Omba Mungu ,usiombe ,bila kuchakarika hauwezi fanikiwa kwa lolote.Mambo ya kumuomba we inakuuma nini
We siumesema hakuna Mungu sasa unachukizwa nini ukisikia mtu anasema anamuomba Mungu
Watu tumefanikiwa sababu ya Mungu na ushuhuda tunao aya kasirika
Wewe hata kama humwamini Mungu wewe soma Biblia kama kujifunza maisha.Ndio kikubwa uwe njiani tu usijifungie ndani maana mtu wa kukupa mchongo wa kutoka ni mmoja tu. Unakutana nae kwenye harakati zako tu.
Utajiri ni muhimu na unakupa uhuru wa kuishi popote. Sea wengi wetu maisha ya bongo tunaitafta susbsistence tu. Upate kula na kulala pazuri. Mengine yatajiongeza tu mkuu as long as unalala na kuamkia kwako.Mkuu mbona naelewa sana? Kweli unaniweka kwenye kundi la watu wasiojua changamoto za kulipa kodi? Nilichopinga mimi ni watu kuona kama ndiyo kielelezo cha mafanikio. Yaani nakubali kuwa ni mafanikio lakini siyo kama ndiyo umemaliza kila kitu. Je, utakubaliana na mimi kuwa mtu akiwa na utajiri mkubwa, unaweza kuishi kwenye nyumba za kupanga maisha yako yote na akahesabika ana mafanikio kuliko mtu mwenye nyumba na hana fedha? Kipi ni mafanikio sasa, nyumba au utajiri?
Wewe ni muhindiUsijali utapata mwingine, njoo inbox tuyajenge.😃
Kuna sehemu nimetaja maneno yangu ni sheria au unapachika vikolombwezo vyako?Neno lako sio sheria
Kabisa mkuu 👏🏾👏🏾👏🏾👏🏾Life is not predictable.
Kikubwa fanya kazi kwa bidii na nidhamu ya pesa kuwa nayo.
Ukweli ni kwamba mtu anaekuja kukupa deal ni mtu mmoja tu na kupitia hapo unakuwa mtu mwingine tofauti kabisa kiuchumi
.
Hili nimejifunza kwa watu wangu wengi wa karibu walikuja kuinuliwa na watu
Hapa ndipo nilijifunza kwa udhiirisho kwamba mtu huinuliwa na mtu kupitia ukuu wa Mungu.
Hata mtu unae muona leo ana maisha mazuri ukifuatilia utakuta alikuwa kwnye harakati zake ghafla akatokea mtu akamshirikisha ndio ukawa mwanzo wa kutoka.
Kadhalika wahalifu nao hupiga tukio moja tu na kupitia hapo ndio mwanzo wa kutoka.
So pambana lift itakukuta njiani.
Hasa hawa wanao jifanya kumtaja taja Mungu hapa kwenye huu uzi ndio life limewachapa vibaya mno.Watu wengi hawaamini Mungu na wana maisha mazuri tu , na kuna wanaoamini nakusali ila wamepigika vibaya sana .
Sio tu hayupo.Ni mojawapo tu ya kufuru mkuu lkn siyo mbaya zaidi kuliko zote. Wapo wanaokufuru kwa kusema "Mungu hayupo".
Kwa ninachokijua mimi mpaka sasa...mafanikio ni jambo pana sana...kuwa na nyumba na gari ni sehemu tu ya mafanikio...wapo wenye magari na nyumba lkn hawana watoto, wapo wenye magari na mali nyingine nyingi, ila wanaumwa...wapo wenye watoto wengi na familia zenye furaha ila hawana hayo magari na huenda wamepanga.Habari za Jumapili!
Maisha sio Pouwa! Nakubaliana na wale wanaosema Maisha ni majaliwa. Na jitihada hazizidi kudura.
Wapo waliosoma kwa bidii mila hiyo na waliona taa ya matumaini kulingana na matokeo ya darasani waliyokuwa wakiyapata. Waliamini kuwa maisha yao na hatma yao ipo mikononi mwao kumbe sivyo.
Ilifika hatua wakawa wanadharau wale ambao walikuwa wanaonekana hawana mipango na mikakati kutokana na kutoipenda shule.
Wengi walifikiri kuwa kabla ya miaka 30 tayari wangekuwa wamekomesha jeuri na kiburi cha Umaskini katika maisha yao.
Tayari kichwani walikuwa na picha za jumba kubwa la kifahari ambalo walijua ndio watakayoishi. Bongo zao zilishakuwa na miundombinu ya flyover ambapo gari yao ilikuwa ikipita juu yake huku ndani akiwa yeye na Pisikali moja matata ambayo ndio mkewe.
Kwa wasichana, wao nao walikuwa na maisha yao mazuri katika vichwa vyao. Wanaume Handsome, warefu na wenye vipato na Watanashati walikuwa katika fikra zao.
Sasa miaka imekimbia, hawaelewi nini kimetokea. Matumaini yameyoyoma, ngumi ya matumpa upper cut moja matata imepiga kidevu vijana chali.
Hata zile ramani za majengo na magari walizokuwa nazo miaka hiyo zimefutika.
