Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Telegram z loading........Unataka kusema nini mkuu??🤔🤔
Haaa haaa haaa mwendo wa bundleEndelea kuandika fupi fupi hiv hiv yamebaki masaa mawili ifike tarehe 2april bundle za internet zipande
Mchango wa pesa ili apate GB zakutoshaUnataka kusema nini mkuu??[emoji848][emoji848]
Sijaomba mchango boss,usinielewe vibaya wala sitakuja kuomba mchango.Mchango wa pesa ili apate GB zakutosha
Nami sijamaanisha hivyo Kaka mkubwa ndiyo maana sija quote wewe wala usiwe na hofu.Sijaomba mchango boss,usinielewe vibaya wala sitakuja kuomba mchango.
Nilikuwa na wajulisha wakuu kuhusu vifurushi vya data ni kero .
[emoji1787][emoji1787] Kuna watu wamepinda jamaniEndelea....
Dada anadithia kwamba
Baada ya mganga kufa tukaamua kurudi dar es salaam kwa shemeji huku tukiwa hatuelew jins ya kufanya ndipo shemej akashaur turud kijijini
kwajil ya kutatua mgogoro ambao uliopo na kuchimbua vitu vilivyochimbwa kwenye kiwanja cha nyumbn na mm nikaamua kwenda kumloga yule alieniloga
siku moja nikaenda kwa bibi yangu nikamnasa vibao kwakuw yeye ndio muhusika wa yote
bhas baada ya kumnasa vibao ndugu zangu walinikimbiza sana yan wee acha tu kwakuw nilikuw nina mbio bhas hawakufanikiwa kunikamata kwa maan mm nilishawai kushiriki marathon kule japan 2002 nikaibuka kidedea
IMEKWISHA....
Pumbavu zako ww mtoa stor nmekumalizia stor yako naona unatukalisha kimandazi hapa na bandle limeshapanda shwaini ww
Unataka kusema nini mkuu??[emoji848][emoji848]
Fuatana na mimi sasaInaendelea
Baada ya kumnasa vibao bibi yangu ambaye alikuwa anasemekana ndiye aliyenirogea uchawi wa bundi licha ya kukimbia mbio sana ndugu walinikimbiza sana hadi hadi kijiji kimoja kinaitwa Gezaulole,kata ya Mtakuja wilayani Kilosa.Dada ananisimulia kuwa kutokana na maeneo hayo kuwa na mto mkubwa sana unaotenganisha wilaya ya kilosa na Kigamboni mimi bila kujua hatari yoyote ambayo ingenitokea kwa sababu nilikuwa kama bundi basi niliamua kujitosa kwenye mto huo wenye maji yanayotembea kwa kasi tena kuna mamba wengi.Ndugu zangu walibaki vinywa wazi wasijue la kufanya.Baada ya kuwa nimejitosa kwenye maji kaka yangu mkubwa wa dada yangu aliamua kurudi kijijini kutengeza ngalawa ili angalau jioni aweze kurudi kuniokoa.itaendelea
Ha ha ha ....🤣🤣🤣🙌Fuatana na mimi sasa
Baada ya kuwa nimejirusha kwenye maji dada yangu anaendelea kunisimulia kuwa nilionyesha umahiri wa hali ya juu wa kuyakata maji huku nikizama na kuibuka, katika hali ya mshangao kuna wakati nilizama kwenye maji na nikaibuka na mamba nikiwa nimemkaba koo kisawasawa hali akawa anatoa machozi.Hali ilizidi kuwa ni ya taharuki baada ya yule mamba kunizidi nguvu na kuanza kunishambulia ,watu wote walianza kushika vichwa vyao na kuanza kuomboleza.Ghafla yule shemeji yangu mtu wa Dar es salaam aliamua kujitosa kichwa kichwa kwenye maji kitendo ambacho kiliwashangaza wengi kwa sababu alikuwa hajui kuogelea hasa ukichukulia yeye ni mzaliwa wa Dar es salaam maeneo ya Kazula mimba mkoani Dododoma.itaendelea
Fuatana na mimi sasa
Baada ya kuwa nimejirusha kwenye maji dada yangu anaendelea kunisimulia kuwa nilionyesha umahiri wa hali ya juu wa kuyakata maji huku nikizama na kuibuka, katika hali ya mshangao kuna wakati nilizama kwenye maji na nikaibuka na mamba nikiwa nimemkaba koo kisawasawa hali akawa anatoa machozi.Hali ilizidi kuwa ni ya taharuki baada ya yule mamba kunizidi nguvu na kuanza kunishambulia ,watu wote walianza kushika vichwa vyao na kuanza kuomboleza.Ghafla yule shemeji yangu mtu wa Dar es salaam aliamua kujitosa kichwa kichwa kwenye maji kitendo ambacho kiliwashangaza wengi kwa sababu alikuwa hajui kuogelea hasa ukichukulia yeye ni mzaliwa wa Dar es salaam maeneo ya Kazula mimba mkoani Dododoma.itaendelea
Daah ila watu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji847]Inaendelea
Baada ya kumnasa vibao bibi yangu ambaye alikuwa anasemekana ndiye aliyenirogea uchawi wa bundi licha ya kukimbia mbio sana ndugu walinikimbiza sana hadi hadi kijiji kimoja kinaitwa Gezaulole,kata ya Mtakuja wilayani Kilosa.Dada ananisimulia kuwa kutokana na maeneo hayo kuwa na mto mkubwa sana unaotenganisha wilaya ya kilosa na Kigamboni mimi bila kujua hatari yoyote ambayo ingenitokea kwa sababu nilikuwa kama bundi basi niliamua kujitosa kwenye mto huo wenye maji yanayotembea kwa kasi tena kuna mamba wengi.Ndugu zangu walibaki vinywa wazi wasijue la kufanya.Baada ya kuwa nimejitosa kwenye maji kaka yangu mkubwa wa dada yangu aliamua kurudi kijijini kutengeza ngalawa ili angalau jioni aweze kurudi kuniokoa.itaendelea
Nlitaka kuchangia ila nlivoona neno jemedali nkaona wa ni mmoja ya watu wasomjua Mungu bali unaabudu mtu.OvaHabari wadau poleni sana na msiba wa jemedari Hayati Magufuli.
