Jinsi picha la kurudia chaguzi Tanzania linavyochezwa

Jinsi picha la kurudia chaguzi Tanzania linavyochezwa

Wengine wanatekwa kisha wanalawitiwa huku wakirekodiwa na kutishwa huwa kama hawahami Chadema picha zao ziwekwa.hewani. Tumeingia katika siasa za kishenzi kabisa kuwahi kutokea duniani.
Jiwe anataka kuombewa jamani
 
Watanzania tutazame picha linalolechezwa la kuumalizia mbali upinzani. Ukiangalia wafuatao wamejiuzulu uanachama wao bila sababu mujarabu na chaguzi za wabunge na madiwani zimerudiwa. Akina Mwita Waitara wa jimbo la Ukonga, mbunge wa Monduli, mbunge wa Kinondoni, mbunge wa Liwale.

Hii inatupa picha kuwa hili picha limetengenezwa kwani hata mkuu wan chi mwenyewe baba Jiwe hakemei chochote anaruhusu mamilioni ya pesa za walipa kodi yatumike kurudia chaguzi ili kukipa nguvu chama tawala.

Alitakiwa akemee ili mambo yaishe, lakini kwa kuwa ni upinzani anachekelea ingekuwa CCM wanahama huu mchezo ungeisha mara moja!! Tujiulize sote lengo hasa ni nini? Kwanini inakuwa hivi na haikuwa hivi kipindi cha nyuma?

Hii inafanyika ili kukiua chama kikuu cha upinzani nchini cha CHADEMA katika kuelekea uchaguzi mkuu wa 2020. Wale wanachama na viongozi waaminifu ndiyo wamebakia mifano akina Mwenyekiti Freeman Mbowe, Mchungaji Peter Msigwa, mbunge Joseph Mbilinyi, Mbunge Peter Lijuakali, mbunge Joseph Haule, mbunge Halima Mdee, mbunge Esther Bulaya, Mbunge Esther Matiko, mbunge John Heche, mbunge Tundu Antipas Lissu, mbunge John Mnyika na mbunge Saed Kubenea na wengine ambao sijawataja hapa.

Inafanyikaje? Njia kuu zinazotumika katika nyingi ni Mapandikizi na Kompromati. Kwa mapandikizi ni wanachama hawa kuingizwa katika vyama hivi vya upinzani mapema na kujenga kuaminika hadi kuweza kuingia kwenye vikao muhimu na kukusanya siri muhimu za vyama vya upinzani hasa CHADEMA. Halafu ndiyo sasa na muda unavyoenda wanarudi na kupewa madonge nono ya fedha.

Kompromati ni neno la kirusi (Russian) katika intelijensia ambapo mtu huhujumiwa (black mailing) na kupewa masharti kuwa usipofanya hivi tutaweka mambo yako wazi na tutakuchafua au tutafanya vile. Hapo hauna namna lazima usalimu amri na kuyasikiliza matakwa ya wanaokuhujumu.

Picha hili litavimaliza vyama vikuu vya upinzani kwani CUF tayari chali na CHADEMA ndiyo hivyo. Picha linaweza kwenda hadi kuundwa kwa vyama vingine vya ajabu ili kuonekana kuna upinzani. Kumbuka kikija chama chenye nguvu au upinzani wa kweli huwa vinahujumiwa si mnakumbuka Chama cha Jamii (CCJ) cha marehemu Samwel Sitta na Dr. Harrison Mwakyembe kilivyomalizwa kwenye hatua za usajili.

Hawa walijaribu kwa kumtoa kafari mbunge Fred Mpendazoe na viongozi akina Kiyabo. Ndiyo maana hao akina Kiyabo hatuwasikii tena kwenye siasa wapo kimyaa.

Vyama vinavyoongeza upinzani zaidi kama ACT Wazalendo hivyo vimepeta kwenye usajili ila vimekuja kumalizwa kwa kuwachukua viongozi wake na kupewa nyadhifa serikalini kama tulivyoona kwa Profesa Kitila Mkumbo na Mama Anna Mughwira.

Na katika chaguzi zote ndogo za kurudia ambazo wapinzani wanajirudisha CCM ni mwiko upinzani kushinda na Mkurugenzi na viongozi wengine ole wao washinde wapinzani. Kwa kweli demokrasia inaisha na wananchi wengi ambao hawajui chochote hasa vijijini wakiwa na uelewa mdogo hawana nafasi ya kuchagua viongozi kwa ubora wao hiyo 2020 bali watachagua chama.

