Kagoda: Ni Rostam

Kagoda: Ni Rostam

8. Alipoulizwa kuhusu ushahidi uliotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Salvatory Rweyemamu kuwa yeye Rostam ndiye aliyemuunganisha na Mkurugenzi wa Richmond, Mohammed Gire kufanya kazi ya ushauri wa habari katika kampuni hiyo, Rostam alikana kwa kusema kuwa, alichowahi kufanya ni kumuunganisha kufanya kazi kama hiyo kwa kampuni ya uwakala wa kupakua mizigo bandarini.



Salva si yupo? nae athibitishe aliyosema au kama anafuta usemi wake
 
Kwa maneno yake sasa namfahamu vyema Rostam Aziz

Lula wa Ndali-Mwananzela Mei 6, 2009

Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

AMETIKISA kiberiti tena na waliotikisika wametisika. Alisema atazungumza waliotaka kusikia wamesikia. Waliokuwa wanajali atakachosema sasa hivi wanamuona shujaa!

Siyo mimi. Nilikataa mwaka jana kuwa Rostam ni mtu ambaye anaweza kuitikisa nchi kwa maneno yake. Niliandika wakati ule kuwa "Sipendi Rostam atikise kiberiti bungeni". Baada ya majibu yake niliandika makala nyingine ya "Mtu mzima hatishiwi nyau". Nadhani inabidi nibadili msimamo huo.

Mkutano wake na waandishi wa habari Jumapili iliyopita, umenihakikishia kabisa kuwa msimamo wangu wa awali ulikuwa na makosa. Sikujua kuwa Mbunge huyo ana nguvu kuliko serikali na ujasiri kuliko wa askari. Sasa nimetambua kwa uhakika kabisa Rostam ni mwanasiasa na mfanyabiashara ambaye amekubuhu kwa kila kipimo.

Nimefikia hatima hiyo baada ya kusikia madai yake mazito aliyoyatoa dhidi ya serikali siku ya Jumapili, madai ambayo kimsingi yanaweza kuwa yamethibitisha tuhuma za ufisadi zinazotolewa juu yake. Yamethibitisha kuwa kama kiongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na kama mfanyabiashara hana maadili ya uongozi kwani ameituhumu serikali ya chama chake hadharani na pasipo utata kuwa ni goi goi isiyofuata utawala wa sheria. Na zaidi ya yote amejiweka juu ya serikali hiyo.

Madai hayo mazito dhidi ya serikali yanapaswa kuangaliwa kwa ukaribu na kulaaniwa na kila Mtanzania. Ni madai ambayo ndani yake yamethibitisha kile ambacho wengine tumeamua tukikohofia kwa muda mrefu kuwa kuna tatizo ndani ya serikali. Ni madai mazito ambayo hayawezi kuachwa yapite bila kumulikwa kwa ukaribu.

Ninafahamu vizuri kuwa alisimama kumjibu Reginald Mengi aliyetangulia kutoa tuhuma dhidi yake na ya kuwa ukimsikiliza kwa karibu unaweza kabisa kuamini alikuwa anataja "ufisadi" wa Mengi. Na wala siandiki haya ili kumpamba Mengi.

Ukisogea kwa karibu na kuanza kuangalia kile alichosema utagundua kuwa Rostam amesimama akitoa tuhuma nzito dhidi ya serikali yetu, serikali ambayo tunaamini ilichaguliwa na wananchi na ipo kihalali. Tuhuma hizi ni nzito na haziwezi kuachwa zilivyo.

Kajisimamisha kinyume na serikali.

Kitu cha kwanza ambacho unaweza kukiona kwenye maelezo yake ni geresha ya heshima. Anatangaza kutambua kuwa mawaziri wa serikali wamekwisha kuzungumzia jambo hili pale anaposema "Naelewa kwamba tayari Serikali na vyombo vyake vimeshatoa kauli za kumuonya Mengi kuhusu kauli alizozitoa. Waziri wa Nchi anayeshughulikia Utawala Bora, Mheshimiwa Sofia Simba, amemtahadharisha Mengi kwamba kitendo chake cha kutumia vibaya vyombo vyake vya habari kuwachafua washindani wake wa kibiashara hakikubaliki.

Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa George Mkuchika, amesema Wizara yake inafanya uchunguzi wa matamshi ya Mengi kwa kuupitia mkanda wenye maelezo yake na ikibainika amevunja sheria atachukuliwa hatua."

Anaendelea na kutoa mfano wa kauli ya Waziri Mkuu pamoja na msimamo wa Jeshi la Polisi. Kimsingi, alikiri kuwa serikali imeingilia kati na kama Mbunge aliyeapa kuilinda Katiba ya Tanzania alitakiwa akae kimya na kuviacha vyombo vya sheria kufanya kazi yake.

