Uchaguzi 2020 Joshua Nassari amuomba radhi Rais Magufuli kwa mabaya yote aliyomtendea akiwa CHADEMA!

Uchaguzi 2020 Joshua Nassari amuomba radhi Rais Magufuli kwa mabaya yote aliyomtendea akiwa CHADEMA!

Polepole amekua bilionea kimasihara sana, amegawana pasu kwa pasu pesa ya kuwanunua hao wapuuzi wote.

Polepole amekomba hizo hela za kuwanunua mamluki mpaka ameacha hata kazi yake ya uwakala wa Tigo pesa; ameuza kibanda chake pale Bahari beach!!
 
CCM hakuna njaa Nassari na Mashinji shavu dodo!
Ni kweli. CCM hakuna njaa, CCM ni kambi ya walafi na wanafiki. Walafi na wanafiki ni kama mbwa, bwana wake akiwa kwenye meza anatafuna minofu, yeye anakuwa chini ya meza akidakia makombo anayotupiwa. Siku ni nyingi kimbaumbau naye akaanza kunenepeana, hakuna cha ajabu hapo.


Muangalie vizuri huyu chakubanga, naye mashavu yameanza kutanuka...
 
Kuna mwanazuoni mmoja alisema, "kama wanasiasa wangelikuwa ni wanyama basi wangelikuwa ni nguruwe"

Kuna mwingine ameshauri kuwa haya majaribio ya chanjo ya corona , wafanyiwe wanasiasa ili wakipona tutajua zinafanya kazi na kama wakifa tutakuwa tumeziponya nchi zao!!!
 
Mwalimu nyerere aliwahi kusema. Kuna baadhi ya wanasiasa wanatabia ya umalaya umalaya.wao kununulika kwao Ni rahisi Sana. Wanaweza kuuza heshima yao .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vijana wenye akili wamehama Chadema.

Toka lini malaya wakawa na akili? Wangekuwa na akili wasingejiuza bali wangetuliza akili zao!! Mfano mzuri ni Lijuakali wewe unadhani yule ana akili? Na huyo ndio representative sample ya hao vijana wako!!!
 
Nasari, laana ya Wameru itakua nawe daima. Kumbuka Wameru walikupigania kwa jasho, damu na uhai wao wakati huna chochote mfukoni. Wameru walikutetea dhidi ya fedha lukuki za Lowasa kwa wakati huo wakati mpwaye Siyoi Sumari unagombea nae, ukashinda. Watu hawakuogopa mabomu, watu walijeruhiwa na wengine wakapoteza maisha kukutetea wewe. Leo hii umewasaliti watetezi wako waliokutoa shimoni umeenda kuwalamba miguu watawala. Kumbuka malipo ni hapahapa duniani kabla ya mbinguni. Laana ya damu ya Wameru iliyomwagika iwe nawe daima.
 
John hivi na hiyo ni habari, hivi kuwa ccm ni lazima uwe mjing@ kiasi hiki
 
Back
Top Bottom