Uchaguzi 2020 Joshua Nassari amechukua fomu ya kuomba kupeperusha bendera ya CCM katika jimbo la Arumeru

Uchaguzi 2020 Joshua Nassari amechukua fomu ya kuomba kupeperusha bendera ya CCM katika jimbo la Arumeru

Joshua Nassari amechukua fomu ya kuomba kupeperusha bendera ya CCM katika jimbo la Arumeru.

Joshua Nassari aliwahi kuwa mbunge wa Arumeru kupitia tiketi ya CHADEMA na baadae alivuliwa ubunge na Speaker wa bunge kwa kosa la utoro. Joshua Nassari avuliwa Ubunge wa Arumeru Mashariki kwa “Utoro” Bungeni

Lakini pia alichukua uamuzi wa kwenda mahakamani kupinga uamuzi wa kuvuliwa ubunge napo aliangukia pua baada ya kujikuta akishindwa kesi mahakamani na hivyo kupoteza ubunge wake. Mahakama Kuu Dodoma: Joshua Nassari ashindwa kesi yake ya kuvuliwa ubunge

Baadae alichukua maamuzi magumu kama alivyoyaita na kuamua kuondoka CHADEMA na kuhamia chama cha Mapinduzi, ambako yupo mpaka sasa akiomba ridhaa ya kugombea ubunge tena kupitia CCM kwenye jimbo lilelile la Arumeru. News Alert: - Aliyekuwa Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari na Willy Qulwi Qambalo wa Karatu wajiunga CCM na kupokelewa na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa




View attachment 1509159

Toto JINGA.
 
My life style like movie,
Mwingi ka uduvi,
Ninavyo-rhyme quality ka mtoto wa juzi


Nimemmmiss sana Chid mazee

Mchaka mchaka siwezi choka,
Hata boot likitoboka.

Ngoma imara, ka mduara taratibu nawaokota,
The microphone dokta.

Mikausho ka sanamu,
Serikali naiongoza kwa nidhamu, ya damu!
 
Hii Sasa too much! Kila mtu anataka ubunge loh!

Basi tufanye Watanzania wote Ni wabunge Kisha tuanze kutangaza Nia Tena kugombea kuwa wananchi wa kawaida!
Ubunge umechukuliwa kama kazi rahisi sana, ambayo kila mtu anaweza kufanya. Kwanza vigezo au sifa za kuwa mbunge nazo ni rahisi vilevile. Yaani ujue kusoma na kuandika tu basi.
Kwa hiyo kama ulivyosema inawezekana kweli watz wote ni wabunge, kinachotafutwa ni nani ataingia kwenye ule mjengo maana wote hatutaweza kuenea.
Kuna mtu alisema kazi ya Konda wa daladala inaweza kuwa ngumu kuliko kazi ya mbunge, kwa sababu pamoja na kujua kusoma na kuandila anatakiwa pia ajue MAGAZIJUTO.
 
Mafuasi ya Disco Jocker ndivyo mlivyo, Mtu akijitambua akaachana na Saccos yenu mnamletea.kejeli sana, kazi mnayo mwaka huu
Hizo ni siasa za Tz, kwani Lowassa alipoama mlisemaje? Au mmesahau mlivyomwita kila aina ya jina chafu? Mbona naye alirudi nyumbani na kupokelewa kwa mbwembwe nyingi tu.
Tuvumiliane tu hakuna aliye msafi kihivyo!!!!
 
Mchaka mchaka siwezi choka,
Hata boot likitoboka.

Ngoma imara, ka mduara taratibu nawaokota,
The microphone dokta.

Mikausho ka sanamu,
Serikali naiongoza kwa nidhamu, ya damu!
Eeeeh bwana eeeehh, popompoo pishaa
 
Wanaoumia ni wananchi, wanaweka imani kubwa sana kwa wanasiasa bila kujua siasa ni ajira, unapoona maslahi yapo hatarini unabadilisha ofisi ili uendelee kula.

Pale mtakapotambua kuwa wanasiasa wapo ili kutafuna vitamu ndio mtaacha kutapika nyongo. Let him be, mwacheni ale penye nyama, mnataka atafune penye mifupa tu!!!
 
Mkuu we mkaribishe tu ccm,,asijekupita na hyo nafasi yako,maana watu kutoka upinzani wako smart sana,hawakawii kupewa nafasi zenu..
 
Labda mwenyekiti ampe kwa kuona anakifaa chama, ila jimboni wazee wamesema "hafai". Kule kwa wale jamaa kuna vikao vya chini ya mringaringa (huu ni mti ambao hutoa mbao ngumu na nzuri zenye kama ka wekundu kwa mbali) ... hapa ndio vikao muhimu hufanyika kwa wazee wa mila, ukoo na machifu toka enzi. Ingawa kwa sasa maamuzi ya vikao vya mila hayana sana influence kwa wameru kama ilivyo umasaini kwetu, ila DOGO JANJA Mzee wa maslahi aombe kudra kwa Mola ili abebwe na Mh. Mwenyekiti wa CCM.

La sivyo ajiandae tu kwa teuzi
 
mbona anangangania mkono wa huyo mdada?

ghafla amekuwa mwana kuli-find mwana kuli-get
 
Back
Top Bottom