Joseph Selasini: Mwaka 2020 Mbatia alitupeleka na Anthony Komu kwa Dkt. Bashiru Ally kufanya makubaliano na CCM

Joseph Selasini: Mwaka 2020 Mbatia alitupeleka na Anthony Komu kwa Dkt. Bashiru Ally kufanya makubaliano na CCM

Wacha kiupepo hiki kiendelee kuvuma ili tuendelee kuona uchi wa kuku.
 
  • Kicheko
Reactions: EEX
Hawa chawa wa Ccm ndani ya upinzani wako wengi sana. Zitto, mr30, wote ni hao hao, wakiona wameshindwa ndionhuleta vurugu. Yaani mchawi lazima mwisho wa siku atakuambia tuu amekuulia mtoto.

Ona sasa 30 kaanza kujitaja.
 
Mbatia ni mchumia tumbo tu. Hana uafisa wowote. Uchaguzi wa mwaka 2020 walipoitwa na Magufuli, waliahidiwa vyeo na fedha za kusaidia kampeni zao na wao wapewe baadhi ya nafasi za ubunge na kuwa chama cha upinzani kitiifu kwa mwendazake. Hali ilikuja kubadilika baada ya Chadema kumsimamisha Lissu na kuvutia umati mkubwa wa watu. Magufuli alipoona hali ni mbaya kwake akaamua kutumia dola kupora uchaguzi na akawatupilia mbali hawa wachumia tumbo kwani aliona hawana uwezo wa kupambana na Chadema.

Yap, kula tano mkuu, hapa umesema ukweli wa wazi, na tulisema kabisa kuwa Magufuli alivunja makubaliano yake na kina Mbatia na Lipumba, baada ya kuona kura za CDM zingemuumiza hata yeye. Akaona isiwe tabu bora apore uchaguzi kabisa, maana hata kuiba bado ingekuwa ngumu kwani akina Mbatia hawakuwa na mvuto wowote. Akaagiza usalama wa taifa waende na karatasi za matokeo fake na hayo ndiyo yatangazwe.

Ilifika mpaka mahali Mbatia anapangiwa sehemu za kwenda kufanya kampeni, na ujumbe gani awe anatoa. Baada ya Mbatia kuacha hewani ndio imebidi awaunge mkono cdm kwani huko ccm hana support yoyote.
 
Chadema mfuatilieni vizuri Selasini. Anaonyesha ni janja janja Sana. Atawagombanisha yeye anaondoka. Viongozi ifuatilieni hiyo card. Ikiwezekana anyan'ganywe abaki na Mbatia wake.

Pili chadema kuweni makini na hawa wawili wasibomoe chadema. Hata Mbatia simwamini sana.

Ila Selasini Kuna mchezo anacheza na hayupo peke yake. Hayo maisha tunavyoyaona huku mitaani tunasema ni utapeli.
 
Kwamba inawezekana kweli Mbatia alienda na kina Komu kwa Bashiru ndio maana Mbatia akaonekana akifanya mikutano nje ya eneo lake kwa uhuru bila kusumbuliwa na polisi, naamini hii ilikuwa ni ruhusa aliyopewa toka juu, akaenda mpaka Mbeya.

Huyu Selasini hapa ana hoja ya msingi hasa nikiunganisha na matukio yaliyopita, lakini nae kwanini hakuyasema haya wakati ule? atuambie waliahidiwa nini mpaka wakakaa kimya? nadhani aliambiwa atapewa ubunge ndio maana, hivyo hii hoja yake kwa wakati huu inakosa uzito.
 
Mbatia ni mchumia tumbo tu. Hana uafisa wowote. Uchaguzi wa mwaka 2020 walipoitwa na Magufuli, waliahidiwa vyeo na fedha za kusaidia kampeni zao na wao wapewe baadhi ya nafasi za ubunge na kuwa chama cha upinzani kitiifu kwa mwendazake. Hali ilikuja kubadilika baada ya Chadema kumsimamisha Lissu na kuvutia umati mkubwa wa watu. Magufuli alipoona hali ni mbaya kwake akaamua kutumia dola kupora uchaguzi na akawatupilia mbali hawa wachumia tumbo kwani aliona hawana uwezo wa kupambana na Chadema.
Lissu alivutia umati upi wa watu!!? Unajitekenya na kucheka.
 
