Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

Hao mawakili gani wanaweka sheria bila vifungu? Kua makini police ni zaidi unavyowajua utapotea.
 
Nini kifanyike endapo haki hizo zikikiukwa na police kwa makusudi
 
Askari wenyewe elimu hola....sasa hizo sheria ni tabu tupu....hawzijui na wala hawaoni.....polisi anakuwa hakimu nahapo mhasibu hapo ni bank hapo ni mtawala yeye ndo kila kitu......tz akili ndogo huongoza akili kubwa....
 
Polisi wetu kabla ya maelezo anakuwa ameshakupiga kareti za kutosha. sasa hayo maelezo utatoa saa ngapi?.
 
Wajua Mwana haki kujua haki yako ni vizuri sana sasa wananchi walio wengi wapo vijijini na hata wale was mjini ni wachache ambao wanatambua haki hizi na wajibu Sasa swali kwako wasahidia vipi watu hawa hususani huku vijijini?
 
Askari yeyote haruhusiwi kufanya upekuzi mahali popote pale bila kuwa na Hati ya Upekuzi inayotolewa na Mahakama. Muda rasmi wa kufanya upekuzi ni kuanzia saa 2:30 asubuhi hadi 12:30 jioni.

Upekuzi utafanywa tu wakiwepo watu hawa:

1. Mwenye nyumba au mwakilishi wake
2. Mjumbe au Mwenyekiti wa Mtaa au Afisa Mtendaji
3. Jirani yeyote anayefahamiana na mwenye nyumba au mtu atakayeteuliwa na mwenye nyumba

Kabla ya upekuzi, mtuhumiwa ana haki ya kumpekua au kuwapekua askari kabla ya kuanza upekuzi. Hii ni kuepusha askari kuweka chochote kinachoweza kumweka mtuhumiwa kwenye makosa kijinai, kwani imeshatokea askari kupandikiza misokoto ya bangi au silaha kwenye maeneo yanayokaguliwa na kudai kuvikuta vitu hivyo mahali hapo.

Muhimu zaidi mtuhumiwa anayepekuliwa ana haki ya kuisoma hati ya upekuzi na iwapo hajui kusoma basi asomewe hati hiyo na mtu mwingine ambaye anajua kusoma na ambaye sio askari.

Mlalamikaji anaruhusiwa kuwapo kwenye upekuzi ili aweze kutambua vitu ambavyo ni mali yake iwapo tuhuma zitakuwa ni wizi wa mali au kujipatia mali kinyume cha sheria.

Kama kuna yeyote ambaye amepekuliwa kinyume na taratibu hizi, upekuzi huo utahesabika kuwa batili na hautatambuliwa kisheria.
 
Duuuu nmezikumbuka hz sheria nikiziona nacheka saaaana tz udhalimu tu
 
Kweli kabisa ila huku vijijini! Utapata virungu mpaka ukome.
 
Back
Top Bottom