Kafulila: Hata Ulaya ilijengwa kwa Mikopo toka Marekani Marshall Plan si dhambi kukopa ili kujenga miradi ya maendeleo kama SGR au JNHP

Kafulila: Hata Ulaya ilijengwa kwa Mikopo toka Marekani Marshall Plan si dhambi kukopa ili kujenga miradi ya maendeleo kama SGR au JNHP

Kafulila nimjenga hoja mzuri tatito ni pale aliponunuliwa tu lakini sina tatizo anachoongea japo kuna sehemu anatupiga changa la macho kwa kutetea ugali wake
Sidhani kama jamaa alinunuliwa kwa sababu ni mtu mwenye maisha duni tu, Huyu kijana ni mwadilifu sana aise
 
===
Mhe David Kafulila Mkurugenzi Mkuu wa Ubia nchi PPP amewatoa hofu na mashaka Watanzania kwani Serikali yao ya awamu sita chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan ina nia na dhamira njema dhidi yao.

Kafulila akihojiwa Katika kipindi Cha Television amesema si kosa nchi kukopa kwaajili ya miradi ya maendeleo ila ni dhambi kukopa ili kugharamia mambo kama mishahara na mambo mengine yasiyo ya kimaendeleo yaani matumizi ya kawaida.

Kafulila ameenda mbali zaidi na kuwakumbusha namna Ulaya ilivyojengwa kwa misaada na mikopo toka Marekani ( Marshall Plan ) baada ya Vita kuu ya Pili ya Dunia miaka ya 1948.

Hata hivyo Mhe David Kafulila ameonesha si kweli kwamba Uchumi wa Tanzania unajengwa kwa Mikopo pekee ila ni Kwa sehemu tu,

Kafulila anasema, Tanzania kwa kipindi cha miaka mitatu imekopa fedha nje kiasi cha US$ 5 bilioni wakati Uchumi wake katika kipindi hicho umekua kwa kiasi cha US$ 20 bilioni sawa na tofauti chanya ya US$ 15 bilioni.

Mkurugenzi Mkuu huyo wa UBia amemsifu zaidi Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa jinsi alivyoipokea nchi na kwa kasi hii ya Uchumi ambayo hakuna nchi yoyote Africa Mashariki na Kati kwa miaka hii mitatu iliyofikia kiasi na kasi Kwa kiwango hiki kilichofikiwa na Tanzania ya Dkt Samia Suluhu.

=====​
Asañte Mwandishi
 
Mheshimiwa Kafulila ni kiongozi Mwenye uwezo mkubwa sana wakiuongozi,kujenga hoja, kutetea hoja,kushawishi kwa hoja na kumfanya mtu akamuelewa kwa urahisi na kwa lugha rahisi kabisa.
ushaanza kumpigia upatu na huyu tena
 
Marshal plan iliyojenga Ulaya Hali yao ya tekelinalokujia ilikuwa kama ya kwetu kwamba huo ubia utatutoa huko. Tulikuwa na KADCO, Alliance Air, Mkataba wa SA na ATC , RITES , Iptl, Richmond, nk je ilitutoa huko.
Nyerere alisema tuna hitaji watu sio wezi ndio tunaweza kutoka hapa tulipo.
Siasa Safi sio hii ya kuuuza uza vitu, ndio maana Leo hii wazaramo hawapo darisalam yao. Tabia ya kusaini mikataba ya hovyo hovyo haitatupeleka kokote, na Maendeleo sio maneno. Sasa hivi kuna hela zimelala kwenye JNHEP hazizalishi, SGR ya vipande vipande, TAZARA. Kuna vitu vya miradi vinatakiwa kufanywa na Tumebya Mipango au wachumi kama hatuna tume ya Mipango na na ikifikia kuweka mikataba iwekwe na wanasheria sio yeye au wanasiasa .
Nakubaliana na wewe partially nitakuja kueleza baadae
 
Sidhani kama jamaa alinunuliwa kwa sababu ni mtu mwenye maisha duni tu, Huyu kijana ni mwadilifu sana aise
Kwa hakika Mheshimiwa David Kafulila Ni kiongozi muadilifu, mzalendo, mchapakazi na mwenye dhamira njema na kiu ya kuona Taifa letu linasonga mbele kimaendeleo na kukua kiuchumi kama kinachoendelea kwa sasa chini ya uongozi shupavu, imara na madhubuti Wa Mama yetu mpendwa Daktari Samia Suluhu Hasssan.
 
===
Mhe David Kafulila Mkurugenzi Mkuu wa Ubia nchi PPP amewatoa hofu na mashaka Watanzania kwani Serikali yao ya awamu sita chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan ina nia na dhamira njema dhidi yao.

Kafulila akihojiwa Katika kipindi Cha Television amesema si kosa nchi kukopa kwaajili ya miradi ya maendeleo ila ni dhambi kukopa ili kugharamia mambo kama mishahara na mambo mengine yasiyo ya kimaendeleo yaani matumizi ya kawaida.

Kafulila ameenda mbali zaidi na kuwakumbusha namna Ulaya ilivyojengwa kwa misaada na mikopo toka Marekani ( Marshall Plan ) baada ya Vita kuu ya Pili ya Dunia miaka ya 1948.

Hata hivyo Mhe David Kafulila ameonesha si kweli kwamba Uchumi wa Tanzania unajengwa kwa Mikopo pekee ila ni Kwa sehemu tu,

Kafulila anasema, Tanzania kwa kipindi cha miaka mitatu imekopa fedha nje kiasi cha US$ 5 bilioni wakati Uchumi wake katika kipindi hicho umekua kwa kiasi cha US$ 20 bilioni sawa na tofauti chanya ya US$ 15 bilioni.

Mkurugenzi Mkuu huyo wa UBia amemsifu zaidi Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa jinsi alivyoipokea nchi na kwa kasi hii ya Uchumi ambayo hakuna nchi yoyote Africa Mashariki na Kati kwa miaka hii mitatu iliyofikia kiasi na kasi Kwa kiwango hiki kilichofikiwa na Tanzania ya Dkt Samia Suluhu.

=====​
Safi
 
Back
Top Bottom