Na tunaamini ili nchi iendelee tofauti ya mawazo au changamoto ndiyo inaendeleza nchi zetu hizi ambazo ustaarabu wetu bado. Serikali ikiwa haina upinzani wa kweli na wa nguvu inalala tu na kuzisababisha nchi zizidi kutopea kwenye umasikini uliokithiri. Hapo hakuna mawazo mbadala, hakuna kujiuliza, hakuna uoga wowote.

Sitegemei mtu aje abishe kwa kuleta mifano ya China sijui Korea na kwingine bila kujua wale walishapitia kwenye ustaarabu miaka mingi na hatua waliyofikia ni ya juu sana. Tena wameweka mifumo mizuri sana ambapo mafisadi wanashughulikiwa na utendaji bora wa kazi ndiyo utamaduni wa nchi zao.

Naamini demokrasia ikisimama ndipo tutaweza kusogea bila hivyo tutaendelea kujuta na vizazi vyetu vitabakia pale pale huku wenzetu wakisogea Mbele kwenye nyanja za kisiasa , kiuchumi, kiutamaduni na kisayansi.

Sasa wewe na mimi tutafanyaje? Viongozi wa vyama vyote CCM na upinzani wafanyaje? Hapo ndipo tujiongeze na kufikiria tutasogea vipi?

Sisimamii kwenye chama chochote cha kisiasa nasimama kwa Tanzania nzuri, bora, yenye mafanikio na yenye future inayopendeza kwani hiyo kesho hatutakuwepo ila wajukuu, vitukuu, vilembwe ,vilembwekeza na vining’ina wetu ndiyo wataikuta Tanzania hii ikiwa mbaya au nzuri.

TUTAFAKARI
Ktk hii "orodha ya wanaojiuzuru bila sababu" sijaona jina la yule bwana wa singida aliyetangaza uamuzi wake huko "mbanta" badala ya "umofia" au ni kwa sababu tu yy alitoka yanga kwenda simba(green/yellow to red/white)

Hapa shida naona ni mtu kutoka simba kwenda yanga but siyo yanga kwenda simba.
 
Yaan hii nchi inakera sana huku tunalia serkal haina hera za kulipa wqlimu, na watumishi mbali mbal ila tunatumia mamilion ya tsh kwa kurudia uchaguz wakat mtu kajiuzuru yy mwenyewe bila sababu ya msingi kazi kutubana sisi wajasiliamar wadogo kukutoza kodi kubwa ili wafidie hilo pengo la hera walizotumia ktk uchaguzi
 
Hatutajua maana halisi ya vyama vingi maana walioshika hatamu Pamoja na mashabiki wao wanaamini wapinzani ni maadui (kumbe upinzani ni ushindani) muhimu kila MTZ wa kawaida apambanie maisha yake na familia yake hayo ya wanasiasa si ya kuendekeza utapata presha bure huku wenzako wakineemeka (Siasa za TZ majitaka)
 
Lakini sasa watakaa kimya? Basi sera waziseme kila mbunge katika jimbo lake.
Huko majimboni wanafundishwa kuongea na mkuuuu maana kama ulifuatilia ziara ya kanda ya ziwa ,wabunge wa upinzani walihojiwa pumba zakuwafitinisha na wananchi ila ccm walifagiliwa for nothing
 
Pesa za kuwapandisha watumishi madaraja anasema hamna ila 1.2 billion za kurudia uchaguzi kila mara iko standby.Najuta sana kuzaliwa Tanzania yenye aina hii ya administration/leadership style.

Yaani akitoa tamko kali mnasema anavunja katiba hafati sheria..akifata sheria na katiba mnasema hatoi tamko wala hakemei.

Suala la mtu kuhama chama na uchaguzi kurudiwa ni haki ya kila mtu kisheria na kikatiba. SASA kwanini mnataka rais avunje katiba kwa kukemea???.
Mkiambiwa mnavuta bangi pale ufipa makaburini mnatukana.
 
Ninachokiona hapa kwa mara ya kwanza Magufuli kama Mwenyekiti anabomoa msingi mzuri uliowekwa na wenyeviti waliopita. Same story waliyoitumia CCM kipindi cha kampeni kuelezea mchakato wa upatikanaji wa Lowasa kugombea urais kwa tiketi ya ukawa kuwa haukuzingatia katiba ndio ikasababisha wapiganaji wa ukweli kwenye siasa za upinzani kujiondoa (Slaa na Lipumba) ndivyo itakavyokuwa hatima ya CCM anayojenga Magufuli na wasaidizi wake. Wanapokewa watu toka upinzani ambao hawana utashi wa kweli zaidi ya maslahi ya matumbo yao na kuwaacha wanachama wao wa siku nyingi. Mchakato wa kuteua wagombea haufuati katiba yao ambayo inaeleza wanachama kupiga kura kumpata mgombea.

