Jinsi mapenzi ya mtoto wa Kizulu Durban South Africa yalivyotaka kunitoa roho

Jinsi mapenzi ya mtoto wa Kizulu Durban South Africa yalivyotaka kunitoa roho

Haya tunaendelea, hapa tunaelekea lile tukio lililonifanya nimkimbize Khumbu nikiwa na boxer tu kama nimepandwa na kichaa, of course kila binadamu ana elements za ukichaa maana siku ile sikuamini kama ni mimi.

Nilipoupata ule mpunga kutoka kwa Don wa sembe nikasema afe punda huu mzigo lazima Khumbu apate share, hata kama ataamua kuuchukua wote sawa tu ilimradi roho yangu ipate hitaji lake.

Nikaona njia pekee ni kumuibukia kwao. Maana niliona nikimpigia simu nimwambie kuna hela hapa njoo uchukue atahisi kama namnunua, of course niliamua kumnunua ila niliona kwenda direct ataniona kavu.

Kesho yake sikuingia darasani, asubuhi tu tayari nipo stend kwenye foleni ya kwenda Inanda. By the way kule mnapanda daladala kwa foleni, sio kama huku kupigana vikumbo mwenye nguvu ndio anapanda. Huko ukifika stand unapanga foleni kama upo bank.

Sikutaka kumpigia simu wala kutuma sms. Nilitaka kumfanyia ambush tu. Kuhusu baba watoto wake nilikuwa sijali tena, uwazimu ulikuwa kama umenipanda kichwani. Mara huyu nishafika, bahati nzuri nikamkuta hata nguo za kulalia hajabadilisha. Nikamkuta yeye, bibi yake na mwanae.

Akanikaribisha kwa heshima zote japo alikuwa na sura ya kujiuliza, this nigga what is he here for? Halafu Khumbu ana kicheko flani kama cha wadada wa kiswahili, akacheka akaniangalia, kama vile anajiuliza huyu jamaa vipi asubuhi asubuhi yote hii? Haogopi kufumuliwa ubongo? Anyway demu ukishamula tena mara nyingi hata hazihesabiki hana nguvu kubwa ya kukuintimidate. Kwa hiyo nikamwambia young lady I need you.

Hapa hata chuo sijaenda kwa sababu yako, kwa hiyo leo lazima kieleweke. Simu hupokei, ukipokea unasema uko busy so nimeamua kukufuata kwenu labda utanielewa. Tuliongea mengi na tukakubaliana. Atakuja jioni. Kwa hiyo niondoke nikaendelee na shughuli zangu jioni atakuja. Basi mie nikawaaga nikaondoka. Siku sikutaka tena kwenda chuo japo kuna vipindi vya mchana ningeweza kuviattend. Nikanyoka moja kwa moja supermarket kwenda kufanya mahemezi ya mgeni. Jioni kwenye saa 10 akanipigia akasema amekaribia hivyo niwepo nyumbani. Nikamjibu aje tu nipo nyumbani. Muda si mrefu akawa amefika.

Alipofika nikanotice hajabeba chochote, hana mkoba wake anaokujaga nao, ana kiwallet kidogo dogo hivi. Nikahisi hapa kuna hatari inaenda kutokea. Roho yangu ikawa inaniambia huyu mtu hajaja kulala wala nini, amekuja kusoma mazingira tu kama kuna maisha au hakuna. Tumekaa kidogo akaniomba nikamnunulie vocha dukani, nikahisi huyu ataondoka, nikienda tu dukani nikirudi sitamkuta. Nikamwambia mie kwa kweli nimekumiss sana, naomba kwanza unipe kimoja halafu mambo mengine yafuate.

Halafu nikaamua kuchomekea harakaharaka kama nina hela ili kama ana mpango wa kunikimbia aahirishe, so nikaendelea kumwambia, najua wewe ni mwanamke unahitaji pia hela ya kujikimu hivyo sometimes natakiwa nikuelewe unaposhindwa kuja kunitembelea, japo nilijihisi nimeongea pumba ila nilijipa moyo kwa kufikiria huyu shida yake si ni hela hata kama nikiongea pumba hakuna shida ilimradi nimpa fungu lake. Basi akaniambia, nenda basi ukaoge then nikupe. Kidogo nikaanza kupata matumaini kuwa mzigo napewa, hata kama hatalala haina shida. Nikaingia kwenye kabati nikamtolea rand 400, akazipokea akawa kama kazikunja kunja hivi.

