Kabla ya kumkosoa Rais Samia, tumuombe radhi kwanza Hayati Mkapa na familia yake na washauri wake

Kabla ya kumkosoa Rais Samia, tumuombe radhi kwanza Hayati Mkapa na familia yake na washauri wake

Saga la NBC in the long run limeiyumbisha sana Tanzania kuliko tunavyoweza kufikiri hasa kiuchumi.
Ilikua ni matakwa ya IMF kuiua NBC ili sekta binafsi ya kibenki iweze furukuta lakini kilichoipata NBC leo hamna mpambe anataka kizungumzia. Sekta ya benki imekua Yes... je implication yake kwa uchumi wa nchi ikoje ukilinganisha na nguvu ya NBC ya wakati ule? Je why benki nyingine zisingekuja kupambana na NBC?

Mkapa amekiri mara nyingi hadharani na kwenye kitabu chake kuwa ubinafsishaji kwa sehemu kubwa alikosea maana 80% ya mashirika ya umma yaliingia mifukoni mwa matapeli!

Hoja zile sile waliosimamia watu juu ya uwezo na aina ya mikataba ya hovyo ya ubinafsishaji ndizo zilikuja kuonekana wazi kweli waliopinga walikua na hoja tena kubwa sana.

Vipi NET group Solutions? ATCL? TRL?
Meremeta? Na mengine?

Shida yetu kubwa tunakimbilia sana kwenye petty issues when it comes to analysis

Mfano huu mkataba wa Tanzania na DP World ni wa hovyo usioelezeka! Hoja si kubinafsisha bandari Hoja ni mkataba wa hovyo!

Madini hadi leo yametufikisha wapi ukitulinganisha na Botswana na SA? Mbona kwao pia kuna sector binafsi?
HOJA sio ubinafsishaji hoja aina ya mikataba ya kishenzi ambayo nchi zetu zinaingia.
Mbona unachanganya mambo mazee?Net solutions hawakuja kui improve Tanesco walikuja kuleta mapendekezo na kuiandaa kuiuza..
Net solutions wwalifanikiwa Kwa mfano kukusanya madeni yote ya serikali ingawa Kwa mujibu wa mkataba hawakuruhusiwa kufanya investment za Ku improve Tanesco.. Mkataba ulikuwa kuandaa mazingira ya Ku li privatise kitu ambacho baadae kikawa canceled..

Naona unalazimisha mifano ya ATCL..hutaki mifano ya TBL ,wala hutaki kukubali sehemu ya mabadiliko ya kuuza NBC ilizalisha NMB..bank kubwa kuliko zote Tz ambayo inamilikiwa na watanzania na Serikali asilimia 70...
NBC isingeweza kushindana na mabenki binafsi...
Mbona husemi jinsi Benki zingine za Serikali zilivyofilisika juzi tu?
TIB?
Tanzania womens Bank?
Twiga bank??
 
Sisi wengine tulikuwepo wakati Rais Mkapa (1995-2005)anatukanwa kila siku kuwa "anauza nchi Kwa makaburu".....ilifikia wakati hadi nyimbo zilitungwa zikimuimba naukumbuka wimbo mmoja .."Kama sio juhudi zako Nyerere, Mkapa angeuza nini"???..Mkapa alikuwa anatukanwa kisa ni kuleta wawekezaji wa kampuni zisizo zaidi tano kutoka Afrika kusini..
Walikuja kuwekeza
1.TBL
2.. NBC
Zingine nimezisahau....Leo...

Uwekezaji wa NBC ulipelekea Serikali kuanzisha NMB ambayo nayo waliletwa Waholanzi kununua hisa zisizozidi asilimia 5..waka provide management baadae waholanzi wale wakashangaa jinsi soko lilivyo kubwa wakaomba kununua hisa zaidi now nasikia ni asilimia 25..

Mabadiliko ya sekta nzima ya Benki aliyoyasimamia Rais Mkapa kipindi kile Leo yamepelekea tuwe na sector ya bank kubwa inayofanya kazi Kwa ufanisi...

