Juice na unga wa ngano kutoka viwanda vya Kenya vitaingia Tanzania bila vikwazo na sementi kutoka viwanda vya Tanzania vitaingia Kenya bila vikwazo

Juice na unga wa ngano kutoka viwanda vya Kenya vitaingia Tanzania bila vikwazo na sementi kutoka viwanda vya Tanzania vitaingia Kenya bila vikwazo

Endelea kujidanganya. Mimi naishi Mashariki ya mbali huku na Juice za Azam zinauzwa hadi huku, sembuse Kenya? Kipindi Kikwete anatoka Azam walishaanza kuuza Juice zao Kenya ila mahusiano ya kinchi yaliharibika kipindi cha JPM ndio maana mauzo yalipungua. Haya makubaliano ni neema kwetu. Tatizo watu tumezidi woga. Wakenya ni watu wa kawaida tu.
Tatizo la umaskini wa maarifa, uelewa na negativity, ndiyo chanzo cha umaskini wa Watanzania wengi.

Kuifungua Tanzania na kuufanya uchumi wake uchangamane na Dunia, ndiyo njia sahihi ya kuleta kwa kasi maendeleo ya kiuchumi.

Rais Samia asimame kwenye mstari sahihi, wala asipoteze muda kusikiliza upuuzi wa wajinga wachache wasio na uelewa wowote kwenye masuala ya bishara, uwekezaji na uchumi.

Hongera sana Samia, upo kwenye njia sahihi. Tembelea nchi kama Dubai (UAE), ukapate uzoefu wao wa kina namna walivyoibadilisha nchi yao ndani ya miaka 15. Tembelea nchi kama Botswana, Singapore, Malaysia, Hong Kong upate uzoefu wao, namna biashara huru zilivyoyajenga mataifa yao. Usijifungie kama marehemu aliyekuwa akiua maendeleo ya uchumi, huku akiamini anajenga uchumi wetu kwa kasi.
 
Viwanda vyetu hususani kama vya Azam vijiandae kwa maumivu kwani itakuwa ngumu kushindana na maviwanda ya Kenya. Pia na sisi tunaotaka kujenga tujumba twetu tujiandae maumivu kwani cementi ya kutoka viwanda vyetu ambayo ina ubora wa hali ya juu hususani ile ya Dangote, kiasi kikubwa kitakuwa kinaenda Kenya kwani huko itauzwa bei kubwa. Hii ndiyo win win situation? Tunapata juice kwa bei nafuu na kupata sementi kwa bei ya juu zaidi.

Pia majadiliano ya EPA yameanza ili bidhaa kutoka nchi za Europa nazo ziingie Tanzania bila vikwazo kushindana na bidhaa za viwanda vyetu. Hili ni jambo jema ili kuvifundisha adabu viwanda vyetu ambavyo kila kukicha vinatupandishia bei ya bidhaa zao. Mafuta ya kupikia, sukari na kadhalika bei zake hazikamatiki.


Hii sana wachina wanatengeneza bidhaa mbovu kabisa, mfano tiles za Goodwill na Twyford ni takataka kabisa.

Halafu miradi ya serekali wanalazimisha kununua Bidhaa ya Tanzania.

Lazima tubadilike
 
Yaaani tunakoelekea hii nchi Mungu aingilie kati kenya wajanja sana kuzid Tz tujiandae kuumia kwa hili
Amekamata soko la Rwanda na Burundi tu, hilo la Kenya hawezi kuthubutu hata kidogo. Na hata hilo la Burundi na la Rwanda atanyang'anywa, rais wa Burundi sasa hivi yuko Kenya na yeye keshaweka dole!. Kenyatta safi!
Pessimism ni mbaya, kwahiyo unamuombea kufeli ama.
Yaani mtanzania mwenzako anapambana we unataka afeli
 
Tatizo la umaskini wa maarifa, uelewa na negativity, ndiyo chanzo cha umaskini wa Watanzania wengi.

Kuifungua Tanzania na kuufanya uchumi wake uchangamane na Dunia, ndiyo njia sahihi ya kuleta kwa kasi maendeleo ya kiuchumi.

Rais Samia asimame kwenye mstari sahihi, wala asipoteze muda kusikiliza upuuzi wa wajinga wachache wasio na uelewa wowote kwenye masuala ya bishara, uwekezaji na uchumi.