Rostam hakufanya hivyo kwani vyombo hivyo kwake viko chini yake. Anasema: " Pamoja na kuheshimu na kuthamini maelezo hayo ambayo yamemuumbua Mengi, lakini bado nahisi binafsi nina wajibu wa kutoa maelezo ya kina kuhusu kiherehere hiki cha Mengi."

Anachosema ni kuwa hata kama serikali imeingilia kati na imekwisha kutoa msimamo wake, yeye kama Rostam yuko juu ya serikali hiyo na hivyo haamini kuwa serikali inaweza kumdhibiti Mengi na hivyo anaongeza uzito wake binafsi kwenye suala hilo. Kwa nguvu gani aliyonayo?

Uwezo wa kuchagua msemaji wa Watanzania ameutoa wapi?

Katika tamko lake akahoji Mengi amepata wapi ridhaa ya kuzungumza na wananchi? Akauliza hivi "Mengi ambaye watu wanajiuliza amepata wapi uhalali wa kujifanya msemaji wa Watanzania wakati hawajawahi kumchagua katika nafasi yoyote na hivyo hana ridhaa yao."

Anachojaribu kusema hapa ni kuwa kama mtu hajachaguliwa basi hawezi kuzungumza au kutoa kilio cha Watanzania. Kwamba, hadi uwe umewahi kuchaguliwa basi usijaribu kuwapinga mafisadi au kupambana nao kwani kwa kufanya hivyo hauna ridhaa.

Ina maana maoni ya wahariri wa magazeti, radio na televisheni, viongozi wa dini na watu wa taasisi mbalimbali hawana haki wala uwezo wa kuzungumza na kutoa kilio cha Watanzania kwa sababu moja tu kuwa hawakuchaguliwa! Anataka watu waamini kuwa ukichaguliwa ndiyo una ridhaa ya kutoa kilio cha sauti za Watanzania. Kweli?

Kama ni kweli tungemuuliza Mhe. Rostam, katika Bunge la Muungano ambapo yeye ni mjumbe wake ni lini alisimama kutetea maslahi ya Watanzania? Ni lini alikemea ufisadi wa Meremeta, Deep Green Finance, Mwananchi Gold, Tangold, au EPA? Ni lini yeye mchaguliwa wetu alisimama kutetea wale vijana waliotelekezwa na serikali ya chama chake kule Ukraine? Ni lini alisimama kutaka waliohusika wawajibishwe katika vifo vya watoto 19 kwenye mkoa wake wa Tabora?

Ni lini Rostam amesimama kuwatetea wanafunzi wa vyuo vyetu vikuu ambao kila mwaka wanalazimika kugoma kwa sababu ya uongozi mbovu na sera mbovu ya elimu ya juu? Kuchaguliwa peke yake si ridhaa ya wananchi kwani wengine wamechaguliwa baada ya hadaa ya wananchi hao! Kwani yeye mwenyewe alipitaje kwenye kura za maoni za CCM? Au tumkumbushe?

Ati Mengi ndiye amemfanya avunje ukimya.

Mheshimiwa mchaguliwa Rostam akionyesha kuwa ana uchungu na nchi hii alisema kwenye tamko lake: "…sidhani itakuwa ni haki kuendelea kukaa kimya na kumwacha (Mengi) afanikishe malengo yake hayo. Hatuwezi kukaa kimya maana kufanya hivyo kutakuja kuligharimu vibaya sana Taifa letu."

Kwa haraka haraka unaweza kuamini kuwa tishio kubwa la nchi yetu ni Mengi! Kiasi kwamba hadi Rostam kuja kuzungumza basi Mengi anaitisha sana nchi hii. Ukweli ni kuwa, alichofanya Mengi kinawatisha mafisadi waliokubuhu nchini mwetu ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakionewa haya hata kutajwa majina. Ndiyo sababu Rostam kaamua kuzungumza.

Hebu fikiria; hakuzungumza kwenye suala la Kagoda, hajazungumza juu ya wizi wa Benki Kuu, hajazungumza juu ya wizi wa rada, hajazungumza juu ya rafiki yake Andrew Chenge na suala la Vijisenti, hajazungumza suala la Richmond na Dowans, kote huko mchaguliwa amekaa kimya ati leo Mengi kumtaja ameamua kuvunja "ukimya" kwa maslahi ya nchi? Kwa sauti yake mwenyewe amethibitisha ufisadi wake.