NMB Leo ni kubwa kuliko Zanzibar GDP..na bank zote 3 kubwa Tanzania.. NMB, NBC na Crdb ni kubwa kuliko Uchumi wa Burundi...

Haya yote yasingewekana kama Rais Mkapa angeogopa "kuitwa fisadi anaeuza nchi Kwa Makaburu"...kipindi kile usingeweza kumuelewa Mkapa ...since watu waliokuwa wanaompinga walikuwa Wana influence ya kutosha ..tukianzia na Mwl Nyerere.....Na Magazeti ya Jenerali Ulimwengu yaliyokuwa Yana influence kubwa Sana Kwa jamii ya wasomi na wakosoaji wakubwa..... ungeweza fikiri nchi inauzwa kweli ukifatilia mijadala...

Leo hizo banks zote 3.. NMB na Crdb zinamilkiwa na watanzania asilimia 70 NBC pia Serikali bado ina hisa za kutosha na zote hizo serikali inapokea gawio la kutosha...wale waliokuwa wanasema Mkapa anauza nchi Kwa makaburu wamenyamaza kiimya na sasa wamehamia kwenye "Samia anauza nchi Kwa waarabu" as if nothing happened...wala hawajawi jiuliza walichokuwa wanapinga kipindi kile na Hali ikoje leo? Walikuwa sahihi??

Kama hawakuwa sahihi kwanini wasiombe hata radhi in public hapo hata waliokuwa washauri wa Mkapa ambao bado wako hai wafarijike??...kama Mkapa aliuza nchi Kwa makaburu, hii nchi wanayosema anauza Samia ni ipi tena??

Itoshe kusema TBL ilienda kuwa kampuni inayolipa Kodi kubwa kuliko kampuni zote Tanzania Kwa miaka mingi Sana kama sio mpaka Leo ninavyoandika hapa....lakini shukran pekee aliyoambulia Rais Mkapa ni kuitwa "fisadi anaeuza nchi Kwa makaburu"...

Na wale watukanaji wakubwa Hadi Leo hawajawi kusema "hatukuwa sahihi" tulikosea ...Sana Sana wamevamia basi jipya "la Samia anauza nchi Kwa waarabu" Kwa nguvu mpyaa kabisa ...wazungu wanasema "ignorance is bliss"..

Mtu mjinga ana faida ya kutojijua ujinga wake...anaweza ita hata watu werevu wajinga hadharani bila woga...'ignorance is bliss ".....ungemueleza nini Mtanzania wa kawaida kuwa Mwalimu Nyerere hayuko sahihi ..wakati CEO wa Crdb wakati ule anaenda Hadi Butiama kumuomba Nyerere anunue hata hisa kidogo za Crdb kama kushawishi jamii iamke na Ku embrace"mabadiliko ya uchumi "na Nyerere ananjibu waziwazi mbele ya Tv kuwa hakuna cha mabadiliko wala nini ..ni ubepari na wizi tu kubinafsisha mabenki"...

Kwa watanzania Wengi Nyerere ni close to God ... hawezi kuwa hayuko sahihi..huwa najiuliza kama kipindi kile mwaka 1996 kama Babu yangu angekuwa na Uwezo mdogo Tu na akanunua hisa nyingi Crdb mwaka 1996 mfano hisa zenye thamani ya hata ya milioni 2 mwaka 1996 Leo ingekuwa ni utajiri kiasi gani?but watanzania Wengi hawakuwa na uelewa na waliokuwa wanaopinga mabadiliko ndo hao kina Nyerere na Rais anaeongoza mabadiliko anatukanwa kama "anauza nchi Kwa makaburu"...miaka 17 later ... tunamtukana Rais Kwa kuleta nchini moja ya kampuni 3 kubwa duniani Kwa shughuli za Bandari... Dpworld... kampuni imewekeza kuanzia China Hadi USA Kwa mabingwa wenyewe wa uwekezaji..Hadi Kwa wajerumani mabingwa wa ubaguzi duniani......

