Kafulila: Watanzania zaidi ya mil 40 ni Wakulima mil 28 kati yao ni Wanawake tunapunguza Umasikini kwa nchi yetu kuwekeza zaidi kwenye Sekta ya kilimo

Upuuzi wa 970bl?
Au sijakuelewa
Leta ripoti moja tuu ya ufanisi
mf. Mashamba makubwa ya umwagiliaji yamewezeshwa na serikali tumevuna tani kadhaa nk.
Hapo at least tutakuelewa sio upuuzi wakujificha kwenye bajeti.
Serikali hii inayoshindwa kupata faida hata kwenye biashara rahiiisi ya mafuta itawezesha kilimo gani??
Acha vichekesho vinavyochekesha kwakuwa havichekeshi
 
Machawa wote pro max nchi hii wanatokea Kigoma,Mwajaku,Babalevo,Kafulila

Hivi huu mkoa una nini jamani?
 
Hapo anaongea huku amekunja posho nono
 
Wanapiga siasa tu, hakuna mpango mkakati wala nia yoyote ya dhati ya kuleta mapinduzi katika sekta ya kilimo. Mpango wa kilimo kwanza ulikuwa umeandaliwa vizuri sana, kilichokuja kutokea kilituacha sisi wadau na mshangao mkubwa. Siku wanasiasa wakiwa na nia ya dhati ya kuibadilisha nchi hii, ndio siku tutaona ni kwa kiasi gani tulilala.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…