Rostam amevunja ukimya si kwa sababu ana uchungu na nchi (yawezekana anao) lakini kwa sababu mirija yake iliyochomekwa kwa Watanzania inatishiwa kukatwa. Na hili linamtisha yeye na wengine.

Ugomvi wa Mengi na watu kadhaa

Mojawapo ya mifano inayotolewa mara nyingi ni ya "ugomvi wa Mengi" na watu mbalimbali na kuwa Mengi alitumia mambo hayo kuyafanya ya kitaifa.

Niliposikiliza na baadaye kusoma pole pole majina ya hao ambao Mengi aligongana nao ninaamini kuwa si tu alipaswa kugongana nao bali walikuwa ni watu sahihi kugongana nao (ukiondoa mmoja au wawili). Sitaawangalia kwa kirefu lakini majina yao yanafahamika. Wapo: Wilson Masilingi, Shamim Khan, Edward Lowassa, Basil Mramba, Habari Corporation, Yusuph Manji, Adam Malima, Tanil Somaiya, Lawrence Masha na mwenyewe Rostam Aziz.

Hili mbona ni genge la kushtua sana kugongana na mtu mmoja. Kwenye majina hayo naweza kuwaondoa watu wawili tu kuwa yawezekana mgongano wao ulikuwa wa kikazi lakini wengine wote aidha wamehusika na uporoja wa nchi yetu au bado wanahusika na uporaji huo!

Badala ya kuona kuwa mgongano huo ni wa Mengi dhidi ya hao kwa nini tusiuone kuwa ni mgongano wa watu kadhaa dhidi ya mtu mmoja? Inakuwaje, vigogo wa serikali na chama wote wawe wanagongana na mtu mmoja tu lakini hadi hivi sasa wameshindwa kumkamata kwa uhalifu au kumfikisha mahakamani na wamebakia kuziandama biashara zake?

Dhamira yake njema au kitu kingine?

Rostam ameelezea katika tamko lake sababu kubwa ya "kumuumbua" Mengi kuwa anafanya hivyo kwa sababu ya "kulinusuru Taifa lisije likatumbukia kule Mengi anakotaka kulipeleka."

Nimesema hapo juu, juu ya kuvunja kwake ukimya. Hata hivyo, nitakuwa nina wazimu nikiamini kuwa Rostam amefanya hivyo ili "kulinusuru taifa".

Ndugu zangu, Rostam ana nafasi ya kulinusuru Taifa kutoka mikononi mwa mafisadi wengine. Kwanza kabisa angetutendea mema kweli kama angetuambia Dowans ni kina nani na kwanini tusinunue mitambo yao; Rostam angeweza kutusaidia kweli kwa kupigana na ufisadi wa Benki Kuu au kwa kuleta mswada bungeni wa sheria ambayo ingeipa nguvu taasisi ya Usalama wa Taifa; au kwa kuleta mabadiliko ya Sheria ya Madini au mambo ya fedha.

Kama Mbunge ana nafasi ya kulinusuru Taifa akiwa bungeni na pia akiwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Halmashauri Kuu ya Taifa. Sehemu hizo zote, Rostam hajasimama kujenga hoja au kuonekana akilitetea taifa.

Iweje leo aone tishio kubwa ni Mengi? Hivi haoni kilichotokea Benki Kuu? Wakati Dk. Daudi Ballali ametoroshwa kwenda Marekani mbona hakusimama kupiga kelele arudishwe? Saileth Vithlani yule dalali wa rada si ametoroka kwenda anakojua mbona Rostam hajapiga kelele? Hii dhamira yake njema ya "kulinusuru taifa" ina walakini. Haiwezekani mtu atake kulinusuru taifa wakati maslahi yake ndiyo yako hatarini.

Rostam angesema tu kuwa anafanya hivyo ili "kunusuru" biashara zake! Tungemuelewa wala tusingegongana.

Kwa maneno yake anakiri tabia yake mwenyewe.

Rostam anasema hivi katika maelezo yake "Wanasaikolojia wanasema mtu anapotuhumu wengine kuwa na tabia fulani, mara nyingi huwa yeye ndiye mwenye tabia hizo".

Katika maelezo yake anamtuhumu Mengi kuwa ana "tamaa, uroho, wivu, chuki, fitina, ubaguzi na ubinafsi uliovuka mipaka" na kuwa ni "nyangumi wa ufisadi" nchini.

Kama maneno aliyoyasema kuhusu wanachosema wanasaikolojia je yawezekana kwa kile anachomtuhumu Mengi yeye naye ndiyo hicho hicho? Au anataka kusema kuwa ukweli wa maneno hayo ya wanasaikolojia yana ukweli kwa watu wengine wote isipokuwa Rostam? Kwa upendeleo gani alionao mbinguni?

