Kafulila: Watanzania zaidi ya mil 40 ni Wakulima mil 28 kati yao ni Wanawake tunapunguza Umasikini kwa nchi yetu kuwekeza zaidi kwenye Sekta ya kilimo

Kafulila: Watanzania zaidi ya mil 40 ni Wakulima mil 28 kati yao ni Wanawake tunapunguza Umasikini kwa nchi yetu kuwekeza zaidi kwenye Sekta ya kilimo

Akizungumza katika maadhimisho ya miaka mitatu ya Uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan Mkurugenzi Mkuu wa Ubia nchini PPP Mhe David Kafulila amesema,

Nchi ya Tanzania kwa awamu hii ya sita imeamua kujikita zaidi kwa kuwekeza kwenye Sekta ya Kilimo ambayo inagusa Jamii kubwa ya Watanzania,

Kilimo ndio Sekta ambayo Kila Mtanzania inamgusa kwa namna moja au nyingine huko nyuma haikupewa kipaumbele sana kama ilivyo Leo,

Mathalani, Kilimo bajeti yake imekuwa kutoka TZS 230BL mpaka TZS 970BL karibu mara Nne ,

Sote tunafahamu zaidi ya 70% ya wakulima wote ni Wanawake ambao ni karibu Wanawake mil 28 wanategenea Kilimo na hata hivyo zaidi ya 64% ya Watanzania ambao ni karibu wakulima mil 40 ni wakulima huku zaidi ya 80% ya malighafi zote za viwandani zinatemea Kilimo.


View attachment 2947980
Tomboka malamu
 
Kwenye hili kama ni kweli Wacha tumpongeze Mama
Kilimo Tanzania kinadharaulika sana
Nakumbuka wakati nasoma shule ya msingi walimu walikuwa wanaswali eti what is your father's occupation
Sisi watoto wa wakulima tuliona kama hili swali lilituonea sana tukijibu he is a farmer.
Kilimo kikipendwa tu Tanzania tutainuka sana kiuchumi
 
Na tumefeli kwelikweli mkuu, yaani ni sekta ambayo ingeweza kuboresha maisha ya wananchi wengi walio wakulima. Mpaka leo bado tunalima kwa kutumia zana na mbinu kama alizotumia Nuhu baada ya gharika.
Tunahitaji mabadiliko
 
Tunahitaji mabadiliko
Mabadiliko huja pale waliokabidhiwa wajibu wao wakatimiza wajibu wao. Kwa nia ya dhati na uchungu mkubwa, kwa kuacha ubinafsi na ubadhilifu uliopitiliza, kwa kuacha dharau na kejeli. CCM hawana hiyo nia na hawajawahi kuwa nayo
 
Mimi siwezi kumsikiliza au kusoma Uzi wa 2 mbili na comment tu.najua huyu ana advanced diploma ya uchawa.
 
Mabadiliko huja pale waliokabidhiwa wajibu wao wakatimiza wajibu wao. Kwa nia ya dhati na uchungu mkubwa, kwa kuacha ubinafsi na ubadhilifu uliopitiliza, kwa kuacha dharau na kejeli. CCM hawana hiyo nia na hawajawahi kuwa nayo
CCM ni kubwa acha ku-capitalize tabia za individual kwa CCM yote
 
IMG_20221017_200817.jpg
 
Kafulila arudishwe tena kwenye madaraka anaweza kufa, sio kwa mapambio hayo.

Hata hiyo 2025 uchaguzi ni kupotezeana muda, na Wala sio kwa ubora wa rais, Bali Tanzania hakuna uchaguzi, ila Kuna maonyesho ya ujinga wa mtu Mweusi kwenye box la kura.
ukiskiaga mambo mazuri unaumiaga hadi huruma kamanda dah, pole 🐒
 
Back
Top Bottom