Hongera sana Samia, upo kwenye njia sahihi. Tembelea nchi kama Dubai (UAE), ukapate uzoefu wao wa kina namna walivyoibadilisha nchi yao ndani ya miaka 15. Tembelea nchi kama Botswana, Singapore, Malaysia, Hong Kong upate uzoefu wao, namna biashara huru zilivyoyajenga mataifa yao. Usijifungie kama marehemu aliyekuwa akiua maendeleo ya uchumi, huku akiamini anajenga uchumi wetu kwa kasi.
Ndugu unatofautiana na wadau wengine sehemu ndogo sana......hakuna anayepingana na haya mabadiliko mazuri nchini kwetu kwani ni neema.....wasi wasi wa wadau ni mazingira yetu ya kibiashara hayajaandaliwa kukabiliana na ushindani.......production cost kwa mujibu wa wadau ni kubwa sana hapa kwetu uki compare na nchi shindani.....hii haitaathiri ukuaji wa sekta yetu ya viwanda hapa nchini.....??
 
Ila
Kasome hayo makubaliano. Kenya wanataka hiyo sementi ya Dangote kwani grade yake ndiyo inafaa kwa ujenzi wa madaraja na maghorofa marefu. Sisi tunaweza kuletewa ile ya daraja hafifu inayozalishwa na viwanda vingi vya Kenya.
Ila wabongo sijui mna matatizl ya akili au vipi, aisee.
 
Tusiwe wavivu kufikiri ipo mifumo ya checks and balances.Masuala ya Kodi ni mapana Sana zipo protocol za EAC pia.
Kinaondoshwa ni urasimu na maamuzi ya kibabe ya kishamba na kijinga kwa dunia ya leo.
Wewe ni mtoto ndogo sana kwenye haya mambo huwezi kuekewa kinachojadiliwa hapa
 
Kasome hayo makubaliano. Kenya wanataka hiyo sementi ya Dangote kwani grade yake ndiyo inafaa kwa ujenzi wa madaraja na maghorofa marefu. Sisi tunaweza kuletewa ile ya daraja hafifu inayozalishwa na viwanda vingi vya Kenya.
Kwamba wamespecify kabisa kwenye mkataba wanataka dangote cement?

Kenya kwa sasa wana projects kubwa za ujenzi, mfano nairobi express way , na hawatumii Dangote cement, wanatumia cement zao ambazo zina ubora mzuri kuliko zetu.
Linapokuja swala la standards kenya wapo juu sana kuliko sisi ,
 
Ndugu unatofautiana na wadau wengine sehemu ndogo sana......hakuna anayepingana na haya mabadiliko mazuri nchini kwetu kwani ni neema.....wasi wasi wa wadau ni mazingira yetu ya kibiashara hayajaandaliwa kukabiliana na ushindani.......production cost kwa mujibu wa wadau ni kubwa sana hapa kwetu uki compare na nchi shindani.....hii haitaathiri ukuaji wa sekta yetu ya viwanda hapa nchini.....??
Huyo huwa hana akili, kifupi huwa ni mduni wa hoja na kudharau akili za wengine kujifanya anajua sana.
 
Hivi hapo Ikulu hakuna majasusi wa uchumi?

Si muoni yule vuvuzela wa chadema bwana Yericko Nyerere kwenye hili
Umemsikia waziri wa maswala ya nje ya nchi akiwasiliasha bajeti[emoji1787][emoji1787][emoji1787].

Mungu kwakweli mwaka 2021,katupiga tz 11:0
 
Waheshimiwa huu ni mjadala muhimu kwa taifa letu hivyo lingetakiwa kujadiliwa kwa weledi na sio mihemko, jazba, chuki na ushabiki........

Wataalamu na wasomi waliobobea kwenye masuala ya uchumi na biashara waje jukwaani tuweze kupata maoni na mitazamo ili jamii ya waTanzania itoke gizani....

WATANZANIA wanahitaji kujua matokeo hasi na chanya kwenye makubaliano haya.......


KARIBUNI WATAALAMU, WADAU NA WASOMI......
 
Hii sana wachina wanatengeneza bidhaa mbovu kabisa, mfano tiles za Goodwill na Twyford ni takataka kabisa.

Halafu miradi ya serekali wanalazimisha kununua Bidhaa ya Tanzania.

Lazima tubadilike
Tiles za goodwill na twyford Tanzanzia mara kadhaa nimeshuhudia zikishindwa kuingia kenya kwa sababu ya ubora hafifu, ,
Twyford wana kiwanda kenya lakini products zao ni level za juu kuliko twyford Tanzania

Bila usbishi wakenya wapi vizuri kwenye quality control
 
Back
Top Bottom