Pre GE2025 Kahama: Paul Makonda ataka Caroline apewe eneo la Serikali, Mkurugenzi asema kumiliki Ardhi ni jambo la kisheria sio siasa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Haraka haraka kwenye mada,

Mhe Paul Makonda, mwenezi wetu pole na hongera kwa kazi kubwa na nzuri unayoifanya katika kulijenga Taifa na chama

Ni Mimi Mabula Malunde Sitta.
Hii makala yako ina mambo matatu yanayojionyesha wazi.

Umeandika kumpa hongera Makonda lakini hakika yake umeonyesha kuwa yeye ni mkurupukaji ktk kufanya maamzi. Amegawa eneo la Serikali kwa mvamizi na msingiziaji ambae kashidwa mahakamani mara kadhaa, na viongozi wenzake wa ngazi za juu wanalijuwa hilo, lakini kwa hulka yake ya ukurupukaji kafanya maamuzi ya ovyo akiwa ktk jukwaa la kisiasa. Kwa maana nyingine Makonda amekuwa juu ya mahakama na sheria za nchi.

Pili, umemfagilia sana mkurugenzi wa almashahuri. Inaonyesha wazi una ama uhusiano fulani na huyu mkurugenzi au chuki na yule aliyegawiwa hicho kipande cha ardhi.

Tatu, umeandika kichawa sana. Utampaje hongera na sifa kiongozi ambae katoa maamuzi yasiyo sahihi? Pamoja na kukerwa kwako na hayo maamuzi ya Makonda, inaonyesha kuna jambo unalitafuta kupitia kwake.
 
Ata iyo kauli ya makonda ni kisiasa ime ishia jukwaani,,amna aja ya kujipa stress kuwaza waza hapa
 
.

Tatu, umeandika kichawa sana. Utampaje hongera na sifa kiongozi ambae katoa maamuzi yasiyo sahihi? Pamoja na kukerwa kwako na hayo maamuzi ya Makonda, inaonyesha kuna jambo unalitafuta kupitia kwake.

Mkuu Mimi nime copy & Paste toka kwenye group.
 
Haraka haraka kwenye mada,

Mhe Paul Makonda, mwenezi wetu pole na hongera kwa kazi kubwa na nzuri unayoifanya katika kulijenga Taifa na chama chetu Cha Mapinduzi, hakika unastahili pongezi kwa hili.
Nimependa sana uchapakazi wa huyu Mkurugenzi kama ni kweli kilichoandikwa hapa,


Kidumu Chama Cha Mapinduzi
 
"...hebu nitajie Halmashauri moja inayoongoza kwa ukusanyaji wa Mapato Tanzania kama sio Kahama tena hebu nitajie Halmashauri moja inayoongoza kwa miradi ya maendeleo kwa Fedha za ndani kama sio Kahama au hebu nitajie Wilaya moja inayoitwa Mkoa wa Kikodi hapa Tanzania kama sio Kahama."

1. Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo ilikusanya Tshs billioni 32 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023.

Bado kuna Halmashauri za Manispaa za Temeke na Kinondoni ambazo zilikusanya mapato kuizidi Manispaa ya Ubungo. Kwa hiyo Kahama bado ni mtoto tu kwenye kundi la Manispaa.

Halafu kuhusu ushindani wa makausanyo ya mapato, TAMISEMI wameweka Halmashauri katika makundi: Kuna Miji Midogo, Miji, Manispaa, Wilaya, na Majiji. Kahama ipo kundi la Manispaa, hata hivyo haiwezi kushika namba moja.

2. Kuhusu Wilaya ya Kahama kuwa Mkoa wa Kikodi pekee. Tarafa ya Kariakoo iliyopo Wilaya ya Ilala ni Mkoa wa Kikodi; Tarafa ya Mbagala iliyopo Wilaya ya Temeke ni Mkoa wa Kikodi. Mifano ipo mingi. Kwa hiyo siyo kweli.

3. Halmashauri ya Manispaa ya Kahama haikupandishwa hadhi kutoka Halmashauri ya Wilaya na kuwa Halmashauri ya Manispaa. Isipokuwa, Halmashauri ya Mji wa Kahama ndiyo uliopandishwa hadhi na kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama.

