Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

SEASON 02
CHAPTER 41

“BY INSIDER MAN”

CONTINUE:

Kwa upande wangu, sikutarajia hata kidogo kukutana na mama mkubwa. Niliposogea, nilimsalimia kwa heshima. Alinijibu kwa upole, kisha akaniangalia kwa makini, macho yake yakitua pia kwa Aria aliyekuwa kamshika. Sekunde chache zilivyopita, alinitazama tena na kusema kwa sauti tulivu, “Umefanana sana na mtoto.” Kabla sijapata nafasi ya kujibu, Mama Janeth naye alidakia, akinitazama kwa tabasamu na kusema, “Ni kweli kabisa, mnafanana sana wewe na Aria.”

Niliishia kutabasamu baada ya kusikia maneno yale kutoka kwa mama mkubwa, kisha nikatafuta sehemu ya kuketi. Sebleni palikuwa na wageni wengi sana, hali iliyonifanya nijisikie kutokuwa na utulivu, lakini sikuwa na namna. Nilibaki pale, nikijaribu kuzoea hali ile, huku nikionesha utulivu ambao sikuwa nao ndani yangu.

Baada ya dakika nyingi kupita, niliamua kwenda chumbani kwa Iryn ili kumsalimia na kumjulia hali. Nilipofika, niligundua hakuwa peke yake, alikuwa na wageni wawili. Niliwasalimia wote kwa heshima, na bila kusita, Iryn alinitambulisha kwa marafiki zake akisema, “Hawa ni marafiki zangu, tumesoma nao chuo Ufaransa.”

Nilimuuliza Iryn kuhusu maendeleo ya kidonda chake, na aliniambia kuwa anaendelea vizuri kabisa. Tulipokuwa tunaendelea kuzungumza, ghafla Jimmy aliingia chumbani. Mara tu Iryn alipomuona, uso wake ulibadilika kabisa.

JIMMY: “Hata ukininunia, freshy tu."

IRYN: “Jimmy, nakuchukia sana!"

JIMMY: “Hujaanza leo, na sishangai kabisa.”

IRYN: “Jana ulimpeleka wapi Insider?”

Jimmy alinitazama kwa wasiwasi, akihisi labda nimemueleza Iryn kuhusu tulikokuwa usiku huo. Nilimpa ishara kuwa sina ufahamu wowote juu ya jambo hilo.

JIMMY: “Sawa, tulienda Soho kuburudika, na tulirudi salama."

Iryn, akiwa amekasirika, alitazama pembeni na kuona bakuli karibu yake. Alilichukua kisha akamrushia Jimmy kwa hasira, huku akimfyonza kwa dhihaka.

Na wakati huu, Amara aliingia chumbani na kuanza kuuliza, “Shida ni nini?" Jimmy, kwa haraka, alimnyanyua juu juu na kutoka naye hadi sebleni. Lilikuwa tukio la ghafla na la kufurahisha, kiasi kwamba kila mtu aliishia kucheka, hata wageni.

Niliamua kuondoka chumbani ili kumpa Iryn nafasi na wageni wake. Hata hivyo, wakati nilipokuwa natoka, ghafla nilisikia akiniita kwa sauti ya upole, “Subiri kidogo...”

IRYN: “Darling, where are you going?”

MIMI: “Nipo mke wangu, huna haja ya kuwa na wasiwasi.”

IRYN: “Usije ukanitoroka kama jana ulivyofanya.”

MIMI: “ Leo nipo na wewe baby.”

Baada ya kurudi sebleni, nilitambua kuwa watu watatu hawakuwepo, nao ni dada yangu, Vivian, na Samantha. Nilipouliza, niliambiwa kuwa walitoka kwenda supermarket kununua vitu kwa ajili ya mama mtoto.

Baada ya takriban saa moja, mzee Virgil aliwasili na familia yake yote. Ilikuwa siku ya kipekee kwani niliweza kuwafahamu wadogo zake wote kupitia mama mdogo, kasoro kaka yake ambaye mzee alimzaa na mwanamke mwingine.

Mchana tulikula chakula cha pamoja, ambacho kiliagizwa kutoka kwa wapishi wa nje. Baada ya lunch, mama Janeth alitusalimu na kutuaga, akituambia kwamba anaondoka kwa safari ya kwenda Tanzania, kisha ataendelea na safari yake kwenda Marekani (USA).

Kabla ya mama Janeth kuondoka, tulipata nafasi ya kuzungumza. Nilimshukuru sana kwa kujitoa kwake na kuhakikisha Iryn anajifungua salama. Mama Janeth alinituliza, akisema kwa upole, “Iryn ni binti yangu, huna haja ya kunishukuru kwa hili.”Maneno yake yalikuwa ya faraja, yakiniondolea wasiwasi.

Jioni nilikutana na dada yangu, na tukatafuta sehemu tulivu kwa ajili ya mazungumzo yetu. Mara tu baada ya kuketi, dada alianza kuzungumza kwa hisia, akilalamika kuhusu tabia zangu mpya ambazo nimeanza kuonesha waziwazi mbele ya mama J. Aliuliza kwa upole lakini kwa msisitizo, “Kipindi kile ulipolala nje, ulikuwa wapi?” Akiongeza kwa tahadhari, alisema, “Na kama utathubutu kunidanganya, itakuwa ndio mwisho wa maongezi yetu.” Maneno yake yalikuwa na uzito, yakinifanya nifikirie kwa makini kuhusu majibu yangu.

Niliwaza pale na kuamua ni bora niwe mkweli ili tuweze kumaliza mambo haya.

MIMI: “Nilikuwa na mwanamke mwingine.”

SISTER: “Una matatizo gani? Tuliongea vizuri kabisa kuhusu haya, lakini bado unaendelea kuyafanya. Je, unanidharau mimi dada yako? Nilitegemea utaanza kufocus na watoto wako, lakini unazidi kuhangaika na wanawake wengine?”

MIMI: “Dada yangu, najua nimezingua. Mwanamke huyu alinifata Dodoma mwenyewe, na kipindi kile nilikuwa nimegombana na mama J, na Iryn alikuwa hana dalili za kurudi.”

Majibu yangu yalimfanya dada yangu aonekane mwenye wasiwasi zaidi, lakini pia nilijua ni muhimu kuwa mkweli ili kuweza kuendelea mbele.

SISTER: “Nisikilize kwa makini, bro. Usinione kama mjinga kukusaidia na kesi zako za kila siku ambazo unafanya kwa makusudi. Leo nakupa onyo la mwisho, kama una wanawake nje na hawa mama watoto wako, nikaja kupata kesi, utakuwa umefunga kufuli la mimi kukusaidia.”

MIMI: “Dada yangu, usifike huko, nimekuelewa na sitokuangusha.”

SISTER: “Na kilichofanya uondoke bila kumuaga mama J ni nini? Unaonesha dharau kama hizi kwa mke wako.”

MIMI: “Mimi naondoka tumegombana kwa sababu alimpigia mama yangu simu na kumwambia nililala nje. Niliona ananichonganisha na mama yetu, kwa kitu ambacho hana ushahidi nacho.”

SISTER: “Unataka kuachana na mama J, kisa Iryn?. Ukitaka mambo yako yaanze kuharibika tena, bhasi jichanganye ufanye huo ujinga unaotaka kuufanya, utayakumbuka maneno yangu.”

MIMI: “Siwezi kumuacha mama J, hili nakuapia dada yangu.”

Baada ya kumaliza tofauti zetu, dada aliniahidi kunisaidia kuliweka sawa suala la Iryn. Alinishauri nisubiri mtoto afike miezi sita ndipo nianze hatua za kuwaambia wazazi. Alisema ni bora nianze kumshirikisha mzee, na kisha yeye ndiye atakayemwambia mama. Maneno yake yaliniweka katika hali ya matumaini, kwani nilijua kwamba kwa msaada wake, naweza kupata njia sahihi ya kukabiliana na hali hii.

Dada alinionyesha mbinu ya kuanza kumuandaa kisaikolojia mama J, akisema kwamba nianze kufanya hivi taratibu ili aanze kuhisi mapema kuwa nina mtoto nje. Hata hivyo, nilishindwa kumuelewa alimaanisha nini, hivyo ilibidi nimuulize.

MIMI: “Mbinu gani natakiwa kuanza kuitumia?”

SISTER: “Katika maongezi yenu, unaweza kumuuliza, 'Hivi, ukija kufahamu kuwa nina mtoto nje, utafanyaje?' Inatakiwa uwe unamuuliza mara kwa mara hadi pale atakapozoea na kuona ni jambo la kawaida.”

MIMI: “Dada yangu, sio kwa mama J, hachelewi kulianzisha.”

SISTER: “Hawezi kufanya chochote kwa sababu atakuwa hana ushahidi. Kwa mara ya kwanza atapata shida kadri anavyozidi kusikia kutoka kwako, lakini atazoea na kuona ni jambo la kawaida. Wewe cha kuzingatia ni kuwa unachukua note ya majibu anayotoa, na utakuwa unanitumia.”

Maneno yake yalikuwa na maana, lakini nilihisi bado kuna changamoto kubwa katika kutekeleza mbinu hiyo. Lakini dada alizidi kukazia kwamba mbinu hii itaanza kumuandaa kisaikolojia, na baada ya muda atazoea hali hiyo. Alisisitiza kwamba hata nitakapokuja kumpa taarifa rasmi, haitaleta shida sana na atakuwa na uwezo wa kuelewa vizuri. Maneno yake yalinipa matumaini, kwani niliweza kuona uwezekano wa kumfikia mama J kwa njia ambayo ingekuwa rahisi na ya busara.

Kuhusu suala la kumpa taarifa rasmi, dada alishauri ni bora nisubiri hadi nitakapomalizana na wazee na kila kitu kipo sawa. Alisema kwamba ni hapo ndipo nianze hatua za kumwambia mama J. Dada alinihakikishia kwamba atanisaidia kadri anavyoweza kwa kutumia uwezo wake wote hadi mambo yawe sawa. Maneno yake yalijenga imani ndani yangu, na nilihisi kuwa na msaada wa dada yangu kutanisaidia kukabiliana na changamoto hii.

Baada ya kumaliza maongezi yetu muhimu, dada aliniaga na kuniambia kwamba kesho, Jumapili, ataondoka kurudi Tanzania. Alisisitiza kwamba pindi nitakaporudi Dar es Salaam, nimtaarifu ili aje tuyaweke sawa na mama J.

Nilimuuliza dada kama amelipia tiketi ya ndege, naye akasema kwamba wifi yake, Iryn, alikuwa amelipia tayari na amemwingizia pesa nyingi kwenye akaunti yake, ingawa hakutaka pesa hizo. Dada alifungua app ya benki na kunionesha kiasi ambacho aliingiziwa, na nilibaki nikishangaa.

Mwishoni, dada alinipongeza kwa kuwa baba, akisema kuwa Aria ni damu yetu halali. Maneno yake yalinipa furaha kubwa na kunitia moyo zaidi. Tuliagana kwa kukumbatiana, kisha tukarudi ndani kuendelea na mambo mengine, kwani tulikuwa tumetumia muda mwingi sana kwenye maongezi yetu.

Kibarazani, akina Jimmy walikuwa wanacheza last card, na mimi nilijiunga nao, tukawa jumla wanne: Mimi, Jimmy, Vivian, na Samantha. Mchezo ulikuwa mzuri sana, maana tulianza hadi kuweka hela kwa mshindi, na hali hiyo ilifanya ushindani uwe mkali. Baadaye, dada alikuja na tukawa jumla watano, na mchezo ukawa na ladha mpya, huku kila mmoja akijaribu kushinda kwa njia yake. Kicheko na furaha vilijaza hewa, na ilikuwa ni fursa nzuri ya kuondoa mawazo na kufurahia muda pamoja.

Ninataka niwaambie kuhusu undugu wa Jimmy, Iryn, Vivian, na Samantha. Ninarudisha hadi chapter 9, siku ambayo nilifika Ethiopia kwa mara ya kwanza. Katika siku hiyo, dada watatu walikuja kumpokea Iryn, ambapo alinitambulisha. Yule dada mkubwa ndiye alikuwa Vivian, mtoto wa Pili wa mama mkubwa, huku Jimmy akiwa mtoto wa kwanza akifuatiwa na mdogo wake katika wale wawili waliokuwa wamekuja kumpokea Iryn.

Hawa watatu wa kwanza, Vivian, Jimmy, na mdogo wao, wanatoka kwenye tumbo moja, wakiwa na mama na baba mmoja, ingawa baba yao alishatangulia mbele za haki. Mama mkubwa alizaa watoto wengine wawili na mume mwingine, Samantha na mdogo wake wa mwisho. Huyu mdogo wa mwisho ndiye mmoja kati ya wale dada wawili wadogo ambao Iryn alinifahamisha kama wadogo zake.

Mama mkubwa ana jumla ya watoto watano. Watatu wa kwanza wanashiriki baba mmoja, wakati hawa wawili wa mwisho wanashiriki baba mwingine. Kati ya watoto hao watano, Jimmy pekee ndiye mtoto wa kiume. Kwa Iryn, watoto hawa ni kama binamu zake (cousins), ingawa yeye hupenda kuwaita dada na kaka.


Nilikaa sana pale nyumbani, na hatimaye mimi na Jimmy tuliondoka saa 6 usiku kurudi hotelini. Nilipitia mapokezi kuchukua kadi yangu, na dada wa mapokezi akaniambia kuwa kuna ujumbe wangu. Alinipa kadi na kikaratasi kidogo. Nilielewa kinachoendelea mara moja, na Jimmy aliona yote hayo, akabaki kutabasamu.

Baada ya kuingia chumbani, nilifungua kile kinote na kugundua kuwa ilikuwa ni namba ya simu ya Nala. Niliweka pembeni na kuelekea bafuni kuoga. Baada ya kumaliza kuoga, nilijilaza kitandani, nikiwa nimechoka lakini mawazo yakiwa hayajakaa sawa. Nilianza kuyapitia kwa kina yale mazungumzo yangu na sister, nikitafakari maana yake na mwelekeo wa mambo.

Ukweli ni kwamba, Sister alizungumza mambo mengi sana, lakini kubwa kuliko yote, aliniapia kwamba nikifanya makosa tena, basi atajiondoa kabisa kwenye huu msala, na niachwe nipambane peke yangu. Sister ndiye kiungo muhimu katika kufanikisha hili jambo, hivyo niliona ni busara kutulia na kuwekeza nguvu zangu kwa umakini kwenye familia zangu.

Niliwaza sana kuhusu wazo la kumuacha Mary, lakini kila nilipofikiria, nilijikuta nikipoteza nguvu kwa sababu bado nampenda. Hata hivyo, kutokana na ushauri wa Sister, niliona sina budi kufanya hivyo. Ni bora nimuache mapema kuliko kusubiri na kuleta matatizo makubwa zaidi huko mbeleni.

Niliwaza sana na hatimaye nikaamua kwamba nitakaporudi Dar es Salaam, nitamtafuta Mary ili tuzungumze wazi kuhusu hili suala. Kilichonipa faraja kidogo ni kwamba Mary tayari alikuwa anafahamu kinachoendelea kuhusu mahusiano yangu na Iryn, hivyo nilihisi mazungumzo yetu yangeweza kuwa ya uwazi zaidi.

Jambo lingine lililoanza kunisumbua kichwani ni jinsi wazazi wangu watakavyopokea taarifa za mimi kuzaa na Iryn. Swali kubwa lililozunguka mawazoni mwangu lilikuwa, je, watalichukuliaje suala hili? Nilijua kuwa na mtihani mgumu mbele yangu, lakini kwa sababu Sister aliahidi kunisaidia, nilijisemea kwamba kila kitu kitakuwa sawa. Hata hivyo, sikupuuza uzito wa hali hiyo.

Kwa upande wangu, nilitamani sana kuona Junior na Aria wakifahamiana tangu utotoni ili waweze kujenga uhusiano wa karibu na bond nzuri. Kuhusu hili suala, nilihisi mzee ndiye anayeweza kunipa ushauri mzuri zaidi. Hivyo, nilianza kupata hamasa ya kumtafuta mapema ili tuweze kuzungumza na kupanga namna bora ya kufanikisha hili.
*****

Asubuhi, baada ya kuamka, nilimpigia simu mama J ili kumsalimia, lakini hakupokea, hivyo nilihisi labda alikuwa ameenda kanisani. Niliingia bafuni haraka kuoga na kujiandaa ili tuweze kwenda kwa mama mtoto. Ilikuwa saa mbili asubuhi, na nilihisi muda ulikuwa unayoyoma. Nilimpigia simu Jimmy kumjulisha kuwa tuanze safari, lakini naye hakuwa akipokea. Hatimaye, nikaamua kwenda kumgongea chumbani kwake.

Baada ya kufika kwenye chumba chake, maana yeye alikuwa floor ya juu, niligonga mlango na alitoka kufungua. Alikuwa haja jiandaa, hivyo nilipompa taarifa ya kuondoka, aliniambia nimsubiri ajiandae haraka. Nikamwambia atanikuta kwenye restaurant nikimsubiri.

Nilielekea kwenye restaurant kupata kifungua kinywa, na wakati huo nilikuwa nawasiliana na Iryn, ambaye alikuwa akinisisitizia nianze safari mapema ili niweze kucheza na mtoto. Baada ya nusu saa, nilimuona Jimmy akiwa ameongozana na mwanamke mwenye asili ya kizungu, na nikahisi huenda alikuwa amelala naye. Hali hii iliniacha na maswali mengi kichwani mwangu.

Walipofika, waliketi pamoja nami, na Jimmy alifanya utambulisho wa kawaida, na mimi pia nilimsalimia yule dada. Waliagiza kifungua kinywa, na baada ya kumaliza, tuliondoka kwenye eneo hilo, tukimwacha dada akisubiri usafiri wa kumpeleka kwake.

Wakati tuko kwenye Uber, nilianza kumuuliza Jimmy maswali kuhusu yule mwanamke. Nilikuwa na hamu ya kujua zaidi kuhusu mahusiano yao, na jinsi alivyomjua.

MIMI: “Bro, yule ni nani tena?”

JIMMY: “Tulikutana juzi Soho club, tukabadilishana namba, jana baada ya kuchat naye, nilimpanga aje hotelini akakubali.”

MIMI: “She’s a hoe?”

JIMMY: “I don’t think so, anafanyia kazi kwenye moja ya ubalozi hapa South Africa.”

Nilibaki kimya, nikitafakari kwa undani. Jimmy alikuwa amenishinda kabisa kwa tabia zake. Nilijiuliza mara ngapi ameweza kukutana na wanawake kama yule, na ni wangapi mpaka sasa? Spidi yake ilikuwa ya kutisha, na ilinifanya nishindwe kuelewa vizuri mwelekeo wake. Nilijikuta nawaza kama angeweza kudhibiti hali hii, au kama ilikuwa sehemu ya maisha yake ya kila siku.

Baada ya kuwasili, mazingira yalionekana kuwa kimya na tulivu sana. Tulipofika kibarazani, mtoto wa Jimmy alionekana akicheza peke yake. Jimmy alimnyanyua kwa furaha, kisha tukaingia ndani kuzungumza na mama mtoto ili tupate kujua ratiba ya siku ile.

Pale sebuleni, dada yangu alikuwa amemshika mtoto, na tukaingia kwenye mazungumzo kuhusu safari yake. Alisema anatarajia kuanza safari saa 11 jioni. Wakati huo, Iryn alitoka sebuleni na kuja kukaa pembeni yangu. Alionekana kuzidi kuimarika kadri siku zilivyokuwa zinaenda, jambo lililonipa faraja. Mazungumzo yetu yaliendelea kwa utulivu, na hali ilikuwa ya amani.

Baada ya kula chakula cha mchana, mimi, dada yangu, na mama mkubwa tuliamua kuwa na kikao chetu binafsi. Tulitafuta utulivu nje kwenye bustani, mbali na kelele na muingiliano wa watu wengine. Hapa tuliweza kuzungumza kwa uwazi na utulivu, tukijadili mambo muhimu bila usumbufu wowote. Mazingira yalikuwa tulivu, na kikao kilikuwa na uzito wa kipekee.

Mama alianza kwa kumshukuru sana sister kwa kujitolea kwake kwa kipindi chote hadi Iryn alipojifungua. Sister alisaidia sana, hasa kwenye mazoezi na mbinu mbalimbali za kuhakikisha Iryn anajifungua salama. Kwa kuwa sister yangu tayari alikuwa na watoto wawili, alikuwa na uzoefu mwingi ambao ulimsaidia kumwelekeza Iryn vyema wakati wa ujauzito na hadi wakati wa kujifungua. Mama alionyesha shukrani za dhati kwa mchango wake mkubwa.

Ukiachana na yote, Sister aliweza pia kutengeneza mahusiano mazuri sana na wifi zake, kama Vivian na Samantha. Wote walionekana kumpenda sana dada yangu kwa jinsi alivyojitoa na kujali. Uhusiano wao ulijengeka kwa upendo na uelewa, na hilo lilifanya familia kuwa karibu zaidi.

Kuhusu suala la mimi kumpa mimba binti yake, mama alisema hawezi kusema lolote kwa sababu Iryn mwenyewe alifanya maamuzi yake, na ni mtu mzima ambaye anaelewa vyema anachokifanya. Alionyesha kutambua kwamba Iryn alikuwa na uwezo wa kuchukua maamuzi yake binafsi, na hakutaka kuingilia zaidi. Hii ilileta hali ya unafuu kidogo, ingawa suala hilo bado lilikuwa na uzito wake.

Mama aliniuliza swali ambalo lilikuwa zito kulijibu:

“Una mpango na malengo gani juu ya Iryn?"

Nilihisi uzito wa swali hilo, lakini nilijua dhumuni la mama kuuliza ni nini. Nikajua kwamba ni muhimu kufikiri kwa umakini na kuepuka kutoa ahadi ambazo huenda nisitekeleze. Kwa kutumia busara na tahadhari, nilimjibu hivi:

MIMI: “Asante mama kwa kuniuliza swali hili muhimu. Ninamuheshimu sana Iryn na ninatambua nafasi yake katika maisha yangu. Nimeliona hili suala kwa uzito wake, na ninataka kuhakikisha kwamba mimi na Iryn tunajenga msingi mzuri wa ushirikiano, hasa kwa ajili ya ustawi wa mtoto wetu. Nataka tuchukue mambo hatua kwa hatua, huku tukijadiliana na kupanga vizuri mustakabali wa familia yetu. Ninaendelea kutafakari juu ya mpango mzuri na utakaokuwa bora kwa wote, na nataka kuhakikisha kwamba kila kitu kinawekwa wazi na kwa manufaa ya pande zote mbili.”

Mama na Sister waliniangalia kimya kwa muda, wakitafakari majibu yangu. Mama, hasa, alionekana kutotarajia jibu langu. Niliona machoni mwake kwamba alitarajia kitu tofauti, labda ahadi thabiti au mpango ulio wazi zaidi kuhusu mustakabali wangu na Iryn.

MAMA: “Naona umejibu kwa hekima, lakini bado sijapata uhakika. Wewe na Iryn, mna mpango wa kuwa pamoja au hili ni suala tu la mtoto?”

MIMI: “Naelewa unavyohisi mama, na ni swali lenye uzito. Kwa sasa, mimi na Iryn tunaendelea kuzungumza juu ya mstakabali wetu. Kipaumbele chetu kikubwa ni kuhakikisha mtoto anakua katika mazingira bora, lakini bado tupo kwenye hatua ya kufikiria kwa kina jinsi ya kutatua hali yetu ya kibinafsi. Siwezi kusema kwa hakika wakati huu, ila nataka iwe wazi kwamba sitamtelekeza Iryn wala mtoto wetu.”

MAMA: “Hilo ni jambo jema kusikia, lakini ningependa kuona mnapanga mustakabali wenye utulivu zaidi, hasa kwa ajili ya binti yangu. Matarajio yangu ni kwamba, kama kuna upendo na nia njema, basi mtachukua hatua ya kusonga mbele pamoja.”

MIMI: “Ninakubaliana na wewe kabisa mama, Iryn ni mtu muhimu kwangu na sina mpango wa kufanya maamuzi ya haraka bila kufikiria kila mtu aliyehusika. Ni muhimu kwangu kwamba wote tunakuwa na maelewano mazuri kwa ajili ya mtoto na hatimae, kwa Iryn pia.”

MAMA: “Nashukuru kwa uwazi wako, ningependa tu kuona unachukua hatua thabiti, maana Iryn anastahili uhakika. Si kwamba nakuwekea shinikizo, lakini ningependa kuona binti yangu akiwa kwenye mikono salama.”

MIMI: “Naelewa mama, na ninakuhakikishia kwamba natilia maanani kila kitu unachosema. Nitafanya kila niwezalo kuhakikisha mambo yanaenda vizuri kwa Iryn na mtoto wetu.”

Mama aliniangalia kwa makini, na nilihisi alikua akiwaza, labda akijiuliza, “Huyu jamaa ana akili sana.” Nilijua kuwa niliyajibu maswali yake yote kwa umakini na hekima. Hata dada yangu alionesha tabasamu, akionyesha kushangazwa na jinsi nilivyoweza kujibu maswali ya mama kwa njia ambayo haikuniingiza kwenye mtego.

Mama aliendelea na mazungumzo, akasema angependa kuwajua wazazi wetu, akisisitiza kuwa ni muhimu kwa mustakabali wa mtoto. Aliongeza kwamba sasa sisi tumeshakuwa muunganiko wa familia, na ni muhimu kuimarisha uhusiano huu kwa kuhakikisha kila mmoja anajua historia na asili ya mwingine. Mama alionyesha kuwa na hamu ya kujenga mshikamano ndani ya familia yetu, ili mtoto apate msingi mzuri wa malezi na urithi wa kihisia.

Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, Sister alijiandaa kwa ajili ya safari yake ya kurudi Tanzania. Hali ilikuwa ya huzuni kidogo, lakini pia ya furaha kwa sababu tulikuwa tumepata muda mzuri wa kuzungumza na kujenga uhusiano wetu zaidi.

Saa 9 mchana, Sister alitoka na begi lake na kutuaga pale sebuleni. Tulitoka nje na kupiga picha za pamoja kama kumbukumbu ya wakati wetu mzuri pamoja. Baada ya hapo, mimi na Vivian tulimpa kampani hadi uwanja wa ndege. Safari hiyo ilikuwa ya furaha, ingawa tulihisi huzuni kidogo kwa sababu ya kuachana. Tulizungumza mengi katika gari, tukijadili mipango ya baadaye na sister kuahidi kukutana tena na kina Vivian hivi karibuni.

Tukiwa airport, tulizungumza mambo mengi sana, na Sister aliendelea kunisitiza kwamba nitakaporudi Dar es Salaam, nimpe taarifa ili aje nyumbani kuweka sawa masuala yangu na mama J. Kabla ya kucheck in, aligana na Vivian kwa kukumbatiana kwa upendo, na niliona jinsi walivyokuwa na uhusiano mzuri. Baada ya hapo, tuliondoka maeneo hayo, tukielekea nyumbani, tukiwa njiani story na Vivian ziliendelea na niseme hawa mashem zangu wananikubali na tunapatana sana.

Usiku, niliwasiliana na mama J pamoja na mwanangu Junior. Nilimdanganya kwamba nipo China nikifuatilia mzigo, na baada ya hapo nitatoka kwenda South Africa kumuona Iryn, ambaye amejifungua mtoto. Mama J hakutoa maoni mengi kuhusu hilo, zaidi alisema atawasiliana na Iryn kumpa hongera. Ingawa alionekana kutokuwa sawa na hali hiyo, nilijua ujumbe wangu ulikuwa umemfikia.
*****

Wiki inayofuata, ambayo ilikuwa ni wiki ya kwanza ya mwezi wa 7, idadi ya wageni iliongezeka sana pale kwa Iryn. Ndugu zake kutoka Ethiopia walifika, na pia marafiki zake wa chuo waliosoma pamoja Ufaransa walikuwa wakija na kuondoka. Sebuleni, kila kona ilikuwa imejaa zawadi za mtoto, na hapo ndipo nilipogundua kwa kweli kwamba Iryn alikuwa na mtandao mpana wa watu. Hali hiyo ilionyesha jinsi alivyokuwa akipendwa na kuungwa mkono na watu wengi, na ilifanya moyo wangu ujaze faraja na kujivunia kuwa sehemu ya maisha yake.

Siku ya Jumatano, mama mkubwa aliondoka kurudi Ethiopia ili kuendelea na majukumu yake. Pia, dada wa kazi kutoka Ethiopia alifika nyumbani kusaidia katika kazi mbalimbali. Iryn alieleza kuwa hakutaka dada wa kazi mwenyeji kwa sababu ya tabia zao, hivyo alihitaji mtu ambaye wangeweza kuendana kiutamaduni. Hali hiyo ilionyesha umuhimu wa mazingira yanayofanana na utamaduni wao, na niliona ni busara kwa Iryn kuchagua mtu ambaye angeweza kuleta utulivu na uelewano katika familia.

Siku ya Jumapili, Jimmy pamoja na familia yake waliondoka kurudi Ethiopia, hivyo aliyebaki ni dada Vivian. Baada ya kuondoka kwa Jimmy, nilienda kukaa na Iryn, maana idadi ya watu ilikuwa imepungua, na mle ndani tulikuwa jumla watano. Hali hiyo ilituletea fursa nzuri ya kuzungumza kwa undani zaidi na kujenga uhusiano wetu.

Wiki ya pili ya mwezi wa 7, Jumatatu, bibi yao ‘Momo’ alifika South Africa kumuona kitukuu chake. Aliwasili jioni, na mimi na Samantha tulikwenda kumpokea pale airport. Momo, ambaye sasa ana umri wa miaka 70, ni bibi mwenye uzoefu wa maisha, lakini bado ana nguvu za kujiendesha. Momo ana tabia ya kutabasamu na kuwa na nishati, na nilijua kwamba uwepo wake ungeongeza furaha na umoja katika familia yetu.

Tangu tupo kwenye gari hadi tulipofika nyumbani, Bibi alikuwa na furaha sana na alionyesha hamu kubwa ya kumuona kitukuu wake. Alikuwa akizungumza kwa lugha yao ya nyumbani, lakini Samantha alikuwa ananiambia kila kilichokuwa kinaendelea, akitafsiri maneno ya bibi kwa urahisi. Ilikuwa ni furaha kubwa kusikia shauku ya bibi, na niliweza kuhisi upendo wake wa dhati kwa familia.

Baada ya kufika nyumbani, Iryn hakuwa mbali kumpokea bibi yake, na walikumbatiana kwa furaha na kumkaribisha ndani. Kitu cha kwanza bibi alichomba ni kumuona kitukuu wake, na alifurahi sana baada ya kumuona. Uso wake ulijawa na tabasamu la furaha, na Iryn alionekana pia akifurahia moment hiyo. Nilijua kuwa bibi alikuwa na matumaini makubwa kwa ajili ya kitukuu chake, na nilihisi furaha kuona jinsi familia ilivyokuwa ikijenga uhusiano mzuri katika kizazi tofauti.

