John Mnyika: Kiongozi wa CHADEMA Mzee Ali Mohamed Kibao, adaiwa kushushwa kwenye Basi na kuchukuliwa na watu wasiyojulikana

John Mnyika: Kiongozi wa CHADEMA Mzee Ali Mohamed Kibao, adaiwa kushushwa kwenye Basi na kuchukuliwa na watu wasiyojulikana

nchi inazidi kuelekea giza nene taratiibu. Yalianza zamani kidogo; kasi ikiongezeka taratibu huku ikihanikizwa na ujinga, kiburi, uchawa na tamaa ya fisi.

Muda si muda vilio vitakolea kila pande hata kwa wachimba visima. Wote watalia kwa kupokezana; na kwa ujinga uliokithiri, wasielewe wamefikaje hapo.
Mara dodoma ,mara wapi, uzuri ni kuwa Kila anayeuawa au kutekwa ni Mwanachadema tu.

Tunaomba na watu wengine pia wasio wanachadema nao watekwe na kupotea. Tumechoka sisi tu?
 
Mwaka wa uchaguzi huu. 'Wenye nchi' hawataki vikwazo kwenye harakati zao za kuendelea kudhulumu.Kila kikwazo 'watakiondoa.'
 
Hii ndio Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu, John Mnyika kupitia ukurasa wake rasmi wa Mtandao wa X (Twitter)
---
John Mnyika kupitia ukurasa wake rasmi wa Mtandao wa X (Twitter) anaripoti:

Nimetaarifiwa usiku huu kuwa Mzee Ali Mohamed Kibao Mtaalamu katika Sekretariati CHADEMA amechukuliwa na watu walijitambulisha kuwa ni polisi(bila uniforms).
Walizuia basi la Tashrif alilokuwa amependa kutoka DSM kwenda Tanga kwa gari za kawaida wakaingia na kumfunga pingu.
Tunaendelea kufuatilia kupata taarifa kamili ikiwemo wamempeleka wapi. Nimetoa taarifa hii ya awali ili iwapo kuna yoyote alikuwepo kwenye basi au ana taarifa zozote kuhusu alipopelekwa atupatie au kutupa ushirikiano wa haraka.

Nashauri Kila kiongozi awekewe microchip kwa ajili ya GPS. Halafu kampuni za nje ya nchi zipewe tenda ya kuwafuatilia wakiwa popote duniani
 
Mkuu mamayo huyu anaupiga mwingi!
Siyo dhalimu kabis
Mungu amewafuta machozi, hao watu wantekwa na Magufuli
Hata huyu mama wa kambo afanye nini, hawezi kuta ushetani wa dhalimu magu. Hutaki jinyonge.
 
Vyombo vya usalama viwe makini kidogo na haya mambo, kama kweli kuna utekaji unaohusiana na siasa na tunaufumbia macho kwa sababu labda unatufavor basi tujue tunaeleke kaburini taratibu.

Tutambue mambo ya usalama yanahitaji umakini na busara kubwa sana na sio siasa maana dunia ya leo ina mengi sana tunayoyafahamu na tusiyoyafahamu na yote huwa yanabackfire tukijichanganya.

Hii michezo ikiendelea tutambue hakuna anayekubali uonevu kila siku, Bali tutawajengea watu usugu na kuwafanya waanze kutafuta namna ya kujilinda na hata bargain style itakayofanya wateke ili mbadirishane mateka, lakini pia tutambue huko mitaani hawa watu huishi na viongozi wa kada mbalimbali huku watekwaji nao wakiwa na ndugu zao huko mitaani.
Palestinians imefika mahala hawaogopi tena kufa wala kuumia bali wamebaki na dhamira moja ya kupigana na adui usiku na mchana kwa pamoja, Nasisi sasa tunawalazimisha watu wetu wafike.

