Kahama VS Njombe/Mafinga

Kahama VS Njombe/Mafinga

Je unajua kuwa kahama ilikuwa inashika namba mbili kitaifa ya kwanza ikiwa ni ilala?
Hahaha! Eti nimeishi miaka mitatu alafu unabwabwaja sisi wazawa tusemeje?
.
Mwanza-Shinyanga ni KM 141 na si chache ni nyingi mnooo ni masaa mawili hadi matatu kwa gari.
Njombe ni porini kumejificha watu ni washamba, Kahama wajanja wengi alafu sio wasukuma tu wametoka maeneo mbalimbali ya nchi na jirani
Hebu acheni kulinganisha njombe mkoa na vitu vya ajabu ajabu. Takwimu za kiuchumi zinaonesha njombe ya 3 harafu ulinganishe na kiwilaya sijui cha wapi huko. Kwenye takwimu za kiuchumi kilikuwa cha ngapi na je watu wake wapoje kimaendeleo. Kahama ingekuwa ipo vizuri ingekuwa mkoa basi
 
Je unajua kuwa kahama ilikuwa inashika namba mbili kitaifa ya kwanza ikiwa ni ilala?
Wewe hujui kitu unaandika story za vijiweni unazosikia Kwan watu.Hebu tafuta takwimu sahihi kutoka sehemu sahihi

1.Ilala
2.Mufindi
3.....

Mufindi n ya pili kwa wingi wa viwanda baada ya Ilala.Huko Kuna viwanda vingi Sana vya magogo,mbao,na chai.Ndio sababu inatajwa Mafinga kwasababu n Makao makuu ya Wilaya ya Mufindi
 
Wewe hujui kitu unaandika story za vijiweni unazosikia Kwan watu.Hebu tafuta takwimu sahihi kutoka sehemu sahihi

1.Ilala
2.Mufindi
3.....

Mufindi n ya pili kwa wingi wa viwanda baada ya Ilala.Huko Kuna viwanda vingi Sana vya magogo,mbao,na chai.Ndio sababu inatajwa Mafinga kwasababu n Makao makuu ya Wilaya ya Mufindi
Yani Mufindi inaizidi hadi wilaya ya kibaha?😂
 
Sijasema inalingana no ila inatembea speed kiukuaji kuliko Iringa na Njombe
Umeanza kulinganisha manispaa na wilaya ambayo haijafikia hata hadhi ya kuitwa mji?
.
Endelea kulinganisha Kahama mji na njombe mji kumbuka ulisema hakuna mahotel kahama marefu nikakuonyesha yani Njombe imefunikwa na kahama
 
Kwahiyo hao watu wa Lindi ndo watakuwa wamelala? Kwamba hawatazaliana, hawatafanya biashara, hawatawekeza?
Lindi, na Njombe uchawi mwingi watu hawapendi maendeleo wanaroga sanaaa, hii tabia Rukwa naon wameiacha sasa wanapiga hatua ndefu za maendeleo.
.
Njombe wanaroga hadi mimba kwa hiyo watu hawaendi kuanzisha maisha kule bali kuyatafuta na kuhepa, Lindi watu wanakaa vibarazani kuanzia asubuh hadi linachwea hupotea mida ya kula tu na ukijifanya mjuaji unaleta vimaendeleo unapigwa juju afadhali Ruangwa naiona ikija kuitoa Lindi manispaa
 
