Jinsi vijana wanavyotengeneza pesa kila siku kwa kutengeza maudhui TikTok

Jinsi vijana wanavyotengeneza pesa kila siku kwa kutengeza maudhui TikTok

FRESHMAN

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2011
Posts
9,137
Reaction score
34,793
Habari wadau,

Nilikuwa nawadharau sana vijana wanaoimbaimba na kucheza cheza TikTok. Nawaona wapuuzi hawana kazi ya kufanya na wajinga.

Mtoto wa shangazi yangu ni mmojawapo wa hao wapuuzi wa TikTok. Ana followers laki 6 huko TikTok. Ni binti ana miaka 21 na anasoma chuo kikuu kimojawapo nchini.

Shangazi alikuwa analalamika anahisi mtoto wake amekuwa tapeli ama amepata madanga. Maana amekuwa na pesa huku hana ajira yeyote, mara kanunua boda boda, mara kanunua simu ya gharama, mara kanunua mavifaa ya saloon ya kike.

Baada ya dogo kuhojiwa sana akafunguka hela anavyozipata. Yupo chuo mwaka wa pili now. Akasema hela anazipata kupitia TikTok. Wasanii wa bongo fleva wanataka nyimbo zao zitrend TikTok.

Hivyo wakitoa nyimbo zao huwa wanawafata watu wenye followers wengi TikTok na kuwaambia waanzishe challenge za nyimbo zao ili kuwainfluence followers wao na wao waige na mwisho nyimbo inakuwa hit song.

Hivyo wasanii huwa wanawalipa hao TikToker wa kuanzisha challenge kama yeye. Mfano yeye anachaji elfu 30 kwa challenge ya wimbo wa msanii.

Wasanii wapo kibao na wengi ma underground na nyimbo mpya zinatoka kila siku. Hivyo kwa siku iliyokuja vizuri anaweza kuhudumia hata wasanii 10 na kuingiza laki 3 easy tu japo pia kuna siku huwa hapati mteja hata mmoja.

Pia kuna wasanii wa Kenya na Nigeria nao wana mchezo huu. Pia waimba nyimbo za injili na kwaya kina Rose Muhando, Bukuku na wengineo nao wameiga mchezo huu. Hivyo ndio inampa hela anazonunua vitu.

Dogo katuonesha inbox yake TikTok na Instagram tukaona wasanii kibao wamemfata DM na wanavyomtumia miamala kaonesha ili kutetea hela zake kwamba anazipata kihalali.

Binafsi nimeshangaa sana na kumpongeza dogo kwa jinsi alivyojiajiri.
 
Kulipa ni nini ?

To each their own..., Kuna Babu yangu kule Bush mwaka mzima anatupia vimbegu kwenye ardhi anasubiri mvua inyeshe ili atoe tule tumbegu maradufu; ingawa serikali na wadau hawamjali lakini ndio anatulisha sisi ingawa yeye benki hana hayo makaratasi yanayoitwa pesa...; lakini katika hii closed system ya maisha naona anachofanya kinalipa sababu ndio kinatupatia huku nishati kina sisi tunaomdharau kwa kukosa kwake pesa...
 
Habari wadau.

Nilikuwa nawadharau sana vijana wanaocheza cheza tik tok. Nawaona wapuuzi hawana kazi ya kufanya na wajinga.

Mtoto wa shangazi yangu ni mmojawapo wa hao wapuuzi wa tik tok. Ana followers laki 6 huko tik tok

Ni binti ana miaka 21 na Anasoma chuo kikuu kimojawapo nchini

Shangazi alikuwa analalamika anahisi mtoto wake amekuwa tapeli ama amepata madanga. Maana amekuwa na pesa huku hana ajira yeyote mara kanunua boda boda. Mara kanunua simu ya gharama, mara kanunua mavifaa ya saloon ya kike.

Baada ya dogo kuhojiwa sana akafunguka hela anavyozipata.


Yupo chuo mwaka wa pili now. Akasema hela anazipata kupitia tik tok.

Wasanii wa bongo fleva wanataka nyimbo zao zitrend tik tok.

Hivyo wakitoa nyimbo zao huwa wanawafata watu wenye followers wengi tik tok na kuwaambia waanzishe challenge za nyimbo zao ili ku wainfluence followers wao na wao waige na mwisho nyimbo inakuwa hit song. Hivyo wasanii huwa wanawalipa hao tik toker wa kuanzisha challenge kama yeye. Mfano yeye analipwa elfu 30 kwa challenge ya wimbo.

Wasanii wapo kibao na wengi ma underground na nyimbo mpya zinatoka kila siku. Hivyo kwa siku anaweza kuhudumia hata wasanii 10 na kuingiza laki 3 easy tu.


Pia kuna wasanii wa kenya na nigeria nao wana mchezo huu.

Pia waimba nyimbo za injili na kwaya kina rose muhando, bukuku na wengineo nao wameiga mchezo huu

Hivyo ndio inampa hela anazonunua vitu.

Dogo katuonesha inbox yake tik tok na instagram tukaona wasanii kibao wamemfata dm na wanavyomtumia miamala kaonesha ili kutetea hela zake kwamba anazipata kihalali.

Binafsi nimeshangaa sana na kumpongeza dogo kwa jinsi alivyojiajiri
Dogo kawapiga, ila kwa kuwa mmeamua kuamini uongo wake yote mema tu.
 
Labda kweli, vipi account yake huwa anapost nyimbo tofauti fofauti kwa muda gani.

Isijekua amekuona wewe ni mjomba na sio uncle janjajanja kakuingiza cha kike ili na wewe ukaaminishe wenzio. Hivi vitoto ni vijanja sana.

All in all mitandaoni kuna easy money kwa wale wanaopenda mitandao.
 
Labda kweli, vipi account yake huwa anapost nyimbo tofauti fofauti kwa muda gani.

Isijekua amekuona wewe ni mjomba na sio uncle janjajanja kakuingiza cha kike ili na wewe ukaaminishe wenzio. Hivi vitoto ni vijanja sana.

All in all mitandaoni kuna easy money kwa wale wanaopenda mitandao.

Account yake ina nyimbo kibao anaimba imba kila siku lazima aimbe imbe nyimbo kazaa .
 
Mbona mimi ni maarufu huko TikTok silipwi pesa hiyo 😬

Hela hulipwi na tik tok. Bali hela unapewa na wasanii watakaokufata ufanye challenge ya nyimbo zao.

Wasanii huwa wanaangalia watu wanaofit kufanya challenge ya nyimbo zao.

Labda wewe ni maarufu ila age imeenda ama huna muonekano wa kuchangamsha tik tok kwa challenge
 
Idadi ya Challenge x 30,000?
Imagine challenge zipo 100, jumla ni 3,000,000, je vitu alivyonavyo na hela aliyoiingiza vinalingana, huenda simu yake tu 2,500,000, vitu vya saluni alinunulia KIKUU? Nguo ananunulia karume? Naomba tuweke hesabu vyema kabla ya kusema kuna mapato lukuki nje na tiktok, tiktok ni bango tu
 
Back
Top Bottom