Jinsi picha la kurudia chaguzi Tanzania linavyochezwa

Jinsi picha la kurudia chaguzi Tanzania linavyochezwa

Ninachokiona hapa kwa mara ya kwanza Magufuli kama Mwenyekiti anabomoa msingi mzuri uliowekwa na wenyeviti waliopita. Same story waliyoitumia CCM kipindi cha kampeni kuelezea mchakato wa upatikanaji wa Lowasa kugombea urais kwa tiketi ya ukawa kuwa haukuzingatia katiba ndio ikasababisha wapiganaji wa ukweli kwenye siasa za upinzani kujiondoa (Slaa na Lipumba) ndivyo itakavyokuwa hatima ya CCM anayojenga Magufuli na wasaidizi wake. Wanapokewa watu toka upinzani ambao hawana utashi wa kweli zaidi ya maslahi ya matumbo yao na kuwaacha wanachama wao wa siku nyingi. Mchakato wa kuteua wagombea haufuati katiba yao ambayo inaeleza wanachama kupiga kura kumpata mgombea.

Cha kujiuliza hawa wapinzani wanaobomoa upinzani, je watakauwa na nafsi ya kuteuliwa tena mwaka 2020 kwenye chaguzi mkuu au watarudishwa kwa wanachama asili matawini wasurubiwe na watu wenye vinyongo? Inshort naona baadhi yao kupotea kwenye ulingo wa siasa mapema mno. Wengi watatumika kama Bazoka/Big G kisha watatupwa.

Unaachambua Siasa kwa hisia...

Huwezi kulinganisha Chama cha Siasa kinachoanzisha Chuo kwa ajili ya kuandaa Watu kifalsafa na vyama vya Upinzani...
Vyama vya Upinzani vina utaratibu mbovu wa kuaandaa Vijana wake, Haiwezekani hata siku moja mtu kama Sosopi aje Amushinde kimaarifa na Hekima Yule RC wa Iringa...
Fikiri mara mbili
 
Lakini na wapinzani wajiulize kwa sasa wana sera gani za kuvutia masikio ya wananchi?
Zamani walikuja na sera nzuri sana sijui kwa sasa wamekuaje?
Sera za upinzani utazisikia wapi wamezuiliwa kufanya mikutano ya hadhara
 
Yaani watu wengine bana ili kuwe na demokrasia eti lazima washinde upinzani!! Upinzani wenyewe wa kutukana matusi tu na vurugu. Wacha ujifie. Ving'ang'anizi wa madaraka kwenye upinzani kwanza watoke halafu waje viongozi serious ndo tutaanza kuongea lugha moya
 
Chadema hata kikifa sawa tu, ila mimi nikiwa kama mwana ccm mtiifu ninaomba ktk chaguzi kuwe na fair ground bila hivyo basi tutangaze Tanzania kwasasa hatuna free and fair election nawaonea huruma sana watani zangu Chadema
 
Kwa hiyo mnataka mtangazwe washindi bila kushinda?
Posho nakupa miye, ulinzi miye, usafiri miye, huduma nyingine zote muhimu nakupa miye....leo hii usimame utangaze mpizani kashinda, utakuwa na "akili" kweli wewe.!
Hivi kauli kama hiyo inapotolewa na mkuu wa kaya kwa wale wanaosimamia uchaguzi na kutangaza matokeo, bado tunategemea kuna uchaguzi guru tena hapo? Vituko vyote tunavyoona na kuvisikia kwenye hizi chaguzi za marudio bila shaka ni utekelezwaji wa hiyo kauli kuanzia ngazi za chini hadi juu. "NASIKITIKA KUTANGAZA MAUAJI YA DEMOKRASIA YANAYOENDELEA"
 
Posho nakupa miye, ulinzi miye, usafiri miye, huduma nyingine zote muhimu nakupa miye....leo hii usimame utangaze mpizani kashinda, utakuwa na "akili" kweli wewe.!
Hivi kauli kama hiyo inapotolewa na mkuu wa kaya kwa wale wanaosimamia uchaguzi na kutangaza matokeo, bado tunategemea kuna uchaguzi guru tena hapo? Vituko vyote tunavyoona na kuvisikia kwenye hizi chaguzi za marudio bila shaka ni utekelezwaji wa hiyo kauli kuanzia ngazi za chini hadi juu. "NASIKITIKA KUTANGAZA MAUAJI YA DEMOKRASIA YANAYOENDELEA"
Kwa kauli hii tu basi hakuna haja ya kufanya uchaguzi tukapoteza hela
 
Wengine wanatekwa kisha wanalawitiwa huku wakirekodiwa na kutishwa huwa kama hawahami Chadema picha zao ziwekwa.hewani. Tumeingia katika siasa za kishenzi kabisa kuwahi kutokea duniani.
 
Lakini na wapinzani wajiulize kwa sasa wana sera gani za kuvutia masikio ya wananchi?
Zamani walikuja na sera nzuri sana sijui kwa sasa wamekuaje?
Hizo Sera wazitolee wapi ilhali wamepigwa marufuku kufanya mikutano?
 
Bado tupo kwenye ujima, wabongo wengi bora liende. Tukifika kiwango cha mwisho kuburuzwa na kyama twawala tutabadilika tu. Huo muda bado, tumshukuru jiwe kwa kubana life kitaa wadwanzi wataona umuhimu wa Uhuru, demokrase na thamani ya kura yao.

Jiwe bana baba, kodi , uwajibikaji na maendeleo huku Uhuru na maendeleo ni kuwa kijani.
 
Aliye kwambia kuwa Magufuli ana uchungu na hela zetu ni nani?
 
Kwa hiyo mnataka mtangazwe washindi bila kushinda?
KWANI CCM IMEWAHI KUSHINDA KWENYE UCHAGUZI GANI? HATA 1992 KWENYE KURA YA MAONI WALICHUKUA MAÖNI YA WACHACHE.HIVYO CCM NI DESTURI YETU KUMCHUKUA MWENYE KURA CHACHE NA KUMTANGAZA MSHINDI.
 
Kwa mbano uliopo hizo sera za kuvutia masikio ya wananchi utazisikia wapi? Hakuna mikutano ya hadhara, vyombo vya habari vinadhibitiwa, mitandao inatungiwa sheria kali, kubambikiwa kesi kwa viongozi n.k. n.k. Kifupi tumerudi nyuma kwa hiyo maendeleo tutayasikia kwa wengine.
UKIONA MWALIMU ANAOGOPA KUCHALENJIWA NA WANF WAKE JUA AKILI YAKE INA UPUPU.
 
Jiwe anataka kuombewa daima,sijui sababu. Tumuombee ili nia yake ovu iweze kufanikiwa?
 
Back
Top Bottom