Kabla ya maisha kuwapiga Watu wengi Knockout, wengi walifikiri wakifika miaka 30 wangekuwa na nyumba na Gari

Kabla ya maisha kuwapiga Watu wengi Knockout, wengi walifikiri wakifika miaka 30 wangekuwa na nyumba na Gari

Your very true, kwa mfano mimi nikitaka tuu kujiendeleza na elimu kama kazi ntapoteza kama biashara itakufa yaani hii napambana nayo zaidi ya miaka kumi inanisumbua.
Now maisha yangu nimeamua yawe autopilot coz nimekutana na fursa nyingi mno local na International lakini hamna hata moja zimenifikisha walau nusu au robo ya ndoto zangu nimebaki kusifiwa tuu nina akili ila sina bahati.

Inauma inauma saana aiseeh
Pole mkuu naelewa sometimes inauma sana pale unapokuwa na potential kubwa lakini haikufikishi unapopataka zaidi ya kupewa empty praises. Mungu afanye, take off yako iwezekane lakini pia kama, utaweza ni vyema kuongea na watu waliofanikiwa maana kama kuna kitu kinasumbua watu ambao wana akili sana ni kufuata certain patterns or formalities. Hopeful bro Ivan Stepanov ataongezea
 
Pole mkuu naelewa sometimes inauma sana pale unapokuwa na potential kubwa lakini haikufikishi unapopataka zaidi ya kupewa empty praises. Mungu afanye, take off yako iwezekane lakini pia kama, utaweza ni vyema kuongea na watu waliofanikiwa maana kama kuna kitu kinasumbua watu ambao wana akili sana ni kufuata certain patterns or formalities. Hopeful bro Ivan Stepanov ataongezea
Jamaa unanielewa saana nakushukuru
 
Habari za Jumapili!

Maisha sio Pouwa! Nakubaliana na wale wanaosema Maisha ni majaliwa. Na jitihada hazizidi kudura.

Wapo waliosoma kwa bidii mila hiyo na waliona taa ya matumaini kulingana na matokeo ya darasani waliyokuwa wakiyapata. Waliamini kuwa maisha yao na hatma yao ipo mikononi mwao kumbe sivyo.

Ilifika hatua wakawa wanadharau wale ambao walikuwa wanaonekana hawana mipango na mikakati kutokana na kutoipenda shule.

Wengi walifikiri kuwa kabla ya miaka 30 tayari wangekuwa wamekomesha jeuri na kiburi cha Umaskini katika maisha yao.
Tayari kichwani walikuwa na picha za jumba kubwa la kifahari ambalo walijua ndio watakayoishi. Bongo zao zilishakuwa na miundombinu ya flyover ambapo gari yao ilikuwa ikipita juu yake huku ndani akiwa yeye na Pisikali moja matata ambayo ndio mkewe.

Kwa wasichana, wao nao walikuwa na maisha yao mazuri katika vichwa vyao. Wanaume Handsome, warefu na wenye vipato na Watanashati walikuwa katika fikra zao.

Sasa miaka imekimbia, hawaelewi nini kimetokea. Matumaini yameyoyoma, ngumi ya matumpa upper cut moja matata imepiga kidevu vijana chali.
Hata zile ramani za majengo na magari walizokuwa nazo miaka hiyo zimefutika.

Yule Mwanamke mrembo akilini waliyemfikiria wangekuja kumuoa wanawaona kwenye magazeti, filamu na kwenye riwaya. Hakuna faraja tena, tumaini limeota mbawa. Wamejiunga kwenye chama cha faraja ya mpito cha Kataa Ndoa.
Hawakumbiki tena ndoto ya kuwa na familia bora baada ya kuyapata maisha mazuri yanayotamanika.
Ni Tekniko Knockout.

Hawakujua kuwa maisha yanakupa yale ambayo hujayaomba na yale ambayo huyataki. Tena maisha hukupa yale ambayo hukudhania kwamba ungekuwa nayo. Kwa sababu maisha ni Nasibu, maisha ni bahati tuu.

Sasa mipango imevurugwa na kuvurugika. Kila kitu pangala pangala! Hata kupanga hawataki kupanga tena. Hata wakisema wapange wanaona wanapoteza muda wao. Sasa ni bora liende túu! Wapo tayari kwa lolote na huo ndio mfumo wa maisha unavyotaka.

Mtu ambaye alipanga kabla ya miaka 30 awe na jumba na gari leo hii hata kodi ya chumba cha laki moja hawezi kuhimili. Unaweza kuona pigo alilopigwa ni zito kwa kiwango kipi.

Kijana, unapopanga mipango yako. Muombe Mungu

Suleiman aliwahi kusema;

Mhubiri 9:11 NEN​

Nimeona kitu kingine tena chini ya jua: Si wenye mbio washindao mashindano au wenye nguvu washindao vita, wala si wenye hekima wapatao chakula au wenye akili nyingi wapatao mali, wala wenye elimu wapatao upendeleo, lakini fursa huwapata wote.