Baada ya bibi kurudi nyumbani, mazingira yalichangamka sana, kwani bibi ni mwongeaji sana, na wajukuu zake wanampenda sana. Bibi alisema ataendelea kukaa na Iryn na hafikirii kurudi Ethiopia mapema, jambo lililomfanya Iryn ajisikie vizuri. Iryn ni mjukuu ambaye bibi yake anampenda sana, na hii ni kwa sababu Iryn humjali sana bibi yake, akimpa huduma na kumuhudumia kwa upendo.

Kwa upande wangu, tangu nilipofika South Africa, tayari wiki mbili zilikuwa zimepita, na nilipanga kuondoka Jumapili ya weekend. Niliangalia hali yangu na kugundua kwamba kuendelea kukaa huku kungeweza kuathiri mambo yangu mengi, kuanzia kampuni hadi biashara zangu. Nilijua ni muhimu kurejea nyumbani ili kusimamia masuala yangu na kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa. Ingawa nilifurahia wakati niliokuwa pamoja na Iryn na familia, nilihisi ni lazima nitafute njia ya kuleta uwiano kati ya majukumu yangu ya kifamilia na biashara zangu.

Kesho yake asubuhi, nilimfata Iryn chumbani ili niweze kuzungumza naye kuhusu suala langu la kuondoka. Pembeni yake kulikuwa na diary, hivyo niliichukua na kuanza kuisoma. Niliona alikuwa akiandika mipango yake, na nilicheka baada ya kuona ameandika mpango wa kuanza gym.

Of course, alikuwa ameanza kunenepa sana kutokana na kuwa mama na vyakula anavyokula, lakini bado haikufanya apoteze uzuri na shape yake. Kinyume chake, niliona kuwa mabadiliko hayo yaliongeza mvuto wake, na alikuwa akionekana kuwa na uzuri wa kipekee ambao unakuja na umama.

MAMA ARIA: “Darling, unacheka nini?”

MIMI: “Nimefurahi kuona una mpango wa kuanza Gym, lakini bado mapema sana.”

MAMA ARIA: “I know, baada ya miezi 3 nitaanza mazoezi ya kupunguza huu mwili.”

Nami, nikasogea kukaa pembeni yake;

MIMI: “Nimekumiss baby mama.”

Iryn alianza kuangalia usawa wa bunduki yangu na akanishika kidevu changu na tukaanza kuangaliana pale;

MAMA ARIA: “Are you horny?”

MIMI: “Ofcourse yes.”

MAMA ARIA: “Pole! nadhani unakumbuka siwezi kusex kwasasa hadi nipone vizuri, doctor alishauri baada ya miezi 3, ila mwezi ujao nitaenda kuangalia maendeleo.”

MIMI: “Naelewa usijali, mimi nitavumilia kwa hili.”

Usawa wa matiti yake ulionekana kulowa maziwa, kwani chuchu zake zilikuwa bado zimesimama. Baada ya kumuona vile, ilibidi nimwambie kwamba analowa, akicheka kidogo kwa aibu. Alijua kwamba hali hiyo ni ya kawaida kwa mama anapokuwa katika kipindi hiki, lakini nilijua kwamba ilikuwa ni muhimu kwake kujisikia vizuri kuhusu mwili wake.

MAMA ARIA: “Mwanao hataki kunyonya, halafu mama yake nina maziwa mengi sana. Uwe unamsaidia mwanao kunyonya, kwani naishia kuyakamua na kuyamwaga. Nikupe unyonye? Yatakusaidia kiafya.”

Nilihisi aibu baada ya kusikia haya maneno kutoka kwa Iryn. Aliponigeukia na kunipa ishara ya kunyonya, sikuona sababu ya kukataa, kwani alikuwa anayamwaga. Nilijisemea, si afadhali nikanywa mimi kuliko yamwagwe. Nilianza kuyanyonya taratibu hadi aliposema basi, ndio kuacha na yalikuwa ni matamu sana.

MAMA ARIA: “Vipi matamu?”

MIMI: “Yeah! Aria anafaidi sana.”

MAMA ARIA: “Mwanao mpole kama wewe, naona huyu atarithi tabia zako.”

MIMI: “Bado mtoto, akikua ndio tutajua tabia zake, hata Junior alikuwa mpole kama Aria, ila sasahivi ni balaa.”

Tulipoanza mazungumzo yetu, alizungumzia suala lake la kurudi shule na akaniambia kuwa analiwazia kwa umakini. Nami nikamshirikisha mpango wangu wa kurudi shule mwezi wa kumi, ambapo alinisisitiza kwa upendo kuwa ni vema nisomee masomo yangu ya masters nchini Afrika Kusini ili tuwe karibu na mtoto wetu.

Ingawa wazo hilo lilikuwa zuri, nilijua kuwa kulikuwa na changamoto nyingi zinazoweza kufanya isiwezekane. Hivyo, nilimpatia jibu lililofikiriwa vizuri, ambalo alielewa kwa upole na busara.

Nilimwambia kwa upole,

Baby mama, nikisomea huku, kumbuka kuwa mambo mengi yanaweza kuyumba, kuanzia kampuni yako hadi miradi yangu. Ufuatiliaji wa karibu ni muhimu sana. Acha mimi nisomee Dar ili niwe karibu na biashara zetu. Kuhusu Aria, nitakuwa nakuja mara kwa mara kuwasalimu, siwezi kukaa muda mrefu bila kumuona binti yangu. Kama vile wakati wa ujauzito wako ulivyokuwa ukija Dar es Salaam mara kwa mara, sasa ni zamu yangu kuja Cape Town. Tutaendelea kuwa karibu, hata kama nitakuwa huku.”

Mama Aria alifurahi sana kusikia maneno yangu, na hakuwa na la kusema zaidi. Baadaye, nilimueleza kuhusu mpango wangu wa kuondoka Jumapili. Hata hivyo, kwenye suala la kuondoka, alionekana kulipokea tofauti na aliniomba niondoke mwisho wa mwezi. Nilijaribu kumsihi kwa upole, na kumuomba aniruhusu niondoke wiki ijayo, huku nikiahidi kuwa nitarudi mapema kwa ajili ya sherehe ya "Simchat Bat" ya mtoto wetu.

Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, aliamua kwenda kuoga. Wakati huo, Aria alikuwa ameamka, hivyo nilimbeba na kutoka naye sebleni ili tupate muda wa kukaa pamoja. Sikuwa na shughuli nyingi za kufanya kipindi hicho nikiwa Afrika Kusini, zaidi ya kutumia muda wangu mwingi kucheza na Aria. Sikutoka kwenda sehemu yoyote mara kwa mara, isipokuwa tu kwenda supermarket pale panapohitajika.

Haikupita muda mrefu kabla mama Aria hajarudi kwenye seating room, na kunijulisha kuhusu ujio wa mgeni. Aliniambia kuwa anayekuja ni kaka yake, ambaye ni wa kwanza kwa upande wa mama mwingine. Nilikuwa nimeshaongelea kidogo kuhusu huyu kaka yake, katika Season 1: EP10.

Mchana ule, kaka yake alifika nyumbani kumsalimia Iryn pamoja na mtoto, akiwa ameongozana na mpenzi wake. Hii ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona kaka yake kwa upande wa baba. Ni kijana mwenye haiba fulani ya "manton," kwa mbali anataka kuendana na rappa AKA.

Tulisalimiana pale, kisha tukaingia kwenye mazungumzo ambapo alinikaribisha sana Afrika Kusini kwa ukarimu. Iryn akaanza kumuuliza kaka yake kuhusu maisha na kazi kwa ujumla. Ingawa kaka yake Iryn yuko vizuri kiuchumi, tatizo lake kubwa ni matumizi ya madawa, jambo ambalo limemuharibu sana. Niliwahi kugusia kuhusu hili hapo awali.

Baada ya kupata chakula cha mchana kwa pamoja, kaka yake na mpenzi wake waliondoka. Mama Aria kisha alinipa taarifa nyingine kwamba siku ya Jumamosi tungeenda nyumbani kwa baba yake. Aliongeza kuwa kuna mambo kadhaa watakayokwenda kuyapanga na mzee wake, na akaniambia atanishirikisha katika hayo mazungumzo siku hiyo.

*****

Hatimaye, siku ya Jumamosi ilifika, siku ambayo ilikuwa ni ya kwenda kwa mzee Virgil, baba mkwe wangu. Mzee Virgil alikuwa akija mara kwa mara nyumbani kumuona mjukuu wake, na kitendo cha Iryn kujifungua kilimfurahisha sana. Hakuwa na maswali mengi kuhusu malengo yangu kwa binti yake, wala hakujishughulisha na hilo. Kile kilichomgusa zaidi kilikuwa ni upendo mkubwa aliokuwa nao kwa mjukuu wake. Ilionekana kana kwamba alikuwa akitamani kwa muda mrefu sana kupata mjukuu, na sasa alikuwa akifurahia kila muda aliokuwa naye.

Saa nne asubuhi, gari lilikuja kutuchukua kwa ajili ya safari ya kwenda nyumbani kwa mzee Virgil. Tuliondoka watatu tu, mimi, Iryn, na Samantha. Safari yetu ilikuwa na umbali wa takriban kilomita 45 hadi kufika nyumbani kwa mzee, Somerset West, ambayo iko pembezoni mwa Cape Town. Huu ni sawa na umbali wa kutoka Mwenge hadi Bagamoyo. Njia ilikuwa nzuri, na tulikuwa na mazungumzo mazuri kwenye gari, tukiwa na hamu ya kufika na kumtembelea mzee.

Mzee aliamua kujenga na kuishi nje kidogo ya mji wa Cape Town, na tulivyoanza kuingia katika maeneo haya, nilikuwa nikiona majumba ya kifahari ambayo yalivutia sana macho yangu. Mazingira ya hapa ni kama Ulaya, ni masafi, na kote ni lami, hakuna vumbi. Nyumba zimepangiliwa kwa ustadi wa hali ya juu, mandhari yake ikiwa ya kijani kibichi. Wakati tunaingia Somerset, tulikuwa tukipishana na magari ya kifahari, hali iliyoongeza uzuri wa eneo hili.

Gari lilipaki nje ya geti kubwa, na haikuchukua muda mrefu likafunguliwa, ingawa pale getini hakuonekana mtu yeyote aliyefungua. Tulipofika ndani, gari lilitembea kwa mwendo wa takriban mita 100, na njiani tulipishana na bustani nzuri ya kuvutia.

Baada ya kufika usawa wa nyumba, tulishuka na mbele yangu nikaona bonge la mjengo wa kifahari, aina ya villa. Ilikuwa nyumba kubwa ya kisasa ya ghorofa moja, na kila kipengele chake kilionekana kuwa kimepangwa kwa umaridadi. Ujenzi wa nyumba hiyo ulikuwa wa kisasa na wa kuvutia, ukionyesha ushawishi wa hali ya juu wa usanifu. Ilionekana kama ni mahali pazuri pa kuishi, ambapo mandhari ya karibu iliongeza uzuri na raha ya mazingira.

Wakati huu, mama yake mdogo alitoka kutupokea akiwa na wanae, na haikuchukua muda mzee Virgil akatoka kumkaribisha binti yake. Alikuwa na furaha kubwa sana kutuona na aliomba kumbeba Aria, Mzee Virgil alionyesha upendo mkubwa kwa mjukuu wake.

Nilisikia sauti ya upole kutoka kwa Iryn ikinikaribisha kwa furaha:

“Baba Aria, hapa ndiyo nyumbani, karibu sana.”

Tulipokuwa tunaingia ndani, nilikutana na bonge la msebule uliojaa mapambo ya thamani kubwa kama crystals na marbles. Nimeingia katika nyumba nyingi za kifahari, lakini sebule ya kwa Mzee Virgil ilikuwa ya kipekee kabisa. Ukarabati wa ndani ulikuwa wa kiwango cha juu, na kila kipande cha samani na mapambo kilionyesha umaridadi na mtindo wa kipekee, ikifanya iwe mahali pa kuvutia.

Iryn alianza kunitambulisha kwa wadogo zake wa pale nyumbani kwa upande wa mama mdogo. Mama mdogo ana watoto watatu tu; mtoto wa kwanza ni wa kike, ambaye nilimfahamu nikiwa hospitalini, alikuwa akitarajia kuanza chuo mwaka huo na wawili ni wa kiume, wenye umri wa miaka 13 na 8. Walionekana kufurahia kuniona na walikuwa na shauku ya kujua kuhusu mimi, hali ambayo ilileta maongezi yawe mengi zaidi.

Baada ya lisaa, wageni watano walifika, na kati yao, mmoja tu alikuwa na asili ya Afrika; wengine wote walikuwa wazungu. Kati ya wageni hao, mmoja alikuwa ni babu, na aliomba amshike Aria. Mzee Virgil alifanya utambulisho pale, akimwambia Iryn kwamba wale ni ndugu zake. Iryn alifurahi sana kusikia hivyo, kwani kwa upande wake alikuwa kwenye mission ya kuwasogeza karibu ndugu wote wa upande wa baba yake. Hali hiyo ilileta hisia za umoja na furaha, na ilikuwa ni fursa nzuri kwa familia kukutana na kuimarisha uhusiano wao.

Tulipata chakula cha mchana pamoja, na baada ya wageni kuondoka, Iryn alitoka nje na mzee wake kufanya mazungumzo. Walionekana kuwa na mazungumzo ya karibu na ya kina, hii ilikuwa ni nafasi nzuri kwao kujadili mambo ya familia na kujenga msingi mzuri wa ushirikiano.

Wakati huu, nilikuwa na mama mdogo tukifanya mazungumzo, ambapo aliendelea kunikaribisha kwa ukarimu. Alizungumza kwa upole, akielezea furaha yake kuwa na familia pamoja na jinsi alivyovutiwa na ujio wangu.

Baada ya lisaa, Iryn aliniita nitoke nje ili tuweze kuzungumza na mzee wake. Alimweleza baba yake jinsi ambavyo nimekuwa msaada mkubwa sana katika biashara zake. Mzee wake alishukuru kwa dhati na kusema niendelee kuwa na moyo huo huo. Alionyesha furaha kubwa kwa mimi kuwa sehemu ya familia yake.

Kuhusu suala la kumzalisha binti yake, mzee hakuwa na neno lolote la kukatisha tamaa. Badala yake, alitutakia mafanikio mema na kusema angetamani kuona tukifika mbali zaidi katika maisha yetu.

Mzee aliondoka pamoja na mjukuu wake, na kutuacha mimi na Iryn tukiendelea na mazungumzo yetu. Iryn alianza kunishirikisha kuhusu kazi kubwa aliyonayo katika kuzisimamia kampuni za baba yake. Aliniambia kuhusu mali mbalimbali anazomiliki baba yake hapa Afrika Kusini, ikiwa ni pamoja na apartments, mashamba ya zabibu, na kampuni ambayo ni miongoni mwa waexporter wakubwa wa wines.

Alielezea jinsi alivyohusika katika kusimamia shughuli hizi na jinsi anavyopanga mipango ya kuziendeleza zaidi. Hali hiyo ilionyesha kiwango cha juu cha kujitolea kwake na uelewa wa biashara, na ilinipa mtazamo mzuri kuhusu familia yao na malengo yao ya kifamilia.

Tangu siku ile tulipokutana na Iryn na kuanza mahusiano yetu, hakujawahi kuwa na wakati ambapo alitaja utajiri wa baba yake. Badala yake, alijikita zaidi katika kunieleza kuhusu majukumu aliyokabidhiwa ya kuwa msimamizi wa kampuni za baba yake. (SEASON 1: EP40)

Hii ndiyo siku nilipogundua kwamba mzee Virgil si mtu wa kawaida, kwani ana utajiri wa kutisha. Lakini ukimwona, unaweza kumchukulia kuwa mtu wa kawaida sana. Kama mnavyojua, wazungu hawana tabia ya kujionesha kama wana fedha, tofauti na sisi Waafrika, ambao mara nyingi tunapenda maonyesho ya kifahari.

Iryn aliendelea kunieleza jinsi mzee wake alivyotokea kunikubali sana. Aliniambia kwamba amemshauri atulie nami, kwani kwa sasa wanaume wengi hawaaminiki. Maneno hayo yalikuwa ya faraja kutoka kwa Iryn, yakiwa na uzito wa maana. Nilimuhakikishia kuwa nitajitahidi kumsaidia kadri ya uwezo wangu, kwa sababu uaminifu ni msingi wa mahusiano yetu.

Nilimuuliza Iryn kuhusu mgawanyo wa mali za mzee na jinsi anavyowaangalia watoto wengine, wakiwemo Smith na kaka yake mkubwa, ambapo jumla yao ni watoto sita wa mzee Virgil. Iryn alijibu kwamba hadi sasa, watoto wanne tu wanatambulika rasmi, ambao ni yeye pamoja na wadogo zake watatu kwa upande wa mamdogo. Aliongeza kuwa kuhusu kaka yake na Smith, bado hawajazungumza na mzee wao kuhusu suala hilo, lakini wanatarajia kuangalia namna nyingine ya kufanikisha mambo yao.

MIMI: “Na vipi kuhusu mama mdogo?”

IRYN: “Mama mdogo si mmoja wa mrithi wa hizi mali. Alifunga ndoa ya mkataba na mzee, na moja ya makubaliano ni kwamba hatahusika kwenye urithi wa mali zaidi ya watoto tu.”

MIMI: “Baba yako ni genius sana.”

IRYN: “Mali nyingi sana mzee kazipata akiwa na mama yangu. Ndiyo maana unaona mimi nikiwa kipaumbele cha kwanza, hata wakati ambapo hatuko kwenye maelewano na mzee. Kwa upande wake, alikuwa anapata tabu sana kuhusu hili.”

Iryn alikuwa huru kunifungukia mambo mengi sana. Alisema kwamba hata kitendo cha kuzaa na mimi si kwamba alikurupuka tu kufanya maamuzi hayo, bali alifikiria kuhusu mustakabali wake na mali za baba yake. Alieleza kwamba kipindi kile baada ya kurudi kutoka South Africa kumwona mzee wake, aliona kuna umuhimu wa kuwa na watoto ambao wataweza kurithi mali hizo, kwani hata yeye atakufa.

Iryn alifikiria kwa kina na kugundua kwamba hakuna mtu anayemuamini zaidi yangu kwa sasa. Alijisemea atafanya kila mbinu ili anizalie mtoto, lakini lengo lake kubwa ni kuhakikisha urithi wa mali za baba yake unakuwa salama. Aliendelea kueleza kwamba, mama mkubwa wake na ndugu zake wanamuona kama mjinga sana, lakini hawajui mipango yake ya siri. Hakuwa na nia ya kuona mali ambazo mama yake alizichuma na baba yake zikipotea kwa watoto wengine. Kwa hiyo, alichukua maamuzi haya magumu, lakini yaliyojikita katika manufaa ya kizazi chake.

Nilishusha pumzi ndefu sana, nikijisemea kwamba kumbe Iryn yuko very calculated na alikuwa na mipango mikubwa ambayo sikuwa na habari nayo. Nilikuwa bado siamini kwamba Iryn anaweza kubeba mimba kwa sababu ya kijinga kama aliyokuwa akinambia, lakini leo ndiyo nimeelewa kuwa alikuwa anawaza extra miles. Iryn alikuwa na malengo ya dhati, na sasa nilianza kuelewa uzito wa maamuzi yake.

IRYN: “Baba Aria, naomba nisamehe sana kwa kutokushirikisha hili mapema, nilijua ipo siku ungekuja kujua ukweli. Nilikuwa nauwezo wa kuzaa na mwanaume yoyote yule ninayemtaka hata kwa kumlipa na nikapata mtoto, lakini niliona wewe ndio unafaa.”

MIMI: “Naomba tuachane na haya, Aria ni mtoto wetu tuangalie namna gani ya kumlea na kumtunza ili tuje tujisifu kuwa naye.”

IRYN: “Babu yake kafurahi sana kumuona, ndio mjukuu wake wa kwanza. Pia unakumbuka nilikwambia kuhusu afya ya mzee wangu? Hana maisha marefu sana hapa duniani ni pesa tu zinafanya anaendelea kuishi.”

MIMI: “Nakumbuka baby, naamini ataishi muda mrefu zaidi hapa duniani, tusichoke kumuombea.”

IRYN: “Natamani kupata mtoto mwingine, hata nikiwa natembea barabarani, kushoto nina Aria na kulia nina mdogo wake nakuwa na bodyguards wangu.”

MIMI: “Naona unanipa greenlight ya kukupa mimba ya pili.”

IRYN: “Yes! Why not, unafikiri atakuwa nani zaidi yako?”

MIMI: “Sawa baby subiri kwanza Aria akue mengine tutapanga.”

Baada ya mazungumzo marefu, tulianza kutembea na kutalii mazingira ya nyumba yao. Aisee, nyumba yao imezungukwa na bustani nzuri, huku ukubwa wa kiwanja ukiwa kama ekari tano. Tuliposhuka chini, tulikuta mizabibu mingi imepandwa, kuzunguka upande wa nyuma nakutana na swimming pool mbili, moja ya wakubwa na nyingine kwa ajili ya watoto. Nyumba hiyo ilikuwa na mvuto wa kipekee, na mbele zaidi kulikuwa na nyumba ndogo ya wafanyakazi ambao kazi yao ni kutengeneza zile bustani na kumwagilia mimea.

Nilishindwa kuelewa kwanini Iryn ameshindwa kukaa na baba yake na ameamua kupanga aishi peke yake. Sikutaka kumuuliza kuhusu hili, kwani nilijua Iryn ana akili sana na huwa hafanyi jambo lolote bila sababu. Nilihisi kuwa kuna mambo mengi nyuma ya uamuzi wake, lakini kwa heshima yake, niliona bora nisubiri hadi atakapojisikia kuzungumzia.

Saa mbili usiku, tulipata dinner ya pamoja, na baada ya hapo tuliagana kuwa tunaondoka. Walitusindikiza hadi nje, ambapo dereva alikuwa amekuja kutufuata tayari. Tukiwa pale nje, mzee aliendelea kuongea na binti yake, na nilipata fursa ya kubaini upendo mkubwa sana alionao kwa Iryn. Mazungumzo yao yalionyesha uhusiano wa karibu na wa kipekee kati yao, na ilikuwa wazi kwamba Iryn alikuwa na nafasi maalum katika moyo wa baba yake.

Dereva aliyekuwa amekuja kutufuata ni ameajiriwa na mzee na kazi yake ni kwaajili ya kuwapeleka watoto shule na kuwarudisha, au kuwapeleka matembezini.

*****

Wiki ya tatu, nilipanga kuondoka Cape Town siku ya Ijumaa, nikijitayarisha kurudi Dar es Salaam na kuendelea na ratiba zangu za kila siku. Hata hivyo, nikiwa South sikuwa na kazi yoyote ya kufanya zaidi, nilijikuta nikicheza sana na Aria, kwani hiyo ndiyo ilikuwa shughuli pekee iliyonipa furaha na kunifanya nijisikie hai.

Kwa upande wa Mary, mawasiliano yetu yalikuwa yanaendelea vizuri, na yeye kwa upande wake alionyesha wazi hamu ya kuniona na alitaka anione mapema iwezekanavyo. Alikuwa akiendelea kuniambia kwa kusisitiza ni kwa sababu ya kutamani kuungana tena na mimi, na alilalamika kidogo kuhusu kuchelewa kwangu kurudi.

Siku ya Jumatano, nilitoka na Iryn kwenda kukagua biashara yake ya saloon, ambayo ni kubwa sana na ina wafanyakazi wengi. Iryn alionekana kuguswa sana na hali ya wafanyakazi, akilalamika kuhusu jinsi watoto wa South walivyo wavivu katika kazi zao. Alisema anafikiria kuandaa mpango wa kuajiri watu kutoka nchi za jirani ili kuongeza ufanisi na kuleta mabadiliko chanya katika biashara yake.

Ijumaa usiku, kabla ya safari yangu, nilikuwa na mazungumzo ya mwisho na baby mama yangu. Katika mazungumzo yetu, habari kubwa aliyonipa ilikuwa kuhusu kufuatilia kampuni ya mzee wake, ambayo alidhulumiwa na wabongo. Alionyesha wasiwasi kuhusu jinsi anavyoweza kusaidia katika kurejesha haki na kuleta uwazi katika mambo haya.

Nakumbuka niliwagusia kidogo kuhusu kampuni za ujenzi na umeme ambazo baba yake alikuwa anazimiliki hapa Dar es Salaam, mwanzoni mwa Season 1: EP 10. Baada ya Rais JPM kuingia madarakani mambo yalibadilika kwa kiasi kikubwa, hasa katika masuala ya tenda na kuamua kufunga kampuni na kurejea South ili kuendeleza kampuni zake zingine, huku akikabiliana na changamoto nyingi kutokana na mabadiliko hayo.

Kuna kampuni moja ya masuala ya electronics ambayo baba yake aliiacha, lakini wabongo wazee wa fursa walicheza na umiliki wake. Ingawa mzee wake alionekana kupotezea suala hilo, Iryn alisisitiza kwamba hali hii haiwezekani na alitaka kuchukua hatua dhidi ya watu waliofanya uhuni huo. Alijua kuwa alikuwa na hati zote zinazohitajika, na hivyo alikusudia kudeal na wahusika ili kurejesha haki na kumaliza tatizo hilo.

Iryn alinikabidhi hati zote na kuniagiza nianze kufuatilia suala hili pamoja na mwanasheria. Alinisihi sana kuhakikisha tunafanikiwa katika juhudi hizi. Aliongeza kuwa atarudi Tanzania mwezi Desemba kuangalia maendeleo ya kesi hiyo, na pia tutajadili kuhusu mradi wa kufanya Dodoma. Alionekana kuwa na matumaini kwamba kwa pamoja tunaweza kupata suluhisho na kuendeleza mipango yetu ya baadaye.

Niliingia chumbani kujiandaa, na Iryn alinifuatia kwa nyuma, akinikumbatia huku akizungusha mikono yake mbele yangu. Tulianza kukumbatiana kwa mahaba mazito, na hisia zangu zilianza kuwa na nguvu sana, kwani ilikuwa muda mrefu sijaonja ile furaha. Hali yangu ilizidi kuwa mbaya, nikijua jinsi nilivyokuwa na tamaa ya kuwa karibu naye.
Tulianza kupigana makisi ya mwisho mwisho lakini sikuwa na uwezo wa kufanya chochote, sababu ya afya yake. Alichokifanya mama mtoto, alikoki RPG kwa mkono wake laini, hadi pale ambapo risasi za moto zilipotoka kwa kasi.

Nilihisi mabadiliko katika mwili wangu, na nikapata wepesi wa haraka. Tulikwenda kuoga pamoja, na nilijiandaa kwa haraka ili niweze kuongea kidogo na Momo na kumuaga kabisa. Nilitaka kuhakikisha kuwa kila kitu kiko sawa kabla ya kuondoka.

Nilimshukuru Momo kwa uwepo wake nyumbani, kwani alikuwa anatusaidia sana kucheza na mtoto. Nilimuaga kwa kumkiss shavuni, na kisha tukaanza safari yetu kwenda airport. Niliongozana na Iryn pamoja na Samantha, ambao walinipa kampani na njiani tulikuwa tunapiga story za mwisho.

Baada ya kufika uwanja wa ndege, niliagana na mama Aria, kwani sikutaka aanze kunisubiri hadi nimalize mchakato wa kucheck-in. Sikuona haja ya wao kufanya hivyo. Nilianza kwa kumkumbatia Samantha, na nikamalizia kwa kumkumbatia mama mtoto. Cha ajabu, alinionyesha upendo kwa kunipa na ulimi, na hiyo ilileta hisia mpya za mshangao na furaha.

Saa 7 usiku, safari yangu ya kurudi Dar es Salaam ilianza, na njiani kote nilikuwa na furaha sana. Nikiwa kwenye ndege, mawazo yangu yalizunguka kuhusiana na watoto wangu, Junior na Aria. Nilitamani sana kuona wanangu wakianza kujuana mapema na kutembeleana, kwani ni damu zangu. Nikaona kuna umuhimu wa kumtafuta mzee wangu na kumshirikisha kuhusu jambo hili mapema ili kila kitu kiwe wazi. Nilijisemea, "I'm running out of time; let me do this." Hali hiyo ilinipa msukumo wa kutenda haraka ili kuhakikisha familia yangu inakuwa na muungano mzuri.

THE END OF SEASON 2

Thank you for your time!
20241002_075529.jpg


Tafadhali mkuu naomba tuyajenge PM
 
BONUS CHAPTER 1

Nimeanza kuandika story hii nikiwa South Africa, ule wakati ambao nilikuwa na muda wa ziada, ndipo nilipoanza kuandika Season 1 na kuwapostia. Lengo langu kuu ni kuwapa ujumbe kuhusu safari ya maisha yangu, kutoka mwanzo hadi sasa, maisha ambayo bado ninaishi. Sikutaka kukata tamaa, hata baada ya kumaliza mkataba wangu na taasisi X niliamua kujiingiza kwenye uber, huku ndo nilikopata mafanikio makubwa sana.

Nilichowaandikia ni kama asilimia 30 ya maisha yangu; bado kuna mengi ambayo sijagusia kutokana na sababu za usalama wangu pia.

Kwa ufupi, tangu Iryn alipojifungua, maisha yangu yalianza kubadilika kwa kasi sana. Niliamua kuelekeza nguvu zangu kwenye familia zangu na kujituma zaidi kutafuta hela kwa bidii.

Mwezi Januari 2024, nilikutana na mzee na kumueleza kuhusu suala la kuzaa na Iryn. Alishtushwa sana na habari hizi, na hakusita kunilaumu vikali juu ya hilo. Hata hivyo, nilijitahidi sana kujitetea, hasa kwa kutumia mbinu nzuri ambazo Sister aliniambia.

Mzee aliweza kuelewa hali halisi, na mwezi Februari mwaka huu alikutana na Iryn. Tulienda Zambia kwa ajili ya hili, na baada ya kumuona Aria, mzee alikiri kwamba ni damu yetu. Changamoto iliyobaki sasa ni namna ya kumwambia mama yangu mzazi. Tumepanga kumtaarifu mwezi huu, na safari hiyo itakuwa mimi, mzee, na sister.

Kuhusu mama J, tuko shwari kabisa, na upendo kati yetu umeendelea kukua kwa kasi; tunapendana sana. Junior mwaka huu alianza shule na anaendelea kufanya vizuri sana darasani. Kampuni ya Masaki bado ipo na inaendelea kufanya vizuri sana, na pia mama mtoto amefungua biashara nyingine hapa Dar es Salaam.

Kuhusu mtoto wetu Aria, sasa ana mwaka mmoja na miezi mitatu, na tumefanana sana. Ninajitahidi kumtembelea mara kwa mara kule South, hata wiki iliyopita nilikuwa huko kumuona.

