Inaendelea
Swala la kuambiwa nitapigwa risasi ya kichwa liliniogopesha sana. Kwa South Africa mtu akikuambia atakuuwa usifikiri anatania, anakuua kweli. Nilianza kuona maisha yangu yapo hatarini.
Nilikaa wiki bila kumtafuta Khumbu maana nilianza kumwogopa japo bado nilikuwa nampenda. Nilimpigia simu na kumwelezea kuwa kuna mtu alinipigia simu akaniambia ataniua kwa kunipiga risasi, na nikamweka wazi “nahisi anayetaka kuniua anataka kuniua kwa sababu yako. Naomba unieleze kwa nini nataka kuuliwa kwa ajili yako, ubaya upi nimekufanyia hadi nistahili kuuawa? Au mimi kukupenda wewe ndio kosa ninalostahili kuuawa?” Khumbu akajifanya hajui chochote kuhusu hilo, ila mimi niliamini ni bwana zake ndio wanaotaka kuniua. Nikaendelea kumwelezea huku nikitia huruma kuwa hata sababu ya yeye kutokuja Bloemfontein licha ya mimi kumtumia nauli ni hao jamaa, nikazidi kumwambia “Khumbu you have wrecked my heart, you have broken my heart into million pieces”, Yeye aliendelea kusisitiza hajui chochote kuhusu hilo. Binafsi niliona kabisa nikiuendekeza moyo wangu nitafia South Africa. Ila jamani acheni, moyo ukipenda ni ngumu sana kujinasua.
Swala la yeye kuja Bloemfontein sikutaka tena kumwuliza maana nilijua nitakuwa najisumbua tu japo nilikuwa natamani atamke “Konda msafi kesho napanda basi nakuja". Nilikuwa natamani aje nimchakate kwa mara ya mwisho maana kila nikifumba macho nakuwa kama naliona umbo lake, tako lake linavyoning’inia, halafu nawaza mimi ndio basi tena kuligusa hili tako dah! roho inauma kinyama, natamani Mungu afanye muujiza Khumbu amfanye kuwa mke wangu, tupotee tukaishi sehemu isiyojulikana, hata tuondoke South Africa tuende hata bara la Antactica, nikawe mimi na Khumbu tu.
Baada ya kuona maisha yangu na Khumbu hayapo tena nikaanza kuwakumbuka dada zangu watanzania. Nikaanza kujiambia mimi ni foreigner tu, sina thamani katika nchi ya watu. Khumbu hawezi kuwaacha kaka zake akanichagua mimi foreigner, acha nirudi Tanzania nikatafute dada zangu na mimi nipate kuthaminiwa. Kuna demu mmoja alikuwa anaishi Sinza nilimuimbisha kipindi flani niliporudi Bongo nikaanza kumfikiria. Pia kuna demu mmoja mbongo nilikutana naye Kampala nikaanza kumkumbuka. Bahati nzuri namba zao na email address ya yule wa Uganda nilikuwa nazo. Nikaanza kuwatafuta. Wote nikawapata, mawasiliano yaliyokufa nikayafufua. Yule aliyekuwa anasoma Uganda akaniambia alishamaliza form six, akaenda Marekani na sasa yupo Mwanza kwa wazazi wake. Nikaanza kujitetea kwa nini nilikuwa kimya kipindi chote hicho na kwa nini leo nimeamua kuibuka na kumtafuta. Mimi bhana ukinipa dakika za kunisikiliza ngumu sana kuchomoa. Labda nisiwe na hela. Nikiwa na hela huwa nakuwa na confidence ya ajabu. Nikamsomesha, nikampanga akapangika, nikamwambia acha niangalie utaratibu wa kurudi Bongo tuje tufanye mchakato wa kuoana kisha turudi tuje tuishi South Africa. Demu alifurahi kweli, akawa anaomba aje South Africa hata leo ili tuishi pamoja. Mie nikamwambia avumilie kidogo tu, ninakuja hadi kwao Mwanza. Basi jina likabadirika nikaanza kuitwa mume. Nikipiga simu hadi marafiki zake wanaitwa ili waongee na shemeji yao, hadi mama mtu anapewa simu anisalimie, wanawake bhana!