Kampuni CEO mmarekani lakini tunaambiwa inakuja "kueneza Uislam"... kampuni imewekeza UK lakini tunaambiwa huko kote imewekeza "fair " Ila kwetu ndo "imeuziwa nchi"...hata serikali inaposema mkataba wa uwekezaji bado kusainiwa hatutaki kuelewa...

Watu unao fikiri Wana uelewa wanatokwa na mapovu kuongea with certain "hatari kubwa Sana " iliyo mbele yetu akija "huyu mwarabu"...na wimbo mpya wa Samia anauza nchi Kwa waarabu ndo unazidi kupandishwa chati Kwa nguvu kubwa... maandamano uchwara yanachochewa na Viongozi wa dini ambao unajiuliza ni Bandari tu au kuna agenda ingine??

The more things change the more they stay the same....
Walio muita Mkapa fisadi anaeuza nchi Kwa makaburu..sasa wanafanya miamala banks zile zile na pengine kununua hisa na kunywa Safari lager huku washasahau "matusi " yote waliyomtwisha Mzee Mkapa...angalau wajitokeze waombe radhi japo hata washauri wa Mzee Mkapa wafarijike...kabla hawajapanda hili basi lingine la "Samia anauza nchi Kwa waarabu"...

Pengine wanaweza wasiwe hai ikitokea haya yote yanayozungumwa Leo yakathibitika kuwa ni uzushi , upumbavu na propaganda za wanasiasa wanaotaka Mama Samia "awapishe kwenye kiti mapema".....ili waombe radhi...Bora kwanza waombe radhi hili la Mkapa ambalo limethibitika bila Shaka kuwa "kelele za Mkapa kuuza nchi Kwa makaburu" ilikuwa uwongo, upumbavu,upeo mdogo kuhusu uchumi na uwekezaji na kudandia mabasi ya propaganda ambayo hujui dereva wake nani.....

...
Mabadiliko ya sekta nzima ya Benki aliyoyasimamia Rais Mkapa kipindi kile Leo yamepelekea tuwe na sector ya bank kubwa inayofanya kazi Kwa ufanisi ....

Maelezo yako ni sahihi kuwa uwekezaji una tija. Ninalopinga kuhusu Mkataba wa bandari ni kampuni ya DPW kuwekeza kupitia mgongo wa nchi yao, Dubai. Mkataba wa IGA, una vifungu vinavyoipa DPW hadhi ya nchi.

Kwa kuwa DPW ina uwezo na uzoefu wa kuendesha bandari, tayari tarehe 28/2/2022 ilikuwa imeingia Mkataba wa Maelewano (Mou) na TPA. Haingii akilini kwa nini DPW haikuendelea na mpango huo, ikajisajiri BRELA kuanza kazi kwa kushirikiana na TPA, badala ya kulazimu Tanzania iingie Mkataba na Dubai, nchi yake, wenye masharti tata km Ibara ya 5(1,4)? Nia ya IGA ni nini wakati kuna makampuni mengi tu km ubinafsishaji wa mabenki wakati wa Mkapa na makampuni ya uchimbaji madini, ambayo naamini hakuna mikataba kati ya Tanzania na nchi zao, kwa kuwa tuna mahusiano ya kidemokrasia.
 
Sisi wengine tulikuwepo wakati Rais Mkapa (1995-2005)anatukanwa kila siku kuwa "anauza nchi Kwa makaburu".....ilifikia wakati hadi nyimbo zilitungwa zikimuimba naukumbuka wimbo mmoja .."Kama sio juhudi zako Nyerere, Mkapa angeuza nini"???..Mkapa alikuwa anatukanwa kisa ni kuleta wawekezaji wa kampuni zisizo zaidi tano kutoka Afrika kusini..
Walikuja kuwekeza
1.TBL
2.. NBC
Zingine nimezisahau....Leo...

Uwekezaji wa NBC ulipelekea Serikali kuanzisha NMB ambayo nayo waliletwa Waholanzi kununua hisa zisizozidi asilimia 5..waka provide management baadae waholanzi wale wakashangaa jinsi soko lilivyo kubwa wakaomba kununua hisa zaidi now nasikia ni asilimia 25..

