JWTZ ifanye uchunguzi dhidi ya tabia na mwenendo wa askari wake Denis Urio

JWTZ ifanye uchunguzi dhidi ya tabia na mwenendo wa askari wake Denis Urio

Jana ilivyokua mahakamani:

Wakili-Kuna msg yoyote/ujumbe wa sauti wowote ulio onyesha Mbowe akikuita wewe ndg Shahid (urio) Hilo jina la 'Homeboy'?

Urio-Hapana

Wakili:Je tukisema wewe ndio umetunga hilo jina la homeboy kwa kujipendekeza kwa Mbowe ili kujifanya unamjua sana tutakua tumekosea?

Urio-Sijui.
haha duh
 
Hii kesi inayoendelea mahakamani imeufungua macho umma wa Watanzania juu ya tabia ya askari huyo.
Aina ya Ushahidi ambao komando Urio ameutoa mahakamani umeacha maswali mengi sana ya umma juu ya tabia ya askari huyu lakini pia hata kuathiri taswira ya jeshi mbele ya umma.

Kuna haya mambo yafuatayo:
1. Je, jeshi lina taarifa za askari wake Denis Urio kumtafutia Mbowe walinzi ambao yeye Urio anasema walipanga kufanya uhaini? —Hata hivyo mahakamani Urio kasema hakuripoti Jeshini bali karipoti kwrnye mamlaka ya kipolisi. Je, hivi ndivyo askari wa JWTZ anavyopaswa kufanya pindi anapopata taarifa za uhaini?

2. Ushahidi wa Urio una matobo mengi, kuna kila sababu ya kudhani kuwa Urio anatoa ushahidi wa uwongo ili kuwaumiza raia wasio na hatia–Hapa JWTZ haina budi kufanya uchunguzi binafsi na kujiridhisha juu ya mwenendo na tabia za askari wake huyu Denis Urio

3. Mbele ya jamii ni vigumu kwa JWTZ kujiweka pembeni katika hii kesi kwa sababu, wananchi wanapata taswira mbaya kuwa JW inatumika kisiasa kuumiza wapinzani—Kwa hiyo ipo haja kwa JWTZ kujisafisha dhidi ya tabia na mwenendo wa Denis Urio kama ulivyothibitika katika ushahidi anaoutoa mahakamani.
Ndugu Missile of the Nation zipo undoubtful facts kadhaa zimefunuliwa na kesi hii;

1. Kuna uwezekano wa 99% huyu Denis Urio si askari wa JW bali alipandikizwa huko na kupachikwa uaskari wa JW na cheo just for a special mission huku CDF Mabeyo akiwa anafahamu fika au akiwa hafahamu kabisa kinachofanyika...

USHAHIDI:

Haya yanathibitishwa na circumstantial evidence inayomzunguka huyu shahidi, mathalani;

å Elimu ya huyu bwana kwa maelezo yake ni sekondari K.4 Haiwezekani mtu mwenye elimu level hii apate cheo cha "u - luteni" hata kama atakuwa mwanajeshi miaka 30 unless afanye K.6 kisha apate ingalau shahada ya chuo kikuu...

å Kama nilivyosema, alikuwa kule kwa kazi maalumu. Haijui basics za kawaida kabisa za kijeshi. Kaifanya hiyo kazi, kaimaliza lakini in a awful and very disgraceful end....

Hata alipokuja mahamakani kutoa huo ushahidi wake, hakutokea na hayupo kazini kitambo tu. Ametokea mafichoni...!!

2. Taasisi zetu (Executive, Judiciary & Parliament) by in large ndizo zimekuwa chanzo cha maovu ktk taifa letu. Yaani ile hali ya lawlessness katika nchi yetu inaanzia juu kwa wenye mamlaka ya kulinda na kutetea katiba na sheria za nchi kuja chini kwa raia Wa kawaida....

Kaatika mazingira tunadhani nini kitatokea huko mbeleni? Honestly, yeyote anaweza kuwa na correct prediction, kuwa tusipobadili hàli peacefully sasa kwaa kusema enough is enough, basi tutakuja kuibadilisha kwa kuamuliwa na wengine...!

Kwa mfano, katika sçenario hii ya mwanajeshi Denis Leo Urio, hebu tujaribu tu kufikiri hili...

Kwamba, iweje mwanajeshi mwenye mafunzo ya kulinda usalama na mipaka ya nchi anavuka mipaka ya majukumu yake na kuanza kushiriki uovu wa kuhujumu haki za raia wa kawaida huku vyombo vyenye mamlaka vikiangalia tu uchafu huu..?

Nani amchunguze nañi sasa kwa sababu the whole system is corrupted..?
 
Mburura kama wewe huna athari yoyote! Lakini ujue kuumbuka kumeanza. Sasa hivi mashetani wanaonekana na pembe zao livi. Refer afande Jumanne asiyejulikana, Huko Mtwara umeona yanayoendelea!
Utasombwa tu na kimbunga nyang'au wahead
Chadema mnajitahidi sana kupotosha ili gaidi asifungwe lakini hamtafanikiwa.

Denis Urio alipewa ruhusa na DCI aendelee kusbirikiana na Mbowe ili mradi tu awe anatoa taarifa ya kila kitu kinachoendelea.we
 
Mbona ameshindwa kuthibitisha?
wewe ndio unasema ameshindwa, lakini wenye kesi wanajua kwanini wamemleta, ili aje aunganishe dot kwenye ushahidi wa yupi ambaye labda ameshatoa ushahidi au anakuja kutoa ushahidi baada yake. ndio maana tunasema msubiri hadi kesi iishe. msikurupuke.
 