Tukisema kwamba upinzani ni Chadema peke yake nchi hii muwe munaelewa,Watu wanakokotwa kwenda kuisaidia CCM halafu mnategemea wawasemee
Hiihii CHADEMA inayotumiwa na Samia atakavyo, au kuna nyingine?
 
View attachment 2239563
Picha: Joseph Selasini

Joseph Selasini: Kuna barua inaonekana kusambaa katika mitandao ya kijamii ikidaiwa kusaini wa na katiba kata wa Makiidi nyumbani kwetu, ikinihusisha mimi na uanachama wa CHADEMA. Niliondoka CHADEMA mwezi Juni 2020, na tangu nilipoondoka CHADEMA sikurejea tena"
Joseph Selasini: Mimi ni mwanachama wa NCCR, barua inayoendelea hivi sasa mitandaoni, imewekwa na watu wenye nia ovu, kama ningeomba kurejea CHADEMA na ningeandika barua, basi ingewekwa barua ya mimi kuomba kurejea CHADEMA na si barua ile"
Joseph Selasini: Sheria ya vyama vya siasa inaitaka kila chama Kuwasilisha kwa msajili wa vyama vya siasa nchini majina ya wanachama wote ambao ni wajumbe wa Kamati Kuu, Halmashauri Kuu, Baraza Kuu na Kamati kuu, hivyo wanaotaka kuthibitisha uanachama wangu, wakatafute hapo"

Joseph Selasini: Tangu ulipofanyika mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM, maneno mengi yamesemwa kwamba kilikuwa na mapinduzi, naomba niseme kwamba hapakuwa na mapinduzi bali kulikuwa na kikao halali cha Halmshauri Kuu kilichotimiza akidi"
Joseph Selasini: Maneno ya kwamba Joseph Selasini amempindua Mbatia ni maneno ya kejeli, uchochezi, uzushi na uongo. Ni maneno yanayojaribu kujenga dhana ya kwamba, wenyeviti wa vyama vya siasa ni wakubwa kuliko katiba ya vyama vyao na hawawezi kujadiliwa"

Joseph Selasini: Halmashauri Kuu ya NCCR Mageuzi na ya chama chochote cha siasa, haina mamlaka ya kikatiba ya kumfukuza Mwenyekiti wa chama, mamlaka ya Halmshauri Kuu ni kumsimamisha mwenyekiti, ni kama mfanyakazi anaposimamishwa kupisha uchunguzi"

Joseph Selasini: Sidhani kama Mwenyekiti aliyeongoza chama kwa miaka 23 anaweza kuogopa mkutano mkuu, au afanye vikao nje ya ya katiba ha utaratibu ili ajenge hofu ili watu wakuunge mkono"

Joseph Selasini: Moja ya jambo ambalo Mwenyekiti wetu (James Mbatia) ambalo anatuhumiwa nalo kwa muda mrefu ni uhusiano wake na Chama cha Mapinduzi (CCM), hata baadhi ya vyama vingine vya siasa vimekuwa vikisema kuwa hatumwelewi Mbatia ana uhusiano gani na CCM"

Joseph Selasini: Mimi na Anthony Komu tuliporudi NCCR Mageuzi mwaka 2020 Mbatia alitupeleka hadi kwa Dkt.Bashiru Ally kwa lengo la kufanya makubaliano ya kuisaidia CCM kwenye uchaguzi,tulipotoka kwenye kikao hicho tulikubaliana mimi na Komu kutoshiriki uharamu huo".
View attachment 2239578

Barua inayodaiwa kuwa ya CHADEMA inayomtaja Selasini kuwa aliomba kadi yao


Chanzo: Dar Mpya Blog
Shauri zenu mnaomwamini Joseph Selasini. Huyu ni msaliti kuanzia kwenye familia yao (hawakuelewana na kaka yake marehemu Masumbuko Lamwai hadi anakufa, baada ya mtafaruku wa NNCR wa kipindi cha Marando).

Hakuaminika Seminari alikofukuzwa na Askofu Pengo miaka ya 1980s, aliwahi kuiba gari ya THB miaka ya 1990s akiwa Transport Officer kwa kisingizio kuwa limeibiwa.

