Nakubaliana na wewe rafikiangu. Hata hili limuungano lifutwe tu maana lina maagano ya kichwani mengi. Mfano mimi sioni faida yeyote ya hawa Waunguja. Halafu mleta hoja unazungumziaje dini? Dini sio Mungu na huwa haileti changes duniani. Nyakati za mfalme Nebukadneza Danieli na Wayahudi 3 zaidi (Shadrach, Meshack & Abnega) walileta changes kwa Serikali yote ya Nebukadneza iliyokuwa Waabudu miungu. Achana na dini tafuta Mungu anaebadilisha mioyo ya watu na MiserikaliNdio mana tunataka tuwe na nchi moja yenye serikali moja ili huu upuuzi unao uwaza mleta mada usiwepo.
Mada ya kulitazama kundi mmoja pekee huwezi kusema inajitosheleza, unless hilo kundi lingekuwa pekee linaloathirika na kile unachokizungumzia, lakini hapa hali ni tofauti yapo na makundi mengine pia...Mada inajitosheleza. Kama unadhani una mawazo bora zaidi na wewe fungua ya kwako.
Nimeandika mada kueleza mtizamo wangu, nawe anzisha mada uweke mtizamo wako!. SimpleMada ya kulitazama kundi mmoja pekee huwezi kusema inajitosheleza, unless hilo kundi lingekuwa pekee linaloathirika na kile unachokizungumzia, lakini kwako unaona inajitosheleza kwasababu ya mtazamo wako wa kibinafsi tu, kama ungekuwa na mtazamo mpana kwa maslahi ya taifa usingeona hivyo.
Naona umekimbilia mawazo ya mjinga mwenzio ili kujiliwaza.Wananipangia mada yangu iweje!
Mbona wao hawakufungua yao ili ibalance[emoji3][emoji3]
Kipindi hiko..Ingekuwa busara tukapata baraza la mawaziri la Tanganyika 1961 - 1963 na baadae ajira serikalini katika kipindi hiko ili tupate kulinganisha. Huenda tunazungumza kwa kuhisi tu lkn mambo sio kama tunavyofikiria.
Mjomba punguza makasiriko, jibu kile ninachokuandikia, kulazimisha kwako kutoka nje ya kile ninachoandika kunazidi kukuonesha ulivyo feki, na umejaa upendeleo kwa kundi lako.Nimeandika mada kueleza mtizamo wangu, nawe anzisha mada uweke mtizamo wako!. Simple
Ngoja nikuupuze. Huna hoja ya msingi zaidi ya kuangalia mambo kwa hisia za udini.Naona umekimbilia mawazo ya mjinga mwenzio ili kujiliwaza.
Hajielewi huyo, ana ugonjwa wa kulalamika miaka mingi sana.!!!Zungumzia na wakristo wa zanzbar pia kama mada yako ipo objective
Kwenye mada yako umezungumzia waislamu, ajabu hutaki niitazame kwa jicho la kidini, sasa sijui unataka niitazame kwa jicho gani jingine[emoji848][emoji848][emoji848]Ngoja nikuupuze. Huna hoja ya msingi zaidi ya kuangalia mambo kwa hisia za udini.
Wazanzibari, kwa mujibu wa Sensa ya 2022, ni Asilimia 1 (01%) ya Watanzania. Wanapangiwaje Asilimia 25 (25%) ya nafasi za Ajira katika Serikali ya Muungano?Katika nchi hii, Muhimili wa Power upo katika makundi makubwa mawili. (a) Wakiristo wa Tanganyika (b) Waislamu wa Zanzibar.
Haya Makundi ndiyo makundi makuu yenye mamlaka za kisiasa hapa nchin...
Ooh! Hapana hujagundua, Waislam sisi tunapata kwa kuangaika sana kuanzia kwenye kuuza maandazi n.k lakini wenzetu wengi huko serikalini wanajichotea Mahela mengi mno na kuyaficha.Lakini unasahau kwamba labda Uchumi wa Tanzania karibia wote kwa >85% umeshikikiwa na Waislamu, leo hii Mtanzania yoyote akitafuta kazi private sector hakwepi Uislamu
Nimeshangaa sana alipomjibu mkuu pale juu kuwa aanzishe uzi wake kuyazungumzia! Sasa sijui objectivityna open mind anayozungumzia ni ipi!Listen, kama ungekuwa na nia njema ungelizungumzia hili suala kwa ujumla wake, kwasababu kiuhalisia, sio waislamu wa Bara pekee wanaokosa teuzi Zanzibar.