Chadema mnajitahidi sana kupotosha ili gaidi asifungwe lakini hamtafanikiwa.

Denis Urio alipewa ruhusa na DCI aendelee kusbirikiana na Mbowe ili mradi tu awe anatoa taarifa ya kila kitu kinachoendelea.
Kosa la hao vijana watatu liko wapi sasa au unaropoka tu na wewe
 
Chadema mnajitahidi sana kupotosha ili gaidi asifungwe lakini hamtafanikiwa.

Denis Urio alipewa ruhusa na DCI aendelee kusbirikiana na Mbowe ili mradi tu awe anatoa taarifa ya kila kitu kinachoendelea.
Hapa hakuna upotoshaji hadi hapa hii kesi ilipofikia ishabuma... akili zako nadhani ni finyu sana na mmefail pakubwa shame upon you viazi wa ccm
 
Shida mnakuja hapa na kujifanya mnajua kumbe wasindikizaji tu. unafikiri kweli jeshi halina taarifa za kutosha na mtu wao hadi anakuja kutoa ushahidi? pia, tuchukulie mfano, Mbowe ambaye alikuwa anamwita urio "homeboy", ameamua kuingia kwake ili amtafutie walinzi na akaamua kumshirikisha huyo homeboy wake uovu anaotaka kuufanya akijua kwamba urio hatamsaliti kwasababu wametoka mbali na ni homeboy, urio akafikisha taarifa ile kwa wakubwa zake, lazima wakubwa zake watamwelekeza akende polisi, na akifika polisi lazima tu watamwambia "ili tumpate mbowe na uovu anaouwaza, jifanye kushirikiana naye".

Hapo watashirikiana hadi kuwapata hao walinzi na mambo yote yaliyoendelea mbowe akiamini kuwa urio yupo upande wake kumbe mwenzake ameshakuwa pandikizi. kumbuka kuwa hayo mambo ua uovu lazima yalikuwepo kitambo na serikali ilikuwa inatafuta namna ya kureveal kupata ushahidi. mbowe akaingia king...na ndio yupo hapo anashangaashangaa tu anatokaje, anasubiri tu huruma za wananchi na serikali. ukweli halisi anaujua mbowe, na Mungu anamuona.
Lakin kwa ushahidi unaoendelea kutolewa mahakamani naona bado hautoshi kumfanya Mbowe aonekane Gaidi, labda tusubiri huko mbele
 
Shida mnakuja hapa na kujifanya mnajua kumbe wasindikizaji tu. unafikiri kweli jeshi halina taarifa za kutosha na mtu wao hadi anakuja kutoa ushahidi? pia, tuchukulie mfano, Mbowe ambaye alikuwa anamwita urio "homeboy", ameamua kuingia kwake ili amtafutie walinzi na akaamua kumshirikisha huyo homeboy wake uovu anaotaka kuufanya akijua kwamba urio hatamsaliti kwasababu wametoka mbali na ni homeboy, urio akafikisha taarifa ile kwa wakubwa zake, lazima wakubwa zake watamwelekeza akende polisi, na akifika polisi lazima tu watamwambia "ili tumpate mbowe na uovu anaouwaza, jifanye kushirikiana naye".

Hapo watashirikiana hadi kuwapata hao walinzi na mambo yote yaliyoendelea mbowe akiamini kuwa urio yupo upande wake kumbe mwenzake ameshakuwa pandikizi. kumbuka kuwa hayo mambo ua uovu lazima yalikuwepo kitambo na serikali ilikuwa inatafuta namna ya kureveal kupata ushahidi. mbowe akaingia king...na ndio yupo hapo anashangaashangaa tu anatokaje, anasubiri tu huruma za wananchi na serikali. ukweli halisi anaujua mbowe, na Mungu anamuona.
Wewe ndo maana inaitwa Chapwa naona unachapwa sana na akili zako za ...
 
Lakin kwa ushahidi unaoendelea kutolewa mahakamani naona bado hautoshi kumfanya Mbowe aonekane Gaidi, labda tusubiri huko mbele
nitacheka sana siku nikija kugundua kuwa co-accuseds na urio wote walikuwa na lao moja, kumkamatisha mbowe aliyekuwa na uchu wa kufanya uovu. na mbowe pale alipo anaweza kuwa anaamini wale wenzie ni wenzie. na chadema wanawatetea kwelikweli. jueni hao ni makombandoo. au hamuelewi?
 
nitacheka sana siku nikija kugundua kuwa co-accuseds na urio wote walikuwa na lao moja, kumkamatisha mbowe aliyekuwa na uchu wa kufanya uovu. na mbowe pale alipo anaweza kuwa anaamini wale wenzie ni wenzie. na chadema wanawatetea kwelikweli. jueni hao ni makombandoo. au hamuelewi?
Sio rahis hivyo boss, Trust me. Kumbuka Chadema na Mbowe walikuwa na nafasi ya kuongea na Serikali kulimaliza hili km Zitto alivyolianzisha lakin wakakataa kabisa, so tusitumie hisia ngoja tusubiri mwisho wake.
 
Chadema mnajitahidi sana kupotosha ili gaidi asifungwe lakini hamtafanikiwa.

Denis Urio alipewa ruhusa na DCI aendelee kusbirikiana na Mbowe ili mradi tu awe anatoa taarifa ya kila kitu kinachoendelea.
Tahira kwa kwangu cha huu DCI na Chain of command ya jeshi wapi na wapi
 
Back
Top Bottom