Tokyo40
JF-Expert Member
- Jun 16, 2013
- 2,065
- 1,925
Salaam wanabodi..mimi na mwenzangu tunatamani sana zao letu la kwanza tupate twins...naomba kuuliza kama kuna njia ya kitibabu ambayo tunaweza kutumia ili tupate twins...je kuna ushauri wowote wa kidaktari ambao tunaweza kuapply ili mke wangu aweze kupata mapacha? Je hili la mapacha linawezekana kama wataalam wanavyo dai la kuchagua jinsia linawezekana..naombeni msaada wakuu.
Sio mapacha tu hata ukitaka jike au dume utapata. Dini na sayansi haipatani. Wana Dini pia walisema ni kufuru kwenda mbinguni kusoma sayari au kutua mwezini. Tukirudi kwenye swali lako, ni rahisi kupata pacha lakini kwa kutumia njia ya sayansi siyo ya mapenzi ya kawaida. nenda hospitali yoyote yenye uwezo wa kutumia technology Ya IVF , Zipo nyingi Afrika Kusini na India . Lakini pia ujue kuwa Ina risks za miscarriage, japo Nina rafiki alifanikiwa India kupata mapacha kwa njia ya IVF na Clomid inasaidia kwa mwanamke kutoa mayai pacha . Wa naotesha mayai mawili (embryos) kwa mwanamke kupata mapacha.