Jinsi Ole Sabaya atavyochomoka kwenye mikono dhalimu iliyombambikia kesi

Kama kesi ndogo nenda kamtoe, aacha kutia kinyaa watu, kesi za kubaka bado zinakuja
 
Sasa kwenye hili hao CHADEMA wameingiaje? Kahojiwa na TAKUKURU ya CHADEMA? Kakamatwa na Polisi wa CHADEMA? Kafikishwa Mahakama ya CHADEMA? Au hata Kisongo ni gereza la CHADEMA?
Mkuu inalekea mishipa ya aibu na kumbukumbu ilishachomoka kitambo
 
Tunatengeneza precedent mbaya,

Ikija awamu ya saba itadeal na watu wa awamu ya sita,

Taifa litakua la visasi tu,

Tunapiga hatua moja mbele tunarudi tano nyuma.

Maskini Tanzania sijui lini utazifikia ndoto zako.
Heri ufe tu uondokane na haya mateso! Na huko utakakoenda kuna mkuu wa malaika uliye kuwa Una mwabudu atakupa raha ya milele!
 
Na bado Wewe! Shukuru sana huruma ya Melo, tungekujua tu, ungemfuata mumeo kwenye fungate yake Kisongo, kuleenyai!
 
Acha propaganda Leta balance report tuelewe mkuu. Kama hana kosa atarudi home kama Kuna kosa sheria itachukua mkondo wake nakuhakikishia yupo Salama na kaamka na amepiga mswaki na kupata breakfast kama watu wengine
Daaah ila wamempaka mafuta aise

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Aliekuambia nafanya kazi za vyombo vya usalama nani? Kama wamepewa hiyo dhamana mbona rais kamuambia Igp wafute kesi walizobambikia watu makosa? Tumia akili bwege mkubwa.
igp afute kesi ambayo bado uchunguzi haujakamilika?
tamko la rais limetoka kabla kesi ya sabaya haijapelekwa mahakamani.

brush your memory man. bwege square ww
 
Hakuna kesi hapo, huwezi kuniambia eti DC katumia silaha kupora 35,000/=. Hivi ktk akili ndogo tu hata ya chekechea unaweza kukibaliana na uzandiki huo wa Chadema? Kinachofanyika kwa Sabaya ni kumdhalilisha tu hakuna lolote hapo. Aliyeporwa milioni 90, aliporwa ktk mazingira yapi na Sabaya? Sheria ya umiliki wa pesa inasemaje? Chadema acheni uzandiki wa hivyo na kwa vile mmeshamfix huyo Rais wenu wa Viti Maalum basi msijione nchi ni ya kwenu
 
Hawa mdogo walijiona wapo peponi...wao kama 4, bado 3 wanaliwa timingi kuingia kwenye 18 za Jamhuri.

Ukipewa madaraka ya kuongoza umma jiheshimu...si mambo ya kihuni huni
 
Kweli maisha yanaenda kwa kasi ya 5g

Yaani eti mataga leo wamekua ni watu wa kuilaumu takukuru na mahakama kua hazitendi haki?
Sasa wanaelewa kwa nini Tundu Lissu alishinikiza kwamba Ole Sabaya "atendewe haki" kwa kupelekwa mahakamani, asiendelee kushikiliwa kwenye PCCB castody. Lissu ni mwanasheria nguli, alijua kabla hajafikishwa mahakamani, tuhuma zinaweza kuyeyuka, lakini tuhuma zikishafika mahakamani sheria tu ndiyo itaamua. Watu walianza kusema Lissu anataka kumsaidia Sabaya. Baada ya Sabaya kufika mahakamani, watu wale wale wameanza kupiga kelele.
 
Ukipanda matofaa utavuna matofaa,
Mbegu za chuki huzaa matunda ya chuki hivyo kwa tuhuma zinazomkabili ushahidi utabainisha sehemu inayomfaa huyo bwaana
 
Kilicho nishangaza eti makosa yote kayafanya January 2021..
Hayo ndiyo yaliyofanyiwa uchunguzi na kufungua case, yapo mengine yanakusanywa. Nenda mahakamani tarehe 18/06 utayasikia na mengine ambayo yanafanyiwa kazi sasahivi.
 
Mwaka jana mwishoni mfanyabiashara na mbunifu wa mavazi Jeffery Mmbungu maarufu kama @Speshoz alifungua kiwanda cha vinywaji vikali, wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro. Kiwanda hicho kinaitwa Daren Fabrics Industries Ltd kinazalisha kinywaji chenye jina Faru John.

Mwezi February mwaka huu, aliyekua Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya alimpigia Jeff na kumwambia kuwa CCM itafanya maadhimisho ya miaka 44 tangu kuanzishwa, na yeye ni miongoni mwa wanakamati wanaoandaa maadhimisho hayo.

