DOKEZO Jinsi ziwa Tanganyika lilivyo na maji mengi

DOKEZO Jinsi ziwa Tanganyika lilivyo na maji mengi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Duniani ziwa Tanganyika ni la pili kwa ukubwa baada ya ziwa Baikal. Ziwa Baikal lina ujazo wa kilomita za ujazo 23,000 huku Tanganyika likiwa na 18,900. Nyasa lina 8,500 na Victoria lina 2,500. Ziwa Victoria linaingia kwenye ziwa Tanganyika karibu mara nane.

Ziwa Tanganyika lina asilimia 18.9 ya maji yote safi yaliyopo kwenye uso wa dunia. Tanzania sisi tunamiliki 46% ya ziwa Tanganyika. Kwa maana hiyo, hilo linatufanya tumiliki asilimia kama 8.5 ya maji safi yote yaliyopo kwenye uso wa dunia. Ukijumlisha na sehwmu za ziwa Nyasa na Victoria utaweza kuta karibia asilimia 11 ya maji yote safi yaliyopo kwenye uso wa dunia yapo Tanzania.

Ukitoa maji yote kwenye ziwa Tanganyika halafu ukasema mito yote duniani itiririke kulijaza, itatumia karibia miezi saba kulijaza. Mto mkubwa wa Amazon utatumia karibu miaka mitatu. Mto Congo utatumia miaka 13.

Ukisema mto Rufiji utiririke kujaza Ziwa Tanganyika utatumia karibu miaka 1,400.

Hili ziwa peke yake linaweza kunywesha kila jiji Tanzania nzima. Na kila mtanzania. Ukipiga hesabu ya watanzania wote milioni 60 na ukipiga hesabu ya kuwa kila mtu, mtu mzima hadi mtoto mchanga anatumia lita mia moja kwa siku utaona kuwa tunahitaji kilomita za ujazo 2.2 kwa mwaka. Kinadharia, kwa idadi hiyo tunaweza kutumia maji ya ziwa hilo kwa miaka 8,500.

Asitokee mtu wa kutuambia tuna upungufu wa maji.

Pia soma; Sasa maji ya Ziwa Tanganyika kutumika kwa wananchi wa Jimbo la Kavu Wilaya ya Mpibwe Mkoani Katavi
 
Katika maziwa yote nchini, Victoria linaongoza kwa kunyonywa, mpaka limelala aisee
emoji3.png
emoji3.png
emoji3.png
emoji3.png
 
Hii imekaa kitaalamu, hatuna akili, hatuna ubunifu,hatuna nia ya kutoka tulipokwama kila siku tuko palepale

hatuwezi kabisa kutumia rasilimali tulizobarikiwa. Hili ziwa lingekuwa uswiss huko lingekuwa na manufaa makubwa sana kwa waswiss.

Ziwa Tanganyika unaambiwa tangu kuumbwa kwake walishavua asilimia 2 tu ya samaki wote waliohai ingekuwa huko mbele hili ziwa lingekuwa na faida kubwa sana kwa nchi, cha ajabu hata waishio jirani na ziwa hili hukosa maji mabombani, tumuombe Mungu atupe akili ya kuziona fursa na kuzitumia Amiin.
 
Hii imekaa kitaalamu, hatuna akili, hatuna ubunifu,hatuna nia ya kutoka tulipokwama kila siku tuko palepale

hatuwezi kabisa kutumia rasilimali tulizobarikiwa. Hili ziwa lingekuwa uswiss huko lingekuwa na manufaa makubwa sana kwa waswiss.

Ziwa Tanganyika unaambiwa tangu kuumbwa kwake walishavua asilimia 2 tu ya samaki wote waliohai ingekuwa huko mbele hili ziwa lingekuwa na faida kubwa sana kwa nchi, cha ajabu hata waishio jirani na ziwa hili hukosa maji mabombani, tumuombe Mungu atupe akili ya kuziona fursa na kuzitumia Amiin.
Kabisa, badala ya kufunga kumuomba Mungu mvua, tufunge tumuombe akili ya kuweza kutumia rasilimali tulizonazo.
 
Back
Top Bottom