Kwa hiyo nikawa nawasiliana na huyu demu karibia kila siku, na kidogo kidogo ikawa inanisaidia kutokumuwaza Khumbu ile kwa sana, japo Khumbu sikuweza kumsahau moja kwa moja. Huyu demu wa Sinza naye ikawa ahadi ni zilezile kama nilizomuahidi huyu aliyekuwa anasoma Uganda. Lengo langu lilikuwa wote kuwaweka karibu ili nikifika Bongo nichague yupi anafaa zaidi maana ilikuwa kama miaka sita imepita toka tuonane. Yule wa Uganda alikuwa ananitumia picha kwenye email, pia alikuwa facebook, so kwenye picha bado alikuwa anaonekana ana mvuto lakini sikutaka kudanganyika na picha. Iko hivi huyu wa Uganda nilikutana naye stand ya mabasi nilikuwa nakata ticket ya kutoka Kampala kuja Dar, nakumbuka kulikuwa na kampuni moja inaitwa Akamba ndio nilikata ticket ya hilo basi. Yeye alimsindikiza mdogo wake kuja kukata ticket. Tukiwa pale kwenye ofisi za Akamba ndio nikamuona. Alikuwa na mdogo wake, nilikuja kujua baadae kuwa yule mwingine alikuwa mdogo wake. Ilikuwa ni pisi moja kali sana black beauty flani ya kihaya. Pale sehemu ya kukatia ticketi sikutaka kumsomeshea pale,nilihisi ningevuta hisia za watu maana foleni nzima alikuwa ana-shine out, hivyo ningemfuata pale lazima watu wangekuwa macho kodo, hivyo kwa kuwa nilijua kwa sababu anasafiri nitapata nafasi ya kumuimbisha kwenye basi maana niliwasikia wanaongea Kiswahili nikajua hawa tunasafiri pamoja, so nikapanga ikifika zamu yangu ya kukata ticket nikamwombe mkatisha ticketi anipe siti ya jirani na huyu black beauty. Kweli ilipofika zamu yangu nikamwomba mkatisha ticket anipe siti ya jirani na huyu black beauty, bila hiyana nikapewa hiyo siti.
Siku ya safari ilikuwa kesho yake, naingia kwenye basi, black beauty simuoni bali namkuta yule mwenzake. Basi nikakaa siti moja na huyu mwenzake kinyonge huku najiuliza ile pisi iko wapi? Ikabidi nianzishe maongezi na huyu mwenzake ili nipate nafasi ya kumwulizia huyu mwenzake waliyekuwa naye jana pale kwenye ofisi za Akamba yuko wapi? Mazungumzo yalipokolea ndio nikamwuliza, mwenzake yuko wapi? Akanijibu yule ni dada ake anaitwa Amina, alimsindikiza tu kuja kukakata ticket, yeye kabaki hajasafiri. Basi baada ya kupata hayo maelezo nikamweleza kuwa dada ako nimemzimia kinoma, na hii siti nilimuomba mkatatisha ticket anipe specifically kwa ajili yake. Basi yule mdogo mtu akacheka sana hadi machozi yakamtoka. Stori zikawa tamu kweli, njia nzima full furaha tu. Bill za chakula tunashare. Akanipa namba yake na ya dada ake, akaniahidi ujumbe wangu ataufikisha kwa dada ake kabla hata mimi sijamtafuta. Nilipofika Dar nilimtafuta baada ya kama siku mbili hivi, demu alifurahi sana. Mdogo mtu tayari alikuwa keshamaliza kazi ya kunitambulisha kwa dada ake, mimi ikawa kazi ya kufukia mabonde tu ambayo mdogo mtu alikuwa hajayaona. So, huo ndio ulikuwa mwanzo wa kujuana na hii pisi kali ya kihaya iliyokuwa inasoma Kampala ambayo kwa kiasi kikubwa ilinisaidia kuniondolea mawazo ya Khumbu.
Nikipata nafasi nitaielezea hii pisi ya Sinza jinsi tulivyokutana maana nayo ina historia kubwa sana kwenye maisha yangu, na ina mchango wa kunisaidia kumsahau Khumbu. In fact hii pisi ninimezaa nayo, niliporudi bongo nikaitandika mimba bila kutarajia, sijui ilinitegeshea.
Kitendo cha kuambiwa nitapigwa risasi na kitendo cha Khumbu kula nauli kilisababisha niamue kujitahidi kumsahau Khumbu. Japo moyo ulikuwa ni vigumu kukubaliana na hili lakini akili ilikuwa inaniambia “Konda msafi kwenu watapeleka jina tu ukiendelea kumng’ang’ania Khumbu".
Niliamua kumrudisha ulingoni yule demu niliyemfanyia vitimbi. Haikuwa hata kazi kubwa kumrejesha. Nilimwambia tu nadhani break imeisha, na sasa nipo sawa kiakili hivyo tunaweza kuendelea na mahusiano yetu.
Huyu demu wa Bloemfontein yeye aliamua kuwekeza kwangu. Ila alikuwa na wasiwasi sana kuwa huenda yeye sio changuo langu maana kila mara alikuwa ananiambia anahisi ananibore. Yule demu kusema ukweli alikuwa na sura ya kawaida ila alikuwa na mkia kufuru. Alikuwa na tako kubwa sana. Nilishawahi kumpiga picha ya uchi halafu nikawarushia masela wa Durban wakasema huo mzigo unahitaji kuwekwa kwenye makumbusho. Yule demu alikuwa na tako kubwa, yaani kubwa.
Itaendelea.