Hata mtaani kwake anakoishi haaminiki
 
View attachment 2239563
Picha: Joseph Selasini

Joseph Selasini: Kuna barua inaonekana kusambaa katika mitandao ya kijamii ikidaiwa kusaini wa na katiba kata wa Makiidi nyumbani kwetu, ikinihusisha mimi na uanachama wa CHADEMA. Niliondoka CHADEMA mwezi Juni 2020, na tangu nilipoondoka CHADEMA sikurejea tena"
Joseph Selasini: Mimi ni mwanachama wa NCCR, barua inayoendelea hivi sasa mitandaoni, imewekwa na watu wenye nia ovu, kama ningeomba kurejea CHADEMA na ningeandika barua, basi ingewekwa barua ya mimi kuomba kurejea CHADEMA na si barua ile"
Joseph Selasini: Sheria ya vyama vya siasa inaitaka kila chama Kuwasilisha kwa msajili wa vyama vya siasa nchini majina ya wanachama wote ambao ni wajumbe wa Kamati Kuu, Halmashauri Kuu, Baraza Kuu na Kamati kuu, hivyo wanaotaka kuthibitisha uanachama wangu, wakatafute hapo"

Joseph Selasini: Tangu ulipofanyika mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM, maneno mengi yamesemwa kwamba kilikuwa na mapinduzi, naomba niseme kwamba hapakuwa na mapinduzi bali kulikuwa na kikao halali cha Halmshauri Kuu kilichotimiza akidi"
Joseph Selasini: Maneno ya kwamba Joseph Selasini amempindua Mbatia ni maneno ya kejeli, uchochezi, uzushi na uongo. Ni maneno yanayojaribu kujenga dhana ya kwamba, wenyeviti wa vyama vya siasa ni wakubwa kuliko katiba ya vyama vyao na hawawezi kujadiliwa"

Joseph Selasini: Halmashauri Kuu ya NCCR Mageuzi na ya chama chochote cha siasa, haina mamlaka ya kikatiba ya kumfukuza Mwenyekiti wa chama, mamlaka ya Halmshauri Kuu ni kumsimamisha mwenyekiti, ni kama mfanyakazi anaposimamishwa kupisha uchunguzi"

Joseph Selasini: Sidhani kama Mwenyekiti aliyeongoza chama kwa miaka 23 anaweza kuogopa mkutano mkuu, au afanye vikao nje ya ya katiba ha utaratibu ili ajenge hofu ili watu wakuunge mkono"

Joseph Selasini: Moja ya jambo ambalo Mwenyekiti wetu (James Mbatia) ambalo anatuhumiwa nalo kwa muda mrefu ni uhusiano wake na Chama cha Mapinduzi (CCM), hata baadhi ya vyama vingine vya siasa vimekuwa vikisema kuwa hatumwelewi Mbatia ana uhusiano gani na CCM"

Joseph Selasini: Mimi na Anthony Komu tuliporudi NCCR Mageuzi mwaka 2020 Mbatia alitupeleka hadi kwa Dkt.Bashiru Ally kwa lengo la kufanya makubaliano ya kuisaidia CCM kwenye uchaguzi,tulipotoka kwenye kikao hicho tulikubaliana mimi na Komu kutoshiriki uharamu huo".
View attachment 2239578

Barua inayodaiwa kuwa ya CHADEMA inayomtaja Selasini kuwa aliomba kadi yao


Chanzo: Dar Mpya Blog
Nimekuelewa kwa tabu sana, tatizo langu ni kitu gani kilisababisha ushindwe kuueleza Umma mambo hayo tokea mwaka 2020 hadi Sasa. Je, visambusa na chai za asali ndivyo tu mlivyoambulia au kuna vingine ?
 
Tukisema kwamba upinzani ni Chadema peke yake nchi hii muwe munaelewa,Watu wanakokotwa kwenda kuisaidia CCM halafu mnategemea wawasemee

una uhakika gani CDM sio mali ya CCM..

unaikumbuka NCCR mageuzi iliyoitoa pumzi CCM mpaka marehemu JKN jasho likamtoka, baada ya hapo Lyatonga yuko wapi?..
 
Mbona viingozi wa upinzani na wachagga tu nchi hii kasoro zitto na rungwe
Acha ukabila wewe, kwanini mnakua na hasira na wachagga kiasi hiki? Kwani wao sio waTanzania? Mtu kapigiwa kura na mikoa yote kwani hawakujua ni Mchagga?

Mie kabila la Mama Samia au Majaliwa hata silifahamu na hainihusu maana Halina msaada wowote kwenye utendaji wa mtu, sasa why bother na kabila la Mbatia au Lipumba?
 
Back
Top Bottom