Mkuu,kutoka Mza to Shy,ni km 164, pia kahama inazidiwa na wilaya nyingi sana kimiundo mbinu,mfano Nzega ,Karagwe,Ngara,Korogwe,Kahama wameshindwa kujenga mitaa kwa kiwango cha Lami,kama wilaya nilizo taja japo hazina vyanzo vikubwa kama kahama,mfano wakati wa masika ukiwa majengo ,nyasubi,igomelo, nk,inabidi uvue viatu na ukunje suluali,Kahama sitendi kuu ya Mabasi ni aibu,sijui hata Buzwagi ikifungwa leo watabaki na kipi cha kujivunia?labda kituo cha Afya kilichopo kalibu na Mgodi Mwendakulima,Kahama inatia aibu.
Yani nzega kamji kapo stend tu pale unalinganishana kahama mji?
Karagwe na Ngara hata usingepataja nakujua sanaaa hapalingani na Kahama hata kidogo kwa kila kitu.
.
Korogwe sijafika naiona tu kwenye picha tena stendi yao ilivyo nzuri, ni kweli Kahama stendi yao ni aibu ila watafanya nini sasa? Geita yenyewe yenye listend kubwa wakati ikiwa Wilaya ilikuwa na stend ya ajabu ya vumbi
.
Hujaitendea haki kuilinganisha Kahama na Ngara pamoja na Karagwe huku bado sana yani wanazidiwa hela hadi wingi wa watu.
.
La mwisho MZA- SHY ni KM 141 tu hizo habari zenu za kuangalia Google mnafeli vingi
 
lakini kwa maoni yangu kahama inakuwa coz ya dhahabu na madini, ila hio madini ikiisa taabu, ukiangaria miji kaa njombe na mafinga they have bright future coz wanategemea kilimo sana, na ile kitu wanastahili wafanye ni kulima kwa njia za kisasa(PRECISION AGRICULTURE) alafu wawekeze kweye proccesing industries, ha hizo watakuwa mbele kabisa
Siku mvua na baridi la Njombe zikiiisha ndio siku madini ya Kahama yani ule ukanda wote yataisha sasa sijui mvua itaacha kuny'esha lini
 
Umeanza kulinganisha manispaa na wilaya ambayo haijafikia hata hadhi ya kuitwa mji?
.
Endelea kulinganisha Kahama mji na njombe mji kumbuka ulisema hakuna mahotel kahama marefu nikakuonyesha yani Njombe imefunikwa na kahama
Mafinga ni Town council toka kitambo sana unless hujui na saizi iko kwenye process ya kuwa manispaa maana vigezo karibu vyote inavyo
 
Siku mvua na baridi la Njombe zikiiisha ndio siku madini ya Kahama yani ule ukanda wote yataisha sasa sijui mvua itaacha kuny'esha lini
Aisee kungekuwa kuna madini kihivyo nadhani ingekuwa city kitambo sasa ni rubbish tu hamna kitu,madini unachimbia mitambo sio sululu
Chunya kwenye madini mchina kaweka smelter kwa nini wasijenga Kahama
 
Mafinga ni Town council toka kitambo sana unless hujui na saizi iko kwenye process ya kuwa manispaa maana vigezo karibu vyote inavyo
😂😂😂😂 yani Mafinga iwe manispaa na Njombe itakuwa nini? Wewe jamaa si ndio ulikuwa hutaki masikhara sasa mbona unayaleta?
.
Yani Manispaa ya Tabora kule Toronto kuwe sawa na Mafinga? Hata njombe haina hadhi ya manispaa ndio maana bado inaitwa Njombe mji
 
Aisee kungekuwa kuna madini kihivyo nadhani ingekuwa city kitambo sasa ni rubbish tu hamna kitu,madini unachimbia mitambo sio sululu
Chunya kwenye madini mchina kaweka smelter kwa nini wasijenga Kahama
Hivi kuna sehemu gani Tanzania tofauti na Kahama na Geita inayotoa dhahabu nyingi Tanzania?
 
mie sijaja huku kupiga selfie km ww mkuu!hahaha hatuendani kbs kiakili mm na ww..yaan nianze kupiga picha majengo ya kahama😂😂..mimi huyu??
😆😆😆😆 Kubali tu hakuna cha kupiga hakuna battle bila picha.piga hata mashimo ya machimbo mkuu
 