Hata wakristo na makundi mengine nao wana tatizo hilo, tena kwangu ni kubwa zaidi na limekuwepo kwa muda mrefu zaidi ya hili tatizo lako uliloleta hapa.
Lakini kuamua kwako kutowazungumzia hawa kwa ujumla wao, badala yake ukajikita kulizungumzia kundi specific ulilo na interest nalo, kumeonesha nia yako na dhamira yako ya upendeleo, hii ni dalili kwamba...
Kwako kama hao waislamu wa Bara wangepata teuzi unazotaka Zanzibar, ungefunga mdomo wako usiyazungumzie makundi mengine, kwasababu unaamini shida yako ingekuwa imemalizwa...
Ndio maana umemjibu mdau aliyekuuliza kuhusu makundi mengine pale juu kwamba aanzishe uzi wake kuzungumzia tatizo lake, wakati kimsingi tatizo lake ndio tatizo lako pia, ila ubinafsi umekufunga akili hulioni hilo.
Ooh! Hapana hujagundua, Waislam sisi tunapata kwa kuangaika sana kuanzia kwenye kuuza maandazi n.k lakini wenzetu wengi huko serikalini wanajichotea Mahela mengi mno na kuyaficha.
Wanatupa data za uongo kuwa sisi ndio matajiri kumbe sikweli. Unaufahamu utajiri wa Edward Lowasa? Marehemu Mfugale? Kijazi, vipi yule mhaya wa Heineken Rugemalila? Prof. Tibaijuka yaani wana mamilion ya dola sema wenzetu wajanja hawasemi katu na hela wameficha huko umangani.
Kikubwa Waislam wengi wanaonekana matajiri kwasababu wali/wanajishughulisha na biashara yaani baada ya kuona mfumo zamani kama uliwakataa wakaanza kuwa wafanyabiashara matokeo yake ikawa heri kwao. Lakini sasa hivi tumejanjaruka na hivi vinafasi vya serikalini jambo ambalo linazolotesha ufanisi wa uchumi bibafsi labda update shimo upige kwelikweli!
Muhimu kuepuka masuala ya udini japokuwa kwenye teuzi huwa haiepukiki kwani inaleta hisia za kipuuzi hata kama aliyeteuliwa hakusaidii chochote.
Mimi muislam ninayejielewa lakini Waislam wenzangu wanaoteuliwa ukiwaendea maofisini wakusaidie wanakupiga danadana tu tena unaweza au unasaidiwa na mkristo tena fresh tu, hapo ndo huwa nashindwa kuelewa udini huwa una nini cha maana; so their appointments have nothing to do with my success!
Kuna Waislam wamenufaika na urafiki wao na Wakristo lakini pia kuna wakristo wamenufaika na urafiki wao na Waislam. Ukikagua viwanda na makampuni mengi ya kiislam utawakuta wako wakristo kibao tena katika nafasi nyeti za HR, IT n.k
Hata Shule kubwa tu kama FEZA, ALMUNTAZIL n.k utawakuta Wakristo kibao tena wakuu wa vitengo wanajinyakulia mishahara minono vivyo hivyo kwa wakristo.
Haya mambo huwa tunayaangalia sisi watu wa chini yaani kajitu kapo kishemundu hakana hata hekari ya mahindi lakini utasikia kanashangilia kuteuliwa boss fulani kisa tu ni dini yake. Upumbavu kama huu unaukuta Afrika hususani Tanzania.
Udini ni sumu, mfano Muislam kama Bashiru Ally aliibuliwa na Magufuli Mkristo kutoka kusiko (Ex nihilo) mpaka kuwa KMK, lakini ukimkuta sehemu utakuta anakwambia Waislam siyo kabisa!
Mtu kama Makonda (natolea mfano) aliibuliwa na Kikwete Muislam kutoka kusiko lakini unaweza kumkuta sehemu anawaponda Waislam na udini.
Nilikaa chini nikagundua kama dini ndo zinaleta mfarakano huu basi hazina maana! Umaana uje kwa kuutanguliza upendo wa ubinadamu wetu ambao Allah alituumba nao.
Wabillah wataufiq!
Mpinga Kristo....Vipi kuhusu Wakristo wa Zanzibar? Japo ni "minority" lakini kupitia hoja yako una maoni gani kuhusu kundi hili? Jielekeze katika haki zao, uhuru wao, na amani yao kupitia katiba ya JMT.
