Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Juma, Naomba Usiruhusu Udhalilishaji Huu Ndani ya Mahakama Zetu!.

Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Juma, Naomba Usiruhusu Udhalilishaji Huu Ndani ya Mahakama Zetu!.


Wanabodi,

Tanzania ni nchi yenye katiba inayoendeshwa kwa misingi ya haki, the rule of law kwa kufuata misingi ya sheria, taratibu na kanuni. Kwenye kila jambo linatekelezwa kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni, mahakamani ni mahali pa kutoa haki, tunaomba usiruhusu vyumba na maeneo ya mahakama kutumika kuwa ni sehemu ya udhalilishaji wa watuhumiwa!. Status ya Watuhumiwa wowote mbele ya sheria ni innocent until proven guilt!. Kwa nini watuhumiwa wadhalilishwe tena mbele ya kamera huku wakipigwa picha na video?!.

Tanzania inafuata mfumo wa sheria wa ya Uingereza, common law, ambapo mtuhumiwa huhesabiwa not guilt until proven guilt. Mfumo huu hauruhusu kuwapiga picha watuhumiwa wowote wakiwa mikononi mwa polisi au ndani ya vyumba vya mahakama. Lengo la kuzuia ni ili kuwaepushia watuhumiwa kuhukumiwa na media, "media trial".

Kitendo walichofanyiwa watuhumiwa hawa wawili, Rugemalila na Sing kuchuchumalishwa chini mbele ya camera za waandishi, ni udhalilishaji wa hali ya juu ya haki za watuhumiwa na ni kinyume cha sheria, taratibu na kanuni!.

Lengo la watuhumiwa kuchuchumalishwa, ni wale watuhumiwa wanaoshikwa kwa kufanya fujo, hivyo huchuchumalishwa ili kuwazuia wasitoroke chini ya ulinzi, hivi kweli Rugemalila na umri ule, na Singasinga na unene ule, walikuwa na tishio lolote la kutoroka chini ya ulinzi hadi kuwa chuchumalisha?!.

Sio mara moja au mbili, watuhumiwa wanafolenishwa na kupigwa picha mikononi mwa polisi. Watuhumiwa wanapigwa picha ndani ya vyumba vya mahakama!. Huu ni ukiukwaji wa haki za watuhumiwa!.

Tanzania – Code of Ethical Practice for media photographers and ...

"Contravene laws or lawful orders prohibiting the taking for pictures in the precincts for courts. The law prohibits the taking of pictures of any person (Judges, jurors and witnesses) involved in a proceeding before the court, whether civil or criminal; or to publish any photograph taken in contravention of the order. It could be in the courtroom, in the precincts of the building in which the court is held, or the persons leaving or entering the precincts".

Kwa msio fahamu, hata watuhumiwa nao ni binadamu na haijalishi wamefanya kosa gani, nao wanastahili heshima na utu wa ubinaadamu wao na sio kudhalilishwa. Watuhumiwa wana haki zao ambao zinapaswa ziheshimiwe.

Hata wahalifu wanaohukumiwa kunyongwa, pia wana haki zao zinazopaswa kuheshimiwa. Mfano mtu aliyehukumiwa kunyongwa mpaka kufa, japo lengo ni afe, kabla adhabu hiyo haijatekelezwa kwanza daktari ataitwa na kumpima akikutwa na ugonjwa wowote, adhabu ile haitekelezwi hadi atibiwe apone kabisa akiwa fit ndipo anyongwe hadi kufa. Kumnyonga mtu mgojwa ni kumuonea!. Kabla ya kunyongwa viongozi wa dini huitwa kumsalisha sala ya toba, kumuungamisha na kumuombea dua na kama ni Muislamu hutazamishwa kibla ndipo hunyongwa!. Lengo la kueleza haya ni kuonyesha kuwa hata wahalifu wana haki.

Hivyo ni ombi maalum kwa Kaimu Jaji Mkuu wetu, Dr. Ibrahim Juma, tunakuomba please usiruhusu maeneo ya mahakama na vyumba vya mahakama kutumika kama sehemu ya udhalilishaji utu wa watuhumiwa huu unaofanywa wanapokuwa mikononi kwa polisi na ndani ya vyumba vya mahakama zetu!.