Cha kujiuliza hawa wapinzani wanaobomoa upinzani, je watakauwa na nafsi ya kuteuliwa tena mwaka 2020 kwenye chaguzi mkuu au watarudishwa kwa wanachama asili matawini wasurubiwe na watu wenye vinyongo? Inshort naona baadhi yao kupotea kwenye ulingo wa siasa mapema mno. Wengi watatumika kama Bazoka/Big G kisha watatupwa.

Wengi wao watafuata njia aliyopitia Alexandre Hleb aliyekuwa mchezaji mahiri wa Arsenal akajiona yuko top akapush transfer to Barcelona. Alipotea ndami ya miaka 2 tu.
 
Ruzuku kwa chadema inapungua taratibuuuu. Kadri wanavyozidi kupungukiwa na wabunge pia hela zao za Ruzuku kama chama nayo inapungua! Mpaka tunafika 2020 chadema wanaweza wasiwe hata na hela za kuendesha kampeni. Poleni sana ndugu zangu wa chadema. Upigaji wa hela za ruzuku unafika ukingoni! Na mwenyekiti anavyoaandamwa ktk biashara zake basi ni tabu tupuuu. Na juzi nasikia wamemkatia umeme ktk hotel yake kule moshi! Eti alikuwa anatumia umeme wa kujiunganishia aka wizi! Slow death hii.
 
Ruzuku kwa chadema inapungua taratibuuuu. Kadri wanavyozidi kupungukiwa na wabunge pia hela zao za Ruzuku kama chama nayo inapungua! Mpaka tunafika 2020 chadema wanaweza wasiwe hata na hela za kuendesha kampeni. Poleni sana ndugu zangu wa chadema. Upigaji wa hela za ruzuku unafika ukingoni! Na mwenyekiti anavyoaandamwa ktk biashara zake basi ni tabu tupuuu. Na juzi nasikia wamemkatia umeme ktk hotel yake kule moshi! Eti alikuwa anatumia umeme wa kujiunganishia aka wizi! Slow death hii.
Hata pembe za ndovu zilikutwa kwenye meli ya chairman Mbowr
 
Picha liko hivi.mwaka 2015 ccm walijichanganya wakampata mgombea boys, Kwenye uchaguzi wa 2015 Mgombea wa ccm hakushinda.

Ikabidi NEC na KiTENGO walazimishe kumtangaza mgombea was ccm mshindi.

Kwa upinzani ule waliogopa sana.ikabidi KITENGO wakaahidi kumsaidia Huyo jamaa yao kanyaboya.kwa miaka 5 yakwanza mpaka 2020 ndo wanaogoza nchi, yeye yupo kama boya tu. Mtamlaumu Bure kichaa wa watu matatizo yote in kitengo.

KITENGo wakaapa kwanza kuusambaratisha upinzani,has a Cuf na chadema(ukawa)

mipango mingine in pamoja na kuvuruga uchumi, ili watu wakose ukwasi, kuzuia bunge live, kuua( Ben saa8, mawazo), kuteka(Roma, nondo), kuhonga wapinzani vyeo(kitila, Dr slaa nk...), kununua wapinzani( waitara, kalanga)

kitengo wameamua kliangamiza taifa almradi MTU wao atawale bila changamoto ya upinzani, kwa sababu ya uwezo wake mdogo
 
Lakini na wapinzani wajiulize kwa sasa wana sera gani za kuvutia masikio ya wananchi?
Zamani walikuja na sera nzuri sana sijui kwa sasa wamekuaje?
JF imekuwaje..... Sasa hizo sera utazisikia wapi na hakuna amsha amsha za Mikutano,midahalo kama zamani. Unaposema hawana sera za kuvutia nani amewakaririsha? Ningefurahi angalau kama ungekuwa umesoma ilani ya CHADEMA na pia umesoma walau bajeti kivuli ya mwaka huu ndio uje useme wapinzani hawana sera ila hizi tabia za kusema wapinzani hawana sera ilihali hata katiba ya CHADEMA wala ilani ya uchaguzi ama bajeti mbadala hujawahi soma inashusha hadhi ya JF.
 
1. Kuua upinzani siyo kazi rahisi kama wanavyofikiri. Upinzani hautakaa ufe mpaka dunia ya binadamu ifike mwisho wake. Historia ya dunia ipo wazi kuwa hakuna mawazo ya binadamu au mfumo wa kibinadamu uliodumu bila kuangamizwa na kuibuka mawazo na mifumo mbadala iliyo imara zaidi. Tanzania aliyoiongoza Nyerere ni tofauti sana na anayoitawala Jiwe (Magufuli). Hii inatokana na kuongezeka sana kwa uelewa wa watu kuhusu mifumo mbalimbali inayotumika duniani kuanzia Uchina mpaka Amerika. Ni suala la muda tu, elimu ya kujitambua yaani angalau kidato cha nne itakuwa imewafikia asilimia kubwa ya watanzania. Kadiri watu wengi wetu watakavyokuwa na elimu ya kujitambua, ndivyo itakavyokuwa ngumu kuwatawala kwa njia ya kuwalaghai.