Vipi kuhusu makundi mengine, mathalani dini za kijadi, Kihindu n.k. Nafikiri ni vyema tukajitazama kama taifa, zaidi ya kujiangalia kupitia itikadi zetu za kidini.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hawa jamaa ukishawazoea hawakusumbui, ndivyo walivyo miaka mingi sana, ni wa kulalamika, wabinafsi...Nimeshangaa sana alipomjibu mkuu pale juu kuwa aanzishe uzi wake kuyazungumzia! Sasa sijui objectivityna open mind anayozungumzia ni ipi!
Uzi wake ungekuwa mzuri zaidi kama asingelalia upande na kujadili makundi yote kwa ujumla wake.
Toka kwenye hicho kilevi kinachotwa diniKatika nchi hii, Muhimili wa Power upo katika makundi makubwa mawili. (a) Wakiristo wa Tanganyika (b) Waislamu wa Zanzibar.
Haya Makundi ndiyo makundi makuu yenye mamlaka za kisiasa hapa nchini.
Hali hii inawaathiri sana Waislamu wa Tanganyika , nitaeleza
a) Kutokana na kwamba kule Zanzibar Waislamu ni Majority, basi nafasi yoyote ya Uteuzi ktk serikali ya Muungano, kama mzanzibari ndiye atateteuliwa, basi kuna probability kubwa kuwa mtu huyo akawa Muislamu. Na hivyo basi wakishateuliwa kushika hizo nyadhifa Inakuwa ni vigumu sana kwa nafasi nyingine zilizobaki kuteua waislamu wengine wa Tanganyika kujaza au kuchukua nafasi hizo zilizobaki, Ili isije kuonekana teuzi zimelalia watu wa dini moja. Kwa hivyo basi, nafasi zilizobaki watateuliwa Wakiristo wa Tanganyika.
Chunguza teuzi nyingi za Serikali, hata serikali hii ya awamu ya Sita. Utaona wazi kuwa kama aliyeteuliwa ni muislamu, basi kunakuwa na uwezekano mkubwa wa mteuliwa huyo ni Muislamu wa Zanzibar badala ya Muislamu wa Tanganyika.
b) Tatizo hilohilo pia linajitokeza katika Ajira na Utumishi. Wazanzibari kwa mujibu wa Makubaliano ya kimuungano, wameshatengewa asilimia 25 za ajira zote za Muungano. Halafu asilimia 75 zimebaki kwa Watanganyika. Sasa huku Tanganyika maana yake ni kwamba Wakiristo wa huku na Waislamu wa huku na watu wachache wa dini nyingine ndo wanagombea asilimia 75 zilizobaki. Hii pia inawaathiri Waislamu wa Tanganyika kwa maana, HR Manager au mamlaka za ajira zinapoletewa requirement ambayo tayari 25% ni watu wa dini moja, Ni vigumu kudhani watakuwa malaika kuongeza namba ya watu wanaofanana na hao ambao tayari wameshalamba shavu. Watataka watu wa Imani nyingine ili kuoffset imbalance ya kiimani. Hapa ndipo Waislamu wa Tanganyika inapokula kwao!
KWA HIYO
1. Huu muungano, kwa namna Ulivyo Waislamu wa Tanganyika ni kama Pawns, ila Wakiristo wa Tanganyika na Waislamu wa Zanzibar ndiyo King Makers
2. Ipo haja ya kukaa mezani seriously na kuangalia aina gani ya Muungano tunayoitaka ( Kama muungano wenyewe unamake sense anyway), Na tukikaa Mezani tuzungumze Masilahi serious ya kila kundi, siyo habari za tumeoleana kwa muda mrefu. Mambo ya kuoa na kuolewa ni personal hayana maslahi mapana kwa Taifa.
3) Waislamu wa Tanganyika sasa nao waamke, waanze kudai uwakilishi zaidi serikalini, katika teuzi mbalimbali za kuhudumu serikalini n.k.
Inabidi wadai kunufaika ipasavyo na matunda ya uhuru (walioupigania sana wakati ule wa kudai uhuru) ikiwemo ajira, na utumishi wa ndani ya serikali
Kwani LATRA ni taasisi ya muungano?Angalia uteuzi ufuatao wa mamlaka ya Uthibiti wa Usafiri ardhini( LATRA).
Walioteuliwa majority ni Waislamu wa Zanzibar na Wakiristo wa Tanganyika.
View attachment 2484241
View attachment 2484243
Sijui kama mambo ya Usafiri wa ardhini ni jambo la Muungano anyway, Lakini unaona mamlaka za Uteuzi zinajaza Waislamu wa Zanzibar tupu. Huku wale wa Tanganyika wakiwa kama Yatima.
Huu muungano ni pasua kichwa!