Ukusanyaji wa taarifa za watu

Kati ya vitu ambavyo vimeonyesha ni jinsi gani Rostam ana nguvu na uwezo mkubwa ni pale ambapo ameweza kukusanya taarifa na takwimu mbalimbali kuhusu kampuni za Mengi, fedha na masuala mbalimbali yanayohusiana nayo.

Ni wazi kuwa hakufanya kazi hiyo yote peke yake, na bila ya shaka, ana watu waliomsaidia kufanya hivyo. Hii ina maana kuwa Rostam mchaguliwa, mwanasiasa na mfanyabiashara safi ameweza kupata taarifa za kibenki (akaunti na kiasi cha fedha) za raia wa mitaani ambaye hajachaguliwa na mwananchi yeyote!

Hii ina maana ya kuwa Rostam ana watu hadi kwenye taasisi za benki na vyombo mbalimbali vya umma ambao wamemfanyia kazi hiyo. Siamini kama watakuwa wamefanya kazi hiyo bure!

Wakati Mengi alipotoa tuhuma zake hakutoa data! Wengi walifikiri ni kwa sababu hazipo lakini nina uhakika alijua kuja na data huwezi kuweka hadharani bila kuonyesha kuwa umevunja sheria kuzipata data hizo!

Ninatuhumu wazi wazi na hadharani kuwa Rostam, Mbunge wa Jamhuri ya Muungano amevunja sheria za mambo ya fedha na nyingine kwa kutoa taarifa za wateja wa benki.

Lakini pia kwa kufanya hivyo amethibitisha kuwa kama ameweza kupata taarifa zote hizo za makampuni ya Mengi ina maana anaweza kupata taarifa za Mtanzania yoyote yule anayejitokeza kumpinga, hizi ni nguvu za kutisha!

Ina maana ya kwamba, wale wanasiasa wote aliowasaidia kuingia madarakani wako mikononi mwake na siku wakimtibua tu atayaweka hadharani. Nakumbuka alivyomuumbua Mtikila kwa mkopo wa milioni tatu!


Uchungu wa bilioni 28 za mikopo

Kati ya vitu ambavyo vimenifurahisha lakini wakati huo huo kuthibitisha aina fulani ya unafiki ni pale anapoonyesha uchungu wa fedha ya mkopo halali ambao alidai kuwa Mengi anadaiwa.

Anasema hivi kuhusu mkopo huo: "Fedha hizi hadi kufikia sasa 2009 pamoja na hesabu ya riba zinafikia takriban bilioni 28. Hivi ndivyo Mengi alivyochangia kuifilisi NBC, benki ya wananchi masikini wa Tanzania. Fedha hizi zilizochukuliwa na Mengi, shilingi bilioni 28, zinaweza kujenga shule za sekondari 100 ambazo zingeweza kuwanufaisha watoto wa kimasikini wa Tanzania."

Binafsi nilicheka na kutikisa kichwa! Rostam ana uchungu wa bilioni 28! Hivi zilipochotwa bilioni 133 toka EPA mbona Rostam hakusema kitu? Waliponunua dege kwa bilioni karibu 50 Rostam alikuwa wapi? Vipi kuhusu rada ya bilioni 40 wakati 21 zikigawiwa kwa makuwadi wa ufisadi Rostam mbona hakusimama kutetea? Rostam alikuwa wapi wakati wengine tunaongoza mapambano ya kupinga kutumia bilioni 60 kununua mitambo ya Dowans wakati Dowans waliingia nchini na kuandikishwa kwa taarifa za uongo?

Zaidi ya yote, ninajiuliza kama Rostam katika uwezo wote alionao ameweza kutupatia taarifa za akaunti za Mengi na madeni ya Mengi na yalitoka wapi na yakawa vipi, ameshindwa nini kujitolea kutumalizia suala la Kagoda?

Rostam ana uwezo na mbinu za kujua wamiliki wa Kagoda na fedha hizo zilienda vipi, wapi, na nani, kwanini DPP asimuombe Rostam kuendesha uchunguzi huo na kutoa taarifa kwa umma jinsi alivyofanya juzi? Hapo tu ndipo nitaamini kuwa kweli Rostam ana uchungu wa masikini wa nchi hii!

Hitimisho

Kimsingi ukweli unabakia kuwa ukweli, Rostam ni mtu mwenye nguvu nchini bila ya shaka kuliko mtu mwingine yeyote.