Vikundi vingi vya kigaidi na marcenaries wapo na kumilikiwa na mataifa makubwa kwamaslahi ya mataifa husika, Mataifa makubwa moja ya silaha yao kubwa kudestabilize nchi ni pale nchi inapogawanyika na kundi moja kuhisi linaonewa linahitaji msaada, basi kundi hilo husaidiwa mara moja ili kuchafua amani na upande mwingine kwa siri huzidi kuchochea hali pia kupitia watawala, hapo mtajikuta mnapigana hovyo hovyo bila hata kujua mnapigania nini.

Mwenyezi Mungu ametutunuku Amani basi tuilinde Kwa kudumisha umoja.
 
Katibu Mkuu, John Mnyika

Akizungumza na taifa kupitia waandishi wa habari baada ya tukio la utekaji wa kiongozi wa CHADEMA mtaalamu Ali Mohamed Kibao mjumbe wa Sekretariat Halmashauri ya Chama Taifa lililofanywa jana jioni ndani ya basi la abiria la Tashrif namba za usajili T343 EES uliofanywa na watu 'wasiojulikana' eneo la Kibo Tegeta Complex nje kidogo ya mji wa DSM, basi la TASHRIF lilizuiwa na magari mawili land cruise na lingine dogo wakiwa na silaha pia pingu .... mashuhuda wanasema pia kulikuwemo 'abiria' asiyejulikana akajumuika na hao watekaji kuondoka na kiongozi wa CHADEMA ....


View: https://m.youtube.com/watch?v=s9Qe9MzzO3o
 
Hii ndio Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu, John Mnyika kupitia ukurasa wake rasmi wa Mtandao wa X (Twitter)
---
John Mnyika kupitia ukurasa wake rasmi wa Mtandao wa X (Twitter) anaripoti:

Nimetaarifiwa usiku huu kuwa Mzee Ali Mohamed Kibao Mtaalamu katika Sekretariati CHADEMA amechukuliwa na watu walijitambulisha kuwa ni polisi(bila uniforms).
Walizuia basi la Tashrif alilokuwa amependa kutoka DSM kwenda Tanga kwa gari za kawaida wakaingia na kumfunga pingu.
Tunaendelea kufuatilia kupata taarifa kamili ikiwemo wamempeleka wapi. Nimetoa taarifa hii ya awali ili iwapo kuna yoyote alikuwepo kwenye basi au ana taarifa zozote kuhusu alipopelekwa atupatie au kutupa ushirikiano wa haraka.

Mm sielewi hii Tanzania yetu kweli kunatofauti gani leo hii na enzi za utumwa ambapo babu zetu na ndugu zetu wengi walibebwa kwa staili kama hizi na hakuna aliyepigana kupinga hilo yaani hapa tofauti ni miaka tu lkn mazingira ni yaleyale tu leo tumesoma shule lkn hatuwezi kulindana hii inaonyesha kwamba hata leo hawa waarabu na wazungu wakiamua kurudi na kuanza kututandika viboko wanaweza na kwa uboya tulionao tena uliojaa ubinafsi tutakubali tu.Polisi wanakataa kwamba sio wao wanaowachukua hawa binadamu wenzetu na sisi tunaendelea kuwavumilia watu ambao tayari jeshi letu zuri limeshawakataa mm nadhani tufike mahali tuseme basi inatosha tuanze ukurasa mpya maana hawa wenzetu wanateswa sana kisa kusema ukweli na kila kiongozi yuko kimya kwa sababu familia zao ziko salama,na ndugu zao wote wako salama.Tukumbuke kwamba watu wakishakataliwa na jeshi la polisi kwamba halihusiki basi hao wanaojitambulisha kama polisi tujue si polisi bali ni majambazi na wezi kama wezi wengine tucheze nao mwanzo mwisho.Tukileta ujinga tutaisha maana watawala tulionao hawana huruma na mtu yeyote watanzania tuamke.
 
Back
Top Bottom