===
Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Ubia nchini PPPC Bwana David Kafulila akihojiwa katika Kipindi Cha One on One Cha Wasafi TV amesema Tanzania katika miaka 25 ijayo inatarajia kujenga Uchumi mkubwa karibu mara mbili ya Uchumi wote wa Africa ya Kusini ya Leo.
Kafulila anaendelea kwa kusema kama Africa ya Kusini ya leo Wana Umeme unaofikia Megawatt 60,000 huku sisi tukitarajia kujenga Uchumi marambili ya Uchumi huo wa Africa Kusini leo maana yake lazima tuwe na Umeme unaozidi umeme wa Africa ya Kusini ya leo ambao ni zaidi ya Megawatt 60,000.
Swali tunaloweza kujiuliza kwa pamoja, ni Je, bila kushirikisha mitaji na Ujuzi toka sekta binafsi PPP Tanzania kwa kutumia Kodi na Mikopo pekee tunaweza kufikia kumiliki umeme wa Megawatt zaidi ya 60 ifikapo mwaka 2050 Jibu ni "HAPANA" lazima PPP ichukue nafasi kwenye hili kwa manufaa ya kizazi hiki na manufaa ya kizazi kijacho.
View attachment 3202423
====