Pre GE2025 John Heche: Dkt. Slaa akifia Gerezani, Rais Samia atawaambia nini Wananchi? Uonevu ni kitu kibaya

Pre GE2025 John Heche: Dkt. Slaa akifia Gerezani, Rais Samia atawaambia nini Wananchi? Uonevu ni kitu kibaya

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

upupu255

Senior Member
Joined
Sep 4, 2024
Posts
119
Reaction score
144
Hapo jana Februari 12, akiwa kwenye mkutano wake wa hadhara Sirari, jimbo la Tarime vijijini, Makamu Mwenyekiti Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Heche amehoji juu ya kukamatwa na kunyimwa dhamana kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Wilbroad Slaa na pia endapo akifariki taarifa itakayotolewa itakuwa ya aina gani.

Soma: Kesi ya Dkt. Slaa imeahirishwa mpaka Februari 18, 2025

"Mzee kama Dkt. Slaa mzee wa miaka 76 amekuwa mbunge kwa miaka 15, amekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA amekuwa Balozi,unamkamata kesi ambayo ina dhamana unatumia mahakama kumuangamiza, hivi akikufia Rais Samia unamtoaje unatuambiaje watu? kwamba amekufa tu kifo cha kawaida, leo wakakuambia Dkt. Slaa hatupo naye tena unawaambiaje watanzania"


 
Oy wanangu ni kweli kabisa Kuna malipo ya Kila unachokifanya . Yes zuri na ovu vyote hivi hulipwa! Na pengine uovu hulipwa Kwa uovu mkubwa kabisa na vilevile wema hulipwa zaidi na zaidi. Kila mmoja ataitumikia karma na usipoitumikia karma vizazi vitalipa!
Huyu Mzee analipwa!
Bado mi nawe . Nasi tutalipwa Kwa kadiri ya uovu na wema wa matendo yetu! Si mbali siku inakuja! Ni wapi? Ni hapahapa
 
Acha aendelee kusota rumande sababu anaweza kuja kukengeuka kwenye kipindi cha kampeni kama mwaka 2015 akawapa ushindi CCM dakika za lala salama!
 
Hii inaweza kuwa njia mojawapo itayowafanya wawe watiifu, kuwatiisha, na itawabadilisha misimamo yao.
 
Hapo jana Februari 12, akiwa kwenye mkutano wake wa hadhara Sirari, jimbo la Tarime vijijini, Makamu Mwenyekiti Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Heche amehoji juu ya kukamatwa na kunyimwa dhamana kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Wilbroad Slaa na pia endapo akifariki taarifa itakayotolewa itakuwa ya aina gani.

Soma: Kesi ya Dkt. Slaa imeahirishwa mpaka Februari 18, 2025

"Mzee kama Dkt. Slaa mzee wa miaka 76 amekuwa mbunge kwa miaka 15, amekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA amekuwa Balozi,unamkamata kesi ambayo ina dhamana unatumia mahakama kumuangamiza, hivi akikufia Rais Samia unamtoaje unatuambiaje watu? kwamba amekufa tu kifo cha kawaida, leo wakakuambia Dkt. Slaa hatupo naye tena unawaambiaje watanzania"


Mama anaupiga mwingi
 
Ila huyu mama hadi aibu..

Hivi Dr Slaa kosa lake kubwa ni lipi?
Atoe ushahidi wa Samia kumpa Mbowe hela ili ashinde uchaguzi chadema. Hakuna mtu mwenye haki ya kuumiza wengine na yeye asiumie!! Slaa ameleta damage kubwa sana kwa heshima ya Mbowe acha alipie gharama yake mshenzi mkubwa.
 
Back
Top Bottom