So, fasta nikaingia bafuni ili nioge fasta nile mzigo. Nilipokuwa bafuni nikawa nasikia kama movements hivi, nikahisi hapa nakimbiwa, nilichofanya nikaufungua kidogo mlango wa bafu ili kama atataka kukimbia nimdake maana mlango wa kutokea lazima upitie mbele ya bafu. Basi bana nikatupa boxer huko, nikafungua bomba mvua nikaanza kuoga, sekunde chache tu baada ya kuanza kuoga nikaona mtu ananyata kuelekea mlangoni, roho ikanilipuka paa!

Basi namipovu yangu nikakurupuka kuwahi mlangoni, nikawa nimechelewa, huyo keshafyatuka kama radi, nikatoka nje kuchungulia nikamuona anaishiria kutoka getini, fasta nikarudi ndani nikavaa boxer nikatoka ili nimfukuze, nikatoka mpaka barabarani kabisa huku natetemeka hata sijielewi, dah! baadae nikajitambua hapa sijavaa chochote, nipo na boxer tu acha nirudi ndani nikatafakari.

Itaendelea...
Daaah 😂😂😂noma sana
 
Sema neno tuu na moyo wangu utakuwa wako forever
emoji7.png
Sema neno tuu na moyo wangu utakuwa wako forever[emoji7]
Ur wish is my command😍
 
Jamani tusipost wala kuleta ujuaji kweye huu uzi ili tufaidi huu uzi, wengine tumeshanunua kinywaji kwa ajili ya kusindikizia uzi [emoji481][emoji481][emoji481][emoji482][emoji482][emoji482][emoji481][emoji481][emoji481][emoji482][emoji482]
 
Tupo tunafuatilia kwa ukaribu uzi special from konda msafi [emoji481][emoji481][emoji481][emoji481][emoji482][emoji482][emoji482][emoji482][emoji481]
 
IMG_2627.JPG
one love [emoji481][emoji481][emoji481][emoji482][emoji482][emoji482][emoji482][emoji482][emoji482]
 
Nataka niende haraka haraka ili hiki kisa nikimalize. Maana hiki kisa kilijiri kutokea 2008 mwezi wa pili au wa tatu hadi 2012 October nilipoamua kurudi nyumbani baada ya kuona nitakufa bure kisa Khumbu. So, nitakuwa naongelea matukio ya muhimu tu. Naomba niyapange hapa haya matukio ili kama kuna tukio nitalisahau mnikumbushe.
Matukio ni kama ifuatavyo.
1. Nilihama kule kwa masela baada ya chuo kuanza chuo, hivyo nilifulia ile mbaya
2. Baada ya kuanza chuo penzi letu liliyumba sana
3.Kuna siku nilimfukuza Khumbu ili nimkamate nimrudishe ndani nimpige miti nikiwa na boxer tu, nilikuwa kama akili zimeniruka.
4. Kuna siku Khumbu nimempanga nije nimle, hela niyokuwa naitegemea kumkirimu masela wakapita nayo, maana nilianza kukaa gheto na masela mavi.
5.Kuna siku Khumbu alitaka kunipeleka polisi baada ya kumpa kibano na matusi juu.
6. Kuna siku Khumbu nilimkuta na mshikaji wanatoka supermarket nilidondosha chozi.
7. Kuna siku nilifanya jaribio la kumla 071 akaridhia ila nikashindwa mwenyewe.
8. Kuna sehemu nilipata kazi province nyingine nikamtumia nauli Khumbu aje ili tufanye yetu, nauli akala na hakuja
9. Kuna siku nilipigiwa simu nikitishiwa kupigwa risasi.
10. Siku naondoka South Africa ilikuwa siku ya majonzi kwa Khumbu.
Hiyo namba saba hapo umenisikitisha kamanda...UNASHINDWAJE SASA....?DAAAH HAMNA MSAADA TUNAWEZA TOA?HATA WA KUKUSAIDIA....[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Back
Top Bottom