Mhe David Kafulila Mkurugenzi Mkuu wa Ubia nchi PPP amewatoa hofu Watanzania kuwa Serikali yao ya awamu sita ina nia na dhamira njema dhidi yao.
Katika kipindi Cha DK 45 Cha ITV Kafulila amesema si kosa nchi kukopa kwaajili ya miradi ya maendeleo ila ni dhambi kukopa ili kugharamia mishahara na mambo mengine yasiyo ya kimaendeleo ( matumizi ya kawaida )
Kafulila ameenda mbali mpaka kuwakumbusha namna Ulaya ilivyojengwa kwa mikopo toka Marekani (MARSHALL PLAN ) baada ya Vita kuu ya Pili vya Dunia miaka ya 1948.
Hata hivyo Kafulila ameonesha si kweli kwamba Uchumi wa Tanzania unajengwa kwa Mikopo pekee ila ni Kwa sehemu tu,
Kafulila anasema, Tanzania kwa kipindi cha miaka mitatu tumekopa nje kiasi cha US$ 5 bilioni wakati Uchumi wetu katika kipindi hicho umekua kwa US$ 20 bilioni sawa na tofauti chanya ya US$ 15 bilioni.
Mkurugenzi Kafulila amemsifu zaidi Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa namna alivyoipokea nchi na kwa kasi hii ya Uchumi ambayo hakuna nchi yoyote Africa Mashariki na Kati kwa miaka mitatu imefikia kiasi na kiwango chake.