Mabadiliko ya sekta nzima ya Benki aliyoyasimamia Rais Mkapa kipindi kile Leo yamepelekea tuwe na sector ya bank kubwa inayofanya kazi Kwa ufanisi...

NMB Leo ni kubwa kuliko Zanzibar GDP..na bank zote 3 kubwa Tanzania.. NMB, NBC na Crdb ni kubwa kuliko Uchumi wa Burundi...

Haya yote yasingewekana kama Rais Mkapa angeogopa "kuitwa fisadi anaeuza nchi Kwa Makaburu"...kipindi kile usingeweza kumuelewa Mkapa ...since watu waliokuwa wanaompinga walikuwa Wana influence ya kutosha ..tukianzia na Mwl Nyerere.....Na Magazeti ya Jenerali Ulimwengu yaliyokuwa Yana influence kubwa Sana Kwa jamii ya wasomi na wakosoaji wakubwa..... ungeweza fikiri nchi inauzwa kweli ukifatilia mijadala...

Leo hizo banks zote 3.. NMB na Crdb zinamilkiwa na watanzania asilimia 70 NBC pia Serikali bado ina hisa za kutosha na zote hizo serikali inapokea gawio la kutosha...wale waliokuwa wanasema Mkapa anauza nchi Kwa makaburu wamenyamaza kiimya na sasa wamehamia kwenye "Samia anauza nchi Kwa waarabu" as if nothing happened...wala hawajawi jiuliza walichokuwa wanapinga kipindi kile na Hali ikoje leo? Walikuwa sahihi??

Kama hawakuwa sahihi kwanini wasiombe hata radhi in public hapo hata waliokuwa washauri wa Mkapa ambao bado wako hai wafarijike??...kama Mkapa aliuza nchi Kwa makaburu, hii nchi wanayosema anauza Samia ni ipi tena??

Itoshe kusema TBL ilienda kuwa kampuni inayolipa Kodi kubwa kuliko kampuni zote Tanzania Kwa miaka mingi Sana kama sio mpaka Leo ninavyoandika hapa....lakini shukran pekee aliyoambulia Rais Mkapa ni kuitwa "fisadi anaeuza nchi Kwa makaburu"...

Na wale watukanaji wakubwa Hadi Leo hawajawi kusema "hatukuwa sahihi" tulikosea ...Sana Sana wamevamia basi jipya "la Samia anauza nchi Kwa waarabu" Kwa nguvu mpyaa kabisa ...wazungu wanasema "ignorance is bliss"..

Mtu mjinga ana faida ya kutojijua ujinga wake...anaweza ita hata watu werevu wajinga hadharani bila woga...'ignorance is bliss ".....ungemueleza nini Mtanzania wa kawaida kuwa Mwalimu Nyerere hayuko sahihi ..wakati CEO wa Crdb wakati ule anaenda Hadi Butiama kumuomba Nyerere anunue hata hisa kidogo za Crdb kama kushawishi jamii iamke na Ku embrace"mabadiliko ya uchumi "na Nyerere ananjibu waziwazi mbele ya Tv kuwa hakuna cha mabadiliko wala nini ..ni ubepari na wizi tu kubinafsisha mabenki"...

Kwa watanzania Wengi Nyerere ni close to God ... hawezi kuwa hayuko sahihi..huwa najiuliza kama kipindi kile mwaka 1996 kama Babu yangu angekuwa na Uwezo mdogo Tu na akanunua hisa nyingi Crdb mwaka 1996 mfano hisa zenye thamani ya hata ya milioni 2 mwaka 1996 Leo ingekuwa ni utajiri kiasi gani?but watanzania Wengi hawakuwa na uelewa na waliokuwa wanaopinga mabadiliko ndo hao kina Nyerere na Rais anaeongoza mabadiliko anatukanwa kama "anauza nchi Kwa makaburu"...miaka 17 later ... tunamtukana Rais Kwa kuleta nchini moja ya kampuni 3 kubwa duniani Kwa shughuli za Bandari... Dpworld... kampuni imewekeza kuanzia China Hadi USA Kwa mabingwa wenyewe wa uwekezaji..Hadi Kwa wajerumani mabingwa wa ubaguzi duniani......