Ndani ya vyumba vya mahakama za Uingereza, India na Afrika Kusini, watuhumiwa hawaruhusiwi kupigwa picha wakiwa ndani ya vyumba vya mahakama, au mikononi mwa polisi. Kama sisi tumerithi sheria za Uingereza, kwa nini tuende kinyume cha wenzetu, unless kwa kufanya hivyo, ndio maendeleo yenyewe!.

Kitendo cha kuwapiga picha watuhumiwa ndani ya vyumba vya mahakama, huku kamera za video zikiwamulika, ni kama kuwahukumu kupitia kitu kinachoitwa "media trial", mtu akiishaonyeshwa kwenye TV ni jambazi, hata akijakukutwa hana hatia, mtaani kila apitapo, watu watanyoosheana vidole, "jambazi yule!"

Naamini polisi wanajua kumpiga picha mtuhumiwa mikononi mwa polisi ni kinyume cha kanuni, kumpiga picha mtuhumiwa akiwa ndani ya chumba cha mahakama ni kinyume cha kanuni, kwa nini haya yanafanyika na tunayanyamazia wakati sheria, taratibu na kanuni zipo wazi?!.

Wanasheria mliopo jf mtatusaidia kwa hili kama tulibadilishwa kutoka kufuata the common law or English Law into American law.

Nimetokea kumfahamu Prof. Ibrahim Juma kwa karibu na sina mashaka kabisa na uadilifu wake katika kutenda haki na kutoa haki ili tuu sio haki itendeke bali pia haki kuonekana imetendeka, "Justice must not only be done but must be seen to be done".

Paskali.
Rejea
Utetezi wa kutetea haki za binaadamu humu jf, sikuanza leo, na wala siwatetei hawa kwa sababu ni matajiri, nimepigia kelele siku nyingi na haya chini ni mabandiko yangu kutetea haki
1. Bango la "Mwizi Mkenya!" Mlimani City ni Ubaguzi!, Udhalilishaji ...

2. Watetezi Wa Kweli wa Haki za Binaadamu Tanzania ni Kina Nani ...

3. Huu ni udhalilishaji wa Polisi kuwavisha mabango watuhumiwa ...

4. Anachofanya Waziri Mkuu, sio sawa, sio haki, sio good governance ...

5. Tukio zima la wachawi wawili waliodondoka na ungo huko kahama ...

6. ITV na "Morbid Curiosity", Very Unprofessional! | JamiiForums ...

7. Siku ya Kupinga Adhabu ya Kifo | JamiiForums | The Home of Great ...

8. Nini hasa maana ya utu? | Page 6 | JamiiForums | The Home of Great ...

9. Swali kuhusu ma-fumanizi, na reaction za wafumaniaji ...

10. Mchawi akamatwa jijini Dar na kuuawa baada ya kudondoka na ungo ...

11. IGP Mwema, Please, Please, Please, Stop This Police Brutality ...

12. Vifo vya Mahabusu Mwanza, IGP Mangu, Usikubali Kudanganywa ...

13. Waziri Nchimbi na IGP Mwema, Mnasubiri Nini Kujiuzulu? | Page 2 ...

14. TISS ni Watekaji, Watesaji na Wauaji!. Wasijadiliwe na Bunge bali ...

15. Chan. Ten:Inastahili Pongezi kwa "Freedom of Expression, Watangaza ...

16. Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na ..

17. Police Brutality in Tanzania: The World has a Right to know ...

18. Character Assassination ni Modus Oparandi ya Madikiteta Katili .

19. Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...

20. Katazo la Rais Kusafiri Nje ya Nchi bila Vibali: Je, Halikiuki .

21. Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote .

22. Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...

23. Naibu Spika Anna Makinda ni Dikteta! |

24. Je, Huu Sio Uvunjaji wa Haki Za Msingi za Binaadamu Unaofanywa na ...

25. Kutoka Geneva: Prof Mchome atoa msimamo kuhusu mpango wa ..

26. Je, Kila utumbuaji ni wa haki, au kuna kumkomoa Kikwete .

27. Kagoda: Kamwe haitafikishwa Mahakamani! | J

28. Kitendo Cha Rev. Mtikila Kugomea Arrest!, Kinastahili Pongezi ...

29. Wito kwa Baba *****: Watendee Haki Kina ***** Wote Ili Nao Wapate ...

30. Udhalimu wa Waarabu Zanzibar na Pemba: Ndugu zetu wali-teswa ...

Hata mimi naamini uliyoyasema ni kweli, lakini nikushukuru kwa kitendo ulichokifanya baada ya kumaliza hoja yako cha kuturejesha kwenye maandiko uliyowahi kuyatoa katika mazingira ya namna hii, maana kuna uzi humu ndani unauliza kama wewe ulikuwa kwenye payroll ya Rugemarila. Sasa na tamka bila shaka yeyote kuwa wewe ni mtetezi wa haki za msingi za binadamu. Hongera sana.
 
