Kuna vitu vingi ambavyo havina faida lakini watu wanaendelea kufanya... Mfano kuendelea kuwa mwajiriwa huku hakuna faida...Mfano je watu wataacha kazi, pamoja na mafao kuwa asilimia 25 tu...
Ulishaingia, kuna mengi ya kufikiria..
Watu wako ulaya au marekani, wakimwambia aliyoko bongo,usije huku hakuna ishu sana, basi mbongo atajibu kama majibu yaliyoko hapa, kama kubaya mbona hawarudi bongo..
Biashara fulani haina faida, aah hataki wengine wapate, ndio maana anasema hivyo..
Mara nyingi aliyopo upande huu hufikiri aliyopo ng'ambo ya fensi anafaaidi..
Mimi kwa kutumia mifano ya biashara nyingine Tanzania, naweza amini hakuna faida sana kwenye fiesta..
Mfano fanya biashara hapa TZ halafu uone mikondo inayotaka hela yako..Leseni jiji, Mapato TRA, OSHA, FIRE, SDL, Brela annual returns, kodi ya chumba cha biashara, mishahara, umeme, maji, ulinzi, uchafu, EFD machine nk.. halafu mtu aseme mbona hawaachi? Jaribu ndipo utagundua maneno ya Kusaga ni kweli,.lakini hapo inakuwa too late...