Kabla ya maisha kuwapiga Watu wengi Knockout, wengi walifikiri wakifika miaka 30 wangekuwa na nyumba na Gari

Kabla ya maisha kuwapiga Watu wengi Knockout, wengi walifikiri wakifika miaka 30 wangekuwa na nyumba na Gari

Ndio kikubwa uwe njiani tu usijifungie ndani maana mtu wa kukupa mchongo wa kutoka ni mmoja tu. Unakutana nae kwenye harakati zako tu.
Wewe hata kama humwamini Mungu wewe soma Biblia kama kujifunza maisha.

Ukiona kisa cha Musa kutokea na Mungu akiwa pembezoni mwa Bahari na kisha Mungu kumuuliza umeshika nini hapo nae kujibu nina fimbo na Mungu akamwabia piga hayo maji

Wana wa Israel uwavushe.

Hili ni somo kubwa

Ili bahati ikukute lazima kuna mazingira unatakiwa uyatengeneze na kuna namna ya kuwa.
 
Mkuu mbona naelewa sana? Kweli unaniweka kwenye kundi la watu wasiojua changamoto za kulipa kodi? Nilichopinga mimi ni watu kuona kama ndiyo kielelezo cha mafanikio. Yaani nakubali kuwa ni mafanikio lakini siyo kama ndiyo umemaliza kila kitu. Je, utakubaliana na mimi kuwa mtu akiwa na utajiri mkubwa, unaweza kuishi kwenye nyumba za kupanga maisha yako yote na akahesabika ana mafanikio kuliko mtu mwenye nyumba na hana fedha? Kipi ni mafanikio sasa, nyumba au utajiri?
Utajiri ni muhimu na unakupa uhuru wa kuishi popote. Sea wengi wetu maisha ya bongo tunaitafta susbsistence tu. Upate kula na kulala pazuri. Mengine yatajiongeza tu mkuu as long as unalala na kuamkia kwako.
 
Neno lako sio sheria
Kuna sehemu nimetaja maneno yangu ni sheria au unapachika vikolombwezo vyako?

Kama ulivyo mtazamo wako kwamba Mungu ndiye mpangaji wa maisha ya watu, Vivyo hivyo na mimi mtazamo wangu mungu huyo siyo mpangaji wa maisha ya binadamu.

Sasa ninyi mnachojaribu kufanya ni kuhalalisha dhana ya huyo Mungu wenu kwamba ndio mpangaji wa maisha ya kila mtu hapa duniani kumbe ni Uongo mtupu.
 
Life is not predictable.

Kikubwa fanya kazi kwa bidii na nidhamu ya pesa kuwa nayo.

Ukweli ni kwamba mtu anaekuja kukupa deal ni mtu mmoja tu na kupitia hapo unakuwa mtu mwingine tofauti kabisa kiuchumi
.
Hili nimejifunza kwa watu wangu wengi wa karibu walikuja kuinuliwa na watu

Hapa ndipo nilijifunza kwa udhiirisho kwamba mtu huinuliwa na mtu kupitia ukuu wa Mungu.


Hata mtu unae muona leo ana maisha mazuri ukifuatilia utakuta alikuwa kwnye harakati zake ghafla akatokea mtu akamshirikisha ndio ukawa mwanzo wa kutoka.

Kadhalika wahalifu nao hupiga tukio moja tu na kupitia hapo ndio mwanzo wa kutoka.

So pambana lift itakukuta njiani.
Kabisa mkuu 👏🏾👏🏾👏🏾👏🏾

Unaweza pambana sana ila kama hujapata mtu wa kukupeleka kwenye next level, uwezekano wa kubaki hapo hapo ni mkubwa

Japo, unaweza kutengeneza mazingira ya kukutana na hao watu ila uamuzi bado utakuwa ni wao katika kupiga push 👏🏾👏🏾
 
Watu wengi hawaamini Mungu na wana maisha mazuri tu , na kuna wanaoamini nakusali ila wamepigika vibaya sana .
Hasa hawa wanao jifanya kumtaja taja Mungu hapa kwenye huu uzi ndio life limewachapa vibaya mno.

Wako hapa kujifariji na umaskini wao kwamba ni mipango ya Mungu kwamba huenda kuna siku watafanikiwa.