I agree with you on this Pascal: "A person is innocent until proven guilty". Hawa watuhumiwa wawili hawana hatia mpaka mahakama itakaposema kuwa wana hatia na kuwapa hukumu stahiki.
 
Pascal upo sahihi 100%. Mahakama ni lazima ikemee na izuie uholela katika mazingira ya mahakama. Lakini pia hata huko mahabusu na magerezani wahusika wafuatilie kuona kama mahabusu na wqfungwa kama wanatendewa haki.

Lazima tupige vita Taifa kuwa na taratibu za hovyo na holela.
 
Dah! Nilifikiri ni mimi tu nimeliona, kutokana na muhemuko wa hili Jambo nikaona ngoja nikae kimya, ni kweli hao jamaa wanatuhumiwa kwa kuhujumu uchumi lakini sikuona sababu yoyote ile ya kuwadharirisha, sasa walipiga magoti ili iweje??

Hivi hakuna kweli aliyejisaidia Haja Big pale?
 
Naona kuna Watu mmeamua kujitoa mhanga 100% katika awamu hii. Haya jamani kila la kheri na yangu macho tu.
 
Mayala ni gt mno humu jf na tunakutegemea.
Mada inayostahili kuanzishwa na wewe humu, inatakiwa "ichote" hadhira sawasawa. Hii ya kutetea mibaka uchumi unatugawa mashabiki wako.
Hiyo common law unayoitetea ina upande mmoja tu wa shilingi, haina upande wa pili.
Ninamaanisha kuwa sheria hiyo ni mahsusi kwa kutetea wahalifu tu, ama tuseme ipo ki haki za binadamu.
Unavyodai kuwa mwizi hawezi kuitwa mwizi hadi hapo mahakama itakapomtia hatiani. Msemo huo unajenga swali, je mwizi akiishatiwa hatiani, ulishawahi hata siku moja kusikia ameitwa mwizi? Baada ya kutiwa hatiani huwekewa "kava" tena na kuitwa mfungwa kwa tuhuma ya wizi a,b,c. Lakini kwa kutiwa kwake hatiani hairuhusiwi kumuita mwizi. Hakuna wakati wowote ambao mwizi anastahili kuitwa mwizi.
Vyombo vya habari kuwaita hao watuhumiwa wezi viko sahihi, kwa kuwa hapa Tanzania matendo maovu yanayofanywa na jamii huwa hairuhusiwi mahali popote kutumia hicho kiambishi katika uhuru wa kujieleza ama kutoa habari ya matendo ya watu hao.
Kwa nyie wasomi mgetunga kiswahili cha kuweza kutumia kutofautisha maneno.
Pia hili la kuchuchumalishwa nalo umelichambua kiubaguzi na kiutetezi zaidi. Kwani 'pozi' hilo hajawahi kufanyiwa mtuhumiwa mwingine ama sheria za ulinzi za askari jela wakiwa na mtuhumiwa "muhimu" hapo mahakamani zinasemaje?
Tunapokuwa kwenye kadhia kubwa za namna hii kitaifa nyie gt's tusaidieni kutudadavulia ili twende sote. Maana wengine tunaona lakini hatuelewi kinachoendelea. Sasa inapofika sehemu gt tegemeo unaanza kupanua ubawa ili kukinga hao mibaka, kwa kauli yoyote ile, sisi wepesi wa kubandika watu vyeo, moja kwa moja tunakuweka upande wa kina TL. Au unabishi?
 

Wanabodi,

Tanzania ni nchi yenye katiba inayoendeshwa kwa misingi ya haki, the rule of law kwa kufuata misingi ya sheria, taratibu na kanuni. Kwenye kila jambo linatekelezwa kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni, mahakamani ni mahali pa kutoa haki, tunaomba usiruhusu vyumba na maeneo ya mahakama kutumika kuwa ni sehemu ya udhalilishaji wa watuhumiwa!. Status ya Watuhumiwa wowote mbele ya sheria ni innocent until proven guilt!. Kwa nini watuhumiwa wadhalilishwe tena mbele ya kamera huku wakipigwa picha na video?!.