4. Ukisema kuna Halmashauri zinakuja Kahama kujifunza basi ni hivi, Kahama wenyewe madiwani walienda Manispaa ya Ubungo kujifunza namna ya kukusanya mapato haswa ya Stendi. Halmashauri nyingine zilizoenda Ubungo ni Mwanza Jiji, Ilemela MC, Tanga Jiji, na wengine wa kule Zanzibar. Hata Arusha Jiji walienda Ubungo.

5. Halmashauri zote nchini zenye mapato makubwa zikeruhusiwa na TAMISEMI kutumia sehemu ya mapato yake kufanya miradi ya maendeleo. Sasa hata kama Kahama inatumia sehemu ya mapato katika miradi ya ndani, haiwezi kuzizidi Halmashauri kama Temeke, Kinondoni na Jiji la Dar es Salaam zenye mapato mengi kuishinda Kahama.

Kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023 Kahama Manispaa ilijiwekea lengo la kukusanya bilioni 10.25 za Kitanzania wakati Manispaa ya Ubungo ilikusanya bilioni 32 za Kitanzania.
 
Mhe Paul Makonda, Mkurugenzi huyu kaitoa Kahama kwenye Halmashauri ya Wilaya hadi leo ni "Municipal council" Waswahili tunasema mnyonge mnyongeni lakini haki yake apewe
WEWE ndio unasema, sio sisi tunasema, speak for your damn self.

Mnyonge mnyongeni my foot! Kwa nini tumnyonge mnyonge? Na tukishamnyonga anapataje haki yake mtu keshakufa ?????

Kahama ina upekee wa kitakwimu sio kwa sababu ya Mkuu wa Wilaya, bali kwa sababu ya uchimbaji. Plain and simple. Who you think you are fooling here ?
 
Wamesema ni Mkurugenzi sio Mkuu wa Wilaya mkuu
 

1. Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo ilikusanya Tshs billioni 32 kwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023.


Je Kahama ilikusanya ngapi?
 

Huwa nasikia jambo kubwa ambalo Mkurugenzi wa Kahama kawazidi wengine ni Uaminifu na Uadilifu tu,

Nasikia jamaa Kila wakimpekua wanakuta mikono yake ni safi,

Ndio maana unaona tuhuma zake ni za kisiasa siasa tu
 
1. Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo ilikusanya Tshs billioni 32 kwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023.


Je Kahama ilikusanya ngapi?
Hapo sasa. Nilitarajia mtoa mada ulete data za Kahama kwa sababu mimi sina ila nina uhakika Ubungo yenye kata 14, imeipiku Kahama kwa sababu, mwaka wa fedha 2021/2022 Manispaa ya Ubungo ilikusanya bilioni 27 za Kitanzania, na kushika nafasi ya 3 katika kundi la Manispaa ikitanguliwa na Manispaa za Temeke na Kinondoni.
 
Uchungu Gani unaosemea Mzee baba. Ana matumizi mabaya ya fedha cc: kipindi Cha Magufuli alifanya manunuzi ya gari 400M
 
Ohoo, sawa! Basi aliyeandika hili bandiko hakuwa huru kuusema ukweli. Kuna vitu vinamtatiza kwenye utendaji wa Makonda lakini akaamua kutonyooka. Unajua tena, uchaguzi uko mita moja tu mbele, watu wanaogopa kukatwa. Lakini niwahakikishie Samia si kama mwendazake aliyewaachia uwanja mpana wa maamzi Polepole na Bashiru.
 
Mheshiwa nyingi km ugoro... Viongozi wa vyama siyo waheshimiwa..
 
1. Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo ilikusanya Tshs billioni 32 kwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023.


Je Kahama ilikusanya ngapi?


Kipindindi cha mwaka wa fedha 2022/203 Kahama ilijiwekea lengo la kukusanya Tshs billioni 10.25.

Kwa hiyo assume Kahama ilikunya kiasi hicho, na Ubungo ilikusanya billion 32.
 
Wamesema ni Mkurugenzi sio Mkuu wa Wilaya mkuu

Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya, Katibu Tawala wa Wilaya....

Distinction without a difference

Point is, Kahama stands out in developmental statistics strictly because of massive mining industry. Simple as. Si kwa sababu ya bureaucrats Halmashauri ya Manispaa ya Kahama.
 
Kwani Tarime hakuna mining, Geita Je? Don't be bias
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…