Habari njema nyingine ni kwamba mwezi wa tisa huu ninatarajia kupata mtoto wa pili na Iryn. Baada ya kuja Disemba mwaka jana, tulikutana na hali hiyo ikapelekea kushika mimba. Ingawa hatukupanga hili, hatukuwa na namna zaidi ya kukubaliana yeye kuzaa. Hali hii imefanya niwe nasafiri mara kwa mara kwenda South Africa.

Kuhusu Mary, alipata kazi Mwanza katika moja ya taasisi nyeti inayoshughulika na masuala ya BOP. Hatuko kwenye mahusiano ya kimapenzi rasmi, lakini bado tunakutana kisela.

Mipango yangu ni kuhakikisha kwamba kufikia mwakani kila kitu kiwe wazi kwa mama J. Hata hivyo, hili linasubiri wazazi watoe maamuzi, kwani tunasubiri kuona mama atachukua hatua gani akijua ukweli. Nia yangu ni kumuoa mama J kwa kufunga naye ndoa, lakini hilo litafanyika tu endapo atajua ukweli na kukubali kwa hiari yake.

Mbali na mama J, pia nina mpango wa kumfanya Iryn awe mke wangu wa pili. Sijui wazazi watasema nini kuhusu hili, lakini anatarajia kupata mtoto wa pili. Hali hii inahusisha majadiliano mazito na maamuzi ambayo ni muhimu kabla ya kuchukua hatua zozote.

Nitarudi kuwapa hadithi fupi pale ambapo nitamuweka wazi mama J kuhusu hili suala. Sijui itakuwa lini—labda mwakani au baada ya miaka miwili au mitatu. Lakini nitawapa mrejesho wa kilichotokea kwa kuwapa Season 3 au lah. Nitawapa muendelezo wa mambo yalivyokuwa, kuanzia niliporudi Dar es Salaam mwezi Julai 2023. Hapa katikatika nimepitia mambo mengi sana, hadi sasa ni vile hamjui kinachoendelea nyuma ya pazia, kumekuwa na vikao vingi sana.

Mwisho kabisa, mwakani Mungu akijalia nitaondoka Tanzania na familia yangu kwenda kufanya kazi nje. Jambo la muhimu tuendelee kuombeana uzima na mapambano mema, tuache chuki na Roho mbaya.

Bonus, inayokuja tutachambua wote fursa zinazopatikana Dar es Salaam na huenda nikawa na thanks giving kwa baadhi ya watu watakao bahatika, nikaangalia namna ya kuwa support kwenye harakati zao. Lakini hadi kufikia sasa nimeshatoa kwa watu wengi tu, ambao walikuwa wanakuja inbox na sababu zilizonyooka, na wengi ni matapeli.

Tukutane kesho!
Hongera.
Mama j akikubali muoe kanisani.kisha iryn muoe kimila basi
 
BONUS CHAPTER 1

Nimeanza kuandika story hii nikiwa South Africa, ule wakati ambao nilikuwa na muda wa ziada, ndipo nilipoanza kuandika Season 1 na kuwapostia. Lengo langu kuu ni kuwapa ujumbe kuhusu safari ya maisha yangu, kutoka mwanzo hadi sasa, maisha ambayo bado ninaishi. Sikutaka kukata tamaa, hata baada ya kumaliza mkataba wangu na taasisi X niliamua kujiingiza kwenye uber, huku ndo nilikopata mafanikio makubwa sana.

Nilichowaandikia ni kama asilimia 30 ya maisha yangu; bado kuna mengi ambayo sijagusia kutokana na sababu za usalama wangu pia.

Kwa ufupi, tangu Iryn alipojifungua, maisha yangu yalianza kubadilika kwa kasi sana. Niliamua kuelekeza nguvu zangu kwenye familia zangu na kujituma zaidi kutafuta hela kwa bidii.

Mwezi Januari 2024, nilikutana na mzee na kumueleza kuhusu suala la kuzaa na Iryn. Alishtushwa sana na habari hizi, na hakusita kunilaumu vikali juu ya hilo. Hata hivyo, nilijitahidi sana kujitetea, hasa kwa kutumia mbinu nzuri ambazo Sister aliniambia.

Mzee aliweza kuelewa hali halisi, na mwezi Februari mwaka huu alikutana na Iryn. Tulienda Zambia kwa ajili ya hili, na baada ya kumuona Aria, mzee alikiri kwamba ni damu yetu. Changamoto iliyobaki sasa ni namna ya kumwambia mama yangu mzazi. Tumepanga kumtaarifu mwezi huu, na safari hiyo itakuwa mimi, mzee, na sister.

Kuhusu mama J, tuko shwari kabisa, na upendo kati yetu umeendelea kukua kwa kasi; tunapendana sana. Junior mwaka huu alianza shule na anaendelea kufanya vizuri sana darasani. Kampuni ya Masaki bado ipo na inaendelea kufanya vizuri sana, na pia mama mtoto amefungua biashara nyingine hapa Dar es Salaam.

Kuhusu mtoto wetu Aria, sasa ana mwaka mmoja na miezi mitatu, na tumefanana sana. Ninajitahidi kumtembelea mara kwa mara kule South, hata wiki iliyopita nilikuwa huko kumuona.

Habari njema nyingine ni kwamba mwezi wa tisa huu ninatarajia kupata mtoto wa pili na Iryn. Baada ya kuja Disemba mwaka jana, tulikutana na hali hiyo ikapelekea kushika mimba. Ingawa hatukupanga hili, hatukuwa na namna zaidi ya kukubaliana yeye kuzaa. Hali hii imefanya niwe nasafiri mara kwa mara kwenda South Africa.

Kuhusu Mary, alipata kazi Mwanza katika moja ya taasisi nyeti inayoshughulika na masuala ya BOP. Hatuko kwenye mahusiano ya kimapenzi rasmi, lakini bado tunakutana kisela.

Mipango yangu ni kuhakikisha kwamba kufikia mwakani kila kitu kiwe wazi kwa mama J. Hata hivyo, hili linasubiri wazazi watoe maamuzi, kwani tunasubiri kuona mama atachukua hatua gani akijua ukweli. Nia yangu ni kumuoa mama J kwa kufunga naye ndoa, lakini hilo litafanyika tu endapo atajua ukweli na kukubali kwa hiari yake.

Mbali na mama J, pia nina mpango wa kumfanya Iryn awe mke wangu wa pili. Sijui wazazi watasema nini kuhusu hili, lakini anatarajia kupata mtoto wa pili. Hali hii inahusisha majadiliano mazito na maamuzi ambayo ni muhimu kabla ya kuchukua hatua zozote.

Nitarudi kuwapa hadithi fupi pale ambapo nitamuweka wazi mama J kuhusu hili suala. Sijui itakuwa lini—labda mwakani au baada ya miaka miwili au mitatu. Lakini nitawapa mrejesho wa kilichotokea kwa kuwapa Season 3 au lah. Nitawapa muendelezo wa mambo yalivyokuwa, kuanzia niliporudi Dar es Salaam mwezi Julai 2023. Hapa katikatika nimepitia mambo mengi sana, hadi sasa ni vile hamjui kinachoendelea nyuma ya pazia, kumekuwa na vikao vingi sana.

Mwisho kabisa, mwakani Mungu akijalia nitaondoka Tanzania na familia yangu kwenda kufanya kazi nje. Jambo la muhimu tuendelee kuombeana uzima na mapambano mema, tuache chuki na Roho mbaya.

Bonus, inayokuja tutachambua wote fursa zinazopatikana Dar es Salaam na huenda nikawa na thanks giving kwa baadhi ya watu watakao bahatika, nikaangalia namna ya kuwa support kwenye harakati zao. Lakini hadi kufikia sasa nimeshatoa kwa watu wengi tu, ambao walikuwa wanakuja inbox na sababu zilizonyooka, na wengi ni matapeli.

Tukutane kesho!
Mkuu, Hali uliyonayo inaonekana kuwa na changamoto nyingi za kihisia, kijamii, na kifamilia. Kuna masuala mazito ya uwazi, mawasiliano, na uamuzi wa kimaadili ambayo yanahitajika kushughulikiwa kwa umakini ili kuepusha madhara ya baadaye.


Baadhi ya mambo ya kuzingatia na ushauri juu ya nini kifanyike:


MAMA NA SAFARI YA KUUJUA UKWELI.


Mkuu,kupitia story yako, yaonekana kwamba mama Ni mtu wa imani Sana (dini) hivyo, kumueleza kuhusu hali hii itahitaji mbinu za busara, kwa heshima na uangalifu mkubwa. Hapa kuna hatua kadhaa unazoweza kuchukua:


1. Maandalizi ya Kihisi

Kutokana na kushikilia dini, mama anaweza kuwa na matarajio makubwa ya kimaadili kwa mtoto wake. Hivyo, ni muhimu kumwandaa kisaikolojia kabla ya kumwambia ukweli wote.


Nini ufanye:

Baba yako, ambaye tayari anajua, anaweza kusaidia katika kumwandaa mama kihisia. Wanapaswa kwanza kumtambulisha mama kwenye hali ya jumla ya maisha ya mtoto wao kabla ya kuingia kwenye undani wa suala la wake wawili.


2. Kuzingatia Dini na Maadili

kwa kuwa mama ni mtu wa dini, unapaswa uzingatie jinsi ya kumueleza kwa mtazamo wa kidini pia. Wewe si malaika una mwili wa nyama na damu kabisaa na Kama tujuavyo, Dini nyingi zinahimiza ukweli, uwazi, na kutubu kwa kosa lolote. Ni muhimu uonyeshe kwamba una nia ya kufanya mambo kwa njia sahihi na ya kidini, hata kama kuna makosa yaliyotokea.


Nini kifanyi:

Unaweza kueleza hatua ulizochukua kurekebisha hali hiyo na kuonyesha nia ya dhati ya kuunda familia yenye mshikamano. Hii inaweza kusaidia kumshawishi mama kuona kuwa, japokuwa mambo hayakuwa sahihi mwanzoni, lakini uko tayari kufuata njia stahiki.


3. Kumshirikisha Baba

Baba, ambaye tayari amekubali hali halisi, anaweza kuwa na jukumu kubwa la kusaidia kufikisha habari hizi kwa mama. Ikiwa mama ana uhusiano mzuri na baba, baba anaweza kuwa mtu wa kwanza kumwambia ili kumtuliza au kumsaidia kuelewa kabla ya kijana wake kujieleza.


Nini kifanyike

Baba na kijana wake mnaweza kushirikiana kumuandaa mama kwa njia ya upole, polepole wakimtoa kwenye hali ya mshtuko.


4.Kuomba Msamaha na Uelewa

Kwa kuwa mama anaweza kuona hili kama kosa kubwa, ni muhimu kuwa na unyenyekevu na kuomba msamaha kwa jambo hilo. Hii inaweza kusaidia kupunguza ukali wa hisia.


Nini kifanyike

Mkuu, unaweza kumwomba mama msamaha kwa kumficha ukweli kwa muda mrefu na kuelezea kwa uwazi jinsi ulivyokuwa na wakati mgumu kulishughulikia suala hili. Hii inaweza kusaidia mama kuelewa changamoto za kijana wake na labda kumsaidia kupita kipindi hiki. Asikuambie mtu mkuu, mama ni mama,na mapenzi juu ya watoto wake hayapimiki, ingawa sio wote, ila Kariba na hulka ya mama yako(kupitia simulizi hii) Atakuelewa tu


5. Kutoa Muda wa Kutafakari

Mama anaweza kuchukua muda mrefu kukubali hali hiyo, hasa kutokana na imani yake ya dini. Hivyo, huwezi kutarajia kukubaliwa mara moja, lakini unaweza kumpa muda wa kutafakari na kupunguza presha. Atakapo lijua hili swala, mpe mama nafasi ya kuchakata habari hizo bila kumlazimisha kukubali haraka. Kuwa mvumilivu na mwenye kuonyesha upendo.


Kwa ujumla, kumweleza mama kutahitaji uwazi, heshima, na uvumilivu mwingi. Ni muhimu kumwonyesha kuwa, licha ya changamoto zilizopo, una nia ya kufanya mambo kuwa bora zaidi.



SAKATA LA MAMA J


Mkuu, changamoto kuu inabaki kuwa namna ya kumwambia Mama J ukweli kuhusu uwepo wa Iryn na watoto waliopo nje. Binafsi, namwona Huyu ndio nahodha, ndio last kadi.


Hii ni hali nyeti sana, kwani kumwambia mke wa kwanza ukweli kuhusu jambo kubwa kama hili kunaweza kusababisha mshtuko, maumivu, au hata kuvunja uaminifu kati yenu. Ili kupunguza madhara, hapa kuna hatua unazoweza kuchukua:


1.Kujitayarisha Kihisia na Kiakili.

Kabla ya kumwambia Mama J, yeye mwenyewe lazima awe tayari kihisia kwa majibu yoyote atakayoyapata (hapa naona ulishaanza kulifanyia kazi).


Mama J anaweza kukasirika, kuumia, kuachika au hata kuchanganyikiwa. Ni lazima uwe tayari kwa hali zote hizo na kuhakikisha kuwa upo thabiti kumueleza ukweli kwa upendo na huruma.


Nini kifanyike

Jiandae kwa mazungumzo hayo kwa kutafakari na kuwa na mpango wazi juu ya namna ya kuwasilisha taarifa hiyo kwa njia isiyo ya mshtuko mkubwa (rejea ushauri wa dada yako; kisaikolojia, alikushauri vizuri).


2.Kumwambia Ukweli kwa Wakati Mzuri


Mda na Wakati wa kutoa habari hizi ni muhimu sana. Ni lazima uchague muda mwafaka ambapo mama J yuko katika hali ya utulivu wa akili na kihisia, ili aweze kushughulikia habari hizo kwa busara.


Uongee na Mama J wakati ambapo hana msongo wa mawazo au changamoto nyingine zinazoweza kuongezeka kwa wakati huo. Ni bora kuepuka kumwambia habari hizo wakati wa ugomvi au changamoto za maisha.


3.Uwazi na Uelewa

Unaweza kumwambia Mama J ukweli kwa njia ya uwazi, ukijaribu kuelezea kwa undani changamoto ulizokutana nazo na jinsi ulivyofika kwenye hali ya kuwa na mke wa pili (Iryn). Muhimu zaidi ni kuelezea sababu zako za kufanya maamuzi hayo bila kumlaumu Mama J au kumfanya aone kana kwamba ameshindwa.


Anza kwa kuonyesha upendo na kujali kwa Mama J, kisha kwa utulivu uelezee hali nzima: "Nimekuwa na jambo gumu moyoni mwangu ambalo nimekuwa nikilitafakari kwa muda mrefu. Naona ni vyema uwe na haki ya kujua ukweli kuhusu maisha yetu." Ukiendelea, unaweza kueleza juu ya Iryn, mtoto wao, na jinsi hali ilivyokuwa hadi sasa.


4.Kujieleza kwa Msamaha na Unyenyekevu.

Ukweli huu unauma, na ni lazima aelewe maumivu atakayosababisha. Hivyo, kujieleza kwa unyenyekevu na kuomba msamaha kwa kumficha Mama J kwa muda mrefu ni hatua ya kwanza muhimu.


Elezea kwa lugha ya msamaha, ukijua kwamba umemuweka Mama J katika hali ngumu bila kujua ukweli: "Nisamehe kwa kutofanya hivi mapema. Nilijua ni jambo gumu na sikutaka kuumiza hisia zako, lakini najua ulikuwa na haki ya kujua."


5.Kutoa Nafasi ya Hisia Zake.

Baada ya kumwambia ukweli, ni muhimu kumruhusu Mama J kuonyesha hisia zake. Atakuwa na mchanganyiko wa hisia: hasira, huzuni, au hata machungu. Ni lazima utoe nafasi ya kusikiliza kwa utulivu bila kuingilia au kujitetea sana wakati huo.


Katika kipindi hiki Ni muhimu sana kumhakikishia kwamba bado unampenda na kwamba ulitaka kumwambia ukweli kwa sababu unaheshimu ndoa( mahusiano) yenu.


6. Kushirikisha Msaada wa Nje.

Mkuu, point 2-5 unafanya endapo unaona waweza kulimudu peke yako, lakini kiuhalisia inawezekana ila Ni ngumu Sana, na probability yakuachana/kuvunjika kwa mahusiano yenu inakuwa kubwa Sana. NASHAURI kutokumuelezea peke yako, ila Kama dada alivyoshauri, unamuandaa kiaina Lengo Ni kupunguza NGUVU YA KUJUA KUTOKA KUTOKUJU


Katika Hali hii naona umuhimu wa kikao na mshauri/washauri wa familia ili kuzungumza hili kwa utulivu zaidi. Ushauri wa kisaikolojia pia unaweza kumsaidia Mama J kukabiliana na mshtuko huo (dada ako naona yupo vizuri Sana kwa hili, na ukizingatia kuwa wanaelewana Sana, hata Kama mama j atajua kuwa dada ako alijua mapema na hakumwambia, halitakuwa tatizo kubwa kwa dada ako kulisolve na kumweka sawa).


Kutoa Muda wa Kurekebisha Ni muhimu Sana Kwani Mama J, atahitaji muda kuchakata habari hizi na kuelewa hali halisi. Ni muhimu asilazimishwe au kushinikizwa kukubali mara moja. kuachiwa muda wa kutafakari Ni muhimu sana na kisha mtaongea zaidi baada ya Mama J kuwa tayari..


NB: Njia bora ni Mama J kuambiwa UKWELI MAPEMA na mtu wa karibu ndani ya familia yako, kabla hajasikia kutoka nga'mbo ya mbali. Na hapa aambiwebukweli kwa upole, huruma, na kujiandaa kwa majibu yoyote utakayopata. Uwazi, unyenyekevu, na uvumilivu ni muhimu ili kuhakikisha kwamba unaweka msingi mzuri wa kuendelea mbele bila kuvunja zaidi uhusiano wao.


NANI WA KUFANYA HIYO KAZI


(Binafsi nadadavua mapendekezo kadha wa kadha ila Kama ulivyosema hii ni 30% tu ya ulichosema hivyo wewe ndie Steringi, unafanya unachoona kipo sawa kwa mazingira uliyojayo)



Mtu anayepaswa kumwambia mama j UKWELI anapaswa kuchaguliwa kwa busara ili kuepusha mshtuko mkubwa na kumrahisishia kuelewa hali halisi. Hapa kuna vigezo vya kuzingatia kuhusu nani wa kumwambia:


1.Baba.

Baba yako anaweza kuwa chaguo zuri kwa sababu anajulikana kwa kuwa na busara, mamlaka, na anaweza kumwambia Mama J kwa njia ya upole na kueleweka. Kwa kawaida, baba anaweza kuchukua jukumu la kueleza hali hiyo kwa namna itakayomlinda mtoto wake (wewe) na kusaidia kufafanua kwamba ni suala ambalo limezingatiwa kwa uzito.

Faida:

✓Ana mamlaka zaidi katika familia, hivyo maneno yake yanaweza kukubalika kwa urahisi.

✓Anaweza kutumia uzoefu wake kuelezea mambo kwa upole na uelewa.


Changamoto:

✓ Ikiwa baba hana uhusiano wa karibu na Mama J, huenda ikawa vigumu kumfikisha ujumbe kwa ufanisi.


2.Mama

Mama yako anaweza kuwa na nafasi nzuri kumwambia Mama J kuhusu hali hii, kwani anaweza kuleta huruma na uelewa wa kina. Ikiwa ana uhusiano mzuri na Mama J, anaweza kumsaidia kupokea habari kwa namna isiyo ya mshtuko na yenye kueleweka zaidi.


Faida:

✓ Anaweza kutumia huruma ya kike na kuelewa hisia za Mama J

✓ Ikiwa ana uhusiano mzuri na Mama J, atasaidia kumtuliza kihisia na kumtia moyo.


Changamoto:

✓ Ikiwa mama yako ni mkali au mwenye mtazamo mkali, anaweza kuleta mvutano badala ya kumsaidia Mama J kupokea habari hizo kwa utulivu.


3. Dada

Dada anaweza kuwa chaguo zuri ikiwa ana uhusiano wa karibu na Mama J na anaweza kumweleza kwa upole na uelewa. Anaweza kumsaidia kwa namna ya kisaikolojia na kihisia, kwani anatambulika kama rafiki na mshirika wa karibu wa familia.


Faida:

✓ Ikiwa ana uhusiano wa karibu na Mama J, anaweza kumweleza kwa njia ya rafiki na isiyo rasmi.

✓ Anaweza kueleza kwa upole na msaada wa kihisia, ikiwezekana akiwa na huruma na upendo.


Changamoto:

✓Dada anaweza kukosa mamlaka au uzito wa kutoa habari hiyo kwa namna ambayo itamfanya Mama J aelewe ukubwa wa hali hiyo.



Uamuzi:

Kwa hali hii, baba anaonekana kuwa chaguo bora zaidi kwa sababu anaweza kuelezea kwa busara na kutumika kama kiunganishi kati yako na Mama J. Ikiwa baba ataungana na mama, inaweza kuwa na uzito zaidi, ambapo mama atasaidia kwa huruma na uelewa zaidi.


Hata hivyo, kumchagua mtu wa kumwambia Mama J kunategemea uhusiano uliopo kati ya Mama J na mtu huyo. Kumbuka, lengo ni kuhakikisha anaambiwa kwa njia ya heshima, utulivu, na huruma ili kuepusha mshtuko mkubwa.


Pendekezo:

Kama kuna uhusiano mzuri kati ya Mama J na mama, baba na dada waambie wote waongee naye pamoja. Baba atatoa uzito wa suala hilo, na mama atatoa faraja ilihali dada atatoa msaada wa kihisia na kisaikolojia.


Upande wa familia ya mama J haitakuwa tabu Sana Kama mama J Atakuelewa na kukubaliana nawe.




SHNIKIZO LA NDOA

(NB: hili Ni baada ya mama J kujua ukweli na kukubaliana nao)


Kushughulikia shinikizo kutoka kwa familia ya Irene na Mama J, ambao wote wanasisitiza ndoa, ni changamoto kubwa, lakini hapa kuna njia kadhaa unazoweza kutumia ili kuleta usawa na kuepuka migogoro mikubwa:


1.Weka Kipaumbele katika Uwazi na Maelewano

Ili uweze kushughulikia hali hii kwa usawa, lazima aluwe muwazi kwa pande zote mbili na jaribu kuleta maelewano kati ya wake hao wawili watarajiwa. Ni muhimu kwa kila mmoja wao kuelewa kuwa unawapenda na unawathamini wote. Uwazi utakusaidia kuondoa dhana za wivu au mashaka kwa pande zote mbili.


Ongee na kila mmoja kwa uwazi kuhusu hali ya ndoa mbili na lengo lako la kuhakikisha kuwa wote wanafurahia ndoa hiyo.


2. Kuzungumza na Wazazi wa Pande Zote.


Kwa kuwa wazazi wa Irene na wazazi wa Mama J wanataka ndoa zao zifungwe, ni vyema kukaa nao na kuwapa ufafanuzi juu ya hali nzima. Unapaswa kuwaomba wazazi uvumilivu huku akijipanga kwa hatua sahihi bila kuchanganya hisia za wake wako wawili.




Unapaswa kuandaa vikao na wazazi wa pande zote mbili na kuwaambia wazi kuhusu nia yako ya kuwaoa wote wawili, lakini kwa mpangilio mzuri na wa busara. Anaweza kuomba msaada wa wazazi hao katika kuratibu taratibu hizo bila kuzidisha mgogoro.


3.Kuchagua Njia Sahihi ya Ndoa

Ikiwa una nia ya kuwaoa wake wote wawili, ni muhimu kufikiria ni taratibu gani za ndoa zitafuatwa na jinsi gani anaweza kufanya hili kwa uwiano bila kuonekana kama anabagua. Katika baadhi ya tamaduni na dini, ndoa nyingi zinaweza kuratibiwa kisheria, lakini zinahitaji kuwa na mpangilio mzuri na wa haki.


Unaweza kufikiria kuwaoa mmoja baada ya mwingine kwa taratibu zinazofaa, huku ukiwa na mpango wa kimaadili na kisheria kuhakikisha wote wanaheshimiwa kwa usawa.


4.Kumshirikisha Mshauri wa Familia au Kiongozi wa Dini.

Ili kuepuka migogoro mikubwa, ni vyema kumshirikisha mshauri wa familia, kiongozi wa dini, au kiongozi wa kijamii ambaye anaweza kusaidia kuleta maelewano kati ya wake hawa wawili na wazazi wao.


Omba ushauri kutoka kwa viongozi wa dini au watu wa karibu ambao wanaweza kuleta amani na kusaidia kuzungumzia suala hili kwa njia ya busara. Wanaweza kutoa mwongozo wa jinsi ya kudhibiti hisia na shinikizo la wazazi.


5.Kutoa Muda wa Kujiandaa kwa Ndoa.

Badala ya kulazimisha ndoa mara moja, ni vyema kumpa kila mmoja muda wa kujipanga. Hii itasaidia kuondoa wasiwasi na hisia za kutokuelewana. Pia, itakupa muda wa kujiandaa kihisia na kiakili kabla ya kuchukua hatua ya kuoa wake wawili.


Unapaswa kuwashauri wazazi wa pande zote mbili kuwa na uvumilivu kwa muda, huku akihakikisha kuwa unaendelea na maandalizi ya ndoa kwa mpangilio unaofaa na utulivu.


Kwa ujumla, unapaswa kusimamia suala hili kwa hekima, uvumilivu, na busara, huku ukizingatia sana hisia na matarajio ya wake zako wawili na wazazi wao. Mazungumzo ya wazi, maelewano, na msaada wa kiroho au kifamilia ni muhimu ili kuepusha migogoro.


SAKATA LA MARY.
(……...…….....)



Mtazo binafsi:
1. Fanya juu chini, usiwe chanzo Cha kuachana na mama J, collect your mistakes. kiufupi pigania na inusuru ndo yako na Mama J

2. Mama Ariana(Iryn) SI mwanamke was kumwacha, nasema hivi SI sababu ya uchumi wake, Bali upendo alionao kwako, usimuumize hisia zake kwako, two children, tayari Ni mke wako pia.

Kumbuka, twaishi mara moja tu hapa chini ya jua



To every Action there is an equal and opposite reaction”

~~ Newton's 3rd law of motion ~~
 
Ila Maguire bana. Eti anamuona Jimmy kama kijana aliepotea kwa wanawake, wakati yeye yupo South na ameacha mke na mtoto mbezi beach wakijua yupo China!

Huyuhuyu aliekula mtu na mdogo wake, anamuona Jimmy ni kijana wa hovyo.

😂😂😂😂
Utofaut wa Jimmy na Insider ni hu Jimmy anatumia note kuwapata warembo wake lakin insider madem wenyewe wanautaka kulingana na story yake alivyoihadithia apa
 
Mkuu, Hali uliyonayo inaonekana kuwa na changamoto nyingi za kihisia, kijamii, na kifamilia. Kuna masuala mazito ya uwazi, mawasiliano, na uamuzi wa kimaadili ambayo yanahitajika kushughulikiwa kwa umakini ili kuepusha madhara ya baadaye.


Baadhi ya mambo ya kuzingatia na ushauri juu ya nini kifanyike:


MAMA NA SAFARI YA KUUJUA UKWELI.


Mkuu,kupitia story yako, yaonekana kwamba mama Ni mtu wa imani Sana (dini) hivyo, kumueleza kuhusu hali hii itahitaji mbinu za busara, kwa heshima na uangalifu mkubwa. Hapa kuna hatua kadhaa unazoweza kuchukua:


1. Maandalizi ya Kihisi

Kutokana na kushikilia dini, mama anaweza kuwa na matarajio makubwa ya kimaadili kwa mtoto wake. Hivyo, ni muhimu kumwandaa kisaikolojia kabla ya kumwambia ukweli wote.


Nini ufanye:

Baba yako, ambaye tayari anajua, anaweza kusaidia katika kumwandaa mama kihisia. Wanapaswa kwanza kumtambulisha mama kwenye hali ya jumla ya maisha ya mtoto wao kabla ya kuingia kwenye undani wa suala la wake wawili.


2. Kuzingatia Dini na Maadili

kwa kuwa mama ni mtu wa dini, unapaswa uzingatie jinsi ya kumueleza kwa mtazamo wa kidini pia. Wewe si malaika una mwili wa nyama na damu kabisaa na Kama tujuavyo, Dini nyingi zinahimiza ukweli, uwazi, na kutubu kwa kosa lolote. Ni muhimu uonyeshe kwamba una nia ya kufanya mambo kwa njia sahihi na ya kidini, hata kama kuna makosa yaliyotokea.


Nini kifanyi:

Unaweza kueleza hatua ulizochukua kurekebisha hali hiyo na kuonyesha nia ya dhati ya kuunda familia yenye mshikamano. Hii inaweza kusaidia kumshawishi mama kuona kuwa, japokuwa mambo hayakuwa sahihi mwanzoni, lakini uko tayari kufuata njia stahiki.


3. Kumshirikisha Baba

Baba, ambaye tayari amekubali hali halisi, anaweza kuwa na jukumu kubwa la kusaidia kufikisha habari hizi kwa mama. Ikiwa mama ana uhusiano mzuri na baba, baba anaweza kuwa mtu wa kwanza kumwambia ili kumtuliza au kumsaidia kuelewa kabla ya kijana wake kujieleza.


Nini kifanyike

Baba na kijana wake mnaweza kushirikiana kumuandaa mama kwa njia ya upole, polepole wakimtoa kwenye hali ya mshtuko.


4.Kuomba Msamaha na Uelewa

Kwa kuwa mama anaweza kuona hili kama kosa kubwa, ni muhimu kuwa na unyenyekevu na kuomba msamaha kwa jambo hilo. Hii inaweza kusaidia kupunguza ukali wa hisia.


Nini kifanyike

Mkuu, unaweza kumwomba mama msamaha kwa kumficha ukweli kwa muda mrefu na kuelezea kwa uwazi jinsi ulivyokuwa na wakati mgumu kulishughulikia suala hili. Hii inaweza kusaidia mama kuelewa changamoto za kijana wake na labda kumsaidia kupita kipindi hiki. Asikuambie mtu mkuu, mama ni mama,na mapenzi juu ya watoto wake hayapimiki, ingawa sio wote, ila Kariba na hulka ya mama yako(kupitia simulizi hii) Atakuelewa tu


5. Kutoa Muda wa Kutafakari

Mama anaweza kuchukua muda mrefu kukubali hali hiyo, hasa kutokana na imani yake ya dini. Hivyo, huwezi kutarajia kukubaliwa mara moja, lakini unaweza kumpa muda wa kutafakari na kupunguza presha. Atakapo lijua hili swala, mpe mama nafasi ya kuchakata habari hizo bila kumlazimisha kukubali haraka. Kuwa mvumilivu na mwenye kuonyesha upendo.


