Kadogosa: Tumetumia umeme wa 336,000 kwenda na kurudi Dar - Morogoro

Kwa umeme huo waliotumia nitashangaa kama nauli ya dar moro kama itazidi sh 3000
Swala la gharama lina chukua mpaka fedha ya mikopo na gharama za ujenzi na ukarabati na muda wa kulipa mikopo ila zinatakiwa kuwa chini kidogo tofauti na mabasi .
 
Wamechukua muda sababu....hawawezi enda full speed...kwenye test....mdogo mdogo test ya pili wataongeza speed kidogo.....test 3 etc....then wataweka constant speed wakianza safari biashara
Hao wanao taka speed hovyo hovyo ni sawa na wapumbavu wanaodhani mtu akinunua gari lenye speed ya km250 kwa saa basi ni lazima hatumie hiyo speed tena muda wote aendeshapo hiyo gari
 
chama cha kupinga watapinga
Hata facts ni kupinga.

Walitakiwa watueleze sababu ya treni ya 180 km/h inakwenda speed ya 38 km/h.

Kama hayo ndiyo majaribio yenyewe... Si waseme tu kwamba tunaanza 30, then 70, then 120 mpaka wafike hiyo speed waliyotuambia mwanzo.
 
Na tunajua mzigo ukiongezeka na nguvukazi pia hivyo siku ikiwa full watu na mizigo itatumia umeme wa sh ngapi??


Maswali ya kujiuliza ni mengi, ila mi nafikiri tubaki tu kwenye suala la mwendokasi ambalo ndilo la msingi zaidi, kuwahisha ufikaji ulio salama na wa haraka katika maeneo ya mbali kama Mwanza n.k
 
Kwa hiyo lengo la kufanya test ni kutaka kujua hiyo train inatumia umeme wa sh. ngapi au mimi ndio sijaelewa.
 
Ndio maana magufuli alisema lazima umeme ushuke bei kwa sababu ikiwa sehemu kubwa unazalishwa kwa maji basi gharama ya uzalishaji lazima itapungua. Uzalishaji kwa njia ya mabwawa ya maji ndio umeme rahisi kabisa. Sasa kina makamba na maharage wake waliona hapo wao wapige kwa kufaidi kwa mishahara na kila aina ya marupurupu manono na upigaji kwa kila namna. Yaani wale wenyewe upungufu mkubwa kwenye gharama ya uzalishaji wa umeme. Wananchi tusikubali ubadhirifu tanesco au serikalini kote. Mitambo itakapokua yote inafanya kazi ni lazima wosia wa magufuli utekelezwe. Tena sio kupunguza bei kwa visenti. Umeme lazima ushuke hadi wazalishaji wa viwandani na watoa huduma waone ulazima kupunguza bei ya bidhaa zao.
 
Kwa umeme huo waliotumia nitashangaa kama nauli ya dar moro kama itazidi sh 3000
Kumbuka Kuna garama za mishahara ,,gahrama za kurudisha fedha ya ujenzi,,gharama ya ukarabati wa miundo mbinu etc
 
Umeme hauwezi kushuka bei, kuna makampuni yanayoiuzia umeme TANESCO yana mikataba mpaka ya miaka 20 mbele yanalipwa capacity charge. Tena mamilioni kwa siku awe amewasha mtambo au hajawasha yeye analipwa, akiwasha kuwauzia umeme ndio balaa.
 
Kuna watu wahujumu usafiri wa SGR ili kulinda wenye mabasi , wakati usafiri wa treni ndio mzuri , sababu ya muda unaotumia njiani na pia nafasi ya kusoma, kutembea, na kutumia maliwato bila kusumbua abiria wengine.
 
Kuna wale wauza dawa za minyoo na sumu ya panya wasiruhusiwe ndani ya tren pia kuingia na mifugo kama kuku n.k
Mkuu jana tu nimeshuhudia kituko cha mwaka, mwandishi aliyealikwa kwenye majaribio ya treni ya mwendokasi alionekana akisifia finishing ya jengo la abiria kwa kushika ukuta na kuchora kwa vidole vyake, alionekana kutest milango kwa kuigongagona na mbaya zaidi alionekana akikwangua na kucha vile viti,hata kuuma viti kwa meno!.....
Fikiria baada ya mwaka mmoja haya mabehewa na jengo la abiria vitakuwa na hali gani baada ya miaka miwili? 😲
 
Na vichwa walivyo nunua gharama zake za uendeshaji zipoje, isije kuwa bei ya kununua rahisi lakini gharama za uendeshaji ni kubwa hivyo tunapigwa kote kote.
 
diesel itakuwa nyingi sana bro. na moro inaweza tumia masaa 10
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…