2. Kadri mfumo mmoja utakavyopambana kujilazimisha kuwa wa kudumu, ndivyo maangamizi yake yatakavyoharakishwa. Historia zote tangia zama za kale kabisa mpaka hapa majuzi zinatupa mifano iliyo hai ambayo sihitaji kuielezea hapa. Mfumo unapokaribia mwisho wake, ishara za kuangamizwa kwake ili kupisha mfumo mpya huambatana na nguvu kubwa ya kutaka kuendelea kujiimarisha, na mara anguko (Muhumu ni wenye akili kujipanga na kuwa na watu wenye "vision" baada ya anguko). Kusipokuwa na mfumo mpya ulio imara wa kushikiia usukani baada ya anguko, tutaishia kwenye maafa ya muda mrefu sana kama Kongo, Libya, Somalia na kwingineko. Mataifa yenye utambuzi huu, huweka space ya mawazo na mifumo mbadala ili endapo litatokea anguko taifa lisiingie hasara ya maangamizi au instability ya muda mrefu.

3. Binadamu mara nyingi hutafuta uhuru (freedom). Kadiri dunia inavyosogea mbele, binadamu amekuwa ni kiumbe wa kujitafutia uhuru zaidi na sauti zaidi ya namna bora ya kujitawala wenyewe kwa wenyewe, na mara nyingi upinzani huchipua pale mtawala atakapojaribu kupora madaraka ya watu. Pamoja na kiu kubwa ya watawala kutaka kujitwalia madaraka ya kidikteta dhidi ya watu, upinzani huwa mkuu zaidi pale watu wanapohisi mamlaka yao imepokwa. Historia za mapinduzi sehemu nyingi duniani zimechagizwa zaidi na vita ya mamlaka kati ya watawala na watu.

Kwa kuhitimisha, mtazamo wangu ninaiona CCM imedhoofika kwa kiwango kikubwa sana. CCM imekuwa dhaifu hadi inaona wakombozi wao wanapatikana kwenye vyama vya upinzani. Hata wale makada waliokuwa wamejiimarisha kuanzia ngazi za chini kabisa, kwenda wilaya, wajumbe wa NEC kila wilaya na utitiri wa viongozi wamekosa nguvu ya kusema chochote. Chama wameachiwa vichaa wachache wakishirikiana na Lumumba na ikulu. Chama kinaendeshwa na sauti kutoka huko juu kwa akina polepole na wateuliwa wengine wasiokijua kabisa chama na wasiokuwa na "connection" yoyote huku chini. CCM imekufa, kinachotawala ni serikali na na vyombo vyake. Hapa kinachoonekana ni serikali na taasisi zake zote ikiwemo majeshi, msajili wa vyama, tume ya uchaguzi, serikali kuu yote na kushuka chini mpaka pale mkono wa Rais unapoishia, wote wanafanya kazi za CCM.

Yapo makosa mengi yanafanywa na hii serikali ya awamu ya tano. Makosa haya yanaifanya kazi ya kuujenga upinzani mioyoni mwa watu iwe nyepesi. Mfano rahisi sana unapatikana hapahapa kwetu. Kadiri upinzani ulivyokandamizwa huko Zanzibar, ndivyo wananchi walivyozidi kuuamini. Mpaka walipoamua kuuhujumu kabisa kwa kupora ushindi uliokuwa wa wazi kabisa 2015. Uporaji ule uliweka mazingira ya kuvunjika kwa huu muungano siku za usoni kwa amani au kwa shari. Dalili zake zipo wazi sana hata kwa wale wa CCM nao wameshaanza kujiona kuwa koloni tu na hata maamuzi yao mpaka yapate kibali kutoka dodoma. Makosa yaleyale yanajirudia huku Tanganyika. Ipo siku itathibitika wazi kuwa CCM haina uwezo wa kushinda chaguzi huru. Chaguzi zitakuwa na ni kati ya matakwa ya watu au matakwa ya serikali.
 
Pesa za kuwapandisha watumishi madaraja anasema hamna ila 1.2 billion za kurudia uchaguzi kila mara iko standby.Najuta sana kuzaliwa Tanzania yenye aina hii ya administration/leadership style.
Wangekuwa wanahama CCM na kwenda CHADEMA uchaguzi usingerudiwa?? Alipohama Nyalandu kwenda CHADEMA uchaguzi hakurudiwa???
 
Back
Top Bottom