Kwa ujumla, kumweleza mama kutahitaji uwazi, heshima, na uvumilivu mwingi. Ni muhimu kumwonyesha kuwa, licha ya changamoto zilizopo, una nia ya kufanya mambo kuwa bora zaidi.



SAKATA LA MAMA J


Mkuu, changamoto kuu inabaki kuwa namna ya kumwambia Mama J ukweli kuhusu uwepo wa Iryn na watoto waliopo nje. Binafsi, namwona Huyu ndio nahodha, ndio last kadi.


Hii ni hali nyeti sana, kwani kumwambia mke wa kwanza ukweli kuhusu jambo kubwa kama hili kunaweza kusababisha mshtuko, maumivu, au hata kuvunja uaminifu kati yenu. Ili kupunguza madhara, hapa kuna hatua unazoweza kuchukua:


1.Kujitayarisha Kihisia na Kiakili.

Kabla ya kumwambia Mama J, yeye mwenyewe lazima awe tayari kihisia kwa majibu yoyote atakayoyapata (hapa naona ulishaanza kulifanyia kazi).


Mama J anaweza kukasirika, kuumia, kuachika au hata kuchanganyikiwa. Ni lazima uwe tayari kwa hali zote hizo na kuhakikisha kuwa upo thabiti kumueleza ukweli kwa upendo na huruma.


Nini kifanyike

Jiandae kwa mazungumzo hayo kwa kutafakari na kuwa na mpango wazi juu ya namna ya kuwasilisha taarifa hiyo kwa njia isiyo ya mshtuko mkubwa (rejea ushauri wa dada yako; kisaikolojia, alikushauri vizuri).


2.Kumwambia Ukweli kwa Wakati Mzuri


Mda na Wakati wa kutoa habari hizi ni muhimu sana. Ni lazima uchague muda mwafaka ambapo mama J yuko katika hali ya utulivu wa akili na kihisia, ili aweze kushughulikia habari hizo kwa busara.


Uongee na Mama J wakati ambapo hana msongo wa mawazo au changamoto nyingine zinazoweza kuongezeka kwa wakati huo. Ni bora kuepuka kumwambia habari hizo wakati wa ugomvi au changamoto za maisha.


3.Uwazi na Uelewa

Unaweza kumwambia Mama J ukweli kwa njia ya uwazi, ukijaribu kuelezea kwa undani changamoto ulizokutana nazo na jinsi ulivyofika kwenye hali ya kuwa na mke wa pili (Iryn). Muhimu zaidi ni kuelezea sababu zako za kufanya maamuzi hayo bila kumlaumu Mama J au kumfanya aone kana kwamba ameshindwa.


Anza kwa kuonyesha upendo na kujali kwa Mama J, kisha kwa utulivu uelezee hali nzima: "Nimekuwa na jambo gumu moyoni mwangu ambalo nimekuwa nikilitafakari kwa muda mrefu. Naona ni vyema uwe na haki ya kujua ukweli kuhusu maisha yetu." Ukiendelea, unaweza kueleza juu ya Iryn, mtoto wao, na jinsi hali ilivyokuwa hadi sasa.


4.Kujieleza kwa Msamaha na Unyenyekevu.

Ukweli huu unauma, na ni lazima aelewe maumivu atakayosababisha. Hivyo, kujieleza kwa unyenyekevu na kuomba msamaha kwa kumficha Mama J kwa muda mrefu ni hatua ya kwanza muhimu.


Elezea kwa lugha ya msamaha, ukijua kwamba umemuweka Mama J katika hali ngumu bila kujua ukweli: "Nisamehe kwa kutofanya hivi mapema. Nilijua ni jambo gumu na sikutaka kuumiza hisia zako, lakini najua ulikuwa na haki ya kujua."


5.Kutoa Nafasi ya Hisia Zake.

Baada ya kumwambia ukweli, ni muhimu kumruhusu Mama J kuonyesha hisia zake. Atakuwa na mchanganyiko wa hisia: hasira, huzuni, au hata machungu. Ni lazima utoe nafasi ya kusikiliza kwa utulivu bila kuingilia au kujitetea sana wakati huo.


Katika kipindi hiki Ni muhimu sana kumhakikishia kwamba bado unampenda na kwamba ulitaka kumwambia ukweli kwa sababu unaheshimu ndoa( mahusiano) yenu.


6. Kushirikisha Msaada wa Nje.

Mkuu, point 2-5 unafanya endapo unaona waweza kulimudu peke yako, lakini kiuhalisia inawezekana ila Ni ngumu Sana, na probability yakuachana/kuvunjika kwa mahusiano yenu inakuwa kubwa Sana. NASHAURI kutokumuelezea peke yako, ila Kama dada alivyoshauri, unamuandaa kiaina Lengo Ni kupunguza NGUVU YA KUJUA KUTOKA KUTOKUJU


Katika Hali hii naona umuhimu wa kikao na mshauri/washauri wa familia ili kuzungumza hili kwa utulivu zaidi. Ushauri wa kisaikolojia pia unaweza kumsaidia Mama J kukabiliana na mshtuko huo (dada ako naona yupo vizuri Sana kwa hili, na ukizingatia kuwa wanaelewana Sana, hata Kama mama j atajua kuwa dada ako alijua mapema na hakumwambia, halitakuwa tatizo kubwa kwa dada ako kulisolve na kumweka sawa).


Kutoa Muda wa Kurekebisha Ni muhimu Sana Kwani Mama J, atahitaji muda kuchakata habari hizi na kuelewa hali halisi. Ni muhimu asilazimishwe au kushinikizwa kukubali mara moja. kuachiwa muda wa kutafakari Ni muhimu sana na kisha mtaongea zaidi baada ya Mama J kuwa tayari..


NB: Njia bora ni Mama J kuambiwa UKWELI MAPEMA na mtu wa karibu ndani ya familia yako, kabla hajasikia kutoka nga'mbo ya mbali. Na hapa aambiwebukweli kwa upole, huruma, na kujiandaa kwa majibu yoyote utakayopata. Uwazi, unyenyekevu, na uvumilivu ni muhimu ili kuhakikisha kwamba unaweka msingi mzuri wa kuendelea mbele bila kuvunja zaidi uhusiano wao.


NANI WA KUFANYA HIYO KAZI


(Binafsi nadadavua mapendekezo kadha wa kadha ila Kama ulivyosema hii ni 30% tu ya ulichosema hivyo wewe ndie Steringi, unafanya unachoona kipo sawa kwa mazingira uliyojayo)



Mtu anayepaswa kumwambia mama j UKWELI anapaswa kuchaguliwa kwa busara ili kuepusha mshtuko mkubwa na kumrahisishia kuelewa hali halisi. Hapa kuna vigezo vya kuzingatia kuhusu nani wa kumwambia:


1.Baba.

Baba yako anaweza kuwa chaguo zuri kwa sababu anajulikana kwa kuwa na busara, mamlaka, na anaweza kumwambia Mama J kwa njia ya upole na kueleweka. Kwa kawaida, baba anaweza kuchukua jukumu la kueleza hali hiyo kwa namna itakayomlinda mtoto wake (wewe) na kusaidia kufafanua kwamba ni suala ambalo limezingatiwa kwa uzito.

Faida:

✓Ana mamlaka zaidi katika familia, hivyo maneno yake yanaweza kukubalika kwa urahisi.

✓Anaweza kutumia uzoefu wake kuelezea mambo kwa upole na uelewa.


Changamoto:

✓ Ikiwa baba hana uhusiano wa karibu na Mama J, huenda ikawa vigumu kumfikisha ujumbe kwa ufanisi.


2.Mama

Mama yako anaweza kuwa na nafasi nzuri kumwambia Mama J kuhusu hali hii, kwani anaweza kuleta huruma na uelewa wa kina. Ikiwa ana uhusiano mzuri na Mama J, anaweza kumsaidia kupokea habari kwa namna isiyo ya mshtuko na yenye kueleweka zaidi.


Faida:

✓ Anaweza kutumia huruma ya kike na kuelewa hisia za Mama J

✓ Ikiwa ana uhusiano mzuri na Mama J, atasaidia kumtuliza kihisia na kumtia moyo.


Changamoto:

✓ Ikiwa mama yako ni mkali au mwenye mtazamo mkali, anaweza kuleta mvutano badala ya kumsaidia Mama J kupokea habari hizo kwa utulivu.


3. Dada

Dada anaweza kuwa chaguo zuri ikiwa ana uhusiano wa karibu na Mama J na anaweza kumweleza kwa upole na uelewa. Anaweza kumsaidia kwa namna ya kisaikolojia na kihisia, kwani anatambulika kama rafiki na mshirika wa karibu wa familia.


Faida:

✓ Ikiwa ana uhusiano wa karibu na Mama J, anaweza kumweleza kwa njia ya rafiki na isiyo rasmi.

✓ Anaweza kueleza kwa upole na msaada wa kihisia, ikiwezekana akiwa na huruma na upendo.


Changamoto:

✓Dada anaweza kukosa mamlaka au uzito wa kutoa habari hiyo kwa namna ambayo itamfanya Mama J aelewe ukubwa wa hali hiyo.



Uamuzi:

Kwa hali hii, baba anaonekana kuwa chaguo bora zaidi kwa sababu anaweza kuelezea kwa busara na kutumika kama kiunganishi kati yako na Mama J. Ikiwa baba ataungana na mama, inaweza kuwa na uzito zaidi, ambapo mama atasaidia kwa huruma na uelewa zaidi.


Hata hivyo, kumchagua mtu wa kumwambia Mama J kunategemea uhusiano uliopo kati ya Mama J na mtu huyo. Kumbuka, lengo ni kuhakikisha anaambiwa kwa njia ya heshima, utulivu, na huruma ili kuepusha mshtuko mkubwa.


Pendekezo:

Kama kuna uhusiano mzuri kati ya Mama J na mama, baba na dada waambie wote waongee naye pamoja. Baba atatoa uzito wa suala hilo, na mama atatoa faraja ilihali dada atatoa msaada wa kihisia na kisaikolojia.


Upande wa familia ya mama J haitakuwa tabu Sana Kama mama J Atakuelewa na kukubaliana nawe.




SHNIKIZO LA NDOA

(NB: hili Ni baada ya mama J kujua ukweli na kukubaliana nao)


Kushughulikia shinikizo kutoka kwa familia ya Irene na Mama J, ambao wote wanasisitiza ndoa, ni changamoto kubwa, lakini hapa kuna njia kadhaa unazoweza kutumia ili kuleta usawa na kuepuka migogoro mikubwa:


1.Weka Kipaumbele katika Uwazi na Maelewano

Ili uweze kushughulikia hali hii kwa usawa, lazima aluwe muwazi kwa pande zote mbili na jaribu kuleta maelewano kati ya wake hao wawili watarajiwa. Ni muhimu kwa kila mmoja wao kuelewa kuwa unawapenda na unawathamini wote. Uwazi utakusaidia kuondoa dhana za wivu au mashaka kwa pande zote mbili.


Ongee na kila mmoja kwa uwazi kuhusu hali ya ndoa mbili na lengo lako la kuhakikisha kuwa wote wanafurahia ndoa hiyo.


2. Kuzungumza na Wazazi wa Pande Zote.


Kwa kuwa wazazi wa Irene na wazazi wa Mama J wanataka ndoa zao zifungwe, ni vyema kukaa nao na kuwapa ufafanuzi juu ya hali nzima. Unapaswa kuwaomba wazazi uvumilivu huku akijipanga kwa hatua sahihi bila kuchanganya hisia za wake wako wawili.




Unapaswa kuandaa vikao na wazazi wa pande zote mbili na kuwaambia wazi kuhusu nia yako ya kuwaoa wote wawili, lakini kwa mpangilio mzuri na wa busara. Anaweza kuomba msaada wa wazazi hao katika kuratibu taratibu hizo bila kuzidisha mgogoro.


3.Kuchagua Njia Sahihi ya Ndoa

Ikiwa una nia ya kuwaoa wake wote wawili, ni muhimu kufikiria ni taratibu gani za ndoa zitafuatwa na jinsi gani anaweza kufanya hili kwa uwiano bila kuonekana kama anabagua. Katika baadhi ya tamaduni na dini, ndoa nyingi zinaweza kuratibiwa kisheria, lakini zinahitaji kuwa na mpangilio mzuri na wa haki.


Unaweza kufikiria kuwaoa mmoja baada ya mwingine kwa taratibu zinazofaa, huku ukiwa na mpango wa kimaadili na kisheria kuhakikisha wote wanaheshimiwa kwa usawa.


4.Kumshirikisha Mshauri wa Familia au Kiongozi wa Dini.

Ili kuepuka migogoro mikubwa, ni vyema kumshirikisha mshauri wa familia, kiongozi wa dini, au kiongozi wa kijamii ambaye anaweza kusaidia kuleta maelewano kati ya wake hawa wawili na wazazi wao.


Omba ushauri kutoka kwa viongozi wa dini au watu wa karibu ambao wanaweza kuleta amani na kusaidia kuzungumzia suala hili kwa njia ya busara. Wanaweza kutoa mwongozo wa jinsi ya kudhibiti hisia na shinikizo la wazazi.


5.Kutoa Muda wa Kujiandaa kwa Ndoa.

Badala ya kulazimisha ndoa mara moja, ni vyema kumpa kila mmoja muda wa kujipanga. Hii itasaidia kuondoa wasiwasi na hisia za kutokuelewana. Pia, itakupa muda wa kujiandaa kihisia na kiakili kabla ya kuchukua hatua ya kuoa wake wawili.


Unapaswa kuwashauri wazazi wa pande zote mbili kuwa na uvumilivu kwa muda, huku akihakikisha kuwa unaendelea na maandalizi ya ndoa kwa mpangilio unaofaa na utulivu.


Kwa ujumla, unapaswa kusimamia suala hili kwa hekima, uvumilivu, na busara, huku ukizingatia sana hisia na matarajio ya wake zako wawili na wazazi wao. Mazungumzo ya wazi, maelewano, na msaada wa kiroho au kifamilia ni muhimu ili kuepusha migogoro.


SAKATA LA MARY.
(……...…….....)



Mtazo binafsi:
1. Fanya juu chini, usiwe chanzo Cha kuachana na mama J, collect your mistakes. kiufupi pigania na inusuru ndo yako na Mama J

2. Mama Ariana(Iryn) SI mwanamke was kumwacha, nasema hivi SI sababu ya uchumi wake, Bali upendo alionao kwako, usimuumize hisia zake kwako, two children, tayari Ni mke wako pia.

Kumbuka, twaishi mara moja tu hapa chini ya jua



To every Action there is an equal and opposite reaction”

~~ Newton's 3rd law of motion ~~
Huu mkeka [emoji92] watu mna moyo wa kuandika sio poa yaani[emoji91][emoji91][emoji91]
 
Mwisho Mzuri Hongera kwa kutupa ya maishani mwako. 🌻🌻🌻

Mary Mary Mary huyo usipoangalia atakuletea balaa tu, hiyo michezo wako sio muzuri. Utafikiri alikupiga kipapai huyo 😉

Nani ulimpenda sana alifariki September 2023? Tueleze kesho. R.I.P.
Pama
 
BONUS CHAPTER 1

Nimeanza kuandika story hii nikiwa South Africa, ule wakati ambao nilikuwa na muda wa ziada, ndipo nilipoanza kuandika Season 1 na kuwapostia. Lengo langu kuu ni kuwapa ujumbe kuhusu safari ya maisha yangu, kutoka mwanzo hadi sasa, maisha ambayo bado ninaishi. Sikutaka kukata tamaa, hata baada ya kumaliza mkataba wangu na taasisi X niliamua kujiingiza kwenye uber, huku ndo nilikopata mafanikio makubwa sana.

Nilichowaandikia ni kama asilimia 30 ya maisha yangu; bado kuna mengi ambayo sijagusia kutokana na sababu za usalama wangu pia.

Kwa ufupi, tangu Iryn alipojifungua, maisha yangu yalianza kubadilika kwa kasi sana. Niliamua kuelekeza nguvu zangu kwenye familia zangu na kujituma zaidi kutafuta hela kwa bidii.

Mwezi Januari 2024, nilikutana na mzee na kumueleza kuhusu suala la kuzaa na Iryn. Alishtushwa sana na habari hizi, na hakusita kunilaumu vikali juu ya hilo. Hata hivyo, nilijitahidi sana kujitetea, hasa kwa kutumia mbinu nzuri ambazo Sister aliniambia.

Mzee aliweza kuelewa hali halisi, na mwezi Februari mwaka huu alikutana na Iryn. Tulienda Zambia kwa ajili ya hili, na baada ya kumuona Aria, mzee alikiri kwamba ni damu yetu. Changamoto iliyobaki sasa ni namna ya kumwambia mama yangu mzazi. Tumepanga kumtaarifu mwezi huu, na safari hiyo itakuwa mimi, mzee, na sister.

Kuhusu mama J, tuko shwari kabisa, na upendo kati yetu umeendelea kukua kwa kasi; tunapendana sana. Junior mwaka huu alianza shule na anaendelea kufanya vizuri sana darasani. Kampuni ya Masaki bado ipo na inaendelea kufanya vizuri sana, na pia mama mtoto amefungua biashara nyingine hapa Dar es Salaam.

Kuhusu mtoto wetu Aria, sasa ana mwaka mmoja na miezi mitatu, na tumefanana sana. Ninajitahidi kumtembelea mara kwa mara kule South, hata wiki iliyopita nilikuwa huko kumuona.

Habari njema nyingine ni kwamba mwezi wa tisa huu ninatarajia kupata mtoto wa pili na Iryn. Baada ya kuja Disemba mwaka jana, tulikutana na hali hiyo ikapelekea kushika mimba. Ingawa hatukupanga hili, hatukuwa na namna zaidi ya kukubaliana yeye kuzaa. Hali hii imefanya niwe nasafiri mara kwa mara kwenda South Africa.

Kuhusu Mary, alipata kazi Mwanza katika moja ya taasisi nyeti inayoshughulika na masuala ya BOP. Hatuko kwenye mahusiano ya kimapenzi rasmi, lakini bado tunakutana kisela.

Mipango yangu ni kuhakikisha kwamba kufikia mwakani kila kitu kiwe wazi kwa mama J. Hata hivyo, hili linasubiri wazazi watoe maamuzi, kwani tunasubiri kuona mama atachukua hatua gani akijua ukweli. Nia yangu ni kumuoa mama J kwa kufunga naye ndoa, lakini hilo litafanyika tu endapo atajua ukweli na kukubali kwa hiari yake.

Mbali na mama J, pia nina mpango wa kumfanya Iryn awe mke wangu wa pili. Sijui wazazi watasema nini kuhusu hili, lakini anatarajia kupata mtoto wa pili. Hali hii inahusisha majadiliano mazito na maamuzi ambayo ni muhimu kabla ya kuchukua hatua zozote.

Nitarudi kuwapa hadithi fupi pale ambapo nitamuweka wazi mama J kuhusu hili suala. Sijui itakuwa lini—labda mwakani au baada ya miaka miwili au mitatu. Lakini nitawapa mrejesho wa kilichotokea kwa kuwapa Season 3 au lah. Nitawapa muendelezo wa mambo yalivyokuwa, kuanzia niliporudi Dar es Salaam mwezi Julai 2023. Hapa katikatika nimepitia mambo mengi sana, hadi sasa ni vile hamjui kinachoendelea nyuma ya pazia, kumekuwa na vikao vingi sana.

Mwisho kabisa, mwakani Mungu akijalia nitaondoka Tanzania na familia yangu kwenda kufanya kazi nje. Jambo la muhimu tuendelee kuombeana uzima na mapambano mema, tuache chuki na Roho mbaya.

Bonus, inayokuja tutachambua wote fursa zinazopatikana Dar es Salaam na huenda nikawa na thanks giving kwa baadhi ya watu watakao bahatika, nikaangalia namna ya kuwa support kwenye harakati zao. Lakini hadi kufikia sasa nimeshatoa kwa watu wengi tu, ambao walikuwa wanakuja inbox na sababu zilizonyooka, na wengi ni matapeli.

Tukutane kesho!
Mungu akubariki na akupe maisha marefu insider. Ambariki mama aria na mtoto alieko tumboni. Nimefurahi kujua mama aria ana mimba ya pili namwombea kila la kheri. Mama j pia namwombea heri na baraka pamoja na dogo juninur. Peace be upon you.
 
SEASON 02
CHAPTER 41

“BY INSIDER MAN”

CONTINUE:

Kwa upande wangu, sikutarajia hata kidogo kukutana na mama mkubwa. Niliposogea, nilimsalimia kwa heshima. Alinijibu kwa upole, kisha akaniangalia kwa makini, macho yake yakitua pia kwa Aria aliyekuwa kamshika. Sekunde chache zilivyopita, alinitazama tena na kusema kwa sauti tulivu, “Umefanana sana na mtoto.” Kabla sijapata nafasi ya kujibu, Mama Janeth naye alidakia, akinitazama kwa tabasamu na kusema, “Ni kweli kabisa, mnafanana sana wewe na Aria.”

Niliishia kutabasamu baada ya kusikia maneno yale kutoka kwa mama mkubwa, kisha nikatafuta sehemu ya kuketi. Sebleni palikuwa na wageni wengi sana, hali iliyonifanya nijisikie kutokuwa na utulivu, lakini sikuwa na namna. Nilibaki pale, nikijaribu kuzoea hali ile, huku nikionesha utulivu ambao sikuwa nao ndani yangu.

Baada ya dakika nyingi kupita, niliamua kwenda chumbani kwa Iryn ili kumsalimia na kumjulia hali. Nilipofika, niligundua hakuwa peke yake, alikuwa na wageni wawili. Niliwasalimia wote kwa heshima, na bila kusita, Iryn alinitambulisha kwa marafiki zake akisema, “Hawa ni marafiki zangu, tumesoma nao chuo Ufaransa.”

Nilimuuliza Iryn kuhusu maendeleo ya kidonda chake, na aliniambia kuwa anaendelea vizuri kabisa. Tulipokuwa tunaendelea kuzungumza, ghafla Jimmy aliingia chumbani. Mara tu Iryn alipomuona, uso wake ulibadilika kabisa.

JIMMY: “Hata ukininunia, freshy tu."

IRYN: “Jimmy, nakuchukia sana!"

JIMMY: “Hujaanza leo, na sishangai kabisa.”

IRYN: “Jana ulimpeleka wapi Insider?”

Jimmy alinitazama kwa wasiwasi, akihisi labda nimemueleza Iryn kuhusu tulikokuwa usiku huo. Nilimpa ishara kuwa sina ufahamu wowote juu ya jambo hilo.

JIMMY: “Sawa, tulienda Soho kuburudika, na tulirudi salama."

Iryn, akiwa amekasirika, alitazama pembeni na kuona bakuli karibu yake. Alilichukua kisha akamrushia Jimmy kwa hasira, huku akimfyonza kwa dhihaka.

Na wakati huu, Amara aliingia chumbani na kuanza kuuliza, “Shida ni nini?" Jimmy, kwa haraka, alimnyanyua juu juu na kutoka naye hadi sebleni. Lilikuwa tukio la ghafla na la kufurahisha, kiasi kwamba kila mtu aliishia kucheka, hata wageni.

Niliamua kuondoka chumbani ili kumpa Iryn nafasi na wageni wake. Hata hivyo, wakati nilipokuwa natoka, ghafla nilisikia akiniita kwa sauti ya upole, “Subiri kidogo...”

IRYN: “Darling, where are you going?”

MIMI: “Nipo mke wangu, huna haja ya kuwa na wasiwasi.”

IRYN: “Usije ukanitoroka kama jana ulivyofanya.”

MIMI: “ Leo nipo na wewe baby.”

Baada ya kurudi sebleni, nilitambua kuwa watu watatu hawakuwepo, nao ni dada yangu, Vivian, na Samantha. Nilipouliza, niliambiwa kuwa walitoka kwenda supermarket kununua vitu kwa ajili ya mama mtoto.

Baada ya takriban saa moja, mzee Virgil aliwasili na familia yake yote. Ilikuwa siku ya kipekee kwani niliweza kuwafahamu wadogo zake wote kupitia mama mdogo, kasoro kaka yake ambaye mzee alimzaa na mwanamke mwingine.

Mchana tulikula chakula cha pamoja, ambacho kiliagizwa kutoka kwa wapishi wa nje. Baada ya lunch, mama Janeth alitusalimu na kutuaga, akituambia kwamba anaondoka kwa safari ya kwenda Tanzania, kisha ataendelea na safari yake kwenda Marekani (USA).

Kabla ya mama Janeth kuondoka, tulipata nafasi ya kuzungumza. Nilimshukuru sana kwa kujitoa kwake na kuhakikisha Iryn anajifungua salama. Mama Janeth alinituliza, akisema kwa upole, “Iryn ni binti yangu, huna haja ya kunishukuru kwa hili.”Maneno yake yalikuwa ya faraja, yakiniondolea wasiwasi.

Jioni nilikutana na dada yangu, na tukatafuta sehemu tulivu kwa ajili ya mazungumzo yetu. Mara tu baada ya kuketi, dada alianza kuzungumza kwa hisia, akilalamika kuhusu tabia zangu mpya ambazo nimeanza kuonesha waziwazi mbele ya mama J. Aliuliza kwa upole lakini kwa msisitizo, “Kipindi kile ulipolala nje, ulikuwa wapi?” Akiongeza kwa tahadhari, alisema, “Na kama utathubutu kunidanganya, itakuwa ndio mwisho wa maongezi yetu.” Maneno yake yalikuwa na uzito, yakinifanya nifikirie kwa makini kuhusu majibu yangu.

Niliwaza pale na kuamua ni bora niwe mkweli ili tuweze kumaliza mambo haya.

MIMI: “Nilikuwa na mwanamke mwingine.”

SISTER: “Una matatizo gani? Tuliongea vizuri kabisa kuhusu haya, lakini bado unaendelea kuyafanya. Je, unanidharau mimi dada yako? Nilitegemea utaanza kufocus na watoto wako, lakini unazidi kuhangaika na wanawake wengine?”

MIMI: “Dada yangu, najua nimezingua. Mwanamke huyu alinifata Dodoma mwenyewe, na kipindi kile nilikuwa nimegombana na mama J, na Iryn alikuwa hana dalili za kurudi.”

Majibu yangu yalimfanya dada yangu aonekane mwenye wasiwasi zaidi, lakini pia nilijua ni muhimu kuwa mkweli ili kuweza kuendelea mbele.

SISTER: “Nisikilize kwa makini, bro. Usinione kama mjinga kukusaidia na kesi zako za kila siku ambazo unafanya kwa makusudi. Leo nakupa onyo la mwisho, kama una wanawake nje na hawa mama watoto wako, nikaja kupata kesi, utakuwa umefunga kufuli la mimi kukusaidia.”

MIMI: “Dada yangu, usifike huko, nimekuelewa na sitokuangusha.”

SISTER: “Na kilichofanya uondoke bila kumuaga mama J ni nini? Unaonesha dharau kama hizi kwa mke wako.”

MIMI: “Mimi naondoka tumegombana kwa sababu alimpigia mama yangu simu na kumwambia nililala nje. Niliona ananichonganisha na mama yetu, kwa kitu ambacho hana ushahidi nacho.”

SISTER: “Unataka kuachana na mama J, kisa Iryn?. Ukitaka mambo yako yaanze kuharibika tena, bhasi jichanganye ufanye huo ujinga unaotaka kuufanya, utayakumbuka maneno yangu.”

MIMI: “Siwezi kumuacha mama J, hili nakuapia dada yangu.”

Baada ya kumaliza tofauti zetu, dada aliniahidi kunisaidia kuliweka sawa suala la Iryn. Alinishauri nisubiri mtoto afike miezi sita ndipo nianze hatua za kuwaambia wazazi. Alisema ni bora nianze kumshirikisha mzee, na kisha yeye ndiye atakayemwambia mama. Maneno yake yaliniweka katika hali ya matumaini, kwani nilijua kwamba kwa msaada wake, naweza kupata njia sahihi ya kukabiliana na hali hii.

Dada alinionyesha mbinu ya kuanza kumuandaa kisaikolojia mama J, akisema kwamba nianze kufanya hivi taratibu ili aanze kuhisi mapema kuwa nina mtoto nje. Hata hivyo, nilishindwa kumuelewa alimaanisha nini, hivyo ilibidi nimuulize.

MIMI: “Mbinu gani natakiwa kuanza kuitumia?”

SISTER: “Katika maongezi yenu, unaweza kumuuliza, 'Hivi, ukija kufahamu kuwa nina mtoto nje, utafanyaje?' Inatakiwa uwe unamuuliza mara kwa mara hadi pale atakapozoea na kuona ni jambo la kawaida.”

MIMI: “Dada yangu, sio kwa mama J, hachelewi kulianzisha.”

SISTER: “Hawezi kufanya chochote kwa sababu atakuwa hana ushahidi. Kwa mara ya kwanza atapata shida kadri anavyozidi kusikia kutoka kwako, lakini atazoea na kuona ni jambo la kawaida. Wewe cha kuzingatia ni kuwa unachukua note ya majibu anayotoa, na utakuwa unanitumia.”

Maneno yake yalikuwa na maana, lakini nilihisi bado kuna changamoto kubwa katika kutekeleza mbinu hiyo. Lakini dada alizidi kukazia kwamba mbinu hii itaanza kumuandaa kisaikolojia, na baada ya muda atazoea hali hiyo. Alisisitiza kwamba hata nitakapokuja kumpa taarifa rasmi, haitaleta shida sana na atakuwa na uwezo wa kuelewa vizuri. Maneno yake yalinipa matumaini, kwani niliweza kuona uwezekano wa kumfikia mama J kwa njia ambayo ingekuwa rahisi na ya busara.

Kuhusu suala la kumpa taarifa rasmi, dada alishauri ni bora nisubiri hadi nitakapomalizana na wazee na kila kitu kipo sawa. Alisema kwamba ni hapo ndipo nianze hatua za kumwambia mama J. Dada alinihakikishia kwamba atanisaidia kadri anavyoweza kwa kutumia uwezo wake wote hadi mambo yawe sawa. Maneno yake yalijenga imani ndani yangu, na nilihisi kuwa na msaada wa dada yangu kutanisaidia kukabiliana na changamoto hii.

Baada ya kumaliza maongezi yetu muhimu, dada aliniaga na kuniambia kwamba kesho, Jumapili, ataondoka kurudi Tanzania. Alisisitiza kwamba pindi nitakaporudi Dar es Salaam, nimtaarifu ili aje tuyaweke sawa na mama J.

Nilimuuliza dada kama amelipia tiketi ya ndege, naye akasema kwamba wifi yake, Iryn, alikuwa amelipia tayari na amemwingizia pesa nyingi kwenye akaunti yake, ingawa hakutaka pesa hizo. Dada alifungua app ya benki na kunionesha kiasi ambacho aliingiziwa, na nilibaki nikishangaa.

