Jinsi nilivyougua miaka mingi na kunusurika kifo baada ya kurogewa uchawi wa bundi

Jinsi nilivyougua miaka mingi na kunusurika kifo baada ya kurogewa uchawi wa bundi

Nine ingia nika smille leo ume andika epsode ndefu kusona nusu story nzima una tumia kumuelezea mganga alaaah ..hujui ata kufupisha story. kutoa vitu visivyo kua na maana..
Acha kusoma, au umeshikiwa kisu shingoni?
 
Endelea..
Baada ya kukutana na yule Mganga mwanamke na kumuelezea matatizo ya kesi inayotukabiri alitupa karatasi nyeupe aliyoitoa katikati ya daftari kongwe lililochakaa kisha akatwambia tuandike majina ya wahusika wa kwenye kesi yetu kuanzia wa kwanza mpaka wa mwisho.

Kisha yule mama akachukua kibuyu chake akachovya kijiti kinene kwenye kibuyu kiasi ambacho kijiti chote kikalowa kwa maji mithiri ya tope jeusi,kisha akachukua karatasi yeye majina ya washitaki wetu na kuyafuta majina yote kwa kile kijiti kilicholowa dawa kutoka kwenye kibuyu huku akiongea maneno yake ya kilugha akinena na kile kibuyu na kukiamuru kufanya mambo.

Kisha akatwambia nendeni mkatundike karatasi hili kwenye kamba na mning'inize chumbani mnapolala,na sisi tulifanya kama tulivyoelekezwa.

Wiki iliyofuata kesi ikasomwa Mahakamani yule aliyetushitaki hakutokea ,kama kawaida ya mahakama kesi ikapigwa karenda.

Kiufupi kesi ilikaa mahakamani baadaye mahakama ili tutaka kumlipa bwana Issa Shaibu kidogo kidogo mpaka deni litakapoisha na wala sio kuchukua nyumba kama ilivyoamuliwa na serikali ya mtaa.

Sababu pesa ilikuwapo bwana Issa Shaibu alilipwa pesa yake mara moja na sisi tukaendelea kusalia kwenye nyumba yetu na tukaendelea kuanza maisha mengine ya kuganga kwa waganga.

Nadhani sasa ndio ulikuwa mwanzo wa tumaini jipya la kupona ,baada ya kukutana na mganga toka mkoani Mbeya wilaya ya Rungwe kijiji kimoja kinaitwa Ikuti .

Huyu mzee alikuwa mtu kutoka ukoo wa machifu wa kabila la Kinyakyusa alikuwa kama ana unabii ,yaani tiba yake alikuwa anaoteswa usiku kitu kinachotokea asubuhi au kesho.

Nakumbuka siku wakati tunasafiri kutoka Dar Es Salaam tunaenda yeye alikuwa na safari ya kwenda sehemu moja inaitwa Mbalali ambayo nayo ipo huko huko mkoa wa Mbeya.

Endelea...
 
Fuatana na mimi sasa
Baada ya kuwa nimejirusha kwenye maji dada yangu anaendelea kunisimulia kuwa nilionyesha umahiri wa hali ya juu wa kuyakata maji huku nikizama na kuibuka, katika hali ya mshangao kuna wakati nilizama kwenye maji na nikaibuka na mamba nikiwa nimemkaba koo kisawasawa hali akawa anatoa machozi.Hali ilizidi kuwa ni ya taharuki baada ya yule mamba kunizidi nguvu na kuanza kunishambulia ,watu wote walianza kushika vichwa vyao na kuanza kuomboleza.Ghafla yule shemeji yangu mtu wa Dar es salaam aliamua kujitosa kichwa kichwa kwenye maji kitendo ambacho kiliwashangaza wengi kwa sababu alikuwa hajui kuogelea hasa ukichukulia yeye ni mzaliwa wa Dar es salaam maeneo ya Kazula mimba mkoani Dododoma.itaendelea
Kazula mimba in Musa chesa voice....🤣🤣🤣...we ni mwehu
 
Mkuu umesema mtu akianza kwenda kwa waganga hawezi kuacha tena. Je hadi Leo wewe unaendelea na hizo imani?!
Unakuwa mlevi,je mtu mlevi ni rahisi kuacha ulevi mara moja?

Hapa pana maana kwamba ukishaingia kwenye mambo ya shetani ni ngumu shetani kukuruhusu utoke kirahisi .
 
Back
Top Bottom