Join the Chain: Wananchi waanza kujaza kumbi, Lissu kuongoza watoa mada, mtikisiko mkubwa wasubiriwa

Hivi yule bosi wa TAKUKURU aliyewahoji viongozi wa chadema kuhusu ruzuku baada ya kudanganywa na Lijuakali yuko wapi ?
Tunaongelea michango mnayokusanya sasa kwenye join the chain usihamishe mada
 
Maana yangu ni kwamba , ukileta uongo kuhusu hela za chadema utapotezwa na Mungu
Mkuu tunatakiwa kuonyesha uwezo mbadala wa kiuongozi...ni pamoja na kujibu hoja kwa hoja haijalishi ikoje na sio vitisho.
Kufa watakufa watu wote usifanye hivyo.
 
Ulitakiwa utoe mrejesho nini kiliongelewa na matokeo yake
Uzi huu niliuanzisha ukiwa Live , lakini kabla hata sijaomba maji ya kunywa wakubwa wakaondoa ile nembo ya Live , kwahiyo ikanifanya niache ku update , nikaacha mtiririko uende kama wakubwa wanavyotaka , ili kuepusha mkanganyiko na wakubwa
 
Mkuu tunatakiwa kuonyesha uwezo mbadala wa kiuongozi...ni pamoja na kujibu hoja kwa hoja haijalishi ikoje na sio vitisho.
Kufa watakufa watu wote usifanye hivyo.
Laana ya Mungu kuhusu uzushi na uongo haina uhusiano na vifo vya kawaida
 
Nimesema wapeni chadema wenzenu huko ripoti ya hizo bilioni 15 mlizokusanya ndani Ya masala mawili mimi sihitaji hiyo ripoti
Chadema ina vikao vya chama ambavyo mambo yote huamuliwa huko , mnashindwa kupata taarifa ya vikao vyetu kwa vile wale mamluki waliokuwa wanavujisha taarifa tumewatimua
 
Kwani jf nayo wameufyata?
Maxence Melo
Ikiwa uzi haukiuki sheria za jf kwanini mnazifuta au ku edit?
Sikusema kwamba waliufuta na ndio maana hata leo upo na tunaujadili , Bali waliondoa alama ya Live , unajua bado ile Join the chain haikueleweka vizuri , wao walidhani join the chain ni tundu lissu kuongea tu , hawakujua kwamba miji yote nchini Tanzania na duniani ilikuwa imeandaa Kumbi na TV zao zile pana , kwa ajili ya kusikia yatakayoongelewa , sasa haya maandalizi hayakuonekana kama yako Live , nadhani ndio maana ile nembo iliondolewa , nadhani walitaka live ianze baada ya Lissu kuanza kuhutubia .

Naamini walikosea kidogo , ila siamini kama waliogopa
 
Siku hizi wanafuta nyuzi nyingi au ku edit mkuu...sijaandika kwa ajili yako pekee
 
Hiki ni kitu kizuri lakini watafanikiwa tu endapo watamuacha hayati JPM to Rest In Peace maana wanaunganisha maji na mafuta hawatafanikiwa kamwe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…