Mwishoni, dada alinipongeza kwa kuwa baba, akisema kuwa Aria ni damu yetu halali. Maneno yake yalinipa furaha kubwa na kunitia moyo zaidi. Tuliagana kwa kukumbatiana, kisha tukarudi ndani kuendelea na mambo mengine, kwani tulikuwa tumetumia muda mwingi sana kwenye maongezi yetu.

Kibarazani, akina Jimmy walikuwa wanacheza last card, na mimi nilijiunga nao, tukawa jumla wanne: Mimi, Jimmy, Vivian, na Samantha. Mchezo ulikuwa mzuri sana, maana tulianza hadi kuweka hela kwa mshindi, na hali hiyo ilifanya ushindani uwe mkali. Baadaye, dada alikuja na tukawa jumla watano, na mchezo ukawa na ladha mpya, huku kila mmoja akijaribu kushinda kwa njia yake. Kicheko na furaha vilijaza hewa, na ilikuwa ni fursa nzuri ya kuondoa mawazo na kufurahia muda pamoja.

Ninataka niwaambie kuhusu undugu wa Jimmy, Iryn, Vivian, na Samantha. Ninarudisha hadi chapter 9, siku ambayo nilifika Ethiopia kwa mara ya kwanza. Katika siku hiyo, dada watatu walikuja kumpokea Iryn, ambapo alinitambulisha. Yule dada mkubwa ndiye alikuwa Vivian, mtoto wa Pili wa mama mkubwa, huku Jimmy akiwa mtoto wa kwanza akifuatiwa na mdogo wake katika wale wawili waliokuwa wamekuja kumpokea Iryn.

Hawa watatu wa kwanza, Vivian, Jimmy, na mdogo wao, wanatoka kwenye tumbo moja, wakiwa na mama na baba mmoja, ingawa baba yao alishatangulia mbele za haki. Mama mkubwa alizaa watoto wengine wawili na mume mwingine, Samantha na mdogo wake wa mwisho. Huyu mdogo wa mwisho ndiye mmoja kati ya wale dada wawili wadogo ambao Iryn alinifahamisha kama wadogo zake.

Mama mkubwa ana jumla ya watoto watano. Watatu wa kwanza wanashiriki baba mmoja, wakati hawa wawili wa mwisho wanashiriki baba mwingine. Kati ya watoto hao watano, Jimmy pekee ndiye mtoto wa kiume. Kwa Iryn, watoto hawa ni kama binamu zake (cousins), ingawa yeye hupenda kuwaita dada na kaka.


Nilikaa sana pale nyumbani, na hatimaye mimi na Jimmy tuliondoka saa 6 usiku kurudi hotelini. Nilipitia mapokezi kuchukua kadi yangu, na dada wa mapokezi akaniambia kuwa kuna ujumbe wangu. Alinipa kadi na kikaratasi kidogo. Nilielewa kinachoendelea mara moja, na Jimmy aliona yote hayo, akabaki kutabasamu.

Baada ya kuingia chumbani, nilifungua kile kinote na kugundua kuwa ilikuwa ni namba ya simu ya Nala. Niliweka pembeni na kuelekea bafuni kuoga. Baada ya kumaliza kuoga, nilijilaza kitandani, nikiwa nimechoka lakini mawazo yakiwa hayajakaa sawa. Nilianza kuyapitia kwa kina yale mazungumzo yangu na sister, nikitafakari maana yake na mwelekeo wa mambo.

Ukweli ni kwamba, Sister alizungumza mambo mengi sana, lakini kubwa kuliko yote, aliniapia kwamba nikifanya makosa tena, basi atajiondoa kabisa kwenye huu msala, na niachwe nipambane peke yangu. Sister ndiye kiungo muhimu katika kufanikisha hili jambo, hivyo niliona ni busara kutulia na kuwekeza nguvu zangu kwa umakini kwenye familia zangu.

Niliwaza sana kuhusu wazo la kumuacha Mary, lakini kila nilipofikiria, nilijikuta nikipoteza nguvu kwa sababu bado nampenda. Hata hivyo, kutokana na ushauri wa Sister, niliona sina budi kufanya hivyo. Ni bora nimuache mapema kuliko kusubiri na kuleta matatizo makubwa zaidi huko mbeleni.

Niliwaza sana na hatimaye nikaamua kwamba nitakaporudi Dar es Salaam, nitamtafuta Mary ili tuzungumze wazi kuhusu hili suala. Kilichonipa faraja kidogo ni kwamba Mary tayari alikuwa anafahamu kinachoendelea kuhusu mahusiano yangu na Iryn, hivyo nilihisi mazungumzo yetu yangeweza kuwa ya uwazi zaidi.

Jambo lingine lililoanza kunisumbua kichwani ni jinsi wazazi wangu watakavyopokea taarifa za mimi kuzaa na Iryn. Swali kubwa lililozunguka mawazoni mwangu lilikuwa, je, watalichukuliaje suala hili? Nilijua kuwa na mtihani mgumu mbele yangu, lakini kwa sababu Sister aliahidi kunisaidia, nilijisemea kwamba kila kitu kitakuwa sawa. Hata hivyo, sikupuuza uzito wa hali hiyo.

Kwa upande wangu, nilitamani sana kuona Junior na Aria wakifahamiana tangu utotoni ili waweze kujenga uhusiano wa karibu na bond nzuri. Kuhusu hili suala, nilihisi mzee ndiye anayeweza kunipa ushauri mzuri zaidi. Hivyo, nilianza kupata hamasa ya kumtafuta mapema ili tuweze kuzungumza na kupanga namna bora ya kufanikisha hili.
*****

Asubuhi, baada ya kuamka, nilimpigia simu mama J ili kumsalimia, lakini hakupokea, hivyo nilihisi labda alikuwa ameenda kanisani. Niliingia bafuni haraka kuoga na kujiandaa ili tuweze kwenda kwa mama mtoto. Ilikuwa saa mbili asubuhi, na nilihisi muda ulikuwa unayoyoma. Nilimpigia simu Jimmy kumjulisha kuwa tuanze safari, lakini naye hakuwa akipokea. Hatimaye, nikaamua kwenda kumgongea chumbani kwake.

Baada ya kufika kwenye chumba chake, maana yeye alikuwa floor ya juu, niligonga mlango na alitoka kufungua. Alikuwa haja jiandaa, hivyo nilipompa taarifa ya kuondoka, aliniambia nimsubiri ajiandae haraka. Nikamwambia atanikuta kwenye restaurant nikimsubiri.

Nilielekea kwenye restaurant kupata kifungua kinywa, na wakati huo nilikuwa nawasiliana na Iryn, ambaye alikuwa akinisisitizia nianze safari mapema ili niweze kucheza na mtoto. Baada ya nusu saa, nilimuona Jimmy akiwa ameongozana na mwanamke mwenye asili ya kizungu, na nikahisi huenda alikuwa amelala naye. Hali hii iliniacha na maswali mengi kichwani mwangu.

Walipofika, waliketi pamoja nami, na Jimmy alifanya utambulisho wa kawaida, na mimi pia nilimsalimia yule dada. Waliagiza kifungua kinywa, na baada ya kumaliza, tuliondoka kwenye eneo hilo, tukimwacha dada akisubiri usafiri wa kumpeleka kwake.

Wakati tuko kwenye Uber, nilianza kumuuliza Jimmy maswali kuhusu yule mwanamke. Nilikuwa na hamu ya kujua zaidi kuhusu mahusiano yao, na jinsi alivyomjua.

MIMI: “Bro, yule ni nani tena?”

JIMMY: “Tulikutana juzi Soho club, tukabadilishana namba, jana baada ya kuchat naye, nilimpanga aje hotelini akakubali.”

MIMI: “She’s a hoe?”

JIMMY: “I don’t think so, anafanyia kazi kwenye moja ya ubalozi hapa South Africa.”

Nilibaki kimya, nikitafakari kwa undani. Jimmy alikuwa amenishinda kabisa kwa tabia zake. Nilijiuliza mara ngapi ameweza kukutana na wanawake kama yule, na ni wangapi mpaka sasa? Spidi yake ilikuwa ya kutisha, na ilinifanya nishindwe kuelewa vizuri mwelekeo wake. Nilijikuta nawaza kama angeweza kudhibiti hali hii, au kama ilikuwa sehemu ya maisha yake ya kila siku.

Baada ya kuwasili, mazingira yalionekana kuwa kimya na tulivu sana. Tulipofika kibarazani, mtoto wa Jimmy alionekana akicheza peke yake. Jimmy alimnyanyua kwa furaha, kisha tukaingia ndani kuzungumza na mama mtoto ili tupate kujua ratiba ya siku ile.

Pale sebuleni, dada yangu alikuwa amemshika mtoto, na tukaingia kwenye mazungumzo kuhusu safari yake. Alisema anatarajia kuanza safari saa 11 jioni. Wakati huo, Iryn alitoka sebuleni na kuja kukaa pembeni yangu. Alionekana kuzidi kuimarika kadri siku zilivyokuwa zinaenda, jambo lililonipa faraja. Mazungumzo yetu yaliendelea kwa utulivu, na hali ilikuwa ya amani.

Baada ya kula chakula cha mchana, mimi, dada yangu, na mama mkubwa tuliamua kuwa na kikao chetu binafsi. Tulitafuta utulivu nje kwenye bustani, mbali na kelele na muingiliano wa watu wengine. Hapa tuliweza kuzungumza kwa uwazi na utulivu, tukijadili mambo muhimu bila usumbufu wowote. Mazingira yalikuwa tulivu, na kikao kilikuwa na uzito wa kipekee.

Mama alianza kwa kumshukuru sana sister kwa kujitolea kwake kwa kipindi chote hadi Iryn alipojifungua. Sister alisaidia sana, hasa kwenye mazoezi na mbinu mbalimbali za kuhakikisha Iryn anajifungua salama. Kwa kuwa sister yangu tayari alikuwa na watoto wawili, alikuwa na uzoefu mwingi ambao ulimsaidia kumwelekeza Iryn vyema wakati wa ujauzito na hadi wakati wa kujifungua. Mama alionyesha shukrani za dhati kwa mchango wake mkubwa.

Ukiachana na yote, Sister aliweza pia kutengeneza mahusiano mazuri sana na wifi zake, kama Vivian na Samantha. Wote walionekana kumpenda sana dada yangu kwa jinsi alivyojitoa na kujali. Uhusiano wao ulijengeka kwa upendo na uelewa, na hilo lilifanya familia kuwa karibu zaidi.

Kuhusu suala la mimi kumpa mimba binti yake, mama alisema hawezi kusema lolote kwa sababu Iryn mwenyewe alifanya maamuzi yake, na ni mtu mzima ambaye anaelewa vyema anachokifanya. Alionyesha kutambua kwamba Iryn alikuwa na uwezo wa kuchukua maamuzi yake binafsi, na hakutaka kuingilia zaidi. Hii ilileta hali ya unafuu kidogo, ingawa suala hilo bado lilikuwa na uzito wake.

Mama aliniuliza swali ambalo lilikuwa zito kulijibu:

“Una mpango na malengo gani juu ya Iryn?"

Nilihisi uzito wa swali hilo, lakini nilijua dhumuni la mama kuuliza ni nini. Nikajua kwamba ni muhimu kufikiri kwa umakini na kuepuka kutoa ahadi ambazo huenda nisitekeleze. Kwa kutumia busara na tahadhari, nilimjibu hivi:

MIMI: “Asante mama kwa kuniuliza swali hili muhimu. Ninamuheshimu sana Iryn na ninatambua nafasi yake katika maisha yangu. Nimeliona hili suala kwa uzito wake, na ninataka kuhakikisha kwamba mimi na Iryn tunajenga msingi mzuri wa ushirikiano, hasa kwa ajili ya ustawi wa mtoto wetu. Nataka tuchukue mambo hatua kwa hatua, huku tukijadiliana na kupanga vizuri mustakabali wa familia yetu. Ninaendelea kutafakari juu ya mpango mzuri na utakaokuwa bora kwa wote, na nataka kuhakikisha kwamba kila kitu kinawekwa wazi na kwa manufaa ya pande zote mbili.”

Mama na Sister waliniangalia kimya kwa muda, wakitafakari majibu yangu. Mama, hasa, alionekana kutotarajia jibu langu. Niliona machoni mwake kwamba alitarajia kitu tofauti, labda ahadi thabiti au mpango ulio wazi zaidi kuhusu mustakabali wangu na Iryn.

MAMA: “Naona umejibu kwa hekima, lakini bado sijapata uhakika. Wewe na Iryn, mna mpango wa kuwa pamoja au hili ni suala tu la mtoto?”

MIMI: “Naelewa unavyohisi mama, na ni swali lenye uzito. Kwa sasa, mimi na Iryn tunaendelea kuzungumza juu ya mstakabali wetu. Kipaumbele chetu kikubwa ni kuhakikisha mtoto anakua katika mazingira bora, lakini bado tupo kwenye hatua ya kufikiria kwa kina jinsi ya kutatua hali yetu ya kibinafsi. Siwezi kusema kwa hakika wakati huu, ila nataka iwe wazi kwamba sitamtelekeza Iryn wala mtoto wetu.”

MAMA: “Hilo ni jambo jema kusikia, lakini ningependa kuona mnapanga mustakabali wenye utulivu zaidi, hasa kwa ajili ya binti yangu. Matarajio yangu ni kwamba, kama kuna upendo na nia njema, basi mtachukua hatua ya kusonga mbele pamoja.”

MIMI: “Ninakubaliana na wewe kabisa mama, Iryn ni mtu muhimu kwangu na sina mpango wa kufanya maamuzi ya haraka bila kufikiria kila mtu aliyehusika. Ni muhimu kwangu kwamba wote tunakuwa na maelewano mazuri kwa ajili ya mtoto na hatimae, kwa Iryn pia.”

MAMA: “Nashukuru kwa uwazi wako, ningependa tu kuona unachukua hatua thabiti, maana Iryn anastahili uhakika. Si kwamba nakuwekea shinikizo, lakini ningependa kuona binti yangu akiwa kwenye mikono salama.”

MIMI: “Naelewa mama, na ninakuhakikishia kwamba natilia maanani kila kitu unachosema. Nitafanya kila niwezalo kuhakikisha mambo yanaenda vizuri kwa Iryn na mtoto wetu.”

Mama aliniangalia kwa makini, na nilihisi alikua akiwaza, labda akijiuliza, “Huyu jamaa ana akili sana.” Nilijua kuwa niliyajibu maswali yake yote kwa umakini na hekima. Hata dada yangu alionesha tabasamu, akionyesha kushangazwa na jinsi nilivyoweza kujibu maswali ya mama kwa njia ambayo haikuniingiza kwenye mtego.

Mama aliendelea na mazungumzo, akasema angependa kuwajua wazazi wetu, akisisitiza kuwa ni muhimu kwa mustakabali wa mtoto. Aliongeza kwamba sasa sisi tumeshakuwa muunganiko wa familia, na ni muhimu kuimarisha uhusiano huu kwa kuhakikisha kila mmoja anajua historia na asili ya mwingine. Mama alionyesha kuwa na hamu ya kujenga mshikamano ndani ya familia yetu, ili mtoto apate msingi mzuri wa malezi na urithi wa kihisia.

Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, Sister alijiandaa kwa ajili ya safari yake ya kurudi Tanzania. Hali ilikuwa ya huzuni kidogo, lakini pia ya furaha kwa sababu tulikuwa tumepata muda mzuri wa kuzungumza na kujenga uhusiano wetu zaidi.

Saa 9 mchana, Sister alitoka na begi lake na kutuaga pale sebuleni. Tulitoka nje na kupiga picha za pamoja kama kumbukumbu ya wakati wetu mzuri pamoja. Baada ya hapo, mimi na Vivian tulimpa kampani hadi uwanja wa ndege. Safari hiyo ilikuwa ya furaha, ingawa tulihisi huzuni kidogo kwa sababu ya kuachana. Tulizungumza mengi katika gari, tukijadili mipango ya baadaye na sister kuahidi kukutana tena na kina Vivian hivi karibuni.

Tukiwa airport, tulizungumza mambo mengi sana, na Sister aliendelea kunisitiza kwamba nitakaporudi Dar es Salaam, nimpe taarifa ili aje nyumbani kuweka sawa masuala yangu na mama J. Kabla ya kucheck in, aligana na Vivian kwa kukumbatiana kwa upendo, na niliona jinsi walivyokuwa na uhusiano mzuri. Baada ya hapo, tuliondoka maeneo hayo, tukielekea nyumbani, tukiwa njiani story na Vivian ziliendelea na niseme hawa mashem zangu wananikubali na tunapatana sana.

Usiku, niliwasiliana na mama J pamoja na mwanangu Junior. Nilimdanganya kwamba nipo China nikifuatilia mzigo, na baada ya hapo nitatoka kwenda South Africa kumuona Iryn, ambaye amejifungua mtoto. Mama J hakutoa maoni mengi kuhusu hilo, zaidi alisema atawasiliana na Iryn kumpa hongera. Ingawa alionekana kutokuwa sawa na hali hiyo, nilijua ujumbe wangu ulikuwa umemfikia.
*****

Wiki inayofuata, ambayo ilikuwa ni wiki ya kwanza ya mwezi wa 7, idadi ya wageni iliongezeka sana pale kwa Iryn. Ndugu zake kutoka Ethiopia walifika, na pia marafiki zake wa chuo waliosoma pamoja Ufaransa walikuwa wakija na kuondoka. Sebuleni, kila kona ilikuwa imejaa zawadi za mtoto, na hapo ndipo nilipogundua kwa kweli kwamba Iryn alikuwa na mtandao mpana wa watu. Hali hiyo ilionyesha jinsi alivyokuwa akipendwa na kuungwa mkono na watu wengi, na ilifanya moyo wangu ujaze faraja na kujivunia kuwa sehemu ya maisha yake.

Siku ya Jumatano, mama mkubwa aliondoka kurudi Ethiopia ili kuendelea na majukumu yake. Pia, dada wa kazi kutoka Ethiopia alifika nyumbani kusaidia katika kazi mbalimbali. Iryn alieleza kuwa hakutaka dada wa kazi mwenyeji kwa sababu ya tabia zao, hivyo alihitaji mtu ambaye wangeweza kuendana kiutamaduni. Hali hiyo ilionyesha umuhimu wa mazingira yanayofanana na utamaduni wao, na niliona ni busara kwa Iryn kuchagua mtu ambaye angeweza kuleta utulivu na uelewano katika familia.

Siku ya Jumapili, Jimmy pamoja na familia yake waliondoka kurudi Ethiopia, hivyo aliyebaki ni dada Vivian. Baada ya kuondoka kwa Jimmy, nilienda kukaa na Iryn, maana idadi ya watu ilikuwa imepungua, na mle ndani tulikuwa jumla watano. Hali hiyo ilituletea fursa nzuri ya kuzungumza kwa undani zaidi na kujenga uhusiano wetu.

Wiki ya pili ya mwezi wa 7, Jumatatu, bibi yao ‘Momo’ alifika South Africa kumuona kitukuu chake. Aliwasili jioni, na mimi na Samantha tulikwenda kumpokea pale airport. Momo, ambaye sasa ana umri wa miaka 70, ni bibi mwenye uzoefu wa maisha, lakini bado ana nguvu za kujiendesha. Momo ana tabia ya kutabasamu na kuwa na nishati, na nilijua kwamba uwepo wake ungeongeza furaha na umoja katika familia yetu.

Tangu tupo kwenye gari hadi tulipofika nyumbani, Bibi alikuwa na furaha sana na alionyesha hamu kubwa ya kumuona kitukuu wake. Alikuwa akizungumza kwa lugha yao ya nyumbani, lakini Samantha alikuwa ananiambia kila kilichokuwa kinaendelea, akitafsiri maneno ya bibi kwa urahisi. Ilikuwa ni furaha kubwa kusikia shauku ya bibi, na niliweza kuhisi upendo wake wa dhati kwa familia.

Baada ya kufika nyumbani, Iryn hakuwa mbali kumpokea bibi yake, na walikumbatiana kwa furaha na kumkaribisha ndani. Kitu cha kwanza bibi alichomba ni kumuona kitukuu wake, na alifurahi sana baada ya kumuona. Uso wake ulijawa na tabasamu la furaha, na Iryn alionekana pia akifurahia moment hiyo. Nilijua kuwa bibi alikuwa na matumaini makubwa kwa ajili ya kitukuu chake, na nilihisi furaha kuona jinsi familia ilivyokuwa ikijenga uhusiano mzuri katika kizazi tofauti.

Baada ya bibi kurudi nyumbani, mazingira yalichangamka sana, kwani bibi ni mwongeaji sana, na wajukuu zake wanampenda sana. Bibi alisema ataendelea kukaa na Iryn na hafikirii kurudi Ethiopia mapema, jambo lililomfanya Iryn ajisikie vizuri. Iryn ni mjukuu ambaye bibi yake anampenda sana, na hii ni kwa sababu Iryn humjali sana bibi yake, akimpa huduma na kumuhudumia kwa upendo.

Kwa upande wangu, tangu nilipofika South Africa, tayari wiki mbili zilikuwa zimepita, na nilipanga kuondoka Jumapili ya weekend. Niliangalia hali yangu na kugundua kwamba kuendelea kukaa huku kungeweza kuathiri mambo yangu mengi, kuanzia kampuni hadi biashara zangu. Nilijua ni muhimu kurejea nyumbani ili kusimamia masuala yangu na kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa. Ingawa nilifurahia wakati niliokuwa pamoja na Iryn na familia, nilihisi ni lazima nitafute njia ya kuleta uwiano kati ya majukumu yangu ya kifamilia na biashara zangu.

Kesho yake asubuhi, nilimfata Iryn chumbani ili niweze kuzungumza naye kuhusu suala langu la kuondoka. Pembeni yake kulikuwa na diary, hivyo niliichukua na kuanza kuisoma. Niliona alikuwa akiandika mipango yake, na nilicheka baada ya kuona ameandika mpango wa kuanza gym.

Of course, alikuwa ameanza kunenepa sana kutokana na kuwa mama na vyakula anavyokula, lakini bado haikufanya apoteze uzuri na shape yake. Kinyume chake, niliona kuwa mabadiliko hayo yaliongeza mvuto wake, na alikuwa akionekana kuwa na uzuri wa kipekee ambao unakuja na umama.

MAMA ARIA: “Darling, unacheka nini?”

MIMI: “Nimefurahi kuona una mpango wa kuanza Gym, lakini bado mapema sana.”

MAMA ARIA: “I know, baada ya miezi 3 nitaanza mazoezi ya kupunguza huu mwili.”

Nami, nikasogea kukaa pembeni yake;

MIMI: “Nimekumiss baby mama.”

Iryn alianza kuangalia usawa wa bunduki yangu na akanishika kidevu changu na tukaanza kuangaliana pale;

MAMA ARIA: “Are you horny?”

MIMI: “Ofcourse yes.”

MAMA ARIA: “Pole! nadhani unakumbuka siwezi kusex kwasasa hadi nipone vizuri, doctor alishauri baada ya miezi 3, ila mwezi ujao nitaenda kuangalia maendeleo.”

MIMI: “Naelewa usijali, mimi nitavumilia kwa hili.”

Usawa wa matiti yake ulionekana kulowa maziwa, kwani chuchu zake zilikuwa bado zimesimama. Baada ya kumuona vile, ilibidi nimwambie kwamba analowa, akicheka kidogo kwa aibu. Alijua kwamba hali hiyo ni ya kawaida kwa mama anapokuwa katika kipindi hiki, lakini nilijua kwamba ilikuwa ni muhimu kwake kujisikia vizuri kuhusu mwili wake.

MAMA ARIA: “Mwanao hataki kunyonya, halafu mama yake nina maziwa mengi sana. Uwe unamsaidia mwanao kunyonya, kwani naishia kuyakamua na kuyamwaga. Nikupe unyonye? Yatakusaidia kiafya.”

Nilihisi aibu baada ya kusikia haya maneno kutoka kwa Iryn. Aliponigeukia na kunipa ishara ya kunyonya, sikuona sababu ya kukataa, kwani alikuwa anayamwaga. Nilijisemea, si afadhali nikanywa mimi kuliko yamwagwe. Nilianza kuyanyonya taratibu hadi aliposema basi, ndio kuacha na yalikuwa ni matamu sana.

MAMA ARIA: “Vipi matamu?”

MIMI: “Yeah! Aria anafaidi sana.”

MAMA ARIA: “Mwanao mpole kama wewe, naona huyu atarithi tabia zako.”

MIMI: “Bado mtoto, akikua ndio tutajua tabia zake, hata Junior alikuwa mpole kama Aria, ila sasahivi ni balaa.”

Tulipoanza mazungumzo yetu, alizungumzia suala lake la kurudi shule na akaniambia kuwa analiwazia kwa umakini. Nami nikamshirikisha mpango wangu wa kurudi shule mwezi wa kumi, ambapo alinisisitiza kwa upendo kuwa ni vema nisomee masomo yangu ya masters nchini Afrika Kusini ili tuwe karibu na mtoto wetu.

Ingawa wazo hilo lilikuwa zuri, nilijua kuwa kulikuwa na changamoto nyingi zinazoweza kufanya isiwezekane. Hivyo, nilimpatia jibu lililofikiriwa vizuri, ambalo alielewa kwa upole na busara.

Nilimwambia kwa upole,

Baby mama, nikisomea huku, kumbuka kuwa mambo mengi yanaweza kuyumba, kuanzia kampuni yako hadi miradi yangu. Ufuatiliaji wa karibu ni muhimu sana. Acha mimi nisomee Dar ili niwe karibu na biashara zetu. Kuhusu Aria, nitakuwa nakuja mara kwa mara kuwasalimu, siwezi kukaa muda mrefu bila kumuona binti yangu. Kama vile wakati wa ujauzito wako ulivyokuwa ukija Dar es Salaam mara kwa mara, sasa ni zamu yangu kuja Cape Town. Tutaendelea kuwa karibu, hata kama nitakuwa huku.”

Mama Aria alifurahi sana kusikia maneno yangu, na hakuwa na la kusema zaidi. Baadaye, nilimueleza kuhusu mpango wangu wa kuondoka Jumapili. Hata hivyo, kwenye suala la kuondoka, alionekana kulipokea tofauti na aliniomba niondoke mwisho wa mwezi. Nilijaribu kumsihi kwa upole, na kumuomba aniruhusu niondoke wiki ijayo, huku nikiahidi kuwa nitarudi mapema kwa ajili ya sherehe ya "Simchat Bat" ya mtoto wetu.

Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, aliamua kwenda kuoga. Wakati huo, Aria alikuwa ameamka, hivyo nilimbeba na kutoka naye sebleni ili tupate muda wa kukaa pamoja. Sikuwa na shughuli nyingi za kufanya kipindi hicho nikiwa Afrika Kusini, zaidi ya kutumia muda wangu mwingi kucheza na Aria. Sikutoka kwenda sehemu yoyote mara kwa mara, isipokuwa tu kwenda supermarket pale panapohitajika.

Haikupita muda mrefu kabla mama Aria hajarudi kwenye seating room, na kunijulisha kuhusu ujio wa mgeni. Aliniambia kuwa anayekuja ni kaka yake, ambaye ni wa kwanza kwa upande wa mama mwingine. Nilikuwa nimeshaongelea kidogo kuhusu huyu kaka yake, katika Season 1: EP10.

Mchana ule, kaka yake alifika nyumbani kumsalimia Iryn pamoja na mtoto, akiwa ameongozana na mpenzi wake. Hii ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona kaka yake kwa upande wa baba. Ni kijana mwenye haiba fulani ya "manton," kwa mbali anataka kuendana na rappa AKA.

Tulisalimiana pale, kisha tukaingia kwenye mazungumzo ambapo alinikaribisha sana Afrika Kusini kwa ukarimu. Iryn akaanza kumuuliza kaka yake kuhusu maisha na kazi kwa ujumla. Ingawa kaka yake Iryn yuko vizuri kiuchumi, tatizo lake kubwa ni matumizi ya madawa, jambo ambalo limemuharibu sana. Niliwahi kugusia kuhusu hili hapo awali.

Baada ya kupata chakula cha mchana kwa pamoja, kaka yake na mpenzi wake waliondoka. Mama Aria kisha alinipa taarifa nyingine kwamba siku ya Jumamosi tungeenda nyumbani kwa baba yake. Aliongeza kuwa kuna mambo kadhaa watakayokwenda kuyapanga na mzee wake, na akaniambia atanishirikisha katika hayo mazungumzo siku hiyo.

*****

Hatimaye, siku ya Jumamosi ilifika, siku ambayo ilikuwa ni ya kwenda kwa mzee Virgil, baba mkwe wangu. Mzee Virgil alikuwa akija mara kwa mara nyumbani kumuona mjukuu wake, na kitendo cha Iryn kujifungua kilimfurahisha sana. Hakuwa na maswali mengi kuhusu malengo yangu kwa binti yake, wala hakujishughulisha na hilo. Kile kilichomgusa zaidi kilikuwa ni upendo mkubwa aliokuwa nao kwa mjukuu wake. Ilionekana kana kwamba alikuwa akitamani kwa muda mrefu sana kupata mjukuu, na sasa alikuwa akifurahia kila muda aliokuwa naye.

Saa nne asubuhi, gari lilikuja kutuchukua kwa ajili ya safari ya kwenda nyumbani kwa mzee Virgil. Tuliondoka watatu tu, mimi, Iryn, na Samantha. Safari yetu ilikuwa na umbali wa takriban kilomita 45 hadi kufika nyumbani kwa mzee, Somerset West, ambayo iko pembezoni mwa Cape Town. Huu ni sawa na umbali wa kutoka Mwenge hadi Bagamoyo. Njia ilikuwa nzuri, na tulikuwa na mazungumzo mazuri kwenye gari, tukiwa na hamu ya kufika na kumtembelea mzee.

Mzee aliamua kujenga na kuishi nje kidogo ya mji wa Cape Town, na tulivyoanza kuingia katika maeneo haya, nilikuwa nikiona majumba ya kifahari ambayo yalivutia sana macho yangu. Mazingira ya hapa ni kama Ulaya, ni masafi, na kote ni lami, hakuna vumbi. Nyumba zimepangiliwa kwa ustadi wa hali ya juu, mandhari yake ikiwa ya kijani kibichi. Wakati tunaingia Somerset, tulikuwa tukipishana na magari ya kifahari, hali iliyoongeza uzuri wa eneo hili.

Gari lilipaki nje ya geti kubwa, na haikuchukua muda mrefu likafunguliwa, ingawa pale getini hakuonekana mtu yeyote aliyefungua. Tulipofika ndani, gari lilitembea kwa mwendo wa takriban mita 100, na njiani tulipishana na bustani nzuri ya kuvutia.