Tanzania inafuata mfumo wa sheria wa ya Uingereza, common law, ambapo mtuhumiwa huhesabiwa not guilt until proven guilt. Mfumo huu hauruhusu kuwapiga picha watuhumiwa wowote wakiwa mikononi mwa polisi au ndani ya vyumba vya mahakama. Lengo la kuzuia ni ili kuwaepushia watuhumiwa kuhukumiwa na media, "media trial".

Kitendo walichofanyiwa watuhumiwa hawa wawili, Rugemalila na Sing kuchuchumalishwa chini mbele ya camera za waandishi, ni udhalilishaji wa hali ya juu ya haki za watuhumiwa na ni kinyume cha sheria, taratibu na kanuni!.

Lengo la watuhumiwa kuchuchumalishwa, ni wale watuhumiwa wanaoshikwa kwa kufanya fujo, hivyo huchuchumalishwa ili kuwazuia wasitoroke chini ya ulinzi, hivi kweli Rugemalila na umri ule, na Singasinga na unene ule, walikuwa na tishio lolote la kutoroka chini ya ulinzi hadi kuwa chuchumalisha?!.

Sio mara moja au mbili, watuhumiwa wanafolenishwa na kupigwa picha mikononi mwa polisi. Watuhumiwa wanapigwa picha ndani ya vyumba vya mahakama!. Huu ni ukiukwaji wa haki za watuhumiwa!.

Tanzania – Code of Ethical Practice for media photographers and ...

"Contravene laws or lawful orders prohibiting the taking for pictures in the precincts for courts. The law prohibits the taking of pictures of any person (Judges, jurors and witnesses) involved in a proceeding before the court, whether civil or criminal; or to publish any photograph taken in contravention of the order. It could be in the courtroom, in the precincts of the building in which the court is held, or the persons leaving or entering the precincts".

Kwa msio fahamu, hata watuhumiwa nao ni binadamu na haijalishi wamefanya kosa gani, nao wanastahili heshima na utu wa ubinaadamu wao na sio kudhalilishwa. Watuhumiwa wana haki zao ambao zinapaswa ziheshimiwe.

Hata wahalifu wanaohukumiwa kunyongwa, pia wana haki zao zinazopaswa kuheshimiwa. Mfano mtu aliyehukumiwa kunyongwa mpaka kufa, japo lengo ni afe, kabla adhabu hiyo haijatekelezwa kwanza daktari ataitwa na kumpima akikutwa na ugonjwa wowote, adhabu ile haitekelezwi hadi atibiwe apone kabisa akiwa fit ndipo anyongwe hadi kufa. Kumnyonga mtu mgojwa ni kumuonea!. Kabla ya kunyongwa viongozi wa dini huitwa kumsalisha sala ya toba, kumuungamisha na kumuombea dua na kama ni Muislamu hutazamishwa kibla ndipo hunyongwa!. Lengo la kueleza haya ni kuonyesha kuwa hata wahalifu wana haki.

Hivyo ni ombi maalum kwa Kaimu Jaji Mkuu wetu, Dr. Ibrahim Juma, tunakuomba please usiruhusu maeneo ya mahakama na vyumba vya mahakama kutumika kama sehemu ya udhalilishaji utu wa watuhumiwa huu unaofanywa wanapokuwa mikononi kwa polisi na ndani ya vyumba vya mahakama zetu!.

Ndani ya vyumba vya mahakama za Uingereza, India na Afrika Kusini, watuhumiwa hawaruhusiwi kupigwa picha wakiwa ndani ya vyumba vya mahakama, au mikononi mwa polisi. Kama sisi tumerithi sheria za Uingereza, kwa nini tuende kinyume cha wenzetu, unless kwa kufanya hivyo, ndio maendeleo yenyewe!.

Kitendo cha kuwapiga picha watuhumiwa ndani ya vyumba vya mahakama, huku kamera za video zikiwamulika, ni kama kuwahukumu kupitia kitu kinachoitwa "media trial", mtu akiishaonyeshwa kwenye TV ni jambazi, hata akijakukutwa hana hatia, mtaani kila apitapo, watu watanyoosheana vidole, "jambazi yule!"