😂😂😂😂 yani Mafinga iwe manispaa na Njombe itakuwa nini? Wewe jamaa si ndio ulikuwa hutaki masikhara sasa mbona unayaleta?
.
Yani Manispaa ya Tabora kule Toronto kuwe sawa na Mafinga? Hata njombe haina hadhi ya manispaa ndio maana bado inaitwa Njombe mji
Unaelewa maana ya kuwa kwenye mchakato?
Manispaa za Lindi,Singida,Sumbawanga,Songea,Shinyanga,Kigoma na Mpanda zimeizidi nini Mafinga na Njombe? Kwa nini zinaitwa manispaa councils?
Kwa taarifa yako manispaa zijazo kabla ya mkulu kusepa ni Njombe,Mafinga,Mbozi(Mlowo+Vwawa),Tunduma,Kahama,Kasulu na Mbalizi itakayokuwa sehemu ya jiji la Mbeya
City councils zitakuwa Moshi,Morogoro,Iringa
 
Hivi kuna sehemu gani Tanzania tofauti na Kahama na Geita inayotoa dhahabu nyingi Tanzania?
Chunya mchina kajenga hadi smelter/kichenjulio tatizo lenu mumeganda huko mazizini mnajua dunia yote iko usukumani.Kwa taarifa yako ukiacha machimbo ya Chunya,watu wanatoka Msumbiji kuja kuuza madini soko la Chunya
 
Unaelewa maana ya kuwa kwenye mchakato?
Manispaa za Lindi,Singida,Sumbawanga,Songea,Shinyanga,Kigoma na Mpanda zimeizidi nini Mafinga na Njombe? Kwa nini zinaitwa manispaa councils?
Kwa taarifa yako manispaa zijazo kabla ya mkulu kusepa ni Njombe,Mafinga,Mbozi(Mlowo+Vwawa),Tunduma,Kahama,Kasulu na Mbalizi itakayokuwa sehemu ya jiji la Mbeya
City councils zitakuwa Moshi,Morogoro,Iringa
Sijawahi kuona Mkoa wenye manispaa zaidi ya moja Tanzania ila kuna majiji yenye manispaa zaidi ya moja mfano Mwanza ma DSM.
.
Singida, Shinyanga, Kigoma na Sumbawanga acha kuziringanisha na uchafu kama Njombe na wilaya yake Mafinga.
.
Yani hapa umegusa pabaya tuendelee kulinganisha Njombe, Lindi na Kahama tu, Mikoa uliyoitaja ni level zingine nikikuwekea picha utalia
 
mie hizo chocho zote bahat nzuri nilipita labda uniambie ww unawaza kusafirisha kilo 300 za maharage kuja dar kama unamaanisha hvyo well n good sasa ww gusa kupata vibali vya kusafirisha asali walau iende Malaysia àu kuexport🍓Uond mzunguko wake ulivyo...utasumbuka wee mwisho wa siku wanaoexport hizi ishu ni watoto wa vibosile wenye connections zao hapa mjini..mie kusafisha mazao kutoka mkoa m1 kwenda mwingine sitak..! ! sijui lakini..!

Wenzetu +254 wanaexport had cabbage..mikabeji ya huko kwenu inaoezeana tu!
Na mm nataka kwa hali na mali nifike kwa hao wachche unaowasema ww!
Endeleeni kujidanganya kwamba kilimo ni uti wa mgongo! labda!
Mzee baba sie kilimo cha kisasa hatuachi kwa vile ni sustanable mambo ya sehemu ya changamoto ambazo zinaendelea kutatuliwa na serikali hata kwenye mazao ya misitu kuna kodi zaidi ya 30 lakini serikali inazidi kuzitatua
Kwamba tuendako soko la mbao soft wood litapotea nk hizo ni hadithi lingeanza kupotea kwa waliotuletea hiki kilimo yaani wazungu.Yaani unatakiwa kusema kwamba tunakoelekea horticulture ndio inakwenda kuwa hot industry ungeeleweka boss
 
Back
Top Bottom