Wanajifariji na fictional character Mungu...😄

Mtu yeyote anaye amini mafanikio ni "kudra za mwenyezi Mungu" huyo ni maskini wa akili na mali.

Hata akikosa kufanikiwa katika jambo fulani ata amini ni mungu ndiye kafanya hivyo kumbe ni mipango yake mibovu.
 
Habari za Jumapili!

Maisha sio Pouwa! Nakubaliana na wale wanaosema Maisha ni majaliwa. Na jitihada hazizidi kudura.

Wapo waliosoma kwa bidii mila hiyo na waliona taa ya matumaini kulingana na matokeo ya darasani waliyokuwa wakiyapata. Waliamini kuwa maisha yao na hatma yao ipo mikononi mwao kumbe sivyo.

Ilifika hatua wakawa wanadharau wale ambao walikuwa wanaonekana hawana mipango na mikakati kutokana na kutoipenda shule.

Wengi walifikiri kuwa kabla ya miaka 30 tayari wangekuwa wamekomesha jeuri na kiburi cha Umaskini katika maisha yao.
Tayari kichwani walikuwa na picha za jumba kubwa la kifahari ambalo walijua ndio watakayoishi. Bongo zao zilishakuwa na miundombinu ya flyover ambapo gari yao ilikuwa ikipita juu yake huku ndani akiwa yeye na Pisikali moja matata ambayo ndio mkewe.

Kwa wasichana, wao nao walikuwa na maisha yao mazuri katika vichwa vyao. Wanaume Handsome, warefu na wenye vipato na Watanashati walikuwa katika fikra zao.

Sasa miaka imekimbia, hawaelewi nini kimetokea. Matumaini yameyoyoma, ngumi ya matumpa upper cut moja matata imepiga kidevu vijana chali.
Hata zile ramani za majengo na magari walizokuwa nazo miaka hiyo zimefutika.

Yule Mwanamke mrembo akilini waliyemfikiria wangekuja kumuoa wanawaona kwenye magazeti, filamu na kwenye riwaya. Hakuna faraja tena, tumaini limeota mbawa. Wamejiunga kwenye chama cha faraja ya mpito cha Kataa Ndoa.
Hawakumbiki tena ndoto ya kuwa na familia bora baada ya kuyapata maisha mazuri yanayotamanika.
Ni Tekniko Knockout.

Hawakujua kuwa maisha yanakupa yale ambayo hujayaomba na yale ambayo huyataki. Tena maisha hukupa yale ambayo hukudhania kwamba ungekuwa nayo. Kwa sababu maisha ni Nasibu, maisha ni bahati tuu.

Sasa mipango imevurugwa na kuvurugika. Kila kitu pangala pangala! Hata kupanga hawataki kupanga tena. Hata wakisema wapange wanaona wanapoteza muda wao. Sasa ni bora liende túu! Wapo tayari kwa lolote na huo ndio mfumo wa maisha unavyotaka.

Mtu ambaye alipanga kabla ya miaka 30 awe na jumba na gari leo hii hata kodi ya chumba cha laki moja hawezi kuhimili. Unaweza kuona pigo alilopigwa ni zito kwa kiwango kipi.

Kijana, unapopanga mipango yako. Muombe Mungu

Suleiman aliwahi kusema;

Mhubiri 9:11 NEN​

Nimeona kitu kingine tena chini ya jua: Si wenye mbio washindao mashindano au wenye nguvu washindao vita, wala si wenye hekima wapatao chakula au wenye akili nyingi wapatao mali, wala wenye elimu wapatao upendeleo, lakini fursa huwapata wote.


Acha Nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kwa ninachokijua mimi mpaka sasa...mafanikio ni jambo pana sana...kuwa na nyumba na gari ni sehemu tu ya mafanikio...wapo wenye magari na nyumba lkn hawana watoto, wapo wenye magari na mali nyingine nyingi, ila wanaumwa...wapo wenye watoto wengi na familia zenye furaha ila hawana hayo magari na huenda wamepanga.
Nadhani tafsiri sahihi ya mafanikio ilenge eneo husika...e.g mafanikio kielemu, mafanikio kifedha, mafanikio kwenye mahusiano na kufanikiwa ktk eneo moja kati ya hayo, haina maana kuwa utafanikiwa ktk eneo jingine.
 