Kampuni CEO mmarekani lakini tunaambiwa inakuja "kueneza Uislam"... kampuni imewekeza UK lakini tunaambiwa huko kote imewekeza "fair " Ila kwetu ndo "imeuziwa nchi"...hata serikali inaposema mkataba wa uwekezaji bado kusainiwa hatutaki kuelewa...

Watu unao fikiri Wana uelewa wanatokwa na mapovu kuongea with certain "hatari kubwa Sana " iliyo mbele yetu akija "huyu mwarabu"...na wimbo mpya wa Samia anauza nchi Kwa waarabu ndo unazidi kupandishwa chati Kwa nguvu kubwa... maandamano uchwara yanachochewa na Viongozi wa dini ambao unajiuliza ni Bandari tu au kuna agenda ingine??

The more things change the more they stay the same....
Walio muita Mkapa fisadi anaeuza nchi Kwa makaburu..sasa wanafanya miamala banks zile zile na pengine kununua hisa na kunywa Safari lager huku washasahau "matusi " yote waliyomtwisha Mzee Mkapa...angalau wajitokeze waombe radhi japo hata washauri wa Mzee Mkapa wafarijike...kabla hawajapanda hili basi lingine la "Samia anauza nchi Kwa waarabu"...

Pengine wanaweza wasiwe hai ikitokea haya yote yanayozungumwa Leo yakathibitika kuwa ni uzushi , upumbavu na propaganda za wanasiasa wanaotaka Mama Samia "awapishe kwenye kiti mapema".....ili waombe radhi...Bora kwanza waombe radhi hili la Mkapa ambalo limethibitika bila Shaka kuwa "kelele za Mkapa kuuza nchi Kwa makaburu" ilikuwa uwongo, upumbavu,upeo mdogo kuhusu uchumi na uwekezaji na kudandia mabasi ya propaganda ambayo hujui dereva wake nani.....
Ubinafsishaji wa Mkapa huwezi kuulingabisha na uuzwaji wa Bandari! Mkataba wa ubinafsishaji ilikuwa na tija na ukomo kuliko huu wa DP WORLD
 
Ulipaswa kuorodhesha mashirika yote yaliyobinafsishwa na mkapa, alafu tuangalie mangapi yamefaulu na mangapi yamefeli. ndio hapo utapata jibu

Mkapa kwenye kitabu chake anakiri alifanya makosa kwenye ubinafsishaji wa mashirika, mengi yalikufa.
 
Ubinafsishaji wa Mkapa huwezi kuulingabisha na uuzwaji wa Bandari! Mkataba wa ubinafsishaji ilikuwa na tija na ukomo kuliko huu wa DP WORLD
Hata hivyo mashirika mengi yalikufa, hayo anayotolea mfani ni machache sana. 80% yalienda na maji, bahati nzuri mkapa aliandika kitabu na alikiri kukosea
 
Mfano huu mkataba wa Tanzania na DP World ni wa hovyo usioelezeka! Hoja si kubinafsisha bandari Hoja ni mkataba wa hovyo!

Madini hadi leo yametufikisha wapi ukitulinganisha na Botswana na SA? Mbona kwao pia kuna sector binafsi?
HOJA sio ubinafsishaji hoja aina ya mikataba ya kishenzi ambayo nchi zetu zinaingia.
Fact...
 
Mbona majibu yametoka..hukusikia?
Imesainiwa IGA.. intergovernmental agreement...Mkataba wa bandari lazima utakuwa na kikomo..na mda wa review utakapo sainiwa.. huelewi nini?Bunge limeridhia serikali iende kuingia mkataba.., mkataba halisi bado...
Mkuu so kikomo ikiwa miaka 100 ni mfano tu, utakuwa mkataba mzuri? Kha mbona vigumu sana kuamini.

