Wakipekee
JF-Expert Member
- Aug 21, 2019
- 6,194
- 10,711
Chanzo nyeti kiasi Kwamba wakikuambia kesho unakufa utaanza kufanya sala na kutubu [emoji2957][emoji1787][emoji1787]Chanzo nyeti ninacho na natamba nacho. Lol
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Chanzo nyeti kiasi Kwamba wakikuambia kesho unakufa utaanza kufanya sala na kutubu [emoji2957][emoji1787][emoji1787]Chanzo nyeti ninacho na natamba nacho. Lol
Acha tu abaki anonymous kama alivyo.Nitamuuliza kama atakubali niwaambie ni nani, ni member mwenzetu hapahapa JF.
Ila sasa nikishawaambia hatokuwa tena chanzo 'nyeti', acha ibaki kuwa siri.
Hii ni kweli kabisaLakini zikiwa nyingi si itakuwa vizuri kwetu walaji kuwa na machaguo mengi Mkuu?
Kha! Haya mambo ya kuuliza makabila yanafaida gani? Kabila halina uhusiano wowote na mafanikio ya mtu, ni kuendekeza upuuzi tu.Hivi huyo jamaa ni mkinga?
Mara Joe mara Jose mara Joseph
Ingekuwa hivyo basi wazaramo wasingekuwa wacheza mdundiko na waangua madafu.Kabila halina uhusiano wowote na mafanikio ya mtu,
Kwa mtu kama Kusaga mpaka anafikia uamuzi wa kuwekeza pesa nyingi maana yake ana uhakika kuwa itamlipa.Hongera kwake...
Sina uhakika kuna wapenzi wengi kiasi gani wa filamu za kitanzania, ila kama wapo wa kutosha basi ni moja ya biashara nzuri...
Kikwazo pekee kitakuwa ni ughali wa internet...
Kwa mtu kama Kusaga mpaka anafikia uamuzi wa kuwekeza pesa nyingi maana yake ana uhakika kuwa itamlipa.
Naona wengi hoja zenu zimebase kwenye matumizi ya vifurushi vya intaneti, lakini naamini akiwa na maudhui bora watu watasukumwa kuangalia bila kujali ugumu wa maisha na kipato kiujumla.Maybe yes, maybe no...Mungu amsaidie afanikiwe kama alivyofanya projections zake
Customer behavior ya Watanzania ni very unpredictable...
Kwa utafiti wangu usio wa kina sana, kwa content ambayo ni HD ukifanya streaming kwa kutumia simu, data usage huwa kati ya 500MB hadi 600MB na ni wastani wa saa nzima na nusu hivi, hii ni sawa na shilingi 1500 (pesa ambayo ni sawa na 20% ya pato la Mtanzania kwa siku)
Netflix ni nini mkuu. Inatumikaje?View attachment 2975932
Ni Joe Kusaga tena…
Waswahili husema mwenye nacho huongezewa, sio sahihi. Mwenye nacho hujiongeza ndipo huongezewa.
Mfanyabiashara na mwekezaji mkubwa nchini aliyejikitika zaidi kwenye tasnia ya burudani, Joseph Kusaga yuko mbioni kuja na App itakayokuwa katika mtindo unaoshabihiana na App maarufu ulimwenguni Netflix.
Ni App ya burudani…
Maudhui makubwa yatakayopatikana ndani ya App hiyo ni burudani. Zikiwemo series na movies za kibongo, habari za michezo na kutakuwemo pia na vipindi vya matukio ya wanamuziki wa Bongo Flava kama vile matukio wakati wa kuchukua video za nyimbo zao (behind the scenes)
Ni uwekezaji mkubwa!
Taarifa zinasema Joe Kusaga amefanya uwekezaji mkubwa sana katika App hiyo, kuanzia ununuzi wa vifaa vya kisasa vinavyosemekana kuwa na uwezo sawa na App nyingine kubwa za kimataifa kama Prime Video, Hulu, Netflix n.k
Pia itakuwa inapatikana kwenye TV za Smart na Android kama zilivyo hizo App nyingine.
Ni mradi wake binafsi.
Huu ni mradi binafsi wa Joe Kusaga nje ya miradi ya familia yake ambayo wanamiliki miradi mingi kwa pamoja ukiwemo Clouds media.
Pia ni mradi wake bila ya ushirika kama ilivyo Wasafi n.k
Kuzinduliwa June mwaka huu
Mpango wa awali wa uzinduzi ulikuwa tarehe 9 June ambayo ni siku ya kuzaliwa ya Joe Kusaga, lakini kuna mambo yalitokea yakapelekea uzinduzi kusogezwa mbele.
Licha ya changamoto hizo zilizojitokeza, bado uzinduzi utafanyika tarehe yoyote ndani ya mwezi huohuo (June).
Kupitia chanzo cheti,
Nifah.
Kwani hiyo app inatumika kwa matumizi gani mkuu?Naona wengi hoja zenu zimebase kwenye matumizi ya vifurushi vya intaneti, lakini naamini akiwa na maudhui bora watu watasukumwa kuangalia bila kujali ugumu wa maisha na kipato kiujumla.
Huwa sina mashaka na habari zako za udaku,mara nyingi huwani za kweli,komalia hukuhuku utafika mbali,kule kwenye mpira hebu tuache na simba yetuChanzo nyeti ninacho na natamba nacho. Lol