Yule Mwanamke mrembo akilini waliyemfikiria wangekuja kumuoa wanawaona kwenye magazeti, filamu na kwenye riwaya. Hakuna faraja tena, tumaini limeota mbawa. Wamejiunga kwenye chama cha faraja ya mpito cha Kataa Ndoa.
Hawakumbiki tena ndoto ya kuwa na familia bora baada ya kuyapata maisha mazuri yanayotamanika.
Ni Tekniko Knockout.
Hawakujua kuwa maisha yanakupa yale ambayo hujayaomba na yale ambayo huyataki. Tena maisha hukupa yale ambayo hukudhania kwamba ungekuwa nayo. Kwa sababu maisha ni Nasibu, maisha ni bahati tuu.
Sasa mipango imevurugwa na kuvurugika. Kila kitu pangala pangala! Hata kupanga hawataki kupanga tena. Hata wakisema wapange wanaona wanapoteza muda wao. Sasa ni bora liende túu! Wapo tayari kwa lolote na huo ndio mfumo wa maisha unavyotaka.
Mtu ambaye alipanga kabla ya miaka 30 awe na jumba na gari leo hii hata kodi ya chumba cha laki moja hawezi kuhimili. Unaweza kuona pigo alilopigwa ni zito kwa kiwango kipi.
Kijana, unapopanga mipango yako. Muombe Mungu
Suleiman aliwahi kusema;
Mhubiri 9:11 NEN
Nimeona kitu kingine tena chini ya jua: Si wenye mbio washindao mashindano au wenye nguvu washindao vita, wala si wenye hekima wapatao chakula au wenye akili nyingi wapatao mali, wala wenye elimu wapatao upendeleo, lakini fursa huwapata wote.
Acha Nipumzike sasa
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Hapana mie ni ngozi nyeusi, mfupi halafu Kibongee.Wewe ni muhindi
Na wewe unayejua Mungu huyo yupo, ina kuuma nini ukisikia nimesema hayupo?Mambo ya kumuomba we inakuuma nini
We siumesema hakuna Mungu sasa unachukizwa nini ukisikia mtu anasema anamuomba Mungu
Watu tumefanikiwa sababu ya Mungu na ushuhuda tunao aya kasirika
SureHasa hawa wanao jifanya kumtaja taja Mungu hapa kwenye huu uzi ndio life limewachapa vibaya mno.
Wako hapa kujifariji na umaskini wao kwamba ni mipango ya Mungu kwamba huenda kuna siku watafanikiwa.
Wanajifariji na fictional character Mungu...😄
Mtu yeyote anaye amini mafanikio ni "kudra za mwenyezi Mungu" huyo ni maskini wa akili na mali.
Hata akikosa kufanikiwa katika jambo fulani ata amini ni mungu ndiye kafanya hivyo kumbe ni mipango yake mibovu.
AchA utaniHapana mie ni ngozi nyeusi, mfupi halafu Kibongee.
Mimi hainiumi wewe kusema hakuna MunguNa wewe unayejua Mungu huyo yupo, ina kuuma nini ukisikia nimesema hayupo?
Hata mimi nimefanikiwa pasipo msaada wowote wa huyo Mungu.
Umeaona sasa unavyotumia nguvu kubwa kujifariji ndo maana nilikuambia neno lako sio sheriaSio tu hayupo.
Hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
Kutokuwa na gari siyo shida sana, lakini kutokuwa na nyumba yako ni sawa na kutembea kwenye minefield, ni hatari hasa kama una familia.Unaweza kuwa unaishi kwenye nyumba ya kupanga na unatumia usafiri wa public lakini ukawa na mafanikio kuliko mtu mwenye nyumba na gari.
Mkuu, usiige tembo kuny.. Kukiwa na changamoto kubwa Wahindi wanabebanajiulize kwanini wale wahindi wanaishi kwenye nyumba za kupanga maisha yao yote inamaana hao hawapatagi changamoto ya kodi
Point.Hakuna mjanja wa kuchora fate yangu mimi.
am the only one to do that.
Mungu mwenyewe hafanyi hicho kitu.
Mungu anamuwazia mema kila mtu, na mpango wake ni kila mtu afanikiwe na aishi maisha bora yanayo reflect viwango vya utukufu wake.
Ila sasa ,bad news ni kwamba, Mungu anawapa watu wooote same ground ya kupambania ili kuyafikia mafanikio.
Pambana wewe.. Lala wewe. Hapo Mungu anakaa kando kuwaangalia wajuz wa kufuata principles and systems za ku unlock secretes of riches.
Success is predictable , so as Failure
Roadmap ya mwanadamu iliyochorwa na Mungu, inawahusu wanadamu ambao wameji 'aline' kwenye mipango na makusudi ya Mungu.Sikubaliani na hoja kuwa mipango ya kimaisha ya vijana wengi inaharibika kwasabb hawamhusishi ama hawamuombi Mungu. Wapo walokole ama mashekhe promax wamefika 50 bado hawana hata kitanda.
Kila mtu ana FATE yake, yaani Kila mtu kachorewa roadmap ya maisha yake na mwenyezi Mungu. Ndiyo maana akina Laizer wanaokota tanzanite yenye thamani ya mabilioni wakati wengine hata mia mbovu hamuokoti.
Pamoja kamandaPoint.