Udini upo hilo lipo wazi but process nzima ya uwezekaji sio kabisaaaa.

Kwani nini kila uwekezaji ni wao waarabu?

Tunaogopa kugeuzwa watumwa ndani ya nchi yetu…
 
Mnaotoa.Maelezo mengi ya kutetea uzuzu.Wa Samia mnanikera sana. Kwa kifupi hatutaki bandari wachukue hata mkataba ningeletewa.Mimi..ningewauliza je. ni.win win situation hamsini.kwa hamsini.tofauti na.hapo welcome. again
nilisoma historian.ya.Suez.canal. inasikitisha.hawa.mabeberu.wanatuona.kama kama.hatuna.ubongo.vile
 
Mbona unachanganya mambo mazee?Net solutions hawakuja kui improve Tanesco walikuja kuleta mapendekezo na kuiandaa kuiuza..
Net solutions wwalifanikiwa Kwa mfano kukusanya madeni yote ya serikali ingawa Kwa mujibu wa mkataba hawakuruhusiwa kufanya investment za Ku improve Tanesco.. Mkataba ulikuwa kuandaa mazingira ya Ku li privatise kitu ambacho baadae kikawa canceled..

Naona unalazimisha mifano ya ATCL..hutaki mifano ya TBL ,wala hutaki kukubali sehemu ya mabadiliko ya kuuza NBC ilizalisha NMB..bank kubwa kuliko zote Tz ambayo inamilikiwa na watanzania na Serikali asilimia 70...
NBC isingeweza kushindana na mabenki binafsi...
Mbona husemi jinsi Benki zingine za Serikali zilivyofilisika juzi tu?
TIB?
Tanzania womens Bank?
Twiga bank??
Nimesema pale juu, kuboresha
Mbona unachanganya mambo mazee?Net solutions hawakuja kui improve Tanesco walikuja kuleta mapendekezo na kuiandaa kuiuza..
Net solutions wwalifanikiwa Kwa mfano kukusanya madeni yote ya serikali ingawa Kwa mujibu wa mkataba hawakuruhusiwa kufanya investment za Ku improve Tanesco.. Mkataba ulikuwa kuandaa mazingira ya Ku li privatise kitu ambacho baadae kikawa canceled..

Naona unalazimisha mifano ya ATCL..hutaki mifano ya TBL ,wala hutaki kukubali sehemu ya mabadiliko ya kuuza NBC ilizalisha NMB..bank kubwa kuliko zote Tz ambayo inamilikiwa na watanzania na Serikali asilimia 70...
NBC isingeweza kushindana na mabenki binafsi...
Mbona husemi jinsi Benki zingine za Serikali zilivyofilisika juzi tu?
TIB?
Tanzania womens Bank?
Twiga bank??
Weka kumbukumbu zako sawa... NMB haikuzaliwa kwa kuuza NBC! NmB ilizaliwa kwa kuivunja NBC kisha kuiuza.

Pili hao TBL waliwahi zalisha hasara huko nyuma? TBL serikali iliuza hisa ngapi? Unafuu gani ulipatikana baada ya kuuza TBL? unafahamu TBL,KILOMBERO, NBC, Mkonge ni mashirika yaliuzwa yakiwa yanafanya vizuri sana?
Kwanini unataka tu nijadili ya TBL hutaki ya STAMICO, TRL, NET GROUP SOLUTIONS, MEREMETA, ATCL na mengine? Why unachagua upande?

Mbona SGR, Stiglers Gorge hamkutaka wawekezaji?

Kwani tusingeweza kopa pesa kuboresha bandari zetu? Sawa anapewa mbia kwa mkataba huu wa kishenzi namna hii?

Nimesema pale juu kupata mbia wa kuboresha bandari sio shida, shida ni kuliwa,!!

Mkataba wa DP world na TZ ni wa kishenzi kuliko aliouingia chief Mangungo shida iko hapo.
 