Asili ya nguvu zake hizo ni ujuzi wa mambo mbalimbali juu ya wanasiasa na watumishi mbalimbali. Ni yeye anayejua yaliyotokea wakati wa uchaguzi uliopita kwa vile alikuwa Meneja wa Kampeni).

Ninampa changamoto kuwa kama kweli yeye ni mzalendo wa kweli, ajitokeze na aeleze vyanzo vyote vya fedha za kampeni ya CCM.

Ninampa changamoto pia ajitokeze na kuliambia taifa ni makampuni mangapi yaliyo katika jina lake yeye mwenyewe ili angalau tujue anaposema ametoa ajira kwa watu 6000 tujue kweli ni yeye ndiye aliyefanya hivyo.

Zaidi ya yote, ninatoa changamoto kwa Rostam arudishe fedha yoyote ambayo hakuipata kihalali au anajua haikupatikana kihalali.

Vinginevyo, ninaamini kwa maneno yake mwenyewe na kwa kauli zake amethibitisha kabisa tuhuma za ufisadi wake. Amethibitisha ana nguvu za ajabu, anaweza kuitetemesha nchi na kwa hakika hakuna kiongozi yeyote wa serikali ya nchi hii anayeweza kumnyoshea kidole kwani wote wako mikononi mwake. Nina shaka inawezekana akawa na nguvu kuliko tunavyoweza kufikiria.

Labda siku moja kutakuwa na mtu jasiri ambaye atatuambia asili ya nguvu zake ili hatimaye tuweze kumdhibiti kama alivyodhibitiwa Samson. Vinginevyo, tukikubali hadaa zake kwa wananchi basi tusije kushangaa akiwashambulia mashujaa wa nchi hii!

Binafsi bado ninamuangalia kwani siamini kama anauwezo wa kulipigisha magoti taifa. Sijui labdo anao.

Barua-pepe: lulawanzela@yahoo.co.uk
 
Date::7/13/2009Mwananchi
Na Ramadhan Semtawa

MKURUGENZI wa Mashtaka (DDP), Eliezer Feleshi amesema ni vigumu kuwaburuza mahakamani watuhumiwa wanaohusika na kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd, akisema kufanya hivyo kunaweza kuiweka serikali mahali pagumu kwani serikali inaweza kuwakamata waliotumwa kuchukua fedha, lakini ikashindwa kuwanasa waliowatuma.

Kagoda inadaiwa kuchota Sh40 bilioni kwa kisingizio cha kufanya kazi za Idara ya Usalama wa Taifa, lakini kumekuwa na utata mkubwa kuhusu wamiliki wakuu wa kampuni hiyo.

Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalumu ofisini kwake jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, DPP Feleshi alisema kutokana na ugumu huo, ameagiza upelelezi zaidi wa jalada la Kagoda ili kupata vielelezo na uthibitisho kuhusu pande zote mbili za shilingi.

Mahojiano hayo yalilenga kufahamu nini hasa ugumu wa kufikisha mahakamani watuhumiwa wa Kagoda, wakati baadhi ya watuhumiwa walioiba Sh 90.3 bilioni kutoka makampuni 13, walishafikishwa mahakamani huku uchunguzi wa Sh 42.6 bilioni, ukiendelea nje ya nchi.

"HIvi ninyi (waandishi) mnaitakia mema serikali; hivi sasa kuna baadhi ya kesi zinaendelea kama za akina (majina tunahifadhi), mmeanza kuandika mara serikali hivi yashindwa, sijui hivi..." alisema.

"Hatufanyi mambo kwa kukurupuka, ndiyo maana nimeagiza upelelezi zaidi; leo hii naweza kuagiza fulani akasomewe mashtaka, lakini kesho anakuja kukuonyesha vielelezo kwamba mimi nilitumwa tu kuchukua pesa. "

DPP Feleshi aliongeza kusema: "Hivyo, ni lazima uangalie upande wa pili wa shilingi. Nani kamtuma akachukue hizo fedha na yuko wapi..., au wewe (mwandishi) unapenda kuangalia upande mmoja tu wa shilingi na kufanya maamuzi?"

Alifafanua kwamba fedha hizo ambazo zote zimeibwa katika Akauti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu (BoT), zinahusisha makampuni 12 ikiwemo ya kigeni, hivyo haiwezi kuwa rahisi kubaini wahusika wakuu mara moja.

"Hivi kitu kinachohusisha makampuni 12 tena mengine ya nje unaweza kukifanya kwa urahisi kiasi hicho, unaangalia mtu anakwambia labda mimi nilitumwa tu, sasa hapa tunatafuta nani kamtuma," aliongeza DPP Feleshi.