Mambo ya kumuomba we inakuuma nini
We siumesema hakuna Mungu sasa unachukizwa nini ukisikia mtu anasema anamuomba Mungu

Watu tumefanikiwa sababu ya Mungu na ushuhuda tunao aya kasirika
Na wewe unayejua Mungu huyo yupo, ina kuuma nini ukisikia nimesema hayupo?

Hata mimi nimefanikiwa pasipo msaada wowote wa huyo Mungu.
 
Hasa hawa wanao jifanya kumtaja taja Mungu hapa kwenye huu uzi ndio life limewachapa vibaya mno.

Wako hapa kujifariji na umaskini wao kwamba ni mipango ya Mungu kwamba huenda kuna siku watafanikiwa.

Wanajifariji na fictional character Mungu...😄

Mtu yeyote anaye amini mafanikio ni "kudra za mwenyezi Mungu" huyo ni maskini wa akili na mali.

Hata akikosa kufanikiwa katika jambo fulani ata amini ni mungu ndiye kafanya hivyo kumbe ni mipango yake mibovu.
Sure
 
Na wewe unayejua Mungu huyo yupo, ina kuuma nini ukisikia nimesema hayupo?

Hata mimi nimefanikiwa pasipo msaada wowote wa huyo Mungu.
Mimi hainiumi wewe kusema hakuna Mungu
Ila tofauti yangu mimi na wewe ni kwamba mtu akisema hamna Mungu simshambulii

We sasa mtu akisema Mungu yupo unakua mbogo
 
Hakuna mjanja wa kuchora fate yangu mimi.
am the only one to do that.
Mungu mwenyewe hafanyi hicho kitu.
Mungu anamuwazia mema kila mtu, na mpango wake ni kila mtu afanikiwe na aishi maisha bora yanayo reflect viwango vya utukufu wake.

Ila sasa ,bad news ni kwamba, Mungu anawapa watu wooote same ground ya kupambania ili kuyafikia mafanikio.

Pambana wewe.. Lala wewe. Hapo Mungu anakaa kando kuwaangalia wajuz wa kufuata principles and systems za ku unlock secretes of riches.

Success is predictable , so as Failure
Point.
 
Sikubaliani na hoja kuwa mipango ya kimaisha ya vijana wengi inaharibika kwasabb hawamhusishi ama hawamuombi Mungu. Wapo walokole ama mashekhe promax wamefika 50 bado hawana hata kitanda.

Kila mtu ana FATE yake, yaani Kila mtu kachorewa roadmap ya maisha yake na mwenyezi Mungu. Ndiyo maana akina Laizer wanaokota tanzanite yenye thamani ya mabilioni wakati wengine hata mia mbovu hamuokoti.
Roadmap ya mwanadamu iliyochorwa na Mungu, inawahusu wanadamu ambao wameji 'aline' kwenye mipango na makusudi ya Mungu.
Hawa ni binadamu adimu sana kupatikana katika kipindi hiki.
Wengi wetu, tunamfanya Mungu abadilishe mipango na makusudi yake kwetu kila wakati kutokana na kukosa msimamo thabiti.
Maana unapozaliwa, Mungu ana road map ya maisha Yako yote hapa duniani, utaenda na hii TU iwapo utatembea na Mungu maishani ukimtii Kwa kila jambo(hata kama halikuingii akilini.)
Pale utakapobadilika ukaenda kinyume na maagizo na maelekezo ya Mungu, roadmap hubadilika kutoka kwenye mipango ya maisha kuja mipango ya kukuokoa., na kinyume chake.
Hapo utaona wanadamu wengi (including walokole) tumekuwa hatuna stable roadmap sababu ya kuwa vuguvugu. Kila wakati tunabadilisha roadmap, na kumbuka kila inapobadilika unaanza upya.
Hapa utaona kwamba, watu rahisi kufanikiwa kupitia roadmap ya Mungu ni wale wasiokuwa na time kabisa na Mungu(ambapo Mungu anakuwa roadmap stable kwao akitafuta namna ya kuwarejesha kwake, na wengine ni wale (wachache sana) wanaomtii na kimfuata Mungu Kwa kila neno, ambapo wanapata stability Kwa Mungu katika kufanikisha mipango yao na hasa ya kumtumikia yeye.
 
Back
Top Bottom