Acha Nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
That's is life.... sometimes life give you what you didn't expect
 
Siyo sahihi kuaminisha watu kwamba wanaofanikiwa ni wale wa Mungu tu

Wakati na bahati huwapata wote

Na kuna maelfu ya walokole ni Masikini wa kutupwa

Kufanikiwa ni jitihada na bahati
Maandiko yanasema Mungu ndo humpa mtu nguvu za kupata utajiri...Na kuzielekeza hatua zake haimo katika uwezo wa mwanadamu
 
Sijui kwa watu wengine ila marafiki zangu wengi walioweza kufanya vizuri hadi chuo kikuu wengi zaidi hata ya 70% wana maisha mazuri kiuchumi. Vipanga karibu wote niliosoma nao wako njema. Na wale waliokuwa hawazingatii shule wengi wao hawako vizuri ni wachache waliobahatika kutoboa. Ingawa bahati zinahusika ila ni muhimu kupambana ili kama bahati itakuja ikukute uko tayari kwenda nayo sambamba. Kuna mdogo wangu alihitimu UDSM 2019 akakaa bila kazi hadi mwaka jana mwishoni bahati ya scholarship Ulaya ikamjia. Ile bahati ilikuja kwasababu dogo GPA yake ilikua safi na pia ni mtu mwenye nidhamu.
Nakubaliana na wewe, wote ambao tumefanikiwa kufika chuo kikuu tuko vizuri ulilinganisha na wale walioishia kidato cha tano. Wengi sasa hivi ni senior kwenye taasisi mbalimbali au wana mashirika yao. Elimu, connection vinasaidia sana kumvusha mtu.
 
Kuna kundi kubwa la vijana linasali na kumsifu huyo Mungu lakini bado maisha yao ni pangu pakavu tia mchuzi..

Hakuna mpango wa Mungu kwenye mafanikio ya binadamu.

Sera mbovu, siasa uchwara, mazingira ya rushwa, ujinga, elimu mbovu, serikali za hovyo ndio chanzo cha umaskini na ukosefu wa fursa kwa vijana wengi hasa barani Afrika.





Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
Niongezee tu na kuna kundi kubwa la vijana ulaya ambao ni wa ovyo ufuska na ujinga wote wanafanya wao ila wengi wao uishia kuwa na maisha mazuri sana sababu ni mfumo wa serikali zao unawawezesha kabisa..

Huku kwetu Sera mbovu, siasa uchwara, mazingira ya rushwa, ujinga, elimu mbovu, serikali za hovyo ndio chanzo cha umaskini na ukosefu wa fursa kwa vijana wengi hasa barani Afrika.
 
Nakubaliana na wewe, wote ambao tumefanikiwa kufika chuo kikuu tuko vizuri ulilinganisha na wale walioishia kidato cha tano. Wengi sasa hivi ni senior kwenye taasisi mbalimbali au wana mashirika yao. Elimu, connection vinasaidia sana kumvusha mtu.
Ni kweli. Watu huwa wanajipa moyo kipuuzi sana. Kwamba ambao hawakusoma huwa wanakuja mabosi wa wasomi. Sasa hivi hata huku kwenye biashara wanaokimbiza ni wasomi na kama sio msomi utakuta ni University drop out.
 
Life is not predictable.

Kikubwa fanya kazi kwa bidii na nidhamu ya pesa kuwa nayo.

Ukweli ni kwamba mtu anaekuja kukupa deal ni mtu mmoja tu na kupitia hapo unakuwa mtu mwingine tofauti kabisa kiuchumi
.
Hili nimejifunza kwa watu wangu wengi wa karibu walikuja kuinuliwa na watu

Hapa ndipo nilijifunza kwa udhiirisho kwamba mtu huinuliwa na mtu kupitia ukuu wa Mungu.


Hata mtu unae muona leo ana maisha mazuri ukifuatilia utakuta alikuwa kwnye harakati zake ghafla akatokea mtu akamshirikisha ndio ukawa mwanzo wa kutoka.

Kadhalika wahalifu nao hupiga tukio moja tu na kupitia hapo ndio mwanzo wa kutoka.

So pambana lift itakukuta njiani.
Hivyo vitu vya ghafla ni very rarely ila nathibitisha kabisa connection na mifumo mizuri ndio chachu ya maendelea kwa watu ndio maana kwa Tanzania vijana wengi wanaomba wapate kazi serikaliji huko kuna mfumo mzuri kwa watumishi hivyo walau kuleta unafuu wa maisha..
 
Maandiko yanasema Mungu ndo humpa mtu nguvu za kupata utajiri...Na kuzielekeza hatua zake haimo katika uwezo wa mwanadamu
Maandiko hayo ni hadithi za kutungwa sawa na Hekaya za Abunuwasi.

Maandiko hayo ni fiction stories hazina ukweli wala uhalisia wowote.

Ndio maana ume ambiwa hapo kuna walokole wengi wanajua hayo maandiko lakini kiuchumi ni maskini choka mbaya Höhehahe pangu pakavu tia mchuzi.
 
Back
Top Bottom