Leo nimeamua kuwaletea simulizi ya kweli inayoitwa "jinsi teseka miaka mingi na kunusurika kufa baada ya kurogezewa uchawi wa bundi".
Kwanza niwaombe samahani kwa mwandiko mbaya maana simulizi hii ninapoanza kuiandika inaweza kuonekana fupi ila inaweza ikawa ndefu hivyo basi mniwie radhi kama kutakuwa na kukatishwakatishwa.
Wahusika wa story ni watu wa kweli kabisa wala sio watu wa kufikirika na maeneo ni ya kweli sio ya kufikirika,ila ningeomba kutumia majina ya kufikirika maana sio vizuri kutumia majina yao halisi.
Lengo la kuleta story ni watu wajifunze wajue uchawi na uganga dunia upo na waganga wa kweli wapo,pia kuburudisha hilo ndio lengo.
Twende kwenye story yenyewe...
Ilikuwa mwaka 1975 katika kijiji cha Bunduki kata ya Bunduki wilayani Mvomero mkoa wa Morogoro ndipo simulizi ilipoanzia.
Nakumbuka kipindi hicho nilikuwa darasa la tano katika shule moja ya msingi kijijini hapo ambayo sitopenda kuitaja jina.Siku hiyo nilirudi nyumbani mishale ya saa 8 mchana nikiwa nimechoka sana na nilipofika nyumbani nikakuta kuna kasherehe ka kumtoa mwali, kama unavyojua tamaduni zetu za kiafrika hivyo watu walikuwa wamejaa sana huku wakipiga ngoma ijulikanayo kama Mbeta hii ni ngoma maarufu sana kwa wenyeji wa mkoa wa Morogoro hususa wa kabila la waruguru.
Nilifika nyumbani nikaingia ndani kubadilisha nguo za shule ambazo zilikuwa chafu zilizochakaaa na udongo wa kijijini kama wengi tunavyojua udogo wa Morogoro nakukimbia fasta kwenye ngoma.
Mwanamwali alikuwa ni dada yangu aliyenitangulia kwa sasa ana kama miaka 75 (watu wa zamani sana wengi wao hawajui miaka yao halisi ,hususa wale ambao hawakuenda shule .Huwa wanaweza kukutajia tu kipindi ,msimu au matukio ww ndio utang'amua umri wa makadilio wa mtu huyo kama haufahamu kuhusu matukio au vipindi hivyo vilitokea lini unaweza kushindwa hata kukadiria umri halisi).Hivyo basi umri wa dada kama miaka 75 katika simulizi hii ni kama makadirio tu wala visikupe shaka juu ya ukweli na uhalisia wa simulizi hii..
Basi baada ya kubadilisha nguo na kuingia moja kwa moja kwenye uwanjani ambapo mwanamwali ambaye ni dada yangu anachezwa hapo ndipo story, visa, mkasa, simanzi zilipoanzia.
Hapo kutakuwa na mambo ya kuvunja nazi, makafala ya wanyama kama mbuzi au ng'ombe na shughuri zingine pamoja na kufukia vitu au dawa kwenye makabuli au miti mikubwa kama ni matambiko.
Kwa wenyeji wa Pwani wanatambua utamaduni wetu kama kawaida ngoma inapowekwa uwanjani siku au wiki kabla haiawekwa uwanjani lazima watu waende kwa mganga kuzindika au wanaweza wakawaita wazee kufanya matambiko. Matambiko au mazindiko lazima yatanuwiwa kwamba yeyote atakayekuja kwa ubaya siku ya sherehe au shughuri ya kumtoa mwanamwali wetu basi haondoke kwa ubaya.
Nasi tulifuata taratibu zote za zindiko na matambiko kama utamaduni wetu lakini sasa siku hiyo mambo yalikuwa tofauti yaani chuma kilikutana na chuma.
Tukumbuke tupo mwaka 1975 kipindi hicho dini na imani hazikuwa zimeenea sana kivile hivyo hatukuwa na budi katika kuamini mizimu ,matambiko,mazindiko na vinginevyo.
Inandelea...View attachment 1734464