Jinsi trafiki Dar wanavyopata pesa bila kutumia nguvu

Jinsi trafiki Dar wanavyopata pesa bila kutumia nguvu

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari,

Nimetumia nafsi ya kwanza si kwamba Mimi ni trafiki , hapana bali nawasilisha mazungumzo tu niliyofanya na rafiki yangu mmoja ambaye sasa kahamia Trafiki kutoka kwenye kitengo kingine cha kipolisi hapahapa jijini Dar es salaam.

Huyu kijana ambaye anapenda sana maisha ya starehe alijikuta akiishi maisha magumu licha ya kuwa mtumishi wa umma anayelipwa mshahara na posho kama 2 hivi kwa mwezi.

Madeni kwake hayaishi, hayo ndio maisha yake kabla hajaukwaa utrafiki.

Mpaka mkewe ambaye ni Askari wa Magereza alimkimbia.

Majuzi aliacha lindo kidogo baada ya jamu kupungua ndipo tulipokutana.

Nikamuuliza hii gari ni yako ? Nilimuuliza hivyo kwakuwa najua huyu chalii akipata pesa suala la kuazima au kukodi gari kwaajili ya misele ilikuwa ndio kazi yake.

Akasema it's mine nimenunua kwa kufanya installment yaani alikuwa akilipa mdogo mdogo yard mpaka kamaliza pesa yote Ml. Kumi na ushehe ndani ya miezi kadhaa.

Akasema kuwa usiidharau ile elfu 2 ninayopewa na konda, kwa siku sikosi laki mbili mpaka Tano.

Alisema kuwa wanahakikisha kila daladala inayopita kituo chao inachajiwa 2000 mara moja kwa siku , na wanachokifanya ni kugawanya daladala (yaani zamu zamu) na si kugawanya pesa. Unachokipata ni chako na boss wako utaenda kumpooza baadaye.

Sasa jamaa haishi kwa madeni, mke wake karudiana naye na ana mpango wa kuanza kujenga.

Kuna mambo mengi ya hovyo yanafanywa na madereva wa daladala pamoja na Makonda wao kwa abiria kwakuwa matrafiki wamewageuza kuwa chuma ulete basi huwabeba . Labda wafanye makosa makubwa ndipo watashikwa.
 
Kwamba gari lina tatizo ila huandikiwi faini bora ukauwe abiria huko mbele?

Halafu bado unamuona trafiki ana weledi wa kazi na ana akili timamu?

Nyie ndiyo mizigo nchi hii kuhalalisha rushwa kuliko kujali usalama wa abiria.
Kuna magari ni mabovu ila yanapiga kazi siku nenda rudi.
 
Mi niliwahi fanya biashar ya daladala, kwa kweli wale jamaa wanakera ...maana lazima kuwe na PESA YA TRAFIKI.......

Mpaka AVATAR yangu nikaweka picha yao.....!

rushwa ipo wazi , nje nje , na hakuna wa kuikomesha
 
Kwamba gari lina tatizo ila huandikiwi faini bora ukauwe abiria huko mbele?

Halafu bado unamuona trafiki ana weledi wa kazi na ana akili timamu?

Nyie ndiyo mizigo nchi hii kuhalalisha rushwa kuliko kujali usalama wa abiria.
Maisha hayajawahi kuwa fair, acha kujiona una akili sana
 
1657344749174.png
1657344749174.png
 
Ni kawaida mzee, na traffic wakisema wasimamie sheria kwa 100%, nadhani lazima zifunguliwe thread nyingi za ugumu wa usafiri, maana hakuna daladala ambayo itaingia barabarani,hila baadhi tu,
Na kwa magari madogo ndio hivyo hivyo mtaishia kuzipaki nyumbani pia,
Maana hakuna chombo Cha Moto ambacho kimekamilika kwa 100% au dereva ambae anakidhi vigezo kwa 100%
 
Ni kawaida mzee, na traffic wakisema wasimamie sheria kwa 100%, nadhani lazima zifunguliwe thread nyingi za ugumu wa usafiri, maana hakuna daladala ambayo itaingia barabarani,hila baadhi tu,
Na kwa magari madogo ndio hivyo hivyo mtaishia kuzipaki nyumbani pia,
Maana hakuna chombo Cha Moto ambacho kimekamilika kwa 100% au dereva ambae anakidhi vigezo kwa 100%
Kwahiyo buku mbili ndio suluhisho?
 
Kama umemaliza kwa Tarafiki anaechukua elfu mbili (2000) Sasa unaeda kutuletea habari za wapi TRA, Bandalini, Tanesco, Ma wizarani humo ? Ili Tuone nao wanachukua elfu mbili ? Baada ya hapo Utakuwa umetuletea habari kamili.
Kuna watu wa OSHA nao huwa wanachukua mpaka 500,000 ,1,000,000 kwa mshindo mmoja
Huko kwenye viwandaz
Bado kuna watu TBS teh teh
Nchi hii kila mutu inataka kula

Ova
 
Kuna jamaa namjua alikuwa trafiki anazinguana na boss wake kuhusu hesabu Maana mabosi wana Mgao wao daily sasa bosi anamtishia atamrudisha kituoni kwa maana kwamba awe wa kituoni tu kuandika rb n lindo la kituo. jamaa akambembeleza sana boss, boss kakomaa jamaa akaenda kwao tanga kuloga baada ya wiki boss kahamishiwa mbagala huko yeye kabaki eneo lake la barabarani.
 
Back
Top Bottom