2010 World Cup South Africa, Mzansi for sure,
Mnamkumbuka rafiki yangu Sandile yule mpiga picha wa gazeti la Sunday tribune? Huyu mwana alikuwa poa kinoma. Ni kati ya watu kwenye watu. Jamaa kanipa support sana. Kazini kwakwe palikuwa sio mbali na chuoni. Alipiga picha moja hivi wa uwanja wa Moses Mabida akashinda Award flani hivi. Alikuwa mpiga picha wa hilo gazeti anayeheshimika sana.
Pale kazini kwakwe walikuwa wanatoa chakula for free kwa wafanyakazi, na hiyo ni kampuni moja kubwa sana ya magazeti kwa South africa. Maisha yangu yote ya chuo sikuwa na shida sana kwa upande wa msosi, Sandile alikuwa mwana kinoma.
World cup ilipofika Sandile alinifanyia mpango wa kupata kitambulisho kama mwandishi wa habari. Nilipata accreditation ya kuingia sehemu za VIP kwenye maeneo yote kipindi cha world cup. Nilipata nafasi ya kukaa meza moja na huyu mtunzi wa official song for 2010 world cup sijui wanamuita Kay naan aliyeimba wimbo wa "Wave the flag"
Siku moja Sandile alikuwa anacover story ya world cup mitaa ya Inanda. Inanda ndo kwao na Khumbu. Kipindi cha world cup kulitengwa sehemu za kuonyeshea mpira kwa ajili ya watu ambao hawataweza kwenda uwanjani. Serikali iliweka masinema makubwa ya kuonyeshea mpira nadhani kila township na sehemu za fukwe za bahari. Kwa hiyo kila jioni tukitoka chuo Sandile alikuwa ananichukua tunaenda kwenye hizo sehemu.
Kwenye hizo sehemu kulikuwa na matents yaliyojengwa maalumu kwa ajili ya VIP kama wanasiasa na wasanii wakubwa kama wakina Kay naan (sijui kama jina lake naliandika kwa usahihi). Hizo sehemu ya VIP kulikuwa kama hotel vile, na yeyote anayeingia humo anakula anachotaka bure. Hivyo mimi na Sandile tulikuwa tunaingia humo kwa sababu tulikuwa na accreditation na kucheck world cup kwa raha zote, maana full kula bata na kumeet na watu wazito wazito.
Tulipokuwa Inanda nikapata wazo la kumtafuta Khumbu. Nikawa nafikiria nitamwitaje Khumbu mbele ya Sandile?Kumbuka Sandile alishanionya kuhusu mahusiano yangu na Khumbu.
Itaendelea.