Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Usinicheke unanikumbusha machunguHahah...simu gani hiyo uliyopigwa hadi homa juu?
Usinicheke unanikumbusha machungu
Ilikua tecno phantom
Mida ya saa 5 asubuhi simu yangu inaita, kuangalia ni namba mpya nikapokea. Hallo, upande wa pili ukaitika, naongea na fulani? (akataja jina langu), nikajibu ndiyo.
Unaongea na huduma kwa wateja kutoka Benki tunafanya maboresho kwenye account yako ya benki, hii namba naoma ndiyo imesajiliwa na huduma za benki, nibeep kwa namba nyingine ambayo haijaungwa na benki nikuelekeze cha kufanya. Nikafanya hivyo.
Alipopiga mara ya pili, akaanza kunipa maelekezo nami nikaanza kufata kila anachoniambia bila hiana.
Cha ajabu nikashangaa inaingia meseji "Umefanikiwa kutuma TZS 998800 kwenda namba 07**********". Nilivyoona hiyo meseji nikashtuka moyo ukalia paaaa nikajisemea tayari nimepigwa. Nikakata simu, nikapigwa na bumbuwazi kwanza kwa dakika kadhaa baadae nikapiga namba hiyo ikawa haipatikani.
Ndiyo nikawa nimetapeliwa hivyo. Inauma sana.
Watu sikuhizi hawaogopi kabisa kulogwa
Pole sana mrembo ningelikuwepo karibu wakati uwo ningekuliwaza.Pole sana
Niliwahi kutapeliwa cm nikajifungia chumbani nililia adi nikapata homa
Siwezi kusahau
Watu kama nyie mnatakiwa kupigwa shaba, nchi ina watu wajinga sana wakati huo huo tunasubiria maendeleo. PatheticMida ya saa 5 asubuhi simu yangu inaita, kuangalia ni namba mpya nikapokea. Hallo, upande wa pili ukaitika, naongea na fulani? (akataja jina langu), nikajibu ndiyo.
Unaongea na huduma kwa wateja kutoka Benki tunafanya maboresho kwenye account yako ya benki, hii namba naoma ndiyo imesajiliwa na huduma za benki, nibeep kwa namba nyingine ambayo haijaungwa na benki nikuelekeze cha kufanya. Nikafanya hivyo.
Alipopiga mara ya pili, akaanza kunipa maelekezo nami nikaanza kufata kila anachoniambia bila hiana.
Cha ajabu nikashangaa inaingia meseji "Umefanikiwa kutuma TZS 998800 kwenda namba 07**********". Nilivyoona hiyo meseji nikashtuka moyo ukalia paaaa nikajisemea tayari nimepigwa. Nikakata simu, nikapigwa na bumbuwazi kwanza kwa dakika kadhaa baadae nikapiga namba hiyo ikawa haipatikani.
Ndiyo nikawa nimetapeliwa hivyo. Inauma sana.
Mkuu umesoma tarakimu vizuri sio laki ,ni million moja kasoro mia mbili tuShukuru ni laki boss wajinga hawaishi ndo maana matapeli nao hawaishi
Ameedit digits hazikua hivo, mimi ndo nilikua wa kwanza kusoma threadMkuu umesoma tarakimu vizuri sio laki ,ni million moja kasoro mia mbili tu
Sio kwa ubaya,ila jamaa katapeliwa kizembe sana.Tangu lini watu wa benki wakahitaji password yako tena kwa kupiga simu wewe jamaa umetapeliwa kizembe sana , inaonekana unauzoefu mdogo sana na mambo ya benki anyway ni kheri umejifunza .
Izo njia zote nilifata mkuu ila nilkuja kugundua kuwa nimekosea muamala baada ya muda kupita hela ikawa imeshatolewa na saiv iyo namba haipatkani tenaKwann usngepga huduma kwa mteja ukazuia muamala au kwenye apps ukafanya reverse mbona mnafanya maisha kua magumu nyie watu