Maelezo yako ni sahihi kuwa uwekezaji una tija. Ninalopinga kuhusu Mkataba wa bandari ni kampuni ya DPW kuwekeza kupitia mgongo wa nchi yao, Dubai. Mkataba wa IGA, una vifungu vinavyoipa DPW hadhi ya nchi.

Kwa kuwa DPW ina uwezo na uzoefu wa kuendesha bandari, tayari tarehe 28/2/2022 ilikuwa imeingia Mkataba wa Maelewano (Mou) na TPA. Haingii akilini kwa nini DPW haikuendelea na mpango huo, ikajisajiri BRELA kuanza kazi kwa kushirikiana na TPA, badala ya kulazimu Tanzania iingie Mkataba na Dubai, nchi yake, wenye masharti tata km Ibara ya 5(1,4)? Nia ya IGA ni nini wakati kuna makampuni mengi tu km ubinafsishaji wa mabenki wakati wa Mkapa na makampuni ya uchimbaji madini, ambayo naamini hakuna mikataba kati ya Tanzania na nchi zao, kwa kuwa tuna mahusiano ya kidemokrasia.
Watanzania wengi wana uelewa wa chini sana! Wapambe wengi wanafikiri shida ni DP world kuendesha bandari ilhali hoja kinzani ni mashaka makubwa juu ya mkataba huo!
 
Ulipaswa kuorodhesha mashirika yote yaliyobinafsishwa na mkapa, alafu tuangalie mangapi yamefaulu na mangapi yamefeli. ndio hapo utapata jibu

Mkapa kwenye kitabu chake anakiri alifanya makosa kwenye ubinafsishaji wa mashirika, mengi yalikufa.
Yaliyofaulu ni yale yaliyouzwa ilhali yakizalisha faida kubwa sana sana yaliwapa faida wageni...

Yale yaliyokuwa choka mbaya yaliingia mifukoni mwa wajanja wakalala mbele imebaki historia.
 
Mbona majibu yametoka..hukusikia?
Imesainiwa IGA.. intergovernmental agreement...Mkataba wa bandari lazima utakuwa na kikomo..na mda wa review utakapo sainiwa.. huelewi nini?Bunge limeridhia serikali iende kuingia mkataba.., mkataba halisi bado...
Uko brainwashed sana!

Why inte government agreement na DP world ni kampuni kama zilivyo GGM?

Kumbuka kilichopitishwa na bunge ni kama sheria itakayosimama badala ya TPA act ya 2004. Yajayo hayatatoka nje ya hiki kinachopigiwa kelele leo.
 
Mtu mjinga ana faida ya kutojijua ujinga wake...anaweza ita hata watu werevu wajinga hadharani bila woga...'ignorance is bliss ".....ungemueleza nini Mtanzania wa kawaida kuwa Mwalimu Nyerere hayuko sahihi ..wakati CEO wa Crdb wakati ule anaenda Hadi Butiama kumuomba Nyerere anunue hata hisa kidogo za Crdb kama kushawishi jamii iamke na Ku embrace"mabadiliko ya uchumi "na Nyerere ananjibu waziwazi mbele ya Tv kuwa hakuna cha mabadiliko wala nini ..ni ubepari na wizi tu kubinafsisha mabenki"...
Umeandika mengi lakini sijui kwanini mnapenda kuwazuia watu kuwaza tofauti!
Madocuments si mliyaleta hadharani wenyewe? Sasa yanaposomwa kwanini hamtaki watu watoe mawazo yao hadharani?
NB:
1. Nchi hii Kuna matatizo ya msingi. Ubaguzi. Elimu duni... Maisha magumu. N.k. Stress ni kubwa. Ajabu hamtoi majibu zaidi ya kuwatukana wenye mawazo tofauti.
2. Kwenye uwekezaji umeamua kuelezea mazuri machache. Lakini ya ovyo mengi hujataja kabisa!
3. Ooh kumbe ni kweli. Mwl. JKN aliwakera ikabidi apewe maradhi.
4. So, tutarajie mtamtafuta mwekezaji aje aendeshe bunge? Make nalo haliperform vizuri.
 
Back
Top Bottom