Kuna tofauti. Hela za serikali kama ruzuku hazitakiwi kupitia kwenye akaunti ya mtu binafsi. Kama ni hivyo, swali litakuwa ni kwa nini mlipaji anaingiza pesa katika akaunti binafsi. Aidha, pesa zinazokusanywa na chama hazipaswi kupitia katika akaunti binafsi. Lakini pesa anazotoa Mbowe mwenyewe kuchangia chama ni lazima zitatoka katika akaunti yake. Vile vile pesa anazochangisha yeye binafsi kuna nyingine zitaenda moja kwa moja katika akaunti ya chama na kuna nyingine watoaji watapendelea zaidi kumpa yeye binafsi kuliko chama. Yote haya yana wezekana. Ndio maana KM amesema shutma za jumla hazisaidii. Kama mtoa shutuma anajua kuna pesa zimepita huko nje ya utaratibu atoe detail zake. Zimetoka wapi, kiasi gani na ziliingizwa lini kwenye hiyo akaunti binafsi na ya chama. Nje ya hiyo ni fitna tu.
Amandla...