Baada ya kufika usawa wa nyumba, tulishuka na mbele yangu nikaona bonge la mjengo wa kifahari, aina ya villa. Ilikuwa nyumba kubwa ya kisasa ya ghorofa moja, na kila kipengele chake kilionekana kuwa kimepangwa kwa umaridadi. Ujenzi wa nyumba hiyo ulikuwa wa kisasa na wa kuvutia, ukionyesha ushawishi wa hali ya juu wa usanifu. Ilionekana kama ni mahali pazuri pa kuishi, ambapo mandhari ya karibu iliongeza uzuri na raha ya mazingira.

Wakati huu, mama yake mdogo alitoka kutupokea akiwa na wanae, na haikuchukua muda mzee Virgil akatoka kumkaribisha binti yake. Alikuwa na furaha kubwa sana kutuona na aliomba kumbeba Aria, Mzee Virgil alionyesha upendo mkubwa kwa mjukuu wake.

Nilisikia sauti ya upole kutoka kwa Iryn ikinikaribisha kwa furaha:

“Baba Aria, hapa ndiyo nyumbani, karibu sana.”

Tulipokuwa tunaingia ndani, nilikutana na bonge la msebule uliojaa mapambo ya thamani kubwa kama crystals na marbles. Nimeingia katika nyumba nyingi za kifahari, lakini sebule ya kwa Mzee Virgil ilikuwa ya kipekee kabisa. Ukarabati wa ndani ulikuwa wa kiwango cha juu, na kila kipande cha samani na mapambo kilionyesha umaridadi na mtindo wa kipekee, ikifanya iwe mahali pa kuvutia.

Iryn alianza kunitambulisha kwa wadogo zake wa pale nyumbani kwa upande wa mama mdogo. Mama mdogo ana watoto watatu tu; mtoto wa kwanza ni wa kike, ambaye nilimfahamu nikiwa hospitalini, alikuwa akitarajia kuanza chuo mwaka huo na wawili ni wa kiume, wenye umri wa miaka 13 na 8. Walionekana kufurahia kuniona na walikuwa na shauku ya kujua kuhusu mimi, hali ambayo ilileta maongezi yawe mengi zaidi.

Baada ya lisaa, wageni watano walifika, na kati yao, mmoja tu alikuwa na asili ya Afrika; wengine wote walikuwa wazungu. Kati ya wageni hao, mmoja alikuwa ni babu, na aliomba amshike Aria. Mzee Virgil alifanya utambulisho pale, akimwambia Iryn kwamba wale ni ndugu zake. Iryn alifurahi sana kusikia hivyo, kwani kwa upande wake alikuwa kwenye mission ya kuwasogeza karibu ndugu wote wa upande wa baba yake. Hali hiyo ilileta hisia za umoja na furaha, na ilikuwa ni fursa nzuri kwa familia kukutana na kuimarisha uhusiano wao.

Tulipata chakula cha mchana pamoja, na baada ya wageni kuondoka, Iryn alitoka nje na mzee wake kufanya mazungumzo. Walionekana kuwa na mazungumzo ya karibu na ya kina, hii ilikuwa ni nafasi nzuri kwao kujadili mambo ya familia na kujenga msingi mzuri wa ushirikiano.

Wakati huu, nilikuwa na mama mdogo tukifanya mazungumzo, ambapo aliendelea kunikaribisha kwa ukarimu. Alizungumza kwa upole, akielezea furaha yake kuwa na familia pamoja na jinsi alivyovutiwa na ujio wangu.

Baada ya lisaa, Iryn aliniita nitoke nje ili tuweze kuzungumza na mzee wake. Alimweleza baba yake jinsi ambavyo nimekuwa msaada mkubwa sana katika biashara zake. Mzee wake alishukuru kwa dhati na kusema niendelee kuwa na moyo huo huo. Alionyesha furaha kubwa kwa mimi kuwa sehemu ya familia yake.

Kuhusu suala la kumzalisha binti yake, mzee hakuwa na neno lolote la kukatisha tamaa. Badala yake, alitutakia mafanikio mema na kusema angetamani kuona tukifika mbali zaidi katika maisha yetu.

Mzee aliondoka pamoja na mjukuu wake, na kutuacha mimi na Iryn tukiendelea na mazungumzo yetu. Iryn alianza kunishirikisha kuhusu kazi kubwa aliyonayo katika kuzisimamia kampuni za baba yake. Aliniambia kuhusu mali mbalimbali anazomiliki baba yake hapa Afrika Kusini, ikiwa ni pamoja na apartments, mashamba ya zabibu, na kampuni ambayo ni miongoni mwa waexporter wakubwa wa wines.

Alielezea jinsi alivyohusika katika kusimamia shughuli hizi na jinsi anavyopanga mipango ya kuziendeleza zaidi. Hali hiyo ilionyesha kiwango cha juu cha kujitolea kwake na uelewa wa biashara, na ilinipa mtazamo mzuri kuhusu familia yao na malengo yao ya kifamilia.

Tangu siku ile tulipokutana na Iryn na kuanza mahusiano yetu, hakujawahi kuwa na wakati ambapo alitaja utajiri wa baba yake. Badala yake, alijikita zaidi katika kunieleza kuhusu majukumu aliyokabidhiwa ya kuwa msimamizi wa kampuni za baba yake. (SEASON 1: EP40)

Hii ndiyo siku nilipogundua kwamba mzee Virgil si mtu wa kawaida, kwani ana utajiri wa kutisha. Lakini ukimwona, unaweza kumchukulia kuwa mtu wa kawaida sana. Kama mnavyojua, wazungu hawana tabia ya kujionesha kama wana fedha, tofauti na sisi Waafrika, ambao mara nyingi tunapenda maonyesho ya kifahari.

Iryn aliendelea kunieleza jinsi mzee wake alivyotokea kunikubali sana. Aliniambia kwamba amemshauri atulie nami, kwani kwa sasa wanaume wengi hawaaminiki. Maneno hayo yalikuwa ya faraja kutoka kwa Iryn, yakiwa na uzito wa maana. Nilimuhakikishia kuwa nitajitahidi kumsaidia kadri ya uwezo wangu, kwa sababu uaminifu ni msingi wa mahusiano yetu.

Nilimuuliza Iryn kuhusu mgawanyo wa mali za mzee na jinsi anavyowaangalia watoto wengine, wakiwemo Smith na kaka yake mkubwa, ambapo jumla yao ni watoto sita wa mzee Virgil. Iryn alijibu kwamba hadi sasa, watoto wanne tu wanatambulika rasmi, ambao ni yeye pamoja na wadogo zake watatu kwa upande wa mamdogo. Aliongeza kuwa kuhusu kaka yake na Smith, bado hawajazungumza na mzee wao kuhusu suala hilo, lakini wanatarajia kuangalia namna nyingine ya kufanikisha mambo yao.

MIMI: “Na vipi kuhusu mama mdogo?”

IRYN: “Mama mdogo si mmoja wa mrithi wa hizi mali. Alifunga ndoa ya mkataba na mzee, na moja ya makubaliano ni kwamba hatahusika kwenye urithi wa mali zaidi ya watoto tu.”

MIMI: “Baba yako ni genius sana.”

IRYN: “Mali nyingi sana mzee kazipata akiwa na mama yangu. Ndiyo maana unaona mimi nikiwa kipaumbele cha kwanza, hata wakati ambapo hatuko kwenye maelewano na mzee. Kwa upande wake, alikuwa anapata tabu sana kuhusu hili.”

Iryn alikuwa huru kunifungukia mambo mengi sana. Alisema kwamba hata kitendo cha kuzaa na mimi si kwamba alikurupuka tu kufanya maamuzi hayo, bali alifikiria kuhusu mustakabali wake na mali za baba yake. Alieleza kwamba kipindi kile baada ya kurudi kutoka South Africa kumwona mzee wake, aliona kuna umuhimu wa kuwa na watoto ambao wataweza kurithi mali hizo, kwani hata yeye atakufa.

Iryn alifikiria kwa kina na kugundua kwamba hakuna mtu anayemuamini zaidi yangu kwa sasa. Alijisemea atafanya kila mbinu ili anizalie mtoto, lakini lengo lake kubwa ni kuhakikisha urithi wa mali za baba yake unakuwa salama. Aliendelea kueleza kwamba, mama mkubwa wake na ndugu zake wanamuona kama mjinga sana, lakini hawajui mipango yake ya siri. Hakuwa na nia ya kuona mali ambazo mama yake alizichuma na baba yake zikipotea kwa watoto wengine. Kwa hiyo, alichukua maamuzi haya magumu, lakini yaliyojikita katika manufaa ya kizazi chake.

Nilishusha pumzi ndefu sana, nikijisemea kwamba kumbe Iryn yuko very calculated na alikuwa na mipango mikubwa ambayo sikuwa na habari nayo. Nilikuwa bado siamini kwamba Iryn anaweza kubeba mimba kwa sababu ya kijinga kama aliyokuwa akinambia, lakini leo ndiyo nimeelewa kuwa alikuwa anawaza extra miles. Iryn alikuwa na malengo ya dhati, na sasa nilianza kuelewa uzito wa maamuzi yake.

IRYN: “Baba Aria, naomba nisamehe sana kwa kutokushirikisha hili mapema, nilijua ipo siku ungekuja kujua ukweli. Nilikuwa nauwezo wa kuzaa na mwanaume yoyote yule ninayemtaka hata kwa kumlipa na nikapata mtoto, lakini niliona wewe ndio unafaa.”

MIMI: “Naomba tuachane na haya, Aria ni mtoto wetu tuangalie namna gani ya kumlea na kumtunza ili tuje tujisifu kuwa naye.”

IRYN: “Babu yake kafurahi sana kumuona, ndio mjukuu wake wa kwanza. Pia unakumbuka nilikwambia kuhusu afya ya mzee wangu? Hana maisha marefu sana hapa duniani ni pesa tu zinafanya anaendelea kuishi.”

MIMI: “Nakumbuka baby, naamini ataishi muda mrefu zaidi hapa duniani, tusichoke kumuombea.”

IRYN: “Natamani kupata mtoto mwingine, hata nikiwa natembea barabarani, kushoto nina Aria na kulia nina mdogo wake nakuwa na bodyguards wangu.”

MIMI: “Naona unanipa greenlight ya kukupa mimba ya pili.”

IRYN: “Yes! Why not, unafikiri atakuwa nani zaidi yako?”

MIMI: “Sawa baby subiri kwanza Aria akue mengine tutapanga.”

Baada ya mazungumzo marefu, tulianza kutembea na kutalii mazingira ya nyumba yao. Aisee, nyumba yao imezungukwa na bustani nzuri, huku ukubwa wa kiwanja ukiwa kama ekari tano. Tuliposhuka chini, tulikuta mizabibu mingi imepandwa, kuzunguka upande wa nyuma nakutana na swimming pool mbili, moja ya wakubwa na nyingine kwa ajili ya watoto. Nyumba hiyo ilikuwa na mvuto wa kipekee, na mbele zaidi kulikuwa na nyumba ndogo ya wafanyakazi ambao kazi yao ni kutengeneza zile bustani na kumwagilia mimea.

Nilishindwa kuelewa kwanini Iryn ameshindwa kukaa na baba yake na ameamua kupanga aishi peke yake. Sikutaka kumuuliza kuhusu hili, kwani nilijua Iryn ana akili sana na huwa hafanyi jambo lolote bila sababu. Nilihisi kuwa kuna mambo mengi nyuma ya uamuzi wake, lakini kwa heshima yake, niliona bora nisubiri hadi atakapojisikia kuzungumzia.

Saa mbili usiku, tulipata dinner ya pamoja, na baada ya hapo tuliagana kuwa tunaondoka. Walitusindikiza hadi nje, ambapo dereva alikuwa amekuja kutufuata tayari. Tukiwa pale nje, mzee aliendelea kuongea na binti yake, na nilipata fursa ya kubaini upendo mkubwa sana alionao kwa Iryn. Mazungumzo yao yalionyesha uhusiano wa karibu na wa kipekee kati yao, na ilikuwa wazi kwamba Iryn alikuwa na nafasi maalum katika moyo wa baba yake.

Dereva aliyekuwa amekuja kutufuata ni ameajiriwa na mzee na kazi yake ni kwaajili ya kuwapeleka watoto shule na kuwarudisha, au kuwapeleka matembezini.

*****

Wiki ya tatu, nilipanga kuondoka Cape Town siku ya Ijumaa, nikijitayarisha kurudi Dar es Salaam na kuendelea na ratiba zangu za kila siku. Hata hivyo, nikiwa South sikuwa na kazi yoyote ya kufanya zaidi, nilijikuta nikicheza sana na Aria, kwani hiyo ndiyo ilikuwa shughuli pekee iliyonipa furaha na kunifanya nijisikie hai.

Kwa upande wa Mary, mawasiliano yetu yalikuwa yanaendelea vizuri, na yeye kwa upande wake alionyesha wazi hamu ya kuniona na alitaka anione mapema iwezekanavyo. Alikuwa akiendelea kuniambia kwa kusisitiza ni kwa sababu ya kutamani kuungana tena na mimi, na alilalamika kidogo kuhusu kuchelewa kwangu kurudi.

Siku ya Jumatano, nilitoka na Iryn kwenda kukagua biashara yake ya saloon, ambayo ni kubwa sana na ina wafanyakazi wengi. Iryn alionekana kuguswa sana na hali ya wafanyakazi, akilalamika kuhusu jinsi watoto wa South walivyo wavivu katika kazi zao. Alisema anafikiria kuandaa mpango wa kuajiri watu kutoka nchi za jirani ili kuongeza ufanisi na kuleta mabadiliko chanya katika biashara yake.

Ijumaa usiku, kabla ya safari yangu, nilikuwa na mazungumzo ya mwisho na baby mama yangu. Katika mazungumzo yetu, habari kubwa aliyonipa ilikuwa kuhusu kufuatilia kampuni ya mzee wake, ambayo alidhulumiwa na wabongo. Alionyesha wasiwasi kuhusu jinsi anavyoweza kusaidia katika kurejesha haki na kuleta uwazi katika mambo haya.

Nakumbuka niliwagusia kidogo kuhusu kampuni za ujenzi na umeme ambazo baba yake alikuwa anazimiliki hapa Dar es Salaam, mwanzoni mwa Season 1: EP 10. Baada ya Rais JPM kuingia madarakani mambo yalibadilika kwa kiasi kikubwa, hasa katika masuala ya tenda na kuamua kufunga kampuni na kurejea South ili kuendeleza kampuni zake zingine, huku akikabiliana na changamoto nyingi kutokana na mabadiliko hayo.

Kuna kampuni moja ya masuala ya electronics ambayo baba yake aliiacha, lakini wabongo wazee wa fursa walicheza na umiliki wake. Ingawa mzee wake alionekana kupotezea suala hilo, Iryn alisisitiza kwamba hali hii haiwezekani na alitaka kuchukua hatua dhidi ya watu waliofanya uhuni huo. Alijua kuwa alikuwa na hati zote zinazohitajika, na hivyo alikusudia kudeal na wahusika ili kurejesha haki na kumaliza tatizo hilo.

Iryn alinikabidhi hati zote na kuniagiza nianze kufuatilia suala hili pamoja na mwanasheria. Alinisihi sana kuhakikisha tunafanikiwa katika juhudi hizi. Aliongeza kuwa atarudi Tanzania mwezi Desemba kuangalia maendeleo ya kesi hiyo, na pia tutajadili kuhusu mradi wa kufanya Dodoma. Alionekana kuwa na matumaini kwamba kwa pamoja tunaweza kupata suluhisho na kuendeleza mipango yetu ya baadaye.

Niliingia chumbani kujiandaa, na Iryn alinifuatia kwa nyuma, akinikumbatia huku akizungusha mikono yake mbele yangu. Tulianza kukumbatiana kwa mahaba mazito, na hisia zangu zilianza kuwa na nguvu sana, kwani ilikuwa muda mrefu sijaonja ile furaha. Hali yangu ilizidi kuwa mbaya, nikijua jinsi nilivyokuwa na tamaa ya kuwa karibu naye.
Tulianza kupigana makisi ya mwisho mwisho lakini sikuwa na uwezo wa kufanya chochote, sababu ya afya yake. Alichokifanya mama mtoto, alikoki RPG kwa mkono wake laini, hadi pale ambapo risasi za moto zilipotoka kwa kasi.

Nilihisi mabadiliko katika mwili wangu, na nikapata wepesi wa haraka. Tulikwenda kuoga pamoja, na nilijiandaa kwa haraka ili niweze kuongea kidogo na Momo na kumuaga kabisa. Nilitaka kuhakikisha kuwa kila kitu kiko sawa kabla ya kuondoka.

Nilimshukuru Momo kwa uwepo wake nyumbani, kwani alikuwa anatusaidia sana kucheza na mtoto. Nilimuaga kwa kumkiss shavuni, na kisha tukaanza safari yetu kwenda airport. Niliongozana na Iryn pamoja na Samantha, ambao walinipa kampani na njiani tulikuwa tunapiga story za mwisho.

Baada ya kufika uwanja wa ndege, niliagana na mama Aria, kwani sikutaka aanze kunisubiri hadi nimalize mchakato wa kucheck-in. Sikuona haja ya wao kufanya hivyo. Nilianza kwa kumkumbatia Samantha, na nikamalizia kwa kumkumbatia mama mtoto. Cha ajabu, alinionyesha upendo kwa kunipa na ulimi, na hiyo ilileta hisia mpya za mshangao na furaha.

Saa 7 usiku, safari yangu ya kurudi Dar es Salaam ilianza, na njiani kote nilikuwa na furaha sana. Nikiwa kwenye ndege, mawazo yangu yalizunguka kuhusiana na watoto wangu, Junior na Aria. Nilitamani sana kuona wanangu wakianza kujuana mapema na kutembeleana, kwani ni damu zangu. Nikaona kuna umuhimu wa kumtafuta mzee wangu na kumshirikisha kuhusu jambo hili mapema ili kila kitu kiwe wazi. Nilijisemea, "I'm running out of time; let me do this." Hali hiyo ilinipa msukumo wa kutenda haraka ili kuhakikisha familia yangu inakuwa na muungano mzuri.

THE END OF SEASON 2

Thank you for your time!
🙌
 
BONUS CHAPTER 1

Nimeanza kuandika story hii nikiwa South Africa, ule wakati ambao nilikuwa na muda wa ziada, ndipo nilipoanza kuandika Season 1 na kuwapostia. Lengo langu kuu ni kuwapa ujumbe kuhusu safari ya maisha yangu, kutoka mwanzo hadi sasa, maisha ambayo bado ninaishi. Sikutaka kukata tamaa, hata baada ya kumaliza mkataba wangu na taasisi X niliamua kujiingiza kwenye uber, huku ndo nilikopata mafanikio makubwa sana.

Nilichowaandikia ni kama asilimia 30 ya maisha yangu; bado kuna mengi ambayo sijagusia kutokana na sababu za usalama wangu pia.

Kwa ufupi, tangu Iryn alipojifungua, maisha yangu yalianza kubadilika kwa kasi sana. Niliamua kuelekeza nguvu zangu kwenye familia zangu na kujituma zaidi kutafuta hela kwa bidii.

Mwezi Januari 2024, nilikutana na mzee na kumueleza kuhusu suala la kuzaa na Iryn. Alishtushwa sana na habari hizi, na hakusita kunilaumu vikali juu ya hilo. Hata hivyo, nilijitahidi sana kujitetea, hasa kwa kutumia mbinu nzuri ambazo Sister aliniambia.

Mzee aliweza kuelewa hali halisi, na mwezi Februari mwaka huu alikutana na Iryn. Tulienda Zambia kwa ajili ya hili, na baada ya kumuona Aria, mzee alikiri kwamba ni damu yetu. Changamoto iliyobaki sasa ni namna ya kumwambia mama yangu mzazi. Tumepanga kumtaarifu mwezi huu, na safari hiyo itakuwa mimi, mzee, na sister.

Kuhusu mama J, tuko shwari kabisa, na upendo kati yetu umeendelea kukua kwa kasi; tunapendana sana. Junior mwaka huu alianza shule na anaendelea kufanya vizuri sana darasani. Kampuni ya Masaki bado ipo na inaendelea kufanya vizuri sana, na pia mama mtoto amefungua biashara nyingine hapa Dar es Salaam.

Kuhusu mtoto wetu Aria, sasa ana mwaka mmoja na miezi mitatu, na tumefanana sana. Ninajitahidi kumtembelea mara kwa mara kule South, hata wiki iliyopita nilikuwa huko kumuona.

Habari njema nyingine ni kwamba mwezi wa tisa huu ninatarajia kupata mtoto wa pili na Iryn. Baada ya kuja Disemba mwaka jana, tulikutana na hali hiyo ikapelekea kushika mimba. Ingawa hatukupanga hili, hatukuwa na namna zaidi ya kukubaliana yeye kuzaa. Hali hii imefanya niwe nasafiri mara kwa mara kwenda South Africa.

Kuhusu Mary, alipata kazi Mwanza katika moja ya taasisi nyeti inayoshughulika na masuala ya BOP. Hatuko kwenye mahusiano ya kimapenzi rasmi, lakini bado tunakutana kisela.

Mipango yangu ni kuhakikisha kwamba kufikia mwakani kila kitu kiwe wazi kwa mama J. Hata hivyo, hili linasubiri wazazi watoe maamuzi, kwani tunasubiri kuona mama atachukua hatua gani akijua ukweli. Nia yangu ni kumuoa mama J kwa kufunga naye ndoa, lakini hilo litafanyika tu endapo atajua ukweli na kukubali kwa hiari yake.

Mbali na mama J, pia nina mpango wa kumfanya Iryn awe mke wangu wa pili. Sijui wazazi watasema nini kuhusu hili, lakini anatarajia kupata mtoto wa pili. Hali hii inahusisha majadiliano mazito na maamuzi ambayo ni muhimu kabla ya kuchukua hatua zozote.

Nitarudi kuwapa hadithi fupi pale ambapo nitamuweka wazi mama J kuhusu hili suala. Sijui itakuwa lini—labda mwakani au baada ya miaka miwili au mitatu. Lakini nitawapa mrejesho wa kilichotokea kwa kuwapa Season 3 au lah. Nitawapa muendelezo wa mambo yalivyokuwa, kuanzia niliporudi Dar es Salaam mwezi Julai 2023. Hapa katikatika nimepitia mambo mengi sana, hadi sasa ni vile hamjui kinachoendelea nyuma ya pazia, kumekuwa na vikao vingi sana.

Mwisho kabisa, mwakani Mungu akijalia nitaondoka Tanzania na familia yangu kwenda kufanya kazi nje. Jambo la muhimu tuendelee kuombeana uzima na mapambano mema, tuache chuki na Roho mbaya.

Bonus, inayokuja tutachambua wote fursa zinazopatikana Dar es Salaam na huenda nikawa na thanks giving kwa baadhi ya watu watakao bahatika, nikaangalia namna ya kuwa support kwenye harakati zao. Lakini hadi kufikia sasa nimeshatoa kwa watu wengi tu, ambao walikuwa wanakuja inbox na sababu zilizonyooka, na wengi ni matapeli.

Tukutane kesho!
Mzee mwakani huko nje usiniache tayari niko nje sasa tuongee kwenye hili najua unaweza kunipush sehem tukabadili maisha
 
nashauri tu swala la mama J kuna msemo mmoja wa kizungu unasema “All Men can change but there is only one women we can change for”#insiderman ninavyoona Mungu alikuandikia maisha yako uje umalizie na iryn yote ya hapa duniani kama mamaJ hatopendezwa na ww kua na iryn achana nae tu deal na mwanao Jr bs sometimes ni muhimu kufanya maamuzi magumu kwa ajili ya damu zako zote uziweke pamoja pia isitoshe iryn anampenda sana mwanaoJR OA iryne kama mke mkubwa mpe nafasi ya kipekee kuliko uyo mchaga anko
Unaongea tu ukidhani ni rahisi hivo ...Vuta picha Maisha ameanza na Mama Jr,alafu eti asipoelewa amwache Aishi na Iryn yaani hapa ni do or die,somo linatakiwa liende kwa Mama Jr kama sister Anavoelekeza japo itakuwa ngumu kumeza ila kwa Hali yoyote sioni sababu ya wao kuachana na kiunganishi Ni ndugu Yetu
 
BONUS CHAPTER 1

Nimeanza kuandika story hii nikiwa South Africa, ule wakati ambao nilikuwa na muda wa ziada, ndipo nilipoanza kuandika Season 1 na kuwapostia. Lengo langu kuu ni kuwapa ujumbe kuhusu safari ya maisha yangu, kutoka mwanzo hadi sasa, maisha ambayo bado ninaishi. Sikutaka kukata tamaa, hata baada ya kumaliza mkataba wangu na taasisi X niliamua kujiingiza kwenye uber, huku ndo nilikopata mafanikio makubwa sana.

Nilichowaandikia ni kama asilimia 30 ya maisha yangu; bado kuna mengi ambayo sijagusia kutokana na sababu za usalama wangu pia.

Kwa ufupi, tangu Iryn alipojifungua, maisha yangu yalianza kubadilika kwa kasi sana. Niliamua kuelekeza nguvu zangu kwenye familia zangu na kujituma zaidi kutafuta hela kwa bidii.

Mwezi Januari 2024, nilikutana na mzee na kumueleza kuhusu suala la kuzaa na Iryn. Alishtushwa sana na habari hizi, na hakusita kunilaumu vikali juu ya hilo. Hata hivyo, nilijitahidi sana kujitetea, hasa kwa kutumia mbinu nzuri ambazo Sister aliniambia.

Mzee aliweza kuelewa hali halisi, na mwezi Februari mwaka huu alikutana na Iryn. Tulienda Zambia kwa ajili ya hili, na baada ya kumuona Aria, mzee alikiri kwamba ni damu yetu. Changamoto iliyobaki sasa ni namna ya kumwambia mama yangu mzazi. Tumepanga kumtaarifu mwezi huu, na safari hiyo itakuwa mimi, mzee, na sister.

Kuhusu mama J, tuko shwari kabisa, na upendo kati yetu umeendelea kukua kwa kasi; tunapendana sana. Junior mwaka huu alianza shule na anaendelea kufanya vizuri sana darasani. Kampuni ya Masaki bado ipo na inaendelea kufanya vizuri sana, na pia mama mtoto amefungua biashara nyingine hapa Dar es Salaam.

Kuhusu mtoto wetu Aria, sasa ana mwaka mmoja na miezi mitatu, na tumefanana sana. Ninajitahidi kumtembelea mara kwa mara kule South, hata wiki iliyopita nilikuwa huko kumuona.

Habari njema nyingine ni kwamba mwezi wa tisa huu ninatarajia kupata mtoto wa pili na Iryn. Baada ya kuja Disemba mwaka jana, tulikutana na hali hiyo ikapelekea kushika mimba. Ingawa hatukupanga hili, hatukuwa na namna zaidi ya kukubaliana yeye kuzaa. Hali hii imefanya niwe nasafiri mara kwa mara kwenda South Africa.

Kuhusu Mary, alipata kazi Mwanza katika moja ya taasisi nyeti inayoshughulika na masuala ya BOP. Hatuko kwenye mahusiano ya kimapenzi rasmi, lakini bado tunakutana kisela.

Mipango yangu ni kuhakikisha kwamba kufikia mwakani kila kitu kiwe wazi kwa mama J. Hata hivyo, hili linasubiri wazazi watoe maamuzi, kwani tunasubiri kuona mama atachukua hatua gani akijua ukweli. Nia yangu ni kumuoa mama J kwa kufunga naye ndoa, lakini hilo litafanyika tu endapo atajua ukweli na kukubali kwa hiari yake.

Mbali na mama J, pia nina mpango wa kumfanya Iryn awe mke wangu wa pili. Sijui wazazi watasema nini kuhusu hili, lakini anatarajia kupata mtoto wa pili. Hali hii inahusisha majadiliano mazito na maamuzi ambayo ni muhimu kabla ya kuchukua hatua zozote.

Nitarudi kuwapa hadithi fupi pale ambapo nitamuweka wazi mama J kuhusu hili suala. Sijui itakuwa lini—labda mwakani au baada ya miaka miwili au mitatu. Lakini nitawapa mrejesho wa kilichotokea kwa kuwapa Season 3 au lah. Nitawapa muendelezo wa mambo yalivyokuwa, kuanzia niliporudi Dar es Salaam mwezi Julai 2023. Hapa katikatika nimepitia mambo mengi sana, hadi sasa ni vile hamjui kinachoendelea nyuma ya pazia, kumekuwa na vikao vingi sana.

Mwisho kabisa, mwakani Mungu akijalia nitaondoka Tanzania na familia yangu kwenda kufanya kazi nje. Jambo la muhimu tuendelee kuombeana uzima na mapambano mema, tuache chuki na Roho mbaya.

Bonus, inayokuja tutachambua wote fursa zinazopatikana Dar es Salaam na huenda nikawa na thanks giving kwa baadhi ya watu watakao bahatika, nikaangalia namna ya kuwa support kwenye harakati zao. Lakini hadi kufikia sasa nimeshatoa kwa watu wengi tu, ambao walikuwa wanakuja inbox na sababu zilizonyooka, na wengi ni matapeli.

Tukutane kesho!
Asante sana.
 
Asante sana Insider kwa muda na kujitoa kwako kutuletea story hii yenye mafunzo mengi. Kuna nyakati kwa sababu ya kukosa mtiririko tutakulaumu, ila hii inakuonesha kuwa story hii inagusa wengi na kutamani kutokosa muendelezo. Once again, thank you so much.
 
Nilishangazwa kuona Jimmy akihangaika kuwatafuta wanawake wengine, hasa akiwa na Amara.
Hakika Nyani haoni..... 🤣🤣🤣
Bora yeye Mama mtoto hawa fahamu.. Wewe ni mmmmmh!!!
Unaweza kujiuliza, Isabella ni nani? Ni jirani yetu kule Ethiopia-Bahir, na ni mrembo maarufu sana nchini Ethiopia, pia ni International bi***ch.
Nitakumbuka kugugo labda kama umebadili Jina 😅😅😅
Tuliposhuka chini, tulikuta mizabibu mingi imepandwa, kuzunguka upande wa nyuma nakutana na swimming pool mbili, moja ya wakubwa na nyingine kwa ajili ya watoto.

Wapenda map kama nawaona
Ni muhimu uonyeshe kwamba una nia ya kufanya mambo kwa njia sahihi na ya kidini, hata kama kuna makosa yaliyotokea.

Nimekusoma hivi kidini ni kivipi haswa naye ni Mkristo nafikiri. Fafanua hapa 😊
Hii inaweza kusaidia kumshawishi mama kuona kuwa, japokuwa mambo hayakuwa sahihi mwanzoni, lakini uko tayari kufuata njia stahiki.

Njia ipi hiyo naye ni wa kama ndoa moja kidini.. Ila umeandika mengi akusome vizuri.. Mwishoni na ya dini na ushauri wako ni kule A na kule Z 😅😅😅
Mama J anaweza kukasirika, kuumia, kuachika au hata kuchanganyikiwa. Ni lazima uwe tayari kwa hali zote hizo na kuhakikisha kuwa upo thabiti kumueleza ukweli kwa upendo na huruma.