Alisema ni hatari kwa ofisi yake kukurupuka kuchukua maamuzi ya kufikisha watuhumiwa wa Kagoda mahakamani bila ushahidi wa kutosha, kwani serikali inaweza kuangushwa katika kesi.

Feleshi alitoa wito kwa Watanzania kupeleka uthibitisho wa nani hasa ambaye ni mmiliki wa Kagoda na ofisi yake itamlinda mtoaji taarifa hiyo.

"Kama kuna mtu ana uthibitisho wa vielelezo alete, nitamlinda."

Feleshi alisema Kagoda ni kampuni tata inayohitaji upelelezi zaidi ambao bado unafanywa na Kurugenzi ya Upelelezi ya Makosa ya Jinai (DCI).
Wanasheria mnisaidie; fedha za EPA kupitia kagoda zimeibiwa Benki Kuu (BOT). Kisai cha Tsh. 40bil zimeibiwa kwa staili ya kuforgi nyaraka. DPP anasema walikuwa wanazichukua hizo fedha wanajulikana ila hawezi kuwashtaki eti walitumwa tu. Sasa anatafuta waliowatuma.
(a) amejuaje kwamba hao jamaa walitumwa?
(b) kama walitumwa si watakuwa wamewataja mabossi wao?
(c) fedha nyingi kiasi hicho si unaweza ku-trace kwa kuangalia bank transactions na kuzifuatilia akaunti husika?
(d) kama aliyewatuma ni Rais, au CCM, DPP atachukua hatua gani? atawaachia hao jamaa anaodai walitumwa?
 
Kagoda case closed.
Ukisikia mtu mkubwa kama Feleshi bila aibu anasema tumpelekee habari Kagoda ni nani wakati Mwanakijiji alimpa kila detail, sasa sijui anataka zipi zaidi.
Kamata RA atawataja wote aliokula nao. La sivyo amwache aendelee kutamba na afute kesi zile zingine zote ili sisi ikifika wakati tuamue nini la kuwafanya. Full stop. Wasituchezee akili.
 
sasa kama ulishamjua aliyekuja kuchukua pesa kwa nini usimuulize aliyemtuma kama yeye hausiki, maana hapa hapana logic hata kidogo kwa Bwana Feleshi kuomba watu wampelekee details za kagoda
 
Huyo DPP ni mzembe wa Kazi...
Hajui kwamba mkamatwa na Ngozi ndio mwizi? Ana uhakika gani na mambo aliyoambiwa kwamba walitumwa? Kama walitumwa, basi wapelekwe mahakamani wakathibitishe hilo la kutumwa kwao. Kama waliowatuma ni viongozi wa juu wa serikali , basi hawana budi kujiudhuru ili sheria ichukue mkondo wake... itakuwa jambo jema wakifuata nyayo za Lowasa ayeonyesha kuwajibika....
Kama DPP amekiri kwamba anawafahamu lakini anasema kwamba wametumwa.. atakuwa mzembe wa kutowafikisha mahakamani waliokutwa na ngozi, vinginevyo ataweka precedent kwa wahalifu wote wa wizi kwa wao kutoa kisingizio kama hicho pale tu wanapokamatwa na ataiweka serikali katika wakati mgumu sana kwa ubaguzi wa kuwashitaki walalahoi bila kwanza kuwatafuta wale waliowatuma...
Pia ikumbukwe kwamba, the onus of proof si ya DPP bali ya yule anayesema kwamba ametumwa... Sasa shida iko wapi kama wanajulikana...
 
sasa kama ulishamjua aliyekuja kuchukua pesa kwa nini usimuulize aliyemtuma kama yeye hausiki, maana hapa hapana logic hata kidogo kwa Bwana Feleshi kuomba watu wampelekee details za kagoda

Yeah, Mkuu siunaona anavyosema
"Hatufanyi mambo kwa kukurupuka, ndiyo maana nimeagiza upelelezi zaidi; leo hii naweza kuagiza fulani akasomewe mashtaka, lakini kesho anakuja kukuonyesha vielelezo kwamba mimi nilitumwa tu kuchukua pesa. "

sasa kama mtu analeta vielelezo kuwa alitumwa si ndo ushahidi wa kumkamata mhusika?
 
Wiiizi mtupu! hakuna mpango wowote wa kuwakamata wahusika. Wanajaribu kufunika kombe mwanaharamu apite. Bahati mbaya ni kwamba wanashindwa kusoma alama za nyakati.
 
