni, baada ya kuamka niligundua kwamba mama J karudi na nilienda seblen kukaa, lakini nilimsikia akiongea na simu huku akicheka kwa mbali. Nilitulia pale seblen nikishangaa TV na zilipita dakika tano, bado mama J anaongea na simu. Nilihisi haya si maongezi ya kawaida na nilisogea mpaka dirishani kusikiliza, maana alikuwa kasimama pale kibarazani.

Na aliendelea kuongea, tena kwa sauti ya chini, haya ni baadhi ya maneno aliyokuwa anajibu;

Ndiyo, najua… ah, nimekumisi sana

Wewe pia unajua jinsi unavyonifanya nijisikie… usijali, nitakutafuta muda"

Tutaonana tena, usijali.


Baada ya kuona amemaliza kuongea na simu, nilirudi chumbani kwa spidi ya kunyata ili asinishtukie. Baada ya dakika 5 alirudi chumbani na nilijifanya nimelala, aliweka simu chaji akaondoka. Niliamka kwa lengo la kuikagua simu yake, kwa bahati mbaya alikuwa kabadilisha passcode, hivyo nikawa sina option nyingine.

Nilipata wazo nikague mkoba wake, na nikaona kuna risiti za Samakisamaki, Elements, KFC na nyinginezo. Nilianza kukagua za KFC zilionesha tarehe ya leo, za Elements zilionesha ni weekend iliyopita, lakini kilicho nishangaza zilionesha zimeprintiwa saa 4 usiku.

Nilibaki najiuliza mama J sio mtu wa marafiki wala kutoka out, huku Samakisamaki, Elements alikuwa na nani?. Huyu mtu waliokuwa wanaongea wote kwenye simu ni nani? Hapa sasa nikahisi kuna SOMETHING FISHY kinaendelea.

ITAENDELEA
Umemix Camilla na Claire, and somehow I can't blame your wife. She might have seen you around those places and after all she posses a heart with feelings. Good luck thou.
 
Back
Top Bottom