Naamini polisi wanajua kumpiga picha mtuhumiwa mikononi mwa polisi ni kinyume cha kanuni, kumpiga picha mtuhumiwa akiwa ndani ya chumba cha mahakama ni kinyume cha kanuni, kwa nini haya yanafanyika na tunayanyamazia wakati sheria, taratibu na kanuni zipo wazi?!.

Wanasheria mliopo jf mtatusaidia kwa hili kama tulibadilishwa kutoka kufuata the common law or English Law into American law.

Nimetokea kumfahamu Prof. Ibrahim Juma kwa karibu na sina mashaka kabisa na uadilifu wake katika kutenda haki na kutoa haki ili tuu sio haki itendeke bali pia haki kuonekana imetendeka, "Justice must not only be done but must be seen to be done".

Paskali.
Rejea
Utetezi wa kutetea haki za binaadamu humu jf, sikuanza leo, na wala siwatetei hawa kwa sababu ni matajiri, nimepigia kelele siku nyingi na haya chini ni mabandiko yangu kutetea haki
1. Bango la "Mwizi Mkenya!" Mlimani City ni Ubaguzi!, Udhalilishaji ...

2. Watetezi Wa Kweli wa Haki za Binaadamu Tanzania ni Kina Nani ...

3. Huu ni udhalilishaji wa Polisi kuwavisha mabango watuhumiwa ...

4. Anachofanya Waziri Mkuu, sio sawa, sio haki, sio good governance ...

5. Tukio zima la wachawi wawili waliodondoka na ungo huko kahama ...

6. ITV na "Morbid Curiosity", Very Unprofessional! | JamiiForums ...

7. Siku ya Kupinga Adhabu ya Kifo | JamiiForums | The Home of Great ...

8. Nini hasa maana ya utu? | Page 6 | JamiiForums | The Home of Great ...

9. Swali kuhusu ma-fumanizi, na reaction za wafumaniaji ...

10. Mchawi akamatwa jijini Dar na kuuawa baada ya kudondoka na ungo ...

11. IGP Mwema, Please, Please, Please, Stop This Police Brutality ...

12. Vifo vya Mahabusu Mwanza, IGP Mangu, Usikubali Kudanganywa ...

13. Waziri Nchimbi na IGP Mwema, Mnasubiri Nini Kujiuzulu? | Page 2 ...

14. TISS ni Watekaji, Watesaji na Wauaji!. Wasijadiliwe na Bunge bali ...

15. Chan. Ten:Inastahili Pongezi kwa "Freedom of Expression, Watangaza ...

16. Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na ..

17. Police Brutality in Tanzania: The World has a Right to know ...

18. Character Assassination ni Modus Oparandi ya Madikiteta Katili .

19. Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...

20. Katazo la Rais Kusafiri Nje ya Nchi bila Vibali: Je, Halikiuki .

21. Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote .

22. Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...

23. Naibu Spika Anna Makinda ni Dikteta! |

24. Je, Huu Sio Uvunjaji wa Haki Za Msingi za Binaadamu Unaofanywa na ...

25. Kutoka Geneva: Prof Mchome atoa msimamo kuhusu mpango wa ..

26. Je, Kila utumbuaji ni wa haki, au kuna kumkomoa Kikwete .

27. Kagoda: Kamwe haitafikishwa Mahakamani! | J

28. Kitendo Cha Rev. Mtikila Kugomea Arrest!, Kinastahili Pongezi ...

29. Wito kwa Baba *****: Watendee Haki Kina ***** Wote Ili Nao Wapate ...

30. Udhalimu wa Waarabu Zanzibar na Pemba: Ndugu zetu wali-teswa ...

Mkuu Paskali sijawahi kuthubutu kuipita "post" yako bila kuisoma thoroughly,this is yet another quality post, haina chembe ya unafiki.
 
This how GT deserve, Hongera mkuu Paskali wewe ni mmoja wa watu waliobaki humu ndani uliosababisha niwe mlevi wa JF.
Sio mafake wengine waliovamia humu either kupinga au kusifia kila kitu, they are nonsense at all.
 
Ujue uzuri mmoja wa kukamatwa vibopa utazijua haki nyingine ambazo hata hazisemwi kila siku wanavyokamatwa makapuku.
 
Hiyo ni sawa tu na perp walk.

Dominic Strauss-Kahn alitembezwa mbele ya waandishi akiwa amefungwa pingu.

Wengine wakiwa booked mug shots zao huwekwa public.

Sioni kabisa tatizo la hao wawili kupigwa picha kwenye hali hiyo.
 
Back
Top Bottom