Kahama VS Njombe/Mafinga

makambako tc kazi zinaendelea mradi wa viwanda vya chuma unazidi kuchochea Kasi ya uwekezaji wa sector tofauti hospital na hotel
 
Diwani wa kata ya Kitandililo katika Halmashauri ya mji wa Makambako wilayani Njombe Imani Fute ameliomba taifa la china kuisaidia Tanzani kupata soko la parachichi, chai,korosho na ufuta.

Fute ametoa ombi hilo akiwa nchini china kwenye semina ya diplomasia ya uchumi wakati akizungumza katika semina hiyo yenye wawakilishi 42 kutoka mataifa 11 duniani, ambapo ameiomba china iisaidie Tanzania kwenye soko la mazao hayo huku akitaka ije iwekeze kwenye soko la kimataifa Makambako ambalo eneo limetengwa.

Fute amesema ombi hilo ni kutokana na jitihada za Rais Dkt.Samia Suluhu Hasan katika kukuza uchumi wa wananchi na Taifa letu.

#IceFmHabari
#NisikilizeMimi
Na @cleefmlelwah
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…