Hakuna kitu kibaya kinaumiza mwanamke kama kujua juu ya mchepuko wa mumewe au boyfi au mchumba wake na akadanganywa halafu ndio aje ajue ukweli. Bora hata Insider angemkalisha Iryn mbali kabisa na Mama J, haswa baada ya kuona ameshtukia gemu lao.

Hili jambo aombee miujiza, hata akinyamaza bila kutaka kuachana hii kitu wanasema isikie kwa mwingine haswa mwanamke akifanywa fala na uongo mwingi sana kuwekwa kwake live. Kama kosa moja kubwa aliona U S ya mimba na baada Iryn akaenda kumdanganya na etc.. Namuonea huruma Mama J, amuache amalize masomo yake kwanza. Lolote na liwe tu.. Boraaaaaa nakuwa hafamiani nae kwa u karibu huo au hata hamfahamu mengi na hawana urafiki. Ila kama anao a mumewe napata kitu pesa etc status wachache ataamua kula nao wengine ni payback ya chini ya uvungu nae awe na mchepuko wake maisha yaende. Kama Mama J alikubali kiurahisi aendelee bila lolote basi nae anayajua tayari au ana mtu pembeni au anajipanga.

Kazi ipo, ila wamemfanyia vibaya sana sana kuwa karibu na Iryn. Tangu mwanzo niliona atayakanyaga tu.

Na Dada nae yupo vizuri sana kulinda mengi, ila ndio hivyo WiFi ni WiFi hata mle sahani moja kamwe hawezi kuwa na wewe akaaxha kufata ya Kaka. Na anapeta tu na raha kupita before.. Mama J ooh Mama J.

Maisha levels zinaingilia mengi.
Mtazo binafsi:
1. Fanya juu chini, usiwe chanzo Cha kuachana na mama J, collect your mistakes. kiufupi pigania na inusuru ndo yako na Mama J

2. Mama Ariana(Iryn) SI mwanamke was kumwacha, nasema hivi SI sababu ya uchumi wake, Bali upendo alionao kwako, usimuumize hisia zake kwako, two children, tayari Ni mke wako pia.

Dini inaruhusu? 😂😂😂
Kuna maisha duniani tunaishi tu siku zisonge. A na Z eeeh
 
SEASON 02
CHAPTER 41

“BY INSIDER MAN”

CONTINUE:

Kwa upande wangu, sikutarajia hata kidogo kukutana na mama mkubwa. Niliposogea, nilimsalimia kwa heshima. Alinijibu kwa upole, kisha akaniangalia kwa makini, macho yake yakitua pia kwa Aria aliyekuwa kamshika. Sekunde chache zilivyopita, alinitazama tena na kusema kwa sauti tulivu, “Umefanana sana na mtoto.” Kabla sijapata nafasi ya kujibu, Mama Janeth naye alidakia, akinitazama kwa tabasamu na kusema, “Ni kweli kabisa, mnafanana sana wewe na Aria.”

Niliishia kutabasamu baada ya kusikia maneno yale kutoka kwa mama mkubwa, kisha nikatafuta sehemu ya kuketi. Sebleni palikuwa na wageni wengi sana, hali iliyonifanya nijisikie kutokuwa na utulivu, lakini sikuwa na namna. Nilibaki pale, nikijaribu kuzoea hali ile, huku nikionesha utulivu ambao sikuwa nao ndani yangu.

Baada ya dakika nyingi kupita, niliamua kwenda chumbani kwa Iryn ili kumsalimia na kumjulia hali. Nilipofika, niligundua hakuwa peke yake, alikuwa na wageni wawili. Niliwasalimia wote kwa heshima, na bila kusita, Iryn alinitambulisha kwa marafiki zake akisema, “Hawa ni marafiki zangu, tumesoma nao chuo Ufaransa.”

Nilimuuliza Iryn kuhusu maendeleo ya kidonda chake, na aliniambia kuwa anaendelea vizuri kabisa. Tulipokuwa tunaendelea kuzungumza, ghafla Jimmy aliingia chumbani. Mara tu Iryn alipomuona, uso wake ulibadilika kabisa.

JIMMY: “Hata ukininunia, freshy tu."

IRYN: “Jimmy, nakuchukia sana!"

JIMMY: “Hujaanza leo, na sishangai kabisa.”

IRYN: “Jana ulimpeleka wapi Insider?”

Jimmy alinitazama kwa wasiwasi, akihisi labda nimemueleza Iryn kuhusu tulikokuwa usiku huo. Nilimpa ishara kuwa sina ufahamu wowote juu ya jambo hilo.

JIMMY: “Sawa, tulienda Soho kuburudika, na tulirudi salama."

Iryn, akiwa amekasirika, alitazama pembeni na kuona bakuli karibu yake. Alilichukua kisha akamrushia Jimmy kwa hasira, huku akimfyonza kwa dhihaka.

Na wakati huu, Amara aliingia chumbani na kuanza kuuliza, “Shida ni nini?" Jimmy, kwa haraka, alimnyanyua juu juu na kutoka naye hadi sebleni. Lilikuwa tukio la ghafla na la kufurahisha, kiasi kwamba kila mtu aliishia kucheka, hata wageni.

Niliamua kuondoka chumbani ili kumpa Iryn nafasi na wageni wake. Hata hivyo, wakati nilipokuwa natoka, ghafla nilisikia akiniita kwa sauti ya upole, “Subiri kidogo...”

IRYN: “Darling, where are you going?”

MIMI: “Nipo mke wangu, huna haja ya kuwa na wasiwasi.”

IRYN: “Usije ukanitoroka kama jana ulivyofanya.”

MIMI: “ Leo nipo na wewe baby.”

Baada ya kurudi sebleni, nilitambua kuwa watu watatu hawakuwepo, nao ni dada yangu, Vivian, na Samantha. Nilipouliza, niliambiwa kuwa walitoka kwenda supermarket kununua vitu kwa ajili ya mama mtoto.

Baada ya takriban saa moja, mzee Virgil aliwasili na familia yake yote. Ilikuwa siku ya kipekee kwani niliweza kuwafahamu wadogo zake wote kupitia mama mdogo, kasoro kaka yake ambaye mzee alimzaa na mwanamke mwingine.

Mchana tulikula chakula cha pamoja, ambacho kiliagizwa kutoka kwa wapishi wa nje. Baada ya lunch, mama Janeth alitusalimu na kutuaga, akituambia kwamba anaondoka kwa safari ya kwenda Tanzania, kisha ataendelea na safari yake kwenda Marekani (USA).

Kabla ya mama Janeth kuondoka, tulipata nafasi ya kuzungumza. Nilimshukuru sana kwa kujitoa kwake na kuhakikisha Iryn anajifungua salama. Mama Janeth alinituliza, akisema kwa upole, “Iryn ni binti yangu, huna haja ya kunishukuru kwa hili.”Maneno yake yalikuwa ya faraja, yakiniondolea wasiwasi.

Jioni nilikutana na dada yangu, na tukatafuta sehemu tulivu kwa ajili ya mazungumzo yetu. Mara tu baada ya kuketi, dada alianza kuzungumza kwa hisia, akilalamika kuhusu tabia zangu mpya ambazo nimeanza kuonesha waziwazi mbele ya mama J. Aliuliza kwa upole lakini kwa msisitizo, “Kipindi kile ulipolala nje, ulikuwa wapi?” Akiongeza kwa tahadhari, alisema, “Na kama utathubutu kunidanganya, itakuwa ndio mwisho wa maongezi yetu.” Maneno yake yalikuwa na uzito, yakinifanya nifikirie kwa makini kuhusu majibu yangu.

Niliwaza pale na kuamua ni bora niwe mkweli ili tuweze kumaliza mambo haya.

MIMI: “Nilikuwa na mwanamke mwingine.”

SISTER: “Una matatizo gani? Tuliongea vizuri kabisa kuhusu haya, lakini bado unaendelea kuyafanya. Je, unanidharau mimi dada yako? Nilitegemea utaanza kufocus na watoto wako, lakini unazidi kuhangaika na wanawake wengine?”

MIMI: “Dada yangu, najua nimezingua. Mwanamke huyu alinifata Dodoma mwenyewe, na kipindi kile nilikuwa nimegombana na mama J, na Iryn alikuwa hana dalili za kurudi.”

Majibu yangu yalimfanya dada yangu aonekane mwenye wasiwasi zaidi, lakini pia nilijua ni muhimu kuwa mkweli ili kuweza kuendelea mbele.

SISTER: “Nisikilize kwa makini, bro. Usinione kama mjinga kukusaidia na kesi zako za kila siku ambazo unafanya kwa makusudi. Leo nakupa onyo la mwisho, kama una wanawake nje na hawa mama watoto wako, nikaja kupata kesi, utakuwa umefunga kufuli la mimi kukusaidia.”

MIMI: “Dada yangu, usifike huko, nimekuelewa na sitokuangusha.”

SISTER: “Na kilichofanya uondoke bila kumuaga mama J ni nini? Unaonesha dharau kama hizi kwa mke wako.”

MIMI: “Mimi naondoka tumegombana kwa sababu alimpigia mama yangu simu na kumwambia nililala nje. Niliona ananichonganisha na mama yetu, kwa kitu ambacho hana ushahidi nacho.”

SISTER: “Unataka kuachana na mama J, kisa Iryn?. Ukitaka mambo yako yaanze kuharibika tena, bhasi jichanganye ufanye huo ujinga unaotaka kuufanya, utayakumbuka maneno yangu.”

MIMI: “Siwezi kumuacha mama J, hili nakuapia dada yangu.”

Baada ya kumaliza tofauti zetu, dada aliniahidi kunisaidia kuliweka sawa suala la Iryn. Alinishauri nisubiri mtoto afike miezi sita ndipo nianze hatua za kuwaambia wazazi. Alisema ni bora nianze kumshirikisha mzee, na kisha yeye ndiye atakayemwambia mama. Maneno yake yaliniweka katika hali ya matumaini, kwani nilijua kwamba kwa msaada wake, naweza kupata njia sahihi ya kukabiliana na hali hii.

Dada alinionyesha mbinu ya kuanza kumuandaa kisaikolojia mama J, akisema kwamba nianze kufanya hivi taratibu ili aanze kuhisi mapema kuwa nina mtoto nje. Hata hivyo, nilishindwa kumuelewa alimaanisha nini, hivyo ilibidi nimuulize.

MIMI: “Mbinu gani natakiwa kuanza kuitumia?”

SISTER: “Katika maongezi yenu, unaweza kumuuliza, 'Hivi, ukija kufahamu kuwa nina mtoto nje, utafanyaje?' Inatakiwa uwe unamuuliza mara kwa mara hadi pale atakapozoea na kuona ni jambo la kawaida.”

MIMI: “Dada yangu, sio kwa mama J, hachelewi kulianzisha.”

SISTER: “Hawezi kufanya chochote kwa sababu atakuwa hana ushahidi. Kwa mara ya kwanza atapata shida kadri anavyozidi kusikia kutoka kwako, lakini atazoea na kuona ni jambo la kawaida. Wewe cha kuzingatia ni kuwa unachukua note ya majibu anayotoa, na utakuwa unanitumia.”

Maneno yake yalikuwa na maana, lakini nilihisi bado kuna changamoto kubwa katika kutekeleza mbinu hiyo. Lakini dada alizidi kukazia kwamba mbinu hii itaanza kumuandaa kisaikolojia, na baada ya muda atazoea hali hiyo. Alisisitiza kwamba hata nitakapokuja kumpa taarifa rasmi, haitaleta shida sana na atakuwa na uwezo wa kuelewa vizuri. Maneno yake yalinipa matumaini, kwani niliweza kuona uwezekano wa kumfikia mama J kwa njia ambayo ingekuwa rahisi na ya busara.

Kuhusu suala la kumpa taarifa rasmi, dada alishauri ni bora nisubiri hadi nitakapomalizana na wazee na kila kitu kipo sawa. Alisema kwamba ni hapo ndipo nianze hatua za kumwambia mama J. Dada alinihakikishia kwamba atanisaidia kadri anavyoweza kwa kutumia uwezo wake wote hadi mambo yawe sawa. Maneno yake yalijenga imani ndani yangu, na nilihisi kuwa na msaada wa dada yangu kutanisaidia kukabiliana na changamoto hii.

Baada ya kumaliza maongezi yetu muhimu, dada aliniaga na kuniambia kwamba kesho, Jumapili, ataondoka kurudi Tanzania. Alisisitiza kwamba pindi nitakaporudi Dar es Salaam, nimtaarifu ili aje tuyaweke sawa na mama J.

Nilimuuliza dada kama amelipia tiketi ya ndege, naye akasema kwamba wifi yake, Iryn, alikuwa amelipia tayari na amemwingizia pesa nyingi kwenye akaunti yake, ingawa hakutaka pesa hizo. Dada alifungua app ya benki na kunionesha kiasi ambacho aliingiziwa, na nilibaki nikishangaa.

Mwishoni, dada alinipongeza kwa kuwa baba, akisema kuwa Aria ni damu yetu halali. Maneno yake yalinipa furaha kubwa na kunitia moyo zaidi. Tuliagana kwa kukumbatiana, kisha tukarudi ndani kuendelea na mambo mengine, kwani tulikuwa tumetumia muda mwingi sana kwenye maongezi yetu.

Kibarazani, akina Jimmy walikuwa wanacheza last card, na mimi nilijiunga nao, tukawa jumla wanne: Mimi, Jimmy, Vivian, na Samantha. Mchezo ulikuwa mzuri sana, maana tulianza hadi kuweka hela kwa mshindi, na hali hiyo ilifanya ushindani uwe mkali. Baadaye, dada alikuja na tukawa jumla watano, na mchezo ukawa na ladha mpya, huku kila mmoja akijaribu kushinda kwa njia yake. Kicheko na furaha vilijaza hewa, na ilikuwa ni fursa nzuri ya kuondoa mawazo na kufurahia muda pamoja.

Ninataka niwaambie kuhusu undugu wa Jimmy, Iryn, Vivian, na Samantha. Ninarudisha hadi chapter 9, siku ambayo nilifika Ethiopia kwa mara ya kwanza. Katika siku hiyo, dada watatu walikuja kumpokea Iryn, ambapo alinitambulisha. Yule dada mkubwa ndiye alikuwa Vivian, mtoto wa Pili wa mama mkubwa, huku Jimmy akiwa mtoto wa kwanza akifuatiwa na mdogo wake katika wale wawili waliokuwa wamekuja kumpokea Iryn.

Hawa watatu wa kwanza, Vivian, Jimmy, na mdogo wao, wanatoka kwenye tumbo moja, wakiwa na mama na baba mmoja, ingawa baba yao alishatangulia mbele za haki. Mama mkubwa alizaa watoto wengine wawili na mume mwingine, Samantha na mdogo wake wa mwisho. Huyu mdogo wa mwisho ndiye mmoja kati ya wale dada wawili wadogo ambao Iryn alinifahamisha kama wadogo zake.

Mama mkubwa ana jumla ya watoto watano. Watatu wa kwanza wanashiriki baba mmoja, wakati hawa wawili wa mwisho wanashiriki baba mwingine. Kati ya watoto hao watano, Jimmy pekee ndiye mtoto wa kiume. Kwa Iryn, watoto hawa ni kama binamu zake (cousins), ingawa yeye hupenda kuwaita dada na kaka.


Nilikaa sana pale nyumbani, na hatimaye mimi na Jimmy tuliondoka saa 6 usiku kurudi hotelini. Nilipitia mapokezi kuchukua kadi yangu, na dada wa mapokezi akaniambia kuwa kuna ujumbe wangu. Alinipa kadi na kikaratasi kidogo. Nilielewa kinachoendelea mara moja, na Jimmy aliona yote hayo, akabaki kutabasamu.

Baada ya kuingia chumbani, nilifungua kile kinote na kugundua kuwa ilikuwa ni namba ya simu ya Nala. Niliweka pembeni na kuelekea bafuni kuoga. Baada ya kumaliza kuoga, nilijilaza kitandani, nikiwa nimechoka lakini mawazo yakiwa hayajakaa sawa. Nilianza kuyapitia kwa kina yale mazungumzo yangu na sister, nikitafakari maana yake na mwelekeo wa mambo.

Ukweli ni kwamba, Sister alizungumza mambo mengi sana, lakini kubwa kuliko yote, aliniapia kwamba nikifanya makosa tena, basi atajiondoa kabisa kwenye huu msala, na niachwe nipambane peke yangu. Sister ndiye kiungo muhimu katika kufanikisha hili jambo, hivyo niliona ni busara kutulia na kuwekeza nguvu zangu kwa umakini kwenye familia zangu.

Niliwaza sana kuhusu wazo la kumuacha Mary, lakini kila nilipofikiria, nilijikuta nikipoteza nguvu kwa sababu bado nampenda. Hata hivyo, kutokana na ushauri wa Sister, niliona sina budi kufanya hivyo. Ni bora nimuache mapema kuliko kusubiri na kuleta matatizo makubwa zaidi huko mbeleni.

Niliwaza sana na hatimaye nikaamua kwamba nitakaporudi Dar es Salaam, nitamtafuta Mary ili tuzungumze wazi kuhusu hili suala. Kilichonipa faraja kidogo ni kwamba Mary tayari alikuwa anafahamu kinachoendelea kuhusu mahusiano yangu na Iryn, hivyo nilihisi mazungumzo yetu yangeweza kuwa ya uwazi zaidi.

Jambo lingine lililoanza kunisumbua kichwani ni jinsi wazazi wangu watakavyopokea taarifa za mimi kuzaa na Iryn. Swali kubwa lililozunguka mawazoni mwangu lilikuwa, je, watalichukuliaje suala hili? Nilijua kuwa na mtihani mgumu mbele yangu, lakini kwa sababu Sister aliahidi kunisaidia, nilijisemea kwamba kila kitu kitakuwa sawa. Hata hivyo, sikupuuza uzito wa hali hiyo.

Kwa upande wangu, nilitamani sana kuona Junior na Aria wakifahamiana tangu utotoni ili waweze kujenga uhusiano wa karibu na bond nzuri. Kuhusu hili suala, nilihisi mzee ndiye anayeweza kunipa ushauri mzuri zaidi. Hivyo, nilianza kupata hamasa ya kumtafuta mapema ili tuweze kuzungumza na kupanga namna bora ya kufanikisha hili.
*****

Asubuhi, baada ya kuamka, nilimpigia simu mama J ili kumsalimia, lakini hakupokea, hivyo nilihisi labda alikuwa ameenda kanisani. Niliingia bafuni haraka kuoga na kujiandaa ili tuweze kwenda kwa mama mtoto. Ilikuwa saa mbili asubuhi, na nilihisi muda ulikuwa unayoyoma. Nilimpigia simu Jimmy kumjulisha kuwa tuanze safari, lakini naye hakuwa akipokea. Hatimaye, nikaamua kwenda kumgongea chumbani kwake.

Baada ya kufika kwenye chumba chake, maana yeye alikuwa floor ya juu, niligonga mlango na alitoka kufungua. Alikuwa haja jiandaa, hivyo nilipompa taarifa ya kuondoka, aliniambia nimsubiri ajiandae haraka. Nikamwambia atanikuta kwenye restaurant nikimsubiri.

Nilielekea kwenye restaurant kupata kifungua kinywa, na wakati huo nilikuwa nawasiliana na Iryn, ambaye alikuwa akinisisitizia nianze safari mapema ili niweze kucheza na mtoto. Baada ya nusu saa, nilimuona Jimmy akiwa ameongozana na mwanamke mwenye asili ya kizungu, na nikahisi huenda alikuwa amelala naye. Hali hii iliniacha na maswali mengi kichwani mwangu.

Walipofika, waliketi pamoja nami, na Jimmy alifanya utambulisho wa kawaida, na mimi pia nilimsalimia yule dada. Waliagiza kifungua kinywa, na baada ya kumaliza, tuliondoka kwenye eneo hilo, tukimwacha dada akisubiri usafiri wa kumpeleka kwake.

Wakati tuko kwenye Uber, nilianza kumuuliza Jimmy maswali kuhusu yule mwanamke. Nilikuwa na hamu ya kujua zaidi kuhusu mahusiano yao, na jinsi alivyomjua.

MIMI: “Bro, yule ni nani tena?”

JIMMY: “Tulikutana juzi Soho club, tukabadilishana namba, jana baada ya kuchat naye, nilimpanga aje hotelini akakubali.”

MIMI: “She’s a hoe?”

JIMMY: “I don’t think so, anafanyia kazi kwenye moja ya ubalozi hapa South Africa.”

Nilibaki kimya, nikitafakari kwa undani. Jimmy alikuwa amenishinda kabisa kwa tabia zake. Nilijiuliza mara ngapi ameweza kukutana na wanawake kama yule, na ni wangapi mpaka sasa? Spidi yake ilikuwa ya kutisha, na ilinifanya nishindwe kuelewa vizuri mwelekeo wake. Nilijikuta nawaza kama angeweza kudhibiti hali hii, au kama ilikuwa sehemu ya maisha yake ya kila siku.

Baada ya kuwasili, mazingira yalionekana kuwa kimya na tulivu sana. Tulipofika kibarazani, mtoto wa Jimmy alionekana akicheza peke yake. Jimmy alimnyanyua kwa furaha, kisha tukaingia ndani kuzungumza na mama mtoto ili tupate kujua ratiba ya siku ile.

Pale sebuleni, dada yangu alikuwa amemshika mtoto, na tukaingia kwenye mazungumzo kuhusu safari yake. Alisema anatarajia kuanza safari saa 11 jioni. Wakati huo, Iryn alitoka sebuleni na kuja kukaa pembeni yangu. Alionekana kuzidi kuimarika kadri siku zilivyokuwa zinaenda, jambo lililonipa faraja. Mazungumzo yetu yaliendelea kwa utulivu, na hali ilikuwa ya amani.

Baada ya kula chakula cha mchana, mimi, dada yangu, na mama mkubwa tuliamua kuwa na kikao chetu binafsi. Tulitafuta utulivu nje kwenye bustani, mbali na kelele na muingiliano wa watu wengine. Hapa tuliweza kuzungumza kwa uwazi na utulivu, tukijadili mambo muhimu bila usumbufu wowote. Mazingira yalikuwa tulivu, na kikao kilikuwa na uzito wa kipekee.

Mama alianza kwa kumshukuru sana sister kwa kujitolea kwake kwa kipindi chote hadi Iryn alipojifungua. Sister alisaidia sana, hasa kwenye mazoezi na mbinu mbalimbali za kuhakikisha Iryn anajifungua salama. Kwa kuwa sister yangu tayari alikuwa na watoto wawili, alikuwa na uzoefu mwingi ambao ulimsaidia kumwelekeza Iryn vyema wakati wa ujauzito na hadi wakati wa kujifungua. Mama alionyesha shukrani za dhati kwa mchango wake mkubwa.

Ukiachana na yote, Sister aliweza pia kutengeneza mahusiano mazuri sana na wifi zake, kama Vivian na Samantha. Wote walionekana kumpenda sana dada yangu kwa jinsi alivyojitoa na kujali. Uhusiano wao ulijengeka kwa upendo na uelewa, na hilo lilifanya familia kuwa karibu zaidi.

Kuhusu suala la mimi kumpa mimba binti yake, mama alisema hawezi kusema lolote kwa sababu Iryn mwenyewe alifanya maamuzi yake, na ni mtu mzima ambaye anaelewa vyema anachokifanya. Alionyesha kutambua kwamba Iryn alikuwa na uwezo wa kuchukua maamuzi yake binafsi, na hakutaka kuingilia zaidi. Hii ilileta hali ya unafuu kidogo, ingawa suala hilo bado lilikuwa na uzito wake.

Mama aliniuliza swali ambalo lilikuwa zito kulijibu:

“Una mpango na malengo gani juu ya Iryn?"

Nilihisi uzito wa swali hilo, lakini nilijua dhumuni la mama kuuliza ni nini. Nikajua kwamba ni muhimu kufikiri kwa umakini na kuepuka kutoa ahadi ambazo huenda nisitekeleze. Kwa kutumia busara na tahadhari, nilimjibu hivi:

MIMI: “Asante mama kwa kuniuliza swali hili muhimu. Ninamuheshimu sana Iryn na ninatambua nafasi yake katika maisha yangu. Nimeliona hili suala kwa uzito wake, na ninataka kuhakikisha kwamba mimi na Iryn tunajenga msingi mzuri wa ushirikiano, hasa kwa ajili ya ustawi wa mtoto wetu. Nataka tuchukue mambo hatua kwa hatua, huku tukijadiliana na kupanga vizuri mustakabali wa familia yetu. Ninaendelea kutafakari juu ya mpango mzuri na utakaokuwa bora kwa wote, na nataka kuhakikisha kwamba kila kitu kinawekwa wazi na kwa manufaa ya pande zote mbili.”

Mama na Sister waliniangalia kimya kwa muda, wakitafakari majibu yangu. Mama, hasa, alionekana kutotarajia jibu langu. Niliona machoni mwake kwamba alitarajia kitu tofauti, labda ahadi thabiti au mpango ulio wazi zaidi kuhusu mustakabali wangu na Iryn.

MAMA: “Naona umejibu kwa hekima, lakini bado sijapata uhakika. Wewe na Iryn, mna mpango wa kuwa pamoja au hili ni suala tu la mtoto?”

MIMI: “Naelewa unavyohisi mama, na ni swali lenye uzito. Kwa sasa, mimi na Iryn tunaendelea kuzungumza juu ya mstakabali wetu. Kipaumbele chetu kikubwa ni kuhakikisha mtoto anakua katika mazingira bora, lakini bado tupo kwenye hatua ya kufikiria kwa kina jinsi ya kutatua hali yetu ya kibinafsi. Siwezi kusema kwa hakika wakati huu, ila nataka iwe wazi kwamba sitamtelekeza Iryn wala mtoto wetu.”

MAMA: “Hilo ni jambo jema kusikia, lakini ningependa kuona mnapanga mustakabali wenye utulivu zaidi, hasa kwa ajili ya binti yangu. Matarajio yangu ni kwamba, kama kuna upendo na nia njema, basi mtachukua hatua ya kusonga mbele pamoja.”

MIMI: “Ninakubaliana na wewe kabisa mama, Iryn ni mtu muhimu kwangu na sina mpango wa kufanya maamuzi ya haraka bila kufikiria kila mtu aliyehusika. Ni muhimu kwangu kwamba wote tunakuwa na maelewano mazuri kwa ajili ya mtoto na hatimae, kwa Iryn pia.”

MAMA: “Nashukuru kwa uwazi wako, ningependa tu kuona unachukua hatua thabiti, maana Iryn anastahili uhakika. Si kwamba nakuwekea shinikizo, lakini ningependa kuona binti yangu akiwa kwenye mikono salama.”

MIMI: “Naelewa mama, na ninakuhakikishia kwamba natilia maanani kila kitu unachosema. Nitafanya kila niwezalo kuhakikisha mambo yanaenda vizuri kwa Iryn na mtoto wetu.”

Mama aliniangalia kwa makini, na nilihisi alikua akiwaza, labda akijiuliza, “Huyu jamaa ana akili sana.” Nilijua kuwa niliyajibu maswali yake yote kwa umakini na hekima. Hata dada yangu alionesha tabasamu, akionyesha kushangazwa na jinsi nilivyoweza kujibu maswali ya mama kwa njia ambayo haikuniingiza kwenye mtego.

Mama aliendelea na mazungumzo, akasema angependa kuwajua wazazi wetu, akisisitiza kuwa ni muhimu kwa mustakabali wa mtoto. Aliongeza kwamba sasa sisi tumeshakuwa muunganiko wa familia, na ni muhimu kuimarisha uhusiano huu kwa kuhakikisha kila mmoja anajua historia na asili ya mwingine. Mama alionyesha kuwa na hamu ya kujenga mshikamano ndani ya familia yetu, ili mtoto apate msingi mzuri wa malezi na urithi wa kihisia.

Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, Sister alijiandaa kwa ajili ya safari yake ya kurudi Tanzania. Hali ilikuwa ya huzuni kidogo, lakini pia ya furaha kwa sababu tulikuwa tumepata muda mzuri wa kuzungumza na kujenga uhusiano wetu zaidi.

Saa 9 mchana, Sister alitoka na begi lake na kutuaga pale sebuleni. Tulitoka nje na kupiga picha za pamoja kama kumbukumbu ya wakati wetu mzuri pamoja. Baada ya hapo, mimi na Vivian tulimpa kampani hadi uwanja wa ndege. Safari hiyo ilikuwa ya furaha, ingawa tulihisi huzuni kidogo kwa sababu ya kuachana. Tulizungumza mengi katika gari, tukijadili mipango ya baadaye na sister kuahidi kukutana tena na kina Vivian hivi karibuni.

Tukiwa airport, tulizungumza mambo mengi sana, na Sister aliendelea kunisitiza kwamba nitakaporudi Dar es Salaam, nimpe taarifa ili aje nyumbani kuweka sawa masuala yangu na mama J. Kabla ya kucheck in, aligana na Vivian kwa kukumbatiana kwa upendo, na niliona jinsi walivyokuwa na uhusiano mzuri. Baada ya hapo, tuliondoka maeneo hayo, tukielekea nyumbani, tukiwa njiani story na Vivian ziliendelea na niseme hawa mashem zangu wananikubali na tunapatana sana.

Usiku, niliwasiliana na mama J pamoja na mwanangu Junior. Nilimdanganya kwamba nipo China nikifuatilia mzigo, na baada ya hapo nitatoka kwenda South Africa kumuona Iryn, ambaye amejifungua mtoto. Mama J hakutoa maoni mengi kuhusu hilo, zaidi alisema atawasiliana na Iryn kumpa hongera. Ingawa alionekana kutokuwa sawa na hali hiyo, nilijua ujumbe wangu ulikuwa umemfikia.
*****

Wiki inayofuata, ambayo ilikuwa ni wiki ya kwanza ya mwezi wa 7, idadi ya wageni iliongezeka sana pale kwa Iryn. Ndugu zake kutoka Ethiopia walifika, na pia marafiki zake wa chuo waliosoma pamoja Ufaransa walikuwa wakija na kuondoka. Sebuleni, kila kona ilikuwa imejaa zawadi za mtoto, na hapo ndipo nilipogundua kwa kweli kwamba Iryn alikuwa na mtandao mpana wa watu. Hali hiyo ilionyesha jinsi alivyokuwa akipendwa na kuungwa mkono na watu wengi, na ilifanya moyo wangu ujaze faraja na kujivunia kuwa sehemu ya maisha yake.

Siku ya Jumatano, mama mkubwa aliondoka kurudi Ethiopia ili kuendelea na majukumu yake. Pia, dada wa kazi kutoka Ethiopia alifika nyumbani kusaidia katika kazi mbalimbali. Iryn alieleza kuwa hakutaka dada wa kazi mwenyeji kwa sababu ya tabia zao, hivyo alihitaji mtu ambaye wangeweza kuendana kiutamaduni. Hali hiyo ilionyesha umuhimu wa mazingira yanayofanana na utamaduni wao, na niliona ni busara kwa Iryn kuchagua mtu ambaye angeweza kuleta utulivu na uelewano katika familia.

