Job Ndugai: Ipo siku Tanzania itapigwa mnada, Watu tukishakopa tunapiga makofi kujipongeza. Deni la Taifa ni 70 Trilioni

Job Ndugai: Ipo siku Tanzania itapigwa mnada, Watu tukishakopa tunapiga makofi kujipongeza. Deni la Taifa ni 70 Trilioni

Ndugai ana hoja kubwa bahati mbaya watanzania hawapendi kufikiri wamempuuza sana, hatupendi kuchambua bali kushabikia.

Ndugai nasema ana hoja kubwa naomba ajibiwe kitaalamu, sitaki kuamini kuwa ndugai kajiropokea tu
Wajukuu watamsaidia kupata majibu
 
Hoja ya ndugui ni unafiki ...


Watanzania hatuwezi kukaa kujadili unafiki ....

Watanzania tunaakili Sana mseee[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]

Tupo zaidi ya million 56 ,inamaana wewe pekee yako ndio umeona ndugai anahoja ???[emoji28][emoji28][emoji28]
 
Spika wa bunge la jamhuri ya muungano JOB NDUGAI amedai kuwa kulingana na mwenendo wa deni la taifa kufikia trilion 70 ipo siku nchi ya Tanzania itapigwa mnada amenena maneno hayo baada ya kusema kwamba tozo zote zamiamala ya simu zilizopitishwa na bunge zilipitishwa kwa lazima kwani wananchi hawakuridhia kama inavyosema na baadhi ya wanasiasa.

Kwa maneno hayo naona kuna mambo yanaendelea huko Lumumba yapo mambo hayajakaa sawa ukiona spika anaanza kulalamikalalamika! Alianza kuhusiana na serikali kuhamia Dodoma kuwa kwa sasa kazi zote za serikali na makongamano zimerudishwa Dar-es-Salaam.

Mheshimiwa Ndugai popote ulipo nakwambia hivi wewe na viongozi wako mnaifanyia nini hii nchi mbona mnakaa mnalalamika lalamika wakati chama ni cha kwenu na chama chenu ndicho kimeunda serikali.?

=====

UPDATES;

=====

=> Watu wengi wanatulaumu sana, ninyi ndio Wasomi. Hebu fikiria, Juzi mama kaenda kukopa 1.3 Trilioni deni.

=> Na tuna majengo hivi sasa ya Madarasa, ya Vituo vya afya, ambayo yanajengwa kwa tozo. Hivi ipi bora? Sisi Watanzania wa miaka 60 ya Uhuru tuendelee kukopa na Madeni au tubanane banane hapa tujenge wenyewe bila madeni Makubwa yasiyoeleweka? Ni lini tutajenga wenyewe?

=> Tutembeze bakuri ndo heshima? na tukishakopa tunapiga makofi! Sisi wa kukopa kila siku?

=> Tukasema pitisha Tozo, anayetaka asiyetaka, pitisha Tozo. Lazima tuanze kujenga wenyewe. Nani atatufanyia? Yupo wapi huyo Mjomba? Tukapitisha Tozo.

=> Sasa 2025 itaamua. Mkitoa waliopo sawa. Waje watakaokuwa kazi yao kwenda kukopa endepo hiyo ndo namna ya kuendesha Nchi.

=> Hivi sasa deni letu ni 70 Trilioni. Hivi ninyi si Wasomi? Is that healthy? Kuna siku nyi itapigwa mnada hii. Madeni Madeni Madeni

=> Bajeti yetu Trilioni 30, Trilioni 10 kati ya hizo kwa Mwaka tunalipa Madeni.

=> Tumeenda Kukopa 1.3 Trilioni, Tunapiga Makofi. Tunawapa Wazungu Trilioni 10 Mariba Matupu. Wanatufanya Sisi Mazezeta. Hela yako Mwenyewe. Anachukua hela yako, halafu anakupa Kidogo Unashangilia.

=> Toza fanya hivi, tujitegemee, Tusimame wenyewe. Kuna ubaya gani? Hata msomi anatupinga.
View attachment 2060338

Zaidi, soma: Thread 'Spika Ndugai: Rais Samia naomba unisamehe kwa sintofahamu iliyotokana na kauli yangu🙏' News Alert: - Spika Ndugai: Rais Samia naomba unisamehe kwa sintofahamu iliyotokana na kauli yangu🙏
Dah!
Ukweli mchungu!
 
Ukweli kwa sasa mama anasifia anaupiga mwingi lakini hali ni tete! Kwanza katika uongozi wake mimi siwezi kumsifia kwa lolote kwani ni mzembe kufatilia mambo ya kitaifa anawaamini watendaji wake huku wakimpa taarifa za uongo bila kuzifanyia kazi kwa sasa baadhi ya miradi haiendi ipasavyo, mheshimiwa raisi kwa muangalia yeye hana tabia za udokozi lakini hao vijana wake angewafatilia sana wasimpotoshe kwani kwa sasa malalamiko ni makubwa katika nyanja mbalimbali zinazohusu nchi.
 
There is a dark fate from the speech. Mpaka 2025 mengi yatatokea.
 
Kama Ndugai aliomba msamaha akasamehewa kwanini hakuna sehemu yoyote ya dunia hii iliyokiri kwamba yuko huko? Mbona kosa la Ndugai ni dogo kuliko la Mbowe lakini Mbowe tunaye mitaani yuko huru, kasamehewa (maana hawezi kushindikana kufungwa)?
 
Kama Ndugai aliomba msamaha akasamehewa kwanini hakuna sehemu yoyote ya dunia hii iliyokiri kwamba yuko huko? Mbona kosa la Ndugai ni dogo kuliko la Mbowe lakini Mbowe tunaye mitaani yuko huru, kasamehewa (maana hawezi kushindikana kufungwa)?
Magaidi hutetewa mno
 
Halafu kuna watu walikuwa wanawadharau Wagogo! Ona sasa utabiri wa Job, na haya yanayotokea sasa!

Sema tu alizingua kuomba ule msamaha wake uliofeli. Bora angekomaa na msimamo wake mwanzo mwisho.
 
Halafu kuna watu walikuwa wanawadharau Wagogo! Ona sasa utabiri wa Job, na haya yanayotokea sasa!

Sema tu alizingua kuomba ule msamaha wake uliofeli. Bora angekomaa na msimamo wake mwanzo mwisho.
Ilibidi zombie msamaha ili kuokoa mafao yake.
La sivyo Nabii Ndugai angeambulia patupu.
 
Hao UN walipinga ujenzi wa bwawa la umeme kwamba ni kuharibu mazingira lakini sasa hivi wanapinga kuwahamisha wamasai ili kulinda mazingira!

Mtu mweusi amka
 
Back
Top Bottom