Akataka kiwanda hicho kichangie TZS 10M kufanikisha maadhimisho hayo. Jeff akamwambia hana uwezo wa kuchangia 10M, lakini akaahidi kuchangia 1M. Sabaya akamnanga kwamba serikali ya CCM ndiyo iliyomuwekea mazingira mazuri ya kibiashara hadi akaweza kufungua kiwanda, kwahiyo kuchangia 1M ni dharau kwa chama, anatakiwa achangie kiasi kisichopungua 10M.

Jeff akamwambia hana pesa hiyo. Sabaya akamwambia nimepitia transaction zako TRA najua unafanya mauzo ya mamilioni ya shilingi. Jeff akamwambia bado kiwanda ni kichanga na hakijaanza kujiendesha kwa faida kiasi cha kumpa Sabaya 10M.

Mwezi May mwaka huu Sabaya akavamia kiwanda hicho akiwa na mabaunsa wake. Wakawa-harass sana wafanyakazi waliokuwepo. Sabaya akiongozana na waandishi wa vyombo 11 vya habari akatangaza kukifunga kiwanda hicho kwa madai kinajiendesha bila vibali.

Vyombo vya habari vikaripoti kuwa kiwanda hicho kimefungwa kwa kufanya uzalishaji wa vinywaji vikali bila kuwa na kibali. Jeff akashangaa kwa sababu alikua na vibali vyote.

Ana leseni ya BRELA nambari 142255766 iliyotolewa July mwaka 2020. Ana leseni ya TRA nambari 142255766 iliyolewa July 2020. Ana leseni ya biashara nambari 03356294 iliyotolewa na Halmashauri ya wilaya ya Hai tarehe 25 September 2020.

Ana Leseni ya mkemia mkuu wa serikali nambari B002C000255 iliyotolewa October mwaka 2020, pia ana Leseni ya TBS nambari 3082 iliyotolewa December 2020. Pia kabla ya kuanza uzalishaji alipewa barua ya ruhusa kutoka TBS yenye Kumbukumbu nambari QA/QCCA/3215/17.

Sasa akashangaa imekuaje kiwanda kifungwe kwa kukosa vibali wakati vibali vyote anavyo? Akampigia Sabaya kumuuliza. Akamwambia aende ofisini.

Alipofika ofisini, wakaongea na akamuonesha nakala za vibali. Sabaya akatoka ofisini na kumuacha ndani. Aliporudi akamnyang'anya simu zote, na kumuamuru akae chini. Akaita mabaunsa wake, wakamvua viatu na mkanda na kumpeleka rumande.

Taarifa za kukamatwa kwake zikafika kwa viongozi mbalimbali wa serikali. Wizara ya ya viwanda na biashara ikatoa tamko kuwa kiwanda hicho kinajiendesha kwa mujibu wa sheria. Wizara ya uwekezaje, ofisi ya Mkemia mkuu wa serikali, Shirika la viwango (TBS), pamoja na ofisi ya BRELA wakaingilia kati na kueleza kuwa kiwanda hicho kinajiendesha kihalali.

Kesho yake Meneja wa TRA mkoa wa Kilimanjaro akafanya press na kutoa ufafanuzi kuwa kiwanda hicho kinaendeshwa kwa mujibu wa sheria. Taarifa hiyo ikaeleza kuwa mwezi April kiwanda hicho kilipewa stika za 200M na kiliweza kuhuisha stika za 93M. Pia kwa siku chache za mwezi May (kabla hakijafungwa) kilikua kimehuisha stika za 13M.

Taarifa ya TRA ikaeleza kuwa kiwanda hicho hakijawahi kuwa na mgogoro wowote na serikali wala hakijawahi kujiendesha bila kuwa na vibali. Ikatangaza kukifungulia kiwanda hicho na kukiruhusu kiendelee na uzalishaji.

Media zote zilizoripoti kuwa kiwanda hicho kimefungwa zilialikwa kwenye Press ya TRA ili ziujulishe umma kwamba taarifa ya Sabaya haikua sahihi, na kwamba kiwanda hicho kimeruhusiwa kuendelea na uzalishaji.

Lakini Sabaya akazuia media hizo zisiripoti taarifa hiyo ya TRA. Ni ITV pekee walioamua kusimama katika misingi ya taaluma na kutoa ufafanuzi kwa umma. Media nyingine ziliamua kusimama na Sabaya. What a shame?

Tayari Jeff ameshaenda TAKUKURU kuwasilisha ushahidi wake. Pia atawasilisha malalamiko Baraza la habari nchini (MCT) ili media zilizomchafua na zikakataa kumsafisha zichukuliwe hatua, kwa sababu habari ya kiwanda hicho kufungwa imeathiri mauzo kwa kiasi kikubwa.!
 
Aachiwe huru ili wananchi tumshughulikie kisawasawa!
 
Mamlaka ya Uteuzi ikuteue uwe WAKILI WA SERIKALI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…