Job Ndugai: Ipo siku Tanzania itapigwa mnada, Watu tukishakopa tunapiga makofi kujipongeza. Deni la Taifa ni 70 Trilioni

Job Ndugai: Ipo siku Tanzania itapigwa mnada, Watu tukishakopa tunapiga makofi kujipongeza. Deni la Taifa ni 70 Trilioni

Mama asiwasahau hawa watoto wa yatima maana watasema siri zote, bado wana uchungu wa baba yao
 
Maneno mujarrabu kutoka kwa mwamba
Kalamu ya Baba Askofu Benson Lwakalinda Bagonza

UMOJA au UHURU WA MIHIMILI?!

Spika kakosoa.
Rais kajibu.
Nani yuko sahihi?

Ugumu uko hapa:

1. Ukiishakuwa kiongozi unapoteza haki ya kulalamika. Rais kaonyesha uongozi kwa kukopa. Spika kapoteza uongozi kwa kulalamika.

2. Tunahitaji uhuru wa mihimili siyo Umoja wa mihimili. Maslahi ya walipa Kodi yapo katika uhuru wa mihimili si Umoja wa mihimili.

3. Watawala wasipigane vijembe. Simba akinguruma anamsaidia mwindaji ajue mahali Simba alipo. Rais azingatie moyoni.

4. Spika kapatia kutujulisha hatari za mikopo. Atujulishe na hatari ya kulipa mishahara wasio wabunge. Amalizie kutujulisha uhalali wa sheria zinazotungwa na wasio wabunge.

5. Mikopo ikisababisha nchi ipigwe mnada, bunge na mahakama watakosa uhalali wa kutumia sheria zilizotungwa na wasio wabunge.

6. Spika anashabikia tozo kuliko mikopo. Tozo ni maumivu yetu. Zimeua matumaini ya kuishi ili tuweze kwenda madarasa yanayojengwa na tozo.

6. Tukumbushane: Wakikosekana wapinzani wa kweli, CCM itatengeneza wake wa ndani. Tumempata Kiongozi Mkuu wa upinzani bungeni. Mmemwona? Vaeni miwani.

CCM imara inahitaji Upinzani Imara siyo upinzani wa ndani.

Kazi Iendelee.
 
Baada ya tafakari ya muda mrefu sana nimelazimika kuyaelewa maneno ya Spika Job Ndugai. Naungana nae.

Ni wazi kuwa maneno yake yamekuja wakati sahihi. Ameongea kama mwananchi wa kawaida kabisa... Na kwa vile yupo ndani ndani huko kuna mengi anayajua!

Cha ajabu sisi wananchi wa kawaida ndo wale wale tunaompiga vita na kumkashifu. Tulipaswa tuwe na harakati huru na endelevu za kutaka kujua matumizi ya fedha za mikopo na zile za tozo! Isije ikawa tunatumika kama dhamana ya mikopo ili wateule wachache wazidi kuneemeka.

Dalili za matumizi ya kufuru na anasa zipo wazi kabla hata ya SSH. Je, hatupaswi kwenda mbali zaidi kuhoji uhalali wa mikopo/tozo na matumizi yake?? Au tukishaambiwa na watawala basi tuufyate zaidi ya maandiko!
Kwanini takwimu za makusanyo ya tozo haziwekwi wazi?
 
Hiv nan ambaye alikuwa makin????Achen chuki hii nchi tatizo kubwa ni hili katba chakavu la kulindana
Mambo ni bora liende tu tunakosa umakini kwenye mambo ya msingi.

Sasa kama tuna resources za kila lakini bado tunakimbilia mikopo kama Taifa tunafeli.
 
Nadhani father Michongo ujumbe ameupata Sasa..kesho atakuja kusema hamkunielewa
 
Kile ni kichaka cha Mwigulu... anajichotea tu!!
Vodacom walitoa tathmini ya miamala wanayokamilisha kwa mwezi kufikia 10T transactions. Sasa pigia hesabu kila muamala serikali ile buku tu ni bei gani wanapata? Halafu ati makusanyo yalikuwa 48B tu 😅😅😅
 
Ndugai anapaswa kujua kwamba kama angesimama imara Magufuli asingethubutu kukopa fedha halafu akaendelea kuuhadaa umma kwamba tunatumia fedha zetu za ndani.

Udhaifu wa Ndugai ndiyo umepelekea taifa kufika hapa lilipo. Bunge chini ya Ndugai lilimuacha Magufuli akaongoza nchi kama vile anaongoza familia yake na sasa kila kitu kimeharibika.
Achana na JPM, kalaumu ndugu na jamaa za familia yenu mnavyoparangana.
 
Ni vile tu msamiati wa neno kujiuzulu kwa mwafrika huwa hauna nafasi.lakini huyo maza alitakiwa akae pembeni tu,hii nchi imemshinda for sure.
Huyo Ndungai nae unafiki tu.
 
Ohh Mama anakuja kuunganisha taifa mbona taifa haliungani? Ohh Mama anaponya majeraha mbona sioni kinachoendelea nchini? Tume kuwa taifa la kulalamika tena , no leadership.

Mama mama wapi kelele tu with zero impacts.
 
Tukuunganisha ya job na ya polepole na ya nape tutapata tu sentensi kamili
 
Back
Top Bottom