Siku ya Jumapili, Jimmy pamoja na familia yake waliondoka kurudi Ethiopia, hivyo aliyebaki ni dada Vivian. Baada ya kuondoka kwa Jimmy, nilienda kukaa na Iryn, maana idadi ya watu ilikuwa imepungua, na mle ndani tulikuwa jumla watano. Hali hiyo ilituletea fursa nzuri ya kuzungumza kwa undani zaidi na kujenga uhusiano wetu.

Wiki ya pili ya mwezi wa 7, Jumatatu, bibi yao ‘Momo’ alifika South Africa kumuona kitukuu chake. Aliwasili jioni, na mimi na Samantha tulikwenda kumpokea pale airport. Momo, ambaye sasa ana umri wa miaka 70, ni bibi mwenye uzoefu wa maisha, lakini bado ana nguvu za kujiendesha. Momo ana tabia ya kutabasamu na kuwa na nishati, na nilijua kwamba uwepo wake ungeongeza furaha na umoja katika familia yetu.

Tangu tupo kwenye gari hadi tulipofika nyumbani, Bibi alikuwa na furaha sana na alionyesha hamu kubwa ya kumuona kitukuu wake. Alikuwa akizungumza kwa lugha yao ya nyumbani, lakini Samantha alikuwa ananiambia kila kilichokuwa kinaendelea, akitafsiri maneno ya bibi kwa urahisi. Ilikuwa ni furaha kubwa kusikia shauku ya bibi, na niliweza kuhisi upendo wake wa dhati kwa familia.

Baada ya kufika nyumbani, Iryn hakuwa mbali kumpokea bibi yake, na walikumbatiana kwa furaha na kumkaribisha ndani. Kitu cha kwanza bibi alichomba ni kumuona kitukuu wake, na alifurahi sana baada ya kumuona. Uso wake ulijawa na tabasamu la furaha, na Iryn alionekana pia akifurahia moment hiyo. Nilijua kuwa bibi alikuwa na matumaini makubwa kwa ajili ya kitukuu chake, na nilihisi furaha kuona jinsi familia ilivyokuwa ikijenga uhusiano mzuri katika kizazi tofauti.

Baada ya bibi kurudi nyumbani, mazingira yalichangamka sana, kwani bibi ni mwongeaji sana, na wajukuu zake wanampenda sana. Bibi alisema ataendelea kukaa na Iryn na hafikirii kurudi Ethiopia mapema, jambo lililomfanya Iryn ajisikie vizuri. Iryn ni mjukuu ambaye bibi yake anampenda sana, na hii ni kwa sababu Iryn humjali sana bibi yake, akimpa huduma na kumuhudumia kwa upendo.

Kwa upande wangu, tangu nilipofika South Africa, tayari wiki mbili zilikuwa zimepita, na nilipanga kuondoka Jumapili ya weekend. Niliangalia hali yangu na kugundua kwamba kuendelea kukaa huku kungeweza kuathiri mambo yangu mengi, kuanzia kampuni hadi biashara zangu. Nilijua ni muhimu kurejea nyumbani ili kusimamia masuala yangu na kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa. Ingawa nilifurahia wakati niliokuwa pamoja na Iryn na familia, nilihisi ni lazima nitafute njia ya kuleta uwiano kati ya majukumu yangu ya kifamilia na biashara zangu.

Kesho yake asubuhi, nilimfata Iryn chumbani ili niweze kuzungumza naye kuhusu suala langu la kuondoka. Pembeni yake kulikuwa na diary, hivyo niliichukua na kuanza kuisoma. Niliona alikuwa akiandika mipango yake, na nilicheka baada ya kuona ameandika mpango wa kuanza gym.

Of course, alikuwa ameanza kunenepa sana kutokana na kuwa mama na vyakula anavyokula, lakini bado haikufanya apoteze uzuri na shape yake. Kinyume chake, niliona kuwa mabadiliko hayo yaliongeza mvuto wake, na alikuwa akionekana kuwa na uzuri wa kipekee ambao unakuja na umama.

MAMA ARIA: “Darling, unacheka nini?”

MIMI: “Nimefurahi kuona una mpango wa kuanza Gym, lakini bado mapema sana.”

MAMA ARIA: “I know, baada ya miezi 3 nitaanza mazoezi ya kupunguza huu mwili.”

Nami, nikasogea kukaa pembeni yake;

MIMI: “Nimekumiss baby mama.”

Iryn alianza kuangalia usawa wa bunduki yangu na akanishika kidevu changu na tukaanza kuangaliana pale;

MAMA ARIA: “Are you horny?”

MIMI: “Ofcourse yes.”

MAMA ARIA: “Pole! nadhani unakumbuka siwezi kusex kwasasa hadi nipone vizuri, doctor alishauri baada ya miezi 3, ila mwezi ujao nitaenda kuangalia maendeleo.”

MIMI: “Naelewa usijali, mimi nitavumilia kwa hili.”

Usawa wa matiti yake ulionekana kulowa maziwa, kwani chuchu zake zilikuwa bado zimesimama. Baada ya kumuona vile, ilibidi nimwambie kwamba analowa, akicheka kidogo kwa aibu. Alijua kwamba hali hiyo ni ya kawaida kwa mama anapokuwa katika kipindi hiki, lakini nilijua kwamba ilikuwa ni muhimu kwake kujisikia vizuri kuhusu mwili wake.

MAMA ARIA: “Mwanao hataki kunyonya, halafu mama yake nina maziwa mengi sana. Uwe unamsaidia mwanao kunyonya, kwani naishia kuyakamua na kuyamwaga. Nikupe unyonye? Yatakusaidia kiafya.”

Nilihisi aibu baada ya kusikia haya maneno kutoka kwa Iryn. Aliponigeukia na kunipa ishara ya kunyonya, sikuona sababu ya kukataa, kwani alikuwa anayamwaga. Nilijisemea, si afadhali nikanywa mimi kuliko yamwagwe. Nilianza kuyanyonya taratibu hadi aliposema basi, ndio kuacha na yalikuwa ni matamu sana.

MAMA ARIA: “Vipi matamu?”

MIMI: “Yeah! Aria anafaidi sana.”

MAMA ARIA: “Mwanao mpole kama wewe, naona huyu atarithi tabia zako.”

MIMI: “Bado mtoto, akikua ndio tutajua tabia zake, hata Junior alikuwa mpole kama Aria, ila sasahivi ni balaa.”

Tulipoanza mazungumzo yetu, alizungumzia suala lake la kurudi shule na akaniambia kuwa analiwazia kwa umakini. Nami nikamshirikisha mpango wangu wa kurudi shule mwezi wa kumi, ambapo alinisisitiza kwa upendo kuwa ni vema nisomee masomo yangu ya masters nchini Afrika Kusini ili tuwe karibu na mtoto wetu.

Ingawa wazo hilo lilikuwa zuri, nilijua kuwa kulikuwa na changamoto nyingi zinazoweza kufanya isiwezekane. Hivyo, nilimpatia jibu lililofikiriwa vizuri, ambalo alielewa kwa upole na busara.

Nilimwambia kwa upole,

Baby mama, nikisomea huku, kumbuka kuwa mambo mengi yanaweza kuyumba, kuanzia kampuni yako hadi miradi yangu. Ufuatiliaji wa karibu ni muhimu sana. Acha mimi nisomee Dar ili niwe karibu na biashara zetu. Kuhusu Aria, nitakuwa nakuja mara kwa mara kuwasalimu, siwezi kukaa muda mrefu bila kumuona binti yangu. Kama vile wakati wa ujauzito wako ulivyokuwa ukija Dar es Salaam mara kwa mara, sasa ni zamu yangu kuja Cape Town. Tutaendelea kuwa karibu, hata kama nitakuwa huku.”

Mama Aria alifurahi sana kusikia maneno yangu, na hakuwa na la kusema zaidi. Baadaye, nilimueleza kuhusu mpango wangu wa kuondoka Jumapili. Hata hivyo, kwenye suala la kuondoka, alionekana kulipokea tofauti na aliniomba niondoke mwisho wa mwezi. Nilijaribu kumsihi kwa upole, na kumuomba aniruhusu niondoke wiki ijayo, huku nikiahidi kuwa nitarudi mapema kwa ajili ya sherehe ya "Simchat Bat" ya mtoto wetu.

Baada ya kumaliza mazungumzo yetu, aliamua kwenda kuoga. Wakati huo, Aria alikuwa ameamka, hivyo nilimbeba na kutoka naye sebleni ili tupate muda wa kukaa pamoja. Sikuwa na shughuli nyingi za kufanya kipindi hicho nikiwa Afrika Kusini, zaidi ya kutumia muda wangu mwingi kucheza na Aria. Sikutoka kwenda sehemu yoyote mara kwa mara, isipokuwa tu kwenda supermarket pale panapohitajika.

Haikupita muda mrefu kabla mama Aria hajarudi kwenye seating room, na kunijulisha kuhusu ujio wa mgeni. Aliniambia kuwa anayekuja ni kaka yake, ambaye ni wa kwanza kwa upande wa mama mwingine. Nilikuwa nimeshaongelea kidogo kuhusu huyu kaka yake, katika Season 1: EP10.

Mchana ule, kaka yake alifika nyumbani kumsalimia Iryn pamoja na mtoto, akiwa ameongozana na mpenzi wake. Hii ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona kaka yake kwa upande wa baba. Ni kijana mwenye haiba fulani ya "manton," kwa mbali anataka kuendana na rappa AKA.

Tulisalimiana pale, kisha tukaingia kwenye mazungumzo ambapo alinikaribisha sana Afrika Kusini kwa ukarimu. Iryn akaanza kumuuliza kaka yake kuhusu maisha na kazi kwa ujumla. Ingawa kaka yake Iryn yuko vizuri kiuchumi, tatizo lake kubwa ni matumizi ya madawa, jambo ambalo limemuharibu sana. Niliwahi kugusia kuhusu hili hapo awali.

Baada ya kupata chakula cha mchana kwa pamoja, kaka yake na mpenzi wake waliondoka. Mama Aria kisha alinipa taarifa nyingine kwamba siku ya Jumamosi tungeenda nyumbani kwa baba yake. Aliongeza kuwa kuna mambo kadhaa watakayokwenda kuyapanga na mzee wake, na akaniambia atanishirikisha katika hayo mazungumzo siku hiyo.

*****

Hatimaye, siku ya Jumamosi ilifika, siku ambayo ilikuwa ni ya kwenda kwa mzee Virgil, baba mkwe wangu. Mzee Virgil alikuwa akija mara kwa mara nyumbani kumuona mjukuu wake, na kitendo cha Iryn kujifungua kilimfurahisha sana. Hakuwa na maswali mengi kuhusu malengo yangu kwa binti yake, wala hakujishughulisha na hilo. Kile kilichomgusa zaidi kilikuwa ni upendo mkubwa aliokuwa nao kwa mjukuu wake. Ilionekana kana kwamba alikuwa akitamani kwa muda mrefu sana kupata mjukuu, na sasa alikuwa akifurahia kila muda aliokuwa naye.

Saa nne asubuhi, gari lilikuja kutuchukua kwa ajili ya safari ya kwenda nyumbani kwa mzee Virgil. Tuliondoka watatu tu, mimi, Iryn, na Samantha. Safari yetu ilikuwa na umbali wa takriban kilomita 45 hadi kufika nyumbani kwa mzee, Somerset West, ambayo iko pembezoni mwa Cape Town. Huu ni sawa na umbali wa kutoka Mwenge hadi Bagamoyo. Njia ilikuwa nzuri, na tulikuwa na mazungumzo mazuri kwenye gari, tukiwa na hamu ya kufika na kumtembelea mzee.

Mzee aliamua kujenga na kuishi nje kidogo ya mji wa Cape Town, na tulivyoanza kuingia katika maeneo haya, nilikuwa nikiona majumba ya kifahari ambayo yalivutia sana macho yangu. Mazingira ya hapa ni kama Ulaya, ni masafi, na kote ni lami, hakuna vumbi. Nyumba zimepangiliwa kwa ustadi wa hali ya juu, mandhari yake ikiwa ya kijani kibichi. Wakati tunaingia Somerset, tulikuwa tukipishana na magari ya kifahari, hali iliyoongeza uzuri wa eneo hili.

Gari lilipaki nje ya geti kubwa, na haikuchukua muda mrefu likafunguliwa, ingawa pale getini hakuonekana mtu yeyote aliyefungua. Tulipofika ndani, gari lilitembea kwa mwendo wa takriban mita 100, na njiani tulipishana na bustani nzuri ya kuvutia.

Baada ya kufika usawa wa nyumba, tulishuka na mbele yangu nikaona bonge la mjengo wa kifahari, aina ya villa. Ilikuwa nyumba kubwa ya kisasa ya ghorofa moja, na kila kipengele chake kilionekana kuwa kimepangwa kwa umaridadi. Ujenzi wa nyumba hiyo ulikuwa wa kisasa na wa kuvutia, ukionyesha ushawishi wa hali ya juu wa usanifu. Ilionekana kama ni mahali pazuri pa kuishi, ambapo mandhari ya karibu iliongeza uzuri na raha ya mazingira.

Wakati huu, mama yake mdogo alitoka kutupokea akiwa na wanae, na haikuchukua muda mzee Virgil akatoka kumkaribisha binti yake. Alikuwa na furaha kubwa sana kutuona na aliomba kumbeba Aria, Mzee Virgil alionyesha upendo mkubwa kwa mjukuu wake.

Nilisikia sauti ya upole kutoka kwa Iryn ikinikaribisha kwa furaha:

“Baba Aria, hapa ndiyo nyumbani, karibu sana.”

Tulipokuwa tunaingia ndani, nilikutana na bonge la msebule uliojaa mapambo ya thamani kubwa kama crystals na marbles. Nimeingia katika nyumba nyingi za kifahari, lakini sebule ya kwa Mzee Virgil ilikuwa ya kipekee kabisa. Ukarabati wa ndani ulikuwa wa kiwango cha juu, na kila kipande cha samani na mapambo kilionyesha umaridadi na mtindo wa kipekee, ikifanya iwe mahali pa kuvutia.

Iryn alianza kunitambulisha kwa wadogo zake wa pale nyumbani kwa upande wa mama mdogo. Mama mdogo ana watoto watatu tu; mtoto wa kwanza ni wa kike, ambaye nilimfahamu nikiwa hospitalini, alikuwa akitarajia kuanza chuo mwaka huo na wawili ni wa kiume, wenye umri wa miaka 13 na 8. Walionekana kufurahia kuniona na walikuwa na shauku ya kujua kuhusu mimi, hali ambayo ilileta maongezi yawe mengi zaidi.

Baada ya lisaa, wageni watano walifika, na kati yao, mmoja tu alikuwa na asili ya Afrika; wengine wote walikuwa wazungu. Kati ya wageni hao, mmoja alikuwa ni babu, na aliomba amshike Aria. Mzee Virgil alifanya utambulisho pale, akimwambia Iryn kwamba wale ni ndugu zake. Iryn alifurahi sana kusikia hivyo, kwani kwa upande wake alikuwa kwenye mission ya kuwasogeza karibu ndugu wote wa upande wa baba yake. Hali hiyo ilileta hisia za umoja na furaha, na ilikuwa ni fursa nzuri kwa familia kukutana na kuimarisha uhusiano wao.

Tulipata chakula cha mchana pamoja, na baada ya wageni kuondoka, Iryn alitoka nje na mzee wake kufanya mazungumzo. Walionekana kuwa na mazungumzo ya karibu na ya kina, hii ilikuwa ni nafasi nzuri kwao kujadili mambo ya familia na kujenga msingi mzuri wa ushirikiano.

Wakati huu, nilikuwa na mama mdogo tukifanya mazungumzo, ambapo aliendelea kunikaribisha kwa ukarimu. Alizungumza kwa upole, akielezea furaha yake kuwa na familia pamoja na jinsi alivyovutiwa na ujio wangu.

Baada ya lisaa, Iryn aliniita nitoke nje ili tuweze kuzungumza na mzee wake. Alimweleza baba yake jinsi ambavyo nimekuwa msaada mkubwa sana katika biashara zake. Mzee wake alishukuru kwa dhati na kusema niendelee kuwa na moyo huo huo. Alionyesha furaha kubwa kwa mimi kuwa sehemu ya familia yake.

Kuhusu suala la kumzalisha binti yake, mzee hakuwa na neno lolote la kukatisha tamaa. Badala yake, alitutakia mafanikio mema na kusema angetamani kuona tukifika mbali zaidi katika maisha yetu.

Mzee aliondoka pamoja na mjukuu wake, na kutuacha mimi na Iryn tukiendelea na mazungumzo yetu. Iryn alianza kunishirikisha kuhusu kazi kubwa aliyonayo katika kuzisimamia kampuni za baba yake. Aliniambia kuhusu mali mbalimbali anazomiliki baba yake hapa Afrika Kusini, ikiwa ni pamoja na apartments, mashamba ya zabibu, na kampuni ambayo ni miongoni mwa waexporter wakubwa wa wines.

Alielezea jinsi alivyohusika katika kusimamia shughuli hizi na jinsi anavyopanga mipango ya kuziendeleza zaidi. Hali hiyo ilionyesha kiwango cha juu cha kujitolea kwake na uelewa wa biashara, na ilinipa mtazamo mzuri kuhusu familia yao na malengo yao ya kifamilia.

Tangu siku ile tulipokutana na Iryn na kuanza mahusiano yetu, hakujawahi kuwa na wakati ambapo alitaja utajiri wa baba yake. Badala yake, alijikita zaidi katika kunieleza kuhusu majukumu aliyokabidhiwa ya kuwa msimamizi wa kampuni za baba yake. (SEASON 1: EP40)

Hii ndiyo siku nilipogundua kwamba mzee Virgil si mtu wa kawaida, kwani ana utajiri wa kutisha. Lakini ukimwona, unaweza kumchukulia kuwa mtu wa kawaida sana. Kama mnavyojua, wazungu hawana tabia ya kujionesha kama wana fedha, tofauti na sisi Waafrika, ambao mara nyingi tunapenda maonyesho ya kifahari.

Iryn aliendelea kunieleza jinsi mzee wake alivyotokea kunikubali sana. Aliniambia kwamba amemshauri atulie nami, kwani kwa sasa wanaume wengi hawaaminiki. Maneno hayo yalikuwa ya faraja kutoka kwa Iryn, yakiwa na uzito wa maana. Nilimuhakikishia kuwa nitajitahidi kumsaidia kadri ya uwezo wangu, kwa sababu uaminifu ni msingi wa mahusiano yetu.

Nilimuuliza Iryn kuhusu mgawanyo wa mali za mzee na jinsi anavyowaangalia watoto wengine, wakiwemo Smith na kaka yake mkubwa, ambapo jumla yao ni watoto sita wa mzee Virgil. Iryn alijibu kwamba hadi sasa, watoto wanne tu wanatambulika rasmi, ambao ni yeye pamoja na wadogo zake watatu kwa upande wa mamdogo. Aliongeza kuwa kuhusu kaka yake na Smith, bado hawajazungumza na mzee wao kuhusu suala hilo, lakini wanatarajia kuangalia namna nyingine ya kufanikisha mambo yao.

MIMI: “Na vipi kuhusu mama mdogo?”

IRYN: “Mama mdogo si mmoja wa mrithi wa hizi mali. Alifunga ndoa ya mkataba na mzee, na moja ya makubaliano ni kwamba hatahusika kwenye urithi wa mali zaidi ya watoto tu.”

MIMI: “Baba yako ni genius sana.”

IRYN: “Mali nyingi sana mzee kazipata akiwa na mama yangu. Ndiyo maana unaona mimi nikiwa kipaumbele cha kwanza, hata wakati ambapo hatuko kwenye maelewano na mzee. Kwa upande wake, alikuwa anapata tabu sana kuhusu hili.”

Iryn alikuwa huru kunifungukia mambo mengi sana. Alisema kwamba hata kitendo cha kuzaa na mimi si kwamba alikurupuka tu kufanya maamuzi hayo, bali alifikiria kuhusu mustakabali wake na mali za baba yake. Alieleza kwamba kipindi kile baada ya kurudi kutoka South Africa kumwona mzee wake, aliona kuna umuhimu wa kuwa na watoto ambao wataweza kurithi mali hizo, kwani hata yeye atakufa.

Iryn alifikiria kwa kina na kugundua kwamba hakuna mtu anayemuamini zaidi yangu kwa sasa. Alijisemea atafanya kila mbinu ili anizalie mtoto, lakini lengo lake kubwa ni kuhakikisha urithi wa mali za baba yake unakuwa salama. Aliendelea kueleza kwamba, mama mkubwa wake na ndugu zake wanamuona kama mjinga sana, lakini hawajui mipango yake ya siri. Hakuwa na nia ya kuona mali ambazo mama yake alizichuma na baba yake zikipotea kwa watoto wengine. Kwa hiyo, alichukua maamuzi haya magumu, lakini yaliyojikita katika manufaa ya kizazi chake.

Nilishusha pumzi ndefu sana, nikijisemea kwamba kumbe Iryn yuko very calculated na alikuwa na mipango mikubwa ambayo sikuwa na habari nayo. Nilikuwa bado siamini kwamba Iryn anaweza kubeba mimba kwa sababu ya kijinga kama aliyokuwa akinambia, lakini leo ndiyo nimeelewa kuwa alikuwa anawaza extra miles. Iryn alikuwa na malengo ya dhati, na sasa nilianza kuelewa uzito wa maamuzi yake.

IRYN: “Baba Aria, naomba nisamehe sana kwa kutokushirikisha hili mapema, nilijua ipo siku ungekuja kujua ukweli. Nilikuwa nauwezo wa kuzaa na mwanaume yoyote yule ninayemtaka hata kwa kumlipa na nikapata mtoto, lakini niliona wewe ndio unafaa.”

MIMI: “Naomba tuachane na haya, Aria ni mtoto wetu tuangalie namna gani ya kumlea na kumtunza ili tuje tujisifu kuwa naye.”

IRYN: “Babu yake kafurahi sana kumuona, ndio mjukuu wake wa kwanza. Pia unakumbuka nilikwambia kuhusu afya ya mzee wangu? Hana maisha marefu sana hapa duniani ni pesa tu zinafanya anaendelea kuishi.”

MIMI: “Nakumbuka baby, naamini ataishi muda mrefu zaidi hapa duniani, tusichoke kumuombea.”

IRYN: “Natamani kupata mtoto mwingine, hata nikiwa natembea barabarani, kushoto nina Aria na kulia nina mdogo wake nakuwa na bodyguards wangu.”

MIMI: “Naona unanipa greenlight ya kukupa mimba ya pili.”

IRYN: “Yes! Why not, unafikiri atakuwa nani zaidi yako?”

MIMI: “Sawa baby subiri kwanza Aria akue mengine tutapanga.”

Baada ya mazungumzo marefu, tulianza kutembea na kutalii mazingira ya nyumba yao. Aisee, nyumba yao imezungukwa na bustani nzuri, huku ukubwa wa kiwanja ukiwa kama ekari tano. Tuliposhuka chini, tulikuta mizabibu mingi imepandwa, kuzunguka upande wa nyuma nakutana na swimming pool mbili, moja ya wakubwa na nyingine kwa ajili ya watoto. Nyumba hiyo ilikuwa na mvuto wa kipekee, na mbele zaidi kulikuwa na nyumba ndogo ya wafanyakazi ambao kazi yao ni kutengeneza zile bustani na kumwagilia mimea.

Nilishindwa kuelewa kwanini Iryn ameshindwa kukaa na baba yake na ameamua kupanga aishi peke yake. Sikutaka kumuuliza kuhusu hili, kwani nilijua Iryn ana akili sana na huwa hafanyi jambo lolote bila sababu. Nilihisi kuwa kuna mambo mengi nyuma ya uamuzi wake, lakini kwa heshima yake, niliona bora nisubiri hadi atakapojisikia kuzungumzia.

Saa mbili usiku, tulipata dinner ya pamoja, na baada ya hapo tuliagana kuwa tunaondoka. Walitusindikiza hadi nje, ambapo dereva alikuwa amekuja kutufuata tayari. Tukiwa pale nje, mzee aliendelea kuongea na binti yake, na nilipata fursa ya kubaini upendo mkubwa sana alionao kwa Iryn. Mazungumzo yao yalionyesha uhusiano wa karibu na wa kipekee kati yao, na ilikuwa wazi kwamba Iryn alikuwa na nafasi maalum katika moyo wa baba yake.

Dereva aliyekuwa amekuja kutufuata ni ameajiriwa na mzee na kazi yake ni kwaajili ya kuwapeleka watoto shule na kuwarudisha, au kuwapeleka matembezini.

*****

Wiki ya tatu, nilipanga kuondoka Cape Town siku ya Ijumaa, nikijitayarisha kurudi Dar es Salaam na kuendelea na ratiba zangu za kila siku. Hata hivyo, nikiwa South sikuwa na kazi yoyote ya kufanya zaidi, nilijikuta nikicheza sana na Aria, kwani hiyo ndiyo ilikuwa shughuli pekee iliyonipa furaha na kunifanya nijisikie hai.

Kwa upande wa Mary, mawasiliano yetu yalikuwa yanaendelea vizuri, na yeye kwa upande wake alionyesha wazi hamu ya kuniona na alitaka anione mapema iwezekanavyo. Alikuwa akiendelea kuniambia kwa kusisitiza ni kwa sababu ya kutamani kuungana tena na mimi, na alilalamika kidogo kuhusu kuchelewa kwangu kurudi.

Siku ya Jumatano, nilitoka na Iryn kwenda kukagua biashara yake ya saloon, ambayo ni kubwa sana na ina wafanyakazi wengi. Iryn alionekana kuguswa sana na hali ya wafanyakazi, akilalamika kuhusu jinsi watoto wa South walivyo wavivu katika kazi zao. Alisema anafikiria kuandaa mpango wa kuajiri watu kutoka nchi za jirani ili kuongeza ufanisi na kuleta mabadiliko chanya katika biashara yake.

Ijumaa usiku, kabla ya safari yangu, nilikuwa na mazungumzo ya mwisho na baby mama yangu. Katika mazungumzo yetu, habari kubwa aliyonipa ilikuwa kuhusu kufuatilia kampuni ya mzee wake, ambayo alidhulumiwa na wabongo. Alionyesha wasiwasi kuhusu jinsi anavyoweza kusaidia katika kurejesha haki na kuleta uwazi katika mambo haya.

Nakumbuka niliwagusia kidogo kuhusu kampuni za ujenzi na umeme ambazo baba yake alikuwa anazimiliki hapa Dar es Salaam, mwanzoni mwa Season 1: EP 10. Baada ya Rais JPM kuingia madarakani mambo yalibadilika kwa kiasi kikubwa, hasa katika masuala ya tenda na kuamua kufunga kampuni na kurejea South ili kuendeleza kampuni zake zingine, huku akikabiliana na changamoto nyingi kutokana na mabadiliko hayo.

Kuna kampuni moja ya masuala ya electronics ambayo baba yake aliiacha, lakini wabongo wazee wa fursa walicheza na umiliki wake. Ingawa mzee wake alionekana kupotezea suala hilo, Iryn alisisitiza kwamba hali hii haiwezekani na alitaka kuchukua hatua dhidi ya watu waliofanya uhuni huo. Alijua kuwa alikuwa na hati zote zinazohitajika, na hivyo alikusudia kudeal na wahusika ili kurejesha haki na kumaliza tatizo hilo.

Iryn alinikabidhi hati zote na kuniagiza nianze kufuatilia suala hili pamoja na mwanasheria. Alinisihi sana kuhakikisha tunafanikiwa katika juhudi hizi. Aliongeza kuwa atarudi Tanzania mwezi Desemba kuangalia maendeleo ya kesi hiyo, na pia tutajadili kuhusu mradi wa kufanya Dodoma. Alionekana kuwa na matumaini kwamba kwa pamoja tunaweza kupata suluhisho na kuendeleza mipango yetu ya baadaye.

Niliingia chumbani kujiandaa, na Iryn alinifuatia kwa nyuma, akinikumbatia huku akizungusha mikono yake mbele yangu. Tulianza kukumbatiana kwa mahaba mazito, na hisia zangu zilianza kuwa na nguvu sana, kwani ilikuwa muda mrefu sijaonja ile furaha. Hali yangu ilizidi kuwa mbaya, nikijua jinsi nilivyokuwa na tamaa ya kuwa karibu naye.
Tulianza kupigana makisi ya mwisho mwisho lakini sikuwa na uwezo wa kufanya chochote, sababu ya afya yake. Alichokifanya mama mtoto, alikoki RPG kwa mkono wake laini, hadi pale ambapo risasi za moto zilipotoka kwa kasi.

Nilihisi mabadiliko katika mwili wangu, na nikapata wepesi wa haraka. Tulikwenda kuoga pamoja, na nilijiandaa kwa haraka ili niweze kuongea kidogo na Momo na kumuaga kabisa. Nilitaka kuhakikisha kuwa kila kitu kiko sawa kabla ya kuondoka.

Nilimshukuru Momo kwa uwepo wake nyumbani, kwani alikuwa anatusaidia sana kucheza na mtoto. Nilimuaga kwa kumkiss shavuni, na kisha tukaanza safari yetu kwenda airport. Niliongozana na Iryn pamoja na Samantha, ambao walinipa kampani na njiani tulikuwa tunapiga story za mwisho.

Baada ya kufika uwanja wa ndege, niliagana na mama Aria, kwani sikutaka aanze kunisubiri hadi nimalize mchakato wa kucheck-in. Sikuona haja ya wao kufanya hivyo. Nilianza kwa kumkumbatia Samantha, na nikamalizia kwa kumkumbatia mama mtoto. Cha ajabu, alinionyesha upendo kwa kunipa na ulimi, na hiyo ilileta hisia mpya za mshangao na furaha.

Saa 7 usiku, safari yangu ya kurudi Dar es Salaam ilianza, na njiani kote nilikuwa na furaha sana. Nikiwa kwenye ndege, mawazo yangu yalizunguka kuhusiana na watoto wangu, Junior na Aria. Nilitamani sana kuona wanangu wakianza kujuana mapema na kutembeleana, kwani ni damu zangu. Nikaona kuna umuhimu wa kumtafuta mzee wangu na kumshirikisha kuhusu jambo hili mapema ili kila kitu kiwe wazi. Nilijisemea, "I'm running out of time; let me do this." Hali hiyo ilinipa msukumo wa kutenda haraka ili kuhakikisha familia yangu inakuwa na muungano mzuri.

THE END OF SEASON 2

Thank you for your time!
You are talented in storytelling, this is another line you could use to make good money, apart from what you are currently doing
 
Back
Top Bottom