Wanasheria mnisaidie; fedha za EPA kupitia kagoda zimeibiwa Benki Kuu (BOT). Kisai cha Tsh. 40bil zimeibiwa kwa staili ya kuforgi nyaraka. DPP anasema walikuwa wanazichukua hizo fedha wanajulikana ila hawezi kuwashtaki eti walitumwa tu. Sasa anatafuta waliowatuma.
(a) amejuaje kwamba hao jamaa walitumwa?
(b) kama walitumwa si watakuwa wamewataja mabossi wao?
(c) fedha nyingi kiasi hicho si unaweza ku-trace kwa kuangalia bank transactions na kuzifuatilia akaunti husika?
(d) kama aliyewatuma ni Rais, au CCM, DPP atachukua hatua gani? atawaachia hao jamaa anaodai walitumwa?
hakuna haja ya kujadili kagoda kama ufisadii kwani kwa ujumla wake CCM na serikali yake ndo waliotufikisha kwenye wizi wa aina hizii (ufisadi wa fedha na madaraka).

tunahitaji kuhamasisha maendeleo ya jumla kama maji safi na salama, elimu, afya, umeme, barabara, utawala bora, kilimo na viwanda na kukemea vipingamizi vyake kama vile uongozi mbovu(wizi, ulafi, uwezo mdogo) na sera na sheria kandamizi (katiba ya wote ipatikane) katika kufikia maendeleo hayooo...

hatuna haja ya kutoa nafasi kubwa ya media kuzungumzia feleshi na kagoda!!! haijengi wa kuhamasisha maendeleo ya msingi kwa mlalahoi..

inawezekana kuleta mabadiliko kwa kuwa na uongozi mbadala kuanzia kijiji hadi taifa..
maendeleo yanawezekana kwani iweje barabara za kuunganisha mikoa zijengwe ndani ya muda mfupi tena baadhi kwa kodi yetu..gafla leo hata umaliziaji wa km 5 (sam mujoma) ni taaabuuuu????

lagosi ilihamia abuja from nothing na leo miundo mbinu ya abuja ni ya kuigwaaa...waliwezajee???

CHANGE WE CAN BELIEVE IN..
 
Wanasheria mnisaidie; fedha za EPA kupitia kagoda zimeibiwa Benki Kuu (BOT). Kisai cha Tsh. 40bil zimeibiwa kwa staili ya kuforgi nyaraka. DPP anasema walikuwa wanazichukua hizo fedha wanajulikana ila hawezi kuwashtaki eti walitumwa tu. Sasa anatafuta waliowatuma.
(a) amejuaje kwamba hao jamaa walitumwa?
(b) kama walitumwa si watakuwa wamewataja mabossi wao?
(c) fedha nyingi kiasi hicho si unaweza ku-trace kwa kuangalia bank transactions na kuzifuatilia akaunti husika?
(d) kama aliyewatuma ni Rais, au CCM, DPP atachukua hatua gani? atawaachia hao jamaa anaodai walitumwa?
hakuna haja ya kujadili kagoda kama ufisadii kwani kwa ujumla wake CCM na serikali yake ndo waliotufikisha kwenye wizi wa aina hizii (ufisadi wa fedha na madaraka).

tunahitaji kuhamasisha maendeleo ya jumla kama maji safi na salama, elimu, afya, umeme, barabara, utawala bora, kilimo na viwanda na kukemea vipingamizi vyake kama vile uongozi mbovu(wizi, ulafi, uwezo mdogo) na sera na sheria kandamizi (katiba ya wote ipatikane) katika kufikia maendeleo hayooo...

hatuna haja ya kutoa nafasi kubwa ya media kuzungumzia feleshi na kagoda!!! haijengi wa kuhamasisha maendeleo ya msingi kwa mlalahoi..

inawezekana kuleta mabadiliko kwa kuwa na uongozi mbadala kuanzia kijiji hadi taifa..
maendeleo yanawezekana kwani iweje barabara za kuunganisha mikoa zijengwe ndani ya muda mfupi tena baadhi kwa kodi yetu..gafla leo hata umaliziaji wa km 5 (sam mujoma) ni taaabuuuu????

lagosi ilihamia abuja from nothing na leo miundo mbinu ya abuja ni ya kuigwaaa...waliwezajee???

CHANGE WE CAN BELIEVE IN..
 
Kama DPP bwan Feleshi anasema akimkamata mtu aliyechukua fedha za KAGODA haimsaidii kumpata mtu aliyemtuma mtu aliyechukua fedha basi hakuna haja ya yeye kuwepo kwenye cheo hicho kwa maana HAFAI
 
Ukitazama ukweli ni kwamba, Feleshi yupo sahihi kwa upande mmoja, yeye anaweza kuwapandisha mahakamani akiwa na uhakika tu kuwa wanastahili kupandishwa mahakamani.

