Jinsi Radio Free Afrika ilivyoyumba na kupoteza ubora kutokana na Mmiliki wake kuitumia Kisiasa

Jinsi Radio Free Afrika ilivyoyumba na kupoteza ubora kutokana na Mmiliki wake kuitumia Kisiasa

Tamaa ilimponza, angebaki kusimamia media zake zingeendelea kusimama imara.
Kakosa vyote. Atasubiri sana.
Baada ya mmiliki wake kuona jiwe hakutimiza ahadi yake akaweka hadharani kwamba jamaa aliwahi kulalia kitanda cha Milembe hospital.
 
Radio gani Tanganyika haifanyi politics?




KAZI ni kipimo cha UTU
 
Diallo yupo kwenye siasa tabgu anaanzisha hio redio. Tatizo kubwa pale ni PESA,HELA,NJORONJORO
Wewe ndio umeongea vizuri tatizo ni PESA.Imagine miaka ya 2002 radio ya moto ila wafanyakazi wamepaukaa kama magoti ya mbuzi .Wanakaa nyumba moja kama danguro.
 
Hayo mengine ni uongo Ila ukweli ni ushibdani tu ndo unawatoa kwenye soko, ukiangalia kwa makini mmiliki na nahisi hata management yao bado ni watu wa zamani ambao wameendelea kuwa na mitazamo na milengo yao juu ya ufanyaji kazi wa media yao, tofauti na kina efm, wasafi, crown, mjini, furaha na nyinginezo ambao wao wanajali usasa zaidi, na trending ya dunia ya sasa,
Lakini pia HELA ndo kila kitu jamani kama tu zamani wale Kiss fm walikua wanatema yai kama wazungu lakini tukiwa nao mtaani unaishia kusikitika maana unacheka hadi unawaonea huruma, Hata uvumilivu wa watangazaji wa sasa ni kiduchu sana mtu hawez kukaa miez miwili tu hajaona mkeka wa payroll, hivyo watangazaji wenye vipaji wanakata yamaa haraka sana, wanabaki wale wanaoforce had kieleweke
All and all Ahsante RFA kwa great memories utotoni.
 
Back
Top Bottom