Hapo inatakiwa ayapeleke haya mafaili kwa wanaohusika na uchunguzi wa mambo kama haya, nao ni a) Tume ya kuchunguza huu wizi kama ipo. b) TAKUKURU c) Polisi.

Wakimaliza uchunguzi yeye ndie aandae kesi ya kwenda kushinda. Akiipeleka hovyo mahakamani, hii mijitu kama imeweza kuchota mipesa yote namna hiyo, itamshinda kwa mbinu tu.

Hapa ilitakiwa JMK aunde tume huru ya Kuchunguza tena ni vizuri ikawa ni ya ki Mataifa na si ya kiTanzania pekee. kwani mifedha iliyochotwa inahusisha mataifa na makampuni mengine ya ukweli na hewa ya kimataifa.
 
absolutely amazing!!...unajua Tanzania ni Nchi yenye viongozi na system ya ajabu sijapata kuona!! nilipata kusema na ntarudia tena 'Hata tukaweka paka shume pale nyumba nyeupe, bado hilo li-nchi litakwenda tu'.
 
Tusipoteze muda kujadili kesi ya ngedere, hakimu nyani.
Tujadili mambo ya kutusaidia maishani mwetu.

Ila makosa ni yetu wenyewe kuendelea kuwapa wezi kusimamia mali za nchi kwa kuwachagua kila siku. Matatizo yote tunajitakia wenyewe. Tunahitaji kuombewa ili mapepo tuliyotupiwa yanayotulazimisha kuchagua kisichofaa kila wakati yatoke kwa jina la Yesu.
 
huyu msukuma feleshi ovyo sana!!

anadiliki kutwambia hiv?huu ujinga sana
 
Mambo mengine!! Hapa huyu DPP hakuwa na cha kusema, akaamua kusema chochote! Maneno kama haya, ni afadhali asingeongea tu kwa sababu inazidisha suspicion ya umma kwa viongozi wakuu.

Watu wanajua Kagoda ni nani kwani yameshaandikwa sana. Sasa unaposema hashitakiki kwa kuwa alitumwa, unazidi kuwachongea tuu. Mi naona afadhali angekaa kimya tu kuliko kuongea hicho alichoongea.

Sijui kama haya yana msaidia yeye au mkuu wake au nani!!! We are still too poor on the art of talking!
 
Feleshi is he serious kwamba ana ujue ukweli kwamba ni serikali iliyo mpa madaraka ilichota ili wakae madarakani ? Lakini Feleshi mwenyewe amekuwa mwana mtandao wa nguvu sana sasa leo mta shangaa haya asemayo ? Is this man corrupt as well ?
 
Feleshi is he serious kwamba ana ujue ukweli kwamba ni serikali iliyo mpa madaraka ilichota ili wakae madarakani ? Lakini Feleshi mwenyewe amekuwa mwana mtandao wa nguvu sana sasa leo mta shangaa haya asemayo ? Is this man corrupt as well ?

Lunyungu!

Pole sna usiumize kichwa chako bure Eliezer Feleshi ni mwanaharamu anatakiwa mashehe wamtoe majini kwa kumpepea halafu apelekwe kuombewa kanisani. Kwa umri mdogo aliokuwa nao akina Mwanyika na Mzee wa Vijisenti aka Bajaji walimweka pale alinde maslahi ya majambazi wa CCM and so far kwa their TOR anafanya kazi vizuri!!

Kama unamjua aliyetumwa kuchota pesa za Kagoda its game over unampeleka kwa Pilato kama atakataa kumtaja aliyemtuma si unamnyonga na zoezi haliishii hapo wote watakaokuja kuwawekea dhamana unaunganisha mpaka asubuhi!!

Huyu juha sijui ni msukuma au Mpare it doesn't matter hawa watu wanaojiita usalama wa TAIFA wako likizo nini!! I want to know watu waliomvet Feleshi na Dr. Idris Rashid wapelekwe mirembe au tuwakate vichwa do we still have state security au Pumba THAT is why siwezi kumsikiliza Pinda kwani hayo ndiyo matunda yake!!!
 
Feleshi is he serious kwamba ana ujue ukweli kwamba ni serikali iliyo mpa madaraka ilichota ili wakae madarakani ? Lakini Feleshi mwenyewe amekuwa mwana mtandao wa nguvu sana sasa leo mta shangaa haya asemayo ? Is this man corrupt as well ?

maneno yake yanaonyesha ni fisadi tu kama wenzake. Hatoshi kwenye kiti cha DPP